Ufunuo
7 Baada ya hayo nikaona malaika+ wanne wamesimama juu ya pembe nne za dunia, wakizishika sana zile pepo+ nne za dunia, ili upepo wowote usivume juu ya dunia au juu ya bahari au juu ya mti wowote.+ 2 Nami nikamwona malaika mwingine akipanda kutoka mashariki,+ akiwa na muhuri wa Mungu aliye hai;+ naye akapaaza sauti kubwa kwa wale malaika wanne waliopewa ruhusa kuidhuru dunia na bahari, 3 akisema: “Msiidhuru dunia au bahari au miti, mpaka baada ya sisi kuwatia muhuri+ watumwa wa Mungu wetu katika mapaji ya nyuso zao.”+
4 Nami nikaisikia hesabu ya wale waliotiwa muhuri, 144,000,+ waliotiwa muhuri kutoka kila kabila+ la wana wa Israeli:+
5 Kutoka kabila la Yuda+ kumi na mbili elfu waliotiwa muhuri;
kutoka kabila la Rubeni+ kumi na mbili elfu;
kutoka kabila la Gadi+ kumi na mbili elfu;
6 kutoka kabila la Asheri+ kumi na mbili elfu;
kutoka kabila la Naftali+ kumi na mbili elfu;
kutoka kabila la Manase+ kumi na mbili elfu;
7 kutoka kabila la Simeoni+ kumi na mbili elfu;
kutoka kabila la Lawi+ kumi na mbili elfu;
kutoka kabila la Isakari+ kumi na mbili elfu;
8 kutoka kabila la Zabuloni+ kumi na mbili elfu;
kutoka kabila la Yosefu+ kumi na mbili elfu;
kutoka kabila la Benyamini+ kumi na mbili elfu waliotiwa muhuri.+
9 Baada ya mambo haya nikaona, na, tazama! umati mkubwa,+ ambao hakuna mtu aliyeweza kuuhesabu, kutoka mataifa+ yote na makabila na vikundi vya watu+ na lugha,+ wamesimama mbele ya kiti cha ufalme+ na mbele ya Mwana-Kondoo, wamevikwa kanzu nyeupe;+ na kulikuwa na matawi ya mitende+ mikononi mwao. 10 Nao wanaendelea kupaaza sauti kubwa, wakisema: “Wokovu unatoka kwa Mungu wetu,+ anayeketi juu ya kiti cha ufalme,+ na Mwana-Kondoo.”+
11 Na malaika+ wote walikuwa wamesimama kukizunguka kile kiti cha ufalme na wale wazee+ na wale viumbe hai wanne,+ nao wakaanguka kifudifudi mbele ya kile kiti cha ufalme na kumwabudu Mungu,+ 12 wakisema: “Amina! Baraka na utukufu na hekima na kutoa shukrani na heshima na uwezo na nguvu+ ziwe kwa Mungu wetu milele na milele. Amina.”+
13 Na mmoja wa wale wazee+ akajibu, akaniambia: “Hawa waliovaa kanzu nyeupe,+ wao ni nani nao walitoka wapi?” 14 Basi nikamwambia mara moja: “Bwana wangu, wewe ndiye unayejua.” Naye akaniambia: “Hawa ndio wale wanaotoka katika ile dhiki kuu,+ nao wamefua kanzu zao na kuzifanya nyeupe+ katika damu+ ya Mwana-Kondoo. 15 Ndiyo sababu wako mbele+ ya kile kiti cha ufalme cha Mungu; nao wanamtolea utumishi mtakatifu+ mchana na usiku katika hekalu lake; na Yule anayeketi juu ya kiti cha ufalme+ atatandaza hema+ lake juu yao. 16 Hawatakuwa na njaa tena wala kuwa na kiu tena, wala jua halitawachoma wala joto lolote lenye kuunguza,+ 17 kwa sababu Mwana-Kondoo,+ aliye katikati ya kile kiti cha ufalme, atawachunga,+ na kuwaongoza kwenye chemchemi za maji+ ya uzima. Na Mungu atafuta kila chozi katika macho yao.”+