Isaya
32 Tazama! Mfalme+ atatawala kwa ajili ya uadilifu;+ nao wakuu+ watatawala wakiwa wakuu kwa ajili ya haki. 2 Na kila mmoja atakuwa kama mahali pa kujificha kutokana na upepo na mahali pa kujificha kutokana na dhoruba ya mvua,+ kama vijito vya maji katika nchi isiyo na maji,+ kama kivuli cha mwamba mzito katika nchi iliyochoka.+
3 Na macho ya wale wanaoona hayatafungamanishwa pamoja, na masikio ya wale wanaosikia yatasikiliza.+ 4 Na moyo wa wale walio na haraka kupita kiasi utafikiria ujuzi,+ na hata ulimi wa wenye kigugumizi utasema upesi mambo yaliyo wazi.+ 5 Mtu asiye na akili hataitwa tena mkarimu; naye mtu asiye na msimamo hatasemwa kuwa ni mheshimiwa;+ 6 kwa sababu mtu asiye na akili atasema upumbavu mtupu,+ na moyo wake utatenda madhara,+ utatenda uasi-imani+ na kusema juu ya Yehova mambo mapotovu, utasababisha nafsi ya mwenye njaa kushinda bila kula,+ naye anasababisha hata mtu mwenye kiu ashinde bila maji ya kunywa. 7 Naye mtu asiye na msimamo, vyombo vyake ni vibaya;+ yeye ametoa shauri kwa ajili ya matendo ya mwenendo mpotovu,+ kuwavunja wenye kuteseka kwa maneno ya uwongo,+ hata maskini anaposema jambo lililo haki.
8 Naye mtu mkarimu, ametoa shauri kwa ajili ya mambo ya ukarimu; naye atasimama kwa ajili ya mambo ya ukarimu.+
9 “Enyi wanawake mnaostarehe, simameni, sikilizeni sauti yangu!+ Enyi binti msiojali, litegeeni sikio neno langu! 10 Katika muda wa mwaka mmoja na siku fulani ninyi msiojali mtafadhaika,+ kwa sababu uvunaji wa zabibu utakuwa umefikia mwisho lakini hakuna mavuno ya matunda yatakayoingizwa ndani.+ 11 Tetemekeni, enyi wanawake mnaostarehe! Fadhaikeni, enyi msiojali! Vueni nguo na kuwa uchi, na kuvaa nguo za magunia viunoni.+ 12 Jipigeni vifua katika kuomboleza+ juu ya mashamba yenye kutamanika,+ juu ya mzabibu wenye kuzaa matunda. 13 Juu ya udongo wa watu wangu inatokea miiba mitupu,+ vichaka vyenye miiba, kwa maana viko juu ya nyumba zote zenye furaha, ndiyo, mji uliochangamka sana.+ 14 Kwa maana mnara wa makao umeachwa,+ kelele za jiji zimeachwa; Ofeli+ na mnara wa mlinzi umekuwa nyika, kwa wakati usio na kipimo furaha ya punda-milia, malisho ya makundi; 15 mpaka roho itakapomiminwa juu yetu kutoka juu,+ na nyika itakuwa imekuwa shamba la matunda, na shamba la matunda lihesabiwe kuwa msitu halisi.+
16 “Na katika nyika haki itakaa, nao uadilifu utakaa katika shamba la matunda.+ 17 Na kazi ya uadilifu wa kweli itakuwa amani;+ na utumishi wa uadilifu wa kweli utakuwa utulivu na usalama mpaka wakati usio na kipimo.+ 18 Na watu wangu watakaa katika makao yenye amani na katika makao ya uhakika kamili na katika mahali pa kupumzika pasipo na usumbufu.+ 19 Na hakika kutanyesha mvua ya mawe wakati msitu utakaposhuka+ na jiji kuteremka katika hali ya kushushwa.+
20 “Wenye furaha ni ninyi mnaopanda mbegu kando ya maji yote,+ mkiifungua miguu ya ng’ombe na ya punda.”+