1 Petro
3 Vivyo hivyo,+ ninyi wake, jitiisheni+ kwa waume zenu wenyewe, ili, ikiwa wowote si watiifu+ kwa lile neno, wavutwe+ bila neno kupitia mwenendo wa wake zao,+ 2 kwa sababu wamekwisha kushuhudia kwa macho mwenendo+ wenu ulio safi kiadili pamoja na heshima kubwa. 3 Na kujipamba kwenu kusiwe kule kusuka nywele+ kwa nje na kule kujivika mapambo ya dhahabu+ au kuvaa mavazi ya nje, 4 bali kuwe yule mtu wa siri+ wa moyoni katika vazi lisiloharibika+ la roho ya utulivu na ya upole,+ ambayo ni ya thamani kubwa machoni pa Mungu. 5 Kwa maana, pia, ndivyo walivyokuwa wakijipamba wale wanawake watakatifu hapo zamani, waliokuwa wakimtumaini Mungu, wakijitiisha kwa waume zao wenyewe, 6 kama Sara alivyokuwa akimtii Abrahamu, akimwita “bwana.”+ Nanyi mmekuwa watoto wake, mradi tu mnaendelea kutenda mema na kutokuwa na woga kwa sababu ya kitisho chochote.+
7 Enyi waume, endeleeni kukaa nao vivyo hivyo+ kulingana na ujuzi,+ mkiwapa heshima+ kama chombo dhaifu zaidi, yaani, mwanamke, kwa kuwa ninyi pia ni warithi+ pamoja nao wa pendeleo lisilostahiliwa la uzima, kusudi sala zenu zisizuiwe.+
8 Mwishowe, ninyi nyote iweni na akili zinazopatana,+ mkionyesha hisia-mwenzi, mkiwa na upendo wa kindugu, wenye huruma nyororo,+ wanyenyekevu katika akili,+ 9 msilipe ubaya kwa ubaya+ au matukano kwa matukano,+ bali, kinyume chake, mkitoa baraka,+ kwa sababu mliitwa kwenye mwendo huu, ili mrithi baraka.
10 Kwa maana, “yeye ambaye anapenda uzima na kuona siku zilizo njema,+ na auzuie ulimi+ wake kutokana na yaliyo mabaya na midomo yake isiseme udanganyifu,+ 11 bali na ageuke kutoka katika yaliyo mabaya+ na kufanya yaliyo mema; na atafute amani na kuifuatilia.+ 12 Kwa maana macho+ ya Yehova yako juu ya waadilifu, na masikio yake yanaielekea dua yao;+ bali uso wa Yehova uko dhidi ya wale wanaotenda mambo mabaya.”+
13 Kwa kweli, ni nani atakayewadhuru ninyi mkiwa na bidii kwa ajili ya yaliyo mema?+ 14 Lakini hata mkiteseka kwa ajili ya uadilifu, ninyi ni wenye furaha.+ Hata hivyo, msikiogope kile kitu wanachokiogopa,+ wala msifadhaike.+ 15 Bali mtakaseni Kristo kuwa Bwana katika mioyo yenu,+ sikuzote mkiwa tayari kujitetea+ mbele ya kila mtu ambaye hutaka kutoka kwenu sababu ya tumaini lililo ndani yenu, lakini mkifanya hivyo kwa tabia-pole+ na heshima kubwa.
16 Iweni na dhamiri njema,+ ili katika lile jambo ambalo wanasema vibaya juu yenu waweze kupata aibu+ wale wanaosema kwa kuushushia heshima mwenendo wenu mwema kuhusiana na Kristo.+ 17 Kwa maana ni afadhali kuteseka kwa sababu mnatenda mema,+ ikiwa mapenzi ya Mungu yanataka hivyo, kuliko kuteseka kwa sababu mnatenda maovu.+ 18 Ndiyo, hata Kristo alikufa mara moja kwa wakati wote kuzihusu dhambi,+ mtu mwadilifu kwa ajili ya wasio waadilifu,+ ili awaongoze ninyi kwa Mungu,+ yeye aliuawa katika mwili,+ lakini akafanywa kuwa hai katika roho.+ 19 Katika hali hiyo pia alienda zake na kuwahubiria roho walio gerezani,+ 20 ambao wakati fulani hawakuwa watiifu+ wakati subira ya Mungu+ ilipokuwa ikingoja katika siku za Noa, safina ilipokuwa ikijengwa,+ ambayo ndani yake watu wachache, yaani, nafsi nane, walichukuliwa salama kupitia maji.+
21 Lile ambalo linalingana na hili linawaokoa ninyi sasa pia,+ yaani, ubatizo, (si kuondolea mbali uchafu wa mwili, bali ombi linalotolewa kwa Mungu ili kupata dhamiri njema,)+ kupitia ufufuo wa Yesu Kristo.+ 22 Yeye yuko mkono wa kuume wa Mungu,+ kwa maana alienda zake mbinguni; na malaika+ na mamlaka na nguvu vilitiishwa kwake.+