Wagalatia
4 Basi nasema kwamba wakati mrithi anapokuwa angali mtoto mchanga hatofautiani hata kidogo na mtumwa,+ ingawa yeye ni bwana wa vitu vyote, 2 bali yeye yuko chini ya watu wenye kusimamia+ na chini ya wasimamizi-nyumba mpaka siku ambayo baba yake aliiweka kimbele. 3 Vivyo hivyo sisi pia, tulipokuwa watoto wachanga, tuliendelea kutumikishwa na mambo ya msingi+ yaliyo ya ulimwengu. 4 Lakini wakati kamili ulipofika,+ Mungu alimtuma Mwana wake,+ aliyezaliwa na mwanamke+ na aliyekuja kuwa chini ya sheria,+ 5 ili awaachilie huru kwa kuwanunua+ wale walio chini ya sheria,+ ili sisi nasi tufanywe kuwa wana.+
6 Sasa kwa sababu ninyi ni wana, Mungu ametuma roho+ ya Mwana wake ndani ya mioyo yetu nayo hupaaza sauti: “Abba, Baba!”+ 7 Basi, wewe si mtumwa tena bali ni mwana; na ikiwa ni mwana, pia ni mrithi kupitia Mungu.+
8 Hata hivyo, wakati hamkumjua Mungu,+ ndipo mlipoitumikia ile ambayo kwa asili si miungu.+ 9 Lakini sasa kwa kuwa mmemjua Mungu, au afadhali zaidi kwamba sasa Mungu amewajua ninyi,+ kwa nini mnarudi tena kwenye mambo ya msingi+ yaliyo dhaifu+ na yasiyo na maana na kutaka kuyatumikia kwa mara nyingine tena?+ 10 Mnashika kwa uangalifu mwingi siku+ na miezi+ na majira na miaka. 11 Mimi naogopa kwa ajili yenu, isiwe kwamba kwa njia fulani nimejitaabisha kwa ajili yenu bila kusudi+ lolote.
12 Akina ndugu, ninawaomba ninyi, Iweni kama nilivyo,+ kwa sababu mimi nilikuwa pia kama mlivyo.+ Hamkunitendea kosa lolote.+ 13 Lakini mnajua kwamba ilikuwa kupitia ugonjwa wa mwili wangu kwamba niliwatangazia ninyi habari njema mara ya kwanza.+ 14 Na lililokuwa jaribu kwenu katika mwili wangu, hamkulitendea kwa dharau au kulitemea mate kwa chuki; bali mlinipokea kama malaika+ wa Mungu, kama Kristo Yesu.+ 15 Basi, iko wapi ile furaha mliyokuwa nayo?+ Kwa maana nawatolea ninyi ushahidi kwamba, kama ingaliwezekana, mngaling’oa macho yenu na kunipa hayo.+ 16 Hivyo basi, je, nimekuwa adui+ yenu kwa sababu nawaambia ninyi kweli?+ 17 Wao wanawatafuta ninyi kwa bidii,+ si kwa uzuri, bali wanataka kuwazuia ninyi kutoka kwangu, ili mwatafute wao kwa bidii.+ 18 Hata hivyo, ni vema kwenu mkitafutwa kwa bidii kwa kusudi zuri+ nyakati zote, na si wakati tu mimi ninapokuwa pamoja nanyi,+ 19 watoto wangu wadogo,+ ambao tena nina maumivu ya kuwazaa mpaka Kristo aumbike ndani yenu.+ 20 Lakini ningependa kuwa pamoja nanyi sasa hivi+ na kusema kwa njia tofauti, kwa sababu nahangaika+ juu yenu.
21 Mniambie, ninyi mnaotaka kuwa chini ya sheria,+ Je, hamsikii Sheria?+ 22 Kwa mfano, imeandikwa kwamba Abrahamu alipata wana wawili, mmoja kwa njia ya kijakazi+ na mmoja kwa njia ya mwanamke huru;+ 23 lakini yule wa kijakazi kwa kweli alizaliwa katika namna ya mwili,+ yule mwingine wa mwanamke huru kupitia ahadi.+ 24 Mambo haya yanasimama yakiwa tukio la mfano;+ kwa maana wanawake hawa wanamaanisha maagano mawili,+ moja kutoka Mlima Sinai,+ ambalo huzaa watoto kwa ajili ya utumwa, na ambalo ni Hagari. 25 Basi Hagari huyu anamaanisha Sinai,+ mlima ulio Arabia, naye analingana na Yerusalemu la leo, kwa maana liko katika utumwa+ pamoja na watoto wake. 26 Lakini Yerusalemu+ la juu liko huru, nalo ni mama yetu.+
27 Kwa maana imeandikwa: “Furahi, wewe mwanamke tasa usiyezaa; paaza sauti na kupaaza kilio kikubwa, wewe mwanamke ambaye huna maumivu ya kuzaa mtoto; kwa maana watoto wa mwanamke aliye na ukiwa ni wengi kuliko wale wa yule aliye na mume.”+ 28 Basi, akina ndugu, sisi ni watoto wa ahadi kama Isaka alivyokuwa.+ 29 Lakini kama ilivyokuwa wakati huo, yule aliyezaliwa katika namna ya mwili alianza kumtesa+ yule aliyezaliwa katika namna ya roho, ndivyo ilivyo pia na sasa.+ 30 Hata hivyo, Andiko linasema nini? “Mfukuze kijakazi na mwana wake, kwa maana mwana wa kijakazi hatakuwa mrithi hata kidogo pamoja na mwana wa mwanamke huru.”+ 31 Kwa hiyo, akina ndugu, sisi ni watoto, si wa kijakazi,+ bali wa yule mwanamke huru.+