Zaburi
Kwa kiongozi juu ya Mayungiyungi.+ Ya Daudi.
69 Uniokoe, Ee Mungu, kwa maana maji yamefika mpaka kwenye nafsi.+
2 Nimezama katika matope mengi, mahali ambapo hapana udongo wa kusimama.+
Nimeingia katika maji mengi,
Na kijito kinachotiririka kimenifagilia mbali.+
3 Nimechoka kwa sababu ya kuita kwangu;+
Koo yangu imekauka.
Macho yangu yameshindwa huku nikimngojea Mungu wangu.+
4 Wale wanaonichukia bila sababu wamekuwa wengi hata kuliko nywele za kichwa changu.+
Wale wanaoninyamazisha, wakiwa ni adui zangu bila sababu, wamekuwa wengi.+
Kisha nikarudisha kile ambacho sikuwa nimechukua kwa unyang’anyi.
6 Wale wanaokutumainia na wasione aibu kwa sababu yangu,+
Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi.+
Wale wanaokutafuta na wasifedheheshwe kwa sababu yangu,+
Ee Mungu wa Israeli.+
9 Kwa maana bidii nyingi kwa ajili ya nyumba yako imenila,+
Na shutuma za wale wanaokushutumu zimeniangukia.+
12 Wale wanaoketi kwenye lango wakaanza kujishughulisha nami,+
Nikawa kiini cha nyimbo za watu wanaokunywa kileo.+
13 Lakini mimi, nilikutolea sala, Ee Yehova,+
Wakati unaofaa, Ee Mungu.+
Katika wingi wa fadhili zako zenye upendo unijibu kwa kweli ya wokovu wako.+
14 Unikomboe kutoka katika matope, ili nisizame.+
Na nikombolewe kutoka kwa wale wanaonichukia+ na kutoka katika kilindi cha maji.+
15 Kijito cha maji yanayotiririka kisinifagilie mbali,+
Wala kilindi kisinimeze,
Wala kisima kisifunge kinywa chake juu yangu.+
16 Unijibu, Ee Yehova, kwa maana fadhili zako zenye upendo ni njema.+
Kulingana na wingi wa rehema zako ugeuke kunielekea,+
19 Wewe mwenyewe umejua shutuma yangu na aibu yangu na fedheha yangu.+
Wote wanaonionyesha uadui wako mbele zako.+
20 Shutuma imeuvunja moyo wangu, nalo jeraha haliwezi kuponywa.+
Nami niliendelea kutumainia mtu fulani aonyeshe kusikitika, lakini hapakuwa na yeyote;+
Na watu wa kufariji, lakini sikupata yeyote.+
21 Lakini walinipa mmea wenye sumu kuwa chakula,+
Na kwa ajili ya kiu yangu wakajaribu kuninywesha siki.+
22 Meza yao iliyo mbele yao na iwe mtego,+
Na vitu vilivyo kwa ajili ya hali njema yao na viwe mnaso.+
26 Kwa maana yule ambaye wewe mwenyewe umempiga, wamemfuatilia,+
Nao wanaendelea kusimulia maumivu ya wale ambao wewe uliwachoma.
31 Hilo pia litampendeza Yehova kuliko ng’ombe-dume,+
Kuliko ng’ombe-dume mchanga mwenye pembe, mwenye kwato zilizogawanyika.+
32 Hakika wapole wataliona hilo; watashangilia.+
Ninyi mnaomtafuta Mungu, moyo wenu na uendelee kuwa hai.+