HABAKUKI
1 Tangazo ambalo nabii Habakuki* alipokea katika maono:
2 Ee Yehova, nililie msaada mpaka lini, lakini wewe hunisikii?+
Nitaomba msaada kwa sababu ya ukatili mpaka lini, lakini huingilii kati?*+
3 Kwa nini unanifanya nione mambo mabaya?
Na kwa nini unavumilia ukandamizaji?
Kwa nini uharibifu na ukatili uko mbele yangu?
Na kwa nini ugomvi na mizozo inaongezeka?
4 Kwa hiyo sheria haifanyi kazi,
Na haki haitekelezwi kamwe.
Kwa maana mwovu amemzingira mwadilifu;
Ndiyo sababu haki imepotoshwa.+
5 “Tazameni miongoni mwa mataifa, kazeni uangalifu!
Tazameni kwa mshangao na kustaajabu;
Kwa maana jambo fulani litatukia katika siku zenu
Ambalo hamtaamini hata mkiambiwa.+
6 Kwa maana tazama, ninawainua Wakaldayo,+
Taifa katili na linalotenda haraka-haraka,
Wanasambaa upesi katika maeneo makubwa sana ya dunia
Ili wachukue kwa nguvu makao ambayo si yao.+
7 Wanatisha na kuogopesha.
Wanaweka sheria* yao wenyewe na mamlaka* yao wenyewe.+
Farasi wao wa vita hukimbia mbele kwa kasi;
Farasi wao hutoka mbali sana.
Wanashuka chini kwa kasi kama tai anayekimbilia chakula.+
9 Wote huja wakikusudia kutenda ukatili.+
Nyuso zao kwa pamoja ni kama upepo wa mashariki,+
Nao huchota mateka kama mchanga.
Wanaicheka kila ngome;+
Wanatengeneza daraja kwa rundo la udongo na kuiteka.
12 Je, wewe si wa tangu milele, Ee Yehova?+
Ee Mungu wangu, Mtakatifu wangu, wewe hufi.*+
Basi, kwa nini unawavumilia wenye hila+
Na kunyamaza mtu mwovu anapommeza mtu mwadilifu kuliko yeye?+
14 Kwa nini unamfanya mwanadamu awe kama samaki wa baharini,
Kama viumbe wanaotambaa ambao hawana mtawala?
15 Hao wote yeye* huwavua kwa ndoano.
Huwakamata kwa wavu wake wa kukokotwa,
Naye huwakusanya katika wavu wake wa kuvulia samaki.
Ndiyo sababu anashangilia sana.+
16 Ndiyo sababu anatoa dhabihu kwa ajili ya wavu wake wa kukokotwa
Na kutoa dhabihu* kwa ajili ya wavu wake wa kuvulia samaki;
Kwa maana nyavu hizo zimemletea utajiri,*
Na chakula chake ni bora.
17 Je, ataendelea kutoa samaki katika wavu wake wa kukokotwa?*
Je, ataendelea kuyaangamiza mataifa bila huruma?+
2 Nitaendelea kusimama katika kituo changu cha ulinzi,+
Nami nitasimama juu ya boma.
Nitaendelea kukaa macho ili nione atakalosema kupitia kwangu
Na lile nitakalojibu nitakapokaripiwa.
2 Kisha Yehova akanijibu:
“Andika maono haya, na uyaandike waziwazi kwenye mabamba,+
3 Kwa maana maono hayo bado yatatimia kwa wakati wake uliowekwa,
Nayo yanasonga haraka kuelekea mwisho* wake, nayo hayatasema uwongo.
Hata yakikawia,* endelea kuyatarajia!*+
Kwa maana hakika yatatimia.
Hayatachelewa!
Lakini mwadilifu ataishi kwa uaminifu wake.*+
5 Kwa kweli, kwa sababu divai ina hila,
Mtu mwenye kiburi hatatimiza lengo lake.
Huendelea kuyakusanya mataifa yote
Na kujikusanyia watu wa mataifa yote.+
6 Je, hao wote hawatasema methali, fumbo, na vitendawili kumshutumu?+
Watasema:
‘Ole wake anayejirundikia vitu visivyo vyake
—Mpaka lini?—
Na kufanya deni lake mwenyewe liwe kubwa hata zaidi!
7 Je, wanaokudai hawatainuka kwa ghafla?
Wataamka na kukutikisa kwa fujo,
Nawe utakuwa kitu cha kuporwa nao.+
8 Kwa sababu ulipora mataifa mengi,
Mataifa mengine yote yatakupora,+
Kwa sababu ulimwaga damu ya wanadamu
Na kwa sababu ya ukatili ulioitendea dunia,
Majiji na wale wanaoishi humo.+
9 Ole wake anayeitafutia nyumba yake faida ya uovu,
Ili aweke kiota chake juu,
Aepuke kunaswa na msiba!
10 Umepanga njama ya aibu dhidi ya nyumba yako.
Kwa kuyaangamiza mataifa mengi unatenda dhambi dhidi yako mwenyewe.*+
11 Kwa maana jiwe litapaza sauti kutoka ukutani,
Na kutoka kwenye mbao za paa, boriti italijibu jiwe hilo.
12 Ole wake anayejenga jiji kwa umwagaji wa damu,
Na kuusimamisha mji kwa ukosefu wa uadilifu!
13 Tazama! Je, si Yehova wa majeshi anayesababisha mataifa yafanye kazi kwa bidii ili kuulisha moto,
Na kusababisha mataifa yajichoshe bure?+
15 Ole wake anayewapa wenzake kinywaji,
Na kuongeza ghadhabu na hasira ndani yake ili awaleweshe,
Kusudi atazame uchi wao!
16 Utajaa kabisa aibu badala ya utukufu.
Wewe pia—kunywa na kufunua hali yako ya kutotahiriwa.*
Kikombe kilicho kwenye mkono wa kuume wa Yehova kitazunguka na kufika kwako,+
Na fedheha itafunika kabisa utukufu wako;
17 Kwa sababu ukatili ulioitendea Lebanoni utakufunika,
Na maangamizi yaliyowatisha wanyama yatakujia,
Kwa sababu ulimwaga damu ya wanadamu
Na kwa sababu ya ukatili ulioitendea dunia,
Uliyoyatendea majiji na wale wanaoishi humo.+
18 Sanamu ya kuchongwa ina faida gani
Na mtu ndiye aliyeichonga?
Sanamu ya chuma* na mwalimu wa uwongo ana faida gani,
Hata ingawa yule aliyeitengeneza anaitumaini,
Akitengeneza miungu ya ubatili ambayo haiwezi kuongea?+
19 Ole wake anayekiambia kipande cha ubao, “Amka!”
Au anayeliambia jiwe lisiloweza kuongea, “Amka! Tufundishe!”
20 Lakini Yehova yuko katika hekalu lake takatifu.+
Dunia yote na inyamaze mbele zake!’”+
3 Sala ya nabii Habakuki, aliyoitoa kama nyimbo za huzuni:*
2 Ee Yehova, nimesikia habari kukuhusu.
Ninaogopa matendo yako, Ee Yehova.
Uyafufue kati ya ile miaka!*
Uyafanye yajulikane kati ya hiyo miaka.*
Nawe ukumbuke kuonyesha rehema wakati wa msukosuko.+
Utukufu wake ulifunika mbingu;+
Na dunia ikajaa sifa yake.
Miale miwili ilimweka kutoka mkononi mwake,
Ambamo nguvu zake zilikuwa zimefichika.
6 Alisimama tuli na kuitikisa dunia.+
Alitazama mara moja tu, akayafanya mataifa yaruke.+
Milima ya milele ikavunjwavunjwa,
Na vilima vya kale vikainama chini.+
Vijia vya zamani za kale ni vyake.
7 Niliona taabu katika mahema ya Kushani.
Vitambaa vya mahema ya nchi ya Midiani vilitetemeka.+
8 Je, umeikasirikia mito, Ee Yehova,
Je, hasira yako inawaka dhidi ya mito?
Au unaikasirikia vikali bahari?+
9 Upinde wako umefunuliwa na uko tayari.
Fito zimepewa* kazi kwa kiapo.* (Sela)
Unaipasua dunia kwa mito.
10 Milima ilipindapinda kwa maumivu ilipokuona.+
Mvua kubwa ilinyesha nchini.
Kilindi cha maji kilinguruma kwa sauti yake.+
Kikainua mikono yake juu.
11 Jua na mwezi vilisimama tuli kwenye makao yake yaliyo juu sana.+
Mishale yako ilitoka kama nuru.+
Radi ya mkuki wako ilikuwa nyangavu.
12 Ulipiga mwendo duniani kwa ghadhabu.
Ukayakanyaga-kanyaga* mataifa kwa hasira.
13 Ulitoka ili kuwaokoa watu wako, kumwokoa mtiwa-mafuta wako.
Ulimpondaponda kiongozi wa* nyumba ya waovu.
Ilifunuliwa wazi kuanzia kwenye msingi hadi juu.* (Sela)
14 Uliwachoma vichwa mashujaa wake kwa silaha* zake mwenyewe
Walipoondoka kwa kishindo ili kunitawanya.
Walishangilia sana kumnyafua kisiri mtu anayeteseka.
15 Ulivuka bahari kwa farasi wako,
Katikati ya mawimbi yaliyoinuka ya maji mengi.
Uozo ukaingia mifupani mwangu;+
Miguu yangu ikatetemeka.
Lakini nangojea kimyakimya ile siku ya taabu,+
Kwa sababu inawajia watu wanaotushambulia.
17 Ingawa huenda mtini usichanue,
Na huenda mizabibu isiwe na matunda;
Ingawa huenda mizeituni isizae,
Na mashamba yasiwe na mazao yoyote;
Ingawa huenda mazizi yasiwe na kondoo,
Na mabanda yasiwe na ng’ombe;
18 Lakini mimi nitashangilia katika Yehova;
Nitakuwa na shangwe katika Mungu wa wokovu wangu.+
19 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova ni nguvu zangu;+
Ataifanya miguu yangu iwe kama ya paa
Na kuniwezesha kutembea mahali palipoinuka.+
Kwa kiongozi; kwa kutumia vinanda vyangu.
Huenda jina hili linamaanisha “Kumbatio Changamfu.”
Au “huniokoi.”
Au “haki.”
Au “heshima.”
Au labda, “nguvu zao ni mungu wao.”
Au labda, “sisi hatutakufa.”
Au “wakaripie.”
Yaani, jeshi la Wakaldayo.
Au “kufukiza moshi wa dhabihu.”
Tnn., “Kwa maana kupitia hizo fungu lake limetiwa mafuta mengi.”
Au labda, “kuchomoa upanga wake.”
Au “kwa ufasaha.”
Au “utimizo.”
Au “Hata ikionekana kwamba yanakawia.”
Au “kuyangojea kwa hamu!”
Au “Tazama! Nafsi yake imefutuka.
Au labda, “imani yake; itikadi yake.”
Au “nafsi.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “dhidi ya nafsi yako.”
Au labda, “na kupepesuka.”
Au “sanamu ya kuyeyushwa.”
Au “nyimbo za maombolezo.”
Au labda, “wakati wetu!”
Au labda, “wakati wetu!”
Angalia Kamusi.
Au “yalikuwa wokovu.”
Au labda, “Mishale imepewa.”
Au labda, “Viapo vya makabila vimesemwa.”
Tnn., “Ukayapura.”
Tnn., “Ulikipondaponda kichwa cha.”
Tnn., “shingoni.”
Tnn., “fito.”
Tnn., “na tumbo langu likatetemeka.”