Isaya
52 Amka, amka, vaa nguvu zako,+ Ee Sayuni! Vaa mavazi yako mazuri,+ Ee Yerusalemu, jiji takatifu!+ Kwa maana mtu asiyetahiriwa na mtu asiye safi hawataingia ndani yako tena.+ 2 Jitikise uwe huru kutoka mavumbini,+ simama, chukua kiti, Ee Yerusalemu. Jifungue pingu za shingo yako, Ee binti Sayuni uliye mateka.+
3 Kwa maana Yehova amesema hivi: “Ninyi mliuzwa bure,+ nanyi mtakombolewa bila pesa.”+
4 Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Watu wangu waliteremka kwenda Misri hapo kwanza ili kukaa wakiwa wageni;+ nayo Ashuru ikawakandamiza bila sababu.”
5 “Na sasa, nina faida gani hapa?” asema Yehova. “Kwa maana watu wangu walichukuliwa bure.+ Wale waliokuwa wakiwatawala waliendelea kupiga mayowe,”+ asema Yehova, “na sikuzote, mchana kutwa, jina langu lilikuwa likivunjiwa heshima.+ 6 Kwa sababu hiyo watu wangu watalijua jina langu,+ kwa sababu hiyo katika siku hiyo, kwa sababu mimi ndiye Yule anayesema.+ Tazama! Ni mimi.”
7 Jinsi inavyopendeza juu ya milima miguu+ ya yeye anayeleta habari njema,+ yeye anayetangaza amani,+ yeye anayeleta habari njema za jambo bora,+ yeye anayetangaza wokovu,+ yeye anayeuambia Sayuni: “Mungu wako amekuwa mfalme!”+
8 Sikiliza! Walinzi+ wako mwenyewe wamepaaza sauti yao.+ Wanaendelea kupiga pamoja vigelegele kwa shangwe; kwa maana wataona jicho kwa jicho+ wakati Yehova atakapokusanya Sayuni tena.+
9 Changamkeni, pigeni pamoja vigelegele kwa shangwe, enyi mahali palipoharibiwa pa Yerusalemu,+ kwa maana Yehova amewafariji watu wake;+ amekomboa Yerusalemu.+ 10 Yehova ameweka wazi mkono wake mtakatifu mbele ya macho ya mataifa yote;+ na miisho yote ya dunia itauona wokovu wa Mungu wetu.+
11 Geukeni, geukeni, tokeni humo,+ msiguse kitu chochote kilicho najisi;+ tokeni katikati yake,+ jiwekeni safi, ninyi mnaovichukua vyombo vya Yehova.+ 12 Kwa maana hamtaondoka na wasiwasi, wala hamtaenda kwa kukimbia.+ Kwa maana Yehova atakuwa akienda mbele yenu,+ na Mungu wa Israeli atakuwa mlinzi wenu wa nyuma.+
13 Tazama! Mtumishi wangu+ atatenda kwa ufahamu.+ Atakuwa na cheo cha juu na hakika yeye atainuliwa na kutukuzwa sana.+ 14 Kwa kadiri ambavyo wengi wamemtazama kwa mshangao+—sura yake ilikuwa imeharibika sana+ kuliko ya mwanadamu mwingine yeyote na umbo lake lenye fahari+ kuliko lile la wana wa binadamu— 15 vivyo hivyo atayashtua mataifa mengi.+ Wafalme watafunga kinywa chao mbele yake,+ kwa sababu kwa kweli wataona yale ambayo hawakuwa wamepata kusimuliwa, nao watafikiria mambo ambayo hawakuwa wamepata kusikia.+