Waebrania
13 Upendo wenu wa kindugu na uendelee.+ 2 Msisahau ukaribishaji-wageni,+ kwa maana kupitia huo watu wengine, bila wao wenyewe kujua, waliwakaribisha malaika.+ 3 Wakumbukeni wale walio katika vifungo vya gereza+ kana kwamba ninyi mmefungwa pamoja nao,+ na wale wanaotendewa vibaya,+ kwa kuwa ninyi wenyewe pia bado mko katika mwili. 4 Ndoa na iheshimiwe kati ya wote, na kitanda cha ndoa kiwe bila unajisi,+ kwa maana Mungu atawahukumu waasherati na wazinzi.+ 5 Namna yenu ya maisha iwe bila upendo wa pesa,+ huku mkiridhika+ na vitu vya sasa.+ Kwa maana yeye amesema: “Sitakuacha wala kukutupa hata kidogo.”+ 6 Hivi kwamba tuwe hodari+ na kusema: “Yehova ni msaidizi wangu; sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?”+
7 Wakumbukeni wale ambao wanaongoza katikati yenu,+ ambao wamelisema neno la Mungu kwenu, nanyi mnapotafakari jinsi mwisho wa mwenendo wao unavyokuwa, igeni+ imani yao.+
8 Yesu Kristo ni yuleyule jana na leo, na milele.+
9 Msichukuliwe mbali na mafundisho mbalimbali na yaliyo mageni;+ kwa maana ni vizuri moyo upewe uthabiti kwa fadhili zisizostahiliwa,+ si kwa vyakula,+ ambavyo wale wanaojishughulisha navyo hawajapata faida.
10 Sisi tuna madhabahu ambayo wale wanaofanya utumishi mtakatifu katika hema hawana mamlaka ya kula kutokana nayo.+ 11 Kwa maana miili ya wale wanyama ambao kuhani mkuu hupeleka damu yao ndani ya mahali patakatifu kwa ajili ya dhambi huteketezwa nje ya kambi.+ 12 Kwa hiyo Yesu pia, ili apate kuwatakasa+ watu kwa damu+ yake mwenyewe, aliteseka nje ya lango.+ 13 Basi, acheni sisi twende kwake nje ya kambi, tukiichukua shutuma aliyoibeba,+ 14 kwa maana sisi hatuna hapa jiji linaloendelea kuwako,+ bali tunatafuta kwa bidii lile litakalokuja.+ 15 Kupitia yeye sikuzote na tumtolee Mungu dhabihu ya sifa,+ yaani, tunda la midomo+ ambayo hulifanyia jina lake tangazo la hadharani.+ 16 Zaidi ya hayo, msisahau kutenda mema+ na kushiriki vitu pamoja na wengine, kwa maana Mungu hupendezwa vema na dhabihu za namna hiyo.+
17 Watiini wale wanaoongoza katikati yenu+ na mnyenyekee,+ kwa maana wanaendelea kuzilinda nafsi zenu kama wale watakaotoa hesabu;+ ili wafanye hivyo kwa shangwe na si kwa kuugua, kwa maana kufanya hivyo kungewadhuru ninyi.+
18 Endeleeni kusali+ kwa ajili yetu, kwa maana sisi tuna uhakika kwamba tuna dhamiri nyoofu, kwa kuwa tunataka kujiendesha kwa unyoofu katika mambo yote.+ 19 Lakini ninawahimiza ninyi zaidi hasa mfanye hivyo, ili nirudishwe kwenu upesi inavyowezekana.+
20 Basi Mungu wa amani,+ aliyemrudisha kutoka kwa wafu+ mchungaji+ mkuu wa kondoo+ kwa damu ya agano linalodumu milele,+ Bwana wetu Yesu, 21 na awape ninyi vifaa vyema vya kila namna ili kufanya mapenzi yake, akifanya katika sisi kupitia Yesu Kristo lile ambalo linapendeza vema machoni pake;+ ambaye kwake kuwe na utukufu milele na milele.+ Amina.
22 Basi ninawahimiza ninyi, akina ndugu, mlivumilie neno hili la kutia moyo, kwa maana mimi, kwa kweli, nimewaandikia barua kwa maneno machache.+ 23 Jueni kwamba ndugu yetu Timotheo+ ameachiliwa, naye akija hivi karibuni sana, nitawaona ninyi nikiwa pamoja naye.
24 Wapeni salamu zangu wale wote wanaoongoza+ katikati yenu na watakatifu wote. Wale walio katika Italia+ wanawatumia ninyi salamu zao.