KITABU CHA NNE
(Zaburi 90 – 106)
Sala ya Musa, mtu wa Mungu wa kweli.+
90 Ee Yehova, wewe mwenyewe umekuwa makao yetu halisi+
Kwa kizazi baada ya kizazi.+
2 Kabla ya kuzaliwa kwa milima,+
Au kutokezwa kwa dunia+ na nchi yenye kuzaa kana kwamba kwa maumivu ya kuzaa,+
Tangu wakati usio na kipimo mpaka wakati usio na kipimo wewe ni Mungu.+
3 Unamfanya mwanadamu anayeweza kufa arudi kuwa kitu kilichopondwa,+
Nawe unasema: “Rudini, enyi wana wa binadamu.”+
4 Kwa maana miaka elfu machoni pako ni kama jana ikiisha kupita,+
Na kama kesha la usiku.+
5 Umewafagilia mbali;+ wanakuwa usingizi tu;+
Asubuhi, wao ni kama majani mabichi ambayo hubadilika.+
6 Asubuhi huchanua maua na lazima yabadilike;+
Jioni, hunyauka na hakika hukauka.+
7 Kwa maana tumefikia mwisho kwa hasira yako,+
Na kwa ghadhabu yako tumetiwa wasiwasi.+
8 Umeyaweka makosa yetu moja kwa moja mbele zako,+
Mambo yetu yaliyofichika mbele za uso wako unaong’aa.+
9 Kwa maana siku zetu zote zimepungua katika ghadhabu yako;+
Tumeimaliza miaka yetu kama mnong’ono tu.+
10 Kwa maana siku za miaka yetu ni miaka 70;+
Na ikiwa kwa sababu ya nguvu za pekee ni miaka 80,+
Hata hivyo hizo husisitiza kuleta taabu na mambo yenye kuumiza;+
Kwa maana lazima zipite upesi, nasi huruka na kwenda zetu.+
11 Ni nani anayejua nguvu za hasira yako+
Na ghadhabu yako kulingana na kukuogopa wewe?+
12 Utuonyeshe jinsi ya kuzihesabu siku zetu hivi kwamba+
Tupate kuuingiza moyo wa hekima.+
13 Urudi, Ee Yehova!+ Mpaka wakati gani?+
Nawe ujute juu ya watumishi wako.+
14 Utushibishe asubuhi kwa fadhili zako zenye upendo,+
Ili tupate kupiga vigelegele kwa shangwe na kufurahi siku zetu zote.+
15 Utufanye tushangilie kulingana na siku ambazo umetutesa,+
Miaka ambayo tumeona msiba.+
16 Utendaji wako na uonekane kwa watumishi wako+
Na fahari yako juu ya wana wao.+
17 Nao uzuri wa Yehova Mungu wetu na uwe juu yetu,+
Na kazi ya mikono yetu uifanye imara juu yetu.+
Naam, kazi ya mikono yetu, uifanye imara.+