Zekaria
11 “Fungua milango yako, Ee Lebanoni,+ ili moto uteketeze kati ya mierezi yako.+ 2 Piga mayowe, Ee mberoshi, kwa maana mwerezi umeanguka; kwa sababu wenye utukufu wameporwa!+ Pigeni mayowe, enyi miti mikubwa sana ya Bashani, kwa maana msitu usiopenyeka umeanguka!+ 3 Sikiliza! Mayowe ya wachungaji,+ kwa maana utukufu wao umeporwa.+ Sikiliza! Kunguruma kwa wana-simba wenye manyoya shingoni, kwa maana vichaka vyenye kiburi kando ya Yordani vimeporwa.+
4 “Yehova Mungu wangu asema hivi, ‘Chunga kundi lililokusudiwa kuuawa,+ 5 ambalo wanunuzi wake huwaua+ ingawa hawahesabiwi hatia.+ Na wale wanaowauza+ husema: “Yehova abarikiwe, huku nami nitapata utajiri.”+ Na wachungaji wao wenyewe hawawaonyeshi huruma yoyote.’+
6 “ ‘Kwa maana sitawahurumia tena wakaaji wa nchi,’+ asema Yehova. ‘Kwa hiyo nawafanya wanadamu wajikute, kila mmoja katika mkono wa mwenzake+ na katika mkono wa mfalme+ wake; nao wataivunja nchi vipande-vipande, nami sitakomboa kwa vyovyote kutoka mkononi mwao.’ ”+
7 Nami nililichunga kundi+ lililokusudiwa kuuawa,+ kwa ajili yenu, enyi wenye kuteseka wa kundi.+ Kwa hiyo nikajichukulia fimbo+ mbili. Moja nikaiita Uzuri,+ na ile nyingine nikaiita Muungano,+ nami nikaanza kulichunga kundi. 8 Mwishowe nikafutilia mbali wachungaji watatu katika mwezi mmoja,+ kwa vile nafsi yangu ilikosa subira+ kwao hatua kwa hatua, na pia nafsi zao zilinichukia. 9 Mwishowe nikasema: “Sitaendelea kuwachunga ninyi.+ Yule anayekufa, na afe. Na yule anayefutiliwa mbali, na afutiliwe mbali.+ Na wale waliobaki, kila mmoja na ale nyama ya mwenzake.”+ 10 Basi nikachukua fimbo yangu inayoitwa Uzuri+ na kuikata vipande-vipande,+ ili kulivunja agano langu ambalo nilikuwa nimefanya pamoja na vikundi vyote vya watu.+ 11 Nalo likavunjwa siku hiyo, na hivyo wenye kuteseka wa kundi+ waliokuwa wakinitazama+ wakajua kwamba hilo lilikuwa neno la Yehova.
12 Ndipo nikawaambia: “Ikiwa vema machoni penu,+ nipeni mshahara wangu; lakini kama sivyo, acheni.” Basi wakalipa mshahara wangu, vipande 30 vya fedha.+
13 Kwa hiyo Yehova akaniambia: “Utupe ndani ya hazina+—thamani tukufu ambayo nimekadiriwa kwa maoni yao.”+ Ndipo nikavichukua vile vipande 30 vya fedha, nami nikavitupa ndani ya hazina katika nyumba ya Yehova.+
14 Kisha nikaikata vipande-vipande fimbo yangu ya pili, inayoitwa Muungano,+ ili kuuvunja undugu+ kati ya Yuda na Israeli.+
15 Kisha Yehova akaendelea kuniambia: “Jichukulie tena vifaa vya mchungaji asiyefaa kitu.+ 16 Kwa maana tazama, ninamwacha mchungaji asimame katika nchi hii.+ Hatawakazia fikira kondoo wanaofutiliwa mbali.+ Hatawatafuta wachanga, wala hatawaponya kondoo waliovunjika.+ Anayesimama hatampa chakula, naye atakula nyama ya aliye mnono,+ atazing’oa kwato za kondoo.+ 17 Ole wake mchungaji wangu asiyefaa kitu,+ anayeliacha kundi!+ Upanga utakuwa juu ya mkono wake na juu ya jicho lake la kuume. Mkono wake utakauka+ bila shaka, na jicho lake la kuume bila shaka litaingia giza.”