1 Timotheo
6 Wale wote walio watumwa chini ya nira na waendelee kuwaona mabwana wao kuwa wenye kustahili heshima kamili,+ ili jina la Mungu na fundisho lisisemwe vibaya kamwe.+ 2 Zaidi ya hayo, wale walio na mabwana+ wenye kuamini wasiwadharau,+ kwa sababu wao ni ndugu.+ Kinyume chake, na wawe watumwa kwa utayari zaidi, kwa sababu wale wanaopokea faida ya utumishi wao mwema ni waamini na wapendwa.
Endelea kufundisha mambo haya+ na kutoa mahimizo haya. 3 Kama mtu yeyote akifundisha fundisho lingine+ na hakubaliani na maneno yenye afya,+ yale ya Bwana wetu Yesu Kristo, wala na fundisho ambalo linapatana na ujitoaji-kimungu,+ 4 yeye anajivuna kwa kiburi,+ haelewi jambo lolote,+ bali ni mgonjwa kiakili+ juu ya maswali na mabishano juu ya maneno.+ Mambo hayo hutokeza wivu,+ mizozo, matukano,+ shuku zenye uovu, 5 mabishano makali juu ya mambo madogo-madogo kwa upande wa watu walioharibika katika akili+ na kuporwa ile kweli,+ wakifikiri kwamba ujitoaji-kimungu ni njia ya kupata faida.+ 6 Kwa hakika, huo ni njia ya kupata faida kubwa,+ huu ujitoaji-kimungu+ pamoja na ujitoshelevu.+ 7 Kwa maana hatukuleta chochote katika ulimwengu, wala hatuwezi kuchukua chochote nje.+ 8 Kwa hiyo, tukiwa na chakula na kitu cha kujifunika, tutaridhika na vitu hivyo.+
9 Hata hivyo, wale ambao wameazimia kuwa matajiri huanguka katika jaribu+ na mtego na tamaa nyingi za kijinga na zenye kudhuru,+ ambazo hutumbukiza watu katika maangamizi na uharibifu.+ 10 Kwa maana kupenda+ pesa ni chanzo+ cha mambo mabaya ya namna zote,+ na kwa kujitahidi kufikia upendo huo wengine wamepotoshwa kutoka kwenye imani nao wamejichoma wenyewe kila mahali kwa maumivu mengi.+
11 Hata hivyo, wewe, Ee mtu wa Mungu, yakimbie mambo hayo.+ Lakini fuatilia uadilifu, ujitoaji-kimungu, imani, upendo, uvumilivu, tabia-pole.+ 12 Pigana pigano zuri la imani,+ ushike imara ule uzima wa milele ambao uliitiwa nawe ukatoa tangazo zuri la hadharani+ mbele ya mashahidi wengi.
13 Machoni pa Mungu, ambaye huvihifadhi vitu vyote hai, na machoni pa Kristo Yesu, ambaye akiwa shahidi+ alifanya tangazo zuri la hadharani+ mbele ya Pontio Pilato,+ mimi nakupa wewe maagizo+ 14 kwamba uishike amri katika njia isiyo na doa na isiyolaumika mpaka wakati wa ufunuo+ wa Bwana wetu Yesu Kristo. 15 Ufunuo huo yule Mwenye Uwezo Mkubwa+ aliye wa pekee na mwenye furaha atauonyesha katika nyakati zake wenyewe zilizowekwa,+ yeye Mfalme+ wa wale wanaotawala wakiwa wafalme na Bwana+ wa wale wanaotawala wakiwa mabwana, 16 yeye peke yake asiyeweza kufa,+ anayekaa katika nuru isiyoweza kufikiwa,+ ambaye hakuna hata mmoja kati ya wanadamu amemwona au anaweza kumwona.+ Kwake yeye na kuwe heshima+ na nguvu milele. Amina.
17 Uwape maagizo wale walio matajiri+ katika mfumo wa mambo wa sasa wasitake makuu,+ na waweke tumaini lao, si katika utajiri usio hakika,+ bali katika Mungu, ambaye hutupa sisi vitu vyote kwa wingi ili tuvifurahie;+ 18 wafanye mema,+ wawe matajiri katika matendo mazuri,+ wawe wakarimu, tayari kushiriki,+ 19 wakijiwekea wenyewe kwa usalama hazina+ ya msingi mzuri+ kwa ajili ya wakati ujao, ili waushike imara uzima ulio wa kweli.+
20 Ee Timotheo, linda lililowekwa amana kwako,+ ukigeuka mbali kutoka kwenye maneno matupu ambayo huchafua mambo matakatifu na kutoka kwenye maneno yanayopingana ya ule unaoitwa kwa uwongo “ujuzi.”+ 21 Kwa maana kwa kujisifia ujuzi wa namna hiyo wengine wamegeuka kutoka kwenye imani.+
Fadhili zisizostahiliwa na ziwe pamoja nanyi.