Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bi12 Yona 1:1-4:11
  • Yona

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yona
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Yona

Yona

1 Neno la Yehova likaanza kumjia Yona+ mwana wa Amitai, na kusema: 2 “Ondoka, uende Ninawi+ lile jiji kubwa, ukalitangazie kwamba ubaya wao umefika mbele zangu.”+

3 Naye Yona akasimama na kukimbia kwenda Tarshishi+ kutoka mbele za Yehova;+ mwishowe akafika Yopa+ na kupata meli inayokwenda Tarshishi. Basi akatoa malipo yake ya kusafiri, akashuka chini ndani ya meli, apate kwenda pamoja nao Tarshishi kutoka mbele za Yehova.

4 Na Yehova mwenyewe akavumisha upepo mkubwa baharini,+ kukawa na tufani kubwa+ baharini; nayo meli ikawa karibu kuvunjika. 5 Nao wanamaji wakaanza kuogopa na kuomba msaada, kila mmoja kwa mungu wake.+ Nao wakawa wakitupa baharini vyombo vilivyokuwa ndani ya meli, ili kuipunguzia uzito wake.+ Lakini Yona alikuwa ameshuka na kuingia sehemu za ndani kabisa za chombo hicho chenye ghorofa, naye akajilaza chini, akalala usingizi mzito.+ 6 Mwishowe kapteni wa meli akamkaribia na kumwambia: “Una nini wewe, mwenye kulala usingizi? Simama, mwite mungu wako!+ Huenda Mungu wa kweli ataonyesha kuwa anatujali, nasi hatutaangamia.”+

7 Nao wakaanza kusemezana: “Njooni, tupige kura,+ tupate kujua ni kwa sababu ya nani tuna taabu hii.”+ Nao wakaendelea kupiga kura, mwishowe kura ikamwangukia Yona.+ 8 Basi wakamwambia: “Tafadhali tuambie, ni kwa sababu ya nani tuna taabu hii?+ Unafanya kazi gani, nawe unatoka wapi? Unatoka nchi gani, nawe umetoka kwa watu wa taifa gani?”

9 Ndipo akawaambia: “Mimi ni Mwebrania,+ nami namwogopa+ Yehova Mungu wa mbinguni,+ Yeye aliyeifanya bahari na nchi kavu.”+

10 Na watu hao wakaanza kuogopa sana, wakamwambia: “Ni nini hili ambalo umefanya?”+ Kwa maana watu hao walikuwa wamepata kujua kwamba alikuwa akikimbia kutoka mbele za Yehova, kwa sababu alikuwa amewaambia. 11 Mwishowe wakamwambia: “Tukufanyie nini,+ ili bahari itulie kwa ajili yetu?” Kwa maana bahari ilikuwa ikizidi kuchafuka. 12 Basi akawaambia: “Mninyanyue na kunitupa baharini, nayo bahari itatulia kwa ajili yenu; kwa maana najua kwamba ni kwa sababu yangu tufani hii kubwa imewajia.”+ 13 Lakini watu hao wakajaribu kupasua njia, wapate kuirudisha meli kwenye nchi kavu; hata hivyo hawakuweza, kwa sababu bahari ilikuwa ikizidi kuwachafukia.+

14 Nao wakaanza kumwita Yehova na kusema:+ “Ah, sasa, Ee Yehova, tafadhali, tusiangamie kwa sababu ya nafsi ya mtu huyu! Nawe usiweke juu yetu damu isiyo na hatia,+ kwa kuwa wewe mwenyewe, Ee Yehova, umefanya ulivyopenda!”+ 15 Ndipo wakamnyanyua Yona, wakamtupa baharini; na bahari ikaanza kutulia, ikaacha kuchafuka.+ 16 Halafu watu hao wakaanza kumwogopa sana Yehova,+ na hivyo wakamtolea Yehova dhabihu+ na kuweka nadhiri.+

17 Sasa Yehova akamweka samaki mkubwa ammeze Yona,+ naye Yona akawa katika tumbo la samaki huyo siku tatu mchana na usiku.+

2 Ndipo, kutoka ndani ya tumbo la samaki huyo, Yona akasali kwa Yehova Mungu wake+ 2 na kusema:

“Katika taabu yangu nilimwita Yehova,+ naye akanijibu.+

Katika tumbo la Kaburi* nilililia msaada.+

Ulisikia sauti yangu.+

 3 Uliponitupa kwenye vilindi, ndani ya moyo wa bahari kuu,+

Ndipo mto nao ukanizunguka.

Mashuu yako yote na mawimbi yako​​—​yalipita juu yangu.+

 4 Nami nikasema, ‘Nimefukuzwa kutoka mbele za macho yako!+

Nitapataje kuliona tena hekalu lako takatifu?’+

 5 Maji yalinizunguka mpaka katika nafsi;+ kilindi cha maji nacho kikazidi kunizunguka.

Magugu yalinizunguka kichwani.

 6 Nilishuka mpaka sehemu za chini kabisa za milima.

Nayo dunia, mapingo yake yalikuwa juu yangu mpaka wakati usio na kipimo.

Lakini uliinua uhai wangu toka shimoni, Ee Yehova Mungu wangu.+

 7 Nafsi yangu ilipozimia ndani yangu,+ Yehova Ndiye niliyemkumbuka.+

Ndipo sala yangu ikaingia kwako, ndani ya hekalu lako takatifu.+

 8 Nao wale wanaozifuata sanamu zisizo za kweli, wanaziacha fadhili zao wenyewe zenye upendo.+

 9 Lakini mimi, kwa sauti ya kutoa shukrani nitakutolea dhabihu.+

Nilichoweka nadhiri, nitakitimiza.+ Wokovu ni wa Yehova.”+

10 Baadaye Yehova akamwamuru huyo samaki, akamtapika Yona kwenye nchi kavu.+

3 Ndipo neno la Yehova likamjia Yona mara ya pili, na kusema:+ 2 “Ondoka, uende Ninawi lile jiji kubwa, ukalitangazie neno+ ninalokuambia.”

3 Basi Yona akasimama na kwenda Ninawi kulingana na neno la Yehova.+ Sasa Ninawi lilikuwa jiji kubwa kwa Mungu,+ lenye mwendo wa kutembea wa siku tatu. 4 Mwishowe Yona akaanza kuingia jijini mwendo wa kutembea wa siku moja, naye aliendelea kutangaza na kusema: “Bado siku 40 tu, na Ninawi litaangamizwa.”+

5 Nao watu wa Ninawi wakaanza kumwamini Mungu,+ ndipo wakatangaza kufunga na kuvaa nguo za magunia,+ kutoka aliye mkubwa zaidi kati yao mpaka aliye mdogo zaidi. 6 Neno hilo lilipomfikia mfalme wa Ninawi,+ ndipo akasimama kutoka kwenye kiti chake cha ufalme, akavua vazi lake rasmi na kujifunika nguo za magunia na kuketi katika majivu.+ 7 Zaidi ya hayo, akaagiza mwito utolewe, naye akaagiza utolewe katika Ninawi, kwa agizo la kisheria la mfalme na wakubwa wake, na kusema:

“Hakuna mwanadamu wala mnyama wa kufugwa, mifugo wala kundi, anayepaswa kuonja kitu chochote. Yeyote asile chakula. Hata maji wasinywe.+ 8 Nao wajifunike nguo za magunia, mwanadamu na mnyama wa kufugwa; na wamwite Mungu kwa nguvu na warudi,+ kila mmoja kutoka katika njia yake mbaya na kutoka katika jeuri iliyokuwa mikononi mwao. 9 Ni nani anayejua iwapo Mungu wa kweli hatageuka na kujuta+ na kuacha hasira yake inayowaka, tusije tukaangamia?”+

10 Naye Mungu wa kweli akaona matendo yao,+ kwamba walikuwa wamegeuka kutoka katika njia yao mbaya;+ naye Mungu wa kweli akajuta+ juu ya msiba ambao alikuwa amesema ataleta juu yao; naye hakuuleta.+

4 Hata hivyo, jambo hilo halikumpendeza+ Yona hata kidogo, naye akawaka hasira. 2 Kwa hiyo akasali kwa Yehova na kusema: “Ah, sasa, Ee Yehova, je, hili halikuwa hangaiko langu, nilipokuwa katika nchi yangu mwenyewe? Ndiyo sababu nilikimbia na kwenda Tarshishi;+ kwa maana nilijua kwamba wewe ni Mungu mwenye neema na rehema,+ si mwepesi wa hasira na ni mwingi wa fadhili zenye upendo,+ na mwenye kuujuta msiba.+ 3 Na sasa, Ee Yehova, tafadhali, iondoe nafsi yangu+ kutoka kwangu, kwa maana ni afadhali mimi nife kuliko niwe hai.”+

4 Naye Yehova akasema: “Je, umewaka hasira kwa haki?”+

5 Ndipo Yona akaenda nje ya jiji na kuketi upande wa mashariki wa jiji; mwishowe akajitengenezea kibanda hapo, ili apate kuketi chini yake katika kivuli+ mpaka aone litakalolipata jiji hilo.+ 6 Kwa hiyo Yehova Mungu akaweka mtango, kwamba uje juu ya Yona, uwe kivuli juu ya kichwa chake, ili kumwokoa kutoka katika hali yake ya taabu.+ Na Yona akaanza kushangilia sana juu ya mtango huo.

7 Lakini Mungu wa kweli akaweka mdudu+ wakati wa mapambazuko ya kesho yake, ili aushambulie mtango huo; mwishowe ukakauka.+ 8 Na ikawa kwamba, mara jua lilipoangaza, Mungu akaweka pia upepo wenye kukausha wa mashariki+ na jua likazidi kukichoma kichwa cha Yona, hivi kwamba akawa anazimia;+ akaendelea kuomba kwamba nafsi yake ife. Akasema kwa kurudia-rudia: “Afadhali mimi nife kuliko niwe hai.”+

9 Naye Mungu akamwambia Yona: “Je, ni kwa haki wewe kuwaka hasira juu ya mtango huo?”+

Ndipo akasema: “Ni kwa haki mimi kuwaka hasira, kiasi cha kufa.” 10 Lakini Yehova akasema: “Wewe, kwa upande wako, uliusikitikia mtango, ambao hukuufanyia kazi ya taabu wala kuukuza, ambao ulikuwa mmea tu ulioota usiku mmoja na kuangamia kama mmea tu ulioota usiku mmoja. 11 Na mimi, kwa upande wangu, je, sipaswi kusikitikia Ninawi lile jiji kubwa,+ ambalo lina wanadamu zaidi ya 120,000 wasiojua hata kidogo tofauti kati ya mkono wao wa kuume na wa kushoto, na tena wanyama wengi wa kufugwa?”+

[Maelezo ya Chini]

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki