Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bi12 Mika 1:1-7:20
  • Mika

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mika
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Mika

Mika

1 Neno la Yehova lililomjia Mika+ wa Moreshethi, katika siku za Yothamu,+ Ahazi,+ Hezekia,+ wafalme wa Yuda,+ ambalo aliona katika maono kuhusu Samaria+ na Yerusalemu:+

2 “Sikieni, enyi vikundi vya watu, ninyi nyote; kazeni uangalifu, Ee dunia na vyote vinavyokujaza,+ naye Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova na awe shahidi juu yenu,+ Yehova katika hekalu lake takatifu.+ 3 Maana, tazama! Yehova anatoka mahali pake,+ naye atashuka na kukanyaga mahali pa juu pa dunia.+ 4 Na milima itayeyuka chini yake,+ na nchi tambarare za chini zitapasuka, kama nta kwa sababu ya moto,+ kama maji yanayomwagwa kwenye mteremko mkali.

5 “Ni kwa sababu ya maasi ya Yakobo kwamba kuna hayo yote, kwa sababu ya dhambi za nyumba ya Israeli.+ Maasi ya Yakobo ni nini? Je, si Samaria?+ Ni mahali gani pa juu pa Yuda?+ Je, si Yerusalemu? 6 Nami nitalifanya Samaria kuwa rundo la mabomoko ya shambani,+ mahali pa kupanda mizabibu; nami nitamwaga mawe yake katika bonde, na misingi yake nitaifunua.+ 7 Na sanamu zake zote za kuchongwa zitavunjwa vipande-vipande,+ na zawadi zote alizopewa kuwa malipo yake zitateketezwa katika moto;+ na sanamu zake zote nitazifanya kuwa mahame yaliyo ukiwa. Maana alizikusanya kutoka kwa vitu vilivyotolewa kuwa malipo ya kahaba, nazo zitarudi zikiwa kitu kilichotolewa kuwa malipo ya kahaba.”+

8 Kwa sababu hiyo nitaomboleza na kupiga mayowe;+ nitatembea miguu wazi na uchi.+ Nitaomboleza kama mbwa-mwitu, na kuomboleza kama mbuni-jike. 9 Maana jeraha lililo juu yake haliwezi kupona;+ maana limefika mpaka Yuda,+ pigo hilo limefika mpaka lango la watu wangu, mpaka Yerusalemu.+

10 “Msiseme hili katika Gathi; msilie hata kidogo.+

“Katika nyumba ya Afra gaagaa mavumbini.+ 11 Vuka, Ee mwanamke mkaaji wa Shafiri, katika uchi wenye aibu.+ Mwanamke mkaaji wa Saanani hajaondoka. Maombolezo ya Beth-ezeli yatawaondolea ninyi mahali pake pa kusimama. 12 Maana mwanamke mkaaji wa Marothi amengojea mema,+ lakini mabaya yameshuka kutoka kwa Yehova mpaka kwenye lango la Yerusalemu.+ 13 Funga gari kwenye kikundi cha farasi, Ee mwanamke mkaaji wa Lakishi.+ Yeye alikuwa mwanzo wa dhambi kwa binti Sayuni,+ maana ndani yako maasi ya Israeli yamepatikana.+ 14 Kwa hiyo utampa Moresheth-gathi zawadi za kuaga.+ Nyumba za Akzibu+ zilikuwa kama kitu chenye udanganyifu kwa wafalme wa Israeli. 15 Bado nitakuletea mnyang’anyi,+ Ee mwanamke mkaaji wa Maresha.+ Utukufu wa Israeli utakuja mpaka Adulamu.+ 16 Fanya upara, unyoe nywele zako kwa sababu ya wana wa furaha yako tele.+ Panua upara wako kama ule wa tai, kwa sababu wameondoka kwako kwenda uhamishoni.”+

2 “Ole wao wanaopanga mambo yenye kudhuru, na wale wanaozoea kufanya lililo baya, vitandani mwao!+ Wao hulifanya kwenye nuru ya asubuhi,+ kwa sababu hilo liko katika uwezo wa mikono yao.+ 2 Nao wametamani mashamba na kuyanyakua;+ nyumba pia, nao wamezichukua; nao wamempunja mwanamume na nyumba yake,+ mtu na fungu lake la urithi.+

3 “Kwa hiyo Yehova amesema hivi, ‘Tazama, nakusudia msiba+ juu ya familia hii+ ambao hamtaziondoa shingo zenu+ ndani yake, ili msitembee kwa majivuno;+ kwa sababu ni wakati wa msiba.+ 4 Siku hiyo mtu atapaaza neno la kimethali+ kuwahusu ninyi naye ataomboleza, ndiyo, maombolezo.+ Mtu atasema: “Hakika tumeporwa!+ Anabadili fungu la watu wangu.+ Jinsi anavyoliondoa kwangu! Anawagawia wasio waaminifu mashamba yetu wenyewe.” 5 Kwa hiyo hutakuwa na yeyote anayetupa kamba, kwa kura,+ katika kutaniko la Yehova. 6 Ninyi msiache maneno yaanguke.+ Wanaacha maneno yaanguke. Hawataacha maneno yaanguke kuhusu mambo haya. Fedheha hazitaondoka.+

7 “ ‘Je, inasemwa, Ee nyumba ya Yakobo:+ “Roho ya Yehova imekosa kuridhika, au haya ndiyo matendo yake?”+ Je, maneno yangu mwenyewe hayafanyi mema+ kwa yeye anayetembea kwa unyoofu?+

8 “ ‘Na jana watu wangu mwenyewe walisimama kama adui mkaidi.+ Vueni pambo lenye utukufu kutoka mbele ya vazi, kutoka kwa wale wanaopita wakiwa na uhakika, kama wale wanaorudi kutoka vitani. 9 Mnawafukuza wanawake wa watu wangu kutoka katika nyumba ambamo mwanamke ana furaha tele. Mnachukua utukufu wangu+ kutoka kwa watoto wake, mpaka wakati usio na kipimo.+ 10 Ondoka uende,+ kwa sababu hapa si mahali pa kupumzika.+ Kwa sababu ya uhakika wa kwamba amekuwa asiye safi,+ kuna kuvunja-vunja; na kazi hiyo ya kuvunja-vunja ina maumivu.+ 11 Ikiwa mwanamume, anayetembea akifuata upepo na uwongo, amesema uwongo:+ “Nitakuangushia maneno kuhusu divai na kuhusu kileo,” yeye pia atakuwa yule anayewaangushia watu hawa maneno.+

12 “ ‘Hakika nitamkusanya Yakobo, ninyi nyote;+ bila shaka nitawakusanya pamoja wanaobaki wa Israeli.+ Nitawaunganisha, kama kundi zizini, kama kundi la wanyama katikati ya malisho yake;+ huko kutakuwa na kelele za wanadamu.’+

13 “Anayepenyeza atakuja mbele yao:+ watapenya. Nao watapita kati ya lango, nao watatoka nje kwa hilo.+ Na mfalme wao atapita kati mbele yao, Yehova akiwa mbele yao.”+

3 Nami nikasema: “Tafadhali sikieni, ninyi vichwa vya Yakobo na ninyi viongozi wa nyumba ya Israeli.+ Je, si wajibu wenu kujua haki?+ 2 Ninyi mnaochukia yaliyo mema+ na mnaopenda ubaya,+ mnaochuna ngozi kutoka kwa watu na nyama kutoka kwa mifupa yao;+ 3 ninyi ambao pia mmekula nyama ya watu wangu,+ na mmeichuna ngozi yao kutoka kwao, mkaivunja vipande-vipande mifupa yao, na kuiponda vipande-vipande kama kitu kilicho katika chungu chenye mdomo mpana na kama nyama ndani ya chungu cha kupikia.+ 4 Wakati huo watamwomba Yehova msaada, lakini hatawajibu.+ Naye atauficha uso wake kutoka kwao wakati huo,+ kulingana na walivyotenda ubaya kwa matendo yao.+

5 “Yehova amesema hivi juu ya manabii ambao wanawapoteza watu wangu,+ ambao wanauma kwa meno yao+ na ambao hupaaza sauti, ‘Amani!’+ ambao, mtu yeyote asipoweka kitu vinywani mwao, pia hutakasa vita juu yake,+ 6 ‘Basi ninyi mtakuwa na usiku,+ kusiweko maono;+ nanyi mtakuwa na giza, ili msifanye uaguzi. Nalo jua litatua juu ya manabii, na mchana utakuwa mweusi juu yao.+ 7 Waonaji+ wataona aibu,+ na waaguzi+ watakata tamaa. Nao wote watafunika masharubu,+ kwa maana hakuna jibu kutoka kwa Mungu.’ ”+

8 Nami nimejaa nguvu, kwa roho ya Yehova, na ya haki na uwezo,+ ili nimwambie Yakobo maasi yake na Israeli dhambi yake.+

9 Tafadhali sikieni hili, ninyi vichwa vya nyumba ya Yakobo nanyi viongozi wa nyumba ya Israeli,+ mnaochukia haki na mnaopotoa hata kila kitu ambacho kimenyooka;+ 10 mnaojenga Sayuni kwa matendo ya umwagaji wa damu na Yerusalemu kwa ukosefu wa uadilifu.+ 11 Walio vichwa vyake hutoa hukumu ili wale rushwa+ tu, na makuhani wake hufundisha ili tu wapate malipo,+ na manabii wake hufanya uaguzi ili tu wapate pesa;+ hata hivyo wao huendelea kujiegemeza kwa Yehova, wakisema: “Je, Yehova hayuko katikati yetu?+ Hakuna msiba utakaotupata.”+ 12 Basi kwa sababu yenu Sayuni utalimwa kama shamba, na Yerusalemu litakuwa marundo ya mabomoko,+ na mlima wa nyumba hiyo utakuwa kama mahali pa juu pa msitu.

4 Na itatukia katika siku za mwisho+ kwamba mlima+ wa nyumba+ ya Yehova utawekwa imara juu ya kilele cha milima, nao utainuliwa juu ya vilima;+ na vikundi vya watu vitamiminika huko.+ 2 Na mataifa mengi hakika yatakwenda na kusema: “Njooni,+ twendeni juu kwenye mlima wa Yehova na kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo;+ naye atatufundisha njia zake,+ nasi tutatembea katika mapito yake.”+ Kwa maana sheria itatoka katika Sayuni, na neno la Yehova katika Yerusalemu.+ 3 Naye hakika atafanya hukumu kati ya vikundi vingi vya watu,+ na kunyoosha mambo+ kuhusu mataifa yenye nguvu yaliyo mbali.+ Nao watafua panga zao ziwe majembe na mikuki yao iwe miundu.+ Hawatainua upanga, taifa juu ya taifa, wala hawatajifunza vita tena.+ 4 Nao wataketi, kila mtu chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake,+ wala hakutakuwa na mtu yeyote anayewatetemesha;+ kwa maana kinywa cha Yehova wa majeshi kimesema hivyo.+

5 Kwa maana vikundi vyote vya watu vitatembea kila kimoja katika jina la mungu wake;+ bali sisi tutatembea katika jina la Yehova Mungu wetu+ mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+

6 “Katika siku hiyo,” asema Yehova, “nitamkusanya yeye aliyekuwa akichechemea;+ naye aliyekuwa ametawanywa nitamkusanya pamoja,+ yeye ambaye nimemtendea vibaya. 7 Nami nitamfanya yeye aliyekuwa akichechemea awe mabaki,+ na yeye aliyekuwa ameondolewa mbali awe taifa lenye uwezo;+ na Yehova atatawala juu yao akiwa mfalme katika Mlima Sayuni, kutoka sasa na kuendelea mpaka wakati usio na kipimo.+

8 “Wewe nawe, Ee mnara wa kundi, kilima cha binti Sayuni,+ mpaka kwako itakuja, ndiyo, mamlaka ya kwanza itakuja hakika,+ ufalme wa binti Yerusalemu.+

9 “Basi ni kwa nini unaendelea kupiga kelele?+ Je, hamna mfalme ndani yako, au je, mshauri wako mwenyewe ameangamizwa, hata maumivu kama yale ya mwanamke anayezaa yakakushika?+ 10 Ee binti Sayuni, uwe na maumivu makali na utaabike, kama mwanamke anayezaa,+ maana sasa utaenda kutoka katika mji, nawe utakaa katika shamba.+ Nawe utaenda mpaka Babiloni.+ Huko utakombolewa.+ Huko Yehova atakununua kutoka mkononi mwa adui zako.+

11 “Na sasa mataifa mengi yatakusanywa juu yako, wale wanaosema, ‘Acheni atiwe uchafu, nayo macho yetu yautazame Sayuni.’+ 12 Lakini wao nao, hawajapata kujua fikira za Yehova, wala hawajapata kuelewa shauri lake;+ maana atawakusanya pamoja kwenye uwanja wa kupuria kama mafungu ya nafaka iliyokatwa hivi karibuni.+

13 “Simama upure, Ee binti Sayuni;+ maana nitaibadili pembe yako iwe chuma, na kwato zako nitazibadili ziwe shaba, nawe utaponda kabisa vikundi vingi vya watu;+ na kwa kupiga marufuku utamtolea Yehova faida yao isiyo ya haki,+ na mali zao kwa Bwana wa kweli wa dunia yote.”+

5 “Wakati huu unajikatakata,+ Ee binti uliyevamiwa; yeye ametuzingira sisi.+ Watalipiga kwa fimbo shavu la mwamuzi wa Israeli.+

2 “Nawe, Ee Bethlehemu Efratha,+ wewe uliye mdogo sana kuwa kati ya maelfu ya Yuda,+ kutoka kwako+ atanijia yeye atakayekuwa mtawala katika Israeli,+ ambaye asili yake ni kutoka nyakati za kale, kutoka siku za wakati usio na kipimo.+

3 “Kwa hiyo atawatoa+ mpaka wakati ambapo yeye anayezaa anapozaa.+ Na wale ndugu zake wengine watarudi kwa wana wa Israeli.

4 “Naye atasimama na kuchunga kwa nguvu za Yehova,+ katika ukuu wa jina la Yehova Mungu wake.+ Nao wataendelea kukaa,+ maana sasa atakuwa mkuu mpaka miisho ya dunia.+ 5 Na huyu atakuwa amani.+ Lakini wakati Mwashuru atakapokuja katika nchi yetu na kukanyaga juu ya minara yetu ya makao,+ sisi pia tutasimamisha juu yake wachungaji saba, ndiyo, watawala wadogo wanane kutoka kati ya wanadamu. 6 Nao wataichunga nchi ya Ashuru kwa upanga,+ na nchi ya Nimrodi+ katika malango yake. Naye atatukomboa kutoka kwa Mwashuru,+ anapokuja katika nchi yetu na anapokanyaga juu ya eneo letu.

7 “Na mabaki ya Yakobo+ watakuwa katikati ya makabila mengi ya watu kama umande kutoka kwa Yehova,+ kama manyunyu mengi ya mvua juu ya mimea,+ ambayo hayamtumaini mwanadamu wala kuwangojea wana wa mtu wa udongo.+ 8 Na mabaki ya Yakobo watakuwa kati ya mataifa, katikati ya makabila mengi ya watu, kama simba katikati ya wanyama wa msituni, kama mwana-simba mwenye manyoya shingoni katikati ya makundi ya kondoo, ambaye, anapopita kati, hukanyaga-kanyaga na pia hurarua vipande-vipande;+ wala hakuna mkombozi. 9 Mkono wako utainuliwa juu ya wapinzani wako,+ na adui zako wote watakatiliwa mbali.”+

10 “Na itatukia katika siku hiyo,” asema Yehova, “kwamba nitakatilia mbali farasi zako kutoka katikati yako na kuharibu magari yako.+ 11 Nami nitakatilia mbali majiji ya nchi yako na kubomoa mahali pako pote penye ngome.+ 12 Nami nitakatilia mbali ulozi kutoka mkononi mwako, nawe hutaendelea tena kuwa na watu wowote wanaofanya uchawi.+ 13 Nami nitakatilia mbali sanamu zako za kuchongwa na nguzo zako kutoka katikati yako, nawe hutainamia tena kazi ya mikono yako.+ 14 Nami nitang’oa miti yako mitakatifu+ kutoka katikati yako na kuangamiza majiji yako. 15 Na katika hasira na ghadhabu nitalipiza kisasi juu ya mataifa ambayo hayakutii.”+

6 Tafadhali, sikieni jambo ambalo Yehova anasema.+ Simameni, endesheni kesi na milima, vilima na visikie sauti yenu.+ 2 Sikieni, enyi milima, sikieni kesi ya Yehova, pia ninyi vyombo vya kudumu, ninyi misingi ya dunia;+ kwa maana Yehova ana kesi na watu wake, naye atahojiana na Israeli:+

3 “Enyi watu wangu,+ nimewafanya nini? Nami nimewachosha kwa njia gani?+ Toeni ushuhuda juu yangu.+ 4 Kwa maana niliwaleta ninyi kutoka nchi ya Misri,+ nami niliwakomboa kutoka nyumba ya watumwa;+ nami nikawatuma Musa, Haruni na Miriamu+ mbele yenu. 5 Tafadhali, enyi watu wangu, kumbukeni+ lile ambalo Balaki mfalme wa Moabu alishauri,+ na lile ambalo Balaamu mwana wa Beori alimjibu.+ Ilikuwa kutoka Shitimu+ mpaka Gilgali,+ kusudi matendo ya uadilifu ya Yehova yajulikane.”+

6 Nitamkaribia Yehova na nini?+ Nitajiinamisha na nini kwa Mungu aliye juu?+ Je, nimkaribie na matoleo mazima ya kuteketezwa,+ na ndama wenye umri wa mwaka mmoja? 7 Je, Yehova atapendezwa na maelfu ya kondoo-dume, na makumi ya maelfu ya mito ya mafuta?+ Je, nimtoe mwanangu mzaliwa wa kwanza kwa ajili ya maasi yangu, uzao wa tumbo langu kwa ajili ya dhambi ya nafsi yangu?+ 8 Ee mtu wa udongo, yeye amekuambia yaliyo mema.+ Na Yehova anataka nini kutoka kwako ila kutenda haki+ na kupenda fadhili+ na kuwa na kiasi+ katika kutembea na Mungu wako?+

9 Sauti ya Yehova inaliita jiji,+ naye mtu mwenye hekima inayotumika ataliogopa jina lako.+ Ninyi isikieni fimbo na yeye aliyeiweka.+ 10 Je, bado kuna hazina za uovu katika nyumba ya mwovu,+ na kipimo cha efa kilichobanwa ambacho kimeshutumiwa? 11 Je, naweza kuwa safi kiadili nikiwa na mizani ya uovu pamoja na mfuko wa mawe ya mizani ya udanganyifu?+ 12 Kwa maana watu wake mwenyewe walio matajiri wamejaa jeuri, na wakaaji wake mwenyewe wamesema uwongo,+ na ulimi wao una udanganyifu kinywani mwao.+

13 “Nami pia, nitakufanya mgonjwa kwa kukupiga;+ utafanywa ukiwa, kwa sababu ya dhambi zako.+ 14 Nawe utakula wala hutashiba, nawe utakuwa na njaa.+ Nawe utaondoa vitu, lakini hutavichukua na kuvipeleka salama; na chochote ambacho utachukua na kukipeleka salama, nitakitoa kwa upanga.+ 15 Nawe utapanda mbegu, bali hutavuna. Nawe utakanyaga zeituni, bali hutajipaka mafuta; pia divai tamu, bali hutakunywa divai.+ 16 Na sheria za Omri+ na kazi yote ya nyumba ya Ahabu zinafuatwa,+ nanyi mnatembea katika mashauri yao;+ ili mimi niwafanye ninyi kuwa kitu cha kushangaza na wakaaji wake kuwa kitu cha kupigiwa mluzi kwa mshangao;+ nanyi mtachukua shutuma ya vikundi vya watu.”+

7 Ole wangu,+ kwa maana nimekuwa kama mkusanyo wa matunda ya wakati wa kiangazi, kama masalio ya mkusanyo wa zabibu!+ Hakuna kishada cha zabibu za kula, hakuna tini ya mapema, ambayo nafsi yangu inaweza kutamani!+ 2 Mshikamanifu ameangamia kutoka duniani, na kati ya wanadamu hakuna mnyoofu.+ Wote huvizia ili kumwaga damu.+ Huwinda, kila mmoja ndugu yake mwenyewe, kwa wavu wa kukokota.+ 3 Mikono yao iko juu ya lililo baya, ili kulifanya vema;+ mkuu anaomba kitu, naye mwenye kuhukumu hufanya hivyo ili kupata thawabu,+ na mkubwa anasema tamaa iliyo katika nafsi yake mwenyewe;+ nao huisokota. 4 Mtu aliye bora zaidi kwao ni kama mchongoma, aliye mnyoofu zaidi kwao ni mbaya kuliko ukuta wa miiba.+ Siku ya walinzi wako, siku yenu ya kukaziwa fikira, itakuja.+ Sasa kuhangaishwa kwao kutatokea.+

5 Msimwamini mwenzi. Msimtegemee rafiki msiri.+ Linda milango ya kinywa chako kutokana na yeye anayelala kifuani pako.+ 6 Kwa maana mwana anamdharau baba, binti anasimama kumpinga mama yake;+ binti-mkwe kumpinga mama-mkwe wake;+ adui za mtu ni watu wa nyumba yake.+

7 Lakini mimi, nitaendelea kumtazamia Yehova.+ Nitaonyesha mtazamo wa kumngojea Mungu wa wokovu wangu.+ Mungu wangu atanisikia.+

8 Usishangilie juu yangu, Ee mwanamke adui yangu.+ Ijapokuwa nimeanguka, nitasimama;+ ijapokuwa ninakaa gizani,+ Yehova atakuwa nuru kwangu.+ 9 Ghadhabu ya Yehova nitaivumilia​—​kwa maana nimemtendea dhambi+​—​mpaka atakapoendesha kesi yangu na kutekeleza haki kwa ajili yangu.+ Atanileta kwenye nuru; nitautazama uadilifu wake.+ 10 Na adui yangu ataona, aibu itamfunika,+ yeye aliyekuwa akiniambia: “Yuko wapi, Yehova Mungu wako?”+ Macho yangu mwenyewe yatamtazama huyo mwanamke.+ Sasa atakuwa mahali pa kukanyaga-kanyaga, kama matope ya barabarani.+

11 Siku ya kujenga kuta zako za mawe, siku hiyo amri itakuwa mbali kabisa.+ 12 Siku hiyo watakujia hata kutoka Ashuru na majiji ya Misri, na kutoka Misri hata kufika ule Mto;+ na kutoka bahari mpaka bahari, na kutoka mlima mpaka ule mlima.+ 13 Na nchi itakuwa mahame yenye ukiwa kwa sababu ya wakaaji wake, kwa sababu ya matunda ya matendo yao.+

14 Wachunge watu wako kwa fimbo yako,+ kundi la urithi wako, yeye aliyekuwa akikaa peke yake msituni—katikati ya shamba la matunda.+ Na walishe katika Bashani na Gileadi+ kama katika siku za zamani.+

15 “Nitamwonyesha mambo ya ajabu kama katika zile siku ulipokuwa ukitoka nchi ya Misri.+ 16 Mataifa yataona na kuonea aibu uwezo wao wote.+ Wataweka mkono wao juu ya vinywa vyao;+ masikio yao yatakuwa na uziwi. 17 Wataramba mavumbi kama nyoka;+ kama watambaaji wa dunia watatoka katika maboma+ yao wakitetemeka. Watamjia Yehova Mungu wetu wakitetemeka, nao watakuogopa.”+

18 Ni nani aliye Mungu kama wewe,+ anayesamehe kosa na kuuachilia ukosaji+ wa mabaki ya urithi wake?+ Hatashikilia hasira yake milele, kwa maana yeye hupendezwa na fadhili zenye upendo.+ 19 Atatuonyesha rehema tena;+ atayatiisha makosa yetu.+ Nawe utazitupa dhambi zao zote+ katika vilindi vya bahari. 20 Utatoa ukweli aliopewa Yakobo, fadhili zenye upendo alizopewa Abrahamu, ambazo uliwaapia mababu zetu tangu siku za zamani za kale.+

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki