Nahumu
1 Tangazo juu ya Ninawi:+ Kitabu cha maono ya Nahumu Mwelkoshi:
2 Yehova ni Mungu anayetaka watu wajitoe kikamili+ na hulipiza kisasi; Yehova analipiza kisasi+ naye yuko tayari kuonyesha ghadhabu.+ Yehova anawalipiza kisasi wapinzani wake,+ naye ana kinyongo juu ya adui zake.+
3 Yehova si mwepesi wa hasira+ naye ni mkuu katika nguvu,+ wala hatasita kamwe kuadhibu.+
Njia yake imo katika upepo wenye kuharibu na katika dhoruba, na wingu kubwa ndilo mavumbi ya miguu yake.+
4 Anakemea bahari,+ naye huikausha; huikausha mito yote.+
Bashani na Karmeli zimekauka,+ na ua la Lebanoni limekauka.
5 Milima imetikisika kwa sababu yake, vilima navyo vikayeyuka.+
Dunia nayo itainuka kwa sababu ya uso wake; nchi yenye kuzaa pia, na wote wanaokaa ndani yake.+
6 Ni nani anayeweza kusimama mbele ya shutuma zake?+ Ni nani anayeweza kusimama mbele ya joto la hasira yake?+
Ghadhabu yake mwenyewe itamwagwa kama moto,+ nayo miamba itabomolewa kwa sababu yake.
7 Yehova ni mwema,+ yeye ni ngome+ katika siku ya taabu.+
Naye hutambua wale wanaotafuta kimbilio kwake.+
8 Ataangamiza kwa ukamili mahali pake kwa furiko linalopita,+ na giza litawafuata adui zake.+
9 Mtatunga nini juu ya Yehova?+ Yeye anasababisha maangamizi kamili.
Taabu haitazuka mara ya pili.+
10 Ijapokuwa wanasokotwa kama miiba+ nao wamelewa kama kwa pombe yao ya ngano,+ watamezwa kama majani yaliyokauka kabisa.+
11 Kwako atatoka yule anayetunga juu ya Yehova jambo lililo baya,+ akitoa shauri lisilofaa.+
12 Yehova amesema hivi: “Ijapokuwa walikuwa katika hali kamili na wengi walikuwa katika hali hiyo, hata katika hali hiyo watakatwa;+ na mmoja atapita kati. Nami nitakutesa, hivi kwamba nisikutese tena kamwe.+ 13 Na sasa nitaivunja nira yake itoke juu yako,+ na pingu zilizo juu yako nitazikata vipande viwili.+ 14 Basi Yehova ameamuru hivi juu yako, ‘Hakitapandwa chochote tena kamwe juu ya jina lako.+ Nitakatilia mbali sanamu ya kuchongwa na sanamu ya kuyeyushwa kutoka katika nyumba ya miungu yako.+ Nami nitakufanyia kaburi,+ kwa sababu huna maana.’
15 “Tazama! Milimani, miguu ya mtu anayeleta habari njema, anayetangaza amani.+ Ee Yuda, fanya sherehe zako.+ Timiza nadhiri zako;+ kwa sababu mtu yeyote asiyefaa kitu hatapita tena kamwe katikati yako.+ Hatakosa kukatiliwa mbali kabisa.”+
2 Yule anayetawanya amekuja mbele ya uso wako.+ Mahali penye ngome na palindwe. Ilinde njia. Vitie nguvu viuno. Itegemeze nguvu sana.+
2 Kwa maana Yehova atakusanya fahari ya Yakobo,+ kama fahari ya Israeli, kwa sababu wanaomaliza wamewamaliza.+ Na machipukizi yao wameyaharibu.+
3 Ngao ya wanaume wake wenye uwezo imetiwa rangi nyekundu; wanaume wake wenye nguvu wamevaa nguo za rangi nyekundu.+ Gari lake la vita ni moto wa vifaa vya chuma katika siku ya kujitayarisha kwake, na mikuki ya mberoshi+ imetikiswa. 4 Magari ya vita yanazidi kuendeshwa kiwazimu barabarani.+ Yanakimbia-kimbia katika viwanja vya watu wote. Kuonekana kwake ni kama mienge. Kama umeme+ yanakimbia-kimbia.
5 Atawakumbuka watu wake wenye fahari.+ Watajikwaa wanapotembea.+ Watafanya haraka kwenda kwenye ukuta wake, na kizuizi kitawekwa imara. 6 Milango ya mito itafunguliwa, nalo jumba la mfalme litayeyushwa. 7 Na imeamuliwa; amefunuliwa; atachukuliwa,+ na vijakazi wake wataomboleza, kama sauti ya njiwa,+ wakipiga-piga mioyo yao.+ 8 Ninawi naye, tangu siku ambazo amekuwako,+ alikuwa kama kidimbwi cha maji;+ lakini wanakimbia. “Simameni tuli! Simameni tuli!” Lakini hakuna anayegeuka.+
9 Poreni fedha; poreni dhahabu;+ kwa maana hakuna kikomo cha vitu vilivyopangwa. Kuna kiasi kikubwa cha namna zote za vyombo vyenye kutamanika.+
10 Utupu na uwazi, na jiji lililofanywa ukiwa!+ Na moyo unayeyuka,+ magoti yanatetemeka,+ maumivu makali yamo katika viuno vyote.+ Na nyuso zao wote zimekuwa na wasiwasi.+ 11 Liko wapi tundu la simba, na pango la wana-simba wenye manyoya shingoni, ambamo simba alitembea na kuingia,+ ambamo mlikuwamo mwana-simba, wala hakuna mtu yeyote aliyekuwa akiwatetemesha?+ 12 Simba alikuwa akirarua-rarua vipande vya kutosha kwa ajili ya watoto wake, naye alikuwa akinyonga kwa ajili ya simba-jike wake. Naye alijaza daima mawindo ndani ya matundu yake na mahali pake pa kujificha alipajaza wanyama walioraruliwa vipande-vipande.+
13 “Tazama! Mimi niko dhidi yako,” asema Yehova wa majeshi,+ “nami nitaliteketeza gari lake la vita katika moshi.+ Na upanga utawameza wana-simba wako wenye manyoya shingoni.+ Nami nitakatilia mbali mawindo yako kutoka duniani, wala haitasikika tena sauti ya wajumbe wako.”+
3 Ole wake jiji la umwagaji wa damu.+ Limejaa udanganyifu na unyang’anyi. Mawindo hayaondoki! 2 Kuna sauti ya mjeledi+ na sauti ya mgongano wa gurudumu, na farasi anayetimua mbio na gari linalorukaruka.+ 3 Mpanda-farasi, na kumetameta kwa upanga, na kumetameta kwa mkuki,+ na watu wengi waliouawa, na rundo kubwa la mizoga; wala hakuna mwisho wa maiti. Wanaendelea kujikwaa kati ya maiti zao; 4 kwa sababu ya wingi wa matendo ya ukahaba ya yule kahaba,+ mwenye kupendeza kwa uvutio, mwanamke stadi wa ulozi, yeye anayeyanasa mataifa kwa matendo yake ya ukahaba na kuzinasa familia kwa ulozi wake.+
5 “Tazama! Mimi niko dhidi yako,”+ asema Yehova wa majeshi, “nami nitaweka upindo wa marinda yako juu ya uso wako, nami nitayafanya mataifa yauone uchi wako,+ na falme aibu yako. 6 Nami nitakutupia machukizo,+ nitakufanya udharaulike; nami nitakuweka uwe tamasha.+ 7 Ndipo itakuwa kwamba kila mtu anayekuona atakukimbia+ naye atasema, ‘Ninawi ameporwa! Ni nani atakayemsikitikia?’ Nitakutafutia wapi wafariji? 8 Je, wewe ni bora kuliko No-amoni,+ aliyekuwa akiketi kando ya mifereji ya Nile?+ Maji yalimzunguka kotekote, mali yake ilikuwa bahari, ukuta wake ulikuwa bahari. 9 Ethiopia na Misri+ pia walikuwa nguvu zake kamili; nazo hazikuwa na kikomo. Waputu na Walibya nao walikuwa msaada kwako.+ 10 Yeye, pia, alikusudiwa uhamisho; alienda utekwani.+ Watoto wake mwenyewe pia wakavunjwa vipande-vipande mbele ya barabara zote.+ Wakapiga kura+ juu ya watu wake waliotukuzwa, na wakuu wake wote wamefungwa kwa pingu.+
11 “Wewe mwenyewe utalewa pia;+ utakuwa kitu kilichofichika.+ Wewe mwenyewe pia utatafuta ngome ya kujikinga kutoka kwa adui.+ 12 Mahali pako pote penye ngome ni kama mitini iliyo na matunda ya kwanza yaliyoiva, ambayo, ikitikiswa-tikiswa, yataanguka katika kinywa cha mwenye kula.+
13 “Tazama! Watu wako ni wanawake katikati yako.+ Bila shaka malango ya nchi yako yatafunguliwa adui zako. Moto utateketeza mapingo yako.+ 14 Jitekee maji kwa ajili ya kuzingirwa.+ Tia nguvu mahali pako penye ngome.+ Ingia matopeni, kanyaga-kanyaga udongoni; kamata kalibu ya matofali. 15 Hata huko utateketezwa na moto. Upanga utakukatilia mbali.+ Nawe utaliwa na upanga kama nzige+ wachanga wanavyokula. Jifanye kuwa hesabu kubwa kama nzige wachanga; jifanye kuwa hesabu kubwa kama nzige. 16 Umezidisha wafanya-biashara wako kuliko nyota za mbinguni.+
“Nzige mchanga naye, huvua ngozi yake; kisha huruka mbali. 17 Walinzi wako ni kama nzige, na maofisa wako wa uandikishaji ni kama kundi la nzige. Wanapiga kambi katika mazizi ya mawe siku yenye baridi. Lazima jua liangaze, nao huruka mbali; na mahali pao hapajulikani.+
18 “Wachungaji wako wamesinzia,+ Ee mfalme wa Ashuru; wenye fahari wako wanakaa katika makao yao.+ Watu wako wametawanywa juu ya milima, wala hakuna anayewakusanya pamoja.+ 19 Hakuna kitulizo cha msiba wako. Pigo lako haliponyeki.+ Wote wanaosikia habari juu yako wewe watakupigia makofi;+ kwa sababu ni nani ambaye ubaya wako haukupita daima juu yake?”+