Habakuki
1 Tangazo ambalo Habakuki nabii aliona katika maono: 2 Ee Yehova, nililie msaada mpaka wakati gani, nawe usisikie?+ Nitakuomba msaada kutokana na jeuri mpaka wakati gani, nawe usiokoe?+ 3 Kwa nini unanionyesha jambo lenye kudhuru, nawe unaendelea kutazama taabu tupu? Na kwa nini kuna uporaji na jeuri mbele yangu, kwa nini kugombana hutokea, kwa nini mzozo huendelezwa?+
4 Basi sheria hufa ganzi, na haki haitendeki kamwe.+ Kwa kuwa mwovu anamzingira mwadilifu, kwa sababu hiyo haki hupotoshwa.+
5 “Oneni, kati ya mataifa, tazameni, mkaangaliane kwa mshangao.+ Shangaeni; kwa maana kuna utendaji ambao mtu anaufanya katika siku zenu, ambao hamtaamini ijapokuwa unasimuliwa.+ 6 Kwa maana, tazama, ninawasimamisha Wakaldayo,+ taifa lenye uchungu na lenye haraka, linaloenda kote duniani ili kumiliki makao yasiyo yake.+ 7 Taifa hilo ni lenye kutisha na lenye kuogopesha. Haki na utukufu wake hutoka ndani yake.+ 8 Na farasi zake ni wepesi kuliko chui, nao ni wakali kuliko mbwa-mwitu wa jioni.+ Na farasi zake wa vita wamekanyaga udongo, na hao farasi zake huja kutoka mbali. Linaruka kama tai anayeharakisha kwenda kula kitu.+ 9 Lote huja ili kufanya jeuri tupu.+ Kukusanywa kwa nyuso zao ni kama upepo wa mashariki,+ nalo linakusanya mateka kama vile mchanga. 10 Nalo linawadhihaki wafalme, nalo linawacheka maofisa wakuu.+ Hata kila mahali penye ngome linapacheka,+ nalo linarundika mavumbi na kupateka. 11 Wakati huo litasonga mbele kama upepo, litapita kati na kuwa na hatia.+ Nguvu zake zinatokana na mungu wake.”+
12 Je, wewe si wa tangu zamani za kale, Ee Yehova?+ Ee Mungu wangu, Mtakatifu wangu, wewe hufi.+ Ee Yehova, umeliweka kwa ajili ya hukumu; na kwa ajili ya kukaripia+ umeliwekea msingi, Ee Mwamba.+
13 Wewe umetakata sana usiweze kuona lililo baya; nawe huwezi kuitazama taabu.+ Kwa nini unawatazama wale wanaotenda kwa hila,+ na kukaa kimya wakati mtu mwovu anapommeza mtu aliye mwadilifu kuliko yeye?+ 14 Na kwa nini unamfanya mtu wa udongo kuwa kama samaki wa baharini, kama vitu vinavyotambaa ambavyo havina mtawala?+ 15 Hao wote amewainua kwa ndoano tu;+ huwakokota katika wavu wake,+ naye huwakusanya katika wavu wake wa kuvulia. Hiyo ndiyo sababu anafurahi na kuwa na shangwe.+ 16 Ndiyo sababu yeye huutolea dhabihu wavu wake wa kukokota na kuufukizia wavu wake wa kuvulia moshi wa dhabihu; kwa maana kwa vitu hivyo fungu lake limetiwa mafuta ya kutosha, na chakula chake ni chenye afya.+ 17 Je, hiyo ndiyo sababu atamwaga vyote vilivyomo katika wavu wake wa kukokota, na je, anapaswa kuyaua mataifa daima, bila kuonyesha huruma?+
2 Nitaendelea kusimama katika kituo changu cha ulinzi,+ nitaendelea kusimama juu ya boma; nitaendelea kuangalia,+ ili kuona atakaloniambia+ na lile nitakalojibu nikikaripiwa.+
2 Yehova naye akanijibu na kusema: “Andika maono hayo, na kuyaweka waziwazi kwenye mabamba,+ ili anayeyasoma kwa sauti aweze kufanya hivyo kwa wepesi.+ 3 Kwa maana maono hayo bado ni ya wakati uliowekwa,+ nayo yanafanya haraka kuelekea mwisho, wala hayatasema uwongo. Hata yakikawia, endelea kuyatarajia; kwa maana bila shaka yatatimia.+ Hayatachelewa.
4 “Tazama! Nafsi yake imejivuna;+ haikuwa nyoofu ndani yake. Lakini mwadilifu, ataendelea kuishi kwa uaminifu wake.+ 5 Na, kwa kweli, kwa sababu divai inatenda kwa hila,+ mwanamume anajidai;+ naye hatafikia mradi wake,+ yeye ambaye ameifanya nafsi yake iwe na nafasi kubwa kama Kaburi,* na aliye kama kifo, asiyeweza kutoshelezwa.+ Naye huendelea kujikusanyia kwake mataifa yote na kujikusanyia kwake vikundi vyote vya watu.+ 6 Je, hawa wote hawatamtungia neno la kimethali+ na maelezo ya kudokeza, mafumbo juu yake? Na mtu atasema, “ ‘Ole wake anayezidisha kisicho chake+—Ee mpaka wakati gani!+—na yule anayefanya deni lake mwenyewe liwe zito! 7 Je, wale wanaodai faida kwako hawatasimama ghafula, na wale wanaokutikisa kwa jeuri waamke, nawe uwe kwao kitu cha kunyakuliwa?+ 8 Kwa sababu wewe mwenyewe uliyapora mataifa mengi, mabaki yote ya vikundi vya watu watakupora,+ kwa sababu ya kumwaga damu ya wanadamu na kwa sababu ya dunia kufanyiwa jeuri, mji na wale wote wanaokaa ndani yake.+
9 “ ‘Ole wake anayeipatia nyumba yake faida ya uovu,+ ili kukiweka kiota chake kileleni, ili kukombolewa kutoka mkononi mwa jambo lenye msiba!+ 10 Umeshauri jambo la aibu kwa nyumba yako, kukatiliwa mbali kwa vikundi vingi vya watu;+ na nafsi yako inafanya dhambi.+ 11 Kwa maana jiwe litalia kwa huzuni kutoka ukutani, na boriti litalijibu kutoka kati ya mbao za paa.+
12 “ ‘Ole wake anayejenga jiji kwa umwagaji wa damu, anayesimamisha imara mji kwa ukosefu wa uadilifu!+ 13 Tazama! Je, si kutoka kwa Yehova wa majeshi kwamba vikundi vya watu vitaendelea kufanya kazi ya taabu kwa ajili ya moto tu, na kwamba vikundi vya mataifa vitajichosha bure tu?+ 14 Kwa maana dunia itajawa na kuujua utukufu wa Yehova kama maji yanavyoifunika bahari.+
15 “ ‘Ole wake anayewapa wenzake kinywaji, akikishikamanisha na ghadhabu na hasira yako, ili kuwalewesha,+ kwa kusudi la kuzitazama sehemu zao za aibu.+ 16 Utashibishwa kwa aibu badala ya utukufu.+ Kunywa pia, wewe mwenyewe,+ ukaonwe kuwa mtu ambaye hajatahiriwa.+ Kikombe cha mkono wa kuume wa Yehova kitakufikia,+ na kutakuwako fedheha juu ya utukufu wako; 17 kwa sababu jeuri iliyofanywa juu ya Lebanoni+ ndiyo itakayokufunika, na tamaa juu ya wanyama wanaowaogopesha, kwa sababu ya kumwaga damu ya wanadamu na jeuri iliyofanyiwa dunia,+ ule mji na wale wote wanaokaa ndani yake.+ 18 Sanamu ya kuchongwa imekuwa na faida gani,+ wakati yeye aliyeifanya ameichonga, sanamu ya kuyeyushwa, na mfundishaji wa uwongo?+ wakati yeye aliyefanya umbo lake ameitegemea,+ kufikia hatua ya kufanya miungu isiyo na thamani ambayo haiwezi kusema?+
19 “ ‘Ole wake anayekiambia kipande cha mti: “Ee amka!” anayeliambia jiwe lisiloweza kusema: “Ee amka! Hizo zenyewe zitafundisha”!+ Tazama! Zimefunikwa kwa dhahabu na fedha,+ wala hamna pumzi yoyote katikati yake.+ 20 Lakini Yehova yumo katika hekalu lake takatifu.+ Kaa kimya mbele zake, dunia yote!’ ”+
3 Sala ya Habakuki nabii katika nyimbo za huzuni: 2 Ee Yehova, nimeisikia habari juu yako.+ Nimeogopa utendaji wako,+ Ee Yehova.
Ufanye hai utendaji wako katikati ya ile miaka! Ufanye ujulikane katikati ya ile miaka. Wakati wa msukosuko, ukumbuke kuonyesha rehema.+
3 Mungu mwenyewe alikuja kutoka Temani, Mtakatifu kutoka Mlima Parani.+ Sela.+
Utukufu wake ulizifunika mbingu;+ na dunia ikajazwa sifa yake.+
4 Nao uangavu wake, ukawa kama vile nuru.+ Alikuwa na miale miwili ikitoka mkononi mwake, na hapo ndipo palipofichwa nguvu zake.+
5 Tauni ikaenda mbele zake,+ na homa kali ilikuwa ikitoka miguuni pake.+
6 Alisimama tuli, apate kuitikisa dunia.+ Aliona, kisha akayarusha mataifa.+
Na milima ya milele ikavunjwa;+ vilima vinavyodumu kwa wakati usio na kipimo vikainama.+ Miendo ya zamani za kale ni yake.
7 Chini ya kitu chenye kudhuru niliona mahema ya Kushani. Vitambaa vya mahema ya nchi ya Midiani+ vikaanza kufadhaika.+
8 Je, ni juu ya mito, Ee Yehova, je, hasira yako imewaka juu ya mito,+ au je, ghadhabu yako iko juu ya bahari?+ Kwa maana ulipanda farasi zako;+ magari yako yalikuwa wokovu.+
9 Katika uchi wake upinde wako hufunuliwa.+ Viapo rasmi vya makabila ndivyo jambo lililosemwa.+ Sela. Ukaipasua dunia kwa mito.+
10 Milima ilikuona; ikawa katika maumivu makali.+ Dhoruba ya maji yenye mngurumo ikapita kati. Kilindi cha maji kikatoa mvumo wake.+ Kikainua mikono yake juu.
11 Jua—mwezi—vilisimama tuli,+ kwenye makao yaliyo juu sana.+ Kama nuru mishale yako mwenyewe ikaenda mfululizo.+ Mng’ao wa mkuki wako ukaangaza.+
12 Kwa shutuma ulipiga mwendo kati ya dunia. Kwa hasira ukayapura mataifa.+
13 Ukajitokeza kwa ajili ya wokovu wa watu wako,+ upate kumwokoa mtiwa-mafuta wako. Ulimvunja vipande-vipande aliye kichwa kutoka kwa nyumba ya mwovu.+ Msingi uliwekwa wazi, mpaka shingoni.+ Sela.
14 Kwa fimbo zake mwenyewe ulikichoma+ kichwa cha mashujaa wake wa vita waliposonga kama tufani ili kunitawanya.+ Upeo wao wa raha ulikuwa kama wa wale wanaokusudia kummeza mwenye kuteseka katika maficho.+
15 Kupitia bahari ulikanyaga kwa farasi zako, kupitia mkusanyo wa maji mengi.+
16 Nilisikia, tumbo langu likaanza kutetemeka; midomo yangu ilitetemeka kwa sababu ya ule mvumo; kuoza kukaanza kuingia katika mifupa yangu;+ na katika hali yangu nikafadhaika, kwamba ningojee kimya siku ya taabu,+ kuja kwake kwa watu,+ apate kuwavamia.
17 Ijapokuwa huenda mtini usichanue,+ kusiwe na mazao kwenye mizabibu; kazi ya mzeituni ikashindwa, matuta yasizae chakula chochote.+ Huenda kundi liondolewe zizini, na kusiwe na mifugo katika mazizi;+
18 Lakini mimi, nitafurahi katika Yehova mwenyewe;+ nitakuwa na shangwe katika Mungu wa wokovu wangu.+
19 Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu ndiye nguvu zangu;+ naye ataifanya miguu yangu kama ile ya paa,+ na mahali pangu pa juu atanitembeza.+
Kwa kiongozi wa
vinanda vyangu.
[Maelezo ya Chini]
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.