Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bi12 Sefania 1:1-3:20
  • Sefania

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sefania
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Sefania

Sefania

1 Neno la Yehova lililomjia Sefania mwana wa Kushi mwana wa Gedalia mwana wa Amaria mwana wa Hezekia katika siku za Yosia+ mwana wa Amoni+ mfalme wa Yuda:

2 “Bila shaka nitakimaliza kila kitu kutoka katika uso wa nchi,” asema Yehova.+

3 “Nitammaliza kabisa mtu wa udongo na mnyama.+ Nitamaliza kiumbe kinachoruka cha mbinguni na samaki wa baharini,+ na vikwazo pamoja na waovu;+ nami nitamkatilia mbali mwanadamu kutoka katika uso wa nchi,”+ asema Yehova. 4 “Nami nitaunyoosha mkono wangu juu ya Yuda na wakaaji wote wa Yerusalemu,+ nami nitakatilia mbali mabaki ya Baali kutoka mahali hapa,+ jina la makuhani wa miungu ya kigeni pamoja na makuhani,+ 5 na wale wanaoliinamia jeshi la mbinguni+ juu ya madari, na wale wanaoinama,+ wakifanya viapo rasmi kwa Yehova+ na kufanya viapo rasmi kupitia kwa Malkamu;+ 6 na wale wanaorudi nyuma wasimfuate Yehova,+ ambao hawakumtafuta Yehova wala kuuliza habari kutoka kwake.”+

7 Kaa kimya mbele za Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova;+ kwa maana siku ya Yehova iko karibu,+ kwa maana Yehova ametayarisha dhabihu;+ amewatakasa+ watu wake walioalikwa.

8 “Na itatukia katika siku ya dhabihu ya Yehova kwamba nitakaza fikira kwa wakuu, na wana wa mfalme,+ na wale wote wanaovaa mavazi ya kigeni.+ 9 Nami nitakaza fikira kwa kila mtu anayepanda jukwaani siku hiyo, wale wanaojaza nyumba ya mabwana zao jeuri na udanganyifu.+ 10 Na kutatokea siku hiyo,” asema Yehova, “sauti ya kilio kutoka katika Lango la Samaki,+ na mayowe kutoka eneo la pili,+ na mshindo mkubwa kutoka vilimani.+ 11 Pigeni mayowe,+ ninyi wakaaji wa Makteshi, kwa maana watu wote walio wafanya-biashara wamenyamazishwa;+ wale wote wanaopima fedha wamekatiliwa mbali.

12 “Na itatukia wakati huo kwamba nitapekua Yerusalemu kwa uangalifu kwa kutumia taa,+ nami nitakaza fikira kwa watu wanaoganda juu ya machicha yao,+ wanaosema moyoni mwao, ‘Yehova hatatenda mema, wala hatatenda mabaya.’+ 13 Na mali yao itakuwa ya kunyakuliwa na nyumba zao zitakuwa mahame yenye ukiwa.+ Nao watajenga nyumba, lakini hawatakaa humo;+ nao watapanda mashamba ya mizabibu, lakini hawatakunywa divai yake.+

14 “Ile siku kuu+ ya Yehova iko karibu.+ Iko karibu, nayo inaharakisha sana.+ Sauti ya siku ya Yehova ni chungu.+ Hapo mwanamume mwenye nguvu anatoa kilio.+ 15 Siku hiyo ni siku ya ghadhabu, siku ya taabu na ya maumivu makali,+ siku ya dhoruba na ya ukiwa, siku ya giza na ya weusi,+ siku ya mawingu na ya weusi mzito, 16 siku ya baragumu na ya king’ora,+ juu ya majiji yenye ngome na juu ya minara mirefu ya pembeni.+ 17 Nami nitawataabisha wanadamu, nao watatembea kama vipofu;+ kwa sababu wamemtendea Yehova dhambi.+ Na damu yao itamwagwa kama mavumbi,+ na matumbo yao kama mavi.+ 18 Fedha yao wala dhahabu yao hazitaweza kuwakomboa katika siku ya ghadhabu ya Yehova;+ bali dunia yote itateketezwa kwa moto wa bidii yake,+ kwa sababu atafanya maangamizi, yenye kutisha kwelikweli, ya wakaaji wote wa dunia.”+

2 Jikusanyeni pamoja, ndiyo, jikusanyeni,+ Ee taifa lisiloona aibu.+ 2 Kabla sheria haijazaa kitu chochote,+ kabla siku hiyo haijapita kama makapi, kabla haijawajilia hasira inayowaka ya Yehova,+ kabla haijawajilia siku ya hasira ya Yehova,+ 3 mtafuteni Yehova,+ ninyi nyote mlio wapole wa dunia,+ ambao mmetenda uamuzi Wake wa hukumu. Utafuteni uadilifu,+ utafuteni upole.+ Huenda+ mkafichwa katika siku ya hasira ya Yehova.+ 4 Maana Gaza litakuwa jiji lililoachwa;+ na Ashkeloni litakuwa mahame yenye ukiwa.+ Nalo Ashdodi,+ watalifukuza katikati ya mchana;+ Ekroni nalo litang’olewa.+

5 “Ole wao wanaokaa katika eneo la bahari, taifa la Wakerethi!+ Neno la Yehova liko kinyume chenu. Ee Kanaani, nchi ya Wafilisti, nitakuangamiza wewe pia, hivi kwamba hakutakuwa na mkaaji.+ 6 Na eneo la bahari litakuwa viwanja vya malisho,+ vyenye visima kwa ajili ya wachungaji na mazizi ya mawe kwa ajili ya kondoo. 7 Nalo litakuwa eneo la mabaki ya nyumba ya Yuda.+ Humo watalisha. Katika nyumba za Ashkeloni, wakati wa jioni, watalala wakiwa wamejinyoosha. Kwa maana Yehova Mungu wao atawakazia fikira zake,+ akusanye na kurudisha walio mateka kati yao.”+

8 “Nimesikia shutuma za Moabu+ na maneno mabaya ya wana wa Amoni,+ ambayo wametumia kuwashutumu watu wangu na kuendelea kujivuna sana juu ya eneo lao. 9 Kwa hiyo, kama ninavyoishi,”+ asema Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, “Moabu atakuwa tu kama Sodoma,+ na wana wa Amoni+ kama Gomora, mahali penye upupu, na shimo la chumvi, na mahame yenye ukiwa, mpaka wakati usio na kipimo.+ Mabaki ya watu wangu watawapora, na mabaki ya taifa langu mwenyewe watawamiliki.+ 10 Haya ndiyo watakayopata badala ya kiburi chao,+ kwa sababu walishutumu na kuendelea kujivuna sana juu ya watu wa Yehova wa majeshi.+ 11 Yehova atakuwa mwenye kuogopesha juu yao;+ kwa maana ataikondesha miungu yote ya dunia,+ na watu watamwinamia,+ kila mmoja kutoka mahali pake, visiwa vyote vya mataifa.+

12 “Ninyi pia, Waethiopia,+ mtakuwa watu waliouawa kwa upanga wangu.+

13 “Naye atanyoosha mkono wake kuelekea kaskazini, naye ataangamiza Ashuru.+ Naye atafanya Ninawi kuwa mahame yenye ukiwa,+ eneo lisilo na maji kama nyika. 14 Na katikati yake, makundi yatalala yakiwa yamejinyoosha, wanyama-mwitu wote wa taifa.+ Mwari na nungunungu+ watakaa usiku kucha palepale kati ya kombe zake za nguzo.+ Sauti itakuwa inaimba dirishani. Kutakuwa na uharibifu kizingitini; kwa maana atafunua mbao za ukutani.+ 15 Hilo ndilo jiji lenye furaha lililokuwa likikaa kwa usalama,+ ambalo lilikuwa linasema moyoni mwake, ‘Mimi ndiye, wala hakuna mwingine yeyote.’+ Lo! Jinsi amekuwa kitu cha kushangaza, mahali pa wanyama-mwitu kulala wakiwa wamejinyoosha! Kila mtu anayepita kando yake atapiga mluzi; atatikisa mkono wake.”+

3 Ole wake anayeasi na kujitia unajisi, jiji lenye kukandamiza!+ 2 Hakusikiliza sauti+ wala kukubali nidhamu.+ Hakumtegemea Yehova.+ Hakumkaribia Mungu wake.+ 3 Wakuu wake katikati yake walikuwa simba wanaonguruma.+ Waamuzi wake walikuwa mbwa-mwitu wa jioni ambao hawakutafuna mifupa mpaka asubuhi.+ 4 Manabii wake walikuwa na dharau, walikuwa watu wenye hila.+ Makuhani wake wamekitia unajisi kilicho kitakatifu; waliitendea sheria jeuri.+ 5 Yehova alikuwa mwadilifu katikati yake;+ hakuwa akifanya ukosefu wowote wa uadilifu.+ Asubuhi baada ya asubuhi aliendelea kutoa uamuzi wake wa hukumu.+ Wakati wa mapambazuko haukukosekana.+ Lakini asiye mwadilifu hakujua aibu yoyote.+

6 “Niliyakatilia mbali mataifa; minara yao ya pembeni ilifanywa ukiwa. Niliziharibu barabara zao, hivi kwamba hakuna yeyote aliyekuwa akipita kati. Majiji yao yalifanywa ukiwa, hivi kwamba hakukuwa na mtu yeyote wala mkaaji yeyote.+ 7 Nikasema, ‘Hakika utaniogopa; utakubali nidhamu’;+ ili makao yake yasikatiliwe mbali+—nitamtaka atoe jibu kwa ajili ya dhambi zake zote.+ Kweli waliharakisha kufanya matendo yao yote yawe yenye uharibifu.+

8 “ ‘Kwa hiyo endeleeni kunitarajia,’+ asema Yehova, ‘mpaka siku nitakaposimama kwenda kuteka nyara,+ kwa maana uamuzi wangu wa hukumu ni kukusanya mataifa,+ nizikusanye falme pamoja, ili nizimwagie shutuma yangu,+ hasira yangu yote yenye kuwaka; kwa maana dunia yote itateketezwa kwa moto wa bidii yangu.+ 9 Kwa maana ndipo nitakapobadilisha lugha ya vikundi vya watu na kuwapa lugha safi,+ ili wote waliitie jina la Yehova,+ wamtumikie bega kwa bega.’+

10 “Kutoka eneo la mito ya Ethiopia, wale wanaonisihi, yaani, binti ya watu wangu waliotawanywa, wataniletea zawadi.+ 11 Siku hiyo hutaona aibu kwa sababu ya matendo yako yote uliyonikosea,+ kwa maana wakati huo nitaondoa katikati yako watu wako wanaofurahi kwa majivuno;+ nawe hutajivuna tena kamwe katika mlima wangu mtakatifu.+ 12 Nami nitaacha wabaki katikati yako watu wanyenyekevu na wa hali ya chini,+ nao watapata kimbilio katika jina la Yehova.+ 13 Na kuhusu mabaki ya Israeli,+ hawatafanya ukosefu wowote wa uadilifu,+ wala kusema uwongo,+ wala hautapatikana kinywani mwao ulimi wenye ujanja;+ kwa maana wao wenyewe watajilisha na kulala wakiwa wamejinyoosha,+ wala hakutakuwa na mtu yeyote anayewatetemesha.”+

14 Paaza kilio kwa shangwe, Ee binti Sayuni! Piga vigelegele,+ Ee Israeli! Shangilia na kufurahia kwa moyo wote, Ee binti Yerusalemu!+ 15 Yehova ameziondoa hukumu juu yako.+ Amemgeuzia mbali adui yako.+ Mfalme wa Israeli, Yehova, yupo katikati yako.+ Hutaogopa msiba tena.+ 16 Siku hiyo Yerusalemu litaambiwa: “Usiogope, Ee Sayuni.+ Mikono yako isilegee.+ 17 Yehova Mungu wako yupo katikati yako. Kama Mwenye nguvu, ataokoa.+ Atakufurahia kwa shangwe.+ Atanyamaza katika upendo wake. Atakushangilia kwa vilio vya furaha.

18 “Wale waliopatwa na huzuni+ kwa kutokuwapo kwenye majira yako ya sherehe nitawakusanya pamoja;+ nao hawakuwapo kwako, kwa sababu ya kuchukua shutuma kwa ajili yake.+ 19 Tazama, ninachukua hatua juu ya wote wanaokutesa, wakati huo;+ nami nitamwokoa yeye anayechechemea,+ na yeye ambaye ametawanywa nitamkusanya pamoja.+ Nami nitawaweka kuwa sifa na kuwa jina katika nchi yote ya aibu yao. 20 Wakati huo nitawaleta ndani ninyi, hata wakati wangu wa kuwakusanya ninyi pamoja. Kwa maana nitawafanya ninyi kuwa jina na sifa kati ya vikundi vyote vya watu wa dunia, ninapowakusanya ili kuwarudisha mateka wenu mbele ya macho yenu,” Yehova amesema.+

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki