Hagai
1 Katika mwaka wa pili wa mfalme Dario,+ mwezi wa sita, siku ya kwanza ya mwezi huo, neno la Yehova lilikuja kupitia nabii Hagai+ kwa ajili ya Zerubabeli+ mwana wa Shealtieli,+ gavana wa Yuda,+ na kwa ajili ya Yoshua+ mwana wa Yehosadaki+ kuhani mkuu, na kusema:
2 “Hivi ndivyo Yehova wa majeshi+ amesema, ‘Kikundi hiki cha watu, kimesema: “Wakati haujaja, wakati wa kujengwa kwa nyumba ya Yehova.” ’ ”+
3 Nalo neno la Yehova likaendelea kuja kupitia nabii Hagai, likisema: 4 “Je, huu ni wakati wa ninyi kukaa katika nyumba zenu zilizofunikwa kwa mbao,+ huku nyumba hii ikiwa imeharibika?+ 5 Na sasa, hivi ndivyo Yehova wa majeshi amesema, ‘Wekeni moyo wenu juu ya njia zenu.+ 6 Mmepanda mbegu nyingi, lakini mavuno ni kidogo.+ Mnakula chakula, lakini hamshibi.+ Mnakunywa, lakini hamlewi. Mnavaa nguo, lakini hakuna yeyote anayepata joto; na yeye anayeajiriwa, anaajiriwa kwa ajili ya mfuko wenye matundu.’ ”+
7 “Yehova wa majeshi amesema hivi, ‘Wekeni moyo wenu juu ya njia zenu.’+
8 “Pandeni mlimani, mkalete miti.+ Jengeni nyumba hii,+ nipate kuifurahia+ na nipate kutukuzwa,’+ asema Yehova.”
9 “ ‘Mlitafuta vitu vingi, lakini tazama kulikuwa na vichache tu;+ nanyi mmevileta ndani ya nyumba, nami nikavipeperusha+—kwa sababu gani?’+ asema Yehova wa majeshi. ‘Kwa sababu nyumba yangu imeharibika, huku mkiwa mbioni, kila mmoja kwa ajili ya nyumba yake mwenyewe.+ 10 Kwa hiyo mbingu zilizuilia umande wake juu yenu, nayo dunia ikazuilia mazao yake.+ 11 Nami nikaendelea kuuita ukavu juu ya dunia, na juu ya milima, na juu ya nafaka, na juu ya divai mpya,+ na juu ya mafuta, na juu ya vitu ambavyo nchi ingetokeza, na juu ya mtu wa udongo, na juu ya wanyama wa kufugwa, na juu ya kazi ngumu yote ya mikono.’ ”+
12 Naye Zerubabeli+ mwana wa Shealtieli, na Yoshua mwana wa Yehosadaki+ kuhani mkuu, na mabaki yote ya watu wakaanza kuisikiliza sauti ya Yehova Mungu wao,+ na maneno ya nabii Hagai,+ kulingana na vile Yehova Mungu wao alivyokuwa amemtuma; nao watu wakaanza kuogopa kwa sababu ya Yehova.+
13 Naye Hagai, mjumbe+ wa Yehova akaendelea kuwaambia watu ujumbe uliotoka kwa Yehova,+ akisema: “ ‘Mimi nipo pamoja nanyi,’+ asema Yehova.”
14 Naye Yehova akaiamsha roho+ ya Zerubabeli mwana wa Shealtieli, gavana wa Yuda, na roho ya Yoshua+ mwana wa Yehosadaki kuhani mkuu, na roho ya mabaki yote ya watu; nao wakaanza kuingia na kufanya kazi katika nyumba ya Yehova wa majeshi Mungu wao.+ 15 Ilikuwa siku ya 24 ya mwezi wa 6, katika mwaka wa pili wa mfalme Dario.+
2 Katika mwezi wa 7,+ siku ya 21 ya mwezi huo, neno la Yehova likaja kupitia nabii Hagai,+ likisema: 2 “Tafadhali, mwambie Zerubabeli+ mwana wa Shealtieli,+ gavana wa Yuda,+ na Yoshua+ mwana wa Yehosadaki+ kuhani mkuu, na mabaki ya watu, ukisema, 3 ‘Ni nani kati yenu anayebaki ambaye aliona nyumba hii katika utukufu wake wa zamani?+ Nanyi mnaionaje sasa? Kwa kulinganisha, je, hii haionekani machoni penu kuwa kama si kitu?’+
4 “ ‘Lakini sasa, uwe na nguvu, Ee Zerubabeli,’ asema Yehova, ‘na uwe na nguvu,+ Ee Yoshua mwana wa Yehosadaki kuhani mkuu.’
“ ‘Nanyi iweni na nguvu, ninyi nyote watu wa nchi,’ asema Yehova, ‘na mfanye kazi.’+
“ ‘Kwa maana nipo pamoja nanyi,’+ asema Yehova wa majeshi. 5 ‘Kumbukeni jambo tuliloagana nanyi mlipotoka Misri,+ na wakati ambapo roho yangu+ ilikuwa ikisimama katikati yenu. Msiogope.’ ”+
6 “Kwa maana Yehova wa majeshi amesema hivi, ‘Bado mara moja—ni kitambo kidogo+—nami nitatikisa mbingu na dunia na bahari na nchi kavu.’+
7 “ ‘Nami nitayatikisa mataifa yote, navyo vitu vyenye kutamanika vya mataifa yote vitaingia;+ nami nitaijaza nyumba hii utukufu,’+ asema Yehova wa majeshi.
8 “ ‘Fedha ni yangu, na dhahabu ni yangu,’+ asema Yehova wa majeshi.
9 “ ‘Utukufu wa nyumba hii ya baadaye utakuwa mkubwa kuliko ule wa ile ya zamani,’+ asema Yehova wa majeshi.
“ ‘Na katika mahali hapa nitawapa amani,’+ asema Yehova wa majeshi.”
10 Katika siku ya 24 ya mwezi wa 9, katika mwaka wa pili wa Dario, neno la Yehova lilimjia nabii Hagai,+ likisema: 11 “Yehova wa majeshi amesema hivi, ‘Tafadhali, uliza makuhani juu ya sheria,+ ukisema: 12 “Mtu akichukua nyama takatifu katika upindo wa vazi lake, naye aguse kwa upindo wake mkate au mchuzi au divai au mafuta au aina yoyote ya chakula, je, kitu hicho kitakuwa kitakatifu?” ’ ”+
Nao makuhani wakajibu, wakasema: “Hapana!”
13 Naye Hagai akaendelea kusema: “Mtu aliye najisi kutokana na nafsi iliyokufa akigusa chochote kati ya vitu hivyo, je, kitu hicho kitakuwa najisi?”+
Nao makuhani wakajibu na kusema: “Kitakuwa najisi.”
14 Basi Hagai akajibu na kusema: “ ‘Hivyo ndivyo kikundi hiki cha watu kilivyo, na hivyo ndivyo taifa hili lilivyo mbele zangu,’+ asema Yehova, ‘na hivyo ndivyo kazi yote ya mikono yao ilivyo, na chochote wanachotoa huko, ni najisi.’+
15 “ ‘Lakini sasa, tafadhali, wekeni moyo wenu+ juu ya hili kuanzia leo na kuendelea, kabla jiwe halijawekwa juu ya jiwe katika hekalu la Yehova,+ 16 tangu mambo hayo yalipotukia—mtu alikuja kwenye rundo la vipimo 20, kumbe kulikuwa na 10; mtu alikuja kwenye mtungi wa kushinikizia ili kuchota vipimo 50 vya pipa la divai, kumbe vilikuwa 20.+ 17 Niliwapiga ninyi kwa kuwaunguza+ na kwa ukungu+ na kwa mvua ya mawe,+ hata kazi yote ya mikono yenu,+ na hakukuwa na yeyote kati yenu aliyegeuka kuja kwangu,’+ asema Yehova—
18 “ ‘Kuanzia leo na kuendelea, tafadhali wekeni moyo wenu+ juu ya hili, kutoka siku ya 24 ya mwezi wa 9, kuanzia siku ambayo msingi wa hekalu la Yehova uliwekwa.+ Wekeni moyo wenu juu ya hili: 19 Je, bado kuna mbegu katika shimo la nafaka?+ Na kufikia sasa, mzabibu na mtini na mkomamanga na mzeituni—je, umezaa? Kuanzia leo hii nitatoa baraka.’ ”+
20 Nalo neno la Yehova likamjia Hagai+ mara ya pili katika siku ya 24 ya mwezi huo,+ likisema: 21 “Mwambie Zerubabeli gavana wa Yuda,+ ‘Nitazitikisa mbingu na dunia.+ 22 Nitakipindua kiti cha falme na kuangamiza nguvu za falme za mataifa.+ Nitalipindua gari na wapandaji wake, na farasi na wapandaji wao wataanguka,+ kila mmoja kwa upanga wa ndugu yake.’ ”+
23 “ ‘Katika siku hiyo,’ asema Yehova wa majeshi, ‘nitakuchukua, Ee Zerubabeli+ mwana wa Shealtieli,+ mtumishi wangu,’ asema Yehova; ‘nami nitakuweka kama pete ya muhuri,+ kwa sababu ni wewe nimechagua,’+ asema Yehova wa majeshi.”+