Zekaria
1 Katika mwezi wa nane mwaka wa pili wa Dario,+ neno la Yehova lilimjia Zekaria+ mwana wa Berekia mwana wa Ido,+ nabii, likisema: 2 “Yehova alikasirika kwa sababu ya baba zenu—alikasirika sana.+
3 “Nawe uwaambie, ‘Yehova wa majeshi amesema hivi: “ ‘Rudini kwangu,’+ asema Yehova wa majeshi, ‘nami nitarudi kwenu,’+ Yehova wa majeshi amesema.” ’
4 “ ‘Msiwe kama baba zenu+ ambao manabii wa kale waliwaita,+ wakisema: “Yehova wa majeshi amesema hivi, ‘Tafadhali, rudini mwache njia zenu mbaya na mwache matendo yenu mabaya.’ ” ’+
“ ‘Lakini hawakusikiliza, wala hawakunitegea sikio,’+ asema Yehova.
5 “ ‘Basi baba zenu wako wapi?+ Na je, manabii+ waliendelea kuishi mpaka wakati usio na kipimo? 6 Hata hivyo, je, maneno yangu na masharti yangu ambayo niliwaamuru watumishi wangu manabii,+ hayakuwapata baba zenu?’+ Basi wakarudi na kusema: ‘Kulingana na yale ambayo Yehova wa majeshi alikusudia akilini kututendea,+ kulingana na njia zetu na kulingana na matendo yetu, ndivyo alivyotutendea sisi.’ ”+
7 Katika siku ya 24 ya mwezi wa 11, yaani, mwezi wa Shebati, katika mwaka wa pili wa Dario,+ neno la Yehova lilimjia Zekaria+ mwana wa Berekia mwana wa Ido,+ nabii, likisema: 8 “Niliona wakati wa usiku, na tazama! mtu+ fulani aliyepanda farasi mwekundu,+ naye alikuwa amesimama tuli katikati ya miti ya mihadasi+ iliyokuwa katika mahali penye kina kirefu; na nyuma yake kulikuwa na farasi wekundu, wenye rangi nyekundu yenye kumetameta, na weupe.”+
9 Ndipo nikauliza: “Hawa ni nani, bwana wangu?”+
Basi malaika aliyekuwa akisema nami akaniambia:+ “Mimi mwenyewe nitakuonyesha hawa ni nani.”
10 Ndipo yule mtu aliyekuwa amesimama tuli katikati ya ile mihadasi akajibu na kusema: “Hawa ndio wale ambao Yehova amewatuma watembee huku na huku duniani.”+ 11 Nao wakamjibu malaika wa Yehova aliyekuwa amesimama katikati ya mihadasi na kusema: “Tumetembea huku na huku duniani,+ na tazama! dunia yote imetulia wala haina usumbufu.”+
12 Basi malaika wa Yehova akajibu na kusema: “Ee Yehova wa majeshi, ni mpaka wakati gani utakosa kulionyesha rehema Yerusalemu na majiji ya Yuda,+ ambayo umeshutumu hii miaka 70?”+
13 Naye Yehova akamjibu malaika aliyekuwa akisema nami, kwa maneno mema, maneno yenye kufariji;+ 14 na malaika aliyekuwa akisema nami akaendelea kuniambia: “Paaza sauti, na kusema, ‘Yehova wa majeshi amesema hivi: “Nimekuwa na wivu, wivu mkubwa, kwa ajili ya Yerusalemu na kwa ajili ya Sayuni.+ 15 Nina hasira kubwa juu ya mataifa yenye starehe;+ kwa sababu mimi nilikasirika kidogo tu,+ bali wao waliuzidisha msiba.” ’+
16 “Basi Yehova amesema hivi, ‘ “Nitarudi Yerusalemu kwa rehema nyingi.+ Nyumba yangu itajengwa ndani yake,”+ asema Yehova wa majeshi, “na kamba ya kupimia itanyooshwa juu ya Yerusalemu.” ’+
17 “Paaza sauti tena, na kusema, ‘Yehova wa majeshi amesema hivi: “Bado majiji yangu yatafurikwa na wema tena;+ na Yehova bado atajuta juu ya Sayuni+ na bado atalichagua Yerusalemu.” ’ ”+
18 Nami nikainua macho yangu nikaona; na tazama! kulikuwa na pembe nne.+ 19 Kwa hiyo nikamwambia malaika aliyekuwa akisema nami: “Hizi ni nini?” Naye akaniambia: “Hizi ndizo zile pembe zilizotawanya Yuda,+ Israeli+ na Yerusalemu.”+
20 Tena Yehova akanionyesha mafundi wanne. 21 Ndipo nikauliza: “Hawa wanakuja kufanya nini?”
Naye akaendelea kusema: “Hizi ndizo zile pembe+ zilizotawanya Yuda hata ikawa kwamba hakuna yeyote aliyeinua kichwa chake; na hizi nyingine zitakuja kuzitetemesha, kuziangusha chini pembe za mataifa ambayo yanainua pembe juu ya nchi ya Yuda, ili kumtawanya.”+
2 Nami nikainua macho yangu nikaona; na tazama! kulikuwa na mtu, naye alikuwa na kamba ya kupimia+ mkononi mwake. 2 Basi nikasema: “Unaenda wapi?”
Naye akaniambia: “Kupima Yerusalemu, ili kuona jinsi upana wake ulivyo na jinsi urefu wake ulivyo.”+
3 Na tazama! malaika aliyekuwa akisema nami akatoka, na kulikuwa na malaika mwingine akitoka kwenda kukutana naye. 4 Ndipo akamwambia: “Kimbia, useme na yule kijana pale, umwambie, “ ‘Yerusalemu litakaliwa na watu+ kama nchi ya mashambani iliyo wazi, kwa sababu ya wingi wa watu na wanyama wa kufugwa walio ndani yake.+ 5 Nami mwenyewe nitakuwa kwake,” asema Yehova, “ukuta wa moto kuzunguka pande zote,+ nami nitakuwa utukufu ndani yake.” ’ ”+
6 “Haya! Haya! Ikimbieni basi, nchi ya kaskazini,”+ asema Yehova.
“Maana nimewatawanya ninyi kotekote kuelekea pepo nne za mbingu,”+ asema Yehova.
7 “Haya, Sayuni!+ Ponyoka, wewe unayekaa na binti Babiloni.+ 8 Kwa maana Yehova wa majeshi amesema hivi, ‘Baada ya utukufu+ amenituma kwa mataifa yaliyokuwa yakiwapora ninyi;+ kwa maana yeye anayewagusa ninyi+ anaigusa mboni ya jicho langu.+ 9 Maana tazama, ninatikisa mkono wangu juu yao,+ nao watakuwa nyara kwa watumwa wao.’+ Nanyi mtajua ya kwamba Yehova wa majeshi amenituma mimi.+
10 “Paaza sauti na kushangilia, Ee binti Sayuni;+ kwa maana mimi naja,+ nami nitakaa katikati yako,”+ asema Yehova. 11 “Na mataifa mengi yatajiunga na Yehova siku hiyo,+ nao watakuwa watu wangu;+ nami nitakaa katikati yako.” Nawe utajua kwamba Yehova wa majeshi amenituma kwako.+ 12 Na Yehova atamiliki Yuda iwe fungu lake katika nchi takatifu,+ naye atalichagua Yerusalemu tena.+ 13 Nyamazeni, watu wote, mbele za Yehova,+ kwa maana ameamka+ kutoka katika makao yake matakatifu.+
3 Naye akanionyesha Yoshua+ kuhani mkuu akiwa amesimama mbele ya malaika wa Yehova, naye Shetani+ akiwa amesimama kwenye mkono wake wa kuume ili kumpinga.+ 2 Kisha malaika+ wa Yehova akamwambia Shetani: “Yehova akukemee,+ Ee Shetani, ndiyo, Yehova akukemee, yeye ambaye analichagua Yerusalemu!+ Je, huyu si kipande cha mti kilichonyakuliwa kutoka motoni?”+
3 Yoshua naye alikuwa amevaa mavazi machafu+ akiwa amesimama mbele ya malaika. 4 Ndipo akajibu na kuwaambia wale waliosimama mbele yake: “Mvueni mavazi hayo machafu.” Naye akaendelea kumwambia: “Ona, nimekuondolea kosa lako,+ nawe umevikwa kanzu za fahari.”+
5 Basi nikasema: “Na wamvike kilemba safi kichwani pake.”+ Nao wakaweka kilemba hicho safi kichwani pake na kumvika mavazi; naye malaika wa Yehova alikuwa amesimama karibu. 6 Ndipo malaika wa Yehova akaanza kumtolea Yoshua ushahidi, akisema: 7 “Yehova wa majeshi amesema hivi, ‘Ukitembea katika njia zangu, nawe ukishika wajibu wangu,+ basi wewe ndiye utakayeihukumu nyumba yangu+ na kuzitunza nyua zangu pia; nami nitakupa uhuru wa kuingia katikati ya hawa wanaosimama karibu.’
8 “ ‘Tafadhali sikia, Ee Yoshua kuhani mkuu, wewe pamoja na wenzako wanaoketi mbele yako, kwa maana wao ni watu wanaotumika kuwa ishara;+ kwa maana, tazama, mimi namleta ndani Chipukizi+ mtumishi wangu!+ 9 Kwa maana tazama! jiwe+ ambalo nimeweka mbele ya Yoshua! Juu ya jiwe hilo moja kuna macho saba.+ Tazama, mimi ninachora mchoro wake,’+ asema Yehova wa majeshi, ‘nami nitaondolea mbali kosa la nchi hiyo katika siku moja.’+
10 “ ‘Katika siku hiyo,’ asema Yehova wa majeshi, ‘Mtaitana mtu na mwenzake, mkiwa chini ya mzabibu na mkiwa chini ya mtini.’ ”+
4 Na malaika aliyekuwa akisema nami akarudi na kuniamsha, kama mtu anayeamshwa kutoka katika usingizi.+ 2 Ndipo akaniambia: “Unaona nini?”+
Basi nikasema: “Nimeona, na tazama! kuna kinara cha taa, chote ni cha dhahabu,+ na bakuli liko juu yake. Na taa zake saba ziko juu yake, ndiyo, saba;+ na taa zilizo juu yake zina mirija saba. 3 Na kuna mizeituni miwili kando yake,+ mmoja upande wa kuume wa bakuli na mwingine upande wake wa kushoto.”
4 Ndipo nikamuuliza malaika aliyekuwa akisema nami: “Vitu hivi vinamaanisha nini, bwana wangu?”+ 5 Basi malaika aliyekuwa akisema nami akajibu na kuniambia: “Je, kweli wewe hujui maana ya vitu hivi?”
Ndipo nikasema: “Sijui, bwana wangu.”+
6 Basi akajibu na kuniambia: “Hili ndilo neno la Yehova kwa Zerubabeli, akisema, “Si kwa jeshi,+ wala kwa nguvu,+ bali kwa roho yangu,”+ Yehova wa majeshi amesema. 7 Wewe ni nani, Ee mlima mkubwa?+ Utakuwa nchi tambarare mbele ya Zerubabeli.+ Naye ataleta jiwe la juu kabisa.+ Nalo litapaaziwa sauti:+ “Linavutia kama nini! Linavutia kama nini!” ’ ”+
8 Kisha neno la Yehova likaendelea kunijia, likisema: 9 “Mikono ya Zerubabeli ndiyo imeweka msingi wa nyumba hii,+ na mikono yake mwenyewe itaikamilisha.+ Nanyi mtajua ya kuwa Yehova wa majeshi amenituma kwenu ninyi.+ 10 Kwa maana ni nani ameidharau siku ya mambo madogo?+ Nao watafurahi+ na kuona timazi mkononi mwa Zerubabeli. Haya saba ndiyo macho ya Yehova.+ Yanaenda huku na huku duniani kote.”+
11 Nami nikamjibu, nikamwambia: “Hii mizeituni miwili upande wa kuume wa kinara cha taa na upande wake wa kushoto inamaanisha nini?”+ 12 Kisha nikamjibu, nikamwambia mara ya pili: “Yale mafungu mawili ya matawi ya mizeituni ambayo, kwa njia ya mifereji miwili ya dhahabu, yanamimina umajimaji wa dhahabu kutoka ndani yake ni nini?”
13 Basi akaniambia: “Je, kweli wewe hujui maana ya vitu hivi?”
Ndipo nikasema: “Sijui, bwana wangu.”+
14 Ndipo akasema: “Hawa ndio wale watiwa-mafuta+ wawili wanaosimama kando ya Bwana wa dunia yote.”+
5 Ndipo nikainua tena macho yangu nikaona; na tazama! kitabu cha kukunjwa+ kinachoruka. 2 Basi akaniuliza: “Unaona nini?”+
Nami nikasema: “Naona kitabu cha kukunjwa kinachoruka, urefu wake ni mikono 20, na upana wake ni mikono 10.”
3 Ndipo akaniambia: “Hii ndiyo laana inayotoka kwenda juu ya uso wa dunia yote,+ kwa sababu kila mtu anayeiba,+ kulingana na hiyo, upande huu, hakupewa adhabu; na kila mtu anayefanya kiapo rasmi,+ kulingana na hiyo, upande ule mwingine,+ hakupewa adhabu. 4 ‘Nimeifanya hiyo iende,’ asema Yehova wa majeshi, ‘nayo itaingia katika nyumba ya mwizi na katika nyumba ya mtu anayefanya kiapo rasmi katika jina langu kwa uwongo;+ nayo itakaa katikati ya nyumba yake na kuiangamiza pamoja na mbao zake na mawe yake.’ ”+
5 Ndipo malaika aliyekuwa akisema nami akatokea na kuniambia: “Tafadhali, inua macho yako, uone ni kitu gani hiki kinachotoka kwenda.”
6 Basi nikasema: “Ni nini hicho?”
Naye akasema: “Hiki ndicho kipimo cha efa kinachotoka kwenda.” Naye akaendelea kusema: “Hii ndiyo sura yao katika dunia yote.” 7 Na tazama! kifuniko cha mviringo cha madini ya risasi kiliinuliwa; na tazama, mwanamke fulani amekaa ndani ya efa hiyo. 8 Basi akasema: “Huyu ni Uovu.” Naye akamtupa mwanamke huyo tena ndani ya ile efa,+ halafu akatupa kifuniko kile cha risasi juu ya mdomo wa ile efa.
9 Ndipo nikainua macho yangu na kuona, na tazama, kulikuwa na wanawake wawili wakija, na upepo ulikuwa katika mabawa yao. Nao walikuwa na mabawa kama mabawa ya korongo. Nao hatua kwa hatua wakainua ile efa kati ya dunia na mbingu. 10 Basi nikamwambia malaika aliyekuwa akisema nami: “Wanaipeleka wapi efa hii?”
11 Naye akaniambia: “Wanaenda kumjengea+ mwanamke huyo nyumba katika nchi ya Shinari;+ nayo itafanywa imara, naye atawekwa hapo katika mahali pake anapopaswa kuwa.”
6 Ndipo nikainua tena macho yangu nikaona; na tazama! kulikuwa na magari manne yakija kutoka katikati ya milima miwili, na milima hiyo ilikuwa milima ya shaba. 2 Kulikuwa na farasi wekundu+ katika gari la kwanza; na farasi weusi+ katika gari la pili. 3 Na katika gari la tatu kulikuwa na farasi weupe;+ na katika gari la nne, farasi wenye madoadoa, wenye madoa ya rangi mchanganyiko.+
4 Ndipo nikajibu na kumwambia yule malaika aliyekuwa akisema nami: “Magari haya ni nini, bwana wangu?”+
5 Basi malaika akanijibu: “Hizi ndizo roho nne+ za mbingu zinazotoka+ baada ya kusimama mbele za Bwana+ wa dunia yote.+ 6 Na kuhusu gari lile walimo farasi weusi, wanaenda nchi ya kaskazini;+ na wale weupe wataenda kuelekea upande wa nyuma wa ile bahari; na wale wenye madoadoa wataenda katika nchi ya kusini.+ 7 Na wale wenye madoa ya rangi mchanganyiko,+ wataenda na kuzidi kutafuta mahali pa kwenda, ili kutembea huku na huku duniani.”+ Kisha akasema: “Nendeni, tembeeni huku na huku duniani.” Nao wakaanza kutembea huku na huku duniani.
8 Naye akanipaazia sauti na kuniambia, akisema: “Ona, wale wanaoenda nchi ya kaskazini ndio wamefanya roho+ ya Yehova itulie katika nchi ya kaskazini.”+
9 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, likisema: 10 “Kitu fulani kichukuliwe kutoka kwa watu waliohamishwa,+ kutoka kwa Heldai na Tobaya na Yedaya; nawe mwenyewe uje siku hiyo, nawe uingie katika nyumba ya Yosia mwana wa Sefania+ pamoja na hawa ambao wametoka Babiloni. 11 Nawe uchukue fedha na dhahabu, ufanye taji la fahari,+ uliweke juu ya kichwa cha Yoshua+ mwana wa Yehosadaki kuhani mkuu. 12 Nawe umwambie,
“‘Yehova wa majeshi amesema hivi: “Tazama, mtu+ ambaye jina lake ni Chipukizi.+ Naye atachipuka kutoka mahali pake mwenyewe, naye atalijenga hekalu la Yehova.+ 13 Naye mwenyewe atalijenga hekalu la Yehova, naye atachukua heshima;+ ataketi na kutawala juu ya kiti chake cha ufalme, naye atakuwa kuhani juu ya kiti chake cha ufalme,+ na shauri la amani+ litakuwa kati ya vyeo hivyo viwili. 14 Na lile taji la fahari litakuja kuwa la Helemu na Tobaya na Yedaya+ na Heni mwana wa Sefania kama ukumbusho+ katika hekalu la Yehova. 15 Na wale walio mbali watakuja na kujenga katika hekalu la Yehova.”+ Nanyi mtajua ya kuwa Yehova wa majeshi mwenyewe amenituma kwenu.+ Nayo yatatukia—bila shaka ikiwa mtaisikiliza sauti ya Yehova Mungu wenu.’ ”+
7 Tena ikawa kwamba katika mwaka wa nne wa Mfalme Dario+ neno la Yehova lilimjia Zekaria, siku ya nne ya mwezi wa tisa, yaani, mwezi wa Kislevu.+ 2 Na watu wa Betheli wakawatuma Shareza na Regem-meleki na watu wake ili kuutuliza+ uso wa Yehova, 3 na kuwaambia makuhani+ wa nyumba ya Yehova wa majeshi, na manabii, wakisema: “Je, nilie mwezi wa tano,+ na kufunga, kama ambavyo nimefanya miaka hii mingi iliyopita?”+
4 Na neno la Yehova wa majeshi likaendelea kunijia, na kusema: 5 “Waambie watu wote wa nchi na makuhani, ‘Mlipofunga+ na kuomboleza katika mwezi wa 5 na mwezi wa 7,+ mkafanya hivyo kwa miaka 70,+ je, kweli mlifunga kwa ajili yangu mimi?+ 6 Na wakati mlikula na wakati mlikunywa, je, si ninyi mliokula, na je, si ninyi mliokunywa? 7 Je, haiwapasi kutii maneno+ ambayo Yehova alisema kupitia manabii wa kale,+ wakati Yerusalemu lilipokuwa na watu, likistarehe, pamoja na majiji yake yenye kulizunguka pande zote, na watu walipokuwa wakikaa Negebu+ na Shefela?’ ”+
8 Nalo neno la Yehova likaendelea kumjia Zekaria, na kusema: 9 “Yehova wa majeshi amesema hivi, ‘Fanyeni hukumu kwa haki ya kweli;+ na mtendeane kwa fadhili zenye upendo+ na rehema;+ 10 wala msimpunje mjane+ yeyote na mvulana yeyote asiye na baba,+ wala mkaaji mgeni+ au mwenye kuteseka,+ wala msipangiane jambo lolote baya mioyoni mwenu.’+ 11 Lakini waliendelea kukataa kusikiliza,+ nao wakaendelea kugeuza bega kwa ukaidi,+ wakafanya masikio yao kuwa magumu mno yasiweze kusikia.+ 12 Nayo mioyo yao+ wakaifanya kuwa kama jiwe gumu ili isitii sheria+ na maneno ambayo Yehova wa majeshi alipeleka kwa roho yake,+ kupitia manabii wa kale;+ hata Yehova wa majeshi akakasirika sana.”+
13 “ ‘Basi ikawa kwamba, kama vile alivyoita wala hawakusikiliza,+ vivyo hivyo wao waliita na mimi sikusikiliza,’+ Yehova wa majeshi amesema. 14 ‘Ndipo nikawatupa kama tufani kotekote katika mataifa+ yote ambayo hawakuyajua;+ nayo nchi imeachwa ukiwa nyuma yao, bila kuwa na mtu yeyote anayepita kati yake wala anayerudi;+ nao wakaifanya nchi yenye kutamanika+ kuwa kitu cha kushangaza.’ ”
8 Nalo neno la Yehova wa majeshi likaendelea kuja, na kusema: 2 “Yehova wa majeshi+ asema hivi, ‘Nitakuwa na wivu mkubwa+ kwa ajili ya Sayuni, nami nitakuwa na wivu kwa ajili yake kwa ghadhabu kubwa.’ ”+
3 “Yehova asema hivi, ‘Nitarudi Sayuni+ na kukaa katikati ya Yerusalemu; na Yerusalemu+ litaitwa jiji la ukweli,+ na mlima wa Yehova+ wa majeshi, ule mlima mtakatifu.’ ”+
4 “Yehova wa majeshi asema hivi, ‘Wanaume wazee na wanawake wazee watakaa tena katika viwanja vya watu wote vya Yerusalemu,+ kila mmoja na fimbo yake+ mkononi mwake kwa sababu ya wingi wa siku zake. 5 Navyo viwanja vya watu wote vya jiji vitajaa wavulana na wasichana wakicheza katika viwanja vyake vya watu wote.’ ”+
6 “Yehova wa majeshi asema hivi, ‘Ijapokuwa jambo hili lionekane gumu mno machoni pa mabaki ya watu hawa katika siku hizo, je, lionekane gumu mno machoni pangu pia?’+ asema Yehova wa majeshi.”
7 “Yehova wa majeshi asema hivi, ‘Tazama, mimi ninawaokoa watu wangu kutoka katika nchi ya mashariki na kutoka katika nchi ya magharibi.+ 8 Nami nitawaleta ndani, nao watakaa katikati ya Yerusalemu;+ nao watakuwa watu wangu,+ nami nitakuwa Mungu wao katika ukweli na katika uadilifu.’ ”+
9 “Yehova wa majeshi asema hivi, ‘Mikono yenu na iwe na nguvu,+ ninyi ambao siku hizi mnayasikia maneno haya kutoka katika kinywa cha manabii,+ katika siku ulipowekwa msingi wa nyumba ya Yehova wa majeshi, ili hekalu lijengwe.+ 10 Kwa maana kabla ya siku hizo hapakuwa na mshahara wa wanadamu;+ wala hapakuwa na mshahara wa wanyama wa kufugwa; na kwa yule anayetoka na yule anayeingia hapakuwa na amani kwa sababu ya adui,+ kwa maana nilizidi kuwatupa wanadamu wote mmoja juu ya mwingine.’+
11 “ ‘Na sasa sitakuwa kwa mabaki ya watu hawa kama nilivyokuwa kwao siku za zamani,’+ asema Yehova wa majeshi. 12 ‘Kwa maana kutakuwa na mbegu ya amani;+ mzabibu utazaa matunda yake,+ na dunia itatoa mazao yake,+ na mbingu zitatoa umande wake;+ nami nitawafanya mabaki+ ya watu hawa warithi vitu hivyo vyote.+ 13 Na itakuwa kwamba kama vile mlivyokuwa laana katikati ya mataifa,+ enyi nyumba ya Yuda na nyumba ya Israeli,+ ndivyo nitakavyowaokoa, nanyi mtakuwa baraka.+ Msiogope.+ Mikono yenu na iwe na nguvu.’+
14 “Kwa maana Yehova wa majeshi asema hivi, ‘ “Kama vile nilivyoazimia akilini kuwatendea ninyi msiba kwa sababu mababu zenu walinikasirisha,”+ Yehova wa majeshi asema, “wala sikujuta,+ 15 ndivyo nitakavyoazimia akilini katika siku hizi kulitendea vema Yerusalemu pamoja na nyumba ya Yuda.+ Msiogope.” ’+
16 “ ‘Haya ndiyo mambo ambayo mnapaswa kufanya:+ Semeni ukweli kila mtu na mwenzake.+ Hukumuni kwa hukumu ya kweli na ya amani malangoni mwenu.+ 17 Nanyi msipangiane mabaya mioyoni mwenu,+ wala msipende kiapo chochote cha uwongo;+ kwa maana nimeyachukia mambo hayo yote,’+ asema Yehova.”
18 Nalo neno la Yehova wa majeshi likaendelea kunijia, na kusema: 19 “Yehova wa majeshi amesema hivi, ‘Kufunga kwa mwezi wa nne,+ na kufunga kwa mwezi wa tano,+ na kufunga kwa mwezi wa saba,+ na kufunga kwa mwezi wa kumi+ itakuwa furaha na kushangilia na majira mema ya sherehe+ kwa nyumba ya Yuda. Basi pendeni kweli na amani.’+
20 “Yehova wa majeshi asema hivi, ‘Bado itakuwa kwamba vikundi vya watu na wakaaji wa majiji mengi watakuja;+ 21 na wakaaji wa jiji moja watawaendea wale wa jiji lingine, wakisema: “Twendeni kwa bidii+ tukautulize uso+ wa Yehova na kumtafuta Yehova wa majeshi. Mimi nami nitaenda pia.”+ 22 Na vikundi vingi vya watu na mataifa yenye nguvu watakuja kumtafuta Yehova wa majeshi katika Yerusalemu+ na kuutuliza uso wa Yehova.’
23 “Yehova wa majeshi asema hivi, ‘Na itakuwa katika siku hizo kwamba watu kumi kutoka katika lugha zote za mataifa+ watashika,+ ndiyo, wataushika upindo wa nguo ya mtu aliye Myahudi,+ wakisema: “Tutakwenda pamoja nanyi,+ kwa maana tumesikia ya kuwa Mungu yupo pamoja nanyi.” ’ ”+
“Neno la Yehova linashindana na nchi ya Hadraki, nalo linapumzika Damasko;+ kwa maana Yehova ameweka jicho juu ya mtu wa udongo+ na juu ya makabila yote ya Israeli. 2 Na Hamathi+ litapakana naye pia; Tiro+ na Sidoni,+ kwa maana ana hekima sana.+ 3 Tiro nalo likajijengea boma, na kukusanya fedha kama mavumbi na dhahabu kama matope ya barabarani.+ 4 Tazama! Yehova mwenyewe atamfukuza, naye hakika atalipiga na kuliangusha baharini jeshi lake;+ naye mwenyewe atateketezwa motoni.+ 5 Ashkeloni litaona na kuogopa; Gaza nalo pia litakuwa na maumivu makali sana; Ekroni+ pia, kwa sababu tumaini lake analotazamia+ litaona aibu. Na mfalme ataangamizwa kutoka Gaza, nalo Ashkeloni halitakaliwa na watu.+ 6 Na mwana-haramu+ ataketi huko Ashdodi,+ nami nitakikatilia mbali kiburi cha Mfilisti.+ 7 Nami nitaviondoa vitu vyake vyenye madoa ya damu kinywani mwake na kuyaondoa machukizo yake kutoka katikati ya meno+ yake, naye mwenyewe atabaki kwa ajili ya Mungu wetu; naye atakuwa kama shehe+ katika Yuda,+ na Ekroni kama Myebusi.+ 8 Nami nitapiga kambi kama mlinzi wa mbele kwa ajili ya nyumba yangu,+ ili kusiwe na mtu yeyote anayepita kati wala anayerudi; wala msimamizi wa kazi+ hatapita tena kwao, kwa maana sasa nimeyaona kwa macho yangu.+
9 “Shangilia sana, Ee binti Sayuni.+ Piga kelele za ushindi,+ Ee binti Yerusalemu. Tazama! mfalme+ wako anakuja kwako.+ Yeye ni mwadilifu, ndiyo, ameokolewa;+ ni mnyenyekevu,+ naye amepanda juu ya punda, juu ya mnyama mkomavu, mwana wa punda-jike.+ 10 Nami nitalikatilia mbali gari la vita kutoka katika Efraimu na farasi kutoka katika Yerusalemu.+ Na upinde wa mapigano+ utakatiliwa mbali. Naye atasema amani kwa mataifa;+ na utawala wake utakuwa kutoka bahari mpaka bahari na kutoka Mto mpaka miisho ya dunia.+
11 “Nawe pia, Ee mwanamke, nitawatoa wafungwa+ wako kutoka katika shimo ambalo halina maji kwa kutumia damu ya agano+ lako.
12 “Rudini katika ngome,+ enyi wafungwa wa lile tumaini.+
“Pia, leo ninakuambia, ‘Nitakulipa fungu lililo mara mbili,+ Ee mwanamke. 13 Kwa maana nitamkanyaga Yuda kama upinde wangu. Nami nitamtia Efraimu katika upinde, nami nitawaamsha wana wako, Ee Sayuni, kupigana na wana wako,+ Ee Ugiriki,+ nami nitakufanya kama upanga wa mwanamume mwenye nguvu.’+ 14 Na Yehova mwenyewe ataonekana juu yao,+ na mshale wake utaenda kama umeme.+ Naye Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova atapiga baragumu,+ ataenda pamoja na dhoruba za upepo wa kusini.+ 15 Yehova wa majeshi mwenyewe atawalinda wao, nao watakula+ na kuyatiisha mawe ya kombeo. Nao watakunywa+—wafanye kelele—kana kwamba kuna divai; nao watajazwa kama bakuli, kama pembe za madhabahu.+
16 “Na Yehova Mungu wao atawaokoa+ katika siku hiyo kama kundi la watu wake;+ kwa maana watakuwa kama mawe ya taji yanayong’aa juu ya nchi yake.+ 17 Kwa maana lo! jinsi ulivyo mkuu wema wake,+ na jinsi ulivyo mkuu uzuri wake!+ Nafaka ndiyo itakayowasitawisha vijana, na divai mpya nayo itawasitawisha mabikira.”+
10 “Mwombeni Yehova mvua+ wakati wa mvua ya masika,+ Yehova anayefanya mawingu ya dhoruba,+ ambaye huwapa mvua kubwa,+ na kumpa kila mmoja mimea shambani.+ 2 Kwa maana terafimu+ zimesema mambo ya uchawi; nao waaguzi wameona maono ya uwongo,+ nao huendelea kusema ndoto za bure, nao hujaribu kufariji kwa ubatili.+ Ndiyo sababu wataondoka kama kundi;+ watateseka, kwa sababu hakuna mchungaji.+
3 “Hasira yangu imewaka juu ya wachungaji,+ nami nitawatoza hesabu+ viongozi walio kama mbuzi;+ kwa maana Yehova wa majeshi ameelekeza fikira zake kwa kundi lake,+ nyumba ya Yuda, naye amewafanya kama farasi+ wake mwenye heshima katika mapigano. 4 Kutoka kwake kuna mkuu,+ kutoka kwake kuna mtawala anayetegemeza,+ kutoka kwake kuna upinde wa mapigano;+ kwake hutoka kila msimamizi wa kazi,+ wote pamoja. 5 Nao watakuwa kama wanaume wenye nguvu+ wanaokanyaga matope ya barabarani katika mapigano.+ Nao watajihusisha katika mapigano, kwa maana Yehova yupo pamoja nao;+ na hao wapanda-farasi wataona aibu.+ 6 Nami nitaifanya nyumba ya Yuda iwe kuu, nami nitaiokoa nyumba ya Yosefu.+ Nami nitawapa makao, kwa maana nitawaonyesha rehema;+ nao watakuwa kama watu ambao sikutupilia mbali;+ kwa maana mimi ni Yehova Mungu wao, nami nitawajibu.+ 7 Na wale wa Efraimu watakuwa kama mwanamume mwenye nguvu,+ na moyo wao utashangilia kana kwamba kutokana na divai.+ Na wana wao wenyewe wataona nao hakika washangilie;+ moyo wao utashangilia katika Yehova.+
8 “ ‘Nitawapigia mluzi+ na kuwakusanya pamoja; kwa maana nitawakomboa,+ nao watakuwa wengi, kama wale ambao wamekuwa wengi.+ 9 Nami nitawatawanya kama mbegu katikati ya mataifa,+ nao watanikumbuka wakiwa mbali;+ nao wataamka pamoja na wana wao na kurudi.+ 10 Nami nitawarudisha kutoka nchi ya Misri;+ nitawakusanya pamoja kutoka Ashuru;+ nami nitawaleta katika nchi ya Gileadi+ na Lebanoni, wala nafasi haitapatikana kwa ajili yao.+ 11 Naye atapita baharini kwa taabu;+ na ndani ya bahari atayapiga mawimbi,+ na vilindi vyote vya Nile vitakauka.+ Nacho kiburi cha Ashuru kitashushwa,+ na fimbo ya enzi+ ya Misri itaondoka.+ 12 Nami nitawafanya wawe wakuu katika Yehova,+ nao watatembea huku na huku katika jina lake,’+ asema Yehova.”
11 “Fungua milango yako, Ee Lebanoni,+ ili moto uteketeze kati ya mierezi yako.+ 2 Piga mayowe, Ee mberoshi, kwa maana mwerezi umeanguka; kwa sababu wenye utukufu wameporwa!+ Pigeni mayowe, enyi miti mikubwa sana ya Bashani, kwa maana msitu usiopenyeka umeanguka!+ 3 Sikiliza! Mayowe ya wachungaji,+ kwa maana utukufu wao umeporwa.+ Sikiliza! Kunguruma kwa wana-simba wenye manyoya shingoni, kwa maana vichaka vyenye kiburi kando ya Yordani vimeporwa.+
4 “Yehova Mungu wangu asema hivi, ‘Chunga kundi lililokusudiwa kuuawa,+ 5 ambalo wanunuzi wake huwaua+ ingawa hawahesabiwi hatia.+ Na wale wanaowauza+ husema: “Yehova abarikiwe, huku nami nitapata utajiri.”+ Na wachungaji wao wenyewe hawawaonyeshi huruma yoyote.’+
6 “ ‘Kwa maana sitawahurumia tena wakaaji wa nchi,’+ asema Yehova. ‘Kwa hiyo nawafanya wanadamu wajikute, kila mmoja katika mkono wa mwenzake+ na katika mkono wa mfalme+ wake; nao wataivunja nchi vipande-vipande, nami sitakomboa kwa vyovyote kutoka mkononi mwao.’ ”+
7 Nami nililichunga kundi+ lililokusudiwa kuuawa,+ kwa ajili yenu, enyi wenye kuteseka wa kundi.+ Kwa hiyo nikajichukulia fimbo+ mbili. Moja nikaiita Uzuri,+ na ile nyingine nikaiita Muungano,+ nami nikaanza kulichunga kundi. 8 Mwishowe nikafutilia mbali wachungaji watatu katika mwezi mmoja,+ kwa vile nafsi yangu ilikosa subira+ kwao hatua kwa hatua, na pia nafsi zao zilinichukia. 9 Mwishowe nikasema: “Sitaendelea kuwachunga ninyi.+ Yule anayekufa, na afe. Na yule anayefutiliwa mbali, na afutiliwe mbali.+ Na wale waliobaki, kila mmoja na ale nyama ya mwenzake.”+ 10 Basi nikachukua fimbo yangu inayoitwa Uzuri+ na kuikata vipande-vipande,+ ili kulivunja agano langu ambalo nilikuwa nimefanya pamoja na vikundi vyote vya watu.+ 11 Nalo likavunjwa siku hiyo, na hivyo wenye kuteseka wa kundi+ waliokuwa wakinitazama+ wakajua kwamba hilo lilikuwa neno la Yehova.
12 Ndipo nikawaambia: “Ikiwa vema machoni penu,+ nipeni mshahara wangu; lakini kama sivyo, acheni.” Basi wakalipa mshahara wangu, vipande 30 vya fedha.+
13 Kwa hiyo Yehova akaniambia: “Utupe ndani ya hazina+—thamani tukufu ambayo nimekadiriwa kwa maoni yao.”+ Ndipo nikavichukua vile vipande 30 vya fedha, nami nikavitupa ndani ya hazina katika nyumba ya Yehova.+
14 Kisha nikaikata vipande-vipande fimbo yangu ya pili, inayoitwa Muungano,+ ili kuuvunja undugu+ kati ya Yuda na Israeli.+
15 Kisha Yehova akaendelea kuniambia: “Jichukulie tena vifaa vya mchungaji asiyefaa kitu.+ 16 Kwa maana tazama, ninamwacha mchungaji asimame katika nchi hii.+ Hatawakazia fikira kondoo wanaofutiliwa mbali.+ Hatawatafuta wachanga, wala hatawaponya kondoo waliovunjika.+ Anayesimama hatampa chakula, naye atakula nyama ya aliye mnono,+ atazing’oa kwato za kondoo.+ 17 Ole wake mchungaji wangu asiyefaa kitu,+ anayeliacha kundi!+ Upanga utakuwa juu ya mkono wake na juu ya jicho lake la kuume. Mkono wake utakauka+ bila shaka, na jicho lake la kuume bila shaka litaingia giza.”
12 Tangazo:
“Neno la Yehova kuhusu Israeli,” asema Yehova, Yeye anayetandaza mbingu+ na kuweka msingi wa dunia+ na kufanyiza roho+ ya mwanadamu ndani yake. 2 “Tazama, mimi ninafanya Yerusalemu+ kuwa bakuli linalosababisha kuyumba-yumba kwa vikundi vyote vya watu kuzunguka pande zote;+ na pia atakuja kuzingira Yuda, naam, Yerusalemu.+ 3 Na itatukia katika siku hiyo+ kwamba nitafanya Yerusalemu kuwa jiwe+ lenye kulemea vikundi vyote vya watu. Wale wote wanaoliinua bila shaka watajitia mikwaruzo mikali; na mataifa yote ya dunia hakika yatakusanyika+ kupigana naye. 4 Katika siku hiyo,”+ asema Yehova, “nitamtia mshangao kila farasi+ na kumtia wazimu+ mpandaji wake; nami nitafungua macho+ yangu juu ya nyumba ya Yuda, nami nitampofusha kila farasi wa vikundi vya watu. 5 Na mashehe+ wa Yuda watasema moyoni mwao, ‘Wakaaji wa Yerusalemu ni nguvu kwangu katika Yehova wa majeshi Mungu wao.’+ 6 Katika siku hiyo nitawafanya mashehe wa Yuda kama chombo cha moto kati ya miti+ na kama mwenge wenye moto katika fungu la nafaka iliyokatwa hivi karibuni,+ nao watateketeza vikundi vyote vya watu kuzunguka pande zote upande wa mkono wa kuume na wa kushoto;+ na Yerusalemu litakaliwa tena na watu mahali pake mwenyewe, katika Yerusalemu.+
7 “Naye Yehova hakika ataokoa mahema ya Yuda kwanza, kusudi uzuri wa nyumba ya Daudi na uzuri wa wakaaji wa Yerusalemu usiwe mkuu mno kuliko Yuda. 8 Katika siku hiyo Yehova atakuwa ulinzi kuzunguka wakaaji wa Yerusalemu;+ na yeye anayejikwaa kati yao atakuwa katika siku hiyo kama Daudi,+ na nyumba ya Daudi kama Mungu,+ kama malaika wa Yehova mbele yao.+ 9 Na itatukia katika siku hiyo kwamba nitatafuta kuyaangamiza mataifa yote yanayokuja kupigana na Yerusalemu.+
10 “Nami nitamimina juu ya nyumba ya Daudi na juu ya wakaaji wa Yerusalemu roho ya kibali+ na maombi,+ nao watamtazama Yule waliyemchoma,+ nao wataomboleza juu Yake kama kuombolezea mwana wa pekee; na kutakuwa na maombolezo machungu juu yake kama vile kunapokuwa na maombolezo juu ya mwana mzaliwa wa kwanza.+ 11 Katika siku hiyo maombolezo katika Yerusalemu yatakuwa makubwa, kama maombolezo ya Hadadrimoni katika nchi tambarare ya bonde la Megido.+ 12 Na nchi hakika itaomboleza,+ kila familia peke yake; familia ya nyumba ya Daudi peke yake, na wanawake wao peke yao;+ familia ya nyumba ya Nathani+ peke yake, na wanawake wao peke yao; 13 familia ya nyumba ya Lawi+ peke yake, na wanawake wao peke yao; familia ya Washimei+ peke yake, na wanawake wao peke yao; 14 familia zote zitakazobaki, kila familia peke yake, na wanawake wao peke yao.+
13 “Katika siku hiyo+ nyumba ya Daudi na wakaaji wa Yerusalemu watafunguliwa kisima+ kwa ajili ya dhambi+ na kwa ajili ya chukizo.+
2 “Na itatukia katika siku hiyo,” asema Yehova wa majeshi, “kwamba nitakatilia mbali majina ya sanamu kutoka katika nchi,+ nayo hayatakumbukwa tena kamwe; nami nitaondoa pia katika nchi manabii+ na roho ya uchafu.+ 3 Na itatukia kwamba mtu akitoa unabii tena, baba yake na mama yake, waliomzaa, watamwambia pia, ‘Wewe hutaishi, kwa maana umesema uwongo katika jina la Yehova.’ Na baba yake na mama yake, waliomzaa, watamchoma kwa silaha kwa sababu ametoa unabii.+
4 “Na itatukia katika siku hiyo kwamba manabii wataona aibu,+ kila mmoja kwa sababu ya maono yake anapotoa unabii; nao hawatavaa vazi rasmi la manyoya+ kwa kusudi la kudanganya. 5 Naye atasema, ‘Mimi si nabii. Mimi ni mtu anayelima udongo, kwa sababu mtu fulani wa udongo alinichukua tangu ujana wangu.’ 6 Na mtu atamwambia, ‘Haya majeraha mwilini mwako kati ya mikono yako ni nini?’ Naye atajibu, ‘Ni yale niliyotiwa nyumbani mwa wale wanaonipenda sana.’ ”
7 “Ee upanga, amka juu ya mchungaji+ wangu, juu ya mwanamume ambaye ni mwenzangu,”+ asema Yehova wa majeshi. “Mpige mchungaji,+ na wale wa kundi watawanyike;+ nami nitageuza mkono wangu juu ya wale wasio na maana.”+
8 “Na itatukia katika nchi yote,” asema Yehova, “kwamba sehemu mbili ndani yake ndizo zitakazokatiliwa mbali na kwisha;+ lakini sehemu ya tatu itaachwa ndani yake.+ 9 Nami nitaleta sehemu hiyo ya tatu kupitia moto;+ nami nitawasafisha kama vile fedha inavyosafishwa,+ na kuwajaribu kama vile dhahabu inavyojaribiwa.+ Nayo italiitia jina langu, nami nitaijibu.+ Nitasema, ‘Ni watu wangu,’+ nayo itasema, ‘Yehova ni Mungu wangu.’ ”+
14 “Tazama! Kuna siku ambayo inakuja, siku ya Yehova,+ na nyara yenu itagawanywa katikati yenu. 2 Nami nitakusanya mataifa yote yalete vita+ juu ya Yerusalemu; na jiji hilo litatekwa+ na nyumba zitanyakuliwa, na wanawake watalalwa kinguvu.+ Na nusu ya jiji itaenda uhamishoni;+ lakini watu watakaobaki,+ hawatakatiliwa mbali kutoka katika jiji hilo.+
3 “Na Yehova ataenda na kupiga vita juu ya mataifa+ hayo kama katika siku yake ya vita, katika siku ya pigano.+ 4 Na miguu yake itasimama katika siku hiyo juu ya mlima wa mizeituni, ulioko mbele ya Yerusalemu, upande wa mashariki;+ na mlima wa mizeituni+ utapasuliwa katikati,+ kutoka mashariki na upande wa magharibi. Kutakuwa na bonde kubwa sana; na nusu ya mlima ule itasogezwa upande wa kaskazini, na nusu yake upande wa kusini. 5 Nanyi mtakimbilia bonde la milima yangu;+ kwa sababu bonde la milima hiyo litafika mpaka Aseli. Nanyi mtakimbia, kama vile mlivyokimbia kwa sababu ya lile tetemeko la nchi katika siku za Uzia mfalme wa Yuda.+ Na Yehova Mungu wangu atakuja,+ watakatifu wote wakiwa pamoja naye.+
6 “Na itatukia katika siku hiyo kwamba nuru+ yenye thamani haitakuwapo—vitu vitagandamana.+ 7 Nayo itakuwa siku moja inayojulikana kuwa ni ya Yehova.+ Haitakuwa mchana, wala haitakuwa usiku;+ na itatukia kwamba wakati wa jioni kutakuwa na nuru.+ 8 Na itatukia siku hiyo kwamba maji yaliyo hai+ yatatoka katika Yerusalemu,+ nusu yake kuelekea upande wa bahari ya mashariki+ na nusu yake kuelekea upande wa bahari ya magharibi.+ Itakuwa hivi wakati wa kiangazi na wa majira ya baridi kali.+ 9 Na Yehova atakuwa mfalme juu ya dunia yote.+ Katika siku hiyo Yehova atakuwa mmoja,+ na jina lake litakuwa moja.+
10 “Nchi yote itageuzwa na kuwa kama Araba,+ kutoka Geba+ mpaka Rimoni+ upande wa kusini wa Yerusalemu; nalo litainuka na kukaliwa na watu mahali pake,+ kutoka Lango la Benyamini+ mpaka mahali pa Lango la Kwanza, mpaka Lango la Pembeni, na kutoka Mnara wa Hananeli+ mpaka mitungi ya kushinikizia ya mfalme. 11 Na watu watakaa ndani yake; wala kutengwa kwa ajili ya maangamizi hakutatokea tena,+ na Yerusalemu litakaliwa katika usalama.+
12 “Na hii ndiyo tauni ambayo Yehova atatumia kuwapiga watu wote watakaofanya mapigano ya kijeshi juu ya Yerusalemu:+ Nyama ya mtu itaoza, huku akiwa amesimama kwa miguu yake;+ na macho ya mtu yataoza yakiwa katika matundu yake, na ulimi wake utaoza ukiwa kinywani mwake.
13 “Na itatukia katika siku hiyo kwamba mvurugo kutoka kwa Yehova utaenea katikati yao;+ na kila mmoja wao ataukamata mkono wa mwenzake, na mkono wake utainuka juu ya mkono wa mwenzake. 14 Yuda nayo pia itapiga vita katika Yerusalemu; na mali za mataifa yote kuzunguka pande zote zitakusanywa, dhahabu na fedha na mavazi kwa wingi mno.+
15 “Na hivyo ndivyo tauni ya farasi, nyumbu, ngamia, na punda-dume, na kila aina ya mnyama wa kufugwa atakayekuwa katika kambi hizo, itakavyokuwa, kama tauni hiyo.
16 “Na itatukia kwamba, kila mtu atakayebaki wa mataifa yote yanayokuja juu ya Yerusalemu,+ watapanda pia mwaka baada ya mwaka+ ili kumwinamia Mfalme,+ Yehova wa majeshi,+ na kufanya sherehe ya vibanda.+ 17 Na itatukia kwamba, yeyote asiyepanda+ kuja Yerusalemu kutoka katika familia+ za dunia ili kumwinamia Mfalme, Yehova wa majeshi, mvua haitamnyeshea.+ 18 Na watu wa familia ya Misri wasipokuja wala kuingia, mvua pia haitakuwa juu yao. Kutatokea tauni ambayo Yehova hutumia kuyapiga yale mataifa yasiyopanda kuja kufanya sherehe ya vibanda. 19 Hiyo ndiyo itakayokuwa adhabu kwa ajili ya dhambi ya Misri na dhambi ya mataifa yote yasiyopanda kuja kufanya sherehe ya vibanda.+
20 “Katika siku hiyo juu ya kengele za farasi kutakuwa na+ maneno ‘Utakatifu ni wa Yehova!’+ Na vyungu vya kupikia vyenye mdomo mpana+ vilivyo katika nyumba ya Yehova vitakuwa kama mabakuli+ yaliyo mbele ya madhabahu.+ 21 Na kila chungu cha kupikia chenye mdomo mpana katika Yerusalemu na katika Yuda kitakuwa kitu kitakatifu kwa Yehova wa majeshi, na wale wote wanaotoa dhabihu wataingia na kuchukua kutoka ndani yake na kuchemshia ndani yake.+ Na katika siku hiyo hakutakuwa na Mkanaani+ tena katika nyumba ya Yehova wa majeshi.”+