Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bi12 Malaki 1:1-4:6
  • Malaki

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Malaki
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Malaki

Malaki

1 Tangazo:

Neno la Yehova+ kuhusu Israeli kupitia Malaki:

2 “Nimewapenda ninyi,”+ Yehova amesema.

Nanyi mmesema: “Umetupenda kwa njia gani?”+

“Je, Esau hakuwa ndugu ya Yakobo?”+ asema Yehova. “Lakini nilimpenda Yakobo,+ 3 naye Esau+ nikamchukia; mwishowe nikafanya milima yake kuwa ukiwa+ na urithi wake kuwa wa mbwa-mwitu wa nyikani.”+

4 “Kwa sababu Edomu anaendelea kusema, ‘Tumevunjwa-vunjwa, lakini tutarudi na kujenga mahali palipoharibiwa,’ Yehova wa majeshi amesema hivi, ‘Wao watajenga; lakini mimi nitabomoa.+ Na watu watawaita wao kuwa “eneo la uovu” na “watu ambao Yehova ameshutumu+ mpaka wakati usio na kipimo.” 5 Na macho yenu wenyewe yataona hilo, nanyi mtasema: “Yehova na atukuzwe juu ya eneo la Israeli.” ’ ”+

6 “ ‘Mwana humheshimu baba;+ na mtumishi humheshimu bwana-mkuu wake.+ Basi ikiwa mimi ni baba,+ iko wapi heshima yangu?+ Na ikiwa mimi ni Bwana-Mkuu, uko wapi woga+ kwa ajili yangu?’ Yehova wa majeshi amewaambia ninyi, enyi makuhani mnaolidharau jina langu.+

“ ‘Nanyi mmesema: “Tumelidharau jina lako kwa njia gani?” ’

7 “ ‘Kwa kutoa juu ya madhabahu yangu mkate uliotiwa unajisi.’+

“ ‘Nanyi mmesema: “Tumekutia unajisi kwa njia gani?” ’

“ ‘Kwa kusema: “Meza+ ya Yehova ni kitu cha kudharauliwa.”+ 8 Na mnapotoa mnyama kipofu kwa ajili ya dhabihu mnasema: “Si vibaya.” Na mnapotoa mnyama kilema au mgonjwa mnasema: “Si vibaya.” ’ ”+

“Tafadhali, mleteni kwa gavana wenu. Je, atawafurahia ninyi, au je, atawapokea kwa fadhili?” Yehova wa majeshi amesema.

9 “Na sasa, tafadhali, utulizeni uso+ wa Mungu, ili apate kutuonyesha kibali.+ Jambo hilo limetoka mkononi mwenu. Je, atampokea yeyote wenu kwa fadhili?” Yehova wa majeshi amesema.

10 “Ni nani pia aliye kati yenu atakayefunga milango?+ Nanyi hamtaiwasha madhabahu yangu—bure.+ Sipendezwi nanyi hata kidogo,” Yehova wa majeshi amesema, “nami sifurahii toleo la zawadi kutoka mkononi mwenu.”+

11 “Kwa maana tangu kuchomoza kwa jua mpaka kutua kwake jina langu litakuwa kuu kati ya mataifa,+ na kila mahali moshi wa dhabihu+ utafukizwa, toleo litafanywa kwa jina langu, pia zawadi safi;+ kwa kuwa jina langu litakuwa kuu kati ya mataifa,”+ Yehova wa majeshi amesema.

12 “Lakini ninyi mnanitia unajisi+ kwa kusema, ‘Meza ya Yehova ni kitu kilichotiwa unajisi, na matunda ya meza hiyo, yaani, chakula cha meza hiyo, ni kitu cha kudharauliwa.’+ 13 Nanyi mmesema, ‘Tazama! Jambo hili linachosha kama nini!’+ nanyi mmeitolea pumzi puani kwa dharau,” Yehova wa majeshi amesema. “Nanyi mmeleta kitu ambacho kimenyakuliwa, na chenye kilema, na kilicho kigonjwa;+ ndiyo, mmekileta kama zawadi. Je, naweza kukifurahia mkononi mwenu?”+ Yehova amesema.

14 “Naye amelaaniwa anayetenda kwa ujanja wakati kuna mnyama dume katika kundi lake, naye anaweka nadhiri na kutoa dhabihu ya kilema kwa Yehova.+ Kwa maana mimi ni Mfalme mkuu,”+ Yehova wa majeshi amesema, “na jina langu litakuwa lenye kuogopesha kati ya mataifa.”+

2 “Na sasa amri hii inawahusu ninyi, enyi makuhani.+ 2 Ikiwa hamtasikiliza,+ na ikiwa hamtaiweka moyoni+ ili kulipa jina langu utukufu,”+ Yehova wa majeshi amesema, “mimi pia nitaleta juu yenu laana,+ nami nitazilaani baraka zenu.+ Ndiyo, hata nimeilaani baraka, kwa sababu hamwitii moyoni.”

3 “Tazama! Naikemea mbegu iliyopandwa kwa sababu yenu,+ nami nitawapaka mavi juu ya nyuso zenu, mavi ya sherehe zenu; na mtu fulani atawapeleka mahali ilipo. 4 Nanyi mtajua kwamba nimewapelekea ninyi amri hii,+ ili agano+ langu pamoja na Lawi liendelee,”+ Yehova wa majeshi amesema.

5 “Nalo agano langu lilikuwa naye, ambalo ni la uzima na la amani,+ nami nikaendelea kumpa hayo, pamoja na woga. Naye akaendelea kuniogopa;+ ndiyo, kwa sababu ya jina langu yeye mwenyewe aliingiwa na hofu.+ 6 Sheria ya kweli ilikuwa katika kinywa chake,+ wala ukosefu wa uadilifu haukupatikana midomoni mwake. Kwa amani na kwa unyoofu alitembea nami,+ na wale aliogeuza kutoka katika kosa walikuwa wengi.+ 7 Kwa maana midomo ya kuhani ndiyo inayopaswa kutunza ujuzi, na sheria ndiyo ambayo watu wanapaswa kutafuta kutoka kinywani mwake;+ kwa maana yeye ndiye mjumbe wa Yehova wa majeshi.+

8 “Lakini ninyi—mmegeuka kando mkaiacha njia.+ Mmesababisha wengi kujikwaa katika sheria.+ Mmeliharibu agano la Lawi,”+ Yehova wa majeshi amesema. 9 “Nami pia, kwa upande wangu, nitawafanya mdharauliwe na kuwa wa hali ya chini kwa watu wote,+ kama vile ambavyo ninyi hamkuwa mkizishika njia zangu, lakini mlikuwa mkionyesha ubaguzi katika sheria.”+

10 “Je, sisi sote hatuna baba mmoja?+ Je, sisi hatukuumbwa na Mungu mmoja?+ Kwa nini basi tunatendeana kwa hila,+ katika kutia unajisi agano la mababu zetu?+ 11 Yuda ametenda kwa hila, na chukizo limefanywa katika Israeli na katika Yerusalemu;+ kwa maana Yuda ameutia unajisi utakatifu wa Yehova,+ ambao Yeye amependa, naye amemchukua binti ya mungu wa kigeni awe bibi-arusi.+ 12 Yehova atamkatilia mbali kila mmoja anayefanya hivyo,+ yeye ambaye yuko macho na yeye anayejibu, kutoka katika mahema ya Yakobo, na yeye anayemtolea Yehova wa majeshi toleo la zawadi.”+

13 “Hili nalo ndilo jambo la pili ambalo ninyi hufanya, na matokeo yake ni madhabahu ya Yehova kufunikwa kwa machozi, kwa kulia na kuugua, hivi kwamba hakuna tena kugeukia toleo la zawadi wala kufurahia kitu chochote kutoka mkononi mwenu.+ 14 Nanyi mmesema, ‘Kwa sababu gani?’+ Kwa sababu hii, kwamba Yehova ametoa ushahidi kati yako na mke wa ujana wako,+ ambaye wewe umemtendea kwa hila, ingawa yeye ni mwenzako naye ni mke wa agano lako.+ 15 Na kuna mtu ambaye hakufanya hivyo, kwa vile alikuwa na baki la roho. Huyo naye alikuwa akitafuta nini? Uzao wa Mungu.+ Nanyi jilindeni kuhusiana na roho yenu,+ na yeyote asimtendee kwa hila mke wa ujana wake.+ 16 Kwa maana yeye amechukia talaka,”+ Yehova, Mungu wa Israeli, amesema; “na yule ambaye amefunika vazi lake kwa jeuri,”+ Yehova wa majeshi amesema. “Nanyi mjilinde roho yenu, nanyi msitende kwa hila.+

17 “Ninyi mmemchosha Yehova kwa maneno yenu,+ nanyi mmesema, ‘Tumemchosha kwa njia gani?’ Kwa kusema, ‘Kila mtu anayefanya mabaya ni mwema machoni pa Yehova, naye amependezwa na watu wa aina hiyo’;+ au, ‘Yuko wapi Mungu wa haki?’ ”+

3 “Tazama! ninamtuma mjumbe wangu,+ naye atafungua njia mbele zangu.+ Na kwa ghafula Bwana wa kweli+ atakuja kwenye hekalu Lake,+ ambaye ninyi mnamtafuta, na mjumbe+ wa agano+ mnayependezwa naye.+ Tazama! Atakuja hakika,” asema Yehova wa majeshi.+

2 “Lakini ni nani atakayeistahimili siku ya kuja kwake,+ naye ni nani atakayesimama wakati atakapoonekana?+ Kwa maana atakuwa kama moto wa msafishaji+ na kama sabuni+ ya wafuaji wa nguo.+ 3 Naye ataketi kama msafishaji na mtakasaji wa fedha+ naye atawatakasa wana wa Lawi;+ naye atawasafisha kama dhahabu+ na kama fedha, nao watakuwa kwa Yehova watu wanaotoa toleo la zawadi+ katika uadilifu. 4 Na toleo la zawadi la Yuda na la Yerusalemu litakuwa lenye kumpendeza Yehova,+ kama katika siku za zamani na kama katika miaka ya kale.+

5 “Nami nitawakaribia ninyi ili kuhukumu,+ nami nitakuwa shahidi wa haraka+ juu ya walozi,+ na juu ya wazinzi,+ na juu ya wale wanaoapa kwa uwongo,+ na juu ya wale wanaoupunja mshahara wa mfanyakazi,+ na mjane+ na mvulana asiye na baba,+ na wale wanaomfukuza mkaaji mgeni,+ wala hawakuniogopa mimi,”+ Yehova wa majeshi amesema.

6 “Kwa maana mimi ni Yehova; sikubadilika.+ Nanyi ni wana wa Yakobo; hamjafikia mwisho wenu.+ 7 Tangu siku za mababu zenu mmeyaacha masharti yangu wala hamkuyashika.+ Rudini kwangu, nami nitarudi kwenu,”+ Yehova wa majeshi amesema.

Nanyi mmesema: “Tutarudi kwa njia gani?”

8 “Je, mtu wa udongo atamnyang’anya Mungu? Lakini ninyi mnaninyang’anya mimi.”

Nanyi mmesema: “Tumekunyang’anya kwa njia gani?”

“Katika sehemu za kumi na katika michango. 9 Kwa laana mnanilaani,+ nanyi mnaninyang’anya mimi—taifa zima. 10 Leteni ghalani sehemu zote za kumi,+ ili kuwe na chakula nyumbani mwangu;+ nanyi, tafadhali, mnijaribu kwa njia hii,”+ Yehova wa majeshi amesema, “kama sitawafungulia ninyi malango ya mbinguni+ na kuwamwagia baraka hata kusiwe na uhitaji tena.”+

11 “Nami kwa ajili yenu nitakikemea kile kinachokula,+ nacho hakitawaharibia mazao ya udongo, wala mzabibu ulio shambani hautakuwa bila matunda kwenu,”+ Yehova wa majeshi amesema.

12 “Na mataifa yote yatawatangaza ninyi kuwa wenye furaha,+ kwa maana ninyi wenyewe mtakuwa nchi yenye kupendeza,”+ Yehova wa majeshi amesema.

13 “Maneno yenu yamekuwa yenye nguvu kinyume changu,”+ Yehova amesema.

Nanyi mmesema: “Sisi tumesemezana nini kinyume chako?”+

14 “Mmesema, ‘Hakuna faida kumtumikia Mungu.+ Na kwa vile tumeshika wajibu wetu kwake, na tumetembea kwa huzuni kwa sababu ya Yehova wa majeshi, kuna faida gani?+ 15 Na sasa tunawatangaza watu wenye kimbelembele kuwa wenye furaha.+ Pia, watendaji wa uovu wamejengwa.+ Wao pia wamemjaribu Mungu nao huendelea kuponyoka.’ ”+

16 Wakati huo wale wenye kumwogopa Yehova+ wakasemezana, kila mmoja na mwenzake, na Yehova akaendelea kutoa uangalifu na kusikiliza.+ Na kitabu cha kumbukumbu kikaanza kuandikwa mbele zake+ kwa ajili ya wale wenye kumwogopa Yehova na kwa ajili ya wale wanaolifikiria jina lake.+

17 “Nao watakuwa wangu,”+ Yehova wa majeshi amesema, “siku ile nitakapotokeza mali ya pekee.+ Nami nitawaonyesha huruma, kama vile mwanamume anavyomwonyesha huruma mwana wake ambaye anamtumikia.+ 18 Nanyi mtaona tena tofauti kati ya mwadilifu na mwovu,+ kati ya mtu anayemtumikia Mungu na mtu ambaye hajamtumikia.”+

4 “Kwa maana, tazama! siku ile inakuja ambayo inawaka kama tanuru,+ na wote wenye kimbelembele na wote wanaotenda uovu watakuwa kama majani makavu.+ Na siku hiyo inayokuja itawateketeza,” Yehova wa majeshi amesema, “hivi kwamba haitawaachia wao mzizi wala tawi.+ 2 Na kwenu ninyi mnaoliogopa jina langu, jua la uadilifu litaangaza,+ likiwa na kiponyaji katika mabawa yake;+ nanyi mtatoka nje na kuukanyaga udongo kama ndama waliononeshwa.”+

3 “Nanyi mtawakanyagia chini waovu, kwa maana watakuwa kama mavumbi chini ya nyayo za miguu yenu siku ile nitakayochukua hatua,”+ asema Yehova wa majeshi.

4 “Ikumbukeni sheria ya Musa mtumishi wangu niliyomwamuru katika Horebu kuhusu Israeli wote, hata masharti na maamuzi ya hukumu.+

5 “Tazama! Nawatumia ninyi nabii Eliya+ kabla ya kuja kwa ile siku ya Yehova iliyo kuu na yenye kuogopesha.+ 6 Naye atageuza moyo wa akina baba urudi kwa wana, na moyo wa wana urudi kwa akina baba; ili nisije kuipiga dunia na kuiangamiza.”+

(Mwisho wa tafsiri ya Maandiko ya Kiebrania na Kiaramu.

Tafsiri inayofuata ni ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki