Kulingana na Mathayo
1 Kitabu cha historia+ ya Yesu Kristo, mwana wa Daudi,+ mwana wa Abrahamu:+
Isaka akamzaa Yakobo;+
Yakobo akamzaa Yuda+ na ndugu zake;
3 Yuda akamzaa Perezi+ na Zera kwa Tamari;
Perezi akamzaa Hezroni;+
Hezroni akamzaa Ramu;+
4 Ramu akamzaa Aminadabu;
Aminadabu akamzaa Nashoni;+
Nashoni akamzaa Salmoni;+
5 Salmoni akamzaa Boazi kwa Rahabu;+
Boazi akamzaa Obedi kwa Ruthu;+
Obedi akamzaa Yese;+
Daudi akamzaa Sulemani+ kupitia mke wa Uria;
7 Sulemani akamzaa Rehoboamu;+
Rehoboamu akamzaa Abiya;
Yehoshafati akamzaa Yehoramu;+
Yehoramu akamzaa Uzia;
9 Uzia akamzaa Yothamu;
Ahazi akamzaa Hezekia;+
Amoni+ akamzaa Yosia;
11 Yosia+ akamzaa Yekonia+ na ndugu zake wakati wa ule uhamisho wa kwenda Babiloni.+
12 Baada ya ule uhamisho wa kwenda Babiloni Yekonia akamzaa Shealtieli;+
Shealtieli akamzaa Zerubabeli;+
13 Zerubabeli akamzaa Abiudi;
Abiudi akamzaa Eliakimu;
Eliakimu akamzaa Azori;
14 Azori akamzaa Sadoki;
Sadoki akamzaa Akimu;
Akimu akamzaa Eliudi;
15 Eliudi akamzaa Eleazari;
Eleazari akamzaa Mathani;
Mathani akamzaa Yakobo;
16 Yakobo akamzaa Yosefu mume wa Maria, ambaye kwake Yesu alizaliwa,+ anayeitwa Kristo.+
17 Basi, vizazi vyote kutoka Abrahamu mpaka Daudi vilikuwa vizazi kumi na vinne, na kutoka Daudi mpaka uhamisho wa kwenda Babiloni vizazi kumi na vinne, na kutoka uhamisho wa kwenda Babiloni mpaka Kristo vizazi kumi na vinne.
18 Lakini kuzaliwa kwa Yesu Kristo kulikuwa katika njia hii. Katika wakati ambapo Maria mama yake alikuwa amechumbiwa+ na Yosefu, alionekana kuwa ana mimba kwa njia ya roho takatifu+ kabla ya wao kuungana pamoja. 19 Hata hivyo, Yosefu mume wake, kwa sababu alikuwa mwadilifu na hakutaka kumtia aibu mbele ya watu,+ alikusudia kumtaliki+ kwa siri. 20 Lakini alipokuwa amekwisha kufikiria mambo haya, tazama! malaika wa Yehova alimtokea katika ndoto, akisema: “Yosefu, mwana wa Daudi, usiogope kumchukua Maria mke wako na kwenda naye nyumbani, kwa maana mimba iliyo ndani yake imetokana na roho takatifu.+ 21 Yeye atazaa mwana, nawe lazima umwite jina lake Yesu,+ kwa maana ataokoa+ watu wake+ kutoka katika dhambi zao.”+ 22 Yote haya kwa kweli yalitukia ili litimizwe lile lililosemwa na Yehova+ kupitia nabii wake,+ akisema: 23 “Tazama! Bikira+ atapata mimba naye atazaa mwana, nao watamwita jina lake Imanueli,”+ ambalo linapotafsiriwa humaanisha, “Mungu Yuko Pamoja Nasi.”+
24 Ndipo Yosefu akaamka kutoka katika usingizi na kufanya kama malaika wa Yehova alivyokuwa amemwagiza, naye akamchukua mke wake na kwenda naye nyumbani. 25 Lakini hakufanya ngono naye+ mpaka alipozaa mwana;+ na Yosefu akamwita jina lake Yesu.+
2 Baada ya Yesu kuzaliwa katika Bethlehemu+ ya Yudea siku za Mfalme Herode,+ tazama! wanajimu+ kutoka sehemu za mashariki walikuja Yerusalemu, 2 wakisema: “Yuko wapi yule mfalme+ wa Wayahudi aliyezaliwa? Kwa maana tuliiona nyota+ yake wakati tulipokuwa mashariki, nasi tumekuja kumsujudia.” 3 Aliposikia hilo Mfalme Herode akafadhaika, na Yerusalemu yote pamoja naye; 4 na alipowakusanya pamoja wakuu wa makuhani na waandishi wote wa watu akaanza kuuliza habari kutoka kwao juu ya ni wapi Kristo alipaswa kuzaliwa. 5 Wakamwambia: “Katika Bethlehemu+ ya Yudea; kwa maana hivi ndivyo ilivyoandikwa kupitia nabii, 6 ‘Nawe, Ee Bethlehemu+ ya nchi ya Yuda, wewe si jiji dogo zaidi kati ya magavana wa Yuda; kwa maana kutoka kwako wewe atakuja mwenye kuongoza,+ atakayewachunga+ watu wangu, Israeli.’ ”
7 Ndipo Herode akawaita wale wanajimu kwa siri na kuhakikisha kwa uangalifu kutoka kwao wakati wa kuonekana kwa ile nyota; 8 na, wakati alipokuwa akiwatuma Bethlehemu, akasema: “Nendeni mkamtafute kwa uangalifu yule mtoto mchanga, na mkiisha kumpata nileteeni habari, ili mimi vilevile nipate kwenda na kumsujudia.”+ 9 Walipokuwa wamemsikiliza mfalme, waliondoka wakaenda; na, tazama! nyota waliyokuwa wameona wakati walipokuwa mashariki+ ikaenda mbele yao, mpaka ikaja kutua juu ya mahali alipokuwa yule mtoto mchanga. 10 Walipoona ile nyota walishangilia sana. 11 Nao walipoingia ndani ya ile nyumba wakamwona huyo mtoto mchanga pamoja na Maria mama yake, wakaanguka chini na kumsujudia mtoto. Pia wakafungua hazina zao na kumtolea zawadi, dhahabu na ubani na manemane. 12 Hata hivyo, kwa sababu walipewa onyo la kimungu+ katika ndoto wasirudi kwa Herode, wakaondoka kwenda nchi yao kwa njia nyingine.
13 Walipokuwa wamekwisha kuondoka, tazama! malaika wa Yehova+ akamtokea Yosefu katika ndoto, akisema: “Simama, mchukue huyo mtoto mchanga na mama yake mkimbie kuingia Misri, mkae huko mpaka nikupe agizo; kwa maana Herode yuko karibu kumtafuta huyo mtoto amwangamize.” 14 Kwa hiyo akasimama na kuchukua pamoja naye mtoto huyo mchanga na mama yake wakati wa usiku, akaondoka na kuingia Misri, 15 naye akakaa huko mpaka kufa kwa Herode, ili litimizwe+ lile lililosemwa na Yehova kupitia nabii wake, akisema: “Kutoka Misri+ nilimwita mwanangu.”
16 Ndipo Herode, alipoona ameshindwa akili na wale wanajimu, akaingiwa na ghadhabu kubwa, akatuma watu na kuagiza wavulana wote katika Bethlehemu na katika wilaya zake zote wauawe, kuanzia umri wa miaka miwili kwenda chini, kulingana na wakati aliokuwa amehakikisha kwa uangalifu kutoka kwa wale wanajimu.+ 17 Ndipo likatimizwa lile lililosemwa kupitia nabii Yeremia, akisema: 18 “Sauti ilisikiwa katika Rama,+ kulia na kuomboleza kwingi; ni Raheli+ aliyekuwa akiwalilia watoto wake, naye hakutaka kufarijiwa, kwa sababu hawako tena.”
19 Herode alipokuwa amekufa, tazama! malaika wa Yehova akamtokea Yosefu katika ndoto+ huko Misri 20 naye akasema: “Simama, mchukue huyo mtoto mchanga na mama yake, ushike njia na kuingia katika nchi ya Israeli, kwa maana wale waliokuwa wakiitafuta nafsi ya mtoto huyo wamekufa.” 21 Kwa hiyo akasimama na kumchukua huyo mtoto mchanga na mama yake na kuingia katika nchi ya Israeli. 22 Lakini aliposikia kwamba Arkelao alikuwa akitawala akiwa mfalme wa Yudea badala ya Herode baba yake, akaogopa kuondoka kwenda huko. Zaidi ya hayo, kwa kuwa alipewa onyo la kimungu katika ndoto,+ akaondoka, akaingia eneo la Galilaya,+ 23 akaja kukaa katika jiji linaloitwa Nazareti,+ ili lipate kutimizwa lile lililosemwa kupitia manabii: “Yeye ataitwa Mnazareti.”+
3 Katika siku hizo Yohana Mbatizaji+ alikuja akihubiri katika nyika+ ya Yudea, 2 akisema: “Tubuni,+ kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia.”+ 3 Huyu, kwa kweli, ndiye anayesemwa kupitia nabii Isaya+ kwa maneno haya: “Sikilizeni! Mtu fulani anapaaza sauti nyikani, ‘Tayarisheni+ njia ya Yehova! Nyoosheni barabara zake.’ ” 4 Lakini Yohana huyu mavazi yake yalikuwa ya manyoya ya ngamia+ na alikuwa na mshipi wa ngozi+ kiunoni mwake; nacho chakula chake kilikuwa nzige+ na asali ya mwituni.+ 5 Ndipo Yerusalemu na Yudea yote na nchi yote kandokando ya Yordani zikamwendea, 6 naye akawabatiza watu katika Mto Yordani,+ wakiungama waziwazi dhambi zao.
7 Alipoona wengi wa Mafarisayo na Masadukayo+ wakija kwenye ubatizo, akawaambia: “Ninyi uzao wa nyoka-vipiri,+ ni nani ambaye amewaonyesha ninyi kuikimbia ghadhabu+ inayokuja? 8 Kwa hiyo basi zaeni matunda yanayofaa toba;+ 9 na msiseme moyoni mwenu, ‘Abrahamu ndiye baba yetu.’+ Kwa maana ninawaambia ninyi kwamba Mungu anaweza kumwinulia Abrahamu+ watoto kutoka katika mawe haya. 10 Tayari shoka+ limewekwa kwenye mzizi wa miti; basi, kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa+ na kutupwa ndani ya moto.+ 11 Mimi ninawabatiza ninyi kwa maji+ kwa sababu ya toba+ yenu; lakini yule anayekuja+ nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, ambaye viatu vyake mimi sistahili kuvivua.+ Huyo atawabatiza ninyi kwa roho takatifu+ na kwa moto.+ 12 Sepetu yake ya kupepetea imo mkononi mwake, naye atausafisha uwanja wake wa kupuria, na kukusanya ngano yake katika ghala+ lakini makapi atayateketeza kwa moto+ usioweza kuzimwa.”
13 Ndipo Yesu akaja kutoka Galilaya+ mpaka Yordani kwa Yohana, kusudi ambatize.+ 14 Lakini Yohana akajaribu kumzuia, akisema: “Mimi ndiye ninayehitaji kubatizwa na wewe, na je, wewe unakuja kwangu?” 15 Yesu akajibu, akamwambia: “Acha iwe hivyo, wakati huu, kwa maana katika njia hiyo inafaa kwetu kufanya yote yaliyo ya uadilifu.”+ Ndipo akaacha kumzuia. 16 Baada ya kubatizwa Yesu akapanda mara moja kutoka katika maji; na, tazama! mbingu zikafunguliwa,+ naye akaona roho ya Mungu ikishuka kama njiwa,+ ikija juu yake.+ 17 Tazama! Kulikuwa pia na sauti+ kutoka mbinguni iliyosema: “Huyu ni Mwanangu,+ mpendwa,+ ambaye nimemkubali.”+
4 Ndipo Yesu akaongozwa na roho kuingia nyikani+ ili kujaribiwa+ na Ibilisi. 2 Alipokuwa amefunga siku 40,+ mchana na usiku, akaona njaa. 3 Pia, Mjaribu+ akaja na kumwambia: “Ikiwa wewe ni mwana wa Mungu,+ yaambie mawe haya yawe mikate.” 4 Lakini akajibu na kusema: “Imeandikwa, ‘Mwanadamu ataishi, si kwa mkate tu, bali kwa kila neno linalotoka katika kinywa cha Yehova.’ ”+
5 Ndipo Ibilisi akamchukua, akaenda pamoja naye, na kuingia katika lile jiji takatifu,+ naye akamsimamisha juu ya mnara wa hekalu 6 na kumwambia: “Ikiwa wewe ni mwana wa Mungu, jitupe chini;+ kwa maana imeandikwa, ‘Atawaagiza malaika zake kukuhusu wewe, nao watakuchukua mikononi mwao, ili usipate kamwe kuugonga mguu wako juu ya jiwe.’ ”+ 7 Yesu akamwambia: “Tena imeandikwa, ‘Usimjaribu Yehova Mungu wako.’ ”+
8 Tena Ibilisi akamchukua, akaenda pamoja naye kwenye mlima mrefu isivyo kawaida, na kumwonyesha falme zote za ulimwengu+ na utukufu wazo, 9 naye akamwambia: “Nitakupa mambo yote haya+ ukianguka chini na kunifanyia tendo la ibada.”+ 10 Ndipo Yesu akamwambia: “Nenda zako, Shetani! Kwa maana imeandikwa, ‘Yehova Mungu wako ndiye unayepaswa kumwabudu,+ na yeye peke yake+ ndiye unayepaswa kumtolea utumishi mtakatifu.’ ”+ 11 Ndipo Ibilisi akamwacha,+ na, tazama! malaika wakaja na kuanza kumhudumia.+
12 Sasa aliposikia kwamba Yohana alikuwa amekamatwa,+ aliondoka akaingia Galilaya.+ 13 Zaidi ya hayo, baada ya kuondoka Nazareti, alikuja na kukaa katika Kapernaumu+ kando ya bahari katika wilaya za Zabuloni na Naftali,+ 14 ili lipate kutimizwa lile lililosemwa kupitia Isaya nabii, akisema: 15 “Ewe nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, kando ya barabara ya bahari, katika upande ule mwingine wa Yordani, Galilaya+ ya mataifa! 16 watu wanaokaa katika giza+ waliona nuru kuu,+ na kwa habari ya wale wanaokaa katika eneo la kivuli cha kifo, nuru+ iliwazukia.”+ 17 Kutoka wakati huo na kuendelea Yesu alianza kuhubiri na kusema: “Tubuni,+ kwa maana ufalme+ wa mbinguni umekaribia.”
18 Alipokuwa akitembea kando ya bahari ya Galilaya aliona ndugu wawili, Simoni+ anayeitwa Petro+ na Andrea ndugu yake, wakishusha wavu wa kuvulia samaki ndani ya bahari, kwa maana walikuwa wavuvi. 19 Naye akawaambia: “Nifuateni, nami nitawafanya ninyi kuwa wavuvi wa watu.”+ 20 Mara moja wakaziacha nyavu,+ wakamfuata. 21 Pia, alipoendelea mbele kutoka hapo akaona wengine wawili+ waliokuwa ndugu, Yakobo mwana wa Zebedayo+ na Yohana ndugu yake, katika mashua pamoja na Zebedayo baba yao, wakitengeneza nyavu zao, naye akawaita. 22 Mara moja wakaacha ile mashua na baba yao, wakamfuata.
23 Ndipo akaenda akizunguka+ katika Galilaya+ yote, akifundisha katika masinagogi+ yao na kuhubiri habari njema ya ufalme na kuponya kila namna ya ugonjwa+ na kila namna ya udhaifu katikati ya watu. 24 Na habari juu yake ikaenea katika Siria+ yote; nao wakamletea wote waliokuwa na hali mbaya,+ waliokuwa wakitaabishwa na magonjwa na kuteswa kwa namna mbalimbali, wenye roho waovu na wenye kifafa+ na watu waliopooza, naye akawaponya. 25 Kwa sababu hiyo umati mkubwa ukamfuata kutoka Galilaya+ na Dekapoli na Yerusalemu+ na Yudea na kutoka upande ule mwingine wa Yordani.
5 Alipouona umati akapanda mlimani; na baada ya kuketi wanafunzi wake wakamjia; 2 naye akafungua kinywa chake na kuanza kuwafundisha, akisema:
3 “Wenye furaha ni wale wanaotambua uhitaji wao wa kiroho,+ kwa kuwa ufalme wa mbinguni ni wao.+
4 “Wenye furaha ni wale wanaoomboleza, kwa kuwa watafarijiwa.+
5 “Wenye furaha ni wale walio na tabia-pole,+ kwa kuwa watairithi dunia.+
6 “Wenye furaha ni wale walio na njaa na walio na kiu+ kwa ajili ya uadilifu, kwa kuwa watashibishwa.+
7 “Wenye furaha ni wale walio na rehema,+ kwa kuwa wataonyeshwa rehema.
8 “Wenye furaha ni wale walio safi moyoni,+ kwa kuwa watamwona Mungu.+
9 “Wenye furaha ni wale wanaofanya amani,+ kwa kuwa wataitwa ‘wana+ wa Mungu.’
10 “Wenye furaha ni wale ambao wameteswa+ kwa ajili ya uadilifu, kwa kuwa ufalme wa mbinguni ni wao.
11 “Wenye furaha ni ninyi wakati watu wanapowashutumu+ na kuwatesa+ na kusema kwa uwongo kila namna ya jambo baya juu yenu kwa ajili yangu. 12 Shangilieni na kuruka kwa shangwe,+ kwa kuwa thawabu+ yenu ni kubwa mbinguni; kwa maana hivyo ndivyo walivyowatesa manabii+ waliokuwa kabla yenu.
13 “Ninyi ndio chumvi+ ya dunia; lakini chumvi ikipoteza nguvu zake, ladha yake itarudishwaje? Haitumiki tena kwa kitu chochote bali ni ya kutupwa nje+ ili ikanyagwe-kanyagwe na watu.
14 “Ninyi ndio nuru ya ulimwengu.+ Jiji haliwezi kufichwa likiwa limesimama juu ya mlima. 15 Watu huwasha taa na kuiweka, si chini ya kikapu cha kupimia,+ bali juu ya kinara cha taa, nayo huangazia watu wote waliomo ndani ya nyumba. 16 Vivyo hivyo acheni nuru+ yenu iangaze mbele ya watu, ili wapate kuona matendo yenu mazuri+ na kumpa utukufu+ Baba yenu aliye mbinguni.
17 “Msifikiri nilikuja kuharibu Sheria+ au Manabii. Sikuja kuharibu, bali kutimiza;+ 18 kwa maana kwa kweli ninawaambia ninyi kwamba mbingu na dunia zingepitilia mbali+ upesi zaidi kuliko herufi moja ndogo zaidi au nukta moja ya herufi kupitilia mbali kutoka katika Sheria na mambo yote yasitukie.+ 19 Kwa hiyo, yeyote yule anayevunja+ moja ya amri hizi ndogo zaidi na kufundisha wanadamu hivyo, yeye ataitwa ‘mdogo zaidi’ kuhusiana na ufalme wa mbinguni.+ Kwa habari ya yeyote anayezifanya na kuzifundisha,+ huyo ataitwa ‘mkubwa’+ kuhusiana na ufalme wa mbinguni. 20 Kwa maana ninawaambia ninyi kwamba ikiwa uadilifu wenu hauzidi ule wa waandishi na Mafarisayo,+ hamtaingia+ kamwe katika ufalme wa mbinguni.
21 “Ninyi mlisikia kwamba watu wa kale waliambiwa, ‘Usiue;+ lakini yeyote yule anayeua+ atatoa hesabu mahakamani.’+ 22 Hata hivyo, ninawaambia ninyi kwamba kila mtu anayeendelea kuwa na ghadhabu+ na ndugu yake atatoa hesabu+ mahakamani; lakini yeyote yule anayemwambia ndugu yake neno la dharau lisilosemeka atatoa hesabu katika Mahakama Kuu Zaidi; na yeyote yule anayesema, ‘Wewe mpumbavu wa kudharauliwa!’ atastahili Gehena* ya moto.+
23 “Basi, ikiwa unaleta zawadi yako kwenye madhabahu+ na hapo ukumbuke kwamba ndugu yako ana jambo fulani juu yako,+ 24 acha zawadi yako hapo mbele ya madhabahu, na uende zako; kwanza fanya amani yako pamoja na ndugu yako,+ na ndipo, ukiisha kurudi, itoe zawadi yako.+
25 “Uwe tayari kusuluhisha mambo upesi pamoja na mtu anayekushtaki mahakamani, wakati unapokuwa pamoja naye njiani kwenda huko, ili kwa njia fulani mlalamikaji+ asikutie mikononi mwa hakimu, naye hakimu kwa mtumishi wa mahakama, nawe utupwe ndani ya gereza. 26 Nakuambia kwa kweli, Hakika wewe hutatoka humo mpaka uwe umemaliza kulipa sarafu ya mwisho iliyo ya thamani ndogo sana.+
27 “Ninyi mlisikia kwamba ilisemwa, ‘Usifanye uzinzi.’+ 28 Lakini mimi ninawaambia ninyi kwamba kila mtu ambaye anaendelea kumtazama mwanamke+ na kumtamani tayari amefanya uzinzi+ pamoja naye moyoni mwake.+ 29 Ikiwa, sasa, hilo jicho lako la kuume linakufanya ukwazike, ling’oe ulitupilie mbali nawe.+ Kwa maana kuna faida zaidi kwako kimoja cha viungo vyako kipotee kuliko mwili wako wote utupwe+ ndani ya Gehena.* 30 Pia, mkono wako wa kuume ukikufanya ukwazike, ukate na kuutupilia mbali nawe.+ Kwa maana kuna faida zaidi kwako kimoja cha viungo vyako kipotee kuliko mwili wako wote uanguke ndani ya Gehena.*
31 “Zaidi ya hayo ilisemwa, ‘Yeyote yule anayemtaliki+ mke wake, na ampe cheti cha talaka.’+ 32 Hata hivyo, mimi ninawaambia ninyi kwamba kila mtu anayemtaliki mke wake, isipokuwa kwa sababu ya uasherati,+ anamweka katika hali ya kuweza kufanya uzinzi,+ na yeyote yule anayemwoa mwanamke aliyetalikiwa anafanya uzinzi.+
33 “Tena mlisikia kwamba watu wa kale waliambiwa, ‘Usiape+ bila kutimiza, bali lazima umtimizie Yehova nadhiri zako.’+ 34 Hata hivyo, mimi ninawaambia ninyi: Msiape+ hata kidogo, wala kwa mbingu, kwa sababu hizo ni kiti cha ufalme cha Mungu;+ 35 wala kwa dunia, kwa sababu hiyo ni kiti cha miguu yake;+ wala kwa Yerusalemu, kwa sababu hilo ni jiji+ la yule Mfalme mkuu. 36 Wala usiape kwa kichwa chako, kwa sababu huwezi kugeuza unywele mmoja kuwa mweupe au mweusi. 37 Acheni tu neno lenu Ndiyo limaanishe Ndiyo, Siyo yenu, Siyo;+ kwa maana linalozidi hayo linatoka kwa yule mwovu.+
38 “Ninyi mlisikia kwamba ilisemwa, ‘Jicho kwa jicho na jino kwa jino.’+ 39 Hata hivyo, mimi ninawaambia ninyi: Msimpinge yeye aliye mwovu; bali yeyote anayekupiga kofi kwenye shavu+ lako la kuume, mgeuzie lile lingine pia. 40 Na ikiwa mtu anataka kwenda mahakamani pamoja nawe na kulichukua vazi lako la ndani, acha alichukue vazi lako la nje pia;+ 41 na mtu fulani aliye na mamlaka akikulazimisha uingie katika utumishi wa kilometa moja, nenda pamoja naye kilometa mbili.+ 42 Mpe yeye anayekuomba, wala usimpe kisogo yule anayetaka umkopeshe bila faida.+
43 “Ninyi mlisikia kwamba ilisemwa, ‘Mpende jirani+ yako na kumchukia adui yako.’+ 44 Hata hivyo, mimi ninawaambia ninyi: Endeleeni kuwapenda adui zenu+ na kusali kwa ajili ya wale wanaowatesa ninyi;+ 45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni,+ kwa kuwa yeye hulichomoza jua lake juu ya watu waovu na wema na hunyesha mvua juu ya watu waadilifu na wasio waadilifu.+ 46 Kwa maana mkiwapenda wale wanaowapenda ninyi, mna thawabu gani?+ Je, wakusanya-kodi pia hawafanyi jambo hilohilo? 47 Na mkiwasalimu ndugu zenu tu, mnafanya jambo gani linalozidi lile la kawaida? Je, watu wa mataifa pia hawafanyi jambo hilohilo? 48 Lazima ninyi basi muwe wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.+
6 “Iweni waangalifu sana kwamba msionyeshe uadilifu+ wenu mbele ya watu kusudi mwonekane nao; ama sivyo hamtakuwa na thawabu kwa Baba yenu aliye mbinguni. 2 Kwa sababu hiyo wakati unapotoa zawadi za rehema,+ usipige tarumbeta+ mbele yako, kama vile wanafiki wanavyofanya katika masinagogi na barabarani, ili watukuzwe na watu. Kwa kweli ninawaambia ninyi, Wanapata thawabu yao kwa ukamili. 3 Lakini wewe, unapotoa zawadi za rehema, usiache mkono wako wa kushoto ujue lile ambalo mkono wako wa kuume unafanya, 4 ili zawadi zako za rehema zitolewe katika siri; ndipo Baba yako anayetazama akiwa mahali pa siri atakulipa.+
5 “Pia, wakati mnaposali, msiwe kama wanafiki; kwa sababu wanapenda kusali wakiwa wamesimama+ katika masinagogi na kwenye pembe za njia pana ili waonekane na watu.+ Kwa kweli ninawaambia ninyi, Wanapata thawabu yao kwa ukamili. 6 Lakini wewe unaposali, ingia ndani ya chumba chako cha faragha+ na, baada ya kufunga mlango wako, sali kwa Baba yako aliye mahali pa siri;+ ndipo Baba yako anayetazama akiwa mahali pa siri atakulipa. 7 Lakini mnaposali, msiseme mambo yaleyale tena na tena,+ kama vile watu wa mataifa wanavyofanya, kwa maana wao huwaza watasikiwa kwa kutumia maneno mengi. 8 Kwa hiyo, msijifanye kama wao, kwa maana Mungu Baba yenu anajua ni vitu gani mnavyohitaji+ hata kabla hamjamwomba.
“ ‘Baba yetu uliye mbinguni, jina+ lako na litakaswe.+ 10 Ufalme+ wako na uje. Mapenzi yako+ na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni.+ 11 Utupe leo mkate wetu kwa ajili ya siku hii;+ 12 na utusamehe madeni yetu, kama vile ambavyo sisi pia tumewasamehe wadeni wetu.+ 13 Na usituingize katika jaribu,+ bali utukomboe kutokana na yule mwovu.’+
14 “Kwa maana ikiwa mnawasamehe watu makosa yao, Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi pia;+ 15 lakini ikiwa hamtawasamehe watu makosa yao, Baba yenu naye hatawasamehe makosa yenu.+
16 “Wakati mnapofunga,+ msiwe na nyuso zenye huzuni kama wanafiki, kwa maana wao hukunja nyuso zao ili waonekane na watu kuwa wanafunga.+ Kwa kweli ninawaambia ninyi, Wanapata thawabu yao kwa ukamili. 17 Lakini wewe, unapofunga, paka kichwa chako mafuta na unawe uso wako,+ 18 ili uonekane kuwa unafunga, si na wanadamu, bali na Baba yako aliye mahali pa siri;+ ndipo Baba yako anayetazama akiwa mahali pa siri atakulipa.
19 “Acheni kujiwekea hazina+ duniani, ambako nondo na kutu hula, na ambako wezi huvunja na kuiba. 20 Badala yake, jiwekeeni hazina mbinguni,+ ambako nondo na kutu havili,+ na ambako wezi hawavunji na kuiba. 21 Kwa maana mahali ilipo hazina yako, ndipo moyo wako utakapokuwa pia.
22 “Taa ya mwili ni jicho.+ Basi, ikiwa jicho lako ni rahisi, mwili wako wote utakuwa mwangavu; 23 lakini ikiwa jicho lako ni bovu,+ mwili wako wote utakuwa wenye giza. Ikiwa kwa kweli nuru iliyo ndani yako ni giza, jinsi lilivyo kubwa giza hilo!+
24 “Hakuna anayeweza kuwatumikia mabwana wawili; kwa maana ama atamchukia mmoja na kumpenda yule mwingine,+ ama atashikamana na mmoja na kumdharau yule mwingine. Hamwezi kutumikia Mungu na Utajiri.+
25 “Kwa sababu hiyo ninawaambia ninyi: Acheni kuhangaika+ juu ya nafsi zenu kuhusu kile mtakachokula au kile mtakachokunywa, au juu ya miili yenu kuhusu kile mtakachovaa.+ Je, nafsi haimaanishi zaidi ya chakula na mwili zaidi ya mavazi?+ 26 Waangalieni kwa makini ndege+ wa mbinguni, kwa sababu hawapandi mbegu au kuvuna au kukusanya ghalani; na bado Baba yenu wa mbinguni huwalisha wao. Je, ninyi si bora kuliko wao?+ 27 Ni nani kati yenu kwa kuhangaika anaweza kuongeza kipimo cha mkono mmoja kwenye uhai wake?+ 28 Pia, katika lile jambo la mavazi, kwa nini mnahangaika? Jifunzeni kwa mayungiyungi+ ya shamba, jinsi yanavyokua; hayafanyi kazi, wala hayasokoti; 29 lakini ninawaambia ninyi kwamba hata Sulemani+ katika utukufu wake wote hakupambwa kama moja la haya. 30 Basi, ikiwa Mungu huivika hivyo mimea ya shambani, ambayo ipo hapa leo na kesho hutupwa ndani ya jiko, je, yeye hataona ni afadhali zaidi awavike, ninyi wenye imani kidogo?+ 31 Kwa hiyo msihangaike+ kamwe na kusema, ‘Tutakula nini?’ au, ‘Tutakunywa nini?’ au, ‘Tutavaa nini?’ 32 Kwa maana vyote hivi ndivyo vitu ambavyo mataifa yanafuatilia kwa tamaa. Kwa maana Baba yenu wa mbinguni anajua mnahitaji vitu hivi vyote.+
33 “Basi, endeleeni kuutafuta kwanza ufalme na uadilifu wake,+ nanyi mtaongezewa hivi vitu vingine vyote.+ 34 Kwa hiyo, msihangaike kamwe juu ya kesho,+ kwa maana kesho itakuwa na mahangaiko yake yenyewe. Unatosha kila siku ubaya wake.
7 “Acheni kuhukumu+ ili msihukumiwe; 2 kwa maana kwa hukumu mnayohukumu, mtahukumiwa;+ na kwa kipimo mnachopimia, watawapimia ninyi.+ 3 Basi, kwa nini unautazama unyasi ulio katika jicho la ndugu yako, lakini hulifikirii boriti lililo katika jicho lako mwenyewe?+ 4 Au unawezaje kumwambia ndugu yako, ‘Niruhusu niutoe unyasi ulio katika jicho lako’; wakati, tazama! boriti limo katika jicho lako mwenyewe?+ 5 Mnafiki! Kwanza toa boriti lililo katika jicho lako mwenyewe, na ndipo utakapoona waziwazi jinsi ya kuutoa unyasi ulio katika jicho la ndugu yako.
6 “Msiwape mbwa kitu kitakatifu,+ wala msitupe lulu zenu mbele ya nguruwe, ili wasizikanyage-kanyage+ chini ya miguu yao na kugeuka na kuwararua ninyi.
7 “Endeleeni kuomba,+ nanyi mtapewa; endeleeni kutafuta, nanyi mtapata; endeleeni kupiga hodi,+ nanyi mtafunguliwa. 8 Kwa maana kila mtu anayeomba hupokea,+ na kila mtu anayetafuta hupata, na kila mtu anayepiga hodi atafunguliwa. 9 Kwa kweli, ni nani kati yenu ambaye mwana wake+ akimwomba mkate—je, atampa jiwe? 10 Au, labda, akiomba samaki—je, atampa nyoka? 11 Kwa hiyo, ikiwa ninyi, mjapokuwa waovu,+ mnajua jinsi ya kuwapa watoto wenu zawadi zilizo nzuri, je, Baba yenu aliye mbinguni hatawapa hata zaidi vitu vyema+ wale wanaomwomba?
12 “Kwa hiyo, mambo yote mnayotaka watu wawatendee ninyi,+ lazima mwatendee wao pia vivyo hivyo; hii, kwa kweli, ndiyo maana ya Sheria na Manabii.+
13 “Ingieni kupitia lango jembamba;+ kwa sababu barabara inayoongoza kwenye uharibifu ni pana na kubwa, na wengi ndio wanaoipitia; 14 lakini lango ni jembamba na barabara inayoongoza kwenye uzima ina nafasi ndogo, na wachache ndio wanaoipata.+
15 “Jihadharini na manabii wa uwongo+ ambao wanakuja kwenu katika mavazi ya kondoo,+ lakini ndani wao ni mbwa-mwitu+ wenye kunyafua. 16 Kwa matunda yao mtawatambua.+ Je, watu hukusanya zabibu kutoka kwenye miiba au tini kutoka kwenye michongoma?+ 17 Vivyo hivyo kila mti mzuri huzaa matunda mazuri, lakini kila mti uliooza huzaa matunda yasiyofaa;+ 18 mti mzuri hauwezi kuzaa matunda yasiyofaa, wala mti uliooza hauwezi kuzaa matunda mazuri. 19 Kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa ndani ya moto.+ 20 Basi, kwa kweli kwa matunda yao mtawatambua watu hao.+
21 “Si kila mtu anayeniambia, ‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika ufalme wa mbinguni, bali yule anayefanya+ mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni ndiye atakayeingia.+ 22 Wengi wataniambia siku hiyo, ‘Bwana, Bwana,+ hatukutoa unabii katika jina lako, na kufukuza roho waovu katika jina lako, na kufanya matendo mengi yenye nguvu katika jina lako?’+ 23 Na hata hivyo nitawaambia waziwazi: Sikuwajua ninyi kamwe!+ Ondokeni kwangu, ninyi wenye matendo ya uasi-sheria.+
24 “Kwa hiyo kila mtu anayesikia maneno yangu haya na kuyatenda atafananishwa na mtu mwenye busara, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba.+ 25 Na mvua ikanyesha na mafuriko yakaja na pepo zikavuma na kuipiga nyumba hiyo, lakini haikuporomoka, kwa maana msingi wake ulikuwa umejengwa juu ya mwamba. 26 Zaidi ya hayo, kila mtu anayesikia maneno yangu haya na hayatendi+ atafananishwa na mtu mpumbavu,+ aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga. 27 Na mvua ikanyesha na mafuriko yakaja na pepo zikavuma na kuigonga nyumba hiyo,+ nayo ikaporomoka, na anguko lake lilikuwa kubwa.”+
28 Basi wakati Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, umati ukashangazwa+ na njia yake ya kufundisha; 29 kwa maana alikuwa akiwafundisha kama mtu mwenye mamlaka,+ na si kama waandishi wao.
8 Alipokwisha kushuka kutoka mlimani umati mkubwa ukamfuata. 2 Na, tazama! mtu mwenye ukoma+ akaja, akaanza kumsujudia, na kusema: “Bwana, ikiwa tu unataka, unaweza kunitakasa.” 3 Kwa hiyo, akaunyoosha mkono wake, akamgusa, na kusema: “Ninataka. Takasika.”+ Na mara moja ukoma wake ukatakasika.+ 4 Ndipo Yesu akamwambia: “Usimwambie mtu yeyote,+ bali nenda, ukajionyeshe kwa kuhani,+ na kutoa zawadi+ ambayo Musa aliagiza, ili iwe ushahidi kwao.”
5 Alipoingia Kapernaumu,+ ofisa-jeshi mmoja akamjia, akimsihi 6 na kusema: “Bwana, mtumishi wangu amelazwa nyumbani akiwa na ugonjwa wa kupooza, akiteseka vibaya sana.” 7 Akamwambia: “Nitakapofika huko nitamponya.” 8 Ofisa huyo akamjibu, akasema: “Bwana, mimi sistahili hivi kwamba wewe uingie chini ya paa yangu, lakini sema neno tu na mtumishi wangu atapona. 9 Kwa maana mimi pia niko chini ya mamlaka, nikiwa na askari-jeshi chini yangu, nami humwambia huyu, ‘Ondoka uende zako!’+ naye huondoka na kwenda zake, na kwa mwingine, ‘Njoo!’ naye huja, na kwa mtumwa wangu, ‘Fanya hili!’ naye hulifanya.” 10 Aliposikia hilo, Yesu akashangaa na kuwaambia wale waliokuwa wakimfuata: “Ninawaambia ninyi kweli, Sijapata yeyote katika Israeli mwenye imani kubwa kama hii.+ 11 Lakini ninawaambia ninyi kwamba wengi kutoka sehemu za mashariki na sehemu za magharibi+ watakuja na kuketi kwenye meza pamoja na Abrahamu na Isaka na Yakobo katika ufalme+ wa mbinguni;+ 12 lakini wana wa ufalme+ watatupwa nje katika giza. Nao watalia na kusaga meno yao huko.”+ 13 Ndipo Yesu akamwambia ofisa huyo: “Nenda. Na iwe hivyo kwako, kama vile imani yako ilivyo.”+ Na yule mtumishi akapona saa ileile.
14 Na Yesu, alipoingia ndani ya nyumba ya Petro, alimwona mama-mkwe+ wake akiwa amelala chini, akiugua homa.+ 15 Kwa hiyo akaugusa mkono+ wake, na homa ikamwacha, naye akasimama na kuanza kumhudumia.+ 16 Lakini ilipofika jioni, watu walimletea watu wengi walioingiwa na roho waovu; naye akawafukuza hao roho kwa neno moja, naye akawaponya wote waliokuwa na hali mbaya; 17 ili litimizwe lile lililosemwa kupitia nabii Isaya, akisema: “Yeye mwenyewe aliyachukua magonjwa yetu na kuyachukua maradhi yetu.”+
18 Yesu alipoona umati uliokuwa ukimzunguka, akaagiza wang’oe nanga na kwenda upande ule mwingine.+ 19 Na mwandishi fulani akatokea na kumwambia: “Mwalimu, mimi nitakufuata mahali popote unapoenda.”+ 20 Lakini Yesu akamwambia: “Mbweha wana mapango na ndege wa mbinguni wana viota, lakini Mwana wa binadamu hana mahali popote pa kulaza kichwa chake.”+ 21 Ndipo mwingine kati ya wanafunzi akamwambia: “Bwana, niruhusu kwanza niondoke nikamzike baba yangu.” 22 Yesu akamwambia: “Endelea kunifuata, waache wafu wawazike wafu wao.”+
23 Naye alipopanda ndani ya mashua,+ wanafunzi wake wakamfuata. 24 Sasa, tazama! msukosuko mkubwa ukatokea katika bahari, hivi kwamba mashua ilikuwa ikifunikwa na mawimbi; hata hivyo, yeye alikuwa amelala usingizi.+ 25 Nao wakaja na kumwamsha,+ wakisema: “Bwana, tuokoe, tuko karibu kuangamia!” 26 Lakini akawaambia: “Kwa nini mna moyo wa woga, ninyi wenye imani kidogo?”+ Ndipo, akasimama, akakemea zile pepo na hiyo bahari, kukawa utulivu mkubwa.+ 27 Kwa hiyo watu hao wakashangaa na kusema: “Mtu huyu ni wa namna gani,+ hivi kwamba hata pepo na bahari zinamtii?”
28 Alipofika upande ule mwingine, na kuingia katika nchi ya Wagadarene,+ alikutana na wanaume wawili walioingiwa na roho waovu+ wakitoka kati ya makaburi, wakali isivyo kawaida, hivi kwamba hakuna mtu aliyekuwa na moyo wa kupita katika barabara hiyo. 29 Na, tazama! wakapaaza sauti, na kusema: “Tuna nini nawe, Mwana wa Mungu?+ Je, umekuja hapa kututesa+ kabla ya wakati uliowekwa?”+ 30 Lakini kule mbali nao kulikuwako kundi la nguruwe wengi wakilisha. 31 Kwa hiyo wale roho waovu wakaanza kumsihi, wakisema: “Ukitufukuza, tutume tukaingie katika lile kundi la nguruwe.”+ 32 Basi akawaambia: “Nendeni!” Wakatoka na kwenda zao, wakaingia ndani ya wale nguruwe; na, tazama! kundi zima likatimua mbio, likaruka poromoko, likaingia baharini na kufa majini.+ 33 Lakini wachungaji wakakimbia, wakaenda jijini, na kutoa habari juu ya kila kitu, pamoja na ile habari ya wale watu walioingiwa na roho waovu. 34 Na, tazama! jiji lote likajitokeza ili kukutana na Yesu; na walipokwisha kumwona, wakamsihi aondoke katika wilaya zao.+
9 Basi, akaipanda mashua, akaanza kuvuka na kwenda katika jiji lake.+ 2 Na, tazama! wakamletea mtu aliyepooza akiwa amelala juu ya kitanda.+ Alipoona imani yao Yesu akamwambia yule mwenye kupooza: “Jipe moyo, mwanangu; dhambi zako zimesamehewa.”+ 3 Na, tazama! baadhi ya waandishi wakaambiana wao kwa wao: “Mtu huyu anakufuru.”+ 4 Naye Yesu, akijua fikira zao,+ akasema: “Kwa nini mnafikiri mambo maovu mioyoni mwenu?+ 5 Kwa mfano, ni jambo gani lililo rahisi zaidi, kusema, Dhambi zako zimesamehewa, au kusema, Simama, utembee?+ 6 Hata hivyo, ili mjue kwamba Mwana wa binadamu ana mamlaka duniani ya kusamehe dhambi+—” ndipo akamwambia yule mwenye kupooza: “Simama, chukua kitanda chako, uende nyumbani kwako.”+ 7 Naye akasimama, akaenda nyumbani kwake. 8 Umati ulipoona hilo wakaingiwa na woga, nao wakamtukuza Mungu,+ aliyewapa wanadamu mamlaka+ ya namna hiyo.
9 Halafu, alipokuwa akiondoka mahali hapo, Yesu akamwona mtu anayeitwa Mathayo akiwa ameketi kwenye ofisi ya kodi, naye akamwambia: “Uwe mfuasi wangu.”+ Akasimama mara moja na kumfuata.+ 10 Baadaye, huku akiwa ameketi mezani katika nyumba,+ tazama! wakusanya-kodi wengi na watenda-dhambi wakaja na kuanza kuketi pamoja na Yesu na wanafunzi wake. 11 Mafarisayo walipoona hilo wakaanza kuwaambia wanafunzi wake: “Kwa nini mwalimu wenu anakula pamoja na wakusanya-kodi na watenda-dhambi?”+ 12 Alipowasikia, akasema: “Watu wenye afya hawahitaji tabibu,+ bali wenye kuugua ndio wanaomhitaji. 13 Nendeni, basi, mkajifunze maana ya jambo hili, ‘Ninataka rehema, wala si dhabihu.’+ Kwa maana nilikuja kuwaita, si watu waadilifu, bali watenda-dhambi.”
14 Ndipo wanafunzi wa Yohana wakamjia na kuuliza: “Kwa nini sisi na Mafarisayo hufunga lakini wanafunzi wako hawafungi?”+ 15 Ndipo Yesu akawaambia: “Je, rafiki za bwana-arusi wana sababu ya kuomboleza, maadamu bwana-arusi+ yupo pamoja nao? Lakini siku zitakuja wakati ambapo bwana-arusi ataondolewa+ kwao, ndipo watakapofunga.+ 16 Hakuna mtu anayeshona kiraka cha nguo mpya juu ya vazi la nje la zamani; kwa maana nguvu zake zingelivuta lile vazi la nje nalo lingeraruka vibaya zaidi.+ 17 Wala watu hawaweki divai mpya ndani ya viriba vya divai vilivyozeeka; lakini wakifanya hivyo, vile viriba hupasuka na ile divai humwagika navyo viriba huharibika.+ Bali watu huweka divai mpya ndani ya viriba vipya vya divai, na vitu vyote viwili huhifadhiwa.”+
18 Alipokuwa akiwaambia mambo hayo, tazama! mtawala+ fulani aliyekuwa amekaribia, alianza kumsujudia,+ akisema: “Kufikia sasa binti yangu lazima awe amekufa;+ lakini njoo uweke mkono wako juu yake naye atakuwa hai.”+
19 Basi Yesu akaondoka, akaanza kumfuata; pia wanafunzi wake wakamfuata. 20 Na, tazama! mwanamke mwenye kutaabika miaka kumi na miwili kutokana na mtiririko wa damu+ akaja nyuma na kuugusa upindo wa vazi lake la nje;+ 21 kwa maana alikuwa akisema moyoni mwake: “Nikigusa tu vazi lake la nje nitapona.”+ 22 Yesu akageuka, akamwona, na kusema: “Jipe moyo, binti yangu; imani yako imekuponya.”+ Na kutoka saa hiyo mwanamke huyo akapona.+
23 Basi, alipoingia katika nyumba ya yule mtawala+ na kuwaona wapiga-filimbi na umati wa watu wakipiga kelele kwa kuvurugika,+ 24 Yesu akaanza kusema: “Ondokeni hapa, kwa maana msichana mdogo hakufa, bali analala usingizi.”+ Ndipo wakaanza kumcheka kwa dharau.+ 25 Mara tu umati ulipokuwa umetoka nje, akaingia na kuushika mkono wake,+ na huyo msichana akainuka.+ 26 Bila shaka, habari za jambo hilo zikaenea katika eneo hilo lote.
27 Yesu alipokuwa akipita kutoka huko, wanaume wawili vipofu+ wakamfuata, wakipaaza sauti na kusema: “Uturehemu,+ Mwana wa Daudi.” 28 Alipokuwa amekwisha kuingia katika ile nyumba, wale wanaume vipofu wakamjia, naye Yesu akawauliza: “Je, mna imani+ kwamba ninaweza kufanya hivyo?” Wakamjibu: “Ndiyo, Bwana.” 29 Ndipo akayagusa macho yao,+ akisema: “Na iwe hivyo kwenu kulingana na imani yenu.” 30 Na macho yao yakapata kuona. Zaidi ya hayo, Yesu akawaagiza kwa kusisitiza, akisema: “Msimwambie mtu yeyote jambo hilo.”+ 31 Lakini wao, baada ya kufika nje, wakajulisha habari zake katika eneo hilo lote.+
32 Sasa walipokuwa wakiondoka, tazama! watu wakamletea bubu aliyeingiwa na roho mwovu;+ 33 na yule roho mwovu alipokuwa amekwisha kufukuzwa yule bubu akaongea.+ Basi, ule umati ukashangaa+ na kusema: “Jambo kama hili halijapata kuonekana kamwe katika Israeli.” 34 Lakini Mafarisayo wakaanza kusema: “Yeye huwafukuza roho waovu kwa nguvu za mtawala wa roho waovu.”+
35 Na Yesu akaondoka ili kutembelea majiji na vijiji vyote, akifundisha katika masinagogi yao na kuhubiri habari njema ya ufalme na kuponya kila namna ya magonjwa na kila namna ya udhaifu.+ 36 Alipouona umati akawasikitikia,+ kwa sababu walikuwa wamechunwa ngozi na kutupwa huku na huku kama kondoo wasio na mchungaji.+ 37 Ndipo akawaambia wanafunzi wake: “Ndiyo, mavuno ni mengi, lakini wafanyakazi ni wachache.+ 38 Kwa hiyo, mwombeni Bwana wa mavuno awatume wafanyakazi katika mavuno yake.”+
10 Kwa hiyo akawaita wanafunzi wake kumi na wawili na kuwapa mamlaka juu ya roho wachafu,+ ili wawafukuze na kuponya kila namna ya ugonjwa na kila namna ya udhaifu.
2 Majina ya wale mitume kumi na wawili+ ndiyo haya:+ Kwanza, Simoni, anaiyeitwa Petro,+ na Andrea+ ndugu yake; na Yakobo mwana wa Zebedayo+ na Yohana ndugu yake; 3 Filipo na Bartholomayo;+ Tomasi+ na Mathayo+ mkusanya-kodi; Yakobo mwana wa Alfayo,+ na Thadayo; 4 Simoni Mkananayo,+ na Yuda Iskariote, ambaye baadaye alimsaliti.+
5 Yesu aliwatuma hao kumi na wawili, akiwapa maagizo haya:+ “Msiende katika barabara ya mataifa, na msiingie katika jiji la Wasamaria;+ 6 bali, badala ya hivyo, nendeni kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.+ 7 Mnapoenda, hubirini, mkisema, ‘Ufalme wa mbinguni umekaribia.’+ 8 Ponyeni wagonjwa,+ fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, fukuzeni roho waovu. Mlipokea bure, toeni bure.+ 9 Msichukue dhahabu wala fedha wala shaba kwa ajili ya mikoba yenu ya mshipi,+ 10 wala mfuko wa chakula kwa ajili ya safari, wala mavazi mawili ya ndani, wala viatu wala fimbo; kwa maana mfanyakazi anastahili chakula chake.+
11 “Katika jiji lolote lile au kijiji chochote kile mtakapoingia, tafuteni ni nani humo anayestahili, mkae humo mpaka mtakapoondoka.+ 12 Mnapoingia ndani ya nyumba, wapeni salamu watu wa nyumba hiyo; 13 na ikiwa nyumba hiyo inastahili, acheni amani mnayoitakia ikae juu yake;+ lakini ikiwa haistahili, acheni amani yenu irudi kwenu. 14 Popote pale ambapo mtu hawakaribishi au hasikilizi maneno yenu, mnapoondoka katika nyumba hiyo au jiji hilo yakung’uteni mavumbi kutoka miguuni penu.+ 15 Kwa kweli mimi ninawaambia ninyi, Itakuwa rahisi zaidi kwa nchi ya Sodoma+ na Gomora kwenye Siku ya Hukumu kuliko kwa jiji hilo.+
16 “Tazama! Mimi ninawatuma ninyi kama kondoo katikati ya mbwa-mwitu;+ kwa hiyo jionyesheni wenyewe kuwa wenye kujihadhari kama nyoka+ na hata hivyo wasio na hatia kama njiwa.+ 17 Jihadharini na watu;+ kwa maana watawapeleka mahakamani,+ nao watawapiga ninyi mijeledi+ katika masinagogi yao.+ 18 Naam, mtakokotwa na kupelekwa mbele ya magavana na wafalme+ kwa ajili yangu, ili kuwa ushahidi+ kwao na kwa mataifa. 19 Hata hivyo, watakapowapeleka ninyi, msihangaike juu ya jambo mtakalosema au jinsi mtakavyolisema; kwa maana mtapewa jambo la kusema katika saa hiyo;+ 20 kwa maana wanaosema si ninyi tu, bali ni roho ya Baba yenu inayosema kupitia ninyi.+ 21 Zaidi ya hayo, mtu atamtoa ndugu+ yake afe, na baba mtoto wake, na watoto watainuka juu ya wazazi na kufanya wauawe.+ 22 Nanyi mtachukiwa na watu wote kwa sababu ya jina langu;+ lakini yule atakayevumilia mpaka mwisho ndiye atakayeokolewa.+ 23 Wakati wanapowatesa ninyi katika jiji moja, kimbilieni jiji lingine;+ kwa maana kwa kweli ninawaambia ninyi, Hamtamaliza kuyazunguka+ majiji ya Israeli mpaka Mwana wa binadamu atakapofika.+
24 “Mwanafunzi hampiti mwalimu wake, wala mtumwa hampiti bwana wake.+ 25 Inatosha kwa mwanafunzi kuwa kama mwalimu wake, na mtumwa kama bwana wake.+ Ikiwa watu wamemwita mwenye nyumba Beelzebuli,+ je, hawatawaita hivyo wale watu wa nyumbani mwake hata zaidi? 26 Kwa hiyo msiwaogope; kwa maana hakuna kitu chochote kilichofunikwa ambacho hakitafunuliwa, na cha siri ambacho hakitajulikana.+ 27 Lile ninalowaambia ninyi gizani, lisemeni nuruni; na lile mnalolisikia likinong’onwa, lihubirini juu ya paa za nyumba.+ 28 Na msiwaogope+ wale ambao wanaua mwili lakini hawawezi kuiua nafsi; lakini badala ya hivyo mwogopeni+ yeye anayeweza kuangamiza vyote viwili nafsi na mwili katika Gehena.*+ 29 Je, shomoro wawili hawauzwi kwa sarafu ya thamani ndogo?+ Na bado hakuna hata mmoja wao atakayeanguka chini bila Baba yenu kujua.+ 30 Lakini nywele zenyewe za kichwa chenu zimehesabiwa zote.+ 31 Kwa hiyo msiogope: Ninyi ni bora kuliko shomoro wengi.+
32 “Basi, kila mtu anayekiri mbele ya wanadamu kwamba yuko katika umoja pamoja nami, mimi pia nitakiri mbele za Baba yangu aliye mbinguni kwamba niko katika umoja pamoja naye;+ 33 lakini yeyote yule anayenikana mimi mbele ya watu, mimi pia nitamkana+ mbele za Baba yangu aliye mbinguni. 34 Msifikiri nilikuja kuleta amani duniani; nilikuja kuleta, si amani,+ bali upanga. 35 Kwa maana nilikuja kuleta mgawanyiko, mtu kumpinga baba yake, binti kumpinga mama yake, mke aliye mchanga kumpinga mama-mkwe wake.+ 36 Kwa kweli, adui za mtu watakuwa watu wa nyumbani kwake mwenyewe. 37 Anayempenda baba au mama kuliko mimi hanistahili; naye anayempenda mwana au binti kuliko mimi hanistahili.+ 38 Na yeyote yule asiyeuchukua mti wake wa mateso na kunifuata hanistahili.+ 39 Yeye anayeipata nafsi yake ataipoteza, naye anayeipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataipata.+
40 “Yeye anayewapokea ninyi ananipokea mimi pia, naye anayenipokea mimi anampokea pia yule aliyenituma.+ 41 Anayempokea nabii kwa sababu ni nabii atapata thawabu ya nabii,+ naye anayempokea mtu mwadilifu kwa sababu ni mtu mwadilifu atapata thawabu ya mtu mwadilifu.+ 42 Na yeyote yule anayempa mmoja wa wadogo hawa kikombe tu cha maji baridi ya kunywa kwa sababu ni mwanafunzi, kwa kweli ninawaambia ninyi, huyo hatapoteza thawabu yake kamwe.”+
11 Basi Yesu alipokuwa amemaliza kuwapa maagizo wanafunzi wake kumi na wawili, aliondoka akafundishe na kuhubiri katika majiji yao.+
2 Lakini Yohana, akiwa amekwisha kusikia katika jela+ juu ya kazi za Kristo, akawatuma wanafunzi wake mwenyewe 3 na kumwambia: “Je, wewe ndiye Yule Anayekuja, au tumtarajie mwingine?”+ 4 Yesu akajibu, akawaambia: “Nendeni mkamwambie Yohana mambo mnayosikia na kuona: 5 Vipofu wanaona tena,+ vilema+ wanatembea, wenye ukoma+ wanatakaswa na viziwi+ wanasikia, wafu+ wanafufuliwa, maskini wanatangaziwa habari njema;+ 6 na mwenye furaha ni yule asiyepata ndani yangu sababu ya kukwazika.”+
7 Hao walipokuwa wameondoka na kwenda, Yesu akaanza kuuambia umati habari ya Yohana: “Mlienda nyikani kuona nini?+ Tete likitikiswa na upepo?+ 8 Basi, mlienda kuona nini? Mtu aliyevaa mavazi mororo? Kwani, wale wanaovaa mavazi mororo wamo katika nyumba za wafalme.+ 9 Basi, kwa kweli kwa nini mlitoka kwenda? Kuona nabii? Ndiyo, nawaambia ninyi, na ni zaidi ya nabii.+ 10 Huyu ndiye ambaye imeandikwa hivi kumhusu, ‘Tazama! Mimi mwenyewe ninamtuma mjumbe wangu mbele ya uso wako, ambaye atatayarisha njia yako mbele yako!’+ 11 Kwa kweli nawaambia ninyi, Kati ya wale waliozaliwa na wanawake+ hajatokea mkuu kuliko Yohana Mbatizaji; lakini mtu aliye mdogo zaidi katika ufalme+ wa mbinguni ni mkuu kuliko yeye. 12 Lakini tangu siku za Yohana Mbatizaji mpaka sasa ufalme wa mbinguni ndio mradi ambao watu wanajikaza kuufikia, na wale wanaojikaza wanaufikia.+ 13 Kwa maana wote, Manabii na Sheria, walitoa unabii mpaka kufikia Yohana;+ 14 nanyi mkitaka kukubali hili, Yeye mwenyewe ndiye ‘Eliya ambaye anakusudiwa kuja.’+ 15 Yule aliye na masikio na asikilize.+
16 “Nitakilinganisha kizazi hiki na nani?+ Ni kama watoto wachanga ambao wameketi masokoni wanaowapaazia sauti wachezaji wenzao,+ 17 wakisema, ‘Tuliwapigia ninyi filimbi, lakini hamkucheza dansi; tulitoa sauti za kuomboleza, lakini hamkujipiga-piga kwa huzuni.’+ 18 Kulingana na hilo, Yohana alikuja akiwa hali chakula wala kunywa,+ na bado watu wanasema, ‘Ana roho mwovu’; 19 Mwana wa binadamu alikuja akiwa anakula na kunywa,+ na bado watu wanasema, ‘Tazama! Mtu mlafi na mwenye mazoea ya kunywa divai, rafiki ya wakusanya-kodi na watenda-dhambi.’+ Hata hivyo, hekima huonyeshwa kuwa yenye uadilifu kwa matendo yake.”+
20 Ndipo akaanza kuyashutumu majiji ambamo nyingi za kazi zake zenye nguvu zilikuwa zimetendeka, kwa sababu hayakutubu:+ 21 “Ole wako, Korazini! Ole wako, Bethsaida!+ kwa sababu kama zile kazi zenye nguvu zingalifanyika katika Tiro na Sidoni ambazo zilifanyika ndani yenu, wangalitubu zamani za kale katika nguo ya gunia na majivu.+ 22 Kwa sababu hiyo ninawaambia ninyi, Itakuwa rahisi zaidi kwa Tiro na Sidoni katika Siku ya Hukumu+ kuliko kwenu.+ 23 Na wewe, Kapernaumu,+ je, labda utainuliwa mpaka mbinguni? Utashuka+ chini mpaka katika Kaburi;*+ kwa sababu kama zile kazi zenye nguvu zilizofanyika ndani yako zingalifanyika Sodoma, lingalidumu mpaka leo hii. 24 Kwa sababu hiyo ninawaambia ninyi, Itakuwa rahisi zaidi kwa nchi ya Sodoma katika Siku ya Hukumu kuliko kwenu.”+
25 Wakati huo Yesu akajibu, akasema: “Ninakusifu wewe hadharani, Baba, Bwana wa mbingu na dunia, kwa sababu umewaficha mambo haya wenye hekima na wenye akili na umeyafunua kwa watoto.+ 26 Ndiyo, Ee Baba, kwa sababu kufanya hivyo kulikuwa ndiyo njia iliyokubaliwa nawe. 27 Baba yangu amenipa mimi vitu vyote,+ na hakuna yeyote anayemjua Mwana kabisa ila Baba,+ wala yeyote hamjui Baba kabisa ila Mwana, na yeyote ambaye Mwana anapenda kumfunulia.+ 28 Njooni kwangu, nyote mnaotaabika na kulemewa na mizigo,+ nami nitawaburudisha ninyi. 29 Chukueni nira+ yangu na mjifunze kutoka kwangu,+ kwa maana mimi ni mwenye tabia-pole+ na mnyenyekevu moyoni, nanyi mtapata burudisho+ kwa ajili ya nafsi zenu. 30 Kwa maana nira yangu ni laini na mzigo wangu ni mwepesi.”+
12 Wakati huo Yesu akapita katikati ya mashamba ya nafaka siku ya sabato.+ Wanafunzi wake wakaona njaa na kuanza kukata masuke ya nafaka na kula.+ 2 Walipoona jambo hilo Mafarisayo wakamwambia:+ “Tazama! Wanafunzi wako wanafanya jambo ambalo si halali kufanywa katika siku ya sabato.”+ 3 Yeye akawaambia: “Je, hamjasoma alilofanya Daudi wakati yeye na wale watu waliokuwa pamoja naye walipoona njaa?+ 4 Jinsi alivyoingia ndani ya nyumba ya Mungu nao wakala mikate ya toleo,+ kitu ambacho kisheria yeye, wala wale waliokuwa pamoja naye hawakuruhusiwa+ kula, ila makuhani+ tu? 5 Au, je, hamjasoma katika Sheria+ kwamba siku za sabato makuhani katika hekalu huitendea sabato kama si takatifu na huendelea kuwa bila hatia?+ 6 Lakini ninawaambia ninyi kwamba kitu kikuu kuliko hekalu+ kiko hapa. 7 Hata hivyo, kama mngalielewa maana ya neno hili, ‘Ninataka rehema,+ wala si dhabihu,’+ msingaliwalaumu watu wasio na hatia. 8 Kwa maana Mwana wa binadamu+ ndiye Bwana wa sabato.”+
9 Baada ya kutoka hapo akaingia katika sinagogi lao; 10 na, tazama! mtu mwenye mkono uliopooza!+ Kwa hiyo ili wapate jambo la kumshitaki wakamuuliza, “Je, ni halali kuponya siku ya sabato?”+ 11 Yeye akawaambia: “Ni nani kati yenu aliye na kondoo mmoja na, kondoo huyo akianguka ndani ya shimo+ siku ya sabato, hatamshika na kumtoa nje?+ 12 Yote hayo yakifikiriwa, mwanadamu ni mwenye thamani kama nini kuliko kondoo!+ Kwa hiyo ni halali kufanya jambo zuri siku ya sabato.” 13 Ndipo akamwambia mtu huyo: “Nyoosha mkono wako.” Naye akaunyoosha, nao ukarudishwa kuwa mzima kama ule mkono mwingine.+ 14 Lakini Mafarisayo wakaenda na kufanya shauri juu yake ili wapate kumwangamiza.+ 15 Alipokwisha kujua hilo, Yesu akaondoka. Wengi pia wakamfuata, naye akawaponya wote,+ 16 lakini akawaagiza kwa kusisitiza wasifunue habari zake;+ 17 ili lipate kutimizwa lililosemwa kupitia nabii Isaya, aliyesema:
18 “Tazama! Mtumishi wangu+ ambaye nilimchagua, mpendwa wangu,+ ambaye nafsi yangu ilimkubali! Nitatia roho yangu juu yake,+ na yaliyo haki atayafanya kuwa wazi kwa mataifa. 19 Hatagombeza,+ wala hatapaaza sauti kubwa, wala yeyote hatasikia sauti yake katika njia pana. 20 Hakuna tete lililovunjika ambalo ataliponda, na hakuna utambi wa kitani unaotoa moshi atakaouzima,+ mpaka atakapoileta haki+ kwa mafanikio. 21 Kwa kweli, mataifa yatalitumainia jina lake.”+
22 Ndipo wakamletea mwanamume aliyeingiwa na roho mwovu, aliye kipofu na bubu; naye akamponya, hivi kwamba yule bubu akaongea na kuona. 23 Basi, umati wote ukavutwa na hisia na kuanza kusema:+ “Je, haielekei kuwa labda huyu ndiye Mwana wa Daudi?”+ 24 Waliposikia hilo, Mafarisayo wakasema: “Mtu huyu hatoi roho waovu ila kwa nguvu za Beelzebuli, mtawala wa roho waovu.”+ 25 Akijua fikira zao,+ akawaambia: “Kila ufalme uliogawanyika na kupingana wenyewe unaangamia,+ na kila jiji au nyumba iliyogawanyika na kupingana yenyewe haitasimama. 26 Vivyo hivyo, ikiwa Shetani anamfukuza Shetani, amegawanyika na kujipinga mwenyewe; basi, ufalme wake utasimamaje? 27 Zaidi ya hayo, ikiwa mimi ninawafukuza roho waovu kwa nguvu za Beelzebuli,+ wana wenu wanawafukuza kwa nguvu za nani? Ndiyo sababu wao watakuwa waamuzi wenu. 28 Lakini ikiwa mimi ninawatoa roho waovu kwa nguvu za roho ya Mungu, kwa kweli ufalme wa Mungu umewafikia ninyi ghafula.+ 29 Au yeyote anawezaje kuivamia nyumba ya mtu mwenye nguvu na kukamata mali zake zinazoweza kuchukuliwa, asipomfunga kwanza mtu huyo mwenye nguvu? Na ndipo atakapoipora nyumba yake.+ 30 Yeye asiyekuwa upande wangu ananipinga, naye asiyekusanya pamoja nami anatawanya.+
31 “Kwa hiyo mimi ninawaambia ninyi, Watu watasamehewa kila namna ya dhambi na kufuru, lakini hawatasamehewa kufuru juu ya roho.+ 32 Kwa mfano, yeyote yule anayesema neno baya juu ya Mwana wa binadamu, atasamehewa;+ lakini yeyote yule anayesema vibaya juu ya roho takatifu, hilo hatasamehewa, hapana, si katika mfumo huu wa mambo wala katika ule utakaokuja.+
33 “Ufanyeni mti uwe mzuri na matunda yake yawe mazuri au muufanye mti uoze na matunda yake yaoze; kwa maana kwa matunda yake mti hujulikana.+ 34 Uzao wa nyoka-vipiri,+ mnawezaje kusema mambo mema, wakati ninyi ni waovu?+ Kwa maana kinywa kinasema kutokana na mambo yaliyojaa katika moyo.+ 35 Mtu mwema hutoa mambo mema kutoka katika hazina yake njema,+ lakini mtu mwovu hutoa mambo mabaya kutoka katika hazina yake mbaya.+ 36 Ninawaambia ninyi kwamba kila neno lisilofaa ambalo watu husema, watatoa hesabu+ juu yake katika Siku ya Hukumu; 37 kwa maana kwa maneno yako utatangazwa kuwa mwadilifu, na kwa maneno yako utahukumiwa.”+
38 Ndipo baadhi ya waandishi na Mafarisayo wakamjibu, wakasema: “Mwalimu, tunataka kuona ishara kutoka kwako.”+ 39 Akajibu, akawaambia: “Kizazi kiovu na chenye uzinzi+ kinaendelea kutafuta ishara, lakini hakuna ishara kitakachopewa isipokuwa ishara ya nabii Yona.+ 40 Kwa maana kama vile Yona+ alivyokuwa katika tumbo la yule samaki mkubwa siku tatu mchana na usiku, ndivyo Mwana wa binadamu+ atakavyokuwa katika moyo wa dunia+ siku tatu mchana na usiku.+ 41 Watu wa Ninawi watasimama katika hukumu pamoja na kizazi hiki+ nao watakihukumu kuwa chenye hatia;+ kwa sababu wao walitubu juu ya lile alilohubiri Yona,+ lakini, tazama! mtu mkuu kuliko Yona yuko hapa. 42 Malkia wa kusini+ atasimama katika hukumu pamoja na kizazi hiki naye atakihukumu kuwa chenye hatia; kwa sababu alikuja kutoka miisho ya dunia kuisikia hekima ya Sulemani, lakini, tazama! mtu mkuu kuliko Sulemani yuko hapa.+
43 “Wakati roho mchafu anapomtoka mtu, hupita katika mahali pakavu akitafuta mahali pa kupumzika, na hapati popote.+ 44 Ndipo anasema, ‘Nitarudi kwenye nyumba yangu niliyoihama’; naye anapofika anaikuta haijakaliwa lakini imefagiwa ikawa safi na kupambwa. 45 Ndipo anaondoka na kwenda kuchukua roho tofauti saba walio waovu zaidi kuliko yeye mwenyewe,+ na, baada ya kuingia ndani, wao hukaa humo; na hali ya mwisho ya mtu huyo huwa mbaya zaidi kuliko ile ya kwanza.+ Hivyo ndivyo itakavyokuwa pia kwa kizazi hiki kiovu.”+
46 Alipokuwa bado akisema na umati, tazama! mama yake na ndugu zake+ wakaja na kusimama nje wakitaka kusema naye. 47 Kwa hiyo mtu fulani akamwambia: “Tazama! Mama yako na ndugu zako wamesimama nje, wakitaka kusema nawe.” 48 Akimjibu huyo mwenye kumwambia, akasema: “Mama yangu ni nani, na ndugu zangu ni nani?”+ 49 Naye akinyoosha mkono wake kuelekea wanafunzi wake, akasema: “Tazama! Mama yangu na ndugu zangu!+ 50 Kwa maana yeyote yule anayefanya mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni, huyo ndiye ndugu yangu, na dada yangu, na mama yangu.”
13 Siku hiyo Yesu, akiisha kuondoka katika ile nyumba, alikuwa ameketi kando ya bahari; 2 na umati mkubwa ukamkusanyikia, hivi kwamba akapanda ndani ya mashua na kuketi,+ na umati wote ulikuwa umesimama pwani. 3 Ndipo akawaambia mambo mengi kwa kutumia mifano, akisema: “Tazama! Mpandaji alienda kupanda;+ 4 naye alipokuwa akipanda, mbegu fulani zikaanguka kando ya barabara, na ndege wakaja na kuzila.+ 5 Nyingine zikaanguka mahali penye miamba ambapo hapakuwa na udongo mwingi, zikachipuka mara moja kwa sababu ya kutokuwa na udongo wenye kina.+ 6 Lakini jua lilipochomoza zikaungua, na kwa sababu hazikuwa na mzizi zikanyauka.+ 7 Nyingine, pia, zikaanguka katikati ya miiba, na ile miiba ikamea na kuzisonga.+ 8 Bado nyingine zikaanguka kwenye udongo mzuri nazo zikaanza kuzaa matunda,+ hii mara 100, ile 60, ile nyingine 30.+ 9 Yule aliye na masikio na asikilize.”+
10 Kwa hiyo wanafunzi wakaja na kumwambia: “Kwa nini unasema nao kwa kutumia mifano?”+ 11 Akajibu, akasema: “Ninyi mmepewa uwezo wa kuzielewa siri takatifu+ za ufalme wa mbinguni, lakini wao hawakupewa.+ 12 Kwa maana yeyote aliye na kitu, ataongezewa naye atazidishiwa;+ lakini yeyote ambaye hana, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.+ 13 Ndiyo sababu ninasema nao kwa kutumia mifano, kwa sababu, wakitazama, wanatazama bure, na wakisikia, wanasikia bure, wala hawaelewi;+ 14 na unabii wa Isaya unatimizwa kwao, ambao unasema, ‘Kusikia, mtasikia lakini hamtaelewa maana yake; na, kutazama, mtatazama lakini hamtaona.+ 15 Kwa maana moyo wa watu hawa umekuwa mgumu, nao wamesikia kwa masikio yao bila kuitikia, nao wamefunga macho yao; ili wasione kamwe kwa macho yao na kusikia kwa masikio yao na kuelewa maana kwa mioyo yao na kugeuka, nami niwaponye.’+
16 “Hata hivyo, yenye furaha ni macho+ yenu kwa sababu hayo yanaona, na masikio yenu kwa sababu hayo yanasikia. 17 Kwa maana kwa kweli ninawaambia ninyi, Manabii+ wengi na watu waadilifu walitamani kuyaona mambo mnayoyaona wala hawakuyaona,+ na kuyasikia mambo mnayoyasikia wala hawakuyasikia.+
18 “Basi, sikilizeni mfano wa yule mtu aliyepanda.+ 19 Yeyote anaposikia neno la ufalme lakini haelewi maana yake, yule mwovu+ huja na kunyakua kile ambacho kimepandwa moyoni mwake; huyo ndiye aliyepandwa kando ya barabara. 20 Na yule aliyepandwa mahali penye miamba, huyo ndiye anayelisikia neno na kulipokea mara moja kwa shangwe.+ 21 Lakini hana mzizi ndani yake bali huendelea kwa wakati fulani, na dhiki au mateso vikiisha kutokea kwa sababu ya lile neno yeye hukwazika mara moja.+ 22 Na yule aliyepandwa katikati ya miiba, huyo ndiye anayelisikia neno, lakini mahangaiko ya mfumo huu wa mambo+ na nguvu za udanganyifu wa utajiri hulisonga neno, naye huwa asiyezaa matunda.+ 23 Na yule aliyepandwa juu ya udongo mzuri, huyo ndiye anayelisikia neno na kuelewa maana yake, ambaye kwa kweli huzaa matunda na kutokeza, huyu mara 100, yule 60, yule mwingine 30.”+
24 Akawatolea mfano mwingine, akisema: “Ufalme wa mbinguni umekuwa kama mtu aliyepanda mbegu nzuri katika shamba lake.+ 25 Watu wakiwa wamelala usingizi, adui yake alikuja na kupanda magugu katikati ya ngano, naye akaondoka. 26 Wakati jani lilipoota na kuzaa matunda, magugu yalionekana pia. 27 Kwa hiyo watumwa wa mwenye nyumba wakaja na kumwambia, ‘Bwana, je, hukupanda mbegu nzuri katika shamba lako?+ Imekuwaje basi lina magugu?’+ 28 Akawaambia, ‘Adui, mtu fulani, alifanya hivyo.’+ Wakamwambia, ‘Basi, je, unataka twende kuyakusanya?’ 29 Akasema, ‘Hapana; ili, mnapoyakusanya magugu, msije mkang’oa ngano pamoja nayo. 30 Acheni zikue pamoja mpaka wakati wa mavuno; na katika majira ya mavuno nitawaambia wavunaji, Kwanza kusanyeni magugu na kuyafunga matita-matita ili kuyateketeza motoni,+ ndipo nendeni mkusanye ngano ghalani mwangu.’ ”+
31 Akawatolea mfano mwingine,+ akisema: “Ufalme wa mbinguni ni kama mbegu ya haradali,+ ambayo mtu alichukua na kupanda katika shamba lake; 32 ambayo, kwa kweli, ndiyo mbegu ndogo zaidi kuliko zote, lakini ikiisha kukua huwa ndiyo kubwa zaidi kati ya mboga zote nayo huwa mti, hivi kwamba ndege wa mbinguni+ huja na kupata makao katikati ya matawi yake.”+
33 Akawaambia mfano mwingine: “Ufalme wa mbinguni ni kama chachu,+ ambayo mwanamke alichukua na kuitia katika vipimo vikubwa vitatu vya unga, mpaka tonge lote likachacha.”
34 Yesu aliuambia umati mambo yote hayo kwa mifano. Kwa kweli, hakuwa akisema nao bila mfano;+ 35 ili litimizwe lililosemwa kupitia nabii aliyesema: “Nitakifungua kinywa changu kwa mifano, nitatangaza mambo yaliyofichwa tangu kuwekwa msingi.”+
36 Ndipo baada ya kuuruhusu umati uende akaingia ndani ya nyumba. Na wanafunzi wake wakamjia na kusema: “Tueleze ule mfano wa magugu katika shamba.” 37 Akajibu, akasema: “Mpandaji wa mbegu nzuri ni Mwana wa binadamu; 38 shamba ni ulimwengu;+ nayo mbegu nzuri, hiyo ni wana wa ufalme; lakini magugu ni wana wa yule mwovu,+ 39 na yule adui aliyepanda ni Ibilisi.+ Yale mavuno+ ni umalizio wa mfumo wa mambo,+ na wavunaji ni malaika. 40 Kwa hiyo, kama vile magugu hukusanywa na kuteketezwa kwa moto, ndivyo itakavyokuwa katika umalizio wa mfumo wa mambo.+ 41 Mwana wa binadamu atatuma malaika zake, nao watakusanya kutoka katika ufalme wake vitu vyote ambavyo husababisha kukwazika+ na watu wanaoasi sheria, 42 nao watawatupa ndani ya tanuru ya moto.+ Humo ndimo watalia na kusaga meno yao.+ 43 Wakati huo waadilifu watang’aa+ kwa uangavu kama jua+ katika ufalme wa Baba yao. Yule aliye na masikio na asikilize.+
44 “Ufalme wa mbinguni ni kama hazina iliyofichwa katika shamba, ambayo mtu aliipata na kuificha; na kwa sababu ya shangwe aliyo nayo, anaenda na kuuza+ vitu alivyo navyo na kulinunua shamba hilo.+
45 “Tena ufalme wa mbinguni ni kama mwanabiashara msafiri anayetafuta lulu nzuri. 46 Akiisha kupata lulu moja ya thamani kubwa,+ alienda zake na mara moja akauza vitu vyote alivyokuwa navyo na kuinunua.+
47 “Tena ufalme wa mbinguni ni kama wavu wa kukokota ulioshushwa ndani ya bahari na kukusanya samaki wa kila aina.+ 48 Ulipojaa waliuvuta pwani na, baada ya kuketi, wakakusanya walio wazuri+ ndani ya vyombo, lakini wasiofaa+ wakawatupilia mbali. 49 Hivyo ndivyo itakavyokuwa katika umalizio wa mfumo wa mambo: malaika watatoka kwenda na kuwatenga waovu+ kutoka katikati ya waadilifu+ 50 nao watawatupa ndani ya tanuru ya moto. Humo ndimo watalia na kusaga meno yao.+
51 “Je, mmeelewa maana ya mambo haya yote?” Wakamwambia: “Ndiyo.” 52 Ndipo akawaambia: “Ikiwa ni hivyo, kila mfundishaji wa watu wote, anapofundishwa kuhusiana na ufalme wa mbinguni,+ ni kama mtu, mwenye nyumba, ambaye hutoa katika hazina yake vitu vipya na vya zamani.”+
53 Sasa Yesu alipokuwa amemaliza mifano hiyo alitoka na kupita katikati ya nchi. 54 Na baada ya kuingia eneo lake la nyumbani+ akaanza kuwafundisha katika sinagogi lao,+ hivi kwamba wakastaajabu na kusema: “Mtu huyu alipata wapi hekima hii na kazi hizi zenye nguvu? 55 Je, huyu si mwana wa yule seremala?+ Je, mama yake haitwi Maria, na ndugu zake Yakobo na Yosefu na Simoni na Yuda? 56 Na dada zake, je, wote hawako pamoja nasi?+ Basi, mtu huyu alipata wapi mambo haya yote?”+ 57 Kwa hiyo wakaanza kukwazika kwa sababu yake.+ Lakini Yesu akawaambia: “Nabii hakosi kuheshimiwa ila katika eneo lake la nyumbani na katika nyumba yake mwenyewe.”+ 58 Naye hakufanya kazi nyingi zenye nguvu huko kwa sababu ya ukosefu wao wa imani.+
14 Wakati huo Herode, mtawala wa wilaya, akasikia habari juu ya Yesu+ 2 na kuwaambia watumishi wake: “Huyu ndiye Yohana Mbatizaji. Alifufuliwa kutoka kwa wafu, na ndiyo sababu anatenda kazi zenye nguvu.”+ 3 Kwa maana Herode alikuwa amemkamata Yohana, akamfunga na kumweka gerezani kwa sababu ya Herodia mke wa Filipo ndugu yake.+ 4 Kwa maana Yohana alikuwa akimwambia: “Si halali wewe kuwa na mwanamke huyo.”+ 5 Hata hivyo, ijapokuwa alitaka kumuua, aliuogopa umati, kwa sababu walimwona kuwa nabii.+ 6 Lakini sikukuu ya kuzaliwa+ kwa Herode ilipokuwa ikisherehekewa binti ya Herodia alicheza dansi na kumpendeza sana Herode 7 hivi kwamba akaahidi kwa kiapo kumpa chochote kile ambacho angeomba.+ 8 Ndipo yeye, chini ya mwelekezo wa mama yake, akasema: “Nipe hapa juu ya sahani kichwa cha Yohana Mbatizaji.”+ 9 Ajapokuwa na huzuni, mfalme kwa kufikiria viapo vyake na kwa ajili ya wale wenye kuketi pamoja naye akaamuru apewe hicho;+ 10 naye akatuma watu wakamkate Yohana kichwa huko gerezani. 11 Na kichwa chake kikaletwa juu ya sahani na yule mwanamwali akapewa, naye akampelekea mama yake.+ 12 Mwishowe wanafunzi wake wakaja na kuiondoa maiti na kumzika+ nao wakaja na kumjulisha Yesu. 13 Aliposikia hilo Yesu akaondoka hapo kwa mashua kwenda mahali pasipo na watu ili awe peke yake;+ lakini umati, uliposikia hilo, ukamfuata kwa miguu kutoka katika majiji.
14 Basi alipotokea akaona umati mkubwa; naye akawasikitikia,+ akaponya wagonjwa wao.+ 15 Lakini jioni ilipofika wanafunzi wake wakamjia na kusema: “Mahali hapa hapana watu na saa tayari imesonga sana; acha umati waende zao, ili wapate kwenda vijijini na kujinunulia chakula.”+ 16 Hata hivyo, Yesu akawaambia: “Si lazima waondoke: Ninyi wapeni chakula.”+ 17 Wakamwambia: “Hatuna kitu hapa ila mikate mitano na samaki wawili.”+ 18 akasema: “Vileteni hapa.” 19 Halafu akauamuru umati uketi kwenye majani naye akachukua ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akatoa baraka+ na, baada ya kuimega ile mikate, akawagawia wanafunzi, nao wanafunzi wakaugawia ule umati.+ 20 Kwa hiyo wote wakala wakashiba, nao wakaokota vipande vilivyobaki, vikapu kumi na viwili vilivyojaa.+ 21 Na bado wale waliokula walikuwa wanaume karibu elfu tano, bila kuhesabu wanawake na watoto wachanga.+ 22 Ndipo, bila kukawia, akawaagiza wanafunzi wake waipande mashua na kumtangulia kwenda upande ule mwingine, huku akiwaruhusu umati waende zao.+
23 Mwishowe, baada ya kuwaruhusu umati waende zao, akapanda mlimani akiwa peke yake ili kusali.+ Ingawa ilikuwa jioni, alikuwa huko peke yake. 24 Kufikia sasa mashua ilikuwa mamia mengi ya meta mbali na nchi kavu, ikitaabishwa sana na mawimbi,+ kwa sababu upepo ulikuwa ukivuma kinyume chao. 25 Lakini katika kipindi cha kesha la nne la usiku akawajia, akitembea juu ya bahari.+ 26 Walipomwona akitembea juu ya bahari, wanafunzi wakahangaika, wakisema: “Ni mzuka!”+ Nao wakapaaza sauti katika woga wao. 27 Lakini Yesu akasema nao mara moja kwa maneno haya: “Jipeni moyo, ni mimi;+ msiogope.” 28 Petro akajibu, akamwambia: “Bwana, ikiwa ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji.” 29 Akasema: “Njoo!” Petro akashuka mara moja kutoka kwenye mashua,+ akatembea juu ya maji na kumwendea Yesu. 30 Lakini akiitazama ile dhoruba ya upepo, akaogopa na, alipoanza kuzama, akapaaza sauti: “Bwana, niokoe!” 31 Mara moja Yesu akaunyoosha mkono wake, akamshika na kumwambia: “Wewe mwenye imani kidogo, kwa nini umekuwa na shaka?”+ 32 Na baada ya kupanda katika mashua, dhoruba ya upepo ikapunguka. 33 Ndipo wale waliokuwa ndani ya mashua wakamsujudia, wakisema: “Wewe kwa kweli ni Mwana wa Mungu.”+ 34 Nao wakavuka na kuja kwenye nchi kavu katika Genesareti.+
35 Walipomtambua, watu wa mahali hapo wakapeleka habari katika nchi yote hiyo jirani, na watu wakamletea wale wote waliokuwa wagonjwa.+ 36 Nao wakaanza kumsihi ili wapate kuugusa tu upindo wa vazi lake la nje;+ na wale wote waliougusa wakapona kabisa.
15 Ndipo Mafarisayo na waandishi kutoka Yerusalemu+ wakamjia Yesu, wakasema: 2 “Kwa nini wanafunzi wako huvunja mapokeo ya watu wa zamani? Kwa mfano, hawanawi mikono yao kabla ya kula.”+
3 Akajibu, akawaambia: “Kwa nini ninyi pia huvunja amri ya Mungu kwa sababu ya mapokeo yenu?+ 4 Kwa mfano, Mungu alisema, ‘Mheshimu baba yako na mama yako’;+ na, ‘Yule anayemtukana baba yake au mama yake na afe.’+ 5 Lakini ninyi husema, ‘Yeyote anayemwambia baba yake au mama yake: “Chochote nilicho nacho unachoweza kufaidika nacho kutoka kwangu ni zawadi iliyowekwa wakfu kwa Mungu,” 6 asimheshimu baba yake hata kidogo.’+ Na kwa hiyo ninyi mmelibatilisha neno la Mungu kwa sababu ya mapokeo yenu.+ 7 Ninyi wanafiki,+ Isaya+ kwa kufaa alitoa unabii juu yenu, aliposema, 8 ‘Watu hawa huniheshimu kwa midomo yao, bali moyo wao umepelekwa mbali nami.+ 9 Wao huniabudu bure, kwa sababu wao hufundisha amri za wanadamu kuwa mafundisho.’ ”+ 10 Ndipo akauita umati karibu na kuwaambia: “Sikilizeni na mwelewe maana:+ 11 Mtu hatiwi unajisi na kile kinachoingia ndani ya kinywa chake; bali kinachotoka katika kinywa chake ndicho humtia unajisi.”+
12 Ndipo wanafunzi wakaja na kumwambia: “Je, unajua kwamba Mafarisayo walikwazika waliposikia uliyosema?”+ 13 Akajibu, akasema: “Kila mmea ambao Baba yangu wa mbinguni hakuupanda utang’olewa.+ 14 Waacheni. Wao ni viongozi vipofu. Basi, ikiwa kipofu anamwongoza kipofu, wote wawili wataanguka ndani ya shimo.”+ 15 Petro akamjibu, akamwambia: “Tufafanulie mfano huo.”+ 16 Ndipo akasema: “Je, ninyi pia bado hamwelewi?+ 17 Je, hamjui kwamba kila kitu kinachoingia katika kinywa hupita ndani ya matumbo na huondolewa na kuingia katika shimo la choo? 18 Hata hivyo, mambo yanayotoka katika kinywa hutoka moyoni, na mambo hayo humtia mtu unajisi.+ 19 Kwa mfano, mawazo mabaya hutoka moyoni,+ mauaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushuhuda wa uwongo, makufuru.+ 20 Hayo ndiyo mambo yanayomtia mtu unajisi; lakini kula bila kunawa mikono hakumtii mtu unajisi.”+
21 Sasa Yesu akatoka hapo, akaondoka na kuingia katika sehemu za Tiro na Sidoni,+ 22 Na, tazama! mwanamke Mfoinike+ kutoka katika maeneo hayo akatoka na kupaaza sauti kubwa, akisema: “Uwe na rehema juu yangu,+ Bwana, Mwana wa Daudi. Binti yangu anasumbuliwa sana na roho mwovu.” 23 Lakini yeye hakumjibu neno lolote mwanamke huyo. Kwa hiyo wanafunzi wake wakaja na kuanza kumwomba: “Mwache aende zake; kwa sababu anaendelea kupaaza sauti akitufuata nyuma.” 24 Akajibu, akasema: “Sikutumwa kwa wowote ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.”+ 25 Mwanamke huyo alipokuja akaanza kumsujudia, akisema: “Bwana, nisaidie!”+ 26 Akajibu, akasema: “Si sawa kuuchukua mkate wa watoto na kuwatupia mbwa wadogo.” 27 Yeye akasema: “Ndiyo, Bwana; lakini kwa kweli hao mbwa wadogo hula sehemu ya makombo yanayoanguka kutoka kwenye meza ya mabwana zao.”+ 28 Ndipo Yesu akamjibu, akasema: “Ewe mwanamke, imani yako ni kubwa; acha itendeke kwako kama unavyotaka.” Na binti yake akaponywa tangu saa hiyo na kuendelea.+
29 Kisha kutoka hapo, Yesu akavuka nchi, akaja karibu na bahari ya Galilaya,+ na, baada ya kupanda mlimani,+ akaketi huko. 30 Ndipo umati mkubwa ukamkaribia, wakiwa pamoja na watu waliokuwa viwete, vilema, vipofu, mabubu, na wengine wengi, nao wakawaweka miguuni pake, naye akawaponya;+ 31 hivi kwamba umati wakashangaa walipoona mabubu wakisema na viwete wakitembea na vipofu wakiona, nao wakamtukuza Mungu wa Israeli.+
32 Lakini Yesu akawaita wanafunzi wake na kusema:+ “Ninausikitikia+ umati, kwa sababu tayari wamekaa pamoja nami siku tatu nao hawana chakula; nami sitaki kuwaacha waende zao wakiwa wamefunga. Huenda wakazimia barabarani.” 33 Hata hivyo, wanafunzi wakamwambia: “Katika mahali hapa pasipo na watu tutapata wapi mikate ya kutosha kuushibisha umati huu mkubwa?”+ 34 Ndipo Yesu akawaambia: “Mna mikate mingapi?” Wakasema: “Saba, na samaki wadogo wachache.” 35 Kwa hiyo, baada ya kuuagiza umati uketi chini, 36 akachukua ile mikate saba na wale samaki na, baada ya kushukuru, akamega na kuanza kuwagawia wanafunzi, nao wanafunzi wakawagawia umati.+ 37 Na wote wakala na kushiba, nao wakaokota vipande vilivyobaki, vikapu saba vya chakula vilivyojaa.+ 38 Na bado wale waliokula walikuwa wanaume elfu nne, bila kuhesabu wanawake na watoto wachanga. 39 Mwishowe, baada ya kuacha umati waende zao, akaingia katika mashua na kwenda katika maeneo ya Magadani.+
16 Ndipo Mafarisayo+ na Masadukayo wakamkaribia na, ili kumjaribu, wakamwomba awaonyeshe ishara kutoka mbinguni.+ 2 Akajibu, akawaambia: “[[Inapokuwa jioni ninyi huwa na desturi ya kusema, ‘Kutakuwa na hali nzuri ya hewa, kwa maana anga ni jekundu’; 3 na asubuhi, ‘Kutakuwa na baridi kali, na mvua leo, kwa maana anga ni jekundu, na lenye mawingu mazito.’ Mnajua jinsi ya kufasiri kuonekana kwa anga, lakini ishara za nyakati hamwezi kuzifasiri.]]+ 4 Kizazi kiovu na chenye uzinzi kinaendelea kutafuta ishara, lakini hakuna ishara ambayo kitapewa+ ila ile ishara ya Yona.”+ Ndipo akawaacha, akaenda zake.+
5 Sasa wanafunzi wakavuka mpaka ule upande mwingine na kusahau kuichukua mikate.+ 6 Yesu akawaambia: “Endeleeni kufungua macho yenu na kujihadhari na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo.”+ 7 Kwa hiyo wakaanza kujadiliana, wakisema: “Hatukuchukua mikate yoyote.” 8 Akijua hilo, Yesu akasema: “Kwa nini mnajadiliana, kwa sababu hamna mikate, ninyi wenye imani kidogo?+ 9 Je, bado hamwelewi maana, au je, hamkumbuki ile mikate mitano katika kisa cha wale elfu tano na ni vikapu vingapi mlivyookota?+ 10 Au ile mikate saba katika kisa cha wale elfu nne na ni vikapu vingapi vya chakula mlivyookota?+ 11 Imekuwaje kwamba hamfahamu kwamba sikuongea nanyi juu ya mikate? Bali jihadharini na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo.”+ 12 Ndipo wakafahamu kwamba alisema juu ya kujihadhari, si na chachu ya ile mikate, bali na mafundisho+ ya Mafarisayo na Masadukayo.
13 Sasa alipoingia katika sehemu za Kaisaria Filipi, Yesu akaanza kuwauliza wanafunzi wake: “Watu wanasema Mwana wa binadamu ni nani?”+ 14 Wakasema: “Baadhi yao husema Yohana Mbatizaji,+ wengine Eliya,+ na wengine bado Yeremia au mmoja wa manabii.” 15 Akawaambia: “Ingawa hivyo, ninyi mnasema mimi ni nani?”+ 16 Simoni Petro akajibu, akasema: “Wewe ndiye Kristo,+ Mwana wa Mungu aliye hai.”+ 17 Yesu akajibu, akamwambia: “Mwenye furaha ni wewe, Simoni mwana wa Yona, kwa sababu nyama na damu havikukufunulia hilo, bali Baba yangu aliye mbinguni ndiye aliyekufunulia.+ 18 Pia, ninakuambia, Wewe ni Petro,+ na juu ya mwamba huu+ nitajenga kutaniko langu, na malango ya Kaburi*+ hayatalizidi nguvu.+ 19 Nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni, na lolote utakalofunga duniani litakuwa jambo lililofungwa mbinguni, na lolote utakalofungua duniani litakuwa jambo lililofunguliwa mbinguni.”+ 20 Ndipo akawaagiza wanafunzi kwa kusisitiza wasimwambie yeyote kwamba yeye ni Kristo.+
21 Tangu wakati huo na kuendelea Yesu Kristo akaanza kuwaonyesha wanafunzi wake kwamba ni lazima aende Yerusalemu na kupatwa na mambo mengi kutoka kwa wanaume wazee na wakuu wa makuhani na waandishi, na kuuawa, na siku ya tatu afufuliwe.+ 22 Ndipo Petro akamchukua kando na kuanza kumkemea, akisema: “Jitendee kwa fadhili, Bwana; wewe hutapatwa hata kidogo na jambo hili.”+ 23 Lakini akamgeuzia mgongo wake, akamwambia Petro: “Nenda nyuma yangu, Shetani!+ Wewe ni kikwazo kwangu, kwa sababu wewe unafikiri, si fikira za Mungu,+ bali za wanadamu.”
24 Ndipo Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Mtu yeyote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe na kuuchukua mti wake wa mateso na kunifuata sikuzote.+ 25 Kwa maana yeyote yule anayetaka kuiokoa nafsi yake ataipoteza; lakini yeyote yule anayeipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataipata.+ 26 Kwa maana mtu atapata faida gani akiupata ulimwengu wote lakini aipoteze nafsi yake?+ au mtu atatoa nini ili aipate+ nafsi yake? 27 Kwa maana Mwana wa binadamu anakusudiwa kuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake, na ndipo atakapomlipa kila mmoja kulingana na mwenendo wake.+ 28 Kwa kweli ninawaambia ninyi kwamba kuna baadhi ya wale wanaosimama hapa ambao hawataonja kifo kamwe mpaka kwanza wamwone Mwana wa binadamu akija katika ufalme wake.”+
17 Siku sita baadaye Yesu aliwachukua Petro na Yakobo na Yohana ndugu yake akawapandisha katika mlima mrefu wakiwa peke yao.+ 2 Sura yake ikageuka mbele yao, na uso wake ukang’aa kama jua,+ na mavazi yake ya nje yakang’aa kama nuru.+ 3 Na, tazama! Musa na Eliya wakawatokea, wakiongea naye.+ 4 Petro akamjibu, akamwambia Yesu: “Bwana, ni vizuri kwetu kuwa hapa. Ukitaka, nitasimamisha mahema matatu hapa, moja lako na moja la Musa na moja la Eliya.”+ 5 Alipokuwa bado akisema, tazama! wingu jangavu liliwafunika, na, tazama! kulikuwa na sauti kutoka katika lile wingu, ikisema: “Huyu ni Mwanangu, mpendwa, ambaye nimemkubali;+ msikilizeni.”+ 6 Waliposikia hilo wanafunzi wakaanguka kifudifudi na kuogopa sana.+ 7 Ndipo Yesu akaja karibu, akawagusa, na kusema: “Simameni na msiogope.”+ 8 Walipoinua macho yao, hawakumwona yeyote ila Yesu mwenyewe tu.+ 9 Na walipokuwa wakishuka kutoka mlimani, Yesu akawaamuru, akisema: “Msimwambie mtu yeyote maono hayo mpaka Mwana wa binadamu afufuliwe kutoka kwa wafu.”+
10 Hata hivyo, wanafunzi wakamuuliza swali hili: “Basi, kwa nini waandishi husema kwamba lazima Eliya aje kwanza?”+ 11 Akajibu, akasema: “Eliya, kwa kweli, anakuja naye atarudisha mambo yote.+ 12 Hata hivyo, mimi ninawaambia ninyi kwamba tayari Eliya amekuja nao hawakumtambua bali walimtendea mambo waliyotaka. Katika njia hiyo pia Mwana wa binadamu atateseka mikononi mwao.”+ 13 Ndipo wanafunzi wakafahamu kwamba alikuwa akiwaambia juu ya Yohana Mbatizaji.+
14 Nao walipofika mahali ulipokuwa umati,+ mtu fulani akamkaribia, akampigia magoti, na kusema: 15 “Bwana, uwe na rehema juu ya mwanangu, kwa sababu ana kifafa na ni mgonjwa, kwa maana yeye huanguka ndani ya moto na ndani ya maji mara nyingi;+ 16 nami nilimleta kwa wanafunzi wako, lakini hawakuweza kumponya.”+ 17 Yesu akajibu, akasema: “Enyi kizazi kisicho na imani na kilichopotoka,+ nitaendelea kuwa pamoja nanyi mpaka wakati gani? Nitawavumilia ninyi mpaka wakati gani? Mleteni hapa.” 18 Ndipo Yesu akamkemea, na huyo roho mwovu akamtoka;+ naye mvulana akapona tangu saa hiyo.+ 19 Ndipo wanafunzi wakamjia Yesu faraghani na kusema: “Kwa nini sisi hatukuweza kumfukuza?”+ 20 Akawaambia: “Ni kwa sababu ya imani yenu kidogo, kwa maana kwa kweli ninawaambia, Mkiwa na imani inayotoshana na mbegu ya haradali, mtauambia mlima huu, ‘Ondoka hapa uende pale,’ nao utaondoka, na hakuna jambo litakalowashinda.”+ 21 —
22 Walipokuwa wamekusanyika pamoja katika Galilaya, Yesu akawaambia: “Mwana wa binadamu atasalitiwa mikononi mwa watu,+ 23 nao watamuua, na siku ya tatu atafufuliwa.”+ Kwa hiyo wakahuzunika sana.+
24 Walipofika Kapernaumu watu wanaokusanya kodi ya drakma mbili wakamkaribia Petro na kusema: “Je, mwalimu wenu halipi kodi ya drakma mbili?”+ 25 Akasema: “Analipa.” Hata hivyo, alipoingia ndani ya nyumba Yesu akamtangulia kusema: “Unaonaje, Simoni? Wafalme wa dunia hupokea ushuru au kodi ya kichwa kutoka kwa nani? Kutoka kwa wana wao au kutoka kwa wageni?” 26 Aliposema: “Kutoka kwa wageni,” Yesu akamwambia: “Basi, kwa kweli wana hawalipi kodi. 27 Lakini ili tusiwakwaze,+ wewe nenda baharini, utupe ndoano, na kuchukua samaki wa kwanza atakayetokea, ukifungue kinywa chake, nawe utapata sarafu ya stateri. Ichukue na uwape kwa ajili yangu na kwa ajili yako.”+
18 Katika saa hiyo wanafunzi wakamkaribia Yesu na kusema: “Ni nani kwa kweli aliye mkuu zaidi katika ufalme wa mbinguni?”+ 2 Basi, akamwita mtoto mchanga, akamweka katikati yao+ 3 na kusema: “Kwa kweli ninawaambia ninyi, Msipogeuka na kuwa kama watoto wachanga,+ hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.+ 4 Basi, yeyote atakayejinyenyekeza+ mwenyewe kama mtoto huyu mchanga ndiye aliye mkuu zaidi katika ufalme wa mbinguni;+ 5 na yeyote yule anayempokea mtoto mchanga kama huyu kwa msingi wa jina langu ananipokea mimi pia.+ 6 Lakini yeyote anayemkwaza mmoja wa hawa wadogo wanaoniamini, ingekuwa afadhali afungiwe shingoni jiwe la kusagia+ kama lile ambalo huzungushwa na punda na azamishwe katika bahari kuu.+
7 “Ole wake ulimwengu kwa sababu ya vikwazo! Bila shaka, vikwazo hivyo lazima vije,+ lakini ole wake mtu ambaye kikwazo + huja kupitia kwake! 8 Basi, ikiwa mkono wako au mguu wako unakufanya ukwazike, ukate na kuutupa mbali nawe;+ ni afadhali uingie katika uzima ukiwa kilema au ukiwa kiwete kuliko kutupwa ndani ya moto wa milele ukiwa na mikono miwili au miguu miwili.+ 9 Pia, ikiwa jicho lako linakufanya ukwazike, ling’oe na kulitupa mbali nawe; ni afadhali uingie katika uzima ukiwa na jicho moja kuliko kutupwa katika Gehena* ya moto ukiwa na macho mawili.+ 10 Angalieni msimdharau mmoja wa hawa wadogo; kwa maana ninawaambia ninyi kwamba malaika zao+ mbinguni sikuzote huuona uso wa Baba yangu aliye mbinguni.+ 11 —
12 “Mnaonaje? Mtu akiwa na kondoo 100 na mmoja apotee,+ je, hatawaacha wale 99 milimani na kuondoka kwenda kumtafuta yule anayepotea?+ 13 Naye akimpata, hakika ninawaambia ninyi, yeye humshangilia huyo zaidi kuliko wale 99 ambao hawakupotea.+ 14 Vivyo hivyo Baba yangu aliye mbinguni hatamani kwamba mmoja wa wadogo hawa aangamie.+
15 “Zaidi ya hayo, ndugu yako akitenda dhambi, nenda ufunue kosa lake kati yako na yeye peke yake.+ Akikusikiliza, umempata ndugu yako.+ 16 Lakini asiposikiliza, chukua pamoja nawe mmoja au wawili zaidi, ili kwa kinywa cha mashahidi wawili au watatu kila jambo lipate kuthibitishwa.+ 17 Asipowasikiliza hao, liambie kutaniko. Ikiwa halisikilizi hata kutaniko, mwache awe kwako kama mtu wa mataifa+ na kama mkusanya-kodi.+
18 “Kwa kweli ninawaambia ninyi, Mambo yoyote mtakayofunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni, na mambo yoyote mtakayofungua duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni.+ 19 Tena kwa kweli ninawaambia ninyi, Wawili kati yenu wakikubaliana duniani kuhusu jambo lolote lenye maana ambalo wanapaswa kuomba, litatendeka kwao kwa sababu ya Baba yangu aliye mbinguni.+ 20 Kwa maana palipo na wawili au watatu wakiwa wamekusanyika pamoja katika jina langu,+ hapo mimi nipo katikati yao.”+
21 Ndipo Petro akaja na kumwambia: “Bwana, ndugu yangu atanitendea dhambi mara ngapi nami nimsamehe?+ Mpaka mara 7?”+ 22 Yesu akamwambia: “Ninakuambia, si, Mpaka mara 7, bali, Mpaka mara 77.+
23 “Ndiyo sababu ufalme wa mbinguni umekuwa kama mtu, mfalme,+ aliyetaka kufanya hesabu+ pamoja na watumwa wake. 24 Alipoanza kuzifanya, mtu ambaye alikuwa na deni lake la talanta elfu kumi [=dinari 60,000,000] akaletwa. 25 Lakini kwa sababu hakuwa na uwezo wa kulipa, bwana wake akaagiza yeye na mke wake na watoto wake na vitu vyote alivyokuwa navyo wauzwe na malipo yatolewe.+ 26 Ndipo mtumwa huyo akaanguka chini na kuanza kumsujudia, akisema, ‘Uwe na subira kwangu nami nitakulipa kila kitu.’ 27 Akisikitishwa na hayo, bwana wa mtumwa huyo akamwachilia+ na kufuta deni lake.+ 28 Lakini mtumwa huyo akatoka, akamkuta mmoja wa watumwa wenzake aliyekuwa na deni lake la dinari+ mia moja; akamkamata, akamkaba koo, akisema, ‘Lipa deni lako lote.’ 29 Basi mtumwa mwenzake akaanguka chini na kuanza kumsihi, akisema, ‘Uwe na subira+ kwangu nami nitakulipa.’ 30 Hata hivyo, yeye hakutaka, bali akaenda zake na kufanya atupwe gerezani mpaka alipe deni lake. 31 Kwa hiyo, watumwa wenzake walipoona mambo yaliyokuwa yametendeka, wakahuzunika sana, nao wakaenda na kumweleza bwana wao mambo yote yaliyokuwa yametendeka.+ 32 Ndipo bwana wake akamwita na kumwambia, ‘Mtumwa mwovu, nilifuta lile deni lote kwa ajili yako, uliponisihi. 33 Haikukupasa wewe, nawe, kuwa na rehema+ juu ya mtumwa mwenzako, kama mimi pia nilivyokuwa na rehema+ juu yako?’ 34 Ndipo bwana wake, akiwa na ghadhabu,+ akamtia mikononi mwa walinzi wa jela, mpaka alipe deni lake lote. 35 Vivyo hivyo+ Baba yangu wa mbinguni atashughulika nanyi pia ikiwa kila mmoja wenu hatamsamehe ndugu yake kutoka moyoni mwake.”+
19 Basi Yesu alipokuwa amemaliza maneno hayo, akaondoka Galilaya na kuja kwenye mipaka ya Yudea ng’ambo ya Yordani.+ 2 Pia, umati mkubwa ukamfuata, naye akawaponya huko.+
3 Na Mafarisayo wakamjia, wakikusudia kumjaribu na kusema: “Je, ni halali mwanamume kumtaliki mke wake kwa kila sababu?”+ 4 Akajibu, akasema: “Je, hamkusoma kwamba yeye aliyewaumba hao kutoka mwanzo aliwafanya mwanamume na mwanamke+ 5 na kusema, ‘Kwa sababu hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake+ naye atashikamana na mke wake, na hao wawili watakuwa mwili mmoja’?+ 6 Hivi kwamba wao si wawili tena, bali mwili mmoja. Kwa hiyo, kile ambacho Mungu ameunganisha mtu yeyote asikitenganishe.”+ 7 Wakamwambia: “Basi, kwa nini Musa aliagiza kutoa cheti cha kufukuza na kumtaliki?”+ 8 Akawaambia: “Musa, kwa kufikiria ugumu wenu wa moyo,+ aliwapa ruhusa ya kuwataliki wake zenu, lakini haikuwa hivyo kutoka mwanzo.+ 9 Ninawaambia kwamba mtu yeyote anayemtaliki mke wake na kumwoa mwingine, ila kwa sababu ya uasherati, anafanya uzinzi.”+
10 Wanafunzi wakamwambia: “Ikiwa hivyo ndivyo ilivyo kati ya mwanamume na mke wake, ni afadhali kutooa.”+ 11 Akawaambia: “Si watu wote wanaolipa nafasi neno hilo, ila tu wale walio na hiyo zawadi.+ 12 Kwa maana kuna matowashi waliozaliwa namna hiyo kutoka katika tumbo la uzazi la mama yao,+ na kuna matowashi waliofanywa matowashi na watu, na kuna matowashi ambao wamejifanya wenyewe matowashi kwa sababu ya ufalme wa mbinguni. Yule anayeweza kulipa nafasi na alipe nafasi.”+
13 Ndipo akaletewa watoto wachanga, ili aweke mikono yake juu yao na kutoa sala; lakini wanafunzi wakawakemea.+ 14 Hata hivyo, Yesu akasema: “Waacheni watoto wachanga, na acheni kuwazuia wasinijie, kwa maana ufalme wa mbinguni ni wa watu walio kama wao.”+ 15 Naye akaweka mikono yake juu yao, akaondoka hapo.+
16 Sasa, tazama! mtu fulani akamjia na kusema: “Mwalimu, nifanye wema gani ili niupate uzima wa milele?”+ 17 Akamwambia: “Kwa nini unaniuliza juu ya lililo jema?+ Kuna mmoja tu aliye mwema. Ingawa hivyo, ikiwa unataka kuingia katika uzima, zishike amri sikuzote.”+ 18 Akamwambia: “Amri gani?”+ Yesu akasema: “Naam, Usiue,+ Usifanye uzinzi,+ Usiibe,+ Usitoe ushahidi wa uwongo,+ 19 Mheshimu baba yako na mama yako,+ na, Mpende jirani yako kama wewe mwenyewe.”+ 20 Huyo kijana akamwambia: “Nimeyashika yote hayo; ni nini bado ninachokosa?” 21 Yesu akamwambia: “Ikiwa unataka kuwa mkamilifu, nenda ukauze mali zako na uwape maskini nawe utakuwa na hazina mbinguni,+ kisha uje uwe mfuasi wangu.”+ 22 Huyo kijana aliposikia maneno hayo, akaenda zake akiwa amehuzunika, kwa maana alikuwa na mali nyingi.+ 23 Lakini Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Kwa kweli ninawaambia ninyi kwamba itakuwa vigumu kwa tajiri kuingia katika ufalme wa mbinguni.+ 24 Tena ninawaambia ninyi, Ni rahisi zaidi ngamia kupita katika tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.”+
25 Wanafunzi waliposikia hilo, wakashangaa sana, wakisema: “Ni nani kwa kweli anayeweza kuokolewa?”+ 26 Akiwatazama usoni, Yesu akawaambia: “Kwa wanadamu jambo hilo haliwezekani, lakini kwa Mungu mambo yote yanawezekana.”+
27 Ndipo Petro akamjibu na kumwambia: “Tazama! Tumeacha vitu vyote na kukufuata wewe; kwa kweli kutakuwa na nini kwa ajili yetu?”+ 28 Yesu akawaambia: “Kwa kweli ninawaambia ninyi, Katika uumbaji-mpya Mwana wa binadamu atakapoketi juu ya kiti chake cha ufalme chenye utukufu, ninyi ambao mmenifuata mtaketi pia juu ya viti vya ufalme kumi na viwili, mkiyahukumu yale makabila kumi na mawili ya Israeli.+ 29 Na kila mtu ambaye ameacha nyumba au ndugu au dada au baba au mama au watoto au mashamba kwa ajili ya jina langu atapokea mara nyingi zaidi naye atarithi uzima wa milele.+
30 “Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho na wa mwisho watakuwa wa kwanza.+
20 “Kwa maana ufalme wa mbinguni ni kama mtu, mwenye nyumba, aliyetoka asubuhi na mapema kwenda kuajiri wafanyakazi kwa ajili ya shamba lake la mizabibu.+ 2 Alipokuwa amekubaliana na wafanyakazi hao awalipe dinari moja kwa siku,+ akawatuma katika shamba lake la mizabibu. 3 Akatoka pia karibu saa tatu,+ akaona wengine wasio na kazi wakiwa wamesimama sokoni;+ 4 akawaambia hao, ‘Ninyi pia, nendeni katika shamba la mizabibu, nami nitawapa kilicho haki.’ 5 Kwa hiyo wakaenda. Tena akatoka karibu saa sita+ na saa tisa+ na kufanya vivyo hivyo. 6 Mwishowe, karibu saa kumi na moja akatoka, akakuta wengine wakiwa wamesimama, naye akawaambia, ‘Kwa nini mmekuwa mkisimama hapa mchana wote bila kazi?’ 7 Wakamwambia, ‘Kwa sababu hakuna mtu ambaye ametuajiri.’ Akawaambia, ‘Ninyi pia nendeni katika shamba la mizabibu.’+
8 “Ilipofika jioni,+ bwana wa shamba la mizabibu akamwambia msimamizi wake, ‘Waite wafanyakazi na kuwalipa mshahara wao,+ ukianza na yule wa mwisho mpaka yule wa kwanza.’ 9 Wale watu wa saa kumi na moja walipokuja, wakapokea kila mmoja dinari moja. 10 Kwa hiyo, wale wa kwanza walipokuja, wakakata kauli kwamba wangepokea zaidi; lakini wao pia wakalipwa dinari moja. 11 Walipoipokea wakaanza kumnung’unikia mwenye nyumba+ 12 na kusema, ‘Hawa wa mwisho walifanya kazi kwa saa moja; na bado umewafanya kuwa sawa na sisi tuliofanya kazi ngumu mchana kutwa katika lile joto lenye kuchoma!’ 13 Lakini akamjibu mmoja wao, akasema, ‘Mwenzangu, sikutendei kosa. Tulikubaliana dinari moja, sivyo?+ 14 Chukua kilicho chako uende. Ninataka kumpa huyu wa mwisho sawasawa na wewe.+ 15 Je, si halali kwangu kufanya kile ninachotaka na vitu vyangu mwenyewe? Au jicho lako ni ovu+ kwa sababu mimi ni mwema?’+ 16 Vivyo hivyo walio wa mwisho watakuwa wa kwanza, na walio wa kwanza watakuwa wa mwisho.”+
17 Alipokuwa akikaribia kupanda kwenda Yerusalemu, Yesu akawapeleka wale wanafunzi kumi na wawili+ faraghani na kuwaambia wakiwa barabarani: 18 “Tazameni! Tunapanda kwenda Yerusalemu, na Mwana wa binadamu atatiwa mikononi mwa wakuu wa makuhani na waandishi, nao watamhukumia kifo,+ 19 na watamtia mikononi mwa watu wa mataifa wamdhihaki na kumpiga mijeledi na kumtundika+ juu ya mti, na siku ya tatu atafufuliwa.”+
20 Ndipo mama ya wana wa Zebedayo+ akamkaribia akiwa pamoja na wanawe, akamsujudia na kuomba kitu fulani kutoka kwake.+ 21 Akamuuliza: “Unataka nini?” Akamjibu: “Toa agizo ili hawa wanangu wawili waketi, mmoja upande wako wa kuume na mmoja upande wako wa kushoto, katika ufalme wako.”+ 22 Yesu akamjibu, akasema: “Hamjui kile mnachoomba. Je, mnaweza kunywa kikombe+ ambacho niko karibu kunywa?” Wakamwambia: “Tunaweza.” 23 Akawaambia: “Kwa kweli mtakunywa kikombe changu,+ lakini kuketi upande wangu wa kuume na upande wangu wa kushoto sina haki ya kutoa, bali wataketi wale ambao Baba yangu amewatayarishia.”+
24 Wale wengine kumi waliposikia jambo hilo, wakawaghadhibikia hao ndugu wawili.+ 25 Lakini Yesu akawaita, akasema: “Mnajua kwamba watawala wa mataifa hupiga ubwana juu yao na wakuu hutumia mamlaka juu yao.+ 26 Hivyo sivyo ilivyo katikati yenu;+ bali yeyote anayetaka kuwa mkubwa katikati yenu lazima awe mhudumu wenu,+ 27 na yeyote anayetaka kuwa wa kwanza katikati yenu lazima awe mtumwa wenu.+ 28 Kama vile Mwana wa binadamu alivyokuja, si kuhudumiwa, bali kuhudumu+ na kutoa nafsi yake kuwa fidia badala ya wengi.”+
29 Sasa walipokuwa wakienda kutoka Yeriko+ umati mkubwa ukamfuata. 30 Na, tazama! wanaume wawili vipofu walikuwa wameketi kando ya barabara, waliposikia kwamba Yesu anapitia hapo, wakapaaza sauti, wakisema: “Bwana, uturehemu, Mwana wa Daudi!”+ 31 Lakini umati ukasisitiza kuwaambia wakae kimya; na bado wakapaaza sauti kubwa hata zaidi, wakisema: “Bwana, uturehemu, Mwana wa Daudi!”+ 32 Kwa hiyo Yesu akasimama, akawaita na kusema: “Mnataka niwatendee nini?” 33 Wakamwambia: “Bwana, tunataka macho yetu yafunguliwe.”+ 34 Yesu akawasikitikia, akayagusa macho yao,+ na mara moja wakapata kuona, nao wakamfuata.+
21 Basi, walipokaribia Yerusalemu na kufika Bethfage katika Mlima wa Mizeituni, Yesu akawatuma wawili kati ya wanafunzi wake,+ 2 akawaambia: “Shikeni njia mkaingie katika kijiji mnachokiona mbele yenu, nanyi mara moja mtakuta punda amefungwa, na mwana-punda pamoja naye; wafungueni na kuwaleta kwangu.+ 3 Na mtu akiwaambia jambo lolote, semeni, ‘Bwana anawahitaji.’ Ndipo atawaacha mara moja.”
4 Kwa kweli hilo lilitukia ili litimizwe lililosemwa kupitia nabii, akisema: 5 “Mwambieni binti Sayuni, ‘Tazama! Mfalme wako anakuja kwako,+ mwenye tabia-pole,+ naye amepanda juu ya punda, ndiyo, juu ya mwana-punda, uzao wa mnyama wa kubeba mizigo.’ ”+
6 Kwa hiyo wanafunzi wakaondoka, wakaenda na kufanya kama vile Yesu alivyowaagiza. 7 Nao wakamleta huyo punda na mwana-punda wake, nao wakaweka juu yao mavazi yao ya nje, naye akaketi juu yake.+ 8 Walio wengi katika umati wakatandaza mavazi+ yao ya nje barabarani, nao wengine wakaanza kukata matawi kutoka kwenye miti na kuyatandaza barabarani.+ 9 Na ule umati, wale waliokuwa wakienda mbele yake na wale waliokuwa wakifuata wakawa wakipaaza sauti: “Mwokoe Mwana wa Daudi, tunaomba!+ Aliyebarikiwa ni yule anayekuja katika jina la Yehova!+ Mwokoe, tunaomba, katika vilele vilivyo juu!”+
10 Basi alipoingia Yerusalemu,+ jiji lote likawa na msukosuko, na kusema: “Ni nani huyu?” 11 Umati ukawa ukisema: “Huyu ndiye nabii+ Yesu, kutoka Nazareti ya Galilaya!”
12 Na Yesu akaingia katika hekalu na kuwafukuza wale wote waliokuwa wakiuza na kununua katika hekalu, na kuzipindua meza za wale waliokuwa wakibadili pesa na viti vya wale waliokuwa wakiuza njiwa.+ 13 Naye akawaambia: “Imeandikwa, ‘Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala,’+ lakini ninyi mnaifanya kuwa pango la wanyang’anyi.”+ 14 Pia, vipofu na vilema wakamwendea hekaluni, naye akawaponya.
15 Wakuu wa makuhani na waandishi walipoyaona mambo ya kustaajabisha aliyofanya+ na wale wavulana waliokuwa wakipaaza sauti katika hekalu na kusema: “Mwokoe Mwana wa Daudi, tunaomba!”+ wakaghadhibika 16 na kumwambia: “Je, unasikia mambo ambayo hawa wanasema?” Yesu akawaambia: “Ndiyo. Je, ninyi hamkusoma hili kamwe,+ ‘Kutoka katika kinywa cha watoto na wanaonyonya umetoa sifa’?”+ 17 Naye akawaacha, akaenda nje ya jiji mpaka Bethania na kukaa huko usiku.+
18 Alipokuwa akirudi jijini asubuhi na mapema, aliona njaa.+ 19 Naye akaona mtini kando ya barabara na kuuendea, lakini hakukuta kitu+ juu yake ila majani tu, naye akauambia: “Usizae matunda yoyote tena kamwe, milele.”+ Nao mtini ukanyauka mara moja. 20 Lakini wanafunzi walipoona hilo, wakastaajabu, wakasema: “Imewezekanaje mtini ukanyauka mara moja?”+ 21 Yesu akajibu, akawaambia: “Kwa kweli ninawaambia ninyi, Ikiwa tu mna imani nanyi msitie shaka,+ hamtafanya nililofanya kwa mtini huo tu, bali pia mkiuambia mlima huu, ‘Ondoka, ukatupwe baharini,’ jambo hilo litatukia.+ 22 Na mambo yote mnayoomba katika sala, mkiwa na imani, mtapokea.”+
23 Basi alipoingia ndani ya hekalu, wakuu wa makuhani na wanaume wazee wa watu wakamjia alipokuwa akifundisha, nao wakasema:+ “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Na ni nani aliyekupa mamlaka hiyo?”+ 24 Yesu akajibu, akawaambia: “Mimi pia, nitawauliza ninyi jambo moja. Mkiniambia jambo hilo, mimi pia nitawaambia ninyi ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani:+ 25 Ule ubatizo wa Yohana, ulitoka wapi? Mbinguni au kwa wanadamu?”+ Lakini wakaanza kujadiliana kati yao wenyewe, wakisema: “Tukisema, ‘Ulitoka mbinguni,’ atatuambia, ‘Basi, kwa nini hamkumwamini?’+ 26 Hata hivyo, tukisema, ‘Ulitoka kwa wanadamu,’ tunaogopa umati,+ kwa maana wao wote wanamwona Yohana kuwa nabii.”+ 27 Kwa hiyo wakamjibu Yesu, wakasema: “Hatujui.” Yeye naye akawaambia: “Wala mimi siwaambii ninyi ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani.+
28 “Mnaonaje? Mtu alikuwa na watoto wawili.+ Akamwendea wa kwanza, akasema, ‘Mwanangu, leo nenda ukafanye kazi katika shamba la mizabibu.’ 29 Akajibu, akasema, ‘Nitaenda,+ bwana,’ lakini hakuenda. 30 Akamwendea yule wa pili, akasema jambo hilohilo. Naye akamjibu, akasema, ‘Sitaenda.’ Baadaye akajuta,+ akaenda. 31 Ni yupi kati ya hao wawili aliyefanya mapenzi ya baba yake?”+ Wakasema: “Huyo wa pili.” Yesu akawaambia: “Kwa kweli ninawaambia kwamba wakusanya-kodi na makahaba wanawatangulia ninyi kuingia katika ufalme wa Mungu. 32 Kwa maana Yohana alikuja kwenu katika njia ya uadilifu,+ lakini hamkumwamini.+ Hata hivyo, wakusanya-kodi na makahaba walimwamini,+ nanyi, ijapokuwa mliona hilo, hamkujuta baadaye ili kumwamini.
33 “Sikilizeni mfano mwingine: Kulikuwa na mtu, mwenye nyumba,+ aliyepanda shamba la mizabibu, akaweka ua kulizunguka, akachimba shinikizo la divai ndani yake, akasimamisha mnara,+ akalikodisha kwa wakulima, kisha akasafiri kwenda ng’ambo.+ 34 Majira ya matunda yalipofika, akawatuma watumwa wake kwa wakulima wakapate matunda yake. 35 Hata hivyo, wakulima wakawachukua watumwa wake, wakampiga mmoja sana, mwingine wakamuua, mwingine wakampiga kwa mawe.+ 36 Tena akawatuma watumwa wengine, zaidi ya wale wa kwanza, lakini wakawatendea vivyo hivyo.+ 37 Mwishowe akamtuma mwana wake kwao, akisema, ‘Watamheshimu mwanangu.’ 38 Walipomwona mwana wakulima wakasemezana, ‘Huyu ndiye mrithi;+ njooni, acheni tumuue na kuupata urithi wake!’+ 39 Kwa hiyo wakamchukua na kumtupa nje ya shamba la mizabibu na kumuua.+ 40 Basi, mwenye shamba la mizabibu atakapokuja, atawatendea nini wakulima hao?” 41 Wakamwambia: “Kwa sababu wao ni waovu, atawaharibu+ hao vibaya na kulikodisha shamba la mizabibu kwa wakulima wengine, ambao watampa matunda kwa wakati wake.”+
42 Yesu akawaambia: “Je, hamkusoma kamwe katika Maandiko, ‘Jiwe ambalo wajenzi walilikataa+ ndilo limekuwa jiwe kuu la pembeni.+ Limetokana na Yehova, nalo ni la kustaajabisha machoni petu’? 43 Ndiyo sababu ninawaambia ninyi, Ufalme wa Mungu utachukuliwa kutoka kwenu na kupewa taifa lenye kuzaa matunda yake.+ 44 Pia, mtu atakayeangukia jiwe hilo atavunjika-vunjika. Na yeyote ambaye litamwangukia, litamponda-ponda.”+
45 Basi wakuu wa makuhani na Mafarisayo walipokuwa wamesikia mifano yake, wakajua kwamba alikuwa akisema juu yao.+ 46 Lakini, ijapokuwa walikuwa wakitafuta kumkamata, waliogopa umati, kwa sababu walimwona kuwa nabii.+
22 Yesu akawajibu kwa kuwaambia mifano tena, akisema:+ 2 “Ufalme wa mbinguni umekuwa kama mtu, mfalme, aliyefanya karamu ya ndoa+ kwa ajili ya mwana wake. 3 Naye akatuma watumwa wake wawaite wale walioalikwa kwenye karamu ya ndoa,+ lakini hawakutaka kuja.+ 4 Tena akawatuma watumwa wengine,+ akisema, ‘Waambieni wale walioalikwa: “Tazama! Nimetayarisha chakula changu cha mchana,+ ng’ombe-dume wangu na wanyama waliononeshwa wamechinjwa, na vitu vyote viko tayari. Njooni kwenye karamu ya ndoa.” ’+ 5 Lakini wakaenda zao bila kujali, mmoja kwenye shamba lake mwenyewe, mwingine kwenye kazi yake ya biashara;+ 6 lakini wale wengine wakawashika watumwa wake, wakawatendea kwa dharau na kuwaua.+
7 “Lakini mfalme akawa na ghadhabu, akayatuma majeshi yake na kuwaangamiza wauaji hao na kulichoma jiji lao.+ 8 Ndipo akawaambia watumwa wake, ‘Karamu ya ndoa kwa kweli iko tayari, lakini wale walioalikwa hawakustahili.+ 9 Kwa hiyo nendeni kwenye barabara zinazotoka jijini, na mtu yeyote mtakayemkuta mwalikeni kwenye karamu ya ndoa.’+ 10 Basi watumwa hao wakaenda barabarani na kuwakusanya wote waliowakuta, waovu na wema pia;+ na chumba cha sherehe za arusi kikajaa watu wenye kuketi+ mezani.
11 “Mfalme alipoingia kuwakagua wageni walioalikwa akamwona hapo mtu ambaye hakuwa amevaa vazi la ndoa.+ 12 Kwa hiyo akamwambia, ‘Mwenzangu, uliingiaje humu bila kuvaa vazi la ndoa?’+ Akakosa la kusema. 13 Ndipo mfalme akawaambia watumishi wake, ‘Mfungeni mikono na miguu na kumtupa gizani, kule nje. Huko ndiko atalia na kusaga meno yake.’+
14 “Kwa maana wanaoalikwa ni wengi, lakini wanaochaguliwa ni wachache.”+
15 Ndipo Mafarisayo wakaondoka, wakaenda na kushauriana pamoja kusudi wamtege kwa maneno yake.+ 16 Basi wakawatuma wanafunzi wao kwake, pamoja na wafuasi wa chama cha Herode,+ wakisema: “Mwalimu, tunajua wewe una ukweli nawe hufundisha njia ya Mungu katika kweli, na hujali mtu yeyote, kwa maana wewe hutazami sura ya mtu.+ 17 Kwa hiyo, tuambie, Unaonaje? Je, ni halali kumlipa Kaisari kodi au hapana?”+ 18 Lakini Yesu, akiujua uovu wao, akasema: “Kwa nini mnanijaribu, enyi wanafiki?+ 19 Nionyesheni sarafu ya kodi ya kichwa.” Wakamletea dinari. 20 Naye akawaambia: “Sanamu hii na mwandiko huu ni za nani?”+ 21 Wakasema: “Ni za Kaisari.” Ndipo akawaambia: “Basi, mlipeni Kaisari vitu vya Kaisari, lakini Mungu vitu vya Mungu.”+ 22 Basi, waliposikia hilo, wakastaajabu, wakamwacha na kwenda zao.+
23 Siku hiyo Masadukayo, wale ambao husema hakuna ufufuo, wakamjia na kumuuliza:+ 24 “Mwalimu, Musa alisema, ‘Mtu yeyote akifa bila kuwa na watoto, ndugu yake amwoe mke wake na kumwinulia ndugu yake uzao.’+ 25 Basi kulikuwa na ndugu saba; naye wa kwanza akaoa na kufa, na, kwa kuwa hakuwa na uzao, akamwachia ndugu yake mke wake.+ 26 Ikawa vivyo hivyo pia kwa yule wa pili na yule wa tatu, mpaka wote saba.+ 27 Mwishowe yule mwanamke akafa. 28 Kwa hiyo, katika ufufuo, atakuwa mke wa nani kati ya hao saba? Kwa maana alikuwa mke wao wote.”+
29 Yesu akawajibu, akawaambia: “Ninyi mnakosea, kwa sababu hamjui Maandiko wala nguvu za Mungu;+ 30 kwa maana katika ufufuo wanaume hawaoi wala wanawake hawaolewi,+ bali wao ni kama malaika mbinguni. 31 Kwa habari ya ufufuo wa wafu, je, hamkusoma mliloambiwa na Mungu, akisema,+ 32 ‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu na Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo’?+ Yeye ni Mungu, si wa wafu, bali wa walio hai.”+ 33 Waliposikia hilo, umati wakastaajabishwa na mafundisho yake.+
34 Baada ya Mafarisayo kusikia kwamba alikuwa amewanyamazisha kimya Masadukayo, wakakusanyika pamoja katika kikundi kimoja. 35 Na mmoja wao, mwenye ujuzi wa Sheria,+ akauliza, akimjaribu: 36 “Mwalimu, amri iliyo kuu katika ile Sheria ni gani?”+ 37 Akamwambia: “ ‘Lazima umpende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote.’+ 38 Hii ndiyo amri iliyo kuu na ya kwanza. 39 Ya pili, kama hiyo, ni hii, ‘Mpende jirani yako kama wewe mwenyewe.’+ 40 Sheria yote na Manabii hutegemea amri hizo mbili.”+
41 Na Mafarisayo walipokuwa wamekusanyika pamoja, Yesu akawauliza:+ 42 “Mna maoni gani kuhusu Kristo? Ni mwana wa nani?” Wakamwambia: “Wa Daudi.”+ 43 Akawaambia: “Basi, kwa nini Daudi akiongozwa na roho+ anamwita ‘Bwana,’ akisema, 44 ‘Yehova alimwambia Bwana wangu: “Keti kwenye mkono wangu wa kuume mpaka niwaweke adui zako chini ya miguu yako” ’?+ 45 Kwa hiyo, ikiwa Daudi anamwita ‘Bwana,’ inawezekanaje kwamba yeye ni mwana wake?”+ 46 Na hakuna mtu aliyeweza kumjibu hata neno moja, na tangu siku hiyo na kuendelea hakuna mtu yeyote aliyethubutu tena kumuuliza swali.+
23 Ndipo Yesu akasema na umati na wanafunzi wake,+ akisema: 2 “Waandishi+ na Mafarisayo wamejiketisha katika kiti cha Musa.+ 3 Kwa hiyo mambo yote wanayowaambia ninyi,+ yafanyeni na kuyashika, lakini msifanye kulingana na matendo yao,+ kwa maana wao husema lakini hawatendi. 4 Wao hufunga mizigo mizito na kuiweka juu ya mabega ya watu,+ lakini wao wenyewe hawataki kuisogeza kwa kidole chao.+ 5 Kazi zote wanazozifanya wao huzifanya ili watazamwe na watu;+ kwa maana wanapanua vibweta+ vyenye maandiko ambavyo wao huvaa kama ulinzi, na kuongeza ukubwa wa pindo zenye nyuzinyuzi+ za mavazi yao. 6 Wao hupenda mahali penye kuonekana zaidi+ kwenye milo ya jioni na viti vya mbele katika masinagogi,+ 7 na salamu+ katika masoko na kuitwa Rabi na watu.+ 8 Lakini ninyi, msiitwe Rabi, kwa maana mwalimu+ wenu ni mmoja, lakini ninyi nyote ni ndugu. 9 Zaidi ya hayo, msimwite mtu yeyote baba yenu duniani, kwa maana Baba+ yenu ni mmoja, Yule wa mbinguni. 10 Wala msiitwe ‘viongozi,’+ kwa maana Kiongozi wenu ni mmoja, Kristo. 11 Lakini aliye mkubwa zaidi katikati yenu lazima awe mhudumu wenu.+ 12 Yeyote yule anayejiinua atanyenyekezwa,+ na yeyote yule anayejinyenyekeza atainuliwa.+
13 “Ole wenu ninyi, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! kwa sababu mnawafungia+ watu ufalme wa mbinguni; kwa maana ninyi+ wenyewe hamwingii, wala hamwaruhusu wale wanaoenda huko waingie. 14 ——
15 “Ole wenu ninyi, waandishi na Mafarisayo, wanafiki!+ kwa sababu mnasafiri katika bahari na katika nchi kavu ili kugeuza imani ya mtu mmoja, na anapogeuka ninyi humfanya astahili Gehena* mara mbili zaidi kuliko ninyi wenyewe.
16 “Ole wenu ninyi, viongozi vipofu,+ mnaosema, ‘Mtu yeyote akiapa kwa hekalu, si kitu; lakini mtu yeyote akiapa kwa dhahabu ya hekalu, atakuwa na wajibu.’+ 17 Wapumbavu na vipofu! Kwa kweli, ni kipi kilicho kikubwa zaidi, dhahabu au hekalu ambalo limeitakasa dhahabu?+ 18 Pia, ‘Mtu yeyote akiapa kwa madhabahu, si kitu; lakini mtu yeyote akiapa kwa zawadi iliyo juu yake, atakuwa na wajibu.’ 19 Vipofu! Kwa kweli, ni kipi kilicho kikubwa zaidi, zawadi au madhabahu+ ambayo huitakasa zawadi? 20 Kwa hiyo yeye anayeapa kwa madhabahu anaapa kwa hiyo na kwa vitu vyote vilivyo juu yake; 21 naye anayeapa kwa hekalu anaapa kwa hilo na kwa yeye anayekaa ndani yake;+ 22 naye anayeapa kwa mbingu anaapa kwa kiti cha ufalme cha Mungu+ na kwa yeye anayeketi juu yake.
23 “Ole wenu ninyi, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! kwa sababu ninyi huitoa sehemu ya kumi+ ya mnanaa na dili na bizari, lakini mmepuuza mambo mazito zaidi ya Sheria, yaani, haki+ na rehema+ na uaminifu.+ Ilikuwa lazima kuyafanya mambo haya, na bado kutopuuza yale mambo mengine. 24 Viongozi vipofu,+ ambao humchuja mbu+ lakini hummeza ngamia!+
25 “Ole wenu ninyi, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! kwa sababu ninyi husafisha upande wa nje wa kikombe+ na wa sahani, lakini upande wa ndani vimejaa vitu vilivyoporwa+ na mambo yenye kupita kiasi. 26 Farisayo kipofu,+ kwanza safisha upande wa ndani wa kikombe+ na wa sahani, ili upande wake wa nje upate kuwa safi pia.
27 “Ole wenu ninyi, waandishi na Mafarisayo, wanafiki!+ kwa sababu mnafanana na makaburi yaliyopakwa chokaa,+ ambayo kwa nje yanaonekana kwa kweli kuwa mazuri lakini ndani yamejaa mifupa ya wafu na kila namna ya ukosefu wa usafi. 28 Katika njia hiyo ninyi pia, kwa kweli, mnaonekana kwa nje kuwa waadilifu kwa watu,+ lakini ndani mmejaa unafiki na uasi-sheria.
29 “Ole wenu ninyi, waandishi na Mafarisayo, wanafiki!+ kwa sababu mnajenga makaburi ya manabii na kuyarembesha makaburi ya waadilifu,+ 30 nanyi mnasema, ‘Kama tungekuwa katika siku za mababu zetu, hatungekuwa washiriki pamoja nao katika damu ya manabii.’+ 31 Kwa hiyo mnatoa ushahidi juu yenu wenyewe kwamba ninyi ni wana wa wale waliowaua manabii.+ 32 Hivyo, basi, kijazeni kipimo+ cha mababu zenu.
33 “Nyoka, uzao wa nyoka-vipiri,+ mtaikimbiaje hukumu ya Gehena?*+ 34 Kwa sababu hiyo, tazameni, ninatuma+ kwenu manabii na watu wenye hekima na wafundishaji wa watu wote.+ Baadhi yao mtawaua+ na kuwatundika mtini, na baadhi yao mtawapiga mijeledi+ katika masinagogi yenu na kuwatesa jiji baada ya jiji; 35 ili ije juu yenu damu yote ya uadilifu iliyomwagwa juu ya dunia,+ tangu damu+ ya Abeli+ mwadilifu mpaka damu ya Zekaria mwana wa Barakia, ambaye mlimuua katikati ya patakatifu na madhabahu.+ 36 Kwa kweli ninawaambia ninyi, Mambo yote haya yatakipata kizazi hiki.+
37 “Yerusalemu, Yerusalemu, muuaji wa manabii+ na ambaye huwapiga kwa mawe+ wale waliotumwa kwake,+—ni mara ngapi nilitaka kuwakusanya watoto wako, kama vile kuku anavyokusanya vifaranga vyake chini ya mabawa yake!+ Lakini hamkutaka.+ 38 Tazama! Nyumba yenu+ mmeachiwa hali ya ukiwa.+ 39 Kwa maana ninawaambia ninyi, Hamtaniona kamwe tangu sasa mpaka mtakaposema, ‘Aliyebarikiwa ni yule anayekuja katika jina la Yehova!’ ”+
24 Sasa Yesu akaondoka, akashika njia kutoka hekaluni, lakini wanafunzi wake wakamkaribia na kumwonyesha majengo ya hekalu.+ 2 Akajibu, akawaambia: “Je, hamvioni vitu vyote hivi? Kwa kweli ninawaambia ninyi, Hakuna jiwe litakaloachwa hapa juu ya jiwe nalo lisiangushwe chini.”+
3 Alipokuwa ameketi juu ya Mlima wa Mizeituni, wanafunzi wakamkaribia faraghani, wakisema: “Tuambie, Mambo haya yatakuwa wakati gani, na ni nini itakayokuwa ishara ya kuwapo+ kwako na ya umalizio wa mfumo wa mambo?”+
4 Naye Yesu akajibu, akawaambia: “Jihadharini mtu yeyote asiwapotoshe;+ 5 kwa maana wengi watakuja kwa msingi wa jina langu, wakisema, ‘Mimi ndiye Kristo,’ nao watawapotosha wengi.+ 6 Mtasikia juu ya vita na habari za vita; angalieni kwamba msiogope. Kwa maana mambo hayo lazima yatukie, lakini ule mwisho bado.+
7 “Kwa maana taifa litasimama kupigana na taifa+ na ufalme kupigana na ufalme,+ kutakuwa na upungufu wa chakula+ na matetemeko ya nchi+ mahali pamoja baada ya pengine. 8 Mambo yote hayo ni mwanzo wa maumivu ya taabu.
9 “Ndipo watu watakapowatia ninyi katika dhiki+ na kuwaua+ ninyi, nanyi mtachukiwa+ na mataifa yote kwa sababu ya jina langu.+ 10 Ndipo, pia, watu wengi watakwazika+ na kusalitiana na kuchukiana.+ 11 Na manabii wengi wa uwongo+ watatokea na kuwapotosha wengi;+ 12 na kwa sababu ya kuongezeka kwa uasi-sheria+ upendo wa walio wengi zaidi utapoa.+ 13 Lakini yule ambaye atavumilia+ mpaka mwisho ndiye atakayeokolewa.+ 14 Na hii habari njema+ ya ufalme+ itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote;+ na ndipo ule mwisho+ utakapokuja.
15 “Kwa hiyo, mtakapoona lile chukizo+ linalosababisha ukiwa, kama vile lilivyosemwa kupitia nabii Danieli, likiwa limesimama katika mahali patakatifu,+ (msomaji na atumie utambuzi,) 16 ndipo wale walio katika Yudea waanze kukimbilia+ milimani. 17 Mtu aliye juu ya paa ya nyumba asishuke kuchukua mali kutoka katika nyumba yake; 18 na mtu aliye shambani asirudi nyumbani kuchukua vazi lake la nje. 19 Ole wao wanawake wenye mimba na wale wanaonyonyesha mtoto mchanga katika siku hizo!+ 20 Endeleeni kusali kwamba kukimbia kwenu kusiwe wakati wa majira ya baridi kali, wala siku ya sabato; 21 kwa maana ndipo kutakapokuwa na dhiki kuu+ ya namna ambayo haijapata kutukia tangu mwanzo wa ulimwengu mpaka sasa,+ hapana, wala haitatukia tena. 22 Kwa kweli, kama siku hizo hazingefupishwa, hakuna chochote chenye mwili ambacho kingeokolewa; lakini kwa sababu ya wale waliochaguliwa+ siku hizo zitafupishwa.+
23 “Ndipo mtu yeyote akiwaambia, ‘Tazameni! Kristo huyu hapa,’+ au, ‘Pale!’ msiamini.+ 24 Kwa maana Makristo wa uwongo+ na manabii wa uwongo+ watatokea na kutoa ishara+ kubwa na maajabu ili kuwapotosha, ikiwezekana, hata wale waliochaguliwa.+ 25 Tazameni! Nimewaonya kimbele.+ 26 Kwa hiyo, watu wakiwaambia ninyi, ‘Tazameni! Yuko nyikani,’ msiende; ‘Tazameni! Yumo katika vyumba vya ndani,’ msiamini.+ 27 Kwa maana kama vile umeme+ unavyotokea sehemu za mashariki na kuangaza mpaka sehemu za magharibi, ndivyo kuwapo kwa Mwana wa binadamu kutakavyokuwa.+ 28 Popote mzoga ulipo, hapo ndipo watakapokusanyika+ tai.+
29 “Mara baada ya ile dhiki ya siku hizo jua litatiwa giza,+ nao mwezi+ hautatoa nuru yake, nazo nyota zitaanguka kutoka mbinguni, nazo nguvu za mbingu zitatikiswa.+ 30 Ndipo ishara ya Mwana wa binadamu+ itakapoonekana mbinguni, ndipo makabila yote ya dunia yatakapojipiga-piga yenyewe kwa kuomboleza,+ nayo yatamwona Mwana wa binadamu akija juu ya mawingu ya mbinguni akiwa na nguvu na utukufu mwingi.+ 31 Naye atawatuma malaika zake pamoja na mvumo mkubwa wa tarumbeta,+ nao watawakusanya pamoja watu wake waliochaguliwa+ kutoka kwenye zile pepo nne,+ kutoka mwisho mmoja wa mbingu mpaka mwisho wake mwingine.
32 “Basi jifunzeni jambo hili kutokana na mtini kama mfano: Mara tu tawi lake changa linapokuwa jororo na kutoa majani, mnajua kwamba kiangazi kiko karibu.+ 33 Vivyo hivyo ninyi pia, mnapoona mambo yote hayo, jueni kwamba yuko karibu milangoni.+ 34 Kwa kweli ninawaambia ninyi kwamba kizazi hiki+ hakitapitilia mbali kamwe mpaka mambo yote hayo yatukie. 35 Mbingu na dunia zitapitilia mbali,+ lakini maneno yangu hayatapitilia mbali kamwe.+
36 “Kuhusu siku ile na saa+ ile hakuna mtu anayejua, wala malaika wa mbinguni wala Mwana, ila Baba tu.+ 37 Kwa maana kama vile siku za Noa+ zilivyokuwa, ndivyo kuwapo kwa Mwana wa binadamu kutakavyokuwa.+ 38 Kwa maana kama vile walivyokuwa katika siku hizo kabla ya gharika, wakila na kunywa, wanaume wakioa na wanawake wakiolewa, mpaka siku ambayo Noa+ aliingia ndani ya safina;+ 39 nao hawakujali mpaka gharika ikaja na kuwafagilia mbali wote,+ ndivyo kuwapo kwa Mwana wa binadamu kutakavyokuwa. 40 Wakati huo watu wawili watakuwa shambani: mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa; 41 wanawake wawili watakuwa wakisaga kwenye jiwe la kusagia:+ mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.+ 42 Kwa hiyo, endeleeni kukesha kwa sababu hamjui ni siku gani Bwana yenu atakuja.+
43 “Lakini jueni jambo moja, kwamba ikiwa mwenye nyumba angalijua mwizi anakuja katika kesha gani,+ angaliendelea kukaa macho na hangaliruhusu nyumba yake ivunjwe. 44 Kwa hiyo ninyi pia iweni tayari,+ kwa sababu Mwana wa binadamu atakuja katika saa msiyofikiria.
45 “Ni nani kwa kweli mtumwa mwaminifu na mwenye busara+ ambaye bwana wake alimweka rasmi juu ya watumishi wake wa nyumbani, awape chakula chao kwa wakati unaofaa?+ 46 Mtumwa huyo atakuwa mwenye furaha+ ikiwa bwana wake atakapofika atamkuta akifanya hivyo! 47 Kwa kweli ninawaambia ninyi, Atamweka juu ya mali zake zote.+
48 “Lakini mtumwa huyo mwovu akisema moyoni mwake,+ ‘Bwana wangu anakawia,’+ 49 naye aanze kuwapiga watumwa wenzake na kula na kunywa pamoja na walevi wa kupindukia, 50 bwana wa mtumwa huyo atakuja katika siku ambayo hatazamii na katika saa+ ambayo hajui, 51 naye atamwadhibu kwa ukali+ mkubwa zaidi na kumgawia sehemu yake pamoja na wanafiki. Huko ndiko atalia na kusaga meno.+
25 “Ndipo ufalme wa mbinguni utakuwa kama mabikira kumi waliochukua taa+ zao na kwenda kumpokea bwana-arusi.+ 2 Watano kati yao walikuwa wapumbavu,+ na watano walikuwa wenye busara.+ 3 Kwa maana wale wapumbavu walichukua taa zao lakini hawakuchukua mafuta pamoja nao, 4 lakini wale wenye busara walichukua mafuta katika vyombo vyao pamoja na taa zao. 5 Wakati bwana-arusi alipokuwa anakawia, wote walisinzia na kuanza kulala.+ 6 Katikati ya usiku kukatokea mwito,+ ‘Huyu hapa bwana-arusi! Nendeni mkampokee.’ 7 Ndipo mabikira wote hao wakasimama na kuzitayarisha taa+ zao. 8 Wale wapumbavu wakawaambia wale wenye busara, ‘Tupeni sisi kiasi fulani cha mafuta+ yenu, kwa sababu taa zetu zinakaribia kuzimika.’ 9 Wale wenye busara+ wakawajibu kwa maneno haya, ‘Labda huenda tusiwe na ya kutosha kwa ajili yetu na kwa ajili yenu. Badala yake, shikeni njia mwende kwa wale wanaoyauza mkajinunulie.’ 10 Walipokuwa wakienda zao kununua, bwana-arusi akafika, na wale mabikira waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye kwenye karamu ya arusi;+ nao mlango ukafungwa. 11 Baadaye wale mabikira wengine pia wakaja, wakisema, ‘Bwana, bwana, tufungulie!’+ 12 Akajibu, akasema, ‘Ninawaambia ninyi kweli, Siwajui ninyi.’+
13 “Kwa hiyo, endeleeni kukesha+ kwa sababu hamwijui ile siku wala saa.+
14 “Kwa maana ni kama wakati ambapo mtu,+ akiwa karibu kusafiri ng’ambo,+ aliwaita watumwa wake na kuwapa mali zake.+ 15 Akampa mmoja talanta tano, mwingine mbili, na mwingine moja, kila mmoja kulingana na uwezo wake mwenyewe,+ naye akaenda ng’ambo. 16 Mara moja yule aliyezipokea talanta tano akaenda zake na kufanya biashara nazo na kupata faida ya tano zaidi.+ 17 Vivyo hivyo yule aliyepokea mbili akapata faida ya mbili zaidi. 18 Lakini yule aliyepokea moja tu akaenda zake, na kuchimba katika udongo na kuficha zile fedha za bwana wake.
19 “Baada ya muda mrefu+ bwana wa watumwa hao alikuja na kufanya hesabu pamoja nao.+ 20 Kwa hiyo yule aliyekuwa amepokea talanta tano akaja na kuleta talanta tano zaidi, akisema, ‘Bwana, ulinipa talanta tano; ona, nilipata faida ya talanta tano zaidi.’+ 21 Bwana wake akamwambia, ‘Vema, mtumwa mwema na mwaminifu!+ Ulikuwa mwaminifu+ juu ya mambo machache. Nitakuweka juu ya mambo mengi.+ Ingia katika shangwe+ ya bwana wako.’ 22 Halafu yule aliyekuwa amepokea talanta mbili akaja na kusema, ‘Bwana, ulinipa talanta mbili; ona, nilipata faida ya talanta mbili zaidi.’+ 23 Bwana wake akamwambia, ‘Vema, mtumwa mwema na mwaminifu! Ulikuwa mwaminifu juu ya mambo machache. Nitakuweka juu ya mambo mengi.+ Ingia katika shangwe+ ya bwana wako.’
24 “Mwishowe yule aliyekuwa amepokea talanta moja akaja+ na kusema, ‘Bwana nilijua wewe ni mtu mwenye kudai, ambaye huvuna mahali ambapo hukupanda na kukusanya mahali ambapo hukupepeta. 25 Kwa hiyo nikaogopa+ na kwenda zangu na kuficha talanta yako katika udongo. Tazama, hiki hapa kilicho chako.’ 26 Bwana wake akamjibu, akamwambia, ‘Mtumwa mwovu na goigoi, ulijua, sivyo, kwamba mimi nilivuna mahali ambapo sikupanda na kukusanya mahali ambapo sikupepeta? 27 Hivyo, basi, ulipaswa kuwa umeweka fedha zangu kwa wenye kutunza akiba, na wakati wa kufika kwangu ningekuwa nikipokea kilicho changu pamoja na faida.+
28 “ ‘Kwa hiyo ichukueni talanta hiyo kutoka kwake na kumpa yule aliye na talanta kumi.+ 29 Kwa maana kila mtu aliye na kitu, ataongezewa naye atakuwa na vingi; lakini yule ambaye hana kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.+ 30 Nanyi mtupeni nje katika giza mtumwa huyo asiyefaa kitu. Huko ndiko atalia na kusaga meno yake.’+
31 “Wakati Mwana wa binadamu+ atakapofika katika utukufu wake, na malaika wote pamoja naye,+ ndipo atakapoketi juu ya kiti chake cha ufalme chenye utukufu.+ 32 Na mataifa yote yatakusanyika mbele yake,+ naye atawatenganisha watu,+ mmoja kutoka kwa mwenzake,+ kama vile mchungaji anavyotenganisha kondoo na mbuzi. 33 Naye atawaweka kondoo kwenye mkono wake wa kuume,+ lakini mbuzi kwenye mkono wake wa kushoto.+
34 “Ndipo mfalme atakapowaambia wale walio kwenye mkono wake wa kuume, ‘Njooni, ninyi ambao mmebarikiwa na Baba yangu,+ urithini+ ufalme+ uliotayarishwa kwa ajili yenu tangu kuwekwa msingi wa ulimwengu.+ 35 Kwa maana nilikuwa mwenye njaa nanyi mkanipa chakula;+ nilikuwa na kiu nanyi mkanipa kinywaji. Nilikuwa mgeni nanyi mkanikaribisha;+ 36 nilikuwa uchi,+ nanyi mkanivika. Nilishikwa na ugonjwa nanyi mkanitunza. Nilikuwa gerezani+ nanyi mkanijia.’ 37 Ndipo waadilifu watamjibu kwa maneno haya, ‘Bwana, ni wakati gani tulipokuona ukiwa na njaa na kukulisha, au ukiwa na kiu,+ na kukupa kinywaji?+ 38 Ni wakati gani tulipokuona ukiwa mgeni na kukukaribisha, au ukiwa uchi, na kukuvika? 39 Ni wakati gani tulipokuona ukiwa mgonjwa au gerezani na kukujia?’ 40 Na mfalme+ atajibu na kuwaambia, ‘Kwa kweli ninawaambia ninyi, Kwa kadiri ambayo mlimtendea hilo mmoja wa walio wadogo zaidi+ wa ndugu zangu+ hawa, mlinitendea mimi.’+
41 “Ndipo naye atawaambia, wale walio kwenye mkono wake wa kushoto, ‘Tokeni kwangu mwende zenu,+ ninyi ambao mmelaaniwa, mkaingie katika moto wa milele+ aliotayarishiwa Ibilisi na malaika zake.+ 42 Kwa maana nilikuwa na njaa, lakini hamkunipa chakula chochote,+ nami nilikuwa na kiu,+ lakini hamkunipa kinywaji chochote. 43 Nilikuwa mgeni, lakini hamkunikaribisha; nilikuwa uchi, lakini hamkunivika;+ nilikuwa mgonjwa na gerezani,+ lakini hamkunitunza.’ 44 Ndipo wao pia watamjibu kwa maneno haya, ‘Bwana, ni wakati gani tulipokuona ukiwa na njaa au ukiwa na kiu au ukiwa mgeni au ukiwa uchi au mgonjwa au gerezani na tukakosa kukuhudumia?’ 45 Ndipo atawajibu wao kwa maneno haya, ‘Kwa kweli ninawaambia ninyi, Kwa kadiri ambayo hamkumtendea hilo mmoja wa hawa wadogo zaidi,+ hamkunitendea+ mimi.’+ 46 Na hawa watakatiliwa mbali milele,+ lakini waadilifu wataingia katika uzima wa milele.”+
26 Basi Yesu alipokuwa amemaliza kusema yote hayo, aliwaambia wanafunzi wake: 2 “Mnajua kwamba siku mbili tangu sasa kutakuwa na pasaka,+ naye Mwana wa binadamu atatolewa ili atundikwe mtini.”+
3 Ndipo wakuu wa makuhani na wanaume wazee wa watu wakakusanyika pamoja katika ua wa kuhani mkuu aliyeitwa Kayafa,+ 4 na kushauriana+ pamoja ili wamkamate Yesu kwa hila na kumuua. 5 Hata hivyo, wao wakawa wakisema: “Si kwenye sherehe, ili ghasia zisitokee katikati ya watu.”+
6 Ikawa kwamba Yesu alipokuwa Bethania+ katika nyumba ya Simoni mwenye ukoma,+ 7 mwanamke mwenye chupa ya alabasta iliyo na mafuta ghali yenye marashi+ akamkaribia, naye akaanza kuyamimina juu ya kichwa cha Yesu alipokuwa ameketi mezani. 8 Walipoona hilo wanafunzi wakaghadhibika na kusema: “Hasara hii ni ya nini?+ 9 Kwa maana yangaliweza kuuzwa kwa kiasi kikubwa na kupewa maskini.”+ 10 Akijua jambo hilo,+ Yesu akawaambia: “Kwa nini mnataka kumsumbua mwanamke huyu? Kwa kuwa amenitendea tendo jema.+ 11 Kwa maana ninyi mna maskini+ pamoja nanyi sikuzote, lakini hamtakuwa pamoja nami sikuzote.+ 12 Kwa kuwa mwanamke huyu alipotia mafuta haya yenye marashi juu ya mwili wangu, alifanya hivyo ili kunitayarisha kwa ajili ya maziko.+ 13 Kwa kweli ninawaambia ninyi, Kokote ambako hii habari njema itahubiriwa katika ulimwengu wote, jambo ambalo mwanamke huyu ametenda litasimuliwa pia kuwa kumbukumbu lake.”+
14 Ndipo mmoja wa wale kumi na wawili, anayeitwa Yuda Iskariote,+ akaenda kwa wakuu wa makuhani 15 na kusema: “Mtanipa nini ili nimsaliti kwenu?”+ Wakamwagizia vipande 30 vya fedha.+ 16 Kwa hiyo tangu wakati huo na kuendelea akawa akitafuta nafasi nzuri ya kumsaliti.+
17 Katika siku ya kwanza ya keki zisizo na chachu+ wanafunzi wakamjia Yesu, wakisema: “Ni wapi unapotaka tukutayarishie uile pasaka?”+ 18 Akasema: “Nendeni jijini kwa Fulani-wa-fulani,+ mkamwambie, Mwalimu anasema, ‘Wakati wangu uliowekwa uko karibu; nitasherehekea pasaka pamoja na wanafunzi wangu nyumbani mwako.’ ”+ 19 Nao wanafunzi wakafanya kama Yesu alivyowaagiza, nao wakatayarisha vitu kwa ajili ya pasaka.+
20 Basi, ilipofika jioni,+ alikuwa ameketi mezani pamoja na wale wanafunzi kumi na wawili.+ 21 Walipokuwa wakila, alisema: “Kwa kweli ninawaambia ninyi, Mmoja wenu atanisaliti.”+ 22 Wakiwa wamehuzunishwa sana na jambo hilo, kila mmoja wao akaanza kumwambia: “Bwana, je, ni mimi?”+ 23 Akajibu, akasema: “Yule anayechovya mkono wake pamoja nami katika bakuli ndiye atakayenisaliti.+ 24 Kwa kweli, Mwana wa binadamu anaenda zake, kama ilivyoandikwa+ kumhusu, lakini ole+ wake mtu yule ambaye kupitia kwake Mwana wa binadamu atasalitiwa!+ Ingalikuwa afadhali kwake kama mtu huyo asingalizaliwa.” 25 Yuda, aliyekuwa karibu kumsaliti, akajibu, akasema: “Je, ni mimi, Rabi?” Akamwambia: “Wewe mwenyewe umesema.”
26 Walipokuwa wakiendelea kula, Yesu alichukua mkate+ na, baada ya kutoa baraka, akaumega,+ akawapa wanafunzi, akasema: “Chukueni, mle. Huu unamaanisha mwili wangu.”+ 27 Pia, akachukua kikombe+ na, akiisha kushukuru, akawapa, akisema: “Kinyweeni, ninyi nyote;+ 28 kwa maana hii inamaanisha+ ‘damu+ yangu ya agano,’+ ambayo itamwagwa kwa ajili ya wengi+ kwa msamaha wa dhambi.+ 29 Lakini ninawaambia ninyi, Tangu sasa sitakunywa kamwe divai yoyote ya mzabibu mpaka siku ile nitakapokunywa ikiwa mpya, pamoja nanyi katika ufalme wa Baba yangu.”+ 30 Mwishowe, baada ya kuimba sifa,+ wakatoka na kwenda kwenye Mlima wa Mizeituni.+
31 Ndipo Yesu akawaambia: “Ninyi nyote mtakwazika kuhusiana nami usiku huu, kwa maana imeandikwa, ‘Nitampiga mchungaji, nao kondoo wa kundi watatawanyika huku na huku.’+ 32 Lakini baada ya kufufuliwa nitawatangulia kuingia Galilaya.”+ 33 Lakini Petro akajibu, akamwambia: “Ijapokuwa wengine wote wakwazike kuhusiana nawe, mimi sitakwazika kamwe!”+ 34 Yesu akamwambia: “Kwa kweli ninakuambia wewe, Usiku huu, kabla ya jogoo kuwika, utanikana mara tatu.”+ 35 Petro akamwambia: “Hata nikilazimika kufa pamoja nawe, mimi sitakukana kamwe.” Wale wanafunzi wengine wote wakasema vivyo hivyo pia.+
36 Ndipo Yesu akaja pamoja nao mpaka mahali+ panapoitwa Gethsemane, naye akawaambia wanafunzi: “Ketini hapa ninapoenda pale na kusali.”+ 37 Naye akawachukua Petro na wale wana wawili+ wa Zebedayo pamoja naye, akaanza kuhuzunika na kutaabika sana.+ 38 Ndipo akawaambia: “Nafsi yangu ina huzuni sana, kiasi cha kufa.+ Kaeni hapa na mwendelee kukesha pamoja nami.”+ 39 Naye akasonga mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akasali+ na kusema: “Baba yangu, ikiwezekana, kikombe hiki+ na kipitilie mbali kutoka kwangu. Lakini, si kulingana na mapenzi yangu,+ bali kulingana na mapenzi yako.”+
40 Naye akaja walipokuwa wanafunzi na kuwakuta wamelala usingizi, naye akamwambia Petro: “Je, hamngeweza kukesha hata saa moja pamoja nami?+ 41 Endeleeni kukesha+ na kusali+ sikuzote, ili msiingie katika jaribu.+ Bila shaka, roho inataka, lakini mwili ni dhaifu.”+ 42 Tena, kwa mara ya pili,+ akaenda zake na kusali, akisema: “Baba yangu, ikiwa haiwezekani kipitilie mbali ila nikinywe, acha mapenzi yako yatendeke.”+ 43 Naye akaja tena na kuwakuta wamelala usingizi, kwa maana macho yao yalikuwa mazito.+ 44 Kwa hiyo akawaacha, akaenda zake tena na kusali kwa mara ya tatu,+ akisema mara moja tena neno lilelile. 45 Kisha akaja walipokuwa wanafunzi na kuwaambia: “Wakati kama huu ninyi mnalala usingizi na kupumzika! Tazameni! Saa imekaribia Mwana wa binadamu asalitiwe na kutiwa katika mikono ya watenda-dhambi.+ 46 Simameni, twende. Tazama! Msaliti wangu amekaribia.”+ 47 Na alipokuwa bado akisema, tazama! Yuda,+ mmoja wa wale kumi na wawili, akaja pamoja na umati mkubwa ukiwa na mapanga+ na marungu kutoka kwa wakuu wa makuhani na wanaume wazee wa watu.+
48 Basi msaliti wake alikuwa amewapa ishara, akisema: “Yeyote yule nitakayembusu, huyo ndiye; mkamateni.”+ 49 Naye akaenda moja kwa moja kwa Yesu akasema: “Siku njema, Rabi!”+ na kumbusu+ kwa wororo sana. 50 Lakini Yesu+ akamwambia: “Mwenzangu, uko hapa kwa kusudi gani?” Ndipo wakaja wakaweka mikono juu ya Yesu na kumkamata.+ 51 Lakini, tazama! mmoja wa wale waliokuwa pamoja na Yesu akanyoosha mkono wake akauchomoa upanga wake, akampiga mtumwa wa kuhani mkuu akalikata sikio lake.+ 52 Ndipo Yesu akamwambia: “Rudisha upanga wako mahali pake,+ kwa maana wale wote wanaouchukua upanga wataangamia kwa upanga.+ 53 Au unafikiri kwamba siwezi kumwomba Baba yangu anipe sasa hivi vikosi zaidi ya kumi na viwili vya malaika?+ 54 Hata hivyo, Maandiko yangetimizwaje kwamba lazima itendeke hivi?” 55 Ndipo Yesu akauambia umati: “Je, mmetoka mkiwa na mapanga na marungu kana kwamba ni kwenda juu ya mnyang’anyi ili kunikamata?+ Siku baada ya siku nilikuwa nikiketi katika hekalu+ nikifundisha, na bado hamkunikamata. 56 Lakini yote haya yametukia ili maandiko ya manabii yatimizwe.”+ Ndipo wanafunzi wote wakamwacha na kukimbia.+
57 Wale waliomkamata Yesu wakampeleka kwa Kayafa+ kuhani mkuu, ambako waandishi na wanaume wazee walikuwa wamekusanywa pamoja.+ 58 Lakini Petro akaendelea kumfuata akiwa mbali kiasi, mpaka katika ua+ wa kuhani mkuu, na, baada ya kuingia ndani, akaketi pamoja na watumishi wa nyumbani ili kuona matokeo.+
59 Wakati huohuo wakuu wa makuhani na Sanhedrini nzima walikuwa wakitafuta ushahidi wa uwongo juu ya Yesu ili wamuue,+ 60 lakini hawakupata wowote, ijapokuwa mashahidi wengi wa uwongo walijitokeza.+ Baadaye wawili wakajitokeza 61 na kusema: “Mtu huyu alisema, ‘Ninaweza kuliangusha chini hekalu la Mungu na kulijenga katika siku tatu.’ ”+ 62 Ndipo kuhani mkuu akasimama na kumwambia: “Je, huna jibu? Watu hawa wanashuhudia nini juu yako?”+ 63 Lakini Yesu akaendelea kukaa kimya.+ Kwa hiyo kuhani mkuu akamwambia: “Kwa Mungu aliye hai ninakuweka chini ya kiapo+ utuambie kama wewe ndiye Kristo+ Mwana wa Mungu!” 64 Yesu akamwambia:+ “Wewe mwenyewe umesema.+ Lakini ninawaambia ninyi, Tangu sasa+ mtamwona Mwana wa binadamu+ akiwa ameketi kwenye mkono wa kuume+ wa nguvu na akija juu ya mawingu ya mbinguni.”+ 65 Ndipo kuhani mkuu akayararua mavazi yake ya nje, akisema: “Amekufuru!+ Tunahitaji mashahidi wengine wa nini?+ Tazama! Sasa mmelisikia kufuru.+ 66 Mnaonaje?” Wakamjibu: “Anastahili kufa.”+ 67 Ndipo wakamtemea mate usoni+ na kumpiga+ ngumi. Wengine wakampiga makofi usoni,+ 68 wakisema: “Tutolee unabii, wewe Kristo.+ Ni nani aliyekupiga?”+
69 Basi Petro alikuwa ameketi nje katika ua; na mjakazi akamjia, akisema: “Wewe, pia, ulikuwa pamoja na Yesu Mgalilaya!”+ 70 Lakini akakana mbele yao wote, akisema: “Sijui unalosema.” 71 Alipokuwa amekwisha kutoka na kwenda kwenye chumba kilicho langoni, msichana mwingine alimwona na kuwaambia wale waliokuwa hapo: “Mtu huyu alikuwa pamoja na Yesu Mnazareti.”+ 72 Naye akakana tena, kwa kiapo: “Simjui mtu huyo!”+ 73 Baada ya muda kidogo wale waliokuwa wamesimama kuzunguka wakaja na kumwambia Petro: “Hakika wewe pia ni mmoja wao, kwa maana, kwa kweli, matamshi yako yanakutambulisha wazi.”+ 74 Ndipo akaanza kulaani na kuapa: “Simjui mtu huyo!” Na mara jogoo akawika.+ 75 Naye Petro akakumbuka maneno ambayo Yesu alisema, yaani: “Kabla ya jogoo kuwika, utanikana mara tatu.”+ Naye akaenda nje akalia kwa uchungu.+
27 Asubuhi ilipofika, wakuu wote wa makuhani na wanaume wazee wa watu wakashauriana juu ya Yesu ili auawe.+ 2 Na, baada ya kumfunga, wakampeleka na kumtia mkononi mwa gavana Pilato.+
3 Ndipo Yuda, aliyemsaliti, alipoona kuwa amekwisha kuhukumiwa adhabu, akajuta, akavirudisha vile vipande 30+ vya fedha kwa wakuu wa makuhani na wanaume wazee, 4 akisema: “Nilitenda dhambi niliposaliti damu yenye uadilifu.”+ Wakasema: “Hilo linatuhusu nini? Shauri yako!”+ 5 Basi akatupa vile vipande vya fedha hekaluni akaondoka, akaenda zake akajinyonga.+ 6 Lakini wakuu wa makuhani wakavichukua hivyo vipande vya fedha na kusema: “Si halali kuvitumbukiza katika hazina takatifu, kwa sababu hivyo ni bei ya damu.” 7 Baada ya kushauriana pamoja, wakavitumia kununua shamba la mfinyanzi ili kuzikia wageni. 8 Kwa hiyo shamba hilo limeitwa “Shamba la Damu”+ mpaka leo hii. 9 Ndipo likatimizwa lililosemwa kupitia nabii Yeremia, akisema: “Nao walichukua vile vipande 30 vya fedha,+ ambavyo ni bei juu ya mtu aliyepigwa bei, ambaye baadhi ya wana wa Israeli walimpigia bei, 10 nao wakavitoa kwa ajili ya shamba la mfinyanzi,+ kulingana na lile ambalo Yehova alikuwa ameniamuru.”
11 Yesu sasa akasimama mbele ya gavana; naye gavana akamuuliza: “Je, wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?”+ Yesu akajibu: “Wewe mwenyewe unasema.”+ 12 Lakini, alipokuwa akishtakiwa+ na wakuu wa makuhani na wanaume wazee, hakujibu.+ 13 Ndipo Pilato akamwambia: “Je, husikii ni mambo mangapi wanashuhudia juu yako?”+ 14 Lakini hakumjibu, hata neno moja, hivi kwamba gavana akastaajabu sana.+
15 Sasa kutoka sherehe mpaka sherehe ilikuwa desturi ya gavana kufungulia umati mfungwa mmoja, ambaye walimtaka.+ 16 Wakati huohuo walikuwa wamemshika mfungwa mwenye sifa mbaya anayeitwa Baraba.+ 17 Kwa sababu hiyo walipokuwa wamekusanywa pamoja Pilato akawaambia: “Mnataka niwafungulie nani, Baraba au Yesu anayeitwa Kristo?”+ 18 Kwa maana alijua kwamba walikuwa wamemtia mikononi mwake+ kwa sababu ya wivu.+ 19 Zaidi ya hayo, alipokuwa ameketi juu ya kiti cha hukumu, mke wake akampelekea habari, akisema: “Usijihusishe kamwe na mtu huyo mwadilifu,+ kwa maana niliteseka sana leo katika ndoto+ kwa sababu yake.” 20 Lakini wakuu wa makuhani na wanaume wazee wakaushawishi umati uombe wapewe Baraba,+ lakini Yesu aangamizwe. 21 Sasa gavana akajibu, akawaambia: “Mnataka niwafungulie nani kati ya hawa wawili?” Wakasema: “Baraba.”+ 22 Pilato akawaambia: “Basi, nitafanya nini na Yesu anayeitwa Kristo?” Wote wakasema: “Atundikwe mtini!”+ 23 Akasema: “Kwani, amefanya jambo gani baya?” Bado wao wakaendelea kupaaza sauti hata zaidi: “Atundikwe mtini!”+
24 Alipoona kwamba haikufaidi kitu bali, badala yake, ghasia zilikuwa zikitokea, Pilato alichukua maji+ na kunawa mikono yake mbele ya ule umati, akisema: “Mimi sina hatia ya damu ya mtu huyu. Shauri yenu.” 25 Ndipo watu wote wakajibu, wakasema: “Damu yake iwe juu yetu na juu ya watoto wetu.”+ 26 Ndipo akawafungulia Baraba, lakini akaagiza Yesu apigwe mijeledi+ na kumtoa ili atundikwe mtini.+
27 Ndipo askari-jeshi wa gavana wakampeleka Yesu ndani ya jumba la gavana na kukusanya pamoja kikosi chote cha askari kwake.+ 28 Nao wakamvua kanzu yake, wakampamba kwa joho jekundu,+ 29 nao wakasokota taji kutokana na miiba na kuliweka juu ya kichwa chake na utete katika mkono wake wa kuume. Nao wakapiga magoti mbele yake, wakamfanyia dhihaka,+ wakisema: “Siku njema, ewe Mfalme wa Wayahudi!”+ 30 Nao wakamtemea mate+ na kuuchukua ule utete na kuanza kumpiga kichwani. 31 Mwishowe, walipokuwa wamemdhihaki,+ wakalivua lile joho na kumvika mavazi yake ya nje na kumpeleka akatundikwe mtini.+
32 Walipokuwa wakiondoka walimkuta mzaliwa wa Kirene anayeitwa Simoni.+ Wakamlazimisha aubebe mti wake wa mateso. 33 Nao walipofika mahali panapoitwa Golgotha,+ ndiyo kusema, Mahali pa Fuvu la Kichwa, 34 wakampa divai iliyochanganywa na nyongo+ anywe; lakini, baada ya kuionja, akakataa kuinywa.+ 35 Walipokuwa wamemtundika mtini+ wakagawa mavazi yake ya nje+ kwa kupiga kura,+ 36 na, huku wakiwa wameketi, wakamlinda hapo. 37 Pia, wakabandika juu ya kichwa chake shtaka juu yake, kwa kuandika: “Huyu ni Yesu Mfalme wa Wayahudi.”+
38 Ndipo wanyang’anyi wawili wakatundikwa mtini pamoja naye, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wake wa kushoto.+ 39 Kwa hiyo wapita-njia wakaanza kumtukana,+ wakitikisa+ vichwa vyao 40 na kusema: “Ewe uliyetaka kuliangusha hekalu+ na kulijenga kwa siku tatu, jiokoe mwenyewe! Ikiwa wewe ni mwana wa Mungu, shuka kutoka kwenye mti wa mateso!”+ 41 Vivyo hivyo pia wakuu wa makuhani pamoja na waandishi na wanaume wazee wakaanza kumfanyia dhihaka na kusema:+ 42 “Aliwaokoa wengine; yeye mwenyewe hawezi kujiokoa! Yeye ni Mfalme+ wa Israeli; acheni sasa ashuke kutoka kwenye mti wa mateso nasi tutamwamini.+ 43 Ameweka tegemeo lake katika Mungu; acheni Yeye sasa amwokoe+ ikiwa Yeye anamtaka, kwa maana alisema, ‘Mimi ni Mwana wa Mungu.’ ”+ 44 Vivyo hivyo hata wanyang’anyi waliotundikwa mtini pamoja naye wakaanza kumshutumu.+
45 Tangu saa sita na kuendelea kukawa na giza+ juu ya nchi yote, mpaka saa tisa.+ 46 Karibu saa tisa Yesu akapaaza kilio kwa sauti kubwa, akisema: “Eli, Eli, lama sabakthani?” yaani, “Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?”+ 47 Waliposikia hilo, baadhi ya wale waliokuwa wamesimama hapo wakaanza kusema: “Mtu huyu anamwita Eliya.”+ 48 Na mmoja wao akakimbia mara moja, akachukua sifongo akailowesha kwenye divai kali+ akaiweka juu ya utete na kuanza kumnywesha.+ 49 Lakini wale wengine wao wakasema: “Acha iwe hivyo kwake! Acheni tuone kama Eliya atakuja kumwokoa.”+ [[Mtu mwingine akachukua mkuki na kumchoma ubavuni, na damu na maji vikatoka.]]+ 50 Tena Yesu akapaaza sauti kubwa, akaitoa roho yake.+
51 Na, tazama! pazia+ la patakatifu likapasuka vipande viwili, kutoka juu mpaka chini,+ na dunia ikatetemeka, na miamba ikapasuka.+ 52 Na makaburi yakafunguka na miili mingi ya watakatifu waliokuwa wamelala usingizi ikainuliwa, 53 (na watu, waliokuwa wakitoka kati ya makaburi baada ya kufufuliwa kwake, wakaingia katika jiji takatifu,)+ nayo ikaonwa na watu wengi. 54 Lakini yule ofisa-jeshi na wale waliokuwa pamoja naye wakimlinda Yesu, walipoona tetemeko la nchi na mambo yaliyokuwa yakitendeka, wakaogopa sana, wakisema: “Hakika huyu alikuwa Mwana wa Mungu.”+
55 Zaidi ya hayo, wanawake wengi walikuwa hapo wakitazama wakiwa mbali,+ waliokuwa wamefuatana na Yesu kutoka Galilaya ili kumhudumia;+ 56 ambao kati yao alikuwamo Maria Magdalene, pia Maria mama ya Yakobo na Yose, na mama ya wana wa Zebedayo.+
57 Sasa kwa kuwa ilikuwa jioni, mtu mmoja tajiri wa Arimathea, anayeitwa Yosefu, ambaye yeye mwenyewe pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu, akaja.+ 58 Mtu huyu alimwendea Pilato na kuomba apewe mwili wa Yesu.+ Ndipo Pilato akaamuru apewe huo.+ 59 Na Yosefu akauchukua mwili huo, akaufunga katika kitani safi kizuri,+ 60 na kuulaza katika kaburi lake jipya,+ alilokuwa amechimba katika mwamba. Na, baada ya kuviringisha jiwe kubwa kwenye mlango wa lile kaburi, akaondoka.+ 61 Lakini Maria Magdalene na yule Maria mwingine wakabaki hapo, wakiwa wameketi mbele ya kaburi hilo.+
62 Siku iliyofuata, baada ya yale Matayarisho,+ wakuu wa makuhani na Mafarisayo walikusanyika pamoja mbele ya Pilato, 63 wakisema: “Bwana, tumekumbuka kwamba mjanja huyo alisema alipokuwa bado yuko hai, ‘Baada ya siku tatu+ nitafufuliwa.’ 64 Kwa hiyo amuru kaburi lilindwe mpaka siku ya tatu, ili wanafunzi wake wasipate kamwe kuja na kumwiba+ na kuwaambia watu, ‘Alifufuliwa kutoka kwa wafu!’ na ujanja huu wa mwisho utakuwa mbaya zaidi kuliko ule wa kwanza.” 65 Pilato akawaambia: “Ninyi mna walinzi.+ Nendeni mkalilinde jinsi mnavyojua.” 66 Basi wakaenda na kulilinda kaburi kwa kulitia jiwe muhuri+ na kuweka walinzi.
28 Baada ya siku ya sabato, kulipokuwa kukipambazuka katika siku ya kwanza ya juma, Maria Magdalene na yule Maria mwingine wakaja kulitazama kaburi.+
2 Na, tazama! tetemeko kubwa la nchi lilikuwa limetukia; kwa maana malaika wa Yehova alikuwa ameshuka kutoka mbinguni akakaribia na kuliviringisha jiwe, naye alikuwa ameketi juu yake.+ 3 Alionekana kama umeme,+ na mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji.+ 4 Ndiyo, wale walinzi wakatetemeka na kuwa kama wafu kwa sababu ya kumwogopa.
5 Lakini malaika+ akawajibu wanawake hao, akawaambia: “Msiogope, kwa maana ninajua mnamtafuta Yesu+ aliyetundikwa mtini. 6 Hayupo hapa, kwa maana alifufuliwa,+ kama alivyosema. Njooni, tazameni mahali alipokuwa amelala. 7 Nanyi nendeni upesi mkawaambie wanafunzi wake kwamba amefufuliwa+ kutoka kwa wafu, na, tazama! atawatangulia kuingia Galilaya;+ huko mtamwona. Tazama! Nimewaambia ninyi.”+
8 Kwa hiyo, wakaondoka upesi kaburini, wakiwa na woga na shangwe kubwa, wakakimbia kuwajulisha wanafunzi wake.+ 9 Na, tazama! Yesu akakutana nao na kusema: “Siku njema!” Wao wakakaribia, wakamshika miguu yake, wakamsujudia. 10 Ndipo Yesu akawaambia: “Msiogope! Nendeni, mkawajulishe ndugu zangu,+ ili wapate kwenda zao Galilaya; na huko wataniona.”
11 Walipokuwa wameondoka na kwenda, tazama! baadhi ya walinzi+ wakaingia jijini na kuwaambia wakuu wa makuhani mambo yote yaliyokuwa yametukia. 12 Na walipokuwa wamekusanyika pamoja wakiwa na wanaume wazee na kushauriana, wakawapa hao askari-jeshi kiasi cha kutosha cha vipande vya fedha+ 13 na kusema: “Semeni, ‘Wanafunzi wake+ walikuja wakati wa usiku wakamwiba tulipokuwa tumelala usingizi.’ 14 Na hilo likifika masikioni mwa gavana, tutamshawishi na tutawaondolea ninyi wasiwasi.” 15 Kwa hiyo wakachukua vile vipande vya fedha wakafanya kama walivyoagizwa; na maneno hayo yamesambazwa kotekote kati ya Wayahudi mpaka leo hii.
16 Hata hivyo, wale wanafunzi kumi na mmoja wakaingia Galilaya+ mpaka kwenye mlima ambako Yesu alikuwa amewafanyia mpango, 17 nao walipomwona wakasujudu, lakini baadhi yao walikuwa na shaka.+ 18 Naye Yesu akakaribia na kuwaambia, akisema: “Nimepewa mamlaka yote+ mbinguni na duniani. 19 Kwa hiyo nendeni mkafanye wanafunzi+ kutoka kwa watu wa mataifa yote,+ mkiwabatiza+ katika jina la Baba+ na la Mwana+ na la roho takatifu,+ 20 na kuwafundisha+ kushika+ mambo yote ambayo nimewaamuru ninyi.+ Na, tazama! mimi nipo pamoja nanyi+ siku zote mpaka umalizio wa mfumo wa mambo.”+
[Maelezo ya Chini]
Bonde la Hinomu. Tazama Nyongeza 2.
Bonde la Hinomu. Tazama Nyongeza 2.
Bonde la Hinomu. Tazama Nyongeza 2.
Bonde la Hinomu. Tazama Nyongeza 2.
Hadesi. Tazama Nyongeza 4.
Hadesi. Tazama Nyongeza 4.
Bonde la Hinomu. Tazama Nyongeza 2.
Bonde la Hinomu. Tazama Nyongeza 2.
Bonde la Hinomu. Tazama Nyongeza 2.