Kulingana na Marko
1 Mwanzo wa habari njema juu ya Yesu Kristo: 2 Kama ilivyoandikwa katika nabii Isaya: “(Tazama! Ninamtuma mjumbe wangu mbele ya uso wako, ambaye atakutayarishia njia;)+ 3 sikilizeni! mtu fulani anapaaza sauti nyikani, ‘Tayarisheni njia ya Yehova, nyoosheni barabara zake,’ ”+ 4 Yohana mbatizaji alitokea nyikani, akihubiri ubatizo unaoonyesha toba ili kupata msamaha wa dhambi.+ 5 Kwa sababu hiyo eneo lote la Yudea na wakaaji wote wa Yerusalemu wakamwendea, naye akawabatiza katika Mto Yordani, wakiungama waziwazi dhambi zao.+ 6 Basi Yohana alikuwa amevaa manyoya ya ngamia na mshipi wa ngozi kiunoni mwake,+ na alikuwa akila nzige+ na asali ya mwituni.+ 7 Naye alikuwa akihubiri, akisema: “Baada yangu mtu fulani mwenye nguvu kuliko mimi anakuja; mimi sistahili kuinama nizifungue kamba za viatu vyake.+ 8 Mimi niliwabatiza ninyi kwa maji, lakini yeye atawabatiza ninyi kwa roho takatifu.”+
9 Baada ya siku hizo Yesu akaja kutoka Nazareti ya Galilaya, Yohana akambatiza katika Yordani.+ 10 Mara moja alipopanda kutoka majini akaona mbingu zikifunguka, na roho ikashuka juu yake kama njiwa;+ 11 na sauti ikaja kutoka mbinguni: “Wewe ni Mwanangu, mpendwa; nimekukubali wewe.”+
12 Mara moja ile roho ikamshurutisha aende nyikani.+ 13 Basi akakaa nyikani siku 40,+ akijaribiwa na Shetani,+ naye alikuwa pamoja na wanyama-mwitu, lakini malaika walikuwa wakimhudumia.+
14 Basi baada ya Yohana kukamatwa Yesu akaenda Galilaya,+ akihubiri habari njema ya Mungu+ 15 na kusema: “Wakati uliowekwa umetimizwa,+ na ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni,+ na kuwa na imani katika habari njema.”
16 Alipokuwa akitembea kando ya bahari ya Galilaya alimwona Simoni+ na Andrea ndugu ya Simoni wakitupa nyavu zao huku na huku katika bahari, kwa maana walikuwa wavuvi.+ 17 Kwa hiyo Yesu akawaambia: “Nifuateni, nami nitawafanya ninyi kuwa wavuvi wa watu.”+ 18 Mara moja wakaziacha nyavu zao na kumfuata.+ 19 Baada ya kusonga mbele kidogo akamwona Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana ndugu yake walipokuwa katika mashua yao wakitengeneza nyavu zao;+ 20 na bila kukawia akawaita. Nao wakamwacha baba yao Zebedayo katika mashua hiyo pamoja na watu walioajiriwa, wakamfuata. 21 Nao wakaenda Kapernaumu.+
Mara baada ya hapo ilipokuwa siku ya sabato akaingia katika sinagogi akaanza kufundisha. 22 Nao wakastaajabia njia yake ya kufundisha,+ kwa maana huko alikuwa akiwafundisha kama mwenye mamlaka, na si kama waandishi.+ 23 Pia, wakati uleule katika sinagogi lao kulikuwako na mtu aliyekuwa chini ya nguvu za roho mchafu, naye akapaaza sauti,+ 24 akisema: “Tuna nini nawe, Yesu Mnazareti?+ Je, umekuja kutuangamiza? Ninajua+ wewe ni nani, Mtakatifu+ wa Mungu.”+ 25 Lakini Yesu akamkemea, akisema: “Nyamaza, na umtoke!”+ 26 Na yule roho mchafu, baada ya kumfanya agaegae na kupiga kelele kwa sauti kubwa, akamtoka.+ 27 Basi, watu wote wakashangaa sana hivi kwamba wakaanza mazungumzo kati yao wenyewe, wakisema: “Ni nini hili? Ni fundisho jipya! Yeye anawaagiza kwa nguvu zenye mamlaka hata roho wachafu, nao humtii.”+ 28 Kwa hiyo habari juu yake ikasambaa mara moja pande zote za nchi yote inayozunguka Galilaya.+
29 Nao wakatoka mara moja katika sinagogi wakaingia katika nyumba ya Simoni+ na Andrea pamoja na Yakobo na Yohana. 30 Basi mama-mkwe+ wa Simoni alikuwa amelala chini akiugua homa,+ nao mara moja wakamwambia Yesu juu yake. 31 Naye akamwendea akamwinua, akamshika mkono; na homa ikamwacha,+ naye akaanza kuwahudumia.+
32 Baada ya kuwa jioni, wakati jua lilipokuwa limetua, watu wakaanza kumletea watu wote waliokuwa wagonjwa+ na waliokuwa na roho waovu;+ 33 na jiji lote lilikuwa limekusanyika palepale mlangoni. 34 Kwa hiyo akawaponya wengi waliokuwa na magonjwa ya namna mbalimbali,+ naye akafukuza roho waovu wengi, lakini hakuwa akiwaruhusu roho waovu waseme, kwa sababu walijua kuwa yeye ni Kristo.+
35 Na asubuhi na mapema, kulipokuwa bado kuna giza, akatoka nje akaenda mahali ambapo hapakuwa na watu,+ na huko akaanza kusali.+ 36 Hata hivyo, Simoni na wale waliokuwa pamoja naye wakamtafuta kwa bidii 37 na kumpata, nao wakamwambia: “Watu wote wanakutafuta.” 38 Lakini akawaambia: “Twendeni mahali pengine, katika miji ya vijiji iliyo karibu, ili nipate kuhubiri huko pia,+ kwa maana nilitoka kwa kusudi hilo.”+ 39 Naye akaenda, akihubiri katika masinagogi yao katika Galilaya yote na kufukuza roho waovu.+
40 Huko pia mtu mwenye ukoma akamjia, akimsihi hata kwa kupiga magoti, akamwambia: “Ikiwa tu unataka, unaweza kunitakasa.”+ 41 Ndipo akamsikitikia,+ naye akanyoosha mkono wake akamgusa, akamwambia: “Ninataka. Takasika.”+ 42 Na mara moja ule ukoma ukamtoka, naye akawa safi.+ 43 Zaidi ya hilo, akampa maagizo thabiti na mara moja akamwacha aende, 44 na kumwambia: “Usimwambie mtu yeyote hata jambo moja, bali nenda ujionyeshe kwa kuhani+ na kutoa vile vitu alivyoamuru Musa kwa ajili ya kutakaswa+ kwako, ili kuwa ushahidi kwao.”+ 45 Lakini baada ya kwenda zake mtu huyo akaanza kutangaza sana juu ya hilo na kusambaza jambo hilo kotekote, hivi kwamba Yesu hakuweza tena kuingia waziwazi katika jiji, lakini akakaa nje katika mahali pasipo na watu. Na bado wakaendelea kumjia kutoka pande zote.+
2 Hata hivyo, baada ya siku kadhaa akaingia tena Kapernaumu na habari zikaenea kwamba yuko nyumbani.+ 2 Kwa hiyo wengi wakakusanyika, wengi sana hivi kwamba hapakuwa na nafasi tena, hata karibu na mlango, naye akaanza kuwaambia lile neno.+ 3 Na watu wakaja wakimletea mtu mwenye kupooza akiwa amebebwa na watu wanne.+ 4 Lakini kwa kutoweza kumleta moja kwa moja mpaka alipokuwa Yesu kwa sababu ya umati, wakaiondoa paa juu ya mahali alipokuwa, na baada ya kutoboa tundu wakakiteremsha kitanda ambacho juu yake yule mwenye kupooza alikuwa amelala.+ 5 Na Yesu alipoona imani+ yao akamwambia yule mwenye kupooza: “Mwanangu, dhambi zako zimesamehewa.”+ 6 Basi hapo palikuwa na baadhi ya waandishi, wakiwa wameketi na kuwaza mioyoni mwao:+ 7 “Kwa nini mtu huyu anaongea namna hii? Anakufuru. Nani anayeweza kusamehe dhambi ila mmoja, Mungu?”+ 8 Lakini Yesu, baada ya kutambua mara moja rohoni mwake kwamba walikuwa wakiwaza hivyo ndani yao wenyewe, akawaambia: “Kwa nini mnawaza mambo haya mioyoni mwenu?+ 9 Ni jambo gani lililo rahisi zaidi, kumwambia mwenye kupooza, ‘Umesamehewa dhambi zako,’ au kusema, ‘Simama, uchukue kitanda chako, utembee’?+ 10 Lakini ili mjue kwamba Mwana wa binadamu+ ana mamlaka ya kusamehe dhambi duniani,”+—akamwambia yule mwenye kupooza: 11 “Ninakuambia, Simama, uchukue kitanda chako, uende nyumbani kwako.”+ 12 Ndipo akaondoka, akachukua mara moja kitanda chake, akatembea mbele yao wote na kwenda nje,+ hivi kwamba wote wakastaajabu, nao wakamtukuza Mungu, wakisema: “Hatujaona kamwe jambo kama hilo.”+
13 Tena akaenda kando ya bahari; na umati wote ukaendelea kumjia, naye akaanza kuufundisha. 14 Lakini alipokuwa akipita kandokando, akamwona Lawi+ mwana wa Alfayo akiwa ameketi kwenye ofisi ya kodi, naye akamwambia: “Uwe mfuasi wangu.” Naye akaondoka, akamfuata.+ 15 Baadaye akawa ameketi mezani, nyumbani kwake, na wakusanya-kodi+ wengi na watenda-dhambi walikuwa wameketi pamoja na Yesu na wanafunzi wake, kwa maana walikuwa wengi nao wakaanza kumfuata.+ 16 Lakini waandishi wa Mafarisayo, walipoona alikuwa akila pamoja na watenda-dhambi na wakusanya-kodi, wakaanza kuwaambia wanafunzi wake: “Je, yeye hula pamoja na wakusanya-kodi na watenda-dhambi?”+ 17 Aliposikia hilo Yesu akawaambia: “Wale walio na nguvu hawahitaji tabibu, bali wale walio wagonjwa wanamhitaji. Nilikuja kuwaita, si watu waadilifu, bali watenda-dhambi.”+
18 Basi wanafunzi wa Yohana na Mafarisayo walikuwa na zoea la kufunga. Kwa hiyo wakaja wakamwambia: “Kwa nini wanafunzi wa Yohana na wanafunzi wa Mafarisayo hufunga, lakini wanafunzi wako hawafungi?”+ 19 Na Yesu akawaambia: “Je, wakati bwana-arusi yupo pamoja nao rafiki za bwana-arusi wanaweza kufunga?+ Maadamu wana bwana-arusi pamoja nao hawawezi kufunga.+ 20 Lakini siku zitakuja wakati ambapo bwana-arusi ataondolewa kwao, ndipo watakapofunga siku hiyo.+ 21 Hakuna mtu anayeshona kiraka cha nguo mpya juu ya vazi la nje la zamani; akifanya hivyo, nguvu zake huvuta ile nguo mpya kutoka kwenye lile vazi la zamani, nalo huraruka vibaya zaidi.+ 22 Pia, hakuna mtu anayeweka divai mpya ndani ya viriba vya divai vilivyozeeka; akifanya hivyo, divai hupasua ngozi ya viriba hivyo, na divai hupotea na vilevile ngozi.+ Bali watu huweka divai mpya ndani ya viriba vipya vya divai.”+
23 Basi akawa akipita katikati ya mashamba ya nafaka siku ya sabato, na wanafunzi wake wakaanza kupita waking’oa+ masuke ya nafaka.+ 24 Kwa hiyo Mafarisayo wakaanza kumwambia: “Tazama sasa! Kwa nini wanafanya jambo lisilo halali katika siku ya sabato?”+ 25 Lakini yeye akawaambia: “Je, hamjasoma hata mara moja jambo alilofanya Daudi+ alipokuwa na uhitaji akaona njaa, yeye na wale watu waliokuwa pamoja naye?+ 26 Jinsi alivyoingia ndani ya nyumba ya Mungu, katika lile simulizi juu ya Abiathari+ mkuu wa makuhani, akala mikate ya toleo,+ ambayo si halali+ kwa mtu yeyote kula ila makuhani, naye akawapa wale watu waliokuwa pamoja naye sehemu yake pia?”+ 27 Kwa hiyo akaendelea kuwaambia: “Sabato ilikuja kwa ajili ya mwanadamu,+ wala si mwanadamu kwa ajili ya sabato;+ 28 kwa sababu hiyo Mwana wa binadamu ni Bwana hata wa sabato.”+
3 Mara nyingine tena akaingia katika sinagogi, na mtu mmoja mwenye mkono uliopooza alikuwa humo.+ 2 Kwa hiyo walikuwa wakimchunguza sana waone kama angemponya mtu huyo katika siku ya sabato, ili wapate kumshtaki.+ 3 Naye akamwambia mtu huyo mwenye mkono uliopooza: “Simama uje katikati.” 4 Halafu akawaambia: “Je, katika siku ya sabato ni halali kutenda tendo jema au kutenda tendo baya, kuokoa au kuua nafsi?”+ Lakini wao wakakaa kimya. 5 Na baada ya kuwatazama huku na huku kwa ghadhabu, akiwa amehuzunishwa na jinsi mioyo yao+ ilivyokuwa migumu, akamwambia mtu huyo: “Nyoosha mkono wako.” Naye akaunyoosha, na mkono wake ukapona.+ 6 Ndipo Mafarisayo wakatoka na mara moja wakaanza kufanya baraza pamoja na wafuasi wa chama cha Herode+ juu yake, ili wamwangamize.+
7 Lakini Yesu pamoja na wanafunzi wake wakaondoka kwenda baharini; na umati mkubwa kutoka Galilaya na kutoka Yudea ukamfuata.+ 8 Hata kutoka Yerusalemu na kutoka Idumea na kutoka ng’ambo ya Yordani na kuzunguka Tiro+ na Sidoni, umati mkubwa, uliposikia alikuwa akifanya mambo mengi, ukamjia. 9 Naye akawaambia wanafunzi wake wawe na mashua ndogo sikuzote ya kutumia ili umati usiweze kumsonga. 10 Kwa kuwa aliwaponya watu wengi, wale wote waliokuwa na magonjwa yenye kuhuzunisha walikuwa wakimwangukia ili wamguse.+ 11 Hata roho wachafu,+ walipokuwa wakimwona, walikuwa wakijiangusha wenyewe chini mbele yake na kupaaza sauti, wakisema: “Wewe ndiye Mwana wa Mungu.”+ 12 Lakini mara nyingi aliwaagiza kwa kusisitiza wasifanye ajulikane.+
13 Naye akapanda mlima na kuwaita wale aliotaka,+ nao wakamwendea.+ 14 Naye akafanyiza kikundi cha watu kumi na wawili, ambao pia aliwaita “mitume,” ili waendelee kuwa pamoja naye na awatume wakahubiri+ 15 na kuwa na mamlaka ya kuwafukuza roho waovu.+
16 Na kikundi cha wale kumi na wawili aliofanyiza walikuwa Simoni, ambaye pia alimpa jina Petro,+ 17 na Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana ndugu ya Yakobo+ (hawa pia aliwapa jina Boanerge, ambalo linamaanisha Wana wa Ngurumo), 18 na Andrea na Filipo na Bartholomayo na Mathayo na Tomasi na Yakobo mwana wa Alfayo na Thadayo na Simoni Mkananayo 19 na Yuda Iskariote, ambaye baadaye alimsaliti.+
Naye akaingia ndani ya nyumba. 20 Mara nyingine tena umati ukakusanyika, hivi kwamba hawakuweza hata kula mlo.+ 21 Lakini watu wa jamaa+ yake waliposikia juu ya hilo, wakatoka kwenda kumshika, kwa maana walikuwa wakisema: “Amerukwa na akili.”+ 22 Pia, waandishi walioteremka kutoka Yerusalemu walikuwa wakisema: “Ana Beelzebuli, naye huwafukuza roho waovu kwa njia ya mtawala wa roho waovu.”+ 23 Kwa hiyo, baada ya kuwaita, akaanza kuzungumza nao kwa mifano: “Shetani anawezaje kumfukuza Shetani? 24 Kwani, ufalme ukigawanyika dhidi yake wenyewe, ufalme huo hauwezi kusimama;+ 25 na nyumba ikigawanyika dhidi yake yenyewe, nyumba hiyo haitaweza kusimama.+ 26 Pia, ikiwa Shetani ameinuka dhidi yake mwenyewe na kugawanyika, hawezi kusimama, bali anafikia mwisho.+ 27 Kwa kweli, hakuna yeyote ambaye ameingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu anayeweza kupora+ mali zake zinazoweza kuchukuliwa asipomfunga kwanza mtu huyo mwenye nguvu, na ndipo ataipora nyumba yake.+ 28 Kwa kweli ninawaambia ninyi kwamba wana wa binadamu watasamehewa mambo yote, hata ziwe ni dhambi gani na makufuru wanayofanya kwa kukufuru.+ 29 Hata hivyo, yeyote yule anayekufuru roho takatifu hatapata msamaha milele, bali ana hatia ya dhambi ya milele.”+ 30 Alisema hivyo kwa sababu walikuwa wakisema: “Ana roho mchafu.”+
31 Sasa mama yake na ndugu zake+ wakaja, na, walipokuwa wamesimama nje, wakatuma aitwe.+ 32 Ikawa kwamba, umati ulikuwa umeketi kumzunguka, kwa hiyo wakamwambia: “Tazama! Mama yako na ndugu zako wako nje wanakutafuta.”+ 33 Lakini akajibu, akawaambia: “Mama yangu na ndugu zangu ni nani?”+ 34 Na akiisha kuwatazama huku na huku wale waliokuwa wameketi kumzunguka, akasema: “Tazama, mama yangu na ndugu zangu!+ 35 Yeyote yule anayefanya mapenzi ya Mungu, huyo ndiye ndugu yangu na dada yangu na mama yangu.”+
4 Naye akaanza tena kufundisha kando ya bahari.+ Na umati mkubwa sana ukakusanyika karibu naye, hivi kwamba akapanda ndani ya mashua akaketi baharini, lakini umati wote kando ya bahari ulikuwa pwani.+ 2 Kwa hiyo akaanza kuwafundisha mambo mengi kwa mifano+ na kuwaambia katika kufundisha kwake:+ 3 “Sikilizeni. Tazama! Mpandaji alienda kupanda.+ 4 Naye alipokuwa akipanda, mbegu fulani zikaanguka kando ya barabara, na ndege wakaja wakazila.+ 5 Na mbegu nyingine zikaanguka mahali penye miamba ambapo, bila shaka, hapakuwa na udongo mwingi, nazo zikachipuka mara moja kwa sababu ya kutokuwa na udongo wenye kina.+ 6 Lakini jua lilipochomoza, zikaungua, na kwa sababu hazikuwa na mzizi zikanyauka.+ 7 Na mbegu nyingine zikaanguka katikati ya miiba, na ile miiba ikamea na kuzisonga, nazo hazikuzaa tunda lolote.+ 8 Lakini nyingine zikaanguka kwenye udongo mzuri,+ nazo zikamea na kuongezeka, zikaanza kuzaa matunda, nazo zilikuwa zikizaa matunda 30, na 60 na 100.”+ 9 Kwa hiyo akaongeza neno hili: “Yule aliye na masikio ya kusikiliza, na asikilize.”+
10 Basi alipokuwa peke yake, wale waliomzunguka pamoja na wale kumi na wawili wakaanza kumuuliza juu ya mifano hiyo.+ 11 Naye akaanza kuwaambia: “Ninyi mmepewa siri takatifu+ ya ufalme wa Mungu, lakini kwa wale walio nje mambo yote yanatukia kwa mifano,+ 12 ili, ingawa wanatazama, watazame na bado wasione, na, ingawa wanasikia, wasikie na bado wasielewe, wala wasigeuke kamwe na kusamehewa.”+ 13 Tena akawaambia: “Hamjui mfano huo, kwa hiyo basi mtaelewa namna gani mifano mingine yote?
14 “Mpandaji hulipanda neno.+ 15 Basi, hawa ndio wale walio kando ya barabara ambapo lile neno limepandwa, lakini mara tu baada ya kulisikia Shetani huja+ na kuliondoa neno lililopandwa ndani yao.+ 16 Vivyo hivyo hawa ndio wale waliopandwa mahali penye miamba: mara tu baada ya kulisikia neno, wanalipokea kwa shangwe.+ 17 Lakini hawana mzizi ndani yao wenyewe, bali wao huendelea kuwako kwa wakati fulani; kisha mara tu dhiki au mateso yanapotokea kwa sababu ya lile neno, wao hukwazika.+ 18 Bado kuna wengine wanaopandwa katikati ya miiba; hawa ndio ambao wamelisikia neno,+ 19 lakini mahangaiko+ ya mfumo huu wa mambo na nguvu za udanganyifu za utajiri+ na tamaa+ za mambo yale mengine hupenya na kulisonga neno, nalo hukosa kuzaa matunda.+ 20 Mwishowe, wale waliopandwa kwenye udongo mzuri ndio wale wanaolisikiliza neno na kulipokea vizuri na kuzaa matunda mara 30 na 60 na 100.”+
21 Naye akaendelea kuwaambia: “Je, taa huletwa ili kuwekwa chini ya kikapu cha kupimia au chini ya kitanda? Je, hailetwi ili kuwekwa juu ya kinara cha taa?+ 22 Kwa maana hakuna jambo lililofichwa ila kwa kusudi la kupata kufunuliwa; hakuna lililositiriwa kwa uangalifu ila kwa kusudi la kuja kutokea wazi.+ 23 Yeyote aliye na masikio ya kusikiliza, na asikilize.”+
24 Tena akawaambia: “Sikilizeni kwa makini mambo ambayo mnasikia.+ Kwa kipimo mnachopimia, mtapimiwa hicho,+ ndiyo, mtaongezewa zaidi.+ 25 Kwa maana aliye na kitu ataongezewa; lakini yule ambaye hana kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.”+
26 Kwa hiyo akaendelea kusema: “Katika njia hii ufalme wa Mungu ni kama vile mtu anapotupa mbegu kwenye udongo,+ 27 naye hulala usingizi usiku na huamka mchana, na ile mbegu huota na hukua na kuwa ndefu, naye hajui ni jinsi gani hasa.+ 28 Udongo wenyewe hutokeza matunda hatua kwa hatua, kwanza jani, kisha suke, mwishowe nafaka iliyo kamili katika suke. 29 Lakini mara tu matunda yanaporuhusu, yeye huutia mundu, kwa sababu wakati wa mavuno umefika.”
30 Naye akaendelea kusema: “Tutaufananisha ufalme wa Mungu na nini, au tutauweka katika mfano gani?+ 31 Kama mbegu ya haradali, ambayo ilipopandwa katika udongo ilikuwa ndiyo mbegu ndogo zaidi kuliko zote duniani+— 32 lakini baada ya kupandwa, humea na kuwa kubwa zaidi kuliko mboga nyingine zote na hutokeza matawi makubwa,+ hivi kwamba ndege wa mbinguni+ wanaweza kupata makao chini ya kivuli chake.”+
33 Kwa hiyo alikuwa akisema nao lile neno kwa mifano+ mingi ya namna hiyo, kwa kadiri walivyoweza kusikiliza. 34 Kwa kweli, hakuwa akisema nao bila mfano, lakini kwa faragha alikuwa akiwaeleza wanafunzi wake mambo yote.+
35 Na siku hiyo, ilipokuwa jioni, akawaambia: “Na tuvuke mpaka ukingo ule mwingine wa bahari.”+ 36 Kwa hiyo, walipokuwa wamekwisha kuuruhusu umati uondoke, wakamchukua katika mashua, kama vile alivyokuwa, na kulikuwa na mashua nyinginezo pamoja naye.+ 37 Sasa kukatokea dhoruba kubwa ya upepo wenye nguvu nyingi, na mawimbi yakawa yakiipiga mashua kwa nguvu, hivi kwamba karibu mashua ifunikwe na maji.+ 38 Lakini yeye alikuwa katika tezi, akiwa amelalia mto. Kwa hiyo wakamwamsha na kumwambia: “Mwalimu, je, hujali kwamba tuko karibu kuangamia?”+ 39 Ndipo akaamka, akaukemea upepo na kuiambia bahari: “Nyamaza, utulie!”+ Na upepo ukapunguka, kukawa utulivu mkubwa.+ 40 Kwa hiyo akawaambia: “Kwa nini mna moyo wa woga? Je, bado hamna imani yoyote?” 41 Lakini wakaogopa isivyo kawaida, nao wakawa wakiambiana: “Kwa kweli huyu ni nani, kwa sababu hata upepo na bahari zinamtii?”+
5 Basi, wakafika upande ule mwingine wa bahari na kuingia katika nchi ya Wagerasene.+ 2 Na mara tu alipotoka katika mashua mtu mmoja mwenye roho mchafu akakutana naye kutoka kati ya makaburi.+ 3 Alikuwa akikaa katikati ya makaburi; na kufikia wakati huo hakuna mtu aliyeweza kumfunga hata kwa mnyororo, 4 kwa sababu alikuwa amefungwa mara nyingi kwa pingu na minyororo, lakini akaikata minyororo na kuzivunja pingu; wala hakuna mtu aliyekuwa na nguvu za kumshinda. 5 Na sikuzote, usiku na mchana alikuwa akipaaza sauti makaburini na milimani na kujikatakata kwa mawe. 6 Lakini alipomwona Yesu akiwa mbali akakimbia akamsujudia, 7 na, alipopaaza sauti kubwa,+ akasema: “Nina nini nawe, Yesu, Mwana wa Mungu Aliye Juu Zaidi?+ Ninakuapisha+ kwa Mungu usinitese.”+ 8 Kwa maana alikuwa amemwambia: “Mtoke mtu huyu, wewe roho mchafu.”+ 9 Lakini Yesu akaanza kumuuliza: “Jina lako ni nani?” Naye akamwambia: “Jina langu ni Kikosi,+ kwa sababu tuko wengi.”+ 10 Naye akamsihi mara nyingi asiwafukuze roho hao watoke katika nchi hiyo.+
11 Basi kulikuwa na kundi kubwa la nguruwe+ likilisha mlimani.+ 12 Kwa hiyo wakamsihi, wakisema: “Acha twende kwa wale nguruwe, ili tuingie ndani yao.” 13 Naye akawaruhusu. Ndipo wale roho wachafu wakatoka na kuingia ndani ya wale nguruwe; na lile kundi likatimua mbio, likaruka poromoko, likaingia baharini, wakiwa karibu elfu mbili, nao wakafa maji mmoja baada ya mwingine katika bahari.+ 14 Lakini wachungaji wa nguruwe hao wakakimbia wakapeleka habari jijini na mashambani; na watu wakaja kuona kilichokuwa kimetukia.+ 15 Kwa hiyo wakamjia Yesu, nao wakamwona yule mtu aliyekuwa na roho waovu akiwa ameketi amevaa nguo na akiwa na akili yake timamu, mtu yule aliyekuwa na kile kikosi; nao wakaogopa. 16 Pia, wale waliokuwa wameona jambo hilo wakawasimulia jinsi ilivyokuwa imetukia kwa mtu huyo aliyekuwa na roho waovu na juu ya wale nguruwe. 17 Na kwa hiyo wakaanza kumsihi atoke katika wilaya zao.+
18 Basi alipokuwa akipanda mashua, yule mtu aliyekuwa na roho waovu akaanza kumsihi akae pamoja naye.+ 19 Hata hivyo, hakumruhusu, bali alimwambia: “Nenda nyumbani kwa watu wa jamaa yako,+ ukawaambie mambo yote ambayo Yehova+ amekufanyia na jinsi alivyokuonyesha rehema.”+ 20 Naye akaenda zake akaanza kutangaza katika Dekapoli+ juu ya mambo yote ambayo Yesu alimfanyia, na watu wote wakaanza kustaajabu.+
21 Baada ya Yesu kuvuka tena katika mashua na kurudi mpaka ule ukingo wa bahari wa upande wa pili umati mkubwa ukakusanyika pamoja mahali alipokuwa; naye alikuwa kando ya bahari.+ 22 Sasa mmoja wa maofisa-wasimamizi wa sinagogi, anayeitwa Yairo, akaja na, alipomwona, akamwangukia miguuni+ 23 akamsihi mara nyingi, akisema: “Binti yangu mdogo yuko katika hali mbaya sana. Njoo tafadhali uweke mikono+ yako juu yake ili apone na kuishi.”+ 24 Ndipo akaenda pamoja naye. Nao umati mkubwa ulikuwa ukimfuata na kumsonga.+
25 Basi kulikuwa na mwanamke aliyekuwa na mtiririko wa damu+ kwa miaka kumi na miwili,+ 26 naye alikuwa ameumizwa sana na matabibu wengi+ na alikuwa ametumia mali zake zote naye hakuwa amefaidika bali, badala yake, hali yake ikawa mbaya zaidi. 27 Aliposikia juu ya Yesu, akaja kutoka nyuma katika ule umati na kuligusa+ vazi lake la nje; 28 kwa maana alikuwa akisema: “Nikiyagusa tu mavazi yake ya nje nitapona.”+ 29 Na mara moja chemchemi yake ya damu ikakauka, naye akahisi mwilini mwake kwamba alikuwa amepona ule ugonjwa wenye kuhuzunisha.+
30 Mara moja, pia, Yesu akatambua ndani yake mwenyewe kwamba nguvu+ zilikuwa zimemtoka, naye akageuka huku na huku katika ule umati na kuanza kusema: “Ni nani aliyeyagusa mavazi yangu ya nje?”+ 31 Lakini wanafunzi wake wakaanza kumwambia: “Unaona umati unavyokusonga,+ nawe unasema, ‘Ni nani aliyenigusa?’ ” 32 Hata hivyo, alikuwa akitazama huku na huku ili amwone mwanamke aliyekuwa amefanya hivyo. 33 Lakini huyo mwanamke, akiogopa na kutetemeka, akijua lililokuwa limetukia, akaja, akaanguka chini mbele yake, akamwambia kweli yote.+ 34 Yesu akamwambia: “Binti yangu, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani,+ na uwe na afya njema kutokana na ugonjwa wako wenye kuhuzunisha.”+
35 Alipokuwa bado akisema, watu fulani kutoka nyumbani kwa yule ofisa-msimamizi wa sinagogi wakaja na kusema: “Binti yako amekufa! Kwa nini uendelee kumsumbua mwalimu?”+ 36 Lakini Yesu akasikia yaliyokuwa yakisemwa, akamwambia ofisa-msimamizi wa sinagogi: “Usiogope, uwe tu na imani.”+ 37 Basi hakumruhusu mtu yeyote afuatane naye ila Petro na Yakobo na Yohana ndugu ya Yakobo.+
38 Kwa hiyo wakafika kwenye nyumba ya yule ofisa-msimamizi wa sinagogi, naye akaona ule mvurugo wenye kelele na wale wenye kulia na kupiga kelele nyingi za kuomboleza, 39 na, baada ya kuingia, akawaambia: “Kwa nini mnatokeza mvurugo wenye kelele na kulia? Mtoto mchanga hakufa, bali analala usingizi.”+ 40 Ndipo wakaanza kumcheka kwa dharau. Lakini, akiisha kuwatoa nje wote, akamchukua baba na mama ya huyo mtoto mchanga na walio pamoja naye, naye akaingia mahali alipokuwa mtoto huyo.+ 41 Na, akiushika mkono wa mtoto huyo, akamwambia: “Talitha kumi,” maneno ambayo yanapotafsiriwa, yanamaanisha: “Mwanamwali, ninakuambia, Simama!”+ 42 Na mara yule mwanamwali akasimama akaanza kutembea, kwa maana alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili. Na mara moja wakawa na shangwe kubwa.+ 43 Lakini akawaagiza tena na tena wasimwambie mtu yeyote+ juu ya hilo, naye akasema kwamba mtoto huyo apewe chakula ale.
6 Naye akatoka huko na kuingia katika eneo lake la nyumbani, na wanafunzi wake wakamfuata.+ 2 Ilipofika siku ya sabato, akaanza kufundisha katika sinagogi; na hesabu kubwa zaidi ya wale waliokuwa wakisikiliza wakastaajabu na kusema: “Mtu huyu alipata wapi mambo haya?+ Na kwa nini mtu huyu apewe hekima hii, naye afanye matendo yenye nguvu hivyo kwa mikono yake? 3 Je, huyu si yule seremala+ mwana wa Maria+ na ndugu ya Yakobo+ na Yosefu na Yuda na Simoni?+ Na dada zake wapo hapa pamoja nasi, sivyo?” Kwa hiyo wakaanza kukwazika kwa sababu yake.+ 4 Lakini Yesu akaendelea kuwaambia: “Nabii hakosi kuheshimiwa ila katika eneo lake la nyumbani+ na katikati ya watu wa jamaa yake na katika nyumba yake mwenyewe.”+ 5 Kwa hiyo hakuweza kufanya matendo yenye nguvu huko ila kuweka mikono yake juu ya wagonjwa wachache na kuwaponya. 6 Kwa kweli, alistaajabia ukosefu wao wa imani. Naye akaenda akizunguka vijijini, akifundisha.+
7 Sasa akawaita wale kumi na wawili, akaanza kuwatuma wawili-wawili,+ naye akaanza kuwapa mamlaka juu ya roho wachafu.+ 8 Pia, akawaagiza wasichukue kitu chochote kwa ajili ya safari, wala mkate, wala mfuko wa chakula,+ wala pesa za shaba katika mikoba kwenye mishipi yao ila fimbo tu,+ 9 lakini wafunge viatu, na wasivae mavazi mawili ya ndani.+ 10 Zaidi ya hayo, akawaambia: “Popote mtakapoingia katika nyumba,+ kaeni humo mpaka mtakapoondoka.+ 11 Na mahali popote ambapo hamtapokewa wala kusikilizwa, mnapoondoka yakung’uteni mavumbi yaliyo chini ya miguu yenu ili kuwa ushahidi kwao.”+ 12 Kwa hiyo wakaondoka na kuhubiri ili watu wapate kutubu;+ 13 nao walikuwa wakitoa roho waovu+ wengi na kuwapaka mafuta+ watu wengi waliokuwa wagonjwa na kuwaponya.+
14 Basi Mfalme Herode akasikia, kwa maana jina la Yesu lilikuwa limejulikana na watu wote, na watu walikuwa wakisema: “Yohana mbatizaji amefufuliwa kutoka kwa wafu, na kwa sababu hiyo anatenda kazi zenye nguvu.”+ 15 Lakini wengine walikuwa wakisema: “Ni Eliya.”+ Bado wengine walikuwa wakisema: “Ni nabii kama mmoja wa manabii.”+ 16 Lakini Herode aliposikia hilo akaanza kusema: “Yohana ambaye nilimkata kichwa, ndiye huyo amefufuliwa.”+ 17 Kwa maana Herode mwenyewe alikuwa ametuma watu wakamkamata Yohana na kumfunga gerezani kwa sababu ya Herodia mke wa Filipo ndugu yake, kwa sababu Herode alikuwa amemwoa.+ 18 Kwa maana Yohana alikuwa amemwambia Herode tena na tena: “Si halali wewe kuwa na mke wa ndugu yako.”+ 19 Lakini Herodia alikuwa na kinyongo+ moyoni kumwelekea na alikuwa akitaka kumuua, lakini hakuweza.+ 20 Kwa maana Herode alikuwa akimwogopa+ Yohana, na alimjua kuwa mtu mwadilifu na mtakatifu;+ naye alikuwa akimlinda. Na baada ya kumsikia+ akawa hajui kabisa la kufanya, lakini aliendelea kumsikia kwa furaha.
21 Lakini siku inayofaa+ ikafika wakati Herode alipoandaa mlo wa jioni kwenye sikukuu ya kuzaliwa+ kwake kwa ajili ya wenye daraja la juu na viongozi wake wa kijeshi na walio wa cheo cha kwanza kabisa wa Galilaya. 22 Na binti ya Herodia huyohuyo akaingia, akacheza dansi na kumpendeza Herode na wale wenye kuketi+ pamoja naye. Mfalme akamwambia mwanamwali huyo: “Niombe chochote unachotaka, nami nitakupa.” 23 Ndiyo, akamwapia: “Chochote utakachoniomba, nitakupa hicho,+ hata nusu ya ufalme wangu.”+ 24 Naye akaenda akamwambia mama yake: “Niombe nini?” Akamwambia: “Kichwa cha Yohana mbatizaji.”+ 25 Mara akaingia haraka mpaka mahali alipokuwa mfalme na kutoa ombi lake, akisema: “Nataka unipe sasa hivi kwenye sahani kichwa cha Yohana Mbatizaji.” 26 Ijapokuwa mfalme alikuwa na huzuni sana, lakini hakutaka kumpuuza, kwa kufikiria vile viapo na wale waliokuwa wameketi mezani.+ 27 Kwa hiyo mara moja mfalme akamtuma mlinzi wa mfalme na kumwamuru akalete kichwa chake. Naye akaenda akamkata kichwa gerezani+ 28 akakileta kichwa chake kwenye sahani, naye akampa yule mwanamwali, naye mwanamwali akampa mama yake.+ 29 Wanafunzi wake waliposikia juu ya hilo wakaja wakachukua maiti yake na kuilaza katika kaburi.+
30 Nao mitume wakakusanyika pamoja mbele ya Yesu na kumwambia mambo yote waliyokuwa wamefanya na kufundisha.+ 31 Naye akawaambia: “Njooni, ninyi wenyewe, faraghani katika mahali pasipo na watu+ mpumzike kidogo.”+ Kwa maana watu walikuwa wakija na kwenda, nao hawakuwa hata na wakati wa kula mlo.+ 32 Kwa hiyo wakaenda zao wakiwa katika mashua wakawe peke yao katika mahali pasipo na watu.+ 33 Lakini watu wakawaona wakienda na wengi wakapata kujua hilo, na kutoka katika majiji yote wakakimbia pamoja kwenda huko kwa miguu na kufika mbele yao.+ 34 Basi, aliposhuka, akaona umati mkubwa, lakini akawasikitikia,+ kwa sababu walikuwa kama kondoo wasio na mchungaji.+ Naye akaanza kuwafundisha mambo mengi.+
35 Kufikia wakati huo saa ilikuwa imesonga sana, na wanafunzi wake wakamjia na kuanza kusema: “Mahali hapa hapana watu, na saa tayari imesonga sana.+ 36 Waache waende zao, ili waende mashambani na kwenye vijiji vinavyozunguka wakajinunulie chakula.”+ 37 Akajibu akawaambia: “Ninyi wapeni chakula.” Ndipo wakamwambia: “Je, twende tukanunue mikate yenye thamani ya dinari mia mbili na kuwapa watu ili wale?”+ 38 Akawaambia: “Mna mikate mingapi? Nendeni mkaone!” Baada ya kuhakikisha, wakasema: “Mitano, na samaki wawili.”+ 39 Naye akawaagiza watu wote waketi wakiwa vikundi-vikundi+ juu ya majani mabichi.+ 40 Nao wakajilaza chini katika vikundi vya watu 100 na vya watu 50.+ 41 Sasa akaichukua ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni akatoa baraka,+ akaimega+ ile mikate na kuanza kuwapa wanafunzi, ili wapate kuiweka mbele ya watu hao; naye akawagawanya wale samaki wawili kwa ajili ya watu wote. 42 Kwa hiyo wote wakala, wakashiba;+ 43 nao wakaokota vipande, vikapu kumi na viwili vilivyojaa, mbali na wale samaki. 44 Zaidi ya hayo, wale waliokula ile mikate walikuwa wanaume elfu tano.+
45 Na, bila kukawia, akawaagiza wanafunzi wake waipande mashua na kumtangulia kwenda ukingo wa pili wa bahari kuelekea Bethsaida, huku yeye mwenyewe akiuruhusu umati uende.+ 46 Lakini baada ya kuwaaga akaenda mlimani ili asali.+ 47 Sasa ilipokuwa jioni, mashua ilikuwa katikati ya bahari, lakini yeye alikuwa peke yake kwenye nchi kavu.+ 48 Na alipowaona wakitaabika+ katika kuvuta kwao makasia, kwa maana upepo ulikuwa ukivuma kinyume chao, karibu kesha la nne la usiku akawaendea, akitembea juu ya bahari; lakini alitaka kuwapita. 49 Walipomwona akitembea juu ya bahari wakafikiri: “Ni mzuka!” nao wakapaaza sauti kubwa.+ 50 Kwa maana wote walimwona, wakataabika. Lakini mara moja akasema nao, naye akawaambia: “Jipeni moyo, ni mimi; msiogope.”+ 51 Naye akapanda na kuingia katika mashua pamoja nao, na upepo ukapungua. Ndipo wakashangaa sana ndani yao wenyewe,+ 52 kwa maana hawakuwa wamefahamu maana ya ile mikate, bali mioyo yao ilikuwa mizito isiweze kuelewa.+
53 Na walipovuka mpaka nchi kavu, wakaingia Genesareti na kutia meli nanga hapo karibu.+ 54 Lakini mara tu waliposhuka kutoka katika mashua, watu wakamtambua, 55 nao wakakimbia kuzunguka eneo lote hilo na kuanza kuwachukua huku na huku juu ya vitanda wale waliokuwa wakiugua mpaka kule walikosikia alikuwako. 56 Na kokote alikokuwa akiingia vijijini au majijini au mashambani+ walikuwa wakiweka wale wagonjwa sokoni, nao walikuwa wakiomba ili wapate kuugusa+ tu upindo+ wa vazi lake la nje. Na wote waliougusa wakapona.+
7 Sasa Mafarisayo na baadhi ya waandishi waliokuwa wamekuja kutoka Yerusalemu wakakusanyika kumzunguka.+ 2 Nao walipoona baadhi ya wanafunzi wake wakila mlo wao kwa mikono najisi, yaani, ambayo haijanawishwa+— 3 kwa maana Mafarisayo na Wayahudi wote hawali isipokuwa wawe wamenawa mikono yao mpaka kwenye kiwiko, kwa kushika sana mapokeo ya watu wa nyakati za hapo zamani, 4 na, wanaporudi kutoka sokoni, hawali chakula isipokuwa wawe wamejisafisha kwa kunyunyiza; na kuna mapokeo+ mengine mengi ambayo wamepokea ili kushika sana, ubatizo wa vikombe na mitungi na vyombo vya shaba;+— 5 Kwa hiyo Mafarisayo na waandishi hao wakamuuliza: “Kwa nini wanafunzi wako hawajiendeshi kulingana na mapokeo ya watu wa zamani, bali hula mlo wao kwa mikono iliyo najisi?”+ 6 Akawaambia: “Isaya kwa kufaa alitoa unabii juu yenu wanafiki, kama ilivyoandikwa,+ ‘Watu hawa huniheshimu mimi kwa midomo yao, bali mioyo yao iko mbali nami.+ 7 Wao huniabudu bure, kwa sababu wao hufundisha amri za wanadamu kuwa mafundisho.’+ 8 Mnaiacha amri ya Mungu, na kuyashika sana mapokeo ya wanadamu.”+
9 Zaidi ya hayo, akaendelea kuwaambia: “Kwa ustadi mnaweka kando amri+ ya Mungu kusudi mbaki na mapokeo yenu. 10 Kwa mfano, Musa alisema, ‘Mheshimu baba yako na mama yako,’+ na, ‘Yule anayemtukana baba yake au mama yake na afe.’+ 11 Lakini ninyi husema, ‘Mtu akimwambia baba yake au mama yake: “Chochote nilicho nacho unachoweza kufaidika nacho kutoka kwangu ni korbani,+ (yaani, zawadi iliyowekwa wakfu+ kwa Mungu,)” ’— 12 Ninyi hammruhusu afanye hata jambo moja kwa ajili ya baba yake au mama yake,+ 13 na hivyo mnalibatilisha neno la Mungu+ kwa mapokeo yenu ambayo mlipewa. Nanyi hufanya mambo mengi+ yanayofanana na hilo.” 14 Kwa hiyo, akiuita tena umati kwake, akaendelea kuuambia: “Nisikilizeni, ninyi nyote, mpate maana.+ 15 Hakuna kitu chochote kutoka nje ya mtu kinachoingia ndani yake ambacho kinaweza kumtia unajisi; bali mambo yanayotoka ndani ya mtu ndiyo mambo yanayomtia mtu unajisi.”+ 16 ——
17 Basi alipokuwa ameingia katika nyumba akiwa mbali na umati, wanafunzi wake wakaanza kumuuliza habari ya mfano huo.+ 18 Kwa hiyo akawaambia: “Ninyi pia hamna ufahamu kama wao?+ Je, hamjui kwamba hakuna chochote kutoka nje kinachoingia ndani ya mtu ambacho kinaweza kumtia unajisi, 19 kwa kuwa hicho hupita na kuingia, si ndani ya moyo wake, bali ndani ya matumbo yake, nacho hutoka nje na kuingia ndani ya shimo la choo?”+ Kwa njia hiyo akatangaza vyakula vyote kuwa safi.+ 20 Tena akasema: “Kile ambacho hutoka ndani ya mtu ndicho humtia mtu unajisi;+ 21 kwa maana kutoka ndani, kutoka katika moyo wa watu,+ hutoka mawazo mabaya: uasherati,+ wizi, mauaji,+ 22 uzinzi, kutamani,+ matendo ya uovu, udanganyifu, mwenendo mpotovu,+ jicho lenye wivu, makufuru, majivuno, ukosefu wa akili. 23 Mambo hayo yote maovu hutoka ndani nayo humtia mtu unajisi.”+
24 Akatoka huko, akaenda katika maeneo ya Tiro na Sidoni.+ Naye akaingia katika nyumba wala hakutaka mtu yeyote ajue. Na bado hakuweza kuepuka kutambuliwa;+ 25 lakini mara moja mwanamke ambaye binti yake mdogo alikuwa na roho mchafu akasikia habari zake akaja na kujiangusha chini miguuni pake.+ 26 Yule mwanamke alikuwa wa kutoka Ugiriki, wa taifa la Sirofoinike; naye akawa akimwomba amfukuze roho mwovu kutoka katika binti yake.+ 27 Lakini akaanza kumwambia mwanamke huyo: “Kwanza acha watoto washibe, kwa maana si sawa kuuchukua mkate wa watoto+ na kuwatupia mbwa wadogo.”+ 28 Hata hivyo, mwanamke huyo akajibu, akamwambia: “Ndiyo, bwana, lakini hao mbwa wadogo walio chini ya meza hula sehemu ya makombo+ ya watoto wadogo.”+ 29 Ndipo akamwambia mwanamke huyo: “Kwa sababu umesema hivyo, nenda; yule roho mwovu amemtoka binti yako.”+ 30 Kwa hiyo akaenda nyumbani kwake na kumkuta+ huyo mtoto mchanga akiwa amelazwa kitandani na roho mwovu amemtoka.
31 Basi alipokuwa akirudi kutoka katika maeneo ya Tiro akapitia Sidoni mpaka bahari ya Galilaya akipanda na kupita katikati ya maeneo ya Dekapoli.+ 32 Huko wakamletea mtu aliye kiziwi na mwenye kizuizi cha usemi, nao wakamsihi aweke mkono wake juu yake.+ 33 Naye akamchukua kutoka katika umati na kumpeleka mahali pasipo na watu akaweka vidole vyake ndani ya masikio ya yule mtu na, baada ya kutema mate, akamgusa ulimi wake.+ 34 Naye akatazama juu mbinguni,+ akavuta pumzi+ kwa nguvu na kumwambia: “Efatha,” yaani, “Funguka.” 35 Basi, uwezo wake wa kusikia ukafunguka,+ na kile kifungo cha ulimi wake kikafunguliwa, naye akaanza kusema kama kawaida. 36 Ndipo akawaamuru wasimwambie yeyote;+ lakini kwa kadiri alivyozidi kuwawaamuru, ndivyo walivyozidi kutangaza jambo hilo.+ 37 Kwa kweli, walikuwa wakistaajabu+ sana nao wakasema: “Amefanya mambo yote vema. Anafanya hata viziwi wasikie na wasioweza kusema, waseme.”+
8 Siku hizo, kulipokuwa tena na umati mkubwa nao haukuwa na chakula, akawaita wanafunzi na kuwaambia:+ 2 “Ninausikitikia+ umati, kwa sababu tayari wamekaa nami siku tatu nao hawana chakula; 3 nami nikiwaambia waende nyumbani kwao wakiwa wamefunga, watazimia barabarani. Kwa kweli, baadhi yao wanatoka mbali.” 4 Lakini wanafunzi wake wakamjibu: “Mtu yeyote aliye mahali hapa pasipo na watu atawashibisha watu hawa kwa mikate kutoka wapi?”+ 5 Na bado akaendelea kuwauliza: “Mna mikate mingapi?” Wakasema: “Saba.”+ 6 Naye akauagiza umati uketi chini, naye akaichukua ile mikate saba, akashukuru,+ akaimega, na kuanza kuwapa wanafunzi wake waigawe, nao wakaugawia umati.+ 7 Walikuwa pia na samaki wadogo wachache; na, akiisha kuwabariki, akawaambia wawagawe hao pia.+ 8 Basi wakala na kushiba, nao wakaokota ziada ya vipande vidogo, vikapu saba vya chakula vilivyojaa.+ 9 Ingawa kulikuwa na karibu wanaume elfu nne. Mwishowe akawaacha waende zao.+
10 Na mara akaipanda mashua pamoja na wanafunzi wake akaingia katika zile sehemu za Dalmanutha.+ 11 Tazama, Mafarisayo wakatokea na kuanza kubishana naye, wakitafuta kwake ishara kutoka mbinguni, ili kumjaribu.+ 12 Kwa hiyo akaugua sana+ rohoni mwake, na kusema: “Kwa nini kizazi hiki kinatafuta ishara? Kwa kweli mimi ninasema, Kizazi hiki hakitapewa ishara yoyote.”+ 13 Ndipo akawaacha, akapanda ndani tena, na kwenda mpaka ukingo wa pili wa bahari.
14 Ikawa kwamba walisahau kuichukua mikate, na hawakuwa na kitu katika mashua ila mkate mmoja.+ 15 Naye akaanza kuwaagiza waziwazi na kusema: “Endeleeni kufungua macho yenu, jihadharini na chachu ya Mafarisayo na chachu ya Herode.”+ 16 Kwa hiyo wakaanza kubishana kwa sababu hawakuwa na mikate yoyote.+ 17 Akijua hilo, akawaambia: “Kwa nini mnabishana kwa sababu hamna mikate?+ Je, bado hamjaelewa wala kupata maana? Je, mioyo yenu ni mizito isiweze kuelewa?+ 18 ‘Ijapokuwa mna macho, hamwoni; na ijapokuwa mna masikio, hamsikii?’+ Na je, hamkumbuki, 19 wakati nilipoimega ile mikate mitano+ kwa ajili ya wale wanaume elfu tano, mliokota vikapu vingapi vilivyokuwa vimejaa vipande?” Wakamwambia: “Kumi na viwili.”+ 20 “Nilipoimega ile mikate saba kwa ajili ya wale wanaume elfu nne, mliokota vikapu vingapi vya chakula vilivyokuwa vimejaa vipande?” Nao wakamwambia: “Saba.”+ 21 Ndipo akawaambia: “Je, bado hamjapata maana?”+
22 Sasa wakafika Bethsaida. Tazama, watu wakamletea mtu aliye kipofu, nao wakamsihi amguse.+ 23 Naye akamshika mkono yule mtu aliyekuwa kipofu, akamtoa nje ya kijiji, na, baada ya kutema mate+ juu ya macho yake, Yesu akaweka mikono juu yake na kuanza kumuuliza: “Je, unaona kitu chochote?” 24 Na yule mtu akatazama juu na kuanza kusema: “Ninaona watu, kwa sababu ninaona vitu vinavyoonekana kama miti, lakini vinatembea huku na huku.” 25 Kisha akaweka mikono yake tena juu ya macho ya mtu huyo, na mtu huyo akaona waziwazi, naye akapona, naye alikuwa akiona kila kitu waziwazi. 26 Kwa hiyo akamwagiza aende nyumbani, akisema: “Lakini usiingie kijijini.”+
27 Yesu na wanafunzi wake wakaondoka kwenda vijiji vya Kaisaria Filipi, na njiani akaanza kuwauliza wanafunzi wake, akisema: “Watu wanasema mimi ni nani?”+ 28 Wakamwambia: “Yohana Mbatizaji,+ na wengine, Eliya,+ na wengine bado, Mmoja wa manabii.”+ 29 Naye akawauliza: “Ingawa hivyo, ninyi mnasema mimi ni nani?” Petro akajibu akamwambia: “Wewe ndiye Kristo.”+ 30 Ndipo akawapa onyo kali wasimwambie mtu yeyote juu yake.+ 31 Pia, akaanza kuwafundisha kwamba Mwana wa binadamu lazima apatwe na mateso mengi na kukataliwa na wanaume wazee na wakuu wa makuhani na waandishi na kuuawa,+ na kufufuka siku tatu baadaye.+ 32 Kwa kweli, alikuwa akisema hayo waziwazi. Lakini Petro akamchukua kando na kuanza kumkemea.+ 33 Akageuka, akawatazama wanafunzi wake, akamkemea Petro, na kusema: “Nenda nyuma yangu, Shetani, kwa sababu wewe unafikiri, si fikira za Mungu, bali za wanadamu.”+
34 Basi akauita umati pamoja na wanafunzi wake na kuwaambia: “Mtu yeyote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe na kuuchukua mti wake wa mateso na kunifuata sikuzote.+ 35 Kwa maana yeyote yule anayetaka kuiokoa nafsi yake ataipoteza; lakini yeyote yule anayeipoteza nafsi yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya habari njema ataiokoa.+ 36 Kwa kweli, mtu anapata faida gani ikiwa ataupata ulimwengu wote na kuipoteza nafsi yake?+ 37 Kwa kweli, mtu anaweza kutoa nini ili aipate nafsi yake?+ 38 Kwa maana mtu yeyote yule anayenionea aibu mimi na maneno yangu katika kizazi hiki chenye uzinzi na chenye dhambi, Mwana wa binadamu atamwonea aibu+ yeye pia atakapofika katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu.”+
9 Zaidi ya hayo, akaendelea kuwaambia: “Kwa kweli ninawaambia ninyi, Kuna baadhi ya wale wanaosimama hapa ambao hawataonja kifo kamwe mpaka kwanza wauone ufalme wa Mungu ukiwa tayari umekuja katika nguvu.”+ 2 Basi siku sita baadaye Yesu akawachukua Petro na Yakobo na Yohana pamoja naye, akawapandisha katika mlima mrefu wakiwa peke yao. Sura yake ikageuka mbele yao,+ 3 na mavazi yake ya nje yakametameta, yakawa meupe kuliko vile msafisha-nguo yeyote duniani anavyoweza kuyafanya.+ 4 Pia, Eliya na Musa wakawatokea, nao walikuwa wakiongea na Yesu.+ 5 Petro akajibu, akamwambia Yesu: “Rabi, ni vizuri kwetu kuwa hapa, kwa hiyo na tusimamishe mahema matatu, moja lako na moja la Musa na moja la Eliya.”+ 6 Kwa kweli, hakujua ajibu nini, kwa maana waliogopa sana. 7 Na wingu likatokea, likawafunika, na sauti+ ikatoka katika lile wingu: “Huyu ni Mwanangu,+ mpendwa; msikilizeni.”+ 8 Hata hivyo, kwa ghafula wakatazama huku na huku nao hawakumwona yeyote pamoja nao tena, ila Yesu peke yake.+
9 Walipokuwa wakishuka kutoka kwenye ule mlima, akawaagiza waziwazi wasimsimulie+ mtu yeyote kile walichoona, mpaka baada ya Mwana wa binadamu kufufuka kutoka kwa wafu.+ 10 Nao wakalitia neno hilo moyoni, lakini wakazungumza katikati yao wenyewe maana ya kufufuliwa huko kutoka kwa wafu. 11 Nao wakaanza kumuuliza, wakisema: “Kwa nini waandishi husema kwamba lazima Eliya+ aje kwanza?”+ 12 Akawaambia: “Eliya anakuja kwanza na kurudisha mambo yote;+ lakini kwa nini imeandikwa juu ya Mwana wa binadamu kwamba lazima apatwe na mateso mengi+ na kutendewa kama asiye wa maana?+ 13 Lakini mimi ninawaambia ninyi, Eliya,+ kwa kweli, amekuja, nao walimtendea mambo mengi kama walivyotaka, kama ilivyoandikwa juu yake.”+
14 Sasa, walipowakaribia wale wanafunzi wengine, wakaona umati mkubwa umewazunguka na waandishi wakibishana nao.+ 15 Lakini mara tu umati wote ulipomwona ukashangaa, ukamkimbilia, na kuanza kumsalimu. 16 Naye akawauliza: “Mnabishania nini nao?” 17 Na mmoja kutoka katika ule umati akamjibu: “Mwalimu, nilileta mwanangu kwako kwa sababu ana roho bubu;+ 18 na popote pale anapomkamata humwangusha chini, naye hutoa povu na kusaga meno yake na kupoteza nguvu zake. Nami niliwaambia wanafunzi wako wamfukuze, lakini hawakuweza.”+ 19 Akajibu akawaambia: “Enyi kizazi kisicho na imani,+ nitaendelea kuwa pamoja nanyi mpaka wakati gani? Nitawavumilia ninyi mpaka wakati gani? Mleteni hapa.”+ 20 Kwa hiyo wakampeleka mahali alipokuwa. Lakini alipomwona tu, mara moja yule roho akamfanya yule mtoto agaegae, na baada ya kuanguka chini akajiviringisha, akitoa povu.+ 21 Naye akamuuliza baba yake: “Amekuwa hivi kwa muda gani?” Akasema: “Tangu utoto na kuendelea; 22 na mara kwa mara alikuwa akimtupa ndani ya moto na ndani ya maji ili kumwangamiza.+ Lakini ikiwa unaweza kufanya jambo lolote, utusikitikie na kutusaidia.” 23 Yesu akamwambia: “Maneno hayo, ‘Ikiwa unaweza’! Mambo yote yanawezekana kwa mtu ikiwa ana imani.”+ 24 Mara moja baba ya yule mtoto mchanga akapaaza sauti, akasema: “Nina imani! Unisaidie mahali ambapo ninahitaji imani!”+
25 Yesu, sasa akiona kwamba umati ulikuwa ukikimbia kuwaelekea, akamkemea+ yule roho mchafu, akamwambia: “Wewe roho bubu na kiziwi, ninakuagiza, toka ndani yake wala usimwingie tena.” 26 Na baada ya kupaaza sauti na kugaagaa sana roho huyo akatoka;+ naye mtoto akawa ni kama amekufa, hivi kwamba wengi kati yao wakawa wakisema: “Amekufa!” 27 Lakini Yesu akamshika mkono na kumwinua, naye akainuka.+ 28 Kwa hiyo baada ya kuingia katika nyumba, wanafunzi wake wakaanza kumuuliza faraghani: “Kwa nini sisi hatukuweza kumfukuza?”+ 29 Naye akawaambia: “Hakuna chochote kinachoweza kumtoa roho wa aina hii isipokuwa sala.”+
30 Kutoka huko wakapitia Galilaya, lakini hakutaka mtu yeyote ajue. 31 Kwa maana alikuwa akifundisha wanafunzi wake na kuwaambia: “Mwana wa binadamu atatiwa mikononi mwa watu, nao watamuua, lakini, ijapokuwa atauawa,+ atafufuka siku tatu baadaye.”+ 32 Hata hivyo, walikuwa hawaelewi maneno hayo, nao waliogopa kumuuliza.+
33 Nao wakaingia Kapernaumu. Sasa alipokuwa ndani ya nyumba akawauliza: “Mlikuwa mkibishania nini barabarani?”+ 34 Wakakaa kimya, kwa maana barabarani walikuwa wamebishana wenyewe, ni nani aliye mkuu zaidi.+ 35 Kwa hiyo akaketi na kuwaita wale kumi na wawili na kuwaambia: “Ikiwa mtu yeyote anataka kuwa wa kwanza, lazima awe wa mwisho kati ya wote na mhudumu wa wote.”+ 36 Naye akamchukua mtoto mchanga, akamsimamisha katikati yao, akamkumbatia na kuwaambia:+ 37 “Yeyote yule anayempokea mmoja wa watoto wachanga kama huyu kwa msingi wa jina langu, ananipokea mimi; na yeyote anayenipokea mimi, anapokea, si mimi tu, bali pia yule aliyenituma.”+
38 Yohana akamwambia: “Mwalimu, tulimwona mtu fulani akitoa roho waovu kwa kutumia jina lako nasi tukajaribu kumzuia,+ kwa sababu hakuwa akifuatana nasi.”+ 39 Lakini Yesu akasema: “Msijaribu kumzuia, kwa maana hakuna yeyote atakayefanya matendo yenye nguvu kwa msingi wa jina langu ambaye ataweza kunitukana upesi-upesi;+ 40 kwa maana mtu ambaye hatupingi yuko upande wetu.+ 41 Kwa maana yeyote anayewapa ninyi kikombe+ cha maji ya kunywa kwa sababu ninyi ni watu wa Kristo,+ kwa kweli ninawaambia ninyi, hatapoteza kamwe thawabu yake. 42 Lakini yeyote anayemkwaza mmoja wa hawa wadogo wanaoamini, ingekuwa afadhali ikiwa jiwe la kusagia kama lile ambalo huzungushwa na punda lingewekwa shingoni pake naye atupwe baharini.+
43 “Na mkono wako ukikufanya ukwazike, ukate; ni afadhali uingie katika uzima ukiwa kilema kuliko kwenda ukiwa na mikono miwili na kuingia katika Gehena,* katika moto usioweza kuzimwa.+ 44 —— 45 Na ikiwa mguu wako unakufanya ukwazike, ukate; ni afadhali uingie katika uzima ukiwa kilema+ kuliko kutupwa katika Gehena* ukiwa na miguu miwili.+ 46 —— 47 Na ikiwa jicho lako linakufanya ukwazike, litupe mbali;+ ni afadhali uingie katika ufalme wa Mungu ukiwa na jicho moja kuliko kutupwa katika Gehena*+ ukiwa na macho mawili, 48 mahali ambapo funza wake hafi na ule moto hauzimwi.+
49 “Kwa maana kila mtu lazima atiwe chumvi+ kwa moto. 50 Chumvi ni nzuri; lakini chumvi ikipoteza nguvu zake, mtaikoleza na nini?+ Iweni na chumvi+ ndani yenu, na mdumishe amani+ kati ya mtu na mwenzake.”
10 Kutoka hapo akaondoka na kuja kwenye mipaka ya Yudea na ng’ambo ya Yordani, na tena umati ukamjia, na kama alivyokuwa na desturi ya kufanya akaanza tena kuwafundisha.+ 2 Mafarisayo sasa wakamkaribia na, ili kumjaribu, wakaanza kumuuliza kama ni halali mwanamume kumtaliki mke wake.+ 3 Akajibu akawaambia: “Musa aliwaamuru ninyi nini?” 4 Wakasema: “Musa aliruhusu kuandika cheti cha kufukuza na kumtaliki.”+ 5 Lakini Yesu akawaambia: “Kwa kufikiria ugumu wenu wa moyo+ aliwaandikia ninyi amri hiyo. 6 Hata hivyo, tangu mwanzo wa kuumba ‘Yeye aliwafanya mwanamume na mwanamke.+ 7 Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake, 8 na hao wawili watakuwa mwili mmoja’;+ hivi kwamba wao si wawili tena, bali mwili mmoja. 9 Kwa hiyo kile ambacho Mungu ameunganisha mtu yeyote asikitenganishe.”+ 10 Alipokuwa tena katika nyumba+ wanafunzi wakaanza kumuuliza kuhusu hilo. 11 Naye akawaambia: “Mtu yeyote anayemtaliki mke wake na kumwoa mwingine anafanya uzinzi+ dhidi yake, 12 na mwanamke, baada ya kumtaliki mume wake, akiolewa na mwingine, anafanya uzinzi.”+
13 Sasa watu wakaanza kumletea watoto wachanga ili awaguse; lakini wanafunzi wakawakemea.+ 14 Alipoona hilo, Yesu akaghadhibika na kuwaambia: “Waacheni watoto wachanga waje kwangu; msijaribu kuwazuia, kwa maana ufalme wa Mungu ni wa wale walio kama hao.+ 15 Kwa kweli ninawaambia ninyi, Yeyote yule asiyeupokea ufalme wa Mungu kama mtoto mchanga hataingia kamwe ndani yake.”+ 16 Naye akachukua watoto akawakumbatia na kuanza kuwabariki, akiweka mikono yake juu yao.+
17 Naye alipokuwa akitoka aende, mtu fulani akamkimbilia akapiga magoti mbele yake na kumuuliza: “Mwalimu Mwema, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?”+ 18 Yesu akamwambia: “Kwa nini unaniita mwema?+ Hakuna mtu aliye mwema, ila mmoja, Mungu.+ 19 Wewe unazijua amri, ‘Usiue,+ Usifanye uzinzi,+ Usiibe,+ Usitoe ushahidi wa uwongo,+ Usipunje,+ Mheshimu baba yako na mama yako.’ ”+ 20 Mtu huyo akamwambia: “Mwalimu, mambo yote hayo nimeyashika tangu ujana wangu na kuendelea.” 21 Yesu akamtazama akampenda na kumwambia: “Umekosa jambo moja: Nenda, ukauze vitu ulivyo navyo uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni, kisha uje uwe mfuasi wangu.”+ 22 Lakini akasikitishwa na neno hilo na kwenda zake akiwa amehuzunika, kwa maana alikuwa na mali nyingi.+
23 Baada ya kutazama huku na huku Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Jinsi itakavyokuwa vigumu kwa wale wenye pesa+ kuingia katika ufalme wa Mungu!”+ 24 Lakini wanafunzi wakashangaa+ kwa sababu ya maneno yake. Yesu akajibu akawaambia tena: “Wanangu, jinsi ilivyo vigumu kuingia katika ufalme wa Mungu! 25 Ni rahisi zaidi ngamia kupita katika tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.”+ 26 Bado wakazidi kustaajabu na kumwambia: “Ni nani ambaye, kwa kweli, anaweza kuokolewa?”+ 27 Akiwatazama moja kwa moja Yesu akasema: “Kwa wanadamu haiwezekani, lakini sivyo ilivyo kwa Mungu, kwa maana mambo yote yanawezekana kwa Mungu.”+ 28 Petro akaanza kumwambia: “Tazama! Sisi tuliacha vitu vyote na tumekuwa tukikufuata wewe.”+ 29 Yesu akasema: “Kwa kweli ninawaambia ninyi, Hakuna mtu ambaye ameacha nyumba au ndugu au dada au mama au baba au watoto au mashamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya habari njema+ 30 ambaye hatapata mara mia+ sasa katika kipindi hiki cha wakati, nyumba na ndugu na dada na mama na watoto na mashamba, pamoja na mateso,+ na katika mfumo wa mambo unaokuja uzima wa milele. 31 Hata hivyo, wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na wa mwisho watakuwa wa kwanza.”+
32 Sasa walikuwa barabarani, wakipanda kwenda Yerusalemu, na Yesu alikuwa akienda mbele yao, nao wakashangaa; lakini wale waliofuata wakaanza kuogopa. Mara nyingine tena akawachukua wale kumi na wawili kando na kuanza kuwaambia mambo haya yatakayompata:+ 33 “Tazama, tunapanda kwenda Yerusalemu, na Mwana wa binadamu atatiwa mikononi mwa wakuu wa makuhani, na waandishi, nao watamhukumia kifo na kumtia mikononi mwa watu wa mataifa,+ 34 nao watamdhihaki, watamtemea mate, watampiga mijeledi na kumuua, lakini siku tatu baadaye atafufuka.”+
35 Na Yakobo na Yohana, wana wawili wa Zebedayo,+ wakamwendea na kumwambia: “Mwalimu, tunataka utufanyie chochote tutakachokuomba.”+ 36 Akawaambia: “Mnataka niwafanyie nini?” 37 Wakamwambia: “Uturuhusu kuketi, mmoja kwenye mkono wako wa kuume na mmoja kwenye mkono wako wa kushoto, katika utukufu wako.”+ 38 Lakini Yesu akawaambia: “Hamjui kile mnachoomba. Je, mnaweza kunywa kikombe ambacho ninakunywa, au kubatizwa kwa ubatizo ninaobatizwa?”+ 39 Wakamwambia: “Tunaweza.” Ndipo Yesu akawaambia: “Kikombe ninachokunywa mtakunywa, na ubatizo ninaobatizwa mtabatizwa.+ 40 Hata hivyo, kuketi kwenye mkono wangu wa kuume au kwenye mkono wangu wa kushoto sina haki kutoa,+ bali wataketi wale ambao wametayarishiwa.”
41 Basi, wale wengine kumi waliposikia jambo hilo, wakaanza kuwaghadhibikia Yakobo na Yohana.+ 42 Lakini Yesu, baada ya kuwaita, akawaambia: “Mnajua kwamba wale ambao huonekana kuwa wanatawala mataifa hupiga ubwana juu yao na wakuu wao hutumia mamlaka juu yao.+ 43 Hivyo sivyo ilivyo katikati yenu; bali yeyote yule anayetaka kuwa mkubwa katikati yenu lazima awe mhudumu wenu,+ 44 na yeyote yule anayetaka kuwa wa kwanza katikati yenu lazima awe mtumwa wa wote.+ 45 Kwa maana hata Mwana wa binadamu alikuja, si kuhudumiwa,+ bali kuhudumu na kutoa nafsi yake iwe fidia+ badala ya wengi.”+
46 Nao wakaingia Yeriko. Lakini yeye na wanafunzi wake na umati mkubwa walipokuwa wakitoka Yeriko, Bartimayo (mwana wa Timayo), kipofu aliye mwombaji, alikuwa ameketi kando ya barabara.+ 47 Aliposikia kwamba ni Yesu Mnazareti, akaanza kupaaza sauti na kusema: “Mwana wa Daudi,+ Yesu, unirehemu!”+ 48 Ndipo wengi wakaanza kumwambia kwa ukali anyamaze; lakini akazidi kupaaza sana sauti: “Mwana wa Daudi, unirehemu!”+ 49 Kwa hiyo Yesu akasimama na kusema: “Mwiteni.” Nao wakamwita yule mtu aliye kipofu, wakamwambia: “Jipe moyo, simama, anakuita.”+ 50 Akatupa vazi lake la nje, akaruka na kusimama kwa miguu yake, akamwendea Yesu. 51 Yesu akamjibu, akasema: “Unataka nikufanyie nini?”+ Yule mtu aliye kipofu akamwambia: “Raboni, acha nipate tena kuona.”+ 52 Na Yesu akamwambia: “Nenda, imani yako imekuponya.”+ Na mara moja akapata tena kuona,+ naye akaanza kumfuata barabarani.+
11 Walipokuwa wakikaribia kufika Yerusalemu, Bethfage na Bethania+ kwenye Mlima wa Mizeituni, akatuma wawili kati ya wanafunzi wake+ 2 na kuwaambia: “Nendeni mkaingie katika kijiji mnachokiona mbele yenu, na mara tu mtakapoingia ndani mtamkuta mwana-punda akiwa amefungwa, ambaye hakuna mwanadamu yeyote amepata kuketi juu yake; mfungueni mkamlete.+ 3 Na mtu yeyote akiwaambia, ‘Kwa nini mnafanya hili?’ semeni, ‘Bwana anamhitaji, na atamrudisha hapa mara moja.’ ”+ 4 Kwa hiyo wakaenda zao na kumkuta mwana-punda akiwa amefungwa kwenye mlango, nje kwenye barabara ya kandokando, nao wakamfungua.+ 5 Lakini baadhi ya wale waliokuwa wamesimama hapo wakaanza kuwaambia: “Kwa nini mnamfungua mwana-punda huyu?”+ 6 Wakawaambia hao kama vile Yesu alivyokuwa amesema; nao wakawaacha waende.+
7 Wakamletea Yesu huyo mwana-punda,+ nao wakaweka mavazi yao ya nje juu yake, naye akaketi juu yake.+ 8 Pia, wengi wakatandaza mavazi+ yao ya nje barabarani, lakini wengine wakakata matawi yenye majani+ kutoka katika mashamba.+ 9 Na wale waliokuwa wakitangulia na wale waliokuwa wakifuata nyuma wakawa wakipaaza sauti: “Mwokoe, tunaomba!+ Aliyebarikiwa ni yule anayekuja katika jina la Yehova!+ 10 Ufalme unaokuja wa baba yetu Daudi+ umebarikiwa! Mwokoe, tunaomba, katika vilele vilivyo juu!” 11 Naye akaingia Yerusalemu, katika hekalu; naye akatazama vitu vyote huku na huku, na, kwa kuwa saa ilikuwa tayari imesonga, akatoka kwenda Bethania pamoja na wale kumi na wawili.+
12 Siku iliyofuata, walipokuwa wamekuja kutoka Bethania, akaona njaa.+ 13 Na kutoka mbali akaona mtini uliokuwa na majani, akaenda kuona kama labda angeweza kupata kitu fulani juu yake. Lakini, alipofika mahali ulipokuwa, hakupata kitu ila majani, kwa maana hayakuwa majira ya tini.+ 14 Kwa hiyo, akajibu akauambia: “Mtu yeyote asile matunda kutoka kwako tena kamwe, milele.”+ Nao wanafunzi wake walikuwa wakisikiliza.
15 Sasa wakafika Yerusalemu. Huko akaingia katika hekalu akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza na kununua katika hekalu, naye akazipindua meza za wale waliokuwa wakibadili pesa na viti vya wale waliokuwa wakiuza njiwa;+ 16 naye hakuwa akimruhusu mtu yeyote apitishe chombo hekaluni, 17 lakini akaendelea kufundisha na kusema: “Je, haikuandikwa, ‘Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala+ kwa ajili ya mataifa yote’?+ Lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang’anyi.”+ 18 Na wakuu wa makuhani na waandishi wakasikia, nao wakaanza kutafuta jinsi ya kumwangamiza;+ kwa maana walikuwa wakimwogopa, kwa maana umati wote sikuzote ulikuwa ukistaajabishwa na mafundisho yake.+
19 Na ilipofika jioni, walikuwa wakitoka jijini. 20 Lakini walipokuwa wakipita hapo asubuhi na mapema, wakaona ule mtini tayari umekauka kuanzia kwenye mizizi.+ 21 Kwa hiyo Petro, akakumbuka, akamwambia: “Rabi, ona! ule mtini ulioulaani umekauka.”+ 22 Yesu akajibu, akawaambia: “Iweni na imani katika Mungu. 23 Kwa kweli ninawaambia ninyi kwamba mtu yeyote anayeuambia mlima huu, ‘Ng’oka ukatupwe baharini,’ naye hana shaka moyoni mwake lakini ana imani kwamba yale anayosema yatatukia, itakuwa hivyo kwake.+ 24 Ndiyo sababu ninawaambia ninyi, Mambo yote mnayosali na kuomba juu yake iweni na imani kwamba ni kana kwamba tayari mmeyapokea, nanyi mtayapata.+ 25 Na mnaposimama mkisali, wasameheni+ watu chochote mlicho nacho dhidi yao; ili Baba yenu aliye mbinguni awasamehe makosa yenu ninyi pia.”+ 26 ——
27 Nao wakaja tena Yerusalemu. Na alipokuwa akitembea katika hekalu, wakuu wa makuhani na waandishi na wanaume wazee wakamjia+ 28 na kuanza kumwambia: “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? au ni nani aliyekupa mamlaka ya kufanya mambo haya?”+ 29 Yesu akawaambia: “Nitawauliza ninyi swali moja. Nijibuni, nami pia nitawaambia ninyi ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani.+ 30 Je, ubatizo+ wa Yohana ulitoka mbinguni au kwa wanadamu? Nijibuni.”+ 31 Kwa hiyo wakaanza kujadiliana kati yao wenyewe, wakisema: “Tukisema, ‘Ulitoka mbinguni,’ atasema, ‘Basi, kwa nini hamkumwamini?’+ 32 Lakini je, tutathubutu kusema, ‘Ulitoka kwa wanadamu’?”—Walikuwa wakiuogopa umati, kwa maana umati wote huo ulimwona Yohana kwamba kwa kweli alikuwa nabii.+ 33 Basi, wakamjibu Yesu wakasema: “Hatujui.” Naye Yesu akawaambia: “Wala mimi siwaambii ninyi ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani.”+
12 Pia, akaanza kusema nao kwa kutumia mifano: “Mtu alipanda shamba la mizabibu,+ akaweka ua kulizunguka, akachimba shimo la mtungi wa shinikizo la divai, akasimamisha mnara,+ akalikodisha kwa wakulima,+ kisha akasafiri kwenda ng’ambo.+ 2 Majira yake yalipofika akatuma mtumwa kwa wakulima, ili apate sehemu ya matunda ya shamba la mizabibu kutoka kwa wakulima.+ 3 Lakini wakamchukua, wakampiga na kumfukuza mikono mitupu.+ 4 Na tena akamtuma mtumwa mwingine kwao; na huyo wakampiga kichwani na kumvunjia heshima.+ 5 Naye akamtuma mwingine, na huyo wakamuua; na wengine wengi, baadhi yao waliwapiga na baadhi yao waliwaua. 6 Alikuwa na mmoja zaidi, mwana mpendwa.+ Akamtuma mwisho kwao, akisema, ‘Watamheshimu mwanangu.’+ 7 Lakini wakulima hao wakasemezana, ‘Huyu ndiye mrithi.+ Njooni, acheni tumuue, na urithi utakuwa wetu.’+ 8 Kwa hiyo wakamchukua wakamuua,+ na kumtupa nje ya shamba la mizabibu.+ 9 Mwenye shamba la mizabibu atafanya nini? Atakuja na kuwaangamiza wakulima, na kuwapa wengine+ shamba la mizabibu.+ 10 Je, hamkusoma kamwe andiko hili, ‘Jiwe+ ambalo wajenzi walilikataa, limekuwa jiwe kuu la pembeni.+ 11 Limetokana na Yehova, nalo ni la kustaajabisha machoni petu’?”+
12 Ndipo wakaanza kutafuta jinsi ya kumkamata, lakini waliuogopa umati, kwa maana walijua kwamba alitoa mfano huo juu yao. Kwa hiyo wakamwacha, wakaenda zao.+
13 Halafu wakamtumia baadhi ya Mafarisayo na wafuasi wa chama cha Herode,+ kumnasa kwa maneno yake.+ 14 Walipofika wakamwambia: “Mwalimu, tunajua wewe una ukweli nawe hujali mtu yeyote, kwa maana hutazami sura za watu, bali unafundisha njia ya Mungu kupatana na ile kweli:+ Je, ni halali kumlipa Kaisari kodi ya kichwa au hapana? 15 Je, tulipe, au tusilipe?”+ Akagundua unafiki wao, akawaambia: “Kwa nini mnanijaribu? Nileteeni dinari niitazame.”+ 16 Wakaleta moja. Naye akawaambia: “Sanamu hii na mwandiko huu ni za nani?” Wakamwambia: “Ni za Kaisari.”+ 17 Ndipo Yesu akasema: “Mlipeni Kaisari vitu vya Kaisari,+ lakini Mungu vitu vya Mungu.”+ Nao wakaanza kumstaajabia.+
18 Sasa Masadukayo wakamjia, wale ambao husema hakuna ufufuo, nao wakamuuliza:+ 19 “Mwalimu, Musa alituandikia kwamba ndugu ya mtu akifa na aache mke lakini hakuacha mtoto, ndugu yake+ anapaswa kumchukua mke huyo na kumwinulia ndugu yake uzao kutoka kwa mwanamke huyo.+ 20 Kulikuwa na ndugu saba; na wa kwanza akamchukua mke, lakini alipokufa hakuacha uzao wowote.+ 21 Na yule wa pili akamchukua, lakini akafa bila kuacha uzao; na yule wa tatu vilevile. 22 Na wale saba hawakuacha uzao wowote. Mwishowe yule mwanamke akafa pia.+ 23 Katika ufufuo atakuwa mke wa nani kati yao? Kwa sababu alikuwa mke wa wale saba.”+ 24 Yesu akawaambia: “Je, hiyo siyo sababu ninyi mmekosea, kutojua kwenu Maandiko wala nguvu za Mungu?+ 25 Kwa maana wanapofufuliwa kutoka kwa wafu, wanaume hawaoi wala wanawake hawaolewi, bali wao ni kama malaika wa mbinguni.+ 26 Lakini kuhusu wafu, kwamba wanafufuliwa, je, hamkusoma katika kitabu cha Musa, katika masimulizi juu ya ule mti wa miiba, jinsi Mungu alivyomwambia, ‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu na Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo’?+ 27 Yeye ni Mungu, si wa wafu, bali wa walio hai. Mmekosea sana.”+
28 Sasa mmoja kati ya waandishi aliyekuwa amekuja na kuwasikia wakibishana, akijua kwamba alikuwa amewajibu vizuri, akamuuliza: “Ni amri gani iliyo ya kwanza kati ya zote?”+ 29 Yesu akajibu: “Ya kwanza ni hii, ‘Sikia, Ee Israeli, Yehova Mungu wetu ni Yehova mmoja,+ 30 nawe lazima umpende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote na kwa nguvu zako zote.’+ 31 Ya pili ni hii, ‘Mpende jirani yako kama wewe mwenyewe.’+ Hakuna amri nyingine yoyote iliyo kubwa zaidi kuliko hizi.” 32 Yule mwandishi akamwambia: “Mwalimu, umesema vema kupatana na kweli, ‘Yeye ni Mmoja, na hakuna mwingine ila Yeye’;+ 33 na jambo hili la mtu kumpenda yeye kwa moyo wote na kwa uelewaji wote na kwa nguvu zote na mtu kumpenda jirani kama yeye mwenyewe ni bora zaidi kuliko matoleo yote mazima ya kuteketezwa na dhabihu zote.”+ 34 Ndipo Yesu, akitambua kwamba alikuwa amejibu kwa kutumia akili, akamwambia: “Wewe huko mbali na ufalme wa Mungu.” Lakini hakuna mtu aliyekuwa tena na moyo wa kumuuliza swali.+
35 Hata hivyo, alipokuwa akijibu, Yesu akaanza kusema akifundisha katika hekalu: “Kwa nini waandishi husema kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?+ 36 Kwa roho takatifu+ Daudi mwenyewe alisema, ‘Yehova alimwambia Bwana wangu: “Keti kwenye mkono wangu wa kuume mpaka niwaweke adui zako chini ya miguu yako.” ’+ 37 Daudi mwenyewe anamwita ‘Bwana,’ lakini inawezekanaje kwamba yeye ni mwana wake?”+
Na umati mkubwa ulikuwa ukimsikiliza kwa furaha.+ 38 Na katika mafundisho yake akaendelea kusema: “Jihadharini na waandishi+ ambao hupenda kutembea wakiwa wamevaa kanzu na hupenda salamu katika masoko 39 na viti vya mbele katika masinagogi na mahali penye kuonekana zaidi kwenye milo ya jioni.+ 40 Wao ndio wanaomeza nyumba+ za wajane na kutoa sala ndefu kwa kisingizio; hawa watapokea hukumu nzito zaidi.”+
41 Naye akaketi akitazama masanduku ya hazina+ na kuanza kuangalia jinsi umati ulivyokuwa ukitumbukiza pesa ndani ya masanduku hayo; na matajiri wengi walikuwa wakitumbukiza ndani sarafu nyingi.+ 42 Sasa mjane fulani maskini akaja, akatumbukiza ndani sarafu mbili ndogo, zenye thamani ndogo sana.+ 43 Kwa hiyo akawaita wanafunzi wake na kuwaambia: “Kwa kweli ninawaambia kwamba mjane huyu maskini ametumbukiza nyingi kuliko wote waliokuwa wakitumbukiza pesa ndani ya masanduku ya hazina;+ 44 kwa sababu wote walitumbukiza ndani kutokana na ziada yao, lakini yeye, kutokana na uhitaji wake, alitumbukiza ndani vyote alivyokuwa navyo, riziki yake yote.”+
13 Alipokuwa akitoka hekaluni mmoja wa wanafunzi wake akamwambia: “Mwalimu, ona! jinsi yalivyo mawe haya na majengo haya!”+ 2 Hata hivyo, Yesu akamwambia: “Unayaona majengo haya makubwa?+ Hakuna jiwe litakaloachwa hapa juu ya jiwe+ nalo lisiangushwe chini.”+
3 Na alipokuwa ameketi juu ya Mlima wa Mizeituni, hekalu likiwa linaonekana, Petro+ na Yakobo na Yohana na Andrea wakaanza kumuuliza faraghani:+ 4 “Tuambie, mambo haya yatakuwa wakati gani, na ni nini itakayokuwa ishara ya wakati ambapo mambo yote haya yanakusudiwa kufikia mwisho?”+ 5 Kwa hiyo Yesu akaanza kuwaambia: “Jihadharini mtu yeyote asiwapotoshe.+ 6 Wengi watakuja kwa msingi wa jina langu, wakisema, ‘Mimi ndiye,’ nao watawapotosha wengi.+ 7 Zaidi ya hayo, mnaposikia juu ya vita na habari za vita, msiogope; mambo hayo lazima yatukie, lakini ule mwisho bado.+
8 “Kwa maana taifa litasimama kupigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme,+ kutakuwa na matetemeko ya nchi+ mahali pamoja baada ya pengine, kutakuwa na upungufu wa chakula.+ Hayo ni mwanzo wa maumivu ya taabu.+
9 “Kwa habari yenu, jihadharini; watu watawapeleka mahakamani,+ nanyi mtapigwa katika masinagogi+ na kusimamishwa mbele ya magavana na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushahidi kwao.+ 10 Pia, katika mataifa yote lazima habari njema+ ihubiriwe kwanza.+ 11 Lakini wanapowapeleka, msihangaike kimbele juu ya jambo mtakalosema;+ bali jambo lolote mtakalopewa saa hiyo, semeni hilo, kwa maana si ninyi mnaosema, bali ni roho takatifu.+ 12 Zaidi ya hayo, ndugu atamtoa ndugu yake auawe, na baba atamtoa mtoto,+ na watoto watainuka juu ya wazazi na kufanya wauawe;+ 13 nanyi mtachukiwa na watu wote kwa sababu ya jina langu.+ Lakini yule ambaye atavumilia mpaka mwisho+ ndiye atakayeokolewa.+
14 “Hata hivyo, mtakapoona lile chukizo+ linalosababisha ukiwa likiwa+ limesimama mahali ambapo halipaswi (msomaji na atumie utambuzi),+ ndipo wale walio katika Yudea waanze kukimbilia milimani.+ 15 Mtu aliye juu ya paa ya nyumba asishuke, wala asiingie ndani kuchukua kitu chochote kutoka nyumbani mwake;+ 16 na mtu aliye shambani asirudi kwenye vitu vilivyo nyuma kuchukua vazi lake la nje.+ 17 Ole wao wanawake wenye mimba na wale wanaonyonyesha mtoto mchanga katika siku hizo!+ 18 Endeleeni kusali kwamba yasitukie wakati wa majira ya baridi kali;+ 19 kwa maana siku hizo zitakuwa siku za dhiki+ ya namna ambayo haijatukia tangu mwanzo wa uumbaji ambao Mungu aliumba mpaka wakati huo, na haitatukia tena.+ 20 Kwa kweli, kama Yehova+ hangezifupisha siku hizo, hakuna chochote chenye mwili ambacho kingeokolewa. Lakini amezifupisha siku hizo+ kwa sababu ya waliochaguliwa+ ambao amewachagua.+
21 “Ndipo, pia, mtu yeyote akiwaambia, ‘Tazameni! Kristo huyu hapa,’ ‘Tazameni! ndiye yule pale,’+ msiamini.+ 22 Kwa maana Makristo wa uwongo na manabii wa uwongo watatokea+ na kutoa ishara na maajabu+ ili kupotosha, ikiwezekana, wale waliochaguliwa.+ 23 Basi, jihadharini;+ nimewaambia mambo yote kimbele.+
24 “Lakini katika siku hizo, baada ya dhiki hiyo, jua litatiwa giza, na mwezi hautatoa nuru yake, 25 nazo nyota zitakuwa zikianguka kutoka mbinguni na nguvu zilizo mbinguni zitatikiswa.+ 26 Ndipo watakapomwona Mwana wa binadamu+ akija katika mawingu akiwa na nguvu nyingi na utukufu.+ 27 Ndipo atakapowatuma malaika na kuwakusanya pamoja watu wake waliochaguliwa+ kutoka zile pepo nne, kutoka mwisho wa dunia mpaka mwisho wa mbingu.+
28 “Basi kutokana na mtini jifunzeni mfano huu: Mara tu tawi lake changa linapokuwa jororo na kutoa majani yake, mnajua kwamba kiangazi kiko karibu.+ 29 Vivyo hivyo ninyi pia, mnapoona mambo hayo yakitukia, jueni kwamba yuko karibu, milangoni.+ 30 Kwa kweli ninawaambia ninyi kwamba kizazi hiki hakitapitilia mbali kamwe mpaka mambo yote hayo yatukie.+ 31 Mbingu+ na dunia zitapitilia mbali, lakini maneno+ yangu hayatapitilia mbali.+
32 “Kuhusu siku ile au saa ile hakuna mtu anayejua, wala malaika mbinguni wala Mwana, ila Baba.+ 33 Endeleeni kutazama, Endeleeni kukesha,+ kwa maana hamjui wakati uliowekwa ni gani.+ 34 Ni kama mtu anayesafiri kwenda ng’ambo,+ ambaye aliacha nyumba yake na kuwapa mamlaka watumwa wake, kila mmoja kazi yake, na kumwamuru mtunza-mlango aendelee kukesha. 35 Kwa hiyo endeleeni kukesha,+ kwa maana hamjui bwana wa nyumba anakuja wakati gani, kama ni wakati wa jioni au katikati ya usiku au anapowika jogoo au asubuhi na mapema;+ 36 ili anapofika kwa ghafula, asiwakute mkiwa mmelala usingizi.+ 37 Lakini lile ninalowaambia ninyi ninawaambia wote, Endeleeni kukesha.”+
14 Siku mbili kabla ya pasaka+ na sherehe+ ya keki zisizo na chachu,+ wakuu wa makuhani na waandishi walikuwa wakitafuta jinsi ya kumkamata kwa hila na kumuua;+ 2 kwa maana walisema tena na tena: “Si kwenye sherehe; huenda kukawa na ghasia ya watu.”+
3 Na alipokuwa Bethania katika nyumba ya Simoni mwenye ukoma,+ akiwa ameketi kwenye mlo, mwanamke akaja na chupa ya alabasta iliyo na mafuta yenye marashi, nardo halisi, ghali sana. Akaivunja ili kuifungua na kuanza kuyamimina juu ya kichwa chake.+ 4 Ndipo wengine wakakasirika na kusema katikati yao wenyewe: “Kwa nini hasara hii ya mafuta yenye marashi?+ 5 Kwa maana mafuta hayo yangaliweza kuuzwa kwa dinari zaidi ya mia tatu na kupewa maskini!” Nao walikuwa wamechukizwa sana na mwanamke huyo.+ 6 Lakini Yesu akasema: “Mwacheni. Kwa nini mnataka kumsumbua? Amenifanyia tendo zuri.+ 7 Kwa maana mna maskini+ pamoja nanyi sikuzote, na wakati wowote ule mnapotaka mnaweza kuwafanyia mema sikuzote, lakini mimi hamtakuwa pamoja nami sikuzote.+ 8 Alifanya jambo ambalo aliweza; ameutia mwili wangu mafuta yenye marashi ili kunitayarisha kimbele kwa ajili ya maziko yangu.+ 9 Kwa kweli ninawaambia ninyi, Kokote ambako habari njema itahubiriwa katika ulimwengu wote,+ jambo ambalo mwanamke huyu amefanya litasimuliwa pia kuwa kumbukumbu lake.”+
10 Na Yuda Iskariote, mmoja wa wale kumi na wawili, akaenda zake kwa wakuu wa makuhani ili amsaliti kwao.+ 11 Waliposikia hilo, wakashangilia na kuahidi kumpa fedha.+ Kwa hiyo akaanza kutafuta jinsi ya kumsaliti kwa wakati unaofaa.+
12 Sasa siku ya kwanza ya keki zisizo na chachu,+ wakati ambapo kidesturi walichinja mnyama wa pasaka, wanafunzi+ wake wakamwambia: “Unataka twende wapi tukakutayarishie ule pasaka?”+ 13 Ndipo akawatuma wawili kati ya wanafunzi wake na kuwaambia: “Nendeni jijini, nanyi mtakutana na mwanamume anayebeba chombo cha udongo cha maji.+ Mfuateni, 14 na popote atakapoingia mwambieni mwenye nyumba, ‘Mwalimu anasema: “Kiko wapi chumba cha wageni kwa ajili yangu ambamo ninaweza kula pasaka+ pamoja na wanafunzi wangu?” ’+ 15 Naye atawaonyesha chumba kikubwa cha juu, chenye vifaa kikiwa tayari; na humo tayarisheni kwa ajili yetu.”+ 16 Kwa hiyo wanafunzi wakaenda, nao wakaingia katika jiji na kukipata kama vile alivyowaambia; nao wakafanya matayarisho ya pasaka.+
17 Baada ya kuwa jioni akaja pamoja na wale kumi na wawili.+ 18 Na walipokuwa wameketi mezani wakila, Yesu akasema: “Kwa kweli ninawaambia ninyi, Mmoja wenu, anayekula+ pamoja nami, atanisaliti.”+ 19 Wakaanza kuhuzunika na kumwambia mmoja-mmoja; “Je, ni mimi?”+ 20 Akawaambia: “Ni mmoja wa wale kumi na wawili, anayechovya pamoja nami katika bakuli moja.+ 21 Kwa kweli, Mwana wa binadamu anaenda zake, kama ilivyoandikwa kumhusu, lakini ole wake mtu yule ambaye kupitia kwake Mwana wa binadamu atasalitiwa! Ingalikuwa afadhali kama mtu huyo asingalizaliwa.”+
22 Na walipokuwa wakiendelea kula, akachukua mkate, akatoa baraka, akaumega, akawapa, na kusema: “Chukueni, huu unamaanisha mwili wangu.”+ 23 Naye akichukua kikombe, akashukuru akawapa, nao wote wakakinywea.+ 24 Naye akawaambia: “Hii inamaanisha ‘damu+ yangu ya agano,’+ ambayo itamwagwa+ kwa ajili ya wengi.+ 25 Kwa kweli ninawaambia ninyi, Sitakunywa tena kamwe divai ya mzabibu mpaka siku ile nitakapokunywa ikiwa mpya katika ufalme wa Mungu.”+ 26 Mwishowe, baada ya kuimba sifa,+ wakatoka na kwenda kwenye Mlima wa Mizeituni.+
27 Na Yesu akawaambia: “Ninyi nyote mtakwazika, kwa sababu imeandikwa, ‘Nitampiga mchungaji,+ nao kondoo watatawanyika huku na huku.’+ 28 Lakini baada ya kufufuliwa nitawatangulia kuingia Galilaya.”+ 29 Lakini Petro akamwambia: “Hata ikiwa wengine wote watakwazika, hata hivyo mimi sitakwazika.”+ 30 Ndipo Yesu akamwambia: “Kwa kweli ninakuambia, Wewe leo, ndiyo, usiku huu, kabla ya jogoo kuwika mara mbili, utanikana mara tatu.”+ 31 Lakini akaanza kusema maneno kwa kusisitiza: “Nikilazimika kufa pamoja nawe, sitakukana kamwe.” Pia, wengine wote wakaanza kusema vivyo hivyo.+
32 Kwa hiyo wakafika mahali panapoitwa jina Gethsemane, naye akawaambia wanafunzi wake: “Ketini hapa ninaposali.”+ 33 Akamchukua Petro na Yakobo na Yohana+ pamoja naye, naye akaanza kufadhaika na kutaabika sana.+ 34 Kisha akawaambia: “Nafsi yangu ina huzuni sana,+ kiasi cha kufa. Kaeni hapa na mwendelee kukesha.”+ 35 Naye akasonga mbele kidogo, akaanguka chini na kuanza kusali kwamba, kama ingewezekana, saa hiyo ipite mbali kutoka kwake.+ 36 Naye akaendelea kusema: “Abba, Baba,+ mambo yote yanawezekana kwako; niondolee kikombe hiki. Lakini si lile ninalotaka, bali lile unalotaka.”+ 37 Naye akaja akawakuta wamelala usingizi, naye akamwambia Petro: “Simoni, unalala usingizi? Hukuwa na nguvu za kuendelea kukesha kwa saa moja?+ 38 Endeleeni kukesha na kusali,+ ili msiingie katika jaribu. Bila shaka, roho inataka, lakini mwili ni dhaifu.”+ 39 Naye akaenda zake tena, akasali, akisema neno hilohilo.+ 40 Akaja tena na kuwakuta wamelala usingizi, kwa maana macho yao yalikuwa yamelemewa, na kwa hiyo hawakujua wamjibu nini.+ 41 Naye akaja mara ya tatu na kuwaambia: “Wakati kama huu ninyi mnalala usingizi na kupumzika! Inatosha! Saa imekuja!+ Tazama! Mwana wa binadamu anasalitiwa na kutiwa katika mikono ya watenda-dhambi.+ 42 Simameni, twende.+ Tazama! Msaliti wangu amekaribia.”+
43 Na mara moja, alipokuwa bado akisema, Yuda, mmoja wa wale kumi na wawili, akafika pamoja na umati ukiwa na mapanga na marungu kutoka kwa wakuu wa makuhani na waandishi na wanaume wazee.+ 44 Basi msaliti wake alikuwa amewapa ishara waliyokubaliana, akisema: “Yeyote yule nitakayembusu, huyo ndiye; mkamateni na kumchukua.”+ 45 Naye akaja moja kwa moja akamkaribia na kusema: “Rabi!” na kumbusu+ kwa wororo sana. 46 Kwa hiyo wakaweka mikono juu yake wakamkamata.+ 47 Hata hivyo, mtu fulani kati ya hao waliosimama kando akauchomoa upanga wake, akampiga mtumwa wa kuhani mkuu, akalikata sikio lake.+ 48 Lakini Yesu akawaambia: “Je, mlitoka mkiwa na mapanga na marungu kana kwamba ni kwenda juu ya mnyang’anyi ili kunikamata?+ 49 Nilikuwa pamoja nanyi katika hekalu siku baada ya siku nikifundisha,+ na bado hamkunikamata. Hata hivyo, ni ili Maandiko+ yapate kutimizwa.”+
50 Nao wote wakamwacha+ na kukimbia.+ 51 Lakini kijana fulani aliyekuwa amevaa vazi la kitani bora juu ya mwili wake ulio uchi akaanza kumfuata karibu-karibu; nao wakajaribu kumkamata,+ 52 lakini yeye akaliacha vazi lake la kitani, akakimbia akiwa uchi.
53 Sasa wakampeleka Yesu kwa kuhani mkuu, na wakuu wote wa makuhani na wanaume wazee na waandishi wakakusanyika.+ 54 Lakini Petro, akiwa mbali kiasi, akamfuata+ mpaka katika ua wa kuhani mkuu; naye alikuwa ameketi pamoja na watumishi wa nyumba akiota moto, mbele ya moto mwangavu. 55 Wakati huohuo wakuu wa makuhani na Sanhedrini yote walikuwa wakitafuta ushuhuda juu ya Yesu ili auawe,+ lakini hawakuwa wakipata wowote.+ 56 Kwa kweli, wengi walikuwa wakitoa ushahidi wa uwongo juu yake,+ lakini ushuhuda wao haukupatana.+ 57 Pia, watu fulani walikuwa wakisimama na kutoa ushahidi wa uwongo juu yake, wakisema: 58 “Sisi tulimsikia akisema, ‘Nitaliangusha hekalu hili lililotengenezwa kwa mikono na katika siku tatu nitajenga lingine lisilotengenezwa kwa mikono.’ ”+ 59 Lakini hata kwa misingi hiyo ushuhuda wao haukupatana.
60 Mwishowe kuhani mkuu akasimama katikati yao na kumuuliza Yesu, akisema: “Je, hujibu lolote? Watu hawa wanashuhudia nini juu yako?”+ 61 Lakini akaendelea kukaa kimya na hakutoa jibu hata kidogo.+ Tena kuhani mkuu akaanza kumuuliza na kumwambia: “Wewe ndiye Kristo Mwana wa yule Mbarikiwa?”+ 62 Ndipo Yesu akasema: “Mimi ndiye; nanyi mtamwona Mwana wa binadamu+ akiwa ameketi kwenye mkono wa kuume+ wa nguvu akija pamoja na mawingu ya mbinguni.”+ 63 Ndipo kuhani mkuu akayararua mavazi yake ya ndani+ na kusema: “Tunahitaji mashahidi wengine wa nini?+ 64 Mmelisikia kufuru.+ Ni jambo gani lililo wazi kwenu?” Wao wote wakamhukumu kwamba anastahili kufa. 65 Na wengine wakaanza kumtemea mate+ na kuufunika uso wake wote na kumpiga ngumi na kumwambia: “Toa unabii!” Na, wakimpiga makofi usoni, watumishi wa mahakama wakamchukua.+
66 Sasa Petro alipokuwa chini katika ua, mmoja wa vijakazi wa kuhani mkuu akaja,+ 67 na, alipomwona Petro akiota moto, akamtazama moja kwa moja na kusema: “Wewe, pia, ulikuwa pamoja na yule Mnazareti, Yesu huyu.”+ 68 Lakini akakana, akisema: “Simjui wala sielewi unalosema,” naye akaenda nje kwenye sebule.+ 69 Huko yule kijakazi, alipomwona, akaanza tena kuwaambia wale waliosimama kando: “Huyu ni mmoja wao.”+ 70 Tena akawa akikana hilo. Na mara nyingine tena baada ya muda kidogo wale waliosimama kando wakaanza kumwambia Petro: “Hakika wewe ni mmoja wao, kwa maana, kwa kweli, wewe ni Mgalilaya.”+ 71 Lakini yeye akaanza kulaani na kuapa:+ “Simjui mtu huyu ambaye mnasema juu yake.”+ 72 Na mara jogoo akawika mara ya pili;+ na Petro akakumbuka maneno ambayo Yesu alimwambia: “Kabla ya jogoo kuwika mara mbili, utanikana mara tatu.”+ Naye akaanza kulia.+
15 Na mara tu kulipopambazuka wakuu wa makuhani pamoja na wanaume wazee na waandishi, hata Sanhedrini yote, wakashauriana,+ nao wakamfunga Yesu, wakampeleka na kumtia mikononi mwa Pilato.+ 2 Kwa hiyo Pilato akamuuliza: “Je, wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?”+ Akamjibu, akasema: “Wewe mwenyewe unasema.”+ 3 Lakini wakuu wa makuhani wakaendelea kumshtaki mambo mengi.+ 4 Sasa Pilato akaanza kumuuliza tena, akisema: “Je, huna jibu la kutoa?+ Ona ni mashtaka mangapi wanaleta juu yako.”+ 5 Lakini Yesu hakujibu tena, hivi kwamba Pilato akaanza kustaajabu.+
6 Basi, kutoka sherehe mpaka sherehe alikuwa na kawaida ya kuwafungulia mfungwa mmoja, ambaye waliomba.+ 7 Wakati huo yule aliyeitwa Baraba alikuwa amefungwa pamoja na wachochezi, ambao katika uchochezi wao walikuwa wameua.+ 8 Kwa hiyo umati ukaja na kuanza kuomba kulingana na jambo alilokuwa na kawaida ya kuwafanyia. 9 Pilato akawajibu, akisema: “Mnataka niwafungulie mfalme wa Wayahudi?”+ 10 Kwa maana alijua kwamba wakuu wa makuhani walikuwa wamemtia mikononi mwake+ kwa sababu ya wivu.+ 11 Lakini wakuu wa makuhani wakauchochea umati ili umfanye awafungulie Baraba, badala yake.+ 12 Pilato akajibu tena, akawaambia: “Basi, nitafanya nini na huyu mnayemwita mfalme+ wa Wayahudi?”+ 13 Mara nyingine tena wakapaaza sauti: “Mtundike mtini!”+ 14 Lakini Pilato akaendelea kuwaambia: “Kwani, alifanya jambo gani baya?” Bado wao wakapaaza sauti hata zaidi: “Mtundike mtini!”+ 15 Ndipo Pilato, akitaka kuuridhisha umati,+ akawafungulia Baraba, na, baada ya kuagiza Yesu apigwe mijeledi, akamtoa ili atundikwe mtini.+
16 Sasa askari-jeshi wakampeleka uani, yaani, katika jumba la gavana; nao wakaita kikosi chote cha askari pamoja,+ 17 nao wakampamba kwa vazi la zambarau na kusokota taji la miiba, wakaliweka juu yake.+ 18 Nao wakaanza kumsalimu: “Siku njema,+ ewe Mfalme wa Wayahudi!” 19 Pia, wakawa wakimpiga kichwani kwa utete na kumtemea mate na kumsujudia wakiwa wamepiga magoti.+ 20 Mwishowe, walipokuwa wamemdhihaki, wakamvua lile vazi la zambarau na kumvika mavazi yake ya nje. Nao wakamtoa ili wakamtundike mtini.+ 21 Pia, wakamlazimisha mpita-njia afanye utumishi, mtu fulani anayeitwa Simoni, wa Kirene, aliyekuwa akija kutoka mashambani, baba ya Aleksanda na Rufo, kwamba aubebe mti wake wa mateso.+
22 Kwa hiyo wakampeleka mahali panapoitwa Golgotha, neno ambalo linapotafsiriwa humaanisha, Mahali pa Fuvu la Kichwa.+ 23 Hapa wakajaribu kumpa divai iliyotiwa kileo cha manemane,+ lakini hakuinywa.+ 24 Nao wakamtundika mtini na kugawa mavazi yake ya nje+ kwa kupiga kura juu yake kuhusu nani achukue nini.+ 25 Sasa ilikuwa saa tatu,+ nao wakamtundika mtini. 26 Na maandishi ya shtaka+ juu yake yakaandikwa, “Mfalme wa Wayahudi.”+ 27 Zaidi ya hayo, wakawatundika mtini wanyang’anyi wawili pamoja naye, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wake wa kushoto.+ 28 —— 29 Na wale waliokuwa wakipitia hapo walikuwa wakimtukana,+ wakitikisa vichwa vyao na kusema: “Po! Wewe uliyetaka kuliangusha hekalu na kulijenga kwa siku tatu,+ 30 jiokoe mwenyewe kwa kushuka kutoka kwenye mti wa mateso.”+ 31 Vivyo hivyo pia wakuu wa makuhani walikuwa wakimdhihaki katikati yao wenyewe pamoja na waandishi na kusema: “Aliwaokoa wengine; hawezi kujiokoa mwenyewe!+ 32 Acheni Kristo Mfalme wa Israeli ashuke sasa kutoka kwenye mti wa mateso, ili tupate kuona na kuamini.”+ Hata wale waliotundikwa mtini pamoja naye walikuwa wakimshutumu.+
33 Ilipofika saa sita kukawa na giza juu ya nchi yote mpaka saa tisa.+ 34 Na saa tisa Yesu akapaaza kilio kwa sauti kubwa: “Eli, Eli, lama sabakthani?” maneno ambayo yanapotafsiriwa humaanisha: “Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?”+ 35 Na baadhi ya wale waliokuwa wamesimama karibu, waliposikia, wakaanza kusema: “Tazama! Anamwita Eliya.”+ 36 Lakini mtu fulani akakimbia, akalowesha sifongo katika divai kali, akaiweka juu ya utete, na kuanza kumnywesha,+ akisema: “Acheni iwe hivyo kwake! Acheni tuone kama Eliya atakuja kumshusha.”+ 37 Lakini Yesu akatoa kilio kikubwa, akakata pumzi.+ 38 Na pazia+ la patakatifu likapasuka vipande viwili kutoka juu mpaka chini.+ 39 Sasa yule ofisa-jeshi aliyekuwa amesimama kando yake akimtazama, alipoona kwamba amekufa katika hali hizo, akasema: “Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu.”+
40 Kulikuwa pia na wanawake wakitazama wakiwa mbali,+ kati yao Maria Magdalene na vilevile Maria mama ya Yakobo Mdogo na Yose, na Salome,+ 41 waliokuwa na kawaida ya kufuatana naye+ na kumhudumia alipokuwa Galilaya, na wanawake wengine wengi waliokuwa wamekuja na kupanda pamoja naye mpaka Yerusalemu.+
42 Sasa kwa kuwa ilikuwa jioni, na kwa kuwa yalikuwa ni Matayarisho, yaani, siku inayotangulia sabato, 43 Yosefu wa Arimathea, mshiriki wa Baraza mwenye kusifika, ambaye pia alikuwa akiungojea ufalme wa Mungu, akaja.+ Akajipa moyo kuingia mbele ya Pilato na kuomba apewe mwili+ wa Yesu. 44 Lakini Pilato akataka kujua kama tayari alikuwa amekufa, akamwita yule ofisa-jeshi, akamuuliza kama tayari alikuwa amekufa. 45 Kwa hiyo baada ya kuhakikisha kutoka kwa huyo ofisa-jeshi, akampa Yosefu maiti hiyo.+ 46 Basi akanunua kitani bora na kumshusha, akamfunga katika kile kitani bora na kumlaza+ katika kaburi+ lililokuwa limechimbwa katika mwamba; naye akaviringisha jiwe hata kwenye mlango wa lile kaburi.+ 47 Lakini Maria Magdalene na Maria mama ya Yose wakaendelea kutazama mahali alipokuwa amelazwa.+
16 Kwa hiyo siku ya sabato+ ilipokuwa imepita, Maria Magdalene,+ na Maria mama ya Yakobo, na Salome wakanunua manukato kusudi waje kumpaka.+ 2 Na mapema sana siku ya kwanza+ ya juma wakaja kwenye kaburi, jua lilipokuwa limechomoza.+ 3 Nao walikuwa wakisemezana: “Ni nani atakayetuviringishia lile jiwe kutoka kwenye mlango wa kaburi?” 4 Lakini walipotazama juu, wakaona kwamba jiwe lilikuwa limeviringishwa, ijapokuwa lilikuwa kubwa sana.+ 5 Walipoingia ndani ya kaburi, wakaona kijana ameketi upande wa kuume akiwa amevaa kanzu nyeupe, nao wakafadhaika.+ 6 Akawaambia: “Acheni kufadhaika. Mnamtafuta Yesu Mnazareti, aliyetundikwa mtini.+ Alifufuliwa,+ hayupo hapa. Tazameni! Mahali walipomlaza.+ 7 Lakini nendeni, mkawaambie wanafunzi wake na Petro, ‘Yeye anawatangulia kuingia Galilaya;+ huko mtamwona, kama vile alivyowaambia ninyi.’ ”+ 8 Kwa hiyo walipotoka wakakimbia kutoka kwenye kaburi, kwa maana walikuwa wakitetemeka nao walikuwa na hisia nyingi. Nao hawakumwambia mtu jambo lolote, kwa maana walikuwa wanaogopa.+
UMALIZIO MFUPI
Hati na tafsiri fulani za mwisho-mwisho zina umalizio mfupi baada ya Marko 16:8, kama ifuatavyo:
Lakini mambo yote yaliyokuwa yameamriwa wakayasimulia kwa ufupi kwa wale waliomzunguka Petro. Tena, baada ya mambo hayo, Yesu mwenyewe akapeleka kupitia wao tangazo takatifu na lisiloweza kuharibika la wokovu wa milele kutoka mashariki mpaka magharibi.
UMALIZIO MREFU
Hati nyingine za kale (Codex Alexandrinus, Codex Ephraemi, Codex Bezae) na tafsiri (Latin Vulgate, Curetonian Syriac, Syriac Peshitta) huongeza umalizio mrefu unaofuata, lakini ambao Codex Sinaiticus, Codex Vaticanus, Sinaitic Syriac codex, na Armenian Version huondoa:
9 Baada ya kufufuka mapema siku ya kwanza ya juma akamtokea kwanza Maria Magdalene, ambaye alikuwa amefukuza roho waovu saba kutoka kwake. 10 Maria Magdalene akaenda, akawaambia wale waliokuwa wamekuwa pamoja na Yesu, kwa maana walikuwa wakiomboleza na kulia. 11 Lakini wao, waliposikia alikuwa amefufuka na Maria Magdalene alikuwa amemwona, hawakuamini. 12 Tena, baada ya mambo hayo aliwatokea katika umbo lingine wawili kati yao wakitembea, walipokuwa wakienda mashambani; 13 nao wakarudi wakawaambia wale wengine. Wala hawakuwaamini. 14 Lakini baadaye akawatokea wale kumi na mmoja wenyewe walipokuwa wameketi mezani, naye akaushutumu ukosefu wao wa imani na ugumu wa moyo, kwa sababu hawakuwaamini wale waliokuwa wamemwona sasa akiwa amefufuka kutoka kwa wafu. 15 Naye akawaambia: “Nendeni, mkaingie katika ulimwengu wote na kuhubiri habari njema kwa uumbaji wote. 16 Yeye anayeamini na kubatizwa ataokolewa, lakini yule ambaye hataamini atahukumiwa adhabu. 17 Zaidi ya hayo, ishara hizi zitafuatana na wale wanaoamini: Kwa kutumia jina langu watatoa roho waovu, watasema kwa lugha, 18 nao watainua nyoka kwa mikono yao, na wakinywa kitu chochote chenye kuua hakitawaumiza hata kidogo. Wataweka mikono yao juu ya watu wagonjwa, nao watapona.”
19 Kwa hiyo, basi, Bwana Yesu, alipokuwa amekwisha kusema nao, akachukuliwa juu mpaka mbinguni na kuketi kwenye mkono wa kuume wa Mungu. 20 Basi, wakatoka kwenda na kuhubiri kila mahali, huku Bwana akifanya kazi pamoja nao na kuutegemeza ujumbe huo kupitia ishara zenye kufuatana nao.
[Maelezo ya Chini]
Bonde la Hinomu. Tazama Nyongeza 2.
Bonde la Hinomu. Tazama Nyongeza 2.
Bonde la Hinomu. Tazama Nyongeza 2.