Kulingana na Luka
1 Kwa kuwa wengi wamechukua daraka la kukusanya habari za mambo ya hakika+ tunayosadiki kikamili kati yetu, 2 sawa na vile wale ambao tangu mwanzo+ walikuwa mashahidi wa kujionea+ na watumishi wa ujumbe+ walivyotuletea haya, 3 mimi pia niliazimia, kwa sababu nimefuata kwa uangalifu mambo yote tangu mwanzo kwa usahihi, kukuandikia hayo kwa utaratibu wenye kufuatana,+ mtukufu+ Theofilo,+ 4 ili upate kujua kabisa uhakika wa mambo ambayo umefundishwa kwa mdomo.+
5 Katika siku za Herode,+ mfalme wa Yudea, kulikuwa na kuhani aliyeitwa Zekaria wa mgawanyo wa Abiya,+ naye alikuwa na mke kutoka kwa binti za Haruni,+ na jina lake lilikuwa Elisabeti. 6 Wote wawili walikuwa waadilifu+ mbele za Mungu kwa sababu ya kutembea bila lawama+ kulingana na amri+ zote na matakwa ya kisheria+ ya Yehova.+ 7 Lakini hawakuwa na mtoto, kwa sababu Elisabeti alikuwa tasa,+ nao wote wawili walikuwa wamesonga sana katika miaka.
8 Basi alipokuwa akitenda akiwa kuhani katika mgawo wa mgawanyo+ wake mbele za Mungu, 9 kulingana na desturi ya cheo cha kikuhani ikawa zamu yake kutoa uvumba+ alipoingia katika patakatifu pa Yehova;+ 10 na umati wote wa watu ulikuwa ukisali nje katika saa hiyo ya kutoa uvumba.+ 11 Malaika wa Yehova akamtokea, akiwa amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya uvumba.+ 12 Lakini Zekaria akataabishwa na jambo hilo aliloona, na woga ukamwingia.+ 13 Hata hivyo, malaika akamwambia: “Usiogope, Zekaria, kwa sababu dua yako imekubaliwa,+ na mke wako Elisabeti atamzaa mwana wako, nawe utamwita jina lake Yohana.+ 14 Nawe utakuwa na shangwe na furaha kubwa, na wengi watashangilia+ kuzaliwa kwake; 15 kwa maana atakuwa mkuu mbele za Yehova.+ Lakini asinywe divai na kileo hata kidogo,+ naye atajazwa roho takatifu akiwa katika tumbo la uzazi la mama yake;+ 16 naye atawarudisha wengi wa wana wa Israeli kwa Yehova+ Mungu wao. 17 Pia, atakwenda mbele zake kwa roho na nguvu za Eliya,+ ili kurudisha mioyo+ ya akina baba kwa watoto na wale wasiotii kwenye hekima inayotumika ya waadilifu, ili kuweka tayari kwa ajili ya Yehova+ watu waliotayarishwa.”+
18 Naye Zekaria akamwambia malaika: “Nitakuwaje na uhakika juu ya jambo hili? Kwa maana nina umri mkubwa+ na mke wangu amesonga sana katika miaka.” 19 Malaika akamjibu akamwambia: “Mimi ni Gabrieli,+ anayesimama karibu mbele za Mungu, nami nilitumwa kusema+ na wewe na kukutangazia habari njema ya mambo hayo. 20 Lakini, tazama! utakuwa kimya+ nawe hutaweza kusema mpaka siku ambayo mambo hayo yatatendeka, kwa sababu hukuamini maneno yangu, ambayo yatatimizwa katika wakati wake uliowekwa.” 21 Wakati huohuo watu wakaendelea kumngoja Zekaria,+ nao wakaanza kustaajabia kukawia kwake katika patakatifu. 22 Lakini alipotoka hakuweza kusema nao, nao wakafahamu kwamba alikuwa ameona maono yanayozidi nguvu za asili+ ndani ya patakatifu; naye akawa anawatolea ishara, lakini akaendelea kuwa bubu. 23 Basi, siku za utumishi wake wa watu wote zilipotimia,+ akaenda nyumbani kwake.
24 Lakini baada ya siku hizo Elisabeti mke wake akapata mimba;+ naye akajitenga kwa miezi mitano, akisema: 25 “Hivi ndivyo Yehova ameshughulika nami siku hizi wakati amenipa uangalifu wake ili kuondolea mbali shutuma yangu katikati ya watu.”+
26 Katika mwezi wake wa sita malaika Gabrieli+ alitumwa kutoka kwa Mungu mpaka jiji moja la Galilaya linaloitwa Nazareti, 27 kwa bikira aliyechumbiwa na mwanamume anayeitwa Yosefu wa nyumba ya Daudi; na jina la bikira+ huyo lilikuwa Maria.+ 28 Na Gabrieli alipoingia mbele yake akasema: “Siku njema,+ uliyependelewa sana, Yehova+ yuko pamoja nawe.”+ 29 Lakini Maria akashtushwa sana na maneno hayo na kuanza kuwaza hiyo ingeweza kuwa ni salamu ya namna gani. 30 Kwa hiyo malaika akamwambia: “Usiogope, Maria, kwa maana umepata kibali+ cha Mungu; 31 na, tazama! utachukua mimba katika tumbo lako la uzazi na kuzaa mwana,+ nawe utamwita jina lake Yesu.+ 32 Huyo atakuwa mkuu+ naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Zaidi;+ na Yehova Mungu atampa kiti cha ufalme+ cha Daudi baba yake,+ 33 naye atatawala akiwa mfalme juu ya nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.”+
34 Lakini Maria akamwambia malaika: “Hilo litawezekanaje, kwa kuwa silali+ na mwanamume?” 35 Malaika akamjibu akamwambia: “Roho takatifu+ itakuja juu yako, na nguvu za Aliye Juu Zaidi zitakufunika. Kwa sababu hiyo pia kile kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu,+ Mwana wa Mungu.+ 36 Na, tazama! Elisabeti mtu wa jamaa yako, yeye pia amechukua mimba ya mwana, katika uzee wake, na huu ni mwezi wake wa sita, yeye ambaye huitwa mwanamke tasa;+ 37 kwa sababu kwa Mungu hakuna tangazo lolote lisilowezekana.”+ 38 Ndipo Maria akasema: “Tazama! Kijakazi+ wa Yehova! Na itendeke kwangu kulingana na tangazo lako.” Ndipo malaika akaondoka.
39 Basi Maria akaondoka katika siku hizo akaenda haraka katika nchi yenye milima, mpaka jiji moja la Yuda, 40 naye akaingia nyumbani mwa Zekaria akamsalimu Elisabeti. 41 Basi, Elisabeti aliposikia salamu za Maria, yule mtoto mchanga katika tumbo lake la uzazi akaruka; na Elisabeti akajazwa roho takatifu, 42 naye akapaaza sauti kubwa na kusema: “Wewe ni mbarikiwa kati ya wanawake, na uzao wa tumbo lako la uzazi umebarikiwa!+ 43 Basi imewezekanaje nikapata pendeleo hili, kwamba mama ya Bwana+ wangu aje kwangu? 44 Kwa maana, tazama! Niliposikia salamu zako, mtoto katika tumbo langu la uzazi aliruka kwa furaha kubwa.+ 45 Mwenye furaha pia ni yule aliyeamini, kwa sababu kutakuwa utimizo kamili+ wa mambo aliyoambiwa kutoka kwa Yehova.”+
46 Naye Maria akasema: “Nafsi yangu inamtukuza Yehova,+ 47 na roho yangu haiwezi kuacha kumfurahia+ Mungu Mwokozi+ wangu; 48 kwa sababu ametazama hali ya chini ya kijakazi+ wake. Kwa maana, tazama! tangu sasa na kuendelea vizazi vyote vitanitangaza kuwa mwenye furaha;+ 49 kwa sababu Mwenye nguvu amenitendea makuu, nalo jina lake ni takatifu;+ 50 na kwa vizazi baada ya vizazi rehema yake iko juu ya wale wanaomwogopa.+ 51 Ametenda kwa nguvu kwa mkono wake,+ amewatawanya kotekote wale wenye majivuno katika kusudi la mioyo yao.+ 52 Amewashusha watu wenye nguvu+ kutoka katika viti vya ufalme na kuwainua watu wa hali ya chini;+ 53 amewashibisha kabisa wenye njaa kwa vitu vyema+ na wale waliokuwa na mali amewaacha waende mikono mitupu.+ 54 Amekuja kumsaidia Israeli mtumishi wake,+ kukumbuka rehema,+ 55 sawa na vile alivyowaambia mababu zetu, Abrahamu na uzao wake, milele.”+ 56 Maria akakaa pamoja naye kwa karibu miezi mitatu, akarudi nyumbani kwake.
57 Sasa wakati ukafika wa Elisabeti kuzaa, naye akazaa mwana. 58 Nao majirani na watu wa jamaa yake wakasikia kwamba Yehova alikuwa ameitukuza rehema+ yake kwake, nao wakaanza kushangilia+ pamoja naye. 59 Na katika siku ya nane wakaja kumtahiri huyo mtoto mchanga,+ nao walitaka kumwita kwa jina la baba yake, Zekaria. 60 Lakini mama yake akajibu akasema: “Sivyo hata kidogo! bali ataitwa Yohana.” 61 Ndipo wakamwambia: “Hakuna yeyote kati ya watu wa jamaa yako anayeitwa kwa jina hilo.” 62 Ndipo wakaanza kumuuliza baba yake kwa ishara jina ambalo alitaka aitwe. 63 Naye akaomba bamba na kuandika: “Yohana+ ndilo jina lake.” Ndipo wote wakastaajabu. 64 Kinywa chake kikafunguka+ mara moja na ulimi wake ukalegea naye akaanza kuongea, akimbariki Mungu. 65 Na wale wote waliokuwa wakiishi katika ujirani wao wakaingiwa na woga; na katika nchi yote ya milima ya Yudea mambo yote hayo yakaanza kuzungumzwa pande zote, 66 na wote waliosikia wakaliweka mioyoni+ mwao, wakisema: “Kwa kweli mtoto huyu mchanga atakuwa wa namna gani?” Kwa maana kwa kweli mkono+ wa Yehova ulikuwa pamoja naye.
67 Na Zekaria baba yake akajazwa roho takatifu,+ naye akatoa unabii,+ akisema: 68 “Na abarikiwe Yehova Mungu wa Israeli,+ kwa sababu ameelekeza uangalifu wake na kufanya ukombozi+ kuelekea watu wake.+ 69 Naye ametuinulia pembe+ ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake, 70 sawa na vile, kupitia kinywa cha manabii wake watakatifu tangu zamani za kale,+ amesema 71 juu ya wokovu kutoka kwa adui zetu na kutoka katika mkono wa wale wote wanaotuchukia;+ 72 kufanya rehema kuhusiana na mababu zetu na kulikumbuka agano lake takatifu,+ 73 kiapo ambacho alimwapia Abrahamu babu yetu,+ 74 kutupa sisi, baada ya kuokolewa kutoka katika mikono ya adui,+ pendeleo la kumtolea utumishi mtakatifu bila woga+ 75 kwa ushikamanifu na uadilifu mbele zake siku zetu zote.+ 76 Na wewe, mtoto mchanga, utaitwa nabii wa Aliye Juu Zaidi, kwa maana utakwenda mbele za Yehova ili kutayarisha njia zake,+ 77 kuwapa watu wake ujuzi wa wokovu kwa msamaha wa dhambi zao,+ 78 kwa sababu ya huruma nyororo za Mungu wetu. Kwa huruma hizo tutapata pambazuko+ kutoka juu,+ 79 kuwapa nuru wale wanaokaa katika giza na katika kivuli+ cha kifo, kuelekeza kwa mafanikio miguu yetu katika njia ya amani.”
80 Na huyo mtoto mchanga akaendelea kukua+ na kupata nguvu katika roho, naye akakaa katika majangwa mpaka siku ya kujionyesha waziwazi kwa Israeli.
2 Basi katika siku hizo Kaisari Augusto alitoa amri+ kwamba dunia yote inayokaliwa iandikishwe; 2 (uandikisho huu wa kwanza ulitendeka wakati Kirenio alipokuwa gavana wa Siria;) 3 na watu wote wakaanza kusafiri kwenda kuandikishwa,+ kila mmoja kwenye jiji lake mwenyewe. 4 Yosefu pia akapanda kutoka Galilaya, kutoka jiji la Nazareti, akaingia Yudea, kwenye jiji la Daudi, linaloitwa Bethlehemu,+ kwa sababu alikuwa mshiriki wa nyumba na familia ya Daudi,+ 5 ili apate kuandikishwa pamoja na Maria,+ aliyekuwa amemwoa kama ilivyoahidiwa,+ wakati huu akiwa karibu kuzaa.+ 6 Walipokuwa huko, siku zikatimia apate kuzaa. 7 Naye akamzaa mwana wake, mzaliwa wa kwanza,+ akamfunga vitambaa na kumlaza katika hori,+ kwa sababu hapakuwa na mahali kwa ajili yao katika chumba cha kukaa.
8 Katika nchi hiyo kulikuwako pia wachungaji wakiishi nje, wakichunga makundi yao usiku. 9 Na kwa ghafula malaika+ wa Yehova akasimama kando yao, na utukufu+ wa Yehova ukamulika pande zote kuwazunguka, nao wakaogopa sana. 10 Lakini malaika akawaambia: “Msiogope, kwa maana, tazama! ninawatangazia ninyi habari njema ya shangwe kubwa ambayo watu wote watakuwa nayo,+ 11 kwa sababu leo katika jiji la Daudi,+ Mwokozi+ ambaye ni Kristo Bwana,+ amezaliwa kwenu.+ 12 Na hii ndiyo ishara kwenu: Mtamkuta mtoto akiwa amefungwa vitambaa na akiwa amelala katika hori.” 13 Na kwa ghafula umati wa jeshi la mbingu+ ukawa pamoja na yule malaika, ukimsifu Mungu+ na kusema: 14 “Utukufu katika vilele vilivyo juu+ kwa Mungu, na juu ya dunia amani+ kati ya watu wa nia njema.”+
15 Kwa hiyo malaika walipokuwa wameondoka na kuingia mbinguni, wachungaji wakaanza kusemezana: “Na twende moja kwa moja mpaka Bethlehemu tukaone jambo hili ambalo limetendeka, ambalo Yehova+ ametujulisha.” 16 Nao wakaenda haraka wakamkuta Maria na vilevile Yosefu, na yule mtoto mchanga akiwa amelala katika hori. 17 Walipomwona, wakasema mambo yaliyokuwa yamesemwa kuhusu mtoto huyo mchanga. 18 Na wote waliosikia wakastaajabu juu ya mambo waliyoambiwa na wachungaji, 19 lakini Maria akaanza kuyahifadhi maneno hayo yote, akikata kauli moyoni mwake.+ 20 Basi wachungaji wakarudi, wakimtukuza na kumsifu Mungu kwa ajili ya mambo yote waliyoyasikia na kuyaona, sawa na walivyokuwa wameambiwa.
21 Basi siku nane+ zilipotimia ili kumtahiri,+ akaitwa pia jina lake Yesu,+ lile jina aliloitwa na malaika kabla hajachukuliwa mimba katika tumbo la uzazi.+
22 Pia, siku za kuwatakasa+ hao kulingana na sheria ya Musa zilipotimia, wakamleta Yesu mpaka Yerusalemu ili kumtoa kwa Yehova, 23 sawa na vile ambavyo imeandikwa katika sheria ya Yehova: “Kila mtoto wa kiume anayefungua tumbo la uzazi lazima aitwe mtakatifu kwa Yehova,”+ 24 na kutoa dhabihu kulingana na yanayosemwa katika sheria ya Yehova: “Njiwa-tetere wawili au hua wachanga wawili.”+
25 Na, tazama! palikuwa na mtu mmoja katika Yerusalemu aliyeitwa Simeoni, na mtu huyo alikuwa mwadilifu na mwenye kumheshimu Mungu, akingojea faraja ya Israeli,+ na roho takatifu ilikuwa juu yake. 26 Zaidi ya hayo, alikuwa amefunuliwa kimungu na roho takatifu kwamba hangeona kifo kabla ya kumwona Kristo+ wa Yehova. 27 Akaja sasa katika hekalu chini ya nguvu za roho;+ na wazazi walipomwingiza mtoto mchanga Yesu ili kufanya kwa ajili yake kulingana na zoea la kidesturi la sheria,+ 28 Simeoni mwenyewe akampokea mtoto mikononi mwake akambariki Mungu na kusema: 29 “Sasa, Bwana Mwenye Enzi Kuu, unamwacha mtumwa wako aende akiwa huru+ kwa amani kulingana na tangazo lako; 30 kwa sababu macho yangu yameona njia yako ya kuokoa+ 31 ambayo umetayarisha mbele ya vikundi vyote vya watu,+ 32 nuru+ ya kuondoa utaji+ kwa mataifa+ na utukufu wa watu wako Israeli.” 33 Na baba na mama yake wakaendelea kustaajabia mambo yaliyokuwa yakisemwa juu yake. 34 Pia, Simeoni akawabariki wao, lakini akamwambia Maria mama yake: “Tazama! Huyu amewekwa kwa ajili ya kuanguka+ na kusimama tena kwa wengi katika Israeli+ na kuwa ishara itakayosemwa vibaya+ 35 (ndiyo, upanga mrefu utaichoma nafsi yako),+ ili mawazo ya mioyo mingi yapate kufunuliwa.”+
36 Basi kulikuwako nabii Ana, binti ya Fanueli, wa kabila la Asheri (mwanamke huyu alikuwa amesonga sana katika miaka, na alikuwa ameishi pamoja na mume kwa miaka saba kutoka ubikira wake, 37 naye sasa alikuwa mjane+ mwenye umri wa miaka 84), ambaye alikuwa hakosi kamwe kuwa katika hekalu, akitoa utumishi mtakatifu usiku na mchana+ kwa kufunga na dua. 38 Na saa ileile akakaribia, akaanza kumshukuru Mungu akisema juu ya mtoto huyo kwa wale wote waliokuwa wakiungojea ukombozi wa Yerusalemu.+
39 Kwa hiyo walipokuwa wametimiza mambo yote kulingana na sheria+ ya Yehova, wakarudi kuingia Galilaya kwenye jiji la kwao la Nazareti.+ 40 Na huyo mtoto mchanga akaendelea kukua na kupata nguvu,+ akijawa na hekima, na kuendelea kuwa na kibali+ cha Mungu.
41 Basi wazazi wake walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu+ mwaka baada ya mwaka kwa ajili ya sherehe ya pasaka. 42 Na alipofika umri wa miaka kumi na miwili, walipanda kulingana na desturi+ ya sherehe 43 wakazikamilisha siku. Lakini walipokuwa wakirudi, mvulana huyo, Yesu, alibaki nyuma Yerusalemu, na wazazi wake hawakutambua. 44 Wakidhani kwamba alikuwa katikati ya kundi lililokuwa likisafiri pamoja, walisafiri umbali+ wa siku moja, kisha wakaanza kumtafuta kwa bidii kati ya jamaa zao na wale wanaojuana nao. 45 Lakini, walipokosa kumpata, wakarudi mpaka Yerusalemu, wakimtafuta kwa bidii. 46 Basi, baada ya siku tatu wakampata katika hekalu,+ ameketi katikati ya walimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali. 47 Lakini wale wote waliokuwa wakimsikiliza walikuwa wakishangazwa daima na uelewaji wake na majibu yake.+ 48 Basi walipomwona wakastaajabu, na mama yake akamwambia: “Mtoto, kwa nini umetutendea hivi? Tazama, baba yako nami tumekuwa tukikutafuta tukiwa na hangaiko la akilini.” 49 Lakini akawaambia: “Kwa nini mlilazimika kunitafuta? Je, hamkujua kwamba ni lazima niwe katika nyumba ya Baba yangu?”+ 50 Hata hivyo, hawakufahamu maneno hayo aliyowaambia.+
51 Naye akashuka kwenda pamoja nao mpaka Nazareti, naye akaendelea kujitiisha+ kwao. Pia, mama yake akaweka kwa uangalifu maneno yote hayo moyoni mwake.+ 52 Na Yesu akazidi kufanya maendeleo katika hekima+ na ukuzi wa kimwili, akipata kibali kwa Mungu na wanadamu.+
3 Katika mwaka wa kumi na tano wa kumiliki kwa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato alipokuwa gavana wa Yudea, na Herode+ alipokuwa mtawala wa wilaya ya Galilaya, lakini Filipo ndugu yake alikuwa mtawala wa wilaya wa nchi ya Iturea na Trakoniti, na Lisania alikuwa mtawala wa wilaya ya Abilene, 2 katika siku za mkuu wa makuhani Anasi na za Kayafa,+ tangazo la Mungu likamjia Yohana+ mwana wa Zekaria nyikani.+
3 Basi akaingia katika nchi yote kuzunguka Yordani, akihubiri ubatizo unaoonyesha toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi,+ 4 kama ilivyoandikwa katika kitabu cha maneno ya nabii Isaya: “Sikilizeni! Mtu fulani anapaaza sauti nyikani, ‘Tayarisheni njia ya Yehova, nyoosheni barabara zake.+ 5 Kila mtaro lazima ujazwe, na kila mlima na kilima vifanywe tambarare, palipopindika lazima pawe njia nyoofu na mahali penye miparuzo pawe njia laini;+ 6 na wote wenye mwili wataona njia ya Mungu ya kuokoa.’ ”+
7 Kwa hiyo akaanza kuuambia umati wa watu waliokuwa wakija awabatize: “Ninyi uzao wa nyoka-vipiri,+ ni nani ambaye amewaonyesha ninyi kuikimbia ghadhabu inayokuja?+ 8 Basi zaeni matunda yanayofaa toba.+ Wala msianze kusema ndani yenu wenyewe, ‘Abrahamu ndiye baba yetu.’ Kwa maana ninawaambia ninyi kwamba Mungu ana nguvu za kumwinulia Abrahamu watoto kutoka katika mawe haya. 9 Kwa kweli, tayari shoka limewekwa kwenye mzizi wa miti; kwa hiyo, kila mti usiozaa matunda mazuri unapaswa kukatwa na kutupwa ndani ya moto.”+
10 Na umati ukamuuliza: “Basi, tufanye nini?”+ 11 Akawajibu, akawaambia: “Mtu aliye na mavazi mawili ya ndani na ashiriki pamoja na mtu ambaye hana hata moja, na aliye na vyakula afanye vivyo hivyo.”+ 12 Lakini hata wakusanya-kodi wakaja ili kubatizwa, nao wakamwambia: “Mwalimu, tufanye nini?”+ 13 Akawaambia: “Msidai zaidi ya kiwango cha kodi.”+ 14 Pia, wale walio katika utumishi wa kijeshi wakamuuliza: “Na sisi pia tufanye nini?” Naye akawaambia: “Msimsumbue mtu yeyote wala kumshtaki+ mtu yeyote kwa uwongo, bali mtosheke na posho lenu.”+
15 Basi kwa kuwa watu walikuwa wakitarajia na wote walikuwa wakiwaza mioyoni mwao juu ya Yohana: “Je, labda yeye ndiye Kristo?”+ 16 Yohana akajibu, akawaambia wote: “Mimi ninawabatiza ninyi kwa maji; lakini mwenye nguvu kuliko mimi anakuja, ambaye kamba ya viatu vyake mimi sistahili kuifungua.+ Yeye atawabatiza ninyi kwa roho takatifu na moto.+ 17 Sepetu yake ya kupepetea imo mkononi mwake ili kuusafisha kabisa uwanja wake wa kupuria na kukusanya+ ngano ndani ya ghala lake, lakini makapi+ atayateketeza kwa moto+ usioweza kuzimwa.”
18 Kwa hiyo alitoa pia mahimizo mengine mengi na kuendelea kuwatangazia watu habari njema. 19 Lakini kwa kuwa alikuwa amemkaripia Herode mtawala wa wilaya kuhusu Herodia mke wa ndugu yake na kuhusu matendo yote maovu ambayo Herode alikuwa amefanya,+ 20 aliongeza hili pia kwa matendo yote hayo: alimfungia Yohana gerezani.+
21 Basi watu wote walipokuwa wamebatizwa, Yesu+ pia akabatizwa na, alipokuwa akisali, mbingu+ ilifunguliwa 22 na roho takatifu katika umbo la njiwa ikashuka juu yake, na sauti ikatoka mbinguni: “Wewe ni Mwanangu, mpendwa; nimekukubali wewe.”+
23 Tena, Yesu mwenyewe, alipoanza kazi yake,+ alikuwa na umri wa karibu miaka 30,+ akiwa mwana,+ kama alivyoonwa,
wa Yosefu,+
mwana wa Heli,
24 mwana wa Mathati,
mwana wa Lawi,
mwana wa Melki,
mwana wa Yanai,
mwana wa Yosefu,
25 mwana wa Matathia,
mwana wa Amosi,
mwana wa Nahumu,
mwana wa Esli,
mwana wa Nagai,
26 mwana wa Maathi,
mwana wa Matathia,
mwana wa Semei,
mwana wa Yoseki,
mwana wa Yoda,
27 mwana wa Yoanani,
mwana wa Resa,
mwana wa Zerubabeli,+
mwana wa Shealtieli,+
mwana wa Neri,
28 mwana wa Melki,
mwana wa Adi,
mwana wa Kosamu,
mwana wa Elmadamu,
mwana wa Eri,
29 mwana wa Yesu,
mwana wa Eliezeri,
mwana wa Yorimu,
mwana wa Mathati,
mwana wa Lawi,
30 mwana wa Simioni,
mwana wa Yuda,
mwana wa Yosefu,
mwana wa Yonamu,
mwana wa Eliakimu,
31 mwana wa Melea,
mwana wa Mena,
mwana wa Matatha,
mwana wa Nathani,+
mwana wa Daudi,+
mwana wa Obedi,+
mwana wa Boazi,+
mwana wa Salmoni,+
mwana wa Nashoni,+
mwana wa Isaka,+
mwana wa Abrahamu,+
mwana wa Tera,+
mwana wa Nahori,+
mwana wa Reu,+
mwana wa Pelegi,+
mwana wa Eberi,+
mwana wa Shela,+
36 mwana wa Kainani,
mwana wa Arpakshadi,+
mwana wa Shemu,+
mwana wa Noa,+
mwana wa Lameki,+
mwana wa Enoko,+
mwana wa Yaredi,+
mwana wa Mahalaleeli,+
mwana wa Kainani,+
mwana wa Sethi,+
mwana wa Adamu,+
mwana wa Mungu.
4 Basi Yesu, akiwa amejaa roho takatifu, akarudi kutoka Yordani, naye akaongozwa na roho huku na huku nyikani+ 2 kwa siku 40,+ alipokuwa akijaribiwa+ na Ibilisi. Zaidi ya hayo, hakula chochote katika siku hizo, na kwa hiyo, zilipomalizika, akaona njaa. 3 Ndipo Ibilisi akamwambia: “Ikiwa wewe ni mwana wa Mungu, liambie jiwe hili liwe mkate.” 4 Lakini Yesu akamjibu: “Imeandikwa, ‘Mwanadamu hataishi kwa mkate tu.’ ”+
5 Kwa hiyo akamleta juu na kumwonyesha mara moja falme zote za dunia inayokaliwa; 6 naye Ibilisi akamwambia: “Hakika nitakupa mamlaka+ yote hii na utukufu wake, kwa sababu nimepewa, na yeyote ninayetaka mimi humpa.+ 7 Kwa hiyo, ukifanya tendo+ la ibada mbele yangu, yote itakuwa yako.” 8 Yesu akajibu akamwambia: “Imeandikwa, ‘Yehova Mungu+ wako ndiye unayepaswa kumwabudu, na yeye peke yake ndiye unayepaswa kumtolea utumishi mtakatifu.’ ”+
9 Sasa akamwongoza kuingia Yerusalemu, akamsimamisha juu ya mnara+ wa hekalu na kumwambia: “Ikiwa wewe ni mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa;+ 10 kwa maana imeandikwa, ‘Atawaagiza malaika zake kukuhusu wewe, ili wakulinde,’+ 11 nao, ‘Watakuchukua mikononi mwao, ili usipate kamwe kuugonga mguu wako juu ya jiwe.’ ”+ 12 Yesu akajibu, akamwambia: “Imesemwa, ‘Usimjaribu Yehova Mungu wako.’ ”+ 13 Kwa hiyo Ibilisi, akiisha kumaliza majaribu yote, akamwacha mpaka wakati mwingine unaofaa.+
14 Basi Yesu akarudi katika nguvu za roho na kuingia Galilaya.+ Na habari nzuri juu yake zikaenea katika nchi yote inayozunguka.+ 15 Pia, akaanza kufundisha katika masinagogi yao, akiheshimiwa na wote.+
16 Naye akaja mpaka Nazareti,+ ambako alikuwa amelelewa; na, kulingana na desturi yake siku ya sabato, akaingia katika sinagogi,+ naye akasimama ili asome. 17 Kwa hiyo akapewa kitabu cha kukunjwa cha nabii Isaya, naye akakifungua na kupata mahali palipokuwa pameandikwa: 18 “Roho ya Yehova+ iko juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kuwatangazia maskini habari njema, alinituma kuhubiri kuachiliwa huru kwa mateka na kupata kuona tena kwa vipofu, kuacha waliopondeka waende zao wakiwa wameachiliwa huru,+ 19 kuhubiri mwaka wa Yehova wenye kukubalika.”+ 20 Ndipo akakikunja kitabu hicho, akamrudishia mtumishi, akaketi; na wote katika sinagogi wakamkazia macho. 21 Ndipo akaanza kuwaambia: “Leo andiko hili ambalo mmesikia sasa hivi limetimizwa.”+
22 Nao wote wakaanza kutoa ushahidi mwema juu yake wakistaajabia maneno yenye kuvutia+ sana yaliyokuwa yakitoka kinywani mwake, na walikuwa wakisema: “Huyu ni mwana wa Yosefu, sivyo?”+ 23 Ndipo akawaambia: “Bila shaka mtautumia mfano huu kwangu, ‘Tabibu,+ jiponye mwenyewe; mambo+ tuliyosikia kwamba yamekwisha kutukia katika Kapernaumu+ yafanye pia hapa katika eneo la nyumbani kwako.’ ”+ 24 Lakini akawaambia: “Kwa kweli ninawaambia ninyi kwamba hakuna nabii anayekubaliwa katika eneo la nyumbani kwake. 25 Kwa mfano, kwa kweli ninawaambia ninyi, Kulikuwa na wajane wengi katika Israeli siku za Eliya, wakati mbingu ilipofungwa kwa miaka mitatu na miezi sita, hivi kwamba njaa kubwa ikatokea katika nchi yote,+ 26 lakini Eliya hakutumwa kwenda kwa hata mmoja wa wanawake hao, ila tu kwenda Sarefathi+ katika nchi ya Sidoni kwa mjane mmoja. 27 Pia, kulikuwa na wenye ukoma wengi katika Israeli wakati wa nabii Elisha, lakini hakuna hata mmoja wao aliyetakaswa, ila Naamani yule mtu wa Siria.”+ 28 Basi wote hao waliokuwa wakisikia mambo hayo katika sinagogi wakajawa na hasira;+ 29 nao wakaondoka, wakamharakisha kwenda nje ya jiji, nao wakampeleka mpaka ukingo wa mlima ambao jiji lao lilikuwa limejengwa juu yake, ili wamporomoshe chini.+ 30 Lakini akapita katikati yao na kwenda zake.+
31 Naye akashuka kwenda Kapernaumu,+ jiji moja la Galilaya. Naye alikuwa akiwafundisha siku ya sabato; 32 nao wakastaajabishwa na njia yake ya kufundisha,+ kwa sababu maneno yake yalikuwa yenye mamlaka.+ 33 Basi katika sinagogi kulikuwa na mtu mwenye roho,+ roho mwovu, mchafu, naye akapaaza sauti: 34 “Ah! Tuna nini nawe,+ Yesu Mnazareti?+ Je, umekuja kutuangamiza? Ninajua+ wewe ni nani, Mtakatifu wa Mungu.”+ 35 Lakini Yesu akamkemea, akisema: “Nyamaza, na umtoke.” Kwa hiyo, baada ya kumwangusha mtu huyo chini katikati yao, yule roho mwovu akamtoka bila kumuumiza.+ 36 Ndipo wote wakashangaa, nao wakaanza kuongea wao kwa wao, wakisema: “Maneno haya ni ya namna gani, kwa sababu yeye huagiza roho wachafu kwa mamlaka na nguvu, nao hutoka?”+ 37 Kwa hiyo habari juu yake zikaenea katika kila pembe ya nchi yenye kuzunguka.+
38 Baada ya kutoka katika sinagogi akaingia katika nyumba ya Simoni. Basi mama-mkwe wa Simoni alikuwa akitaabishwa na homa kali, nao wakamwomba Yesu kwa ajili yake.+ 39 Kwa hiyo akasimama kando yake akaikemea homa hiyo,+ nayo ikamwacha. Akasimama mara moja akaanza kuwahudumia.+
40 Lakini jua lilipokuwa likitua, wale wote waliokuwa na watu wanaougua magonjwa mbalimbali wakawaleta kwake. Akawa akiwaponya kwa kuweka mikono yake juu ya kila mmoja wao.+ 41 Roho waovu pia wakawa wakiwatoka wengi,+ wakipaaza sauti na kusema: “Wewe ndiye Mwana wa Mungu.”+ Lakini, kwa kuwakemea, hakuwa akiwaruhusu kusema,+ kwa sababu walijua kuwa yeye+ ndiye Kristo.+
42 Hata hivyo, kulipokuwa mchana, akaenda mahali ambapo hapakuwa na watu.+ Lakini umati ukaanza kumtafuta huku na huku na kuja mpaka alipokuwa, nao ukajaribu kumzuia asitoke kwao. 43 Lakini akawaambia: “Ni lazima nitangaze habari njema ya ufalme wa Mungu kwenye majiji mengine pia, kwa sababu nilitumwa kufanya hivyo.”+ 44 Basi akaendelea kuhubiri katika masinagogi ya Yudea.+
5 Pindi moja umati ulipokuwa ukimsonga na kusikiliza neno la Mungu, alikuwa amesimama kando ya ziwa la Genesareti.+ 2 Naye akaona mashua mbili zimeegeshwa kando ya ziwa, lakini wavuvi walikuwa wametoka ndani yake nao walikuwa wakiosha nyavu zao.+ 3 Akapanda ndani ya moja kati ya mashua hizo, iliyokuwa ya Simoni, akamwomba aivute mbali kidogo na nchi kavu. Ndipo akaketi, na kuanza kuufundisha umati akiwa kwenye mashua+ hiyo. 4 Alipoacha kusema, akamwambia Simoni: “Vuta mpaka mahali penye kilindi, nanyi mshushe nyavu+ zenu, mvue.” 5 Lakini Simoni akajibu, akasema: “Mwalimu, tulitaabika usiku wote na hatukupata chochote,+ lakini nitazishusha nyavu kwa amri yako.” 6 Basi, walipofanya hivyo, wakakusanya samaki wengi sana. Kwa kweli, nyavu zao zikaanza kupasuka. 7 Kwa hiyo wakawapungia wenzao mkono katika ile mashua nyingine waje kuwasaidia;+ nao wakaja, wakajaza mashua zote mbili, hivi kwamba zikaanza kuzama. 8 Alipoona hili, Simoni Petro+ akaanguka magotini pa Yesu, akisema: “Ondoka kwangu, kwa sababu mimi ni mtu mwenye dhambi, Bwana.”+ 9 Kwa maana yeye na wote waliokuwa pamoja naye walishangazwa sana na samaki waliovua, 10 na vivyo hivyo Yakobo na Yohana pia, wana wa Zebedayo,+ ambao walikuwa washiriki pamoja na Simoni. Lakini Yesu akamwambia Simoni: “Acha kuogopa. Tangu sasa na kuendelea utakuwa ukiwavua watu wakiwa hai.”+ 11 Kwa hiyo wakazirudisha mashua kwenye nchi kavu, wakaacha kila kitu, wakamfuata.+
12 Pindi nyingine alipokuwa katika moja kati ya majiji hayo, tazama! mwanamume mwenye kujaa ukoma! Alipomwona Yesu akajiangusha kifudifudi akamwomba, akisema: “Bwana, ikiwa tu unataka, unaweza kunitakasa.”+ 13 Kwa hiyo, akaunyoosha mkono wake, akamgusa, na kusema: “Ninataka. Takasika.” Na mara moja ule ukoma ukamtoka.+ 14 Naye akamwagiza mtu huyo asimwambie mtu yeyote:+ “Lakini nenda zako, ukajionyeshe kwa kuhani,+ na kutoa toleo+ la kutakaswa kwako, sawa na vile Musa alivyoamuru, ili kuwa ushahidi kwao.”+ 15 Lakini habari juu yake ilikuwa ikienea hata zaidi, na umati mkubwa ukawa ukikusanyika ili kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao.+ 16 Hata hivyo, akaendelea kukaa faraghani katika majangwa na kusali.+
17 Siku moja alikuwa akifundisha, na Mafarisayo na walimu wa sheria waliokuwa wamekuja kutoka kila kijiji cha Galilaya na Yudea na Yerusalemu walikuwa wameketi hapo; nazo nguvu za Yehova zilikuwa hapo ili aponye.+ 18 Na, tazama! wanaume waliokuwa wamembeba kitandani mtu aliyekuwa amepooza, nao walikuwa wakitafuta njia ya kumwingiza na kumweka mbele yake.+ 19 Kwa hiyo, walipokosa njia ya kumwingiza kwa sababu ya umati, wakapanda juu kwenye paa, na kupitia vigae wakamshusha chini pamoja na kile kitanda kidogo kati ya wale waliokuwa mbele ya Yesu.+ 20 Naye alipoona imani yao akasema: “Ewe mtu, umesamehewa dhambi zako.”+ 21 Basi waandishi na Mafarisayo wakaanza kujadiliana, wakisema: “Ni nani huyu anayesema makufuru?+ Ni nani anayeweza kusamehe dhambi ila Mungu peke yake?”+ 22 Lakini Yesu, akifahamu mawazo yao, akawajibu, akasema: “Ni nini mnachowaza mioyoni mwenu?+ 23 Ni jambo gani lililo rahisi zaidi, kusema, ‘Umesamehewa dhambi zako,’ au kusema, ‘Simama utembee’?+ 24 Lakini ili mjue kwamba Mwana wa binadamu ana mamlaka ya kusamehe dhambi duniani —” akamwambia mtu aliyepooza: “Ninakuambia, Simama, chukua kitanda chako, uende nyumbani.”+ 25 Na mara moja akasimama mbele yao, akachukua kile alichokuwa akilalia, akaenda nyumbani kwake, akimtukuza Mungu.+ 26 Ndipo wote wakashangilia,+ nao wakaanza kumtukuza Mungu, wakaogopa, wakisema: “Tumeona mambo mageni leo!”+
27 Basi baada ya mambo hayo aliondoka na kumwona mkusanya-kodi anayeitwa Lawi akiwa ameketi kwenye ofisi ya kodi, naye akamwambia: “Uwe mfuasi wangu.”+ 28 Na baada ya kuacha kila kitu+ akaondoka akaanza kumfuata. 29 Pia, Lawi akamwandalia karamu kubwa ya kumkaribisha nyumbani kwake; na kulikuwa na umati mkubwa wa wakusanya-kodi na wengine waliokuwa pamoja nao wakiwa wameketi kwenye mlo.+ 30 Ndipo Mafarisayo na waandishi wao wakaanza kuwanung’unikia wanafunzi wake, wakisema: “Kwa nini mnakula na kunywa pamoja na wakusanya-kodi na watenda-dhambi?”+ 31 Yesu akajibu, akawaambia: “Wale walio na afya hawahitaji tabibu,+ bali wale wanaougua ndio wanaomhitaji.+ 32 Nimekuja kuwaita, si watu waadilifu, bali watenda-dhambi watubu.”+
33 Wakamwambia: “Wanafunzi wa Yohana hufunga mara nyingi na kutoa dua, na ndivyo wanavyofanya wale wa Mafarisayo, lakini wako hula na kunywa.”+ 34 Yesu akawaambia: “Je, mnaweza kuwafanya rafiki za bwana-arusi wafunge wakati bwana-arusi yupo pamoja nao?+ 35 Lakini siku zitakuja wakati ambapo kwa kweli bwana-arusi+ ataondolewa kwao;+ ndipo watakapofunga siku hizo.”+
36 Tena, akaendelea kuwapa mfano: “Hakuna mtu ambaye hukata kiraka kutoka katika vazi jipya la nje na kukishonelea katika vazi la nje la zamani; lakini akifanya hivyo, kiraka kipya huraruka na pia kiraka kutoka katika vazi jipya hakilingani na lile vazi la zamani.+ 37 Zaidi ya hayo, hakuna anayeweka divai mpya ndani ya viriba vya divai vilivyozeeka; lakini akifanya hivyo, ndipo divai mpya itavipasua viriba vya divai,+ nayo itamwagika navyo viriba vya divai vitaharibika.+ 38 Lakini divai mpya lazima iwekwe ndani ya viriba vipya vya divai. 39 Hakuna mtu ambaye amekunywa divai ya zamani anayetaka ile mpya; kwa maana husema, ‘Ile ya zamani+ ndiyo nzuri.’ ”
6 Basi siku moja ya sabato alikuwa anapita katikati ya mashamba ya nafaka, na wanafunzi wake walikuwa wakivunja+ na kula masuke ya nafaka, wakiyapukusa kwa mikono yao.+ 2 Ndipo baadhi ya Mafarisayo wakasema: “Kwa nini mnafanya jambo lisilo halali+ katika siku ya sabato?”+ 3 Lakini Yesu akajibu akasema: “Je, hamjasoma kamwe jambo alilofanya Daudi+ wakati yeye na wale watu waliokuwa pamoja naye walipoona njaa?+ 4 Jinsi alivyoingia ndani ya nyumba ya Mungu akapokea mikate ya toleo+ naye akala na kuwapa watu waliokuwa pamoja naye baadhi yake, ambayo si halali kwa mtu yeyote kula ila makuhani tu?”+ 5 Naye akaendelea kuwaambia: “Mwana wa binadamu ndiye Bwana wa sabato.”+
6 Baadaye siku nyingine ya sabato+ akaingia katika sinagogi, akaanza kufundisha. Na kulikuwa na mtu mmoja ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.+ 7 Waandishi na Mafarisayo sasa walikuwa wakimchunguza+ sana waone kama angeponya katika siku ya sabato, ili wapate njia fulani ya kumshtaki.+ 8 Hata hivyo, alijua mawazo yao,+ lakini akamwambia mtu huyo mwenye mkono uliopooza: “Inuka usimame katikati.” Naye akainuka akasimama.+ 9 Ndipo Yesu akawaambia: “Ninawauliza ninyi, Je, katika siku ya sabato ni halali kutenda mema+ au kutenda mabaya, kuokoa au kuangamiza nafsi?”+ 10 Na baada ya kutazama huku na huku kuwaelekea wote, akamwambia mtu huyo: “Nyoosha mkono wako.” Akaunyoosha, na mkono wake ukapona.+ 11 Lakini wakaingiwa na wazimu, nao wakaanza kuzungumza wao kwa wao jambo ambalo wangeweza kumtendea Yesu.+
12 Siku hizo zilipokuwa zikiendelea alienda mlimani kusali,+ naye akaendelea kusali kwa Mungu usiku wote.+ 13 Lakini ilipokuwa mchana akawaita wanafunzi wake akachagua kutoka kati yao kumi na wawili, ambao pia aliwaita “mitume”:+ 14 Simoni, ambaye pia alimwita jina Petro,+ na Andrea ndugu yake, na Yakobo na Yohana,+ na Filipo+ na Bartholomayo, 15 na Mathayo na Tomasi,+ na Yakobo mwana wa Alfayo, na Simoni anayeitwa “mwenye bidii,”+ 16 na Yuda mwana wa Yakobo, na Yuda Iskariote, aliyegeuka kuwa msaliti.+
17 Naye akashuka pamoja nao na kusimama mahali tambarare, na kulikuwa na umati mkubwa wa wanafunzi wake, na umati mkubwa wa watu+ kutoka Yudea yote na Yerusalemu na eneo la pwani la Tiro na Sidoni, waliokuja kumsikia na kuponywa magonjwa yao.+ 18 Hata wale waliotaabishwa na roho wachafu waliponywa. 19 Na umati wote ulikuwa ukitafuta kumgusa,+ kwa sababu nguvu+ zilikuwa zikimtoka na kuwaponya wote.
20 Naye akainua macho yake juu ya wanafunzi wake na kuanza kusema:+
“Wenye furaha ni ninyi maskini,+ kwa sababu ufalme wa Mungu ni wenu.
21 “Wenye furaha ni ninyi mlio na njaa+ sasa, kwa sababu mtashiba.+
“Wenye furaha ni ninyi mnaolia sasa, kwa sababu mtacheka.+
22 “Wenye furaha ni ninyi wakati wowote ule watu wanapowachukia+ ninyi, na wakati wowote ule watu wanapowatenga ninyi na kuwashutumu na kulitupa nje+ jina lenu kuwa ovu kwa ajili ya Mwana wa binadamu. 23 Shangilieni siku hiyo na kuruka, kwa maana, tazama! thawabu yenu ni kubwa mbinguni, kwa maana mambo hayo ndiyo mababu zao walikuwa wakiwafanyia manabii.+
24 “Lakini ole wenu ninyi watu matajiri,+ kwa sababu mnapata faraja yenu kikamili.+
25 “Ole wenu ninyi ambao mmeshiba sasa, kwa sababu mtakaa mkiwa na njaa.+
“Ole, ninyi mnaocheka sasa, kwa sababu mtaomboleza na kulia.+
26 “Ole, wakati wowote ule watu wote wanaposema vema juu yenu, kwa maana mambo kama hayo ndiyo ambayo mababu zao waliwafanyia manabii wa uwongo.+
27 “Lakini mimi ninawaambia ninyi mnaosikiliza, Endeleeni kuwapenda adui zenu,+ kuwafanyia mema+ wale wanaowachukia, 28 kuwabariki wale wanaowalaani, kusali kwa ajili ya wale wanaowatusi.+ 29 Anayekupiga kwenye shavu+ moja, mgeuzie lile lingine pia; na anayechukua+ vazi lako la nje, usimzuilie hata lile vazi la ndani. 30 Mpe kila mtu anayekuomba,+ na yule anayechukua vitu vyako, usimwombe akurudishie.
31 “Pia, kama vile mnavyotaka watu wawatendee ninyi, watendeeni wao vivyo hivyo.+
32 “Na mkiwapenda wale wanaowapenda ninyi, hilo linawapa sifa gani? Kwa maana hata watenda-dhambi huwapenda wale wanaowapenda wao.+ 33 Na mkiwatendea mema wale wanaowatendea ninyi mema, kwa kweli hilo linawapa sifa gani? Hata watenda-dhambi hufanya vivyo hivyo.+ 34 Pia, mkikopesha bila faida+ wale ambao mnatumaini kupokea kutoka kwao, hilo linawapa sifa gani? Hata watenda-dhambi huwakopesha watenda-dhambi bila faida ili wapate kurudishiwa kwa kadiri ileile.+ 35 Badala yake, endeleeni kuwapenda adui zenu na kutenda mema na kukopesha+ bila faida, bila kutumainia kurudishiwa chochote; na thawabu yenu itakuwa kubwa, nanyi mtakuwa wana wa Aliye Juu Zaidi,+ kwa sababu yeye ni mwenye fadhili+ kuwaelekea wasio na shukrani na waovu. 36 Endeleeni kuwa wenye rehema, kama vile Baba yenu alivyo mwenye rehema.+
37 “Zaidi ya hayo, acheni kuhukumu, nanyi hamtahukumiwa;+ na acheni kulaumu, nanyi hamtalaumiwa. Endeleeni kuachilia, nanyi mtaachiliwa.+ 38 Muwe na mazoea ya kuwapa watu, na watu watawapa ninyi.+ Watawamwagia katika mfuko wa nguo zenu kipimo kizuri, kilichoshindiliwa, kilichotikiswa pamoja na kufurika. Kwa maana kwa kipimo mnachopimia, watawapimia ninyi pia.”+
39 Ndipo akawaambia pia mfano: “Je, kipofu anaweza kumwongoza kipofu? Je, wote wawili hawatatumbukia ndani ya shimo?+ 40 Mwanafunzi hampiti mwalimu wake, lakini kila mtu aliyefundishwa kikamili atakuwa kama mwalimu wake.+ 41 Basi, kwa nini unautazama unyasi ulio katika jicho la ndugu yako lakini huliangalii boriti lililo katika jicho lako mwenyewe?+ 42 Unawezaje kumwambia ndugu yako, ‘Ndugu, niruhusu niutoe unyasi ulio katika jicho lako,’ hali wewe mwenyewe hulitazami boriti katika hilo jicho lako?+ Mnafiki! Kwanza toa boriti katika jicho lako mwenyewe,+ ndipo utaona waziwazi jinsi ya kuutoa unyasi ulio katika jicho la ndugu yako.+
43 “Kwa maana hakuna mti mzuri unaozaa matunda yaliyooza; tena hakuna mti uliooza unaozaa matunda mazuri.+ 44 Kwa maana kila mti hujulikana kwa matunda yake.+ Kwa mfano, watu hawakusanyi tini kutoka katika miiba, wala hawakati zabibu kutoka katika mti wa miiba.+ 45 Mtu mwema hutokeza mema katika hazina njema+ ya moyo wake, lakini mtu mwovu hutokeza maovu katika hazina yake mbovu; kwa maana kutokana na wingi wa moyo kinywa chake husema.+
46 “Kwa nini, basi, mnaniita ‘Bwana! Bwana!’ lakini hamfanyi mambo ninayosema?+ 47 Kila mtu anayekuja kwangu na kusikia maneno yangu na kuyatenda, nitawaonyesha ninyi yeye anafanana na nani:+ 48 Huyo anafanana na mtu anayejenga nyumba, ambaye alichimba akaenda chini kina kirefu na kuweka msingi juu ya mwamba. Baadaye, mafuriko+ yalipotokea, mto uliipiga nyumba hiyo kwa nguvu, lakini haukuwa na nguvu za kutosha kuitikisa, kwa sababu ilikuwa imejengwa vizuri.+ 49 Kwa upande mwingine, yule anayesikia na hatendi,+ anafanana na mtu aliyejenga nyumba juu ya udongo bila msingi. Mto uliipiga kwa nguvu, na mara ikaporomoka, na uharibifu+ wa nyumba hiyo ukawa mkubwa.”+
7 Alipokuwa amemaliza maneno yake yote masikioni mwa watu, akaingia Kapernaumu.+ 2 Sasa mtumwa wa ofisa-jeshi mmoja, aliyemthamini sana, alikuwa anaugua na alikuwa karibu kufa.+ 3 Aliposikia juu ya Yesu, akawatuma kwake wanaume wazee wa Wayahudi kumwomba aje na kumponya mtumwa wake. 4 Ndipo wale waliomjia Yesu wakaanza kumsihi kwa bidii, wakisema: “Anastahili wewe umtendee jambo hili, 5 kwa maana analipenda taifa letu+ naye alitujengea sinagogi.” 6 Kwa hiyo Yesu akaondoka pamoja nao. Alipokuwa karibu na nyumba hiyo, yule ofisa-jeshi alikuwa tayari amewatuma rafiki wamwambie: “Bwana, usijisumbue, kwa maana mimi sistahili wewe uingie chini ya paa yangu.+ 7 Ni kwa sababu hiyo mimi niliona kuwa sistahili kuja kwako. Lakini sema neno, naye mtumishi wangu apone. 8 Kwa maana mimi pia niko chini ya mamlaka, nikiwa na askari-jeshi chini yangu, nami humwambia huyu, ‘Ondoka uende zako!’ naye huondoka na kwenda zake, na kwa mwingine, ‘Njoo!’ naye huja, na kwa mtumwa wangu, ‘Fanya hili!’ naye hulifanya.”+ 9 Basi, Yesu aliposikia mambo hayo alimstaajabia, naye akaugeukia umati uliomfuata na kusema: “Ninawaambia ninyi, Hata katika Israeli sijapata imani kubwa kama hii.”+ 10 Na wale waliokuwa wametumwa, waliporudi nyumbani, wakamkuta huyo mtumwa akiwa katika afya njema.+
11 Muda mfupi baadaye akasafiri mpaka jiji linaloitwa Naini, na wanafunzi wake na umati mkubwa walikuwa wakisafiri pamoja naye. 12 Alipokaribia lango la jiji, kumbe! tazama! kulikuwa na mfu+ akiwa anapelekwa nje, mwana mzaliwa-pekee+ wa mama yake. Mbali na hilo, alikuwa ni mjane. Pia umati mkubwa kutoka jijini ulikuwa pamoja naye. 13 Na Bwana alipomwona akamsikitikia,+ akamwambia: “Acha kulia.”+ 14 Ndipo akakaribia na kuligusa sanduku, na wachukuzi wakasimama tuli, naye akasema: “Kijana, ninakuambia, Inuka!”+ 15 Na huyo mfu akaketi na kuanza kusema, naye akamkabidhi kwa mama yake.+ 16 Basi woga+ ukawashika wote, nao wakaanza kumtukuza Mungu, wakisema: “Nabii+ mkuu ameinuliwa katikati yetu,” na, “Mungu amewaelekezea watu wake uangalifu wake.”+ 17 Na habari hii kumhusu ikaenea katika Yudea yote na nchi yote inayozunguka.
18 Sasa wanafunzi wa Yohana wakamjulisha mambo yote haya.+ 19 Kwa hiyo Yohana akawaita wawili kati ya wanafunzi wake na kuwatuma kwa Bwana na kusema: “Je, wewe ndiye Yule Anayekuja au tumtarajie mwingine?”+ 20 Walipofika kwake wanaume hao wakasema: “Yohana Mbatizaji alitutuma kwako na kusema: ‘Wewe ndiye Yule Anayekuja au tumtarajie mwingine?’ ” 21 Saa hiyo akaponya wengi magonjwa+ na maradhi yenye kuhuzunisha na roho waovu, na kuwapa vipofu wengi uwezo wa kuona. 22 Kwa sababu hiyo akajibu, akawaambia hao wawili: “Nendeni,+ mkamwambie Yohana yale mliyoona na kusikia: vipofu+ wanaona, vilema wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa na viziwi wanasikia, na wafu wanafufuliwa, maskini wanaambiwa+ ile habari njema.+ 23 Na mwenye furaha ni yule ambaye hakukwazika juu yangu.”+
24 Wajumbe wa Yohana walipokuwa wamekwenda zao, akaanza kuuambia umati kuhusu Yohana: “Mlienda nyikani kuona nini? Tete likitikiswa na upepo?+ 25 Basi, mlienda kuona nini? Mtu aliyevaa mavazi mororo ya nje?+ Kwani! wale wanaovaa vazi maridadi na wenye kuwa katika anasa wamo katika nyumba za kifalme.+ 26 Basi, kwa kweli mlichoenda kuona ni nini? Nabii?+ Ndiyo, ninawaambia ninyi, na ni zaidi ya nabii.+ 27 Huyu ndiye ambaye imeandikwa hivi kumhusu, ‘Tazama! Ninamtuma mjumbe wangu mbele ya uso wako,+ ambaye atatayarisha njia yako mbele yako.’+ 28 Ninawaambia ninyi, Kati ya wale waliozaliwa na wanawake hakuna hata mmoja aliye mkuu+ kuliko Yohana; lakini mtu aliye mdogo zaidi katika ufalme wa Mungu ni mkuu kuliko yeye.”+ 29 (Na watu wote na wakusanya-kodi, waliposikia hili, wakamtangaza Mungu kuwa mwadilifu,+ wakiwa wamekwisha kubatizwa kwa ubatizo wa Yohana.+ 30 Lakini Mafarisayo na wale wenye ujuzi mwingi wa Sheria walilipuuza shauri+ la Mungu kwao, kwa kuwa hakuwa amewabatiza.)
31 “Basi, mimi nitalinganisha watu wa kizazi hiki na nani, nao ni kama nani?+ 32 Wao ni kama watoto wachanga ambao wameketi sokoni na kupaaziana sauti, na ambao wanasema, ‘Tuliwapigia ninyi filimbi, lakini hamkucheza dansi; tuliomboleza, lakini hamkulia.’+ 33 Kulingana na hilo, Yohana Mbatizaji amekuja akiwa hali mkate wala kunywa divai, lakini mnasema, ‘Ana roho mwovu.’+ 34 Mwana wa binadamu amekuja akila na kunywa, lakini mnasema, ‘Tazama! Mtu mlafi na mwenye mazoea ya kunywa divai, rafiki ya wakusanya-kodi na watenda-dhambi!’+ 35 Hata hivyo, hekima+ huonyeshwa kuwa yenye uadilifu kwa watoto wake wote.”+
36 Basi mmoja wa Mafarisayo akawa akimwomba ale pamoja naye. Basi akaingia katika nyumba+ ya Farisayo huyo na kuketi mezani. 37 Na, tazama! mwanamke aliyejulikana jijini kuwa mtenda-dhambi akapata habari kwamba alikuwa ameketi kwenye mlo katika nyumba ya Farisayo, naye akaleta chupa ya alabasta+ iliyo na mafuta yenye marashi, 38 na, baada ya kukaa miguuni pake, akalia na kuanza kulowesha miguu yake kwa machozi yake naye akawa akiyafuta kwa nywele za kichwa chake. Pia, akaibusu miguu yake kwa wororo na kuipaka mafuta yenye marashi. 39 Alipoona hayo yule Farisayo aliyemwalika akasema moyoni mwake: “Mtu huyu, kama angekuwa nabii,+ angejua mwanamke huyu anayemgusa ni nani na ni mtu wa aina gani, kwamba ni mtenda-dhambi.”+ 40 Lakini Yesu akajibu akamwambia: “Simoni, nina jambo la kukuambia.” Akasema: “Sema, Mwalimu!”
41 “Watu wawili walikuwa na deni kwa mkopeshaji fulani; mmoja alikuwa na deni la dinari+ 500, lakini yule mwingine la 50. 42 Walipokuwa hawana kitu cha kulipa, aliwasamehe+ kwa hiari wote wawili. Kwa hiyo, ni nani kati yao atampenda zaidi?” 43 Simoni akajibu akasema: “Nadhani ni yule ambaye alimsamehe kwa hiari zilizo nyingi zaidi.” Akamwambia: “Umeamua kwa usahihi.” 44 Ndipo akamgeukia yule mwanamke na kumwambia Simoni: “Unamwona mwanamke huyu? Niliingia katika nyumba yako; wewe hukunipa maji+ kwa ajili ya miguu yangu. Lakini mwanamke huyu ameilowesha miguu yangu kwa machozi yake na kuyafuta kwa nywele zake. 45 Wewe hukunibusu+ kamwe; lakini mwanamke huyu, tangu saa nilipoingia, hakuacha kuibusu miguu yangu kwa wororo. 46 Wewe hukukipaka kichwa changu mafuta;+ lakini mwanamke huyu aliipaka miguu yangu mafuta yenye marashi. 47 Kwa hiyo, ninakuambia, dhambi zake, ingawa ni nyingi, zimesamehewa,+ kwa sababu alipenda sana; lakini yule anayesamehewa kidogo, hupenda kidogo.” 48 Ndipo akamwambia mwanamke huyo: “Dhambi zako zimesamehewa.”+ 49 Ndipo wale waliokuwa wameketi mezani pamoja naye wakaanza kusema mioyoni mwao: “Ni nani mtu huyu ambaye hata husamehe dhambi?”+ 50 Lakini akamwambia yule mwanamke: “Imani yako imekuokoa;+ nenda zako kwa amani.”+
8 Upesi baadaye akaanza kusafiri kutoka jiji mpaka jiji na kutoka kijiji mpaka kijiji, akihubiri na kutangaza habari njema ya ufalme wa Mungu.+ Na wale kumi na wawili walikuwa pamoja naye, 2 na wanawake+ fulani waliokuwa wameponywa roho waovu na magonjwa, Maria anayeitwa Magdalene, ambaye roho waovu saba walikuwa wamemtoka,+ 3 na Yoana+ mke wa Kuza, msimamizi wa Herode, na Susana na wanawake wengine wengi, waliokuwa wakiwahudumia kwa mali zao.
4 Sasa umati mkubwa ulipokuwa umekusanyika pamoja na wale waliomwendea kutoka jiji baada ya jiji, akasema kwa njia ya mifano:+ 5 “Mpandaji alienda kupanda mbegu zake. Basi, alipokuwa akipanda, mbegu fulani zikaanguka kando ya barabara zikakanyagwa-kanyagwa, na ndege wa mbinguni wakazila.+ 6 Nyingine zikaanguka juu ya mwamba, na, baada ya kuota, zikakauka kwa sababu ya kutokuwa na umajimaji.+ 7 Nyingine zikaanguka katikati ya miiba, na miiba iliyokua pamoja nazo ikazisonga.+ 8 Nyingine zikaanguka juu ya udongo mzuri, na, baada ya kuota, zikazaa matunda mara mia.”+ Alipokuwa akisema mambo hayo, akapaaza sauti: “Yule aliye na masikio ya kusikiliza, na asikilize.”+
9 Lakini wanafunzi wake wakaanza kumuuliza mfano huo ungeweza kuwa na maana gani.+ 10 Akasema: “Ninyi mmepewa uwezo wa kuzielewa siri takatifu za ufalme wa Mungu, lakini kwa wale wengine zimo kwa mifano,+ ili, ingawa wanatazama, wapate kutazama bure na, ingawa wanasikia, wasiipate maana.+ 11 Basi mfano+ huo unamaanisha hivi: Hizo mbegu ni neno la Mungu.+ 12 Zile zilizo kando ya barabara ni wale ambao wamesikia,+ kisha Ibilisi+ huja na kuliondoa lile neno kutoka mioyoni mwao ili wasipate kuamini na kuokolewa.+ 13 Zile zilizo juu ya mwamba ndio wale ambao, wanapolisikia, hulipokea lile neno kwa shangwe, lakini hawana mzizi; wao huamini kwa muda, lakini wakati wa jaribu wao huanguka.+ 14 Nazo zile zilizoanguka katikati ya miiba, hawa ndio ambao wamesikia, lakini, kwa kuchukuliwa na mahangaiko na utajiri na raha+ za maisha haya, wao husongwa kabisa na hawatimizi chochote.+ 15 Na zile zilizo kwenye udongo mzuri, hawa ndio ambao, baada ya kusikia lile neno kwa moyo+ mzuri na mwema, hulihifadhi na kuzaa matunda kwa uvumilivu.+
16 “Hakuna yeyote ambaye, baada ya kuwasha taa, huifunika na chombo au kuiweka chini ya kitanda, bali huiweka juu ya kinara cha taa, ili wale wanaoingia ndani wapate kuiona nuru.+ 17 Kwa maana hakuna jambo lililofichwa+ ambalo halitafunuliwa, wala kitu chochote kilichofunikwa kwa uangalifu ambacho hakitajulikana kamwe na ambacho hakitakuwa wazi kamwe.+ 18 Kwa hiyo kazieni uangalifu jinsi mnavyosikiliza; kwa maana yeyote aliye na kitu, ataongezewa,+ lakini yeyote ambaye hana kitu, hata kile anachowazia kwamba anacho kitachukuliwa.”+
19 Sasa mama yake na ndugu zake+ wakamjia, lakini hawakuweza kumfikia kwa sababu ya umati.+ 20 Hata hivyo, akaambiwa: “Mama yako na ndugu zako wamesimama nje wakitaka kukuona.”+ 21 Akajibu, akawaambia: “Mama yangu na ndugu zangu ni hawa wanaosikia neno la Mungu na kulitenda.”+
22 Baadaye katika moja kati ya hizo siku yeye na wanafunzi wake waliingia katika mashua, naye akawaambia: “Na tuvuke mpaka upande ule mwingine wa ziwa.” Kwa hiyo wakasafiri.+ 23 Lakini walipokuwa wakisafiri akalala usingizi. Sasa dhoruba ya upepo wenye nguvu nyingi ikashuka juu ya ziwa, nao wakaanza kujawa na maji na kuwa hatarini.+ 24 Mwishowe wakamwendea, wakamwamsha, wakisema: “Mwalimu, Mwalimu, tuko karibu kuangamia!”+ Akaamka, akaukemea+ upepo na mchafuko wa maji, navyo vikatulia, kukawa na utulivu. 25 Ndipo akawaambia: “Imani yenu iko wapi?” Lakini wakiwa wameingiwa na woga, wakastaajabu, wakaambiana: “Kwa kweli huyu ni nani, kwa maana anaagiza hata pepo na maji, nazo zinamtii?”+
26 Nao wakaegesha pwani katika nchi ya Wagerasene, iliyoko upande wa pili wa Galilaya.+ 27 Lakini alipotoka kwenye nchi kavu mwanamume fulani kutoka katika jiji hilo aliyekuwa na roho waovu akakutana naye. Na alikuwa hajavaa mavazi kwa muda mrefu, naye alikuwa akikaa, si nyumbani, bali katikati ya makaburi.+ 28 Alipomwona Yesu akalia kwa sauti kubwa akaanguka chini mbele yake, na kwa sauti kubwa akasema: “Nina nini nawe,+ Yesu Mwana wa Mungu Aliye Juu Zaidi? Ninakuomba, usinitese.”+ 29 (Kwa maana alikuwa akimwagiza huyo roho mchafu amtoke mtu huyo. Kwa maana kwa muda mrefu alikuwa amemshika sana,+ naye alifungwa mara kwa mara kwa minyororo na pingu akiwa chini ya ulinzi, lakini akawa akivivunja vifungo hivyo na kukimbizwa na huyo roho mwovu katika mahali pasipo na watu.) 30 Yesu akamuuliza: “Jina lako ni nani?” Akasema: “Kikosi,” kwa sababu roho wengi waovu walikuwa wamemwingia.+ 31 Nao wakaendelea kumsihi+ asiwaagize waingie katika abiso.+ 32 Sasa hesabu kubwa ya kundi la nguruwe+ ilikuwa ikilisha juu ya mlima; kwa hiyo wakamsihi awaruhusu waingie ndani yao.+ Naye akawapa ruhusa. 33 Ndipo hao roho waovu wakamtoka mtu huyo na kuingia ndani ya wale nguruwe, na lile kundi likatimua mbio, likaruka poromoko, likaingia katika ziwa na kufa maji.+ 34 Lakini wachungaji walipoona lililokuwa limetukia, wakakimbia na kupeleka habari jijini na mashambani.+
35 Ndipo watu wakatokea ili kuona lililokuwa limetukia, nao wakamjia Yesu, wakamkuta yule mtu aliyetokwa na wale roho waovu, akiwa amevaa nguo na akiwa na akili zake timamu, ameketi miguuni pa Yesu; nao wakaogopa.+ 36 Wale waliokuwa wameona jambo hilo wakawaambia jinsi yule mtu aliyekuwa na roho waovu alivyokuwa ameponywa.+ 37 Kwa hiyo umati wote kutoka nchi yenye kuzunguka ya Wagerasene ukamwomba aondoke kwao, kwa sababu walikuwa wameshikwa na woga mkubwa.+ Ndipo akapanda ndani ya mashua na kurudi. 38 Hata hivyo, mwanamume ambaye roho waovu walikuwa wamemtoka akawa akimwomba akae pamoja naye; lakini akamwagiza mtu huyo aende, akisema:+ 39 “Ondoka urudi nyumbani, na uendelee kusimulia mambo ambayo Mungu amekutendea.”+ Basi akaenda zake, akatangaza kotekote katika jiji lote mambo ambayo Yesu alimtendea.+
40 Yesu aliporudi, umati ukampokea kwa fadhili, kwa maana wote walikuwa wakimtarajia.+ 41 Lakini, tazama! mwanamume anayeitwa Yairo akaja, na mtu huyu alikuwa ofisa-msimamizi wa sinagogi. Naye akajiangusha miguuni pa Yesu akaanza kumsihi aingie katika nyumba yake,+ 42 kwa sababu alikuwa na binti mzaliwa-pekee mwenye umri wa miaka karibu kumi na miwili na alikuwa anakufa.+
Alipokuwa akienda umati ukamsonga.+ 43 Na mwanamke, aliyekuwa na mtiririko wa damu+ kwa miaka kumi na miwili, ambaye hakuweza kupata ponyo kutoka kwa yeyote,+ 44 akamkaribia kutoka nyuma akaugusa upindo+ wa vazi lake la nje,+ na mtiririko wake wa damu ukaisha mara moja.+ 45 Kwa hiyo Yesu akasema: “Ni nani aliyenigusa?”+ Wote walipokuwa wakikana hilo, Petro akasema: “Mwalimu, umati unakuzunguka na kukusonga sana.”+ 46 Lakini Yesu akasema: “Mtu fulani amenigusa, kwa maana nilitambua kwamba nguvu+ zilinitoka.”+ 47 Alipoona kwamba hakuepuka kutambuliwa, mwanamke huyo akaja akitetemeka, akaanguka chini mbele yake na kufunua mbele ya watu wote sababu iliyomfanya amguse na jinsi alivyoponywa mara moja.+ 48 Lakini yeye akamwambia: “Binti yangu, imani yako imekuponya;+ nenda kwa amani.”+
49 Alipokuwa bado akisema, mwakilishi fulani wa ofisa-msimamizi wa sinagogi akaja, akisema: “Binti yako amekufa; usiendelee kumsumbua mwalimu.”+ 50 Aliposikia hilo, Yesu akamjibu: “Usiogope, uwe tu na imani,+ naye ataokolewa.” 51 Alipofika kwenye nyumba hiyo hakumruhusu yeyote aingie pamoja naye ila Petro na Yohana na Yakobo na baba na mama ya msichana huyo.+ 52 Lakini watu wote walikuwa wakilia na kujipiga-piga kwa huzuni kwa ajili yake. Kwa hiyo akasema: “Acheni kulia,+ kwa maana hakufa bali analala usingizi.”+ 53 Ndipo wakaanza kumcheka kwa dharau, kwa sababu walijua alikuwa amekufa.+ 54 Lakini akamshika mkono wake akamwita, akisema: “Msichana, inuka!”+ 55 Na roho+ yake ikarudi, naye akainuka+ mara moja, na Yesu akaagiza apewe kitu ale.+ 56 Basi, wazazi wake wakapigwa na bumbuazi; lakini akawaagiza wasimwambie yeyote lililokuwa limetukia.+
9 Ndipo akawaita pamoja wale kumi na wawili, akawapa nguvu na mamlaka juu ya roho wote waovu na za kuponya magonjwa.+ 2 Na kwa hiyo akawatuma kuhubiri ufalme wa Mungu na kuponya, 3 naye akawaambia: “Msichukue kitu chochote kwa ajili ya safari, wala fimbo wala mfuko wa chakula, wala mkate wala fedha; wala msiwe na mavazi mawili ya ndani.+ 4 Lakini popote mtakapoingia katika nyumba, kaeni humo na mwondoke humo.+ 5 Na popote ambapo watu hawawapokei ninyi, mnapoondoka katika jiji hilo+ yakung’uteni mavumbi kutoka miguuni penu ili kuwa ushahidi juu yao.”+ 6 Ndipo walipoanza kuondoka wakapita katika eneo hilo kutoka kijiji mpaka kijiji, wakitangaza habari njema na kuponya kila mahali.+
7 Sasa Herode mtawala wa wilaya akasikia juu ya mambo yote yaliyokuwa yakitukia, naye akafadhaika sana kwa sababu baadhi ya watu walikuwa wakisema kwamba Yohana alikuwa amefufuliwa kutoka kwa wafu,+ 8 lakini wengine kwamba Eliya alikuwa ameonekana, na bado wengine kwamba mtu fulani mmoja wa manabii wa kale alikuwa amefufuliwa. 9 Herode akasema: “Yohana nilimkata kichwa.+ Basi, ni nani huyu ambaye juu yake ninasikia mambo ya namna hiyo?” Kwa hiyo alikuwa akitafuta+ kumwona.
10 Na mitume waliporudi wakamsimulia mambo waliyokuwa wameyafanya.+ Ndipo akawachukua waambatane naye, nao wakaondoka kwenda faraghani+ na kuingia katika jiji linaloitwa Bethsaida. 11 Lakini umati ulipojua, ukamfuata. Naye akawapokea kwa fadhili na kuanza kuwaambia juu ya ufalme wa Mungu,+ naye akawaponya wale wanaohitaji kuponywa.+ 12 Ndipo mchana ukaanza kushuka. Wale kumi na wawili sasa wakaja na kumwambia: “Waambie umati waondoke, waende vijijini na upande wa mashambani wenye kuzunguka na kujipatia makao na wapate chakula, kwa sababu huku nje sisi tuko katika mahali pasipo na watu.”+ 13 Lakini akawaambia: “Ninyi wapeni chakula.”+ Wakasema: “Sisi hatuna kitu zaidi ya mikate mitano na samaki wawili,+ isipokuwa labda sisi wenyewe twende na kununua vyakula kwa ajili ya watu wote hawa.”+ 14 Kwa kweli, walikuwa karibu wanaume 5,000.+ Lakini akawaambia wanafunzi wake: “Waagizeni waketi kama kwenye milo, vikundi-vikundi vya karibu 50 kila kimoja.”+ 15 Nao wakafanya hivyo na kuwaketisha wote. 16 Ndipo akichukua ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akavibariki na kuvimega, akaanza kuwapa wanafunzi waviweke mbele ya umati.+ 17 Kwa hiyo wote wakala, wakashiba, na ziada waliyokuwa nayo ikaokotwa, vikapu kumi na viwili vya vipande.+
18 Baadaye, alipokuwa akisali peke yake, wanafunzi walimjia pamoja, naye akawauliza, akisema: “Umati unasema mimi ni nani?”+ 19 Wakajibu wakasema: “Yohana Mbatizaji; lakini wengine, Eliya, na wengine bado, kwamba mmoja wa manabii wa kale amefufuliwa.”+ 20 Ndipo akawaambia: “Ingawa hivyo, ninyi mnasema mimi ni nani?” Petro akajibu, akasema:+ “Kristo+ wa Mungu.” 21 Ndipo akawaagiza kwa kusisitiza wasimwambie mtu yeyote jambo hilo,+ 22 lakini akasema: “Mwana wa binadamu lazima apatwe na mateso mengi na kukataliwa na wanaume wazee na wakuu wa makuhani na waandishi, na kuuawa,+ na siku ya tatu afufuliwe.”+
23 Ndipo akaendelea kuwaambia wote: “Mtu yeyote akitaka kunifuata, na ajikane+ mwenyewe na kuuchukua mti wake wa mateso siku baada ya siku na kunifuata sikuzote.+ 24 Kwa maana yeyote yule anayetaka kuiokoa nafsi yake ataipoteza; lakini yeyote yule anayeipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ndiye atakayeiokoa.+ 25 Kwa kweli, mtu anapata faida gani ikiwa anaupata ulimwengu wote lakini aipoteze nafsi yake mwenyewe au apate hasara?+ 26 Kwa maana mtu yeyote yule atakayenionea aibu mimi na maneno yangu, Mwana wa binadamu atamwonea aibu mtu huyo atakapofika katika utukufu wake na ule wa Baba na wa malaika watakatifu.+ 27 Lakini ninawaambia ninyi kwa kweli, Kuna baadhi ya wale wanaosimama hapa ambao hawataonja kifo kamwe mpaka kwanza wauone ufalme wa Mungu.”+
28 Kwa kweli, karibu siku nane baada ya maneno hayo, aliambatana na Petro na Yohana na Yakobo wakapanda mlimani ili kusali.+ 29 Naye alipokuwa akisali sura ya uso+ wake ikawa tofauti na vazi lake likawa jeupe kwa kumetameta.+ 30 Pia, tazama! wanaume wawili walikuwa wakiongea naye, Musa na Eliya.+ 31 Hawa walitokea wakiwa na utukufu nao wakaanza kuongea juu ya kuondoka kwake ambako angetimiza huko Yerusalemu.+ 32 Sasa Petro na wale waliokuwa pamoja naye walikuwa wamelemewa na usingizi; lakini walipopata kuamka kabisa waliuona utukufu+ wake na wale wanaume wawili waliosimama pamoja naye. 33 Nao walipokuwa wakitengwa kutoka kwake, Petro akamwambia Yesu: “Mwalimu, ni vizuri kwetu kuwa hapa, kwa hiyo na tusimamishe mahema matatu, moja lako na moja la Musa na moja la Eliya,” naye hakuwa akitambua alilokuwa akisema.+ 34 Lakini alipokuwa akisema mambo haya wingu likatokea na kuanza kuwafunika. Walipokuwa wakiingia katika wingu, wakaogopa.+ 35 Na sauti ikatoka katika lile wingu,+ ikisema: “Huyu ni Mwanangu, ambaye amechaguliwa.+ Msikilizeni.”+ 36 Na ile sauti ilipokuwa ikitokea Yesu alionekana akiwa peke yake.+ Lakini wakaendelea kukaa kimya nao hawakumwambia yeyote siku hizo lolote kati ya mambo waliyoona.+
37 Siku iliyofuata, waliposhuka kutoka mlimani, umati mkubwa ulikutana naye.+ 38 Na, tazama! mwanamume mmoja akapaaza sauti kutoka katika umati, akisema: “Mwalimu, ninakuomba umtazame kidogo mwanangu, kwa sababu yeye ni mzaliwa-pekee+ wangu, 39 na, tazama! roho+ humchukua, na kwa ghafula yeye hupaaza sauti, na huyo roho humfanya agaegae pamoja na kutoa povu, naye hamwachi kabisa baada ya kumchubua. 40 Nami niliwaomba wanafunzi wako wamfukuze roho huyo, lakini hawakuweza.”+ 41 Yesu akajibu akasema: “Enyi kizazi kisicho na imani na kilichopotoka,+ nitaendelea kuwa pamoja nanyi na kuwavumilia ninyi mpaka wakati gani? Mlete hapa mwana wako.”+ 42 Lakini hata alipokuwa akikaribia, yule roho mwovu akamwangusha chini na kumfanya agaegae kwa nguvu nyingi. Hata hivyo, Yesu akamkemea yule roho mchafu na kumponya mvulana naye akamkabidhi baba yake.+ 43 Basi, wote wakaanza kustaajabishwa na nguvu+ kuu za Mungu.
Sasa walipokuwa wote wakistaajabia mambo yote aliyokuwa akifanya, akawaambia wanafunzi wake: 44 “Yawekeni maneno hayo katika masikio yenu, kwa maana Mwana wa binadamu atatiwa mikononi mwa watu.”+ 45 Lakini wao wakashindwa kuelewa maneno hayo. Kwa kweli, yalifichwa ili wasipate kuyafahamu, nao waliogopa kumuuliza juu ya maneno hayo.+
46 Ndipo wakaanza kujadiliana kati yao kuhusu ni nani angekuwa mkuu zaidi kati yao.+ 47 Yesu, akijua mawazo ya mioyo yao, akachukua mtoto mchanga, akamweka kando yake+ 48 na kuwaambia: “Yeyote yule anayempokea mtoto huyu mchanga kwa msingi wa jina langu ananipokea mimi pia, na yeyote anayenipokea, anampokea pia yule aliyenituma.+ Kwa maana anayejiendesha kama aliye mdogo+ zaidi kati yenu nyote ndiye aliye mkuu.”+
49 Yohana akajibu akasema: “Mwalimu, tulimwona mtu fulani akitoa roho waovu+ kwa kutumia jina lako nasi tukajaribu kumzuia,+ kwa sababu hafuatani nasi.”+ 50 Lakini Yesu akamwambia: “Msijaribu kumzuia, kwa maana yule ambaye hayuko kinyume chenu yuko upande wenu.”+
51 Sasa siku zilipokuwa zikikamilika ili yeye achukuliwe juu,+ aliukaza uso wake kwenda Yerusalemu. 52 Kwa hiyo akatuma wajumbe kumtangulia. Nao wakaenda na kuingia katika kijiji cha Wasamaria,+ kumfanyia matayarisho; 53 lakini hawakumpokea, kwa sababu uso wake ulikuwa umekazwa kwenda Yerusalemu.+ 54 Wanafunzi Yakobo na Yohana+ walipoona hilo wakasema: “Bwana, je, unataka tuuambie moto+ ushuke kutoka mbinguni na kuwaangamiza?” 55 Lakini akageuka akawakemea. 56 Basi wakaenda kwenye kijiji tofauti.
57 Sasa walipokuwa wakienda barabarani, mtu fulani akamwambia: “Nitakufuata popote ambapo utaenda.”+ 58 Naye Yesu akamwambia: “Mbweha wana mapango na ndege wa mbinguni wana viota, lakini Mwana wa binadamu hana mahali popote pa kulaza kichwa chake.”+ 59 Ndipo akamwambia mwingine: “Uwe mfuasi wangu.” Mtu huyo akasema: “Niruhusu kwanza niondoke nikamzike baba yangu.”+ 60 Lakini akamwambia: “Waache wafu+ wawazike wafu wao, lakini wewe nenda zako ukautangaze kotekote ufalme wa Mungu.”+ 61 Na bado mwingine akasema: “Nitakufuata, Bwana; lakini kwanza niruhusu niwaage+ watu wa nyumbani mwangu.” 62 Yesu akamwambia: “Hakuna mtu ambaye ameweka mkono wake kwenye jembe la ng’ombe+ na kutazama mambo yaliyo nyuma+ anayefaa kwa ajili ya ufalme wa Mungu.”
10 Baada ya mambo hayo Bwana akachagua wengine 70+ na kuwatuma wawili-wawili,+ wamtangulie kuingia katika kila jiji na mahali ambako yeye mwenyewe alikuwa aende. 2 Ndipo akaanza kuwaambia: “Kwa kweli, mavuno+ ni mengi, lakini wafanyakazi+ ni wachache. Kwa hiyo mwombeni+ Bwana wa mavuno atume wafanyakazi+ katika mavuno yake. 3 Nendeni. Tazama! Ninawatuma ninyi kama wana-kondoo+ katikati ya mbwa-mwitu. 4 Msichukue mkoba, wala mfuko+ wa chakula, wala viatu, nanyi msimkumbatie+ mtu yeyote mkimsalimu barabarani. 5 Popote pale mtakapoingia katika nyumba kwanza semeni, ‘Nyumba hii na iwe na amani.’+ 6 Na ikiwa rafiki wa amani yumo, amani yenu itakaa juu yake.+ Lakini ikiwa hayumo, itawarudia ninyi.+ 7 Kwa hiyo kaeni katika nyumba hiyo,+ mkila na kunywa vitu ambavyo wao wanaandaa,+ kwa maana mfanyakazi anastahili mshahara wake.+ Msiwe mkihama kutoka nyumba mpaka nyumba.+
8 “Pia, popote mtakapoingia katika jiji nao wawapokee, kuleni vitu vilivyowekwa mbele yenu, 9 na mwaponye+ wagonjwa walio humo, na kuendelea kuwaambia, ‘Ufalme+ wa Mungu umekuja karibu nanyi.’ 10 Lakini popote mtakapoingia katika jiji nao hawawapokei,+ tokeni mwende katika njia zake pana na kusema, 11 ‘Hata vumbi lililoshikamana na miguu yetu kutoka katika jiji lenu tunalifuta juu yenu.+ Hata hivyo, wekeni jambo hili akilini, kwamba ufalme wa Mungu umekaribia.’ 12 Ninawaambia ninyi kwamba itakuwa rahisi zaidi kwa Sodoma+ katika siku hiyo kuliko kwa jiji hilo.
13 “Ole wako, Korazini!+ Ole wako, Bethsaida!+ kwa sababu kama zile kazi zenye nguvu ambazo zimetendeka kwenu zingalikuwa zimetendeka katika Tiro na Sidoni, wangalikuwa wametubu zamani za kale wakiwa wameketi katika nguo za magunia na majivu.+ 14 Kwa sababu hiyo itakuwa rahisi zaidi kwa Tiro na Sidoni katika hukumu kuliko kwenu.+ 15 Na wewe, Kapernaumu, je, labda utainuliwa mpaka mbinguni?+ Utashuka chini mpaka katika Kaburi!*+
16 “Yeye anayewasikiliza+ ninyi ananisikiliza mimi pia. Naye anayewapuuza ninyi ananipuuza mimi pia. Zaidi ya hayo, yeye anayenipuuza+ mimi anampuuza pia yule aliyenituma.”
17 Ndipo wale 70 wakarudi wakiwa na shangwe, wakisema: “Bwana, hata roho waovu wanatiishwa+ kwetu kwa kutumia jina lako.” 18 Ndipo akawaambia: “Nilianza kumwona Shetani akiwa tayari ameanguka+ kama umeme kutoka mbinguni. 19 Tazama! Nimewapa ninyi mamlaka ya kukanyaga-kanyaga nyoka+ na nge,+ na juu ya nguvu zote za adui,+ na hakuna kitu kitakachowaumiza ninyi kamwe. 20 Hata hivyo, msishangilie juu ya hili, kwamba roho wanatiishwa kwenu, bali shangilieni kwa sababu majina+ yenu yameandikwa mbinguni.” 21 Katika saa ileile akawa na shangwe+ sana katika roho takatifu, akasema: “Ninakusifu hadharani wewe, Baba, Bwana wa mbingu na dunia, kwa sababu umewaficha kwa uangalifu wenye hekima+ na walio na akili mambo hayo, nawe umeyafunua kwa watoto. Ndiyo, Ee Baba, kwa sababu kufanya hivyo kulikuja kuwa njia inayokubaliwa na wewe. 22 Baba yangu amevitia+ vitu vyote mkononi mwangu, na hakuna anayemjua Mwana ni nani ila Baba;+ na hakuna anayemjua Baba ni nani ila Mwana,+ na yule ambaye Mwana anapenda kumfunulia.”
23 Ndipo akawageukia wanafunzi wakiwa peke yao na kusema: “Yenye furaha ni macho yanayoona mambo ambayo ninyi mnayaona.+ 24 Kwa maana ninawaambia ninyi, Manabii na wafalme wengi walitamani kuyaona+ mambo ambayo ninyi mnayaona lakini hawakuyaona, na kuyasikia mambo ambayo ninyi mnayasikia lakini hawakuyasikia.”
25 Sasa, tazama! mtu fulani mwenye ujuzi mwingi wa Sheria+ akasimama, ili kumjaribu, akasema: “Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?”+ 26 Akamwambia: “Ni mambo gani yameandikwa katika Sheria?+ Wewe unasomaje?” 27 Akajibu, akasema: “ ‘Lazima umpende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa nguvu zako zote na kwa akili+ yako yote,’ na, ‘jirani yako kama wewe mwenyewe.’ ”+ 28 Akamwambia: “Umejibu kwa usahihi; ‘endelea kufanya hivyo nawe utapata uzima.’ ”+
29 Lakini, akitaka kujionyesha kuwa mwadilifu, mtu huyo akamwambia Yesu: “Ni nani kwa kweli aliye jirani yangu?”+ 30 Yesu akajibu akasema: “Mtu fulani alikuwa akishuka kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko akaanguka katikati ya wanyang’anyi, ambao walimvua nguo na pia kumpiga, kisha wakaenda zao, wakamwacha karibu kufa. 31 Sasa, ikatukia kwamba, kuhani fulani alikuwa akishuka katika barabara hiyo, lakini, alipomwona, akapita upande ule mwingine.+ 32 Vivyo hivyo, Mlawi pia, alipofika chini katika mahali hapo na kumwona, akapita kando upande wa pili.+ 33 Lakini Msamaria+ fulani aliyekuwa akisafiri katika barabara ile alikuja, akamkuta na, alipomwona, akamsikitikia. 34 Kwa hiyo akamkaribia akayafunga majeraha yake, na kumwaga mafuta na divai juu yake.+ Kisha akampandisha juu ya mnyama wake mwenyewe akamleta kwenye nyumba ya wageni na kumtunza. 35 Na siku iliyofuata akatoa dinari mbili, akampa hizo mtu aliyekuwa akitunza nyumba hiyo ya wageni, na kusema, ‘Mtunze, na chochote utakachotumia mbali na hiki, mimi nitakulipa nitakaporudi hapa.’ 36 Ni nani kati ya watu hao watatu anayeonekana kwako kuwa alijifanya kuwa jirani+ kwa mtu aliyeanguka katikati ya wanyang’anyi?” 37 Akasema: “Ni yule aliyemtendea kwa rehema.”+ Ndipo Yesu akamwambia: “Nenda, na uwe ukifanya+ vivyo hivyo.”
38 Basi walipokuwa wameenda aliingia katika kijiji fulani. Hapa mwanamke fulani aliyeitwa Martha+ alimkaribisha nyumbani. 39 Mwanamke huyu alikuwa pia na dada aliyeitwa Maria, ambaye, hata hivyo, aliketi miguuni+ pa Bwana na kuendelea kulisikiliza neno lake. 40 Martha naye alikengeushwa+ na kazi nyingi. Kwa hiyo, akaja karibu na kusema: “Bwana, hujali kwamba dada yangu ameniacha peke yangu kushughulikia mambo?+ Kwa hiyo, mwambie aje anisaidie.” 41 Bwana akamjibu akamwambia: “Martha, Martha, wewe unahangaika+ na kusumbuka juu ya mambo mengi.+ 42 Ingawa hivyo, mambo machache+ ndiyo yanayohitajiwa, au moja tu. Yeye, Maria alichagua fungu jema,+ nalo halitaondolewa kwake.”
11 Sasa wakati alipokuwa mahali fulani akisali, alipoacha, mmoja wa wanafunzi wake akamwambia: “Bwana, tufundishe jinsi ya kusali,+ kama vile Yohana pia alivyowafundisha wanafunzi wake.”+
2 Ndipo akawaambia: “Wakati wowote mnaposali,+ semeni, ‘Baba, jina lako na litakaswe.+ Ufalme wako na uje.+ 3 Utupe mkate+ wetu kwa ajili ya siku kulingana na mahitaji ya siku hiyo. 4 Na utusamehe dhambi zetu,+ kwa maana sisi wenyewe pia humsamehe kila mtu aliye na deni letu;+ na usituingize katika jaribu.’ ”+
5 Tena akawaambia: “Ni nani kati yenu aliye na rafiki naye amwendee katikati ya usiku na kumwambia, ‘Rafiki, nikopeshe mikate mitatu, 6 kwa sababu rafiki yangu amenijia sasa hivi kutoka safarini nami sina kitu cha kuweka mbele yake’? 7 Na huyo aliye ndani ajibu na kusema, ‘Acha kunisumbua.+ Tayari mlango umefungwa, na watoto wangu wachanga wako pamoja nami kitandani; siwezi kuamka nikupe chochote.’ 8 Ninawaambia ninyi, Ijapokuwa hataamka ampe chochote kwa sababu ya kuwa rafiki yake, hakika kwa sababu ya kudumu kwake kwa ujasiri,+ ataamka na kumpa vitu anavyohitaji. 9 Basi ninawaambia ninyi, Endeleeni kuomba,+ nanyi mtapewa; endeleeni kutafuta,+ nanyi mtapata; endeleeni kupiga hodi, nanyi mtafunguliwa. 10 Kwa maana kila mtu anayeomba hupokea,+ na kila mtu anayetafuta hupata, na kila mtu anayepiga hodi hufunguliwa. 11 Kwa kweli, ni baba gani kati yenu ambaye, ikiwa mwana+ wake anaomba samaki, labda atampa nyoka badala ya samaki? 12 Au ikiwa pia anaomba yai, atampa nge? 13 Kwa hiyo, ikiwa ninyi, mjapokuwa waovu, mnajua jinsi ya kuwapa watoto+ wenu zawadi zilizo njema, je, Baba aliye mbinguni hatawapa hata zaidi roho takatifu+ wale wanaomwomba!”
14 Baadaye alikuwa akifukuza roho mwovu aliye bubu.+ Baada ya roho huyo mwovu kutoka, yule bubu akazungumza. Nao umati wakastaajabu. 15 Lakini watu fulani kati yao wakasema: “Yeye huwafukuza roho waovu kupitia Beelzebuli mtawala wa roho waovu.”+ 16 Hata hivyo, wengine, ili kumjaribu, wakaanza kutafuta kwake ishara+ kutoka mbinguni. 17 Akijua mawazo+ yao akawaambia: “Kila ufalme uliogawanyika juu yake wenyewe hufanywa ukiwa, na nyumba iliyogawanyika juu yake yenyewe huanguka.+ 18 Kwa hiyo ikiwa Shetani pia amegawanyika juu yake mwenyewe, ufalme wake utasimamaje?+ Kwa sababu ninyi mnasema mimi hufukuza roho waovu kupitia Beelzebuli. 19 Ikiwa ni kupitia Beelzebuli mimi hufukuza roho waovu, wana+ wenu huwafukuza kupitia nani? Kwa hiyo wao watakuwa waamuzi wenu. 20 Lakini ikiwa mimi huwafukuza roho waovu kupitia kidole+ cha Mungu, ufalme wa Mungu kwa kweli umewafikia.+ 21 Wakati mtu mwenye nguvu,+ mwenye silaha za kutosha, anapolinda jumba lake, mali zake hukaa kwa amani. 22 Lakini mtu fulani mwenye nguvu+ zaidi yake anapokuja juu yake na kumshinda,+ yeye huchukua silaha zake zote alizokuwa akitegemea, naye hugawanya vitu ambavyo yeye alimpora. 23 Yule ambaye hayuko upande wangu ananipinga, na yule ambaye hakusanyi pamoja nami anatawanya.+
24 “Wakati roho mchafu anapomtoka mtu, hupita katika mahali palipokauka akitafuta mahali pa kupumzika, na, baada ya kukosa, husema, ‘Nitarudi kwenye nyumba yangu niliyoihama.’+ 25 Naye anapofika huikuta ikiwa imefagiliwa ikawa safi na kupambwa. 26 Ndipo huyo huenda na kuchukua roho saba+ tofauti walio waovu kuliko yeye mwenyewe waambatane naye, na, baada ya kuingia ndani, wao hukaa humo; na hali ya mwisho ya mtu huyo huwa mbaya zaidi kuliko ile ya kwanza.”+
27 Sasa alipokuwa akisema hayo mwanamke fulani katika umati akainua sauti yake akamwambia: “Lenye furaha ni tumbo la uzazi+ lililokuchukua wewe na maziwa uliyonyonya!” 28 Lakini akasema: “Hapana, badala yake, Wenye furaha ni wale wanaolisikia neno la Mungu na kulishika!”+
29 Umati walipokuwa wakisongamana pamoja, akaanza kusema: “Kizazi hiki ni kizazi kiovu; kinatafuta ishara.+ Lakini hakuna ishara ambayo kitapewa ila ishara ya Yona.+ 30 Kwa maana kama vile Yona+ alivyokuwa ishara kwa Waninawi, ndivyo Mwana wa binadamu atakavyokuwa pia kwa kizazi hiki. 31 Malkia+ wa kusini atasimamishwa katika hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki naye atawahukumu kuwa wenye hatia; kwa sababu yeye alikuja kutoka miisho ya dunia ili aisikie hekima ya Sulemani, lakini, tazameni! Aliye mkuu+ kuliko Sulemani yupo hapa. 32 Watu wa Ninawi watasimama katika hukumu pamoja na kizazi hiki nao watakilaumu; kwa maana walitubu kutokana na mahubiri ya Yona;+ lakini, tazameni! Aliye mkuu+ kuliko Yona yupo hapa. 33 Baada ya kuwasha taa, mtu huiweka, si katika ghala wala chini ya kikapu cha kupimia, bali juu ya kinara cha taa,+ ili wale wanaoingia ndani wapate kuiona nuru. 34 Taa ya mwili ni jicho lako. Jicho lako linapokuwa rahisi, mwili wako wote huwa mwangavu+ pia; lakini linapokuwa bovu, mwili wako huwa na giza pia. 35 Kwa hiyo, ukae macho. Labda nuru iliyo ndani yako ni giza.+ 36 Kwa hiyo, ikiwa mwili wako wote ni mwangavu bila sehemu yenye giza hata kidogo, wote utakuwa mwangavu+ kama wakati ambapo taa inakupa nuru kwa miale yake.”
37 Baada ya kusema hayo, Farisayo mmoja akamwomba ale+ pamoja naye. Kwa hiyo akaingia na kuketi mezani. 38 Hata hivyo, Farisayo huyo akashangaa kuona kwamba hakunawa+ kwanza kabla ya chakula hicho. 39 Lakini Bwana akamwambia: “Sasa ninyi Mafarisayo, husafisha upande wa nje wa kikombe na sahani, lakini upande wenu wa ndani+ umejaa uporaji na uovu.+ 40 Ninyi watu msio na akili! Yule aliyeufanya upande wa nje+ aliufanya upande wa ndani pia, sivyo? 41 Hata hivyo, vitoeni viwe kama zawadi za rehema+ vitu vilivyo ndani, na, tazama! vitu vingine vyote ni safi kuwahusu ninyi. 42 Lakini ole wenu ninyi Mafarisayo, kwa sababu ninyi hutoa sehemu ya kumi+ ya mnanaa na mchicha na ya kila mboga nyingine za majani, lakini ninyi hupuuza haki na upendo kwa Mungu! Mambo hayo mlikuwa na wajibu wa kuyafanya, na bado kutoyaacha yale mengine.+ 43 Ole wenu ninyi Mafarisayo, kwa sababu ninyi hupenda viti vya mbele katika masinagogi na salamu katika masoko!+ 44 Ole wenu, kwa sababu ninyi ni kama makaburi yasiyoonekana, hivi kwamba watu hutembea juu yake nao hawajui!”+
45 Mtu fulani kati ya wale wenye ujuzi mwingi+ wa Sheria akajibu, akamwambia: “Mwalimu, kwa kusema mambo hayo unatutusi pia.” 46 Ndipo akasema: “Ole wenu pia ninyi mlio na ujuzi mwingi wa Sheria, kwa sababu ninyi huwatwika watu mizigo iliyo mizito kubebwa, lakini ninyi wenyewe hamwigusi mizigo hiyo kwa kimoja cha vidole vyenu!+
47 “Ole wenu ninyi, kwa sababu ninyi huyajenga makaburi ya manabii, lakini mababu zenu waliwaua!+ 48 Hakika ninyi ni mashahidi wa matendo ya mababu zenu na bado ninyi mnawapa kibali,+ kwa sababu hao waliwaua+ manabii lakini ninyi mnayajenga makaburi yao. 49 Kwa ajili ya hili hekima+ ya Mungu ilisema pia, ‘Nitatuma kwao manabii na mitume, nao watawaua na kuwatesa baadhi yao, 50 ili damu ya manabii+ wote iliyomwagwa tangu kuwekwa msingi wa ulimwengu ipate kudaiwa kutoka kwa kizazi+ hiki, 51 tangu damu ya Abeli+ mpaka damu ya Zekaria,+ aliyeuawa katikati ya madhabahu na ile nyumba.’+ Ndiyo, ninawaambia ninyi, itadaiwa kutoka kwa kizazi hiki.
52 “Ole wenu ninyi wenye ujuzi mwingi wa Sheria, kwa sababu mliuondoa ufunguo wa ujuzi;+ ninyi wenyewe hamkuingia, na wale wanaoingia mliwazuia!”+
53 Basi alipotoka hapo waandishi na Mafarisayo wakaanza kumsonga sana na kumuuliza maswali juu ya mambo zaidi, 54 wakimtega,+ ili wapate+ kitu fulani kutoka kinywani mwake.
12 Wakati huohuo, umati walipokuwa wamekusanyika pamoja kwa maelfu mengi sana hivi kwamba walikuwa wakikanyagana, akaanza kwa kuwaambia kwanza wanafunzi wake: “Jihadharini na chachu+ ya Mafarisayo, ambayo ni unafiki.+ 2 Lakini hakuna kitu kilichofunikwa kwa uangalifu ambacho hakitafunuliwa, na cha siri ambacho hakitajulikana.+ 3 Kwa sababu hiyo mambo mnayosema gizani yatasikiwa nuruni, na mnalonong’ona katika vyumba vya faragha litahubiriwa kutoka katika paa za nyumba.+ 4 Zaidi ya hayo, ninawaambia ninyi, rafiki zangu,+ Msiwaogope wale wanaouua mwili na baada ya hilo hawawezi kufanya jambo lolote zaidi.+ 5 Lakini nitawaonyesha ninyi yule mnayepaswa kumwogopa: Mwogopeni yule+ ambaye baada ya kuua ana mamlaka ya kutupa ndani ya Gehena.*+ Ndiyo, ninawaambia ninyi, Mwogopeni+ Huyo. 6 Shore watano huuzwa kwa sarafu mbili za thamani ndogo, sivyo? Na bado hakuna hata mmoja wao husahaulika mbele za Mungu.+ 7 Lakini hata nywele+ za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. Msiogope; ninyi ni wenye thamani kuliko shore wengi.+
8 “Basi, ninawaambia ninyi, Kila mtu anayekiri+ kuwa pamoja nami mbele ya wanadamu, Mwana wa binadamu atakiri pia kuwa pamoja naye mbele ya malaika za Mungu.+ 9 Lakini yule anayenikana+ mbele ya wanadamu atakanwa mbele ya malaika za Mungu.+ 10 Na kila mtu anayesema neno baya juu ya Mwana wa binadamu, atasamehewa; lakini yule anayekufuru roho takatifu hatasamehewa.+ 11 Lakini watakapowapeleka mbele ya makusanyiko ya watu wote na maofisa wa serikali na mamlaka, msihangaikie jinsi au jambo mtakalojitetea nalo au jambo mtakalosema;+ 12 kwa maana roho takatifu+ itawafundisha ninyi saa ileile mambo mnayopaswa kusema.”+
13 Ndipo mtu fulani kati ya umati akamwambia: “Mwalimu, mwambie ndugu yangu tugawane urithi.” 14 Akamwambia: “Wewe mtu, nani aliyeniweka mimi kuwa mwamuzi+ au mgawaji juu yenu?” 15 Ndipo akawaambia: “Endeleeni kufungua macho yenu na mjilinde na kila namna ya tamaa,+ kwa sababu hata wakati mtu ana vitu vingi uzima wake hautokani na vitu alivyo navyo.”+ 16 Ndipo akawaambia mfano, akisema: “Shamba la mtu fulani tajiri lilizaa vizuri. 17 Kwa sababu hiyo akaanza kuwaza ndani yake mwenyewe, akisema, ‘Nitafanya nini, sasa kwa kuwa sina mahali popote pa kukusanya mazao yangu?’ 18 Kwa hiyo akasema, ‘Nitafanya hivi:+ Nitabomoa maghala yangu na kujenga yaliyo makubwa zaidi, na humo nitakusanya nafaka yangu yote na vitu vyangu vyema vyote;+ 19 nami nitaiambia+ nafsi yangu: “Nafsi yangu, una vitu vyema vingi vilivyokusanywa kwa miaka mingi; starehe, ule, unywe, na kujifurahisha.” ’+ 20 Lakini Mungu akamwambia, ‘Wewe usiye na akili, usiku huu wanadai nafsi yako kutoka kwako.+ Basi, vitu ulivyoviweka akiba vitakuwa vya nani?’+ 21 Hivyo ndivyo huwa kwa mtu anayejikusanyia mwenyewe hazina lakini si tajiri kwa Mungu.”+
22 Ndipo akawaambia wanafunzi wake: “Kwa sababu hiyo ninawaambia ninyi, Acheni kuhangaikia nafsi zenu kuhusu mtakachokula au miili yenu kuhusu mtakachovaa.+ 23 Kwa maana nafsi ina thamani kuliko chakula na mwili kuliko mavazi. 24 Angalieni kwamba kunguru+ hawapandi mbegu wala hawavuni, nao hawana bohari wala ghala, na bado Mungu huwalisha. Ninyi ni wenye thamani kama nini kuliko ndege?+ 25 Ni nani kati yenu ambaye kwa kuhangaika, anaweza kuongeza kipimo cha mkono mmoja kwenye uhai wake?+ 26 Kwa hiyo, ikiwa ninyi hamwezi kufanya jambo dogo zaidi, kwa nini mhangaikie+ mambo yaliyobaki? 27 Angalieni jinsi mayungiyungi hukua;+ hayo hayafanyi kazi wala hayasokoti; lakini ninawaambia ninyi, Hata Sulemani katika utukufu wake wote hakupambwa kama moja kati ya hayo.+ 28 Ikiwa, basi, Mungu huvika hivyo mimea iliyo shambani ambayo leo ipo na kesho hutupwa ndani ya jiko, basi atawavika ninyi hata zaidi, ninyi wenye imani kidogo!+ 29 Kwa hiyo acheni kutafuta mnachoweza kula na mnachoweza kunywa, na acheni kuhangaika kwa wasiwasi;+ 30 kwa maana mataifa ya ulimwengu yanafuatilia kwa bidii mambo yote hayo, lakini Baba yenu anajua mnahitaji mambo hayo.+ 31 Hata hivyo, utafuteni ufalme wake sikuzote, na mambo hayo mtaongezewa.+
32 “Msiogope,+ kundi dogo,+ kwa sababu Baba yenu amekubali kuwapa ninyi ufalme.+ 33 Uzeni+ mali yenu na mtoe zawadi za rehema.+ Jifanyieni wenyewe mikoba ambayo haichakai, hazina isiyopungua kamwe katika mbingu,+ ambapo mwizi hakaribii wala nondo hali. 34 Kwa maana mahali ilipo hazina yenu, hapo pia mioyo yenu itakuwapo.+
35 “Viuno+ vyenu na vifungwe mishipi na taa+ zenu ziwe zikiwaka, 36 nanyi mtakuwa kama watu wanaomngoja bwana+ wao wakati anaporudi kutoka kwenye karamu ya ndoa,+ ili atakapofika+ na kupiga hodi wapate kumfungulia mara moja. 37 Wenye furaha ni watumwa ambao bwana anapofika anawakuta wakikesha!+ Kwa kweli ninawaambia ninyi, Yeye atajifunga+ na kuwaketisha mezani naye atakuja kando na kuwahudumia.+ 38 Naye akifika katika kesha la pili, hata ikiwa ni katika la tatu, na anawakuta hivyo, wenye furaha ni wao!+ 39 Lakini jueni hili, kwamba ikiwa mwenye nyumba angejua mwizi atakuja saa ngapi, angeendelea kukesha naye hangeacha nyumba yake ivunjwe.+ 40 Ninyi pia, endeleeni kuwa tayari, kwa sababu Mwana wa binadamu atakuja katika saa msiyoitazamia.”+
41 Ndipo Petro akasema: “Bwana, unatuambia mfano huu sisi au wote pia?” 42 Naye Bwana akasema: “Ni nani kwa kweli aliye msimamizi-nyumba mwaminifu,+ mwenye busara,+ ambaye bwana wake atamweka rasmi juu ya watumishi wake kuendelea kuwapa kipimo chao cha chakula katika wakati unaofaa?+ 43 Mwenye furaha ni mtumwa huyo, ikiwa bwana wake anapofika anamkuta akifanya hivyo!+ 44 Ninawaambia ninyi kwa kweli, Yeye atamweka rasmi juu ya mali zake zote.+ 45 Lakini ikiwa wakati wowote mtumwa huyo atasema moyoni mwake, ‘Bwana wangu anakawia kuja,’+ naye aanze kuwapiga watumishi na vijakazi, na kula na kunywa na kulewa,+ 46 bwana wa mtumwa huyo atakuja siku ambayo hamtazamii na saa ambayo hajui,+ naye atamwadhibu kwa ukali ulio mkubwa zaidi na kumgawia sehemu pamoja na wale wasio waaminifu.+ 47 Ndipo mtumwa huyo aliyeelewa mapenzi ya bwana wake lakini hakujitayarisha au kufanya kulingana na mapenzi yake atapigwa mapigo mengi.+ 48 Lakini yule ambaye hakuelewa+ na kwa hiyo akafanya mambo yanayostahili mapigo atapigwa machache.+ Kwa kweli, kila mtu ambaye alipewa mengi, atadaiwa+ mengi; na yule ambaye watu wamemweka asimamie mengi, watamdai mengi zaidi kutoka kwake kuliko ilivyo kawaida.+
49 “Nilikuja kuwasha moto+ juu ya dunia, na mimi nitake nini zaidi ikiwa tayari umewaka? 50 Kwa kweli, nina ubatizo wa kubatizwa, na jinsi ninavyotaabika mpaka umalizike!+ 51 Je, mnafikiri nilikuja kuleta amani duniani? Ninawaambia ninyi, kwa kweli, hapana, bali badala yake mgawanyiko.+ 52 Kwa maana tangu sasa na kuendelea kutakuwa na watano katika nyumba moja waliogawanyika, watatu dhidi ya wawili na wawili dhidi ya watatu.+ 53 Watagawanyika, baba dhidi ya mwana, mwana dhidi ya baba, mama dhidi ya binti, binti dhidi ya mama yake, mama-mkwe dhidi ya binti-mkwe wake na binti-mkwe dhidi ya mama-mkwe wake.”+
54 Ndipo akaendelea kuuambia pia umati: “Mnapoona wingu likizuka katika sehemu za magharibi, mara moja ninyi husema, ‘Dhoruba inakuja,’ na huwa hivyo.+ 55 Nanyi mnapoona kwamba upepo wa kusini unavuma, ninyi husema, ‘Kutakuwa na wimbi la joto,’ na hutukia. 56 Wanafiki, mnajua jinsi ya kuchunguza kuonekana kwa dunia na anga, lakini inawezekanaje hamjui jinsi ya kuuchunguza wakati huu maalumu?+ 57 Kwa nini hamjiamulii wenyewe pia yaliyo ya uadilifu?+ 58 Kwa mfano, wakati unapoenda kwa mtawala pamoja na mshitaki wako, anza kazi, mkiwa njiani, kujiondolea mwenyewe ubishi pamoja naye, ili asikukokote mpaka mbele ya hakimu, naye hakimu akukabidhi kwa ofisa wa mahakama, na ofisa wa mahakama akutupe gerezani.+ 59 Ninakuambia, Hutatoka humo mpaka umalize kulipa sarafu ndogo ya mwisho yenye thamani ndogo sana.”+
13 Katika majira hayo kulikuwa na watu fulani waliomletea habari juu ya Wagalilaya+ ambao Pilato alikuwa amechanganya damu yao pamoja na dhabihu zao. 2 Kwa hiyo akajibu, akawaambia: “Je, mnafikiri kwamba Wagalilaya hao walikuwa watenda-dhambi+ wabaya zaidi kuliko Wagalilaya wengine wote kwa sababu wamepatwa na mambo hayo? 3 Ninawaambia ninyi, kwa kweli, hapana; lakini, msipotubu, nyote mtaangamizwa vivyo hivyo.+ 4 Au wale kumi na wanane ambao mnara katika Siloamu uliwaangukia, na kuwaua, je, mnafikiri kwamba walikuwa na deni kubwa zaidi kuliko watu wengine wote waliokuwa wakikaa Yerusalemu? 5 Ninawaambia ninyi, kwa kweli, hapana; lakini, msipotubu, ninyi nyote mtaangamizwa vivyo hivyo.”+
6 Ndipo akaendelea kutoa mfano huu: “Mtu fulani alikuwa na mtini umepandwa katika shamba lake la mizabibu,+ naye akaja akitafuta matunda juu yake,+ lakini hakupata yoyote.+ 7 Ndipo akamwambia mtunza-mizabibu, ‘Kwa miaka mitatu+ sasa nimekuwa nikija kutafuta matunda juu ya mtini huu, lakini sijapata yoyote. Ukate!+ Kwa nini huo uufanye udongo ukae bure?’ 8 Akajibu akamwambia, ‘Bwana, uache+ mwaka huu pia, mpaka niupalilie na kuweka mbolea; 9 na ndipo ukizaa matunda wakati ujao, basi ni vema; lakini ikiwa sivyo, utaukata.’ ”+
10 Basi alikuwa akifundisha katika moja la masinagogi siku ya sabato. 11 Na, tazama! mwanamke mwenye roho+ ya udhaifu kwa miaka kumi na minane, naye alikuwa amepindika vibaya na alikuwa hawezi kusimama wima kamwe. 12 Alipomwona mwanamke huyo, Yesu alisema naye na kumwambia: “Mwanamke, umefunguliwa+ kutoka udhaifu wako.” 13 Naye akaweka mikono yake juu ya mwanamke huyo; naye akanyooka+ mara moja, akaanza kumtukuza Mungu. 14 Lakini ofisa-msimamizi wa sinagogi, akiwa ameghadhibika kwa sababu Yesu alimponya siku ya sabato, akajibu na kuanza kuuambia umati: “Kuna siku sita ambapo kazi inapaswa kufanywa;+ kwa hiyo, njooni mponywe katika siku hizo, wala si siku ya sabato.”+ 15 Hata hivyo, Bwana akamjibu na kusema: “Wanafiki,+ je, kila mmoja wenu siku ya sabato hafungui ng’ombe wake au punda wake kutoka kwenye kibanda na kumpeleka akamnyweshe?+ 16 Basi, je, haikuwa haki mwanamke huyu aliye binti ya Abrahamu,+ na ambaye Shetani alikuwa amemfunga, tazama! miaka kumi na minane, afunguliwe kutoka kwenye kifungo hiki siku ya sabato?” 17 Basi, aliposema mambo hayo, wote waliokuwa wakimpinga wakaanza kuona aibu;+ lakini umati wote wakaanza kuyashangilia mambo matukufu yote aliyofanya.+
18 Kwa hiyo akaendelea kusema: “Ufalme wa Mungu ni kama nini, nami nitaulinganisha na nini?+ 19 Ni kama mbegu ya haradali ambayo mtu alichukua akaiweka katika bustani yake, nayo ikakua ikawa mti, nao ndege wa mbinguni+ wakapata makao katika matawi yake.”+
20 Naye tena akasema: “Nitaulinganisha ufalme wa Mungu na nini? 21 Ni kama chachu, ambayo mwanamke alichukua na kuitia katika vipimo vikubwa vitatu vya unga mpaka tonge lote lilipochacha.”+
22 Naye akasafiri kutoka jiji mpaka jiji na kutoka kijiji mpaka kijiji, akifundisha na kuendelea katika safari yake mpaka Yerusalemu.+ 23 Sasa mtu fulani akamwambia: “Bwana, je, wale wanaookolewa ni wachache?”+ Akawaambia: 24 “Jitahidini+ sana ili mwingie kupitia mlango mwembamba,+ kwa sababu wengi, ninawaambia ninyi, watajaribu kuingia lakini hawataweza,+ 25 wakati mwenye nyumba anapomaliza kusimama na kuufunga mlango, nanyi mnaanza kusimama nje na kupiga hodi mlangoni, mkisema, ‘Bwana, tufungulie.’+ Lakini atawajibu na kuwaambia ninyi, ‘Sijui mnatoka wapi.’+ 26 Ndipo mtakapoanza kusema, ‘Tulikula na kunywa mbele yako, na wewe ulifundisha katika njia zetu pana.’+ 27 Lakini atasema na kuwaambia ninyi, ‘Sijui mnatoka wapi. Ondokeni kwangu, ninyi nyote mnaotenda ukosefu wa uadilifu!’+ 28 Hapo ndipo mtalia na kusaga meno yenu,+ wakati mtakapomwona Abrahamu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu,+ lakini ninyi wenyewe mkiwa mmetupwa nje. 29 Zaidi ya hayo, watu watakuja kutoka sehemu za mashariki na za magharibi, na kutoka kaskazini na kusini,+ nao wataketi mezani katika ufalme wa Mungu.+ 30 Na, tazama! kuna wale wa mwisho watakaokuwa wa kwanza, na kuna wale wa kwanza watakaokuwa wa mwisho.”+
31 Saa ileile Mafarisayo fulani wakaja, wakimwambia: “Toka hapa uende zako, kwa sababu Herode anataka kukuua.” 32 Naye akawaambia: “Nendeni mkamwambie mbweha+ huyo, ‘Tazama! Mimi ninatoa roho waovu na kuponya leo na kesho, na siku ya tatu nitakuwa nimemaliza.’+ 33 Hata hivyo, lazima niende zangu leo na kesho na siku inayofuata, kwa sababu haikubaliki nabii kuangamizwa nje ya Yerusalemu.+ 34 Yerusalemu, Yerusalemu, muuaji+ wa manabii na anayewapiga kwa mawe+ hao waliotumwa kwake—ni mara ngapi nilitaka kuwakusanya watoto wako pamoja kama vile ambavyo kuku hukusanya vifaranga chini ya mabawa yake,+ lakini ninyi hamkutaka!+ 35 Tazama! Nyumba+ yenu mmeachiwa hali ya ukiwa. Ninawaambia, Ninyi hamtaniona kamwe mpaka mtakaposema, ‘Aliyebarikiwa ni yule anayekuja katika jina la Yehova!’ ”+
14 Na pindi fulani alipoingia ndani ya nyumba ya mtu fulani, mmoja kati ya watawala wa Mafarisayo katika siku ya sabato ili kula mlo,+ walikuwa wakimchunguza sana.+ 2 Na, tazama! mbele yake kulikuwa na mtu fulani aliyekuwa na ugonjwa unaosababisha mwili kuvimba. 3 Kwa hiyo Yesu akajibu, akawaambia wale wenye ujuzi mwingi katika Sheria na Mafarisayo, akisema: “Je, ni halali kuponya katika siku ya sabato au sivyo?”+ 4 Lakini wakakaa kimya. Ndipo akamshika mtu huyo, akamponya na kumwacha aende zake. 5 Naye akawaambia: “Ni nani kati yenu, ambaye mwana wake au ng’ombe wake akianguka ndani ya kisima,+ hatamtoa nje mara moja katika siku ya sabato?”+ 6 Nao hawakuweza kumjibu juu ya mambo hayo.+
7 Ndipo akaendelea kuwaambia mfano wale watu walioalikwa, kwa kuwa aliangalia jinsi walivyokuwa wakijichagulia wenyewe mahali penye kuonekana zaidi, akawaambia:+ 8 “Unapoalikwa na mtu fulani kwenye karamu ya ndoa, usiketi mahali penye kuonekana zaidi.+ Huenda wakati huo akawa amemwalika mtu fulani mashuhuri kuliko wewe, 9 naye aliyekualika wewe na yeye, atakuja na kukuambia, ‘Acha mtu huyu aketi mahali hapo.’ Ndipo utakapoanza kuondoka kwa aibu na kuketi mahali pa chini zaidi.+ 10 Lakini unapoalikwa, nenda ukaketi mahali pa chini zaidi,+ ili mtu ambaye amekualika atakapokuja akuambie, ‘Rafiki, nenda juu zaidi.’ Ndipo utakapokuwa na heshima mbele ya wageni wenzako wote walioalikwa.+ 11 Kwa maana kila mtu anayejiinua atanyenyekezwa na yule anayejinyenyekeza atainuliwa.”+
12 Halafu akaendelea pia kumwambia yule mtu aliyemwalika: “Unapoandaa mlo wa mchana au mlo wa jioni, usiwaite rafiki zako au ndugu zako au jamaa zako au jirani zako walio matajiri. Labda wakati fulani huenda nao pia wakakualika na hilo lingekuwa kukulipa. 13 Lakini unapoandaa karamu, alika maskini, viwete, vilema, vipofu;+ 14 nawe utakuwa mwenye furaha, kwa sababu hao hawana kitu cha kukulipa. Kwa maana utalipwa katika ufufuo+ wa walio waadilifu.”
15 Aliposikia hayo mtu fulani kati ya wageni wenzake walioalikwa akamwambia: “Mwenye furaha ni yule anayekula mkate katika ufalme wa Mungu.”+
16 Yesu akamwambia: “Mtu fulani alikuwa akiandaa mlo mkubwa wa jioni, naye akawaalika watu wengi.+ 17 Naye akamtuma nje mtumwa wake kwenye saa ya huo mlo wa jioni ili awaambie walioalikwa, ‘Njooni,+ kwa sababu vitu sasa viko tayari.’ 18 Lakini wote kwa namna moja wakaanza kutoa visingizio.+ Yule wa kwanza akamwambia, ‘Nilinunua shamba nami ninahitaji kwenda kuliona; ninakuomba, Niwie radhi.’+ 19 Na mwingine akasema, ‘Nilinunua jozi tano za ng’ombe nami ninaenda kuwachunguza; ninakuomba, Niwie radhi.’+ 20 Na bado mwingine akasema, ‘Nimeoa+ mke sasa hivi na kwa hiyo siwezi kuja.’ 21 Kwa hiyo yule mtumwa akaja, akamwambia bwana wake mambo hayo. Ndipo mwenye nyumba akawa na ghadhabu na kumwambia mtumwa wake, ‘Nenda upesi katika zile njia pana na njia ndogo za jiji, uwaingize humu maskini na viwete na vipofu na vilema.’+ 22 Baada ya muda yule mtumwa akasema, ‘Bwana, uliloagiza limefanywa, na bado mna nafasi.’ 23 Naye bwana akamwambia yule mtumwa, ‘Nenda barabarani+ na mahali palipozungushiwa ua, na uwashurutishe waingie, ili nyumba yangu ipate kujaa.+ 24 Kwa maana ninawaambia ninyi, Hakuna hata mmoja wa watu wale walioalikwa ambaye ataonja mlo wangu wa jioni.’ ”+
25 Sasa umati mkubwa ulikuwa ukisafiri pamoja naye, naye akageuka na kuwaambia: 26 “Yeyote akija kwangu naye hamchukii baba yake na mama na mke na watoto na ndugu na dada, ndiyo, na hata nafsi+ yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.+ 27 Yeyote yule asiyeuchukua mti wake wa mateso na kunifuata hawezi kuwa mwanafunzi wangu.+ 28 Kwa mfano, ni nani kati yenu anayetaka kujenga mnara ambaye haketi kwanza na kuhesabu gharama,+ ili aone kama ana kiasi cha kutosha kuukamilisha? 29 Kama sivyo, ataweka msingi lakini asiweze kuumaliza, na watazamaji wote wataanza kumdhihaki, 30 wakisema, ‘Mtu huyu alianza kujenga lakini hakuweza kumaliza.’ 31 Au ni mfalme gani, anayeenda kukutana na mfalme mwingine vitani, asiyeketi kwanza na kufanya shauri kama anaweza akiwa na askari 10,000 kukabiliana na yule mtu anayekuja juu yake pamoja na 20,000?+ 32 Ikiwa, kwa kweli, hawezi kufanya hivyo, basi yule akiwa bado yuko mbali sana huyu hutuma nje baraza la mabalozi na kuomba amani.+ 33 Kwa hiyo, iweni na hakika kwamba, hakuna hata mmoja kati yenu asiyeaga mali+ zake zote anayeweza kuwa mwanafunzi wangu.
34 “Chumvi, kwa hakika, ni nzuri. Lakini ikiwa hata hiyo chumvi inapoteza nguvu zake, itakolezwa kwa kitu gani?+ 35 Hiyo haifai kwa ajili ya udongo wala kwa ajili ya mbolea. Watu huitupa nje. Acheni yule aliye na masikio ya kusikiliza, asikilize.”+
15 Sasa wakusanya-kodi+ wote na watenda-dhambi+ wakamkaribia ili wamsikie. 2 Kwa sababu hiyo Mafarisayo na pia waandishi wakanung’unika, wakisema: “Mtu huyu hukaribisha watenda-dhambi na hula pamoja nao.”+ 3 Ndipo akawaambia mfano huu, akisema: 4 “Ni nani kati yenu mwenye kondoo 100, anapopoteza mmoja wao, hatawaacha wale 99 nyikani na kwenda kumtafuta aliyepotea mpaka ampate?+ 5 Na akiisha kumpata humweka juu ya mabega yake na kushangilia.+ 6 Naye anapofika nyumbani huwaita rafiki zake na jirani zake pamoja, akiwaambia, ‘Shangilieni pamoja nami, kwa sababu nimempata kondoo wangu aliyekuwa amepotea.’+ 7 Mimi ninawaambia ninyi kwamba ndivyo kutakavyokuwa na shangwe zaidi mbinguni juu ya mtenda-dhambi mmoja anayetubu+ kuliko juu ya waadilifu 99 ambao hawahitaji kutubu.+
8 “Au ni mwanamke gani mwenye sarafu kumi za drakma, akipoteza sarafu moja ya drakma, hawashi taa na kufagia nyumba yake na kutafuta kwa uangalifu mpaka aipate? 9 Naye akiisha kuipata huwaita wanawake walio rafiki zake na jirani zake pamoja, akisema, ‘Shangilieni pamoja nami, kwa sababu nimeipata sarafu ya drakma niliyoipoteza.’ 10 Hivyo, ninawaambia ninyi, hivyo ndivyo shangwe hutokea kati ya malaika za Mungu juu ya mtenda-dhambi mmoja anayetubu.”+
11 Ndipo akasema: “Mtu fulani alikuwa na wana wawili.+ 12 Na yule mdogo kati yao akamwambia baba yake, ‘Baba, nipe sehemu ya mali iliyo fungu langu.’+ Ndipo akawagawia mali+ yake. 13 Baadaye, baada ya siku zisizokuwa nyingi, mwana huyo mdogo akakusanya pamoja vitu vyote akasafiri ng’ambo na kwenda nchi ya mbali, na huko akatapanya mali yake kwa kuishi maisha ya upotovu.+ 14 Alipokuwa ametumia kila kitu, njaa kali ikatokea kotekote katika nchi hiyo, naye akaanza kuwa na uhitaji. 15 Hata alienda na kujishikamanisha na mmoja wa raia wa nchi hiyo, naye akamtuma aende katika mashamba yake akachunge nguruwe.+ 16 Naye alikuwa akitamani kujishibisha kwa maganda ya karuba ambayo nguruwe hao walikuwa wakila, wala hakuna mtu yeyote aliyekuwa akimpa kitu chochote.+
17 “Aliporudiwa na fahamu zake, akasema, ‘Ni watu wangapi aliowakodi baba yangu ambao wana mkate kwa wingi, na huku mimi ninaangamia hapa kwa njaa kali! 18 Nitaondoka nifunge safari+ kwenda kwa baba yangu na kumwambia: “Baba nimetenda dhambi juu ya mbingu na juu yako wewe.+ 19 Sistahili tena kuitwa mwana wako. Unifanye kama mmoja wa watu wako waliokodiwa.” ’ 20 Kwa hiyo akaondoka akamwendea baba yake. Alipokuwa angali mbali, baba yake akamwona, akamsikitikia, akakimbia, akamwangukia shingoni na kumbusu kwa wororo. 21 Ndipo yule mwana akamwambia, ‘Baba, nimetenda dhambi juu ya mbingu na juu yako,+ sistahili tena kuitwa mwana wako. Unifanye niwe kama mmoja wa watu wako waliokodiwa.’+ 22 Lakini baba huyo akawaambia watumwa wake, ‘Upesi! leteni kanzu, iliyo bora zaidi, mkamvike,+ na mtie pete+ mkononi mwake na viatu miguuni mwake. 23 Nanyi leteni ng’ombe-dume mchanga aliyenoneshwa,+ mchinjeni na tule na kujifurahisha, 24 kwa sababu huyu mwanangu alikuwa amekufa naye yuko hai+ sasa; alikuwa amepotea naye amepatikana.’ Nao wakaanza kujifurahisha.
25 “Sasa mwana wake mkubwa+ alikuwa katika shamba; naye alipoikaribia nyumba akasikia sauti za muziki na dansi. 26 Kwa hiyo akamwita mmoja wa watumishi, akauliza maana ya mambo hayo. 27 Huyo akamwambia, ‘Ndugu+ yako amekuja, na baba+ yako amechinja ng’ombe-dume mchanga aliyenoneshwa, kwa sababu alimpata tena akiwa na afya njema.’ 28 Lakini akawa na ghadhabu na hakutaka kuingia. Ndipo baba yake akatoka, akaanza kumsihi sana.+ 29 Akamjibu, akamwambia baba yake, ‘Nimekutumikia kwa miaka mingi sana wala sijavunja amri yako hata mara moja, hata hivyo hujanipa mwana-mbuzi hata mara moja ili mimi nijifurahishe pamoja na rafiki zangu.+ 30 Lakini mara tu alipofika huyu mwana wako+ aliyekula pamoja na makahaba+ mali yako, ulimchinjia ng’ombe-dume mchanga aliyenoneshwa.’+ 31 Ndipo akamwambia, ‘Mwanangu, wewe umekuwa pamoja nami sikuzote, na vitu vyangu vyote ni vyako;+ 32 lakini ilitupasa tu kujifurahisha na kushangilia, kwa sababu huyu ndugu yako alikuwa amekufa naye yuko hai sasa, alikuwa amepotea naye amepatikana.’ ”+
16 Ndipo akaendelea kuwaambia wanafunzi pia: “Mtu fulani alikuwa tajiri naye alikuwa na msimamizi-nyumba,+ na huyo akashtakiwa kwake kuwa anapoteza mali zake.+ 2 Kwa hiyo akamwita na kumwambia, ‘Ni nini hili ninalosikia juu yako? Toa hesabu+ ya usimamizi wako, kwa maana huwezi tena kuisimamia nyumba.’ 3 Ndipo huyo msimamizi akasema moyoni mwake, ‘Nitafanya nini, kwa kuwa bwana+ wangu atauondolea mbali usimamizi wangu? Sina nguvu za kutosha kulima, ninaona aibu kuombaomba. 4 Ah! Najua nitakalofanya, ili, nitakapoondolewa kwenye usimamizi, watu wanipokee nyumbani mwao.’+ 5 Naye akaita kila mmoja wa wale wenye deni la bwana wake, akamwambia wa kwanza, ‘Unadaiwa kiasi gani na bwana wangu?’ 6 Akasema, ‘Vipimo 100 vya bathi vya mafuta ya zeituni.’ Akamwambia, ‘Chukua hati yako ya mapatano, uketi uandike upesi 50.’ 7 Halafu, akamwambia mwingine, ‘Na wewe, unadaiwa kiasi gani?’ Akasema, ‘Vipimo 100 vya kori vya ngano.’ Akamwambia, ‘Chukua hati yako ya mapatano uandike 80.’ 8 Na bwana wake akamsifu yule msimamizi, kwa sababu alikuwa ametenda kwa hekima inayotumika,+ ingawa si mwadilifu; kwa maana wana wa mfumo huu wa mambo wana hekima zaidi kwa njia inayotumika kuelekea kizazi chao wenyewe kuliko vile walivyo wana wa nuru.+
9 “Pia, ninawaambia ninyi, Jifanyieni rafiki+ kupitia mali+ zisizo za uadilifu, ili, zitakapopunguka wawapokee ninyi katika makao ya milele.+ 10 Mtu aliye mwaminifu katika lililo dogo zaidi ni mwaminifu katika lililo kubwa pia, na mtu ambaye si mwaminifu katika lililo dogo zaidi si mwaminifu katika lililo kubwa pia.+ 11 Kwa hiyo, ikiwa ninyi hamjajionyesha wenyewe kuwa waaminifu kuhusiana na mali zisizo za uadilifu, ni nani atakayewakabidhi ninyi kilicho cha kweli?+ 12 Na ikiwa ninyi hamjajionyesha wenyewe kuwa waaminifu kuhusiana na kilicho cha mwingine,+ ni nani atakayewapa ninyi kilicho chenu wenyewe? 13 Hakuna mtumishi wa nyumbani anayeweza kuwatumikia mabwana wawili; kwa maana, ama atamchukia mmoja na kumpenda mwingine, au atashikamana na mmoja na kumdharau mwingine. Hamwezi kuwa watumwa wa Mungu na wa Mali.”+
14 Sasa Mafarisayo, waliokuwa wapenda-pesa, walikuwa wakisikiliza mambo yote hayo, nao wakaanza kumcheka kwa dharau.+ 15 Kwa hiyo akawaambia: “Ninyi ni wale mnaojitangaza kuwa waadilifu mbele ya macho ya wanadamu,+ lakini Mungu anaijua mioyo+ yenu; kwa sababu kilichoinuka sana kati ya wanadamu ni chukizo machoni pa Mungu.+
16 “Sheria na Manabii walikuwa mpaka Yohana.+ Tangu wakati huo na kuendelea ufalme wa Mungu unatangazwa kuwa habari njema, na kila namna ya mtu anajitahidi kuufikia.+ 17 Kwa kweli, ni rahisi zaidi mbingu na dunia kupitilia mbali+ kuliko nukta+ moja ya herufi ya Sheria kupita bila kutimizwa.+
18 “Kila mtu anayemtaliki mke wake na kuoa mwingine anafanya uzinzi, naye anayemwoa mwanamke aliyetalikiwa kutoka kwa mume anafanya uzinzi.+
19 “Lakini mtu+ fulani alikuwa tajiri, naye alikuwa akijipamba kwa mavazi ya zambarau na kitani, akijifurahisha siku baada ya siku kwa fahari.+ 20 Lakini mwombaji fulani aliyeitwa Lazaro alikuwa akiwekwa kwenye lango lake, akiwa amejaa vidonda 21 naye alikuwa akitamani kujishibisha kwa vitu vilivyokuwa vikianguka kutoka kwenye meza ya yule tajiri. Ndiyo, pia, mbwa walikuwa wakija na kuviramba vidonda vyake. 22 Baadaye yule mwombaji akafa+ naye akachukuliwa na malaika mpaka kifuani+ pa Abrahamu.+
“Pia, yule tajiri akafa+ na kuzikwa. 23 Na katika Kaburi* akayainua macho yake, akiteswa sana,+ naye akamwona Abrahamu kwa mbali na Lazaro akiwa kifuani pamoja naye. 24 Kwa hiyo akaita na kusema, ‘Baba Abrahamu,+ nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake katika maji aupoze ulimi wangu,+ kwa sababu nimo katika maumivu makali katika moto huu unaowaka vikali.’+ 25 Lakini Abrahamu akasema, ‘Mwanangu, kumbuka kwamba ulipokea kwa ukamili vitu vyako vyema katika maisha yako, lakini Lazaro alipokea mabaya. Hata hivyo, sasa anapata faraja hapa lakini wewe umo katika maumivu makali.+ 26 Na mbali na mambo yote haya, shimo+ kubwa limewekwa kati yetu na ninyi,+ hivi kwamba wale wanaotaka kuvuka kutoka hapa kuja kwenu hawawezi, wala watu hawawezi kuvuka kutoka huko kuja kwetu.’+ 27 Ndipo akasema, ‘Ikiwa ni hivyo ninakuomba, baba, umtume kwenye nyumba ya baba yangu, 28 kwa maana nina ndugu watano, ili apate kuwapa ushahidi kamili, ili wao pia wasiingie mahali hapa pa mateso.’ 29 Lakini Abrahamu akasema, ‘Wana Musa+ na Manabii;+ na wawasikilize hao.’+ 30 Ndipo akasema, ‘Kwa kweli, hapana, baba Abrahamu, lakini mtu fulani kutoka kwa wafu akiwaendea watatubu.’ 31 Lakini akamwambia, ‘Ikiwa hawamsikilizi Musa+ na Manabii, wala hawatasadikishwa ikiwa mtu fulani atafufuliwa kutoka kwa wafu.’ ”
17 Ndipo akawaambia wanafunzi wake: “Vikwazo lazima vije.+ Hata hivyo, ole wake ambaye vitakuja kupitia kwake!+ 2 Ingekuwa afadhali zaidi kwake kama jiwe la kusagia lingening’inizwa shingoni mwake naye atupwe ndani ya bahari+ kuliko yeye kumkwaza mmoja wa wadogo hawa.+ 3 Jiangalieni ninyi wenyewe. Ndugu yako akitenda dhambi mkemee,+ na akitubu msamehe.+ 4 Hata ikiwa amekutendea dhambi mara saba kwa siku naye anarudi kwako mara saba, akisema, ‘Ninatubu,’ msamehe.”+
5 Sasa mitume wakamwambia Bwana: “Tupe imani zaidi.”+ 6 Ndipo Bwana akasema: “Kama mngekuwa na imani yenye ukubwa wa mbegu ya haradali, mngeuambia mforsadi huu mweusi, ‘Ng’oka ukapandwe baharini!’ nao ungewatii ninyi.+
7 “Ni nani kati yenu aliye na mtumwa anayelima au anayetunza kundi ambaye atamwambia anapoingia kutoka shambani, ‘Njoo hapa mara moja uketi mezani’? 8 Badala yake, je, hatamwambia, ‘Nitayarishie kitu ili nipate mlo wangu wa jioni, nawe jifunge unihudumie mpaka niwe nimemaliza kula na kunywa, kisha unaweza kula na kunywa’? 9 Je, atamshukuru mtumwa huyo kwa sababu alifanya mambo aliyoagizwa? 10 Ndivyo na ninyi, pia, wakati mmefanya mambo yote mliyoagizwa, semeni, ‘Sisi ni watumwa wasiofaa kitu.+ Jambo ambalo tumefanya ndilo tulilopaswa kufanya.’ ”
11 Naye alipokuwa akienda Yerusalemu alikuwa akipita katikati ya Samaria na Galilaya.+ 12 Alipokuwa akiingia katika kijiji fulani wanaume kumi wenye ukoma+ wakakutana naye, lakini wakasimama mbali. 13 Nao wakapaaza sauti zao na kusema: “Yesu, Mwalimu, tuhurumie!”+ 14 Naye alipowaona akawaambia: “Nendeni mkajionyeshe kwa makuhani.”+ Basi walipokuwa wakienda zao wakatakaswa.+ 15 Mmoja wao, alipoona amepona, akarudi, akimtukuza+ Mungu kwa sauti kubwa. 16 Naye akaanguka kifudifudi miguuni pa Yesu,+ akamshukuru; tena, alikuwa Msamaria.+ 17 Yesu akajibu akasema: “Wale kumi walitakaswa, sivyo? Basi, wako wapi wale wengine tisa? 18 Je, hawakupatikana wowote waliorudi kumpa Mungu utukufu ila mtu huyu wa taifa lingine?” 19 Naye akamwambia: “Ondoka uende zako; imani yako imekuponya.”+
20 Lakini alipoulizwa na Mafarisayo ufalme wa Mungu ungekuja wakati gani,+ akawajibu na kusema: “Ufalme wa Mungu hautakuja kwa wonyesho wenye kutokeza sana, 21 wala watu hawatakuwa wakisema, ‘Ona hapa!’ au, ‘Pale!’+ Kwa maana, tazama! ufalme wa Mungu umo katikati yenu.”+
22 Ndipo akawaambia wanafunzi: “Siku zitakuja mtakapotamani kuiona moja ya siku za Mwana wa binadamu lakini hamtaiona.+ 23 Na watu watawaambia ninyi, ‘Oneni pale!’ au, ‘Oneni hapa!’+ Msitoke kwenda wala msiwafuatilie mbio.+ 24 Kwa maana kama vile umeme,+ unapowaka, hung’aa kutoka sehemu moja chini ya mbingu mpaka sehemu nyingine chini ya mbingu, ndivyo Mwana wa binadamu+ atakavyokuwa. 25 Hata hivyo, kwanza lazima apatwe na mateso mengi na kukataliwa na kizazi hiki.+ 26 Zaidi ya hayo, sawa na vile ilivyotukia katika siku za Noa,+ ndivyo itakavyokuwa pia katika siku za Mwana wa binadamu:+ 27 walikuwa wakila, walikuwa wakinywa, wanaume walikuwa wakioa, wanawake walikuwa wakiolewa, mpaka siku ile ambayo Noa aliingia katika safina, na gharika ikafika na kuwaangamiza wote.+ 28 Vivyo hivyo, kama vile ilivyotukia katika siku za Loti:+ walikuwa wakila, walikuwa wakinywa, walikuwa wakinunua, walikuwa wakiuza, walikuwa wakipanda, walikuwa wakijenga. 29 Lakini siku ambayo Loti alitoka Sodoma kulinyesha moto na kiberiti kutoka mbinguni na kuwaangamiza wote.+ 30 Itakuwa vivyo hivyo siku ile ambayo Mwana wa binadamu atafunuliwa.+
31 “Siku hiyo mtu aliye juu ya paa ya nyumba lakini ambaye vitu vyake vinavyoweza kuchukuliwa vimo katika nyumba asishuke kuvichukua, na mtu aliye nje katika shamba, yeye vivyo hivyo asirudie vitu vilivyo nyuma. 32 Mkumbukeni mke wa Loti.+ 33 Yeyote yule anayetafuta kuitunza nafsi yake kwa ajili yake mwenyewe ataipoteza, lakini yeyote yule anayeipoteza ataihifadhi hai.+ 34 Ninawaambia ninyi, Usiku huo watu wawili watakuwa katika kitanda kimoja; mmoja atachukuliwa, lakini yule mwingine ataachwa.+ 35 Kutakuwa na wanawake wawili wakisaga kwenye jiwe lilelile la kusagia; mmoja atachukuliwa, lakini yule mwingine ataachwa.”+ 36 —— 37 Kwa hiyo wakajibu, wakamwambia: “Wapi, Bwana?” Yeye akawaambia: “Mahali mzoga ulipo,+ hapo ndipo tai watakusanyika.”+
18 Ndipo akaendelea kuwaambia mfano juu ya uhitaji wao wa kusali sikuzote bila kukata tamaa,+ 2 akisema: “Katika jiji fulani kulikuwako mwamuzi fulani ambaye hakuwa akimwogopa Mungu wala hakuwa na heshima kwa mwanadamu. 3 Lakini kulikuwako mjane katika jiji hilo naye akawa akimwendea,+ akisema, ‘Hakikisha kwamba nitapata haki kutoka kwa mshitaki wangu.’ 4 Basi, kwa muda fulani alikuwa hana nia, lakini baadaye akasema moyoni mwake, ‘Ijapokuwa mimi simwogopi Mungu wala simheshimu mwanadamu, 5 hakika, kwa sababu ya kuendelea kwa mjane huyu kunisumbua,+ nitahakikisha kwamba atapata haki, ili asiendelee kuja kunishambulia+ mpaka animalize.’ ” 6 Ndipo Bwana akasema: “Sikieni lile ambalo mwamuzi huyo, ijapokuwa si mwadilifu, alisema! 7 Basi, kwa hakika je, Mungu hatasababisha haki+ ifanywe kwa ajili ya watu wake waliochaguliwa ambao wanampaazia sauti mchana na usiku, hata ingawa ana ustahimilivu+ kwao? 8 Ninawaambia ninyi, Yeye atasababisha watendewe haki upesi.+ Hata hivyo, Mwana wa binadamu atakapofika, je, kwa kweli ataipata imani duniani?”
9 Lakini akawaambia mfano huu pia baadhi ya wale waliokuwa wakiamini kwamba walikuwa waadilifu+ na kuwaona wale wengine kama si kitu:+ 10 “Watu wawili walipanda kuingia hekaluni ili kusali, mmoja alikuwa Farisayo na yule mwingine alikuwa mkusanya-kodi. 11 Yule Farisayo akasimama+ na kuanza kusali+ mambo haya akisema moyoni, ‘Ee Mungu, ninakushukuru ya kuwa mimi si kama wale watu wengine, wanyang’anyi, wasio waadilifu, wazinzi, au hata kama mkusanya-kodi huyu.+ 12 Mimi hufunga mara mbili kwa juma, mimi hutoa sehemu ya kumi ya vitu vyote ninavyojipatia.’+ 13 Lakini yule mkusanya-kodi akiwa amesimama umbali fulani hakutaka hata kuinua macho yake kuelekea mbinguni, bali alikuwa akipiga-piga kifua chake,+ akisema, ‘Ee Mungu, unirehemu mimi mtenda-dhambi.’+ 14 Ninawaambia ninyi, Mtu huyu alishuka kwenda nyumbani kwake akiwa amethibitishwa kuwa mwadilifu+ zaidi kuliko yule mwingine; kwa sababu kila mtu anayejiinua atafedheheshwa, bali yule anayejinyenyekeza atainuliwa.”+
15 Sasa watu wakaanza kumletea pia watoto wao wachanga ili awaguse; lakini walipoona hilo wanafunzi wakaanza kuwakemea.+ 16 Hata hivyo, Yesu akawaita wale watoto, akisema: “Waacheni watoto wachanga waje kwangu, wala msijaribu kuwazuia. Kwa maana ufalme wa Mungu ni wa wale walio kama hao.+ 17 Kwa kweli ninawaambia ninyi, Mtu yeyote ambaye haupokei ufalme wa Mungu kama mtoto mchanga hataingia kamwe ndani yake.”+
18 Na mtawala fulani akamuuliza, akisema: “Mwalimu Mwema, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?”+ 19 Yesu akamwambia: “Kwa nini unaniita mwema? Hakuna mtu aliye mwema, ila mmoja, Mungu.+ 20 Wewe unazijua amri,+ ‘Usifanye uzinzi,+ Usiue,+ Usiibe,+ Usitoe ushahidi wa uwongo,+ Mheshimu baba yako na mama yako.’ ”+ 21 Ndipo akasema: “Yote hayo nimeyashika tangu ujana wangu na kuendelea.”+ 22 Baada ya kusikia hilo, Yesu akamwambia: “Bado kuna jambo moja unalokosa: Uza vitu vyote ulivyo navyo uwagawie maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha uje uwe mfuasi wangu.”+ 23 Aliposikia neno hilo, akahuzunika sana, kwa maana alikuwa tajiri sana.+
24 Yesu akamtazama na kusema: “Jinsi itakavyokuwa vigumu kwa wale walio na pesa kuingia katika ufalme wa Mungu!+ 25 Kwa kweli, ni rahisi zaidi ngamia kupita katika tundu la sindano ya kushonea kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.”+ 26 Wale waliosikia hilo wakasema: “Ni nani anayeweza kuokolewa?” 27 Akasema: “Mambo yasiyowezekana kwa wanadamu yanawezekana kwa Mungu.”+ 28 Lakini Petro akasema: “Tazama! Tumeacha vitu vyetu wenyewe na kukufuata wewe.”+ 29 Akawaambia: “Kwa kweli ninawaambia ninyi, Hakuna yeyote ambaye ameacha nyumba au mke au ndugu au wazazi au watoto kwa ajili ya ufalme wa Mungu+ 30 ambaye hatapata mara nyingi zaidi katika kipindi hiki cha wakati, na katika mfumo wa mambo unaokuja uzima wa milele.”+
31 Ndipo akawachukua wale kumi na wawili kando na kuwaambia: “Tazameni! Tunapanda kwenda Yerusalemu, na mambo yote yaliyoandikwa kupitia manabii+ juu ya Mwana wa binadamu yatatimia.+ 32 Kwa mfano, atatiwa mikononi mwa watu wa mataifa naye atadhihakiwa+ na kutendewa kwa dharau+ na kutemewa mate;+ 33 na baada ya kumpiga mijeledi+ watamuua,+ lakini katika siku ya tatu atafufuka.”+ 34 Hata hivyo, wao hawakupata maana ya lolote kati ya mambo hayo; lakini walikuwa wamefichwa maneno hayo, nao hawakujua mambo yaliyosemwa.+
35 Sasa alipokuwa akikaribia Yeriko mtu fulani aliye kipofu alikuwa ameketi kando ya barabara akiombaomba.+ 36 Kwa sababu aliusikia umati ukipita, akaanza kuuliza maana ya mambo hayo. 37 Wakamwambia: “Yesu Mnazareti anapitia hapa!”+ 38 Ndipo akapaaza sauti, akisema: “Yesu, Mwana wa Daudi, unirehemu!”+ 39 Na wale waliokuwa mbele wakaanza kumwambia kwa kusisitiza anyamaze, lakini ndivyo naye alivyozidi kupaaza sauti: “Mwana wa Daudi, unirehemu.”+ 40 Ndipo Yesu akasimama tuli na kuamuru mtu huyo aletwe kwake.+ Alipokaribia, Yesu akamuuliza: 41 “Unataka nikufanyie nini?”+ Akasema: “Bwana, acha nipate kuona tena.”+ 42 Kwa hiyo Yesu akamwambia: “Ona tena; imani yako imekuponya.”+ 43 Na mara moja akapata kuona tena,+ naye akaanza kumfuata, akimtukuza Mungu.+ Pia, watu wote, walipoona hilo, wakamsifu Mungu.
19 Naye akaingia Yeriko+ na akawa akipita. 2 Sasa kulikuwa na mwanamume anayeitwa Zakayo; naye alikuwa mkuu wa wakusanya-kodi, na alikuwa tajiri. 3 Basi, alikuwa akitafuta kuona+ Yesu huyu ni nani, lakini hangeweza kwa sababu ya umati, kwa sababu alikuwa mfupi. 4 Kwa hiyo akakimbia mbele na kupanda mforsadi-tini kusudi amwone, kwa sababu alikuwa karibu kupitia njia hiyo. 5 Sasa Yesu alipofika hapo, akatazama juu na kumwambia: “Zakayo, shuka haraka, kwa maana leo lazima nikae katika nyumba yako.” 6 Ndipo akafanya haraka, akashuka, akamkaribisha kwa shangwe. 7 Lakini walipoona hilo, wote wakaanza kunung’unika,+ wakisema: “Ameingia apate kukaa pamoja na mwanamume mtenda-dhambi.” 8 Lakini Zakayo akasimama na kumwambia Bwana: “Tazama! Nusu ya mali zangu, Bwana, mimi nitawapa maskini, na chochote nilichomnyang’anya mtu yeyote kwa shtaka la uwongo+ nitarudisha mara nne.”+ 9 Ndipo Yesu akamwambia: “Leo wokovu umekuja kwenye nyumba hii, kwa sababu yeye pia ni mwana wa Abrahamu.+ 10 Kwa maana Mwana wa binadamu alikuja kutafuta na kuokoa kilichopotea.”+
11 Walipokuwa wakisikiliza mambo hayo akatoa mfano kwa kuongezea, kwa sababu alikuwa karibu na Yerusalemu nao walikuwa wakiwazia kwamba ufalme wa Mungu ulikuwa ukikaribia kujionyesha mara moja.+ 12 Kwa hiyo akasema: “Mtu fulani wa ukoo mashuhuri alisafiri mpaka nchi ya mbali ili ajipatie mamlaka ya kifalme kwa ajili yake mwenyewe na kurudi.+ 13 Akaita kumi kati ya watumwa wake akawapa mina kumi na kuwaambia, ‘Fanyeni biashara mpaka nije.’+ 14 Lakini raia zake wakamchukia+ na kutuma baraza la mabalozi kumfuata, na kusema, ‘Hatumtaki mtu huyu awe mfalme juu yetu.’+
15 “Mwishowe aliporudi baada ya kupata mamlaka ya kifalme aliamuru watumwa hao ambao alikuwa amewapa fedha waitwe, ili ahakikishe kile walichokuwa wamepata faida kwa biashara.+ 16 Ndipo wa kwanza akajitokeza, akisema, ‘Bwana, mina yako ilipata faida ya mina kumi.’+ 17 Kwa hiyo akamwambia, ‘Vema, mtumwa mwema! Kwa sababu katika jambo dogo sana umejionyesha mwenyewe kuwa mwaminifu, uwe na mamlaka juu ya majiji kumi.’+ 18 Sasa wa pili akaja, akisema, ‘Mina yako, Bwana, ilileta mina tano.’+ 19 Akamwambia huyu pia, ‘Wewe, pia, usimamie majiji matano.’+ 20 Lakini mwingine akaja, akisema, ‘Bwana, hii hapa mina yako, ambayo niliitunza ikiwa imehifadhiwa katika kitambaa. 21 Unaona, nilikuogopa, kwa sababu wewe ni mtu mgumu; wewe huchukua kile ambacho hukuweka akiba nawe huvuna kile ambacho hukupanda.’+ 22 Akamwambia, ‘Ninakuhukumu kutoka kinywani mwako mwenyewe,+ mtumwa mwovu. Ulijua, sivyo, kwamba mimi ni mtu mgumu, ambaye huchukua kile ambacho sikuweka akiba na kuvuna kile ambacho sikupanda?+ 23 Kwa hiyo kwa nini hukutia fedha zangu katika mahali pa kutunzia akiba? Kisha wakati ambapo ningefika ningezichukua pamoja na faida.’+
24 “Ndipo akawaambia wale waliokuwa wamesimama kando, ‘Chukueni hiyo mina kutoka kwake mkampe yule aliye na mina kumi.’+ 25 Lakini wakamwambia, ‘Bwana, huyo ana mina kumi!’— 26 ‘Ninawaambia ninyi, Kila mtu aliye na kitu, ataongezewa; lakini yule ambaye hana, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.+ 27 Zaidi ya hayo, hao adui zangu ambao hawakutaka niwe mfalme juu yao waleteni hapa mkawaue mbele yangu.’ ”+
28 Kwa hiyo, alipokuwa amesema hayo, akaanza kwenda, akipanda kwenda Yerusalemu.+ 29 Naye alipokaribia Bethfage na Bethania kwenye mlima unaoitwa Mlima wa Mizeituni,+ akatuma wawili kati ya wanafunzi,+ 30 akisema: “Nendeni mkaingie katika kijiji mnachokiona mbele yenu, na ndani yake baada ya kuingia mtamkuta mwana-punda akiwa amefungwa, ambaye hakuna yeyote kati ya wanadamu ambaye amewahi kuketi juu yake. Mfungueni mkamlete.+ 31 Lakini mtu yeyote akiwauliza ninyi, ‘Kwa nini mnamfungua?’ Mwambieni hivi, ‘Bwana anamhitaji.’ ”+ 32 Kwa hiyo wale waliotumwa wakaondoka wakakuta sawa na vile alivyowaambia.+ 33 Lakini walipokuwa wakimfungua mwana-punda, wenyewe wakawaambia: “Kwa nini mnamfungua huyo mwana-punda?”+ 34 Wakasema: “Bwana anamhitaji.”+ 35 Nao wakampeleka kwa Yesu, nao wakayatupa mavazi yao ya nje juu ya huyo mwana-punda na kumweka Yesu juu yake.+
36 Alipokuwa akisonga+ mbele wakawa wakitandaza mavazi yao ya nje barabarani.+ 37 Mara tu alipokaribia barabara ya kushuka Mlima wa Mizeituni umati wote wa wanafunzi wakaanza kushangilia na kumsifu Mungu kwa sauti kubwa juu ya matendo yote yenye nguvu ambayo walikuwa wameona,+ 38 na kusema: “Aliyebarikiwa ni Yule anayekuja akiwa ndiye Mfalme katika jina la Yehova!+ Amani mbinguni, na utukufu katika mahali palipoinuka juu zaidi!”+ 39 Hata hivyo, baadhi ya Mafarisayo kwenye umati wakamwambia: “Mwalimu, wakemee wanafunzi wako.”+ 40 Lakini akajibu akasema: “Ninawaambia ninyi, “Kama hawa wangekaa kimya, mawe+ yangepaaza sauti.”
41 Naye alipokaribia hapo, akalitazama jiji na kulililia,+ 42 akisema: “Kama wewe, naam, wewe, ungalikuwa umefahamu+ leo mambo yanayohusiana na amani—lakini sasa yamefichwa kutoka machoni pako.+ 43 Kwa sababu siku zitakuja juu yako wakati adui zako watakapojenga kukuzunguka ngome+ yenye miti iliyochongoka+ nao watakuzunguka+ na kukutaabisha+ kutoka kila upande, 44 nao watakuangusha chini wewe na watoto wako walio ndani yako,+ nao hawataacha jiwe juu ya jiwe+ ndani yako, kwa sababu hukufahamu wakati wa kukaguliwa kwako.”+
45 Naye akaingia katika hekalu na kuanza kuwafukuza nje wale waliokuwa wakiuza,+ 46 akiwaambia: “Imeandikwa, ‘Na nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala,’+ lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang’anyi.”+
47 Zaidi ya hayo, akawa akifundisha kila siku katika hekalu. Lakini wakuu wa makuhani na waandishi na wakuu kati ya watu walikuwa wakitafuta kumwangamiza;+ 48 na bado hawakufanikiwa, kwa maana watu wote walikuwa wakishikamana sana naye ili wamsikie.+
20 Siku moja alipokuwa akifundisha watu katika hekalu na kutangaza habari njema, wakuu wa makuhani na waandishi pamoja na wanaume wazee wakaja karibu,+ 2 nao wakasema, wakimwambia: “Tuambie unafanya mambo haya kwa mamlaka gani, au ni nani aliyekupa mamlaka hiyo.”+ 3 Akajibu, akawaambia: “Mimi pia nitawauliza ninyi swali, nanyi mniambie:+ 4 Je, ubatizo wa Yohana ulitoka mbinguni au kwa wanadamu?”+ 5 Ndipo kati yao wenyewe wakafikia kauli, wakisema: “Tukisema, ‘Ulitoka mbinguni,’ atasema, ‘Kwa nini hamkumwamini?’+ 6 Lakini tukisema, ‘Ulitoka kwa wanadamu,’ watu wote watatupiga kwa mawe,+ kwa maana wao wamesadikishwa kwamba Yohana+ alikuwa nabii.”+ 7 Kwa hiyo wakajibu kwamba hawakujua chanzo chake. 8 Naye Yesu akawaambia: “Wala mimi siwaambii ninyi ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani.”+
9 Ndipo akaanza kuwaambia watu mfano huu: “Mtu alipanda shamba la mizabibu+ akalikodisha kwa wakulima, naye akasafiri kwenda ng’ambo kwa muda mrefu.+ 10 Lakini majira yake yalipofika akatuma mtumwa+ kwa wakulima,+ ili wampe sehemu ya matunda ya shamba la mizabibu.+ Hata hivyo, wakulima hao wakamfukuza akiwa mikono mitupu,+ baada ya kumpiga sana. 11 Lakini akatuma tena mtumwa tofauti kwao. Huyo pia wakampiga sana na kumvunjia heshima na kumfukuza akiwa mikono mitupu.+ 12 Na bado tena akamtuma wa tatu;+ huyo pia walimjeruhi na kumtupa nje. 13 Ndipo mwenye shamba la mizabibu akasema, ‘Nitafanya nini? Nitamtuma mwanangu mpendwa.+ Labda watamheshimu huyu.’ 14 Wakulima walipomwona wakaanza kujadiliana, wakisema, ‘Huyu ndiye mrithi; acheni tumuue, ili urithi uwe wetu.’+ 15 Ndipo wakamtupa nje+ ya shamba la mizabibu na kumuua.+ Kwa hiyo, mwenye shamba la mizabibu atawafanya nini?+ 16 Atakuja awaangamize wakulima hao na kuwapa wengine shamba hilo la mizabibu.”+
Waliposikia hilo wakasema: “Jambo hilo lisitukie kamwe!” 17 Lakini akawatazama na kusema: “Basi, hili ambalo limeandikwa humaanisha nini, ‘Jiwe ambalo wajenzi walilikataa,+ limekuwa jiwe kuu la pembeni’?+ 18 Kila mtu anayeanguka juu ya jiwe hilo atavunjwa-vunjwa.+ Na yeyote ambaye litamwangukia,+ litamponda-ponda.”+
19 Waandishi na wakuu wa makuhani sasa wakatafuta kunyoosha mkono ili wamkamate saa ileile, lakini waliwaogopa watu; kwa maana walifahamu kwamba alisema mfano huo juu yao.+ 20 Na, baada ya kumtazama sana, wakatuma watu waliokodiwa kwa siri wasingizie kwamba walikuwa waadilifu, ili wapate kumnasa+ katika maneno, ili wamkabidhi kwa serikali na kwa mamlaka ya gavana.+ 21 Nao wakamuuliza, wakisema: “Mwalimu, tunajua wewe husema na kufundisha kwa usahihi na huonyeshi ubaguzi wowote, bali wewe hufundisha njia ya Mungu kupatana na ile kweli:+ 22 Je, ni halali sisi kumlipa Kaisari kodi au hapana?”+ 23 Lakini akagundua ujanja wao na kuwaambia:+ 24 “Nionyesheni dinari. Ina sanamu na mwandiko wa nani?” Wakasema: “Wa Kaisari.”+ 25 Akawaambia: “Kwa vyovyote, basi, mlipeni Kaisari vitu vya Kaisari,+ lakini mlipeni Mungu vitu vya Mungu.”+ 26 Basi, hawakuweza kumnasa katika maneno haya mbele ya watu, bali, wakiwa wameshangazwa na jibu lake, hawakusema kitu.+
27 Hata hivyo, baadhi ya Masadukayo, wale ambao husema hakuna ufufuo, wakaja+ na kumuuliza swali, 28 wakisema: “Mwalimu, Musa+ alituandikia, ‘Ndugu ya mtu akifa akiwa na mke, lakini hakuwa na mtoto, ndugu yake+ anapaswa kumchukua mke huyo na kumwinulia ndugu yake uzao kutoka kwa mwanamke huyo.’+ 29 Basi kulikuwa na ndugu saba; na wa kwanza akamchukua mke na kufa bila mtoto.+ 30 Na wa pili, 31 na wa tatu, wakamchukua mwanamke huyo. Vivyo hivyo hata wa saba: hawakuacha uzao, bali walikufa mmoja baada ya mwingine.+ 32 Mwishowe, yule mwanamke akafa pia.+ 33 Kwa hiyo, katika ufufuo, atakuwa mke wa nani kati yao? Kwa maana wale saba walimchukua kama mke.”+
34 Yesu akawaambia: “Watoto wa mfumo huu wa mambo huoa+ na huolewa, 35 lakini wale ambao wamehesabiwa kustahili+ kuupata mfumo ule wa mambo+ na ufufuo kutoka kwa wafu+ hawaoi wala hawaolewi. 36 Kwa kweli, wala hawawezi kufa+ tena kamwe, kwa maana wao ni kama malaika, nao ni watoto wa Mungu kwa kuwa watoto wa ufufuo.+ 37 Lakini hata Musa alifunua kwamba wafu watafufuliwa, katika masimulizi juu ya ule mti wa miiba,+ anapomwita Yehova ‘Mungu wa Abrahamu na Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo.’+ 38 Yeye ni Mungu, si wa wafu, bali wa walio hai, kwa maana kwake, hao wote wako hai.”+ 39 Baadhi ya waandishi wakajibu, wakasema: “Mwalimu, umesema vema.” 40 Kwa maana hawakuwa tena na ujasiri wa kumuuliza hata swali moja.
41 Naye akawaambia: “Kwa nini wao husema kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?+ 42 Kwa maana Daudi mwenyewe anasema katika kitabu cha Zaburi, ‘Yehova alimwambia Bwana wangu: “Keti kwenye mkono wangu wa kuume 43 mpaka niwaweke adui zako kuwa kiti cha miguu yako.”’+ 44 Basi, Daudi anamwita ‘Bwana’; kwa hiyo inawezekanaje kwamba yeye ni mwana wake?”
45 Ndipo, watu wote wakiwa wanasikiliza akawaambia wanafunzi:+ 46 “Jihadharini na waandishi ambao hutamani kutembea wakiwa wamevaa kanzu nao hupenda salamu katika masoko na viti vya mbele katika masinagogi na mahali penye kuonekana zaidi kwenye milo ya jioni,+ 47 na ambao humeza nyumba za wajane+ na kutoa sala ndefu kwa kisingizio. Hawa watapokea hukumu nzito zaidi.”+
21 Sasa alipotazama juu aliwaona matajiri wakitumbukiza zawadi zao ndani ya masanduku ya hazina.+ 2 Ndipo akaona mjane fulani mwenye uhitaji akitumbukiza humo sarafu ndogo mbili za thamani ndogo sana,+ 3 naye akasema: “Ninawaambia ninyi kwa kweli, Mjane huyu, ijapokuwa ni maskini, ametumbukiza ndani zaidi kuliko hao wote.+ 4 Kwa maana wote hawa walitumbukiza zawadi kutokana na ziada yao, lakini mwanamke huyu kutokana na uhitaji wake alitumbukiza ndani riziki yote aliyokuwa nayo.”+
5 Baadaye, watu fulani walipokuwa wakisema kuhusu hekalu, jinsi lilivyopambwa kwa mawe mazuri na vitu vilivyowekwa wakfu,+ 6 akasema: “Vitu hivi ambavyo ninyi mnaviona, siku zitakuja ambapo hakuna jiwe litakaloachwa hapa juu ya jiwe nalo lisiangushwe chini.”+ 7 Ndipo wakamuuliza, wakisema: “Mwalimu, kwa kweli mambo haya yatakuwa wakati gani, na ni nini itakayokuwa ishara ya wakati ambapo mambo hayo yatatukia?”+ 8 Akasema: “Jihadharini msipotoshwe;+ kwa maana wengi watakuja kwa msingi wa jina langu, wakisema, ‘Mimi ndiye,’ na, ‘Wakati unaofaa umekaribia.’+ Msiwafuate. 9 Zaidi ya hayo, wakati mnaposikia juu ya vita na machafuko, msiogope.+ Kwa maana mambo hayo lazima yatukie kwanza, lakini ule mwisho hautatokea mara moja.”
10 Ndipo akaendelea kuwaambia: “Taifa litasimama kupigana na taifa,+ na ufalme kupigana na ufalme;+ 11 na kutakuwa na matetemeko makubwa ya nchi, na katika mahali pamoja baada ya pengine kutakuwa na tauni na upungufu wa chakula;+ kutakuwa na mambo yenye kuogopesha na ishara kubwa kutoka mbinguni.+
12 “Lakini kabla ya mambo yote hayo watu watawakamata na kuwatesa,+ wakiwakabidhi ninyi kwenye masinagogi na magereza, mkikokotwa na kupelekwa mbele ya wafalme na magavana kwa ajili ya jina langu.+ 13 Utakuwa ushahidi kwenu.+ 14 Kwa hiyo azimieni mioyoni mwenu kwamba hamtafanya mazoezi mapema ya jinsi mtakavyojitetea,+ 15 kwa maana nitawapa ninyi kinywa na hekima, ambayo wapinzani wenu wote wakiwa pamoja hawataweza kushindana nayo wala kubisha.+ 16 Zaidi ya hayo, mtatolewa hata na wazazi+ na ndugu na jamaa zenu na rafiki zenu, nao watafanya wengine kati yenu wauawe;+ 17 nanyi mtachukiwa na watu wote kwa sababu ya jina langu.+ 18 Na bado hata unywele+ mmoja wa vichwa vyenu hautaangamia. 19 Nanyi kwa kuvumilia mtajipatia nafsi zenu.+
20 “Zaidi ya hayo, mtakapoona Yerusalemu limezingirwa+ na majeshi yaliyopiga kambi, ndipo jueni kwamba kufanywa ukiwa kwake kumekaribia.+ 21 Ndipo wale walio katika Yudea waanze kukimbilia milimani, na wale walio katikati yake na waondoke, nao wale walio katika sehemu za mashambani wasiingie ndani;+ 22 kwa sababu hizi ni siku za kupatiliza haki, ili mambo yote yaliyoandikwa yatimizwe.+ 23 Ole wao wanawake wenye mimba na wale wanaonyonyesha mtoto mchanga katika siku hizo!+ Kwa maana kutakuwa na uhitaji mkubwa juu ya nchi na ghadhabu juu ya watu hawa; 24 nao wataanguka kwa makali ya upanga na watapelekwa mateka katika mataifa yote;+ na Yerusalemu litakanyagwa-kanyagwa na mataifa, mpaka nyakati zilizowekwa+ za mataifa zitimie.
25 “Pia, kutakuwa na ishara katika jua+ na mwezi na nyota, na juu ya dunia maumivu makali ya mataifa, bila kujua njia ya kutokea kwa sababu ya kunguruma kwa bahari+ na msukosuko+ wake, 26 huku watu wakizimia kwa woga+ na tarajio la mambo yanayokuja juu ya dunia inayokaliwa;+ kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.+ 27 Na ndipo watakapomwona Mwana wa binadamu+ akija katika wingu akiwa na nguvu na utukufu mwingi.+ 28 Lakini mambo haya yanapoanza kutukia, simameni wima na kuinua vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu unakaribia.”
29 Ndipo akawaambia mfano: “Angalieni mtini na miti mingine yote:+ 30 Wakati inapokuwa tayari imechipuka, kwa kuangalia mnajua wenyewe kwamba sasa kiangazi kiko karibu.+ 31 Vivyo hivyo ninyi pia, wakati mnapoona mambo hayo yakitukia, jueni kwamba ufalme wa Mungu uko karibu.+ 32 Kwa kweli nawaambia ninyi, Kizazi hiki hakitapitilia mbali kamwe mpaka mambo yote yatukie.+ 33 Mbingu na dunia zitapitilia mbali,+ lakini maneno yangu hayatapitilia mbali kamwe.+
34 “Lakini jiangalieni ninyi wenyewe kwamba mioyo yenu isilemewe kamwe na kula kupita kiasi na kunywa sana+ na mahangaiko+ ya maisha, na kwa ghafula siku hiyo iwe juu yenu mara moja+ 35 kama mtego.+ Kwa maana itakuja juu ya wale wote wanaokaa juu ya uso wa dunia yote.+ 36 Basi, endeleeni kukesha+ wakati wote mkiomba dua+ ili mpate kufanikiwa kuponyoka mambo yote hayo yaliyokusudiwa kutukia, na kusimama mbele ya Mwana wa binadamu.”+
37 Kwa hiyo wakati wa mchana alikuwa akifundisha katika hekalu,+ lakini wakati wa usiku alikuwa akitoka kwenda na kukaa juu ya mlima unaoitwa Mlima wa Mizeituni.+ 38 Na watu wote+ walikuwa wakimjia asubuhi katika hekalu ili wamsikie.
22 Sasa sherehe ya keki zisizo na chachu, ile ambayo huitwa Pasaka,+ ilikuwa ikikaribia. 2 Pia, wakuu wa makuhani na waandishi walikuwa wakitafuta njia bora ya kumwondolea mbali,+ kwa maana walikuwa wakiwaogopa watu.+ 3 Lakini Shetani akamwingia Yuda, anayeitwa Iskariote, ambaye alihesabiwa kati ya wale kumi na wawili;+ 4 naye akaenda zake akaongea na wakuu wa makuhani na makapteni wa hekalu juu ya njia bora ya kumsaliti kwao.+ 5 Basi, wakashangilia na kupatana kumpa fedha.+ 6 Kwa hiyo akakubali, naye akaanza kutafuta nafasi nzuri ya kumsaliti kwao bila umati kuwa karibu.+
7 Siku ya keki zisizo na chachu sasa ikafika, ambapo mnyama wa pasaka lazima atolewe dhabihu;+ 8 naye akawatuma Petro na Yohana, akisema: “Nendeni mkatutayarishie pasaka+ ili tule.” 9 Wakamwambia: “Ni wapi unapotaka tuitayarishe?” 10 Akawaambia:+ “Tazameni! Mnapoingia katika jiji, mwanamume anayebeba chombo cha udongo cha maji atakutana nanyi. Mfuateni mwingie katika nyumba ambayo ataingia.+ 11 Nanyi lazima mmwambie mwenye nyumba hiyo, ‘Mwalimu anakuambia wewe: “Kiko wapi chumba cha wageni ambacho humo ninaweza kula pasaka pamoja na wanafunzi wangu?” ’+ 12 Na mtu huyo atawaonyesha ninyi chumba kikubwa cha juu chenye vifaa. Fanyeni matayarisho humo.”+ 13 Kwa hiyo wakaondoka na kukipata kama vile alivyokuwa amewaambia, nao wakatayarisha pasaka.+
14 Mwishowe saa ilipofika, akaketi mezani, na wale mitume pamoja naye.+ 15 Naye akawaambia: “Nimetamani sana kula pasaka hii pamoja nanyi kabla sijateswa; 16 kwa maana ninawaambia ninyi, Sitaila tena mpaka itakapokuwa imetimizwa katika ufalme wa Mungu.”+ 17 Na, akipokea kikombe,+ akashukuru na kusema: “Chukueni hiki mkipitishe kutoka kwa mmoja mpaka kwa mwingine kati yenu; 18 kwa maana ninawaambia ninyi, Kutoka sasa na kuendelea sitakunywa tena divai ya mzabibu mpaka ufalme wa Mungu utakapofika.”+
19 Pia, akachukua mkate,+ akashukuru, akaumega, akawapa, akisema: “Huu unamaanisha mwili+ wangu ambao utatolewa kwa ajili yenu.+ Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.”+ 20 Pia, kikombe+ vivyo hivyo baada ya wao kula mlo wa jioni, akasema: “Kikombe hiki kinamaanisha agano+ jipya kwa msingi wa damu+ yangu, ambayo itamwagwa kwa ajili yenu.+
21 “Lakini, tazameni! mkono wa msaliti+ wangu upo pamoja nami mezani.+ 22 Kwa sababu Mwana wa binadamu anaenda zake kulingana na ilivyopangwa;+ hata hivyo, ole wake mtu yule ambaye kupitia kwake huyo atasalitiwa!”+ 23 Kwa hiyo wakaanza kuulizana ni nani kati yao ambaye kwa kweli ndiye angefanya hivyo.+
24 Hata hivyo, kukatokea pia bishano kali kati yao juu ya ni nani kati yao aliyeonekana kuwa mkuu zaidi ya wote.+ 25 Lakini akawaambia: “Wafalme wa mataifa hupiga ubwana juu yao, na wale walio na mamlaka juu yao huitwa Wafadhili.+ 26 Ingawa hivyo, ninyi hampaswi kuwa hivyo.+ Lakini acheni yule aliye mkuu zaidi ya wote kati yenu awe kama aliye mdogo zaidi ya wote,+ na yule anayetenda kama mkuu kama yule anayehudumu.+ 27 Kwa maana ni nani aliye mkuu zaidi, yule anayeketi mezani au yule anayehudumu? Je, si yule anayeketi mezani? Lakini mimi nimo katikati yenu kama yule anayehudumu.+
28 “Hata hivyo, ninyi ndio mmeshikamana+ nami katika majaribu yangu;+ 29 nami ninafanya agano pamoja nanyi, sawa na vile Baba yangu alivyofanya agano+ pamoja nami, kwa ajili ya ufalme,+ 30 ili mpate kula+ na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu,+ na kuketi juu ya viti vya ufalme+ kuyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
31 “Simoni, Simoni, tazama! Shetani+ amedai kuwapata ninyi ili awapepete kama ngano.+ 32 Lakini nimeomba dua+ kwa ajili yako ili imani yako isififie; na wewe, mara tu utakapokuwa umerudi, watie nguvu+ ndugu zako.” 33 Ndipo akamwambia: “Bwana, mimi niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani na pia katika kifo.”+ 34 Lakini akasema: “Ninakuambia wewe, Petro, Jogoo hatawika leo mpaka uwe umekana mara tatu kuwa hunijui.”+
35 Akawaambia wao pia: “Wakati nilipowatuma+ ninyi bila mkoba na mfuko wa chakula na viatu, je, mlikosa kitu chochote?” Wakasema: “Hapana!” 36 Ndipo akawaambia: “Lakini sasa acheni yule ambaye ana mkoba auchukue, vivyo hivyo pia mfuko wa chakula; na acheni yule asiye na upanga auze vazi lake la nje na kununua mmoja. 37 Kwa maana nawaambia ninyi kwamba lazima hili ambalo limeandikwa litimizwe kwangu, yaani, ‘Naye alihesabiwa pamoja na waasi-sheria.’+ Kwa maana kile kinachonihusu kinatimia.”+ 38 Ndipo wakasema: “Bwana, tazama! hapa pana panga mbili.” Akawaambia: “Inatosha.”
39 Alipotoka nje kama ilivyo desturi alienda kwenye Mlima wa Mizeituni; na wanafunzi pia wakamfuata.+ 40 Baada ya kufika hapo akawaambia: “Salini, ili msiingie katika jaribu.”+ 41 Naye mwenyewe akaondoka kwao karibu umbali wa mtupo wa jiwe, akapiga magoti na kuanza kusali, 42 akisema: “Baba, ikiwa unataka, niondolee kikombe hiki. Hata hivyo, acha, si mapenzi yangu,+ bali yako yatendeke.”+ 43 Ndipo malaika kutoka mbinguni akamtokea akamtia nguvu.+ 44 Lakini akaingia katika maumivu makali, akaendelea kusali kwa bidii zaidi;+ na jasho lake likawa kama matone ya damu yakianguka chini.+ 45 Naye akaondoka baada ya sala, akawaendea wanafunzi, akawakuta wakisinzia kwa huzuni;+ 46 naye akawaambia: “Kwa nini mnalala usingizi? Amkeni msali, ili msiingie katika jaribu.”+
47 Alipokuwa bado akisema, tazama! umati, na yule mtu anayeitwa Yuda, mmoja wa wale kumi na wawili, alikuwa akienda mbele yao;+ naye akamkaribia Yesu ili kumbusu.+ 48 Lakini Yesu akamwambia: “Yuda, je, wewe unamsaliti Mwana wa binadamu kwa busu?”+ 49 Wale waliokuwa kandokando yake walipoona jambo lililokuwa karibu kutukia, wakasema: “Bwana, je, tupige kwa upanga?”+ 50 Mtu fulani kati yao hata alimpiga mtumwa wa kuhani mkuu, akalikata sikio lake la kuume.+ 51 Lakini Yesu akajibu, akasema: “Basi, acheni, inatosha.” Naye akagusa sikio na kumponya.+ 52 Ndipo Yesu akawaambia wakuu wa makuhani na makapteni wa hekalu na wanaume wazee waliokuwa wamekuja hapo kumchukua: “Je, mlitoka mkiwa na mapanga na marungu kana kwamba ni juu ya mnyang’anyi?+ 53 Nilipokuwa pamoja nanyi katika hekalu+ siku baada ya siku hamkunyoosha mikono yenu ili kunikamata.+ Lakini hii ndiyo saa+ yenu na ndiyo mamlaka+ ya giza.”+
54 Ndipo wakamkamata, wakampeleka+ na kumwingiza katika nyumba ya kuhani mkuu;+ lakini Petro alikuwa akifuata kwa umbali fulani.+ 55 Walipowasha moto katikati ya ua na kuketi chini pamoja, Petro alikuwa ameketi katikati yao.+ 56 Lakini kijakazi fulani akamwona ameketi kando ya ule moto mwangavu akamtazama kwa kumchunguza na kusema: “Mtu huyu pia alikuwa pamoja naye.”+ 57 Lakini akakana,+ akisema: “Wee mwanamke, mimi simjui.”+ 58 Na baada ya muda mfupi mtu mwingine akamwona akasema: “Wewe pia ni mmoja wao.” Lakini Petro akasema: “Wee mtu, si mimi.”+ 59 Na baada ya karibu muda wa saa moja kupita mtu mwingine akaanza kusisitiza kwa nguvu: “Kwa hakika mtu huyu pia alikuwa pamoja naye; kwa maana, kwa kweli, yeye ni Mgalilaya!”+ 60 Lakini Petro akasema: “Wee mtu, mimi sijui unalosema.” Na mara tu, alipokuwa bado akisema, jogoo akawika.+ 61 Na Bwana akageuka, akamtazama Petro, na Petro akakumbuka maneno ya Bwana alipomwambia: “Kabla ya jogoo kuwika leo utanikana mara tatu.”+ 62 Naye akaenda nje akalia kwa uchungu.+
63 Sasa wale wanaume waliokuwa wakimlinda kifungoni wakaanza kumdhihaki,+ wakimpiga;+ 64 na baada ya kumfunika wakawa wakiuliza na kusema: “Toa unabii. Ni nani aliyekupiga?”+ 65 Nao wakaendelea kusema mambo mengine mengi ya kumkufuru.+
66 Hatimaye kulipokuwa mchana, kusanyiko la wanaume wazee wa watu, wakuu wa makuhani na waandishi pia, wakakusanyika pamoja,+ nao wakamkokota na kumwingiza ndani ya jumba lao la Sanhedrini, wakisema:+ 67 “Ikiwa wewe ndiye Kristo,+ tuambie.” Lakini akawaambia: “Hata kama ningewaambia, ninyi hamngeamini hata kidogo.+ 68 Zaidi ya hayo, kama ningewauliza ninyi, hamngejibu hata kidogo.+ 69 Hata hivyo, kutoka sasa na kuendelea Mwana wa binadamu+ atakuwa akiketi kwenye mkono wa kuume+ wenye nguvu wa Mungu.”+ 70 Ndipo wote wakasema: “Kwa hiyo, je, wewe ndiye Mwana wa Mungu?” Akawaambia: “Ninyi wenyewe mnasema+ kwamba mimi ndiye.” 71 Wakasema: “Kwa nini tunahitaji ushahidi zaidi?+ Kwa maana sisi wenyewe tumelisikia kutoka katika kinywa chake mwenyewe.”+
23 Kwa hiyo umati huo ukasimama, wote pamoja, na kumpeleka kwa Pilato.+ 2 Ndipo wakaanza kumshtaki,+ wakisema: “Tulimkuta mtu huyu akipindua+ taifa letu na kuwakataza watu wasimlipe Kaisari kodi+ na kusema kwamba yeye mwenyewe ni Kristo mfalme.”+ 3 Sasa Pilato akamuuliza: “Je, wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?” Akamjibu, akasema: “Wewe mwenyewe unasema.”+ 4 Ndipo Pilato akawaambia wakuu wa makuhani na ule umati: “Mimi sioni uhalifu wa mtu huyu.”+ 5 Lakini wao wakaanza kusisitiza, wakisema: “Yeye huwachochea watu kwa kufundisha katika Yudea yote, hata kuanzia Galilaya mpaka hapa.” 6 Aliposikia hilo, Pilato akauliza kama mtu huyo alikuwa Mgalilaya, 7 na, baada ya kuhakikisha kwamba alikuwa wa kutoka eneo la utawala wa Herode,+ akampeleka kwa Herode, ambaye yeye mwenyewe pia alikuwa katika Yerusalemu siku hizo.
8 Herode alipomwona Yesu alishangilia sana, kwa maana kwa muda mrefu alikuwa akitaka kumwona+ kwa sababu alikuwa amesikia+ juu yake, na alikuwa akitumaini kuona ishara fulani kutoka kwake. 9 Sasa akaanza kumuuliza maswali kwa maneno mengi sana; lakini yeye hakumjibu.+ 10 Hata hivyo, wakuu wa makuhani na waandishi wakaendelea kusimama na kumshtaki kwa ukali.+ 11 Ndipo Herode pamoja na askari-jeshi wake walinzi wakamfedhehesha,+ naye akamdhihaki+ kwa kumvika vazi jangavu na kumrudisha kwa Pilato. 12 Wote wawili Herode na Pilato+ sasa wakawa marafiki siku ileile; kwa maana kabla ya hapo walikuwa na uadui kati yao wenyewe.
13 Ndipo Pilato akawaita pamoja wakuu wa makuhani na watawala na watu 14 na kuwaambia: “Mliniletea mtu huyu kama mtu anayewachochea watu waasi, na, tazameni! mimi nilimhoji mbele yenu lakini sikupata katika mtu huyu msingi+ wa mashtaka mnayoleta juu yake. 15 Kwa kweli, wala Herode hakupata, kwa maana alimrudisha kwetu; na, tazama! hajafanya lolote linalostahili kifo.+ 16 Kwa hiyo nitamwadhibu+ na kumfungua.” 17 —— 18 Lakini wakiwa pamoja na umati, wao wote wakapaaza sauti, wakisema: “Mwondolee mbali huyu,+ lakini tufungulie Baraba!”+ 19 (Huyo ni mtu aliyekuwa ametupwa gerezani kwa sababu ya uchochezi wa uasi fulani uliotukia katika jiji na kwa kuua.) 20 Tena Pilato akawapaazia sauti, kwa sababu alitaka kumfungua Yesu.+ 21 Ndipo wakaanza kupiga kelele, wakisema: “Mtundike mtini! Mtundike mtini!”+ 22 Mara ya tatu akawaambia: “Kwa nini, ni jambo gani baya alilofanya mtu huyu? Mimi sikuona jambo lolote linalostahili kifo ndani yake; kwa hiyo nitamwadhibu na kumfungua.”+ 23 Ndipo wakaanza kufanya haraka-haraka, kwa sauti zilizo kubwa, wakidai kwamba atundikwe mtini; na sauti zao zikaanza kushinda.+ 24 Kwa hiyo Pilato akatoa hukumu ili dai lao litimizwe:+ 25 akamfungua+ yule mtu aliyekuwa ametupwa gerezani kwa uchochezi wa uasi na kuua na ambaye wao walikuwa wakidai, lakini akamtia Yesu mikononi mwao wamtendee wanavyopenda.+
26 Sasa walipokuwa wakimpeleka, walimshika Simoni, mzaliwa wa Kirene, akija kutoka mashambani, nao wakamtwika mti wa mateso aubebe nyuma ya Yesu.+ 27 Lakini kulikuwa na umati mkubwa wa watu na wa wanawake ambao walimfuata waliokuwa wakijipiga-piga kwa huzuni na kumwombolezea. 28 Yesu akawageukia wanawake hao na kusema: “Binti za Yerusalemu, acheni kunililia. Badala yake, jililieni ninyi wenyewe na watoto wenu;+ 29 kwa sababu, tazameni! siku zinakuja ambapo watu watasema, ‘Wenye furaha ni wanawake walio tasa, na matumbo ya uzazi ambayo hayakuzaa na maziwa ambayo hayakunyonyesha!’+ 30 Ndipo watakapoanza kuiambia milima, ‘Tuangukieni!’ na vilima, ‘Tufunikeni!’+ 31 Kwa sababu ikiwa wao wanafanya mambo haya wakati mti ni mbichi, itakuwaje utakapokuwa umekauka?”+
32 Lakini watu wengine wawili, watenda-maovu, walikuwa pia wakipelekwa wakauawe pamoja naye.+ 33 Nao walipofika mahali panapoitwa Fuvu la Kichwa,+ huko wakamtundika mtini yeye na wale watenda-maovu, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wake wa kushoto.+ 34 [[Lakini Yesu alikuwa akisema: “Baba, wasamehe,+ kwa maana hawajui wanalofanya.”]] Zaidi ya hayo, ili kugawa mavazi yake, wakapiga kura.+ 35 Na wale watu wakasimama wakitazama.+ Lakini wale watawala walikuwa wakicheka kwa dharau, wakisema:+ “Aliwaokoa wengine; mwacheni ajiokoe mwenyewe, ikiwa huyu ndiye Kristo wa Mungu, Yule Aliyechaguliwa.”+ 36 Hata wale askari wakamdhihaki,+ wakija karibu na kumpa divai kali+ 37 na kusema: “Ikiwa wewe ndiye mfalme wa Wayahudi, jiokoe mwenyewe.” 38 Kulikuwa pia na maandishi juu yake: “Huyu ndiye mfalme wa Wayahudi.”+
39 Lakini mmoja wa wale watenda-maovu waliotundikwa akaanza kumwambia kwa maneno ya matusi:+ “Wewe ndiye Kristo, sivyo? Jiokoe mwenyewe na sisi.” 40 Yule mwingine akamjibu, akamkemea na kusema: “Je, wewe humwogopi Mungu hata kidogo, kwa kuwa sasa umo katika hukumu ileile?+ 41 Nasi, kwa kweli, tuko hivyo kwa haki, kwa maana sisi tunapokea kwa ukamili kile tunachostahili kwa mambo tuliyofanya; lakini mtu huyu hakufanya jambo lolote lisilofaa.”+ 42 Naye akaendelea kusema: “Yesu, unikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.”+ 43 Naye akamwambia: “Kwa kweli mimi nakuambia leo, Utakuwa pamoja nami+ katika Paradiso.”+
44 Basi, kufikia sasa ilikuwa karibu saa sita, na hata hivyo kukawa na giza juu ya dunia yote mpaka saa tisa,+ 45 kwa sababu nuru ya jua ilikosekana; ndipo pazia+ la patakatifu likapasuka katikati.+ 46 Na Yesu akaita kwa sauti kubwa na kusema: “Baba, ninaikabidhi roho yangu mikononi mwako.”+ Alipokuwa amesema jambo hilo, akakata pumzi.+ 47 Kwa sababu ya kuona lililokuwa limetukia yule ofisa-jeshi akaanza kumtukuza Mungu, akisema: “Kwa kweli mtu huyu alikuwa mwadilifu.”+ 48 Na umati wote uliokuwa umekusanyika pamoja hapo kwa ajili ya tukio hilo, walipoyaona mambo yaliyotukia, wakaanza kurudi, wakipiga-piga vifua vyao. 49 Zaidi ya hayo, wale wote waliojuana naye walikuwa wamesimama umbali fulani.+ Pia, wanawake, waliokuwa wamemfuata pamoja kutoka Galilaya, walikuwa wamesimama wakiona mambo haya.+
50 Na, tazama! mwanamume aliyeitwa Yosefu, ambaye alikuwa mshiriki wa Baraza, mtu mwema na mwadilifu+— 51 mtu huyu hakuwa amepiga kura katika kuunga mkono mbinu yao na tendo+—alikuwa wa kutoka Arimathea, jiji moja la Wayudea, naye alikuwa akiungojea ufalme wa Mungu;+ 52 mtu huyu alimwendea Pilato na kuomba apewe mwili wa Yesu.+ 53 Naye akaushusha+ na kuufunga katika kitani bora, naye akamlaza katika kaburi+ lililochongwa katika mwamba, ambamo hakuna mtu aliyepata kulazwa.+ 54 Sasa ilikuwa ni siku ya Matayarisho,+ na nuru ya jioni ya siku ya sabato+ ilikuwa ikikaribia. 55 Lakini wale wanawake, waliokuwa wamekuja pamoja naye kutoka Galilaya, wakafuata, wakalitazama kaburi+ na jinsi mwili wake ulivyolazwa;+ 56 nao wakarudi kutayarisha manukato na mafuta yaliyotiwa marashi.+ Lakini, bila shaka, walipumzika siku ya sabato+ kulingana na amri.
24 Hata hivyo, siku ya kwanza ya juma walienda mapema sana kwenye kaburi, wakichukua yale manukato waliyokuwa wametayarisha.+ 2 Lakini wakapata jiwe limeviringishwa kutoka kwenye kaburi,+ 3 nao walipoingia hawakuupata mwili wa Bwana Yesu.+ 4 Walipokuwa wakifadhaika juu ya hilo, tazama! wanaume wawili waliovaa mavazi yenye kung’aa wakasimama kando yao.+ 5 Kwa kuwa hao wanawake waliogopa sana na kuinamisha nyuso zao chini, wale wanaume wakawaambia: “Kwa nini mnatafuta yule Aliye hai kati ya wafu? 6 [[Hayupo hapa, bali amefufuliwa.]]+ Kumbukeni jinsi alivyowaambia alipokuwa angali katika Galilaya,+ 7 akisema kwamba Mwana wa binadamu lazima atiwe mikononi mwa watu wenye dhambi na kutundikwa mtini na bado siku ya tatu afufuliwe.”+ 8 Kwa hiyo wakakumbuka+ maneno yake, 9 nao wakarudi kutoka kwenye kaburi wakawapa habari ya mambo hayo yote wale kumi na mmoja na wale wengine wote.+ 10 Walikuwa Magdalene Maria, na Yoana,+ na Maria mama ya Yakobo. Pia, wengine kati ya wanawake+ waliokuwa pamoja nao walikuwa wakiwaeleza mitume mambo hayo. 11 Hata hivyo, maneno hayo yalionekana kama upuuzi kwao nao wakawa hawawaamini+ wanawake hao.
12 [[Lakini Petro akaondoka, akakimbia kwenda kwenye kaburi, akainama mbele, akaona vile vitambaa peke yake. Kwa hiyo akaenda zake, akistaajabu ndani yake mwenyewe juu ya lililokuwa limetukia.]]
13 Lakini, tazama! siku ileile wawili kati yao walikuwa safarini kwenda kijiji kilicho umbali wa karibu kilometa kumi na moja kutoka Yerusalemu na kinachoitwa Emau, 14 nao walikuwa wakiongea pamoja juu ya mambo yote haya+ yaliyokuwa yametukia.
15 Sasa walipokuwa wakiongea na kujadiliana, Yesu akakaribia,+ akaanza kutembea pamoja nao; 16 lakini macho yao yalizuiwa wasiweze kumtambua.+ 17 Akawaambia: “Ni mambo gani haya ambayo mnajadiliana kati yenu wenyewe mnapotembea?” Nao wakasimama tuli wakiwa na nyuso zenye huzuni. 18 Yule aliyeitwa Kleopa akajibu, akamwambia: “Je, wewe unakaa peke yako kama mgeni katika Yerusalemu na kwa hiyo huyajui mambo ambayo yametukia humo siku hizi?” 19 Naye akawaambia: “Mambo gani?” Wakamwambia: “Yale mambo kuhusu Yesu Mnazareti,+ aliyekuwa nabii+ mwenye nguvu katika kazi na neno mbele za Mungu na watu wote; 20 na jinsi wakuu wa makuhani wetu na watawala walivyomkabidhi kwenye hukumu ya kifo na kumtundika mtini.+ 21 Lakini sisi tulikuwa tukitumaini kwamba mtu huyu ndiye angekomboa Israeli;+ ndiyo, na mbali na mambo yote haya, hii ndiyo siku ya tatu tangu mambo hayo yalipotukia. 22 Zaidi ya hayo, wanawake+ fulani kutoka kati yetu walitushangaza pia, kwa sababu walikuwa wamefika mapema kwenye kaburi 23 lakini hawakuupata mwili wake nao wakaja wakisema walikuwa pia wameona maono ya malaika yanayozidi nguvu za asili, waliosema kwamba yeye yuko hai. 24 Na zaidi, baadhi ya hao walio pamoja nasi walienda kwenye kaburi;+ nao wakalikuta hivyo, kama vile wale wanawake walivyokuwa wamesema, lakini hawakumwona.”
25 Kwa hiyo akawaambia: “Enyi wasio na akili na wazito katika moyo kuyaamini mambo yote waliyosema manabii!+ 26 Je, haikuwa lazima Kristo kupatwa+ na mambo haya na kuingia katika utukufu wake?”+ 27 Naye akaanzia Musa+ na Manabii+ wote, akawafasiria mambo yanayomhusu yeye mwenyewe katika Maandiko yote.
28 Mwishowe wakaja karibu na kijiji walikokuwa wakienda, naye akajifanya kana kwamba alikuwa akisafiri kwenda mbali zaidi. 29 Lakini wakamkaza, wakisema: “Kaa pamoja nasi, kwa sababu jioni imekaribia na mchana tayari umekwisha.” Ndipo akaingia akae pamoja nao. 30 Naye alipokuwa ameketi pamoja nao kwenye mlo akauchukua mkate, akaubariki, akaumega na kuanza kuwapa.+ 31 Ndipo macho yao yakafunguliwa kikamili nao wakamtambua; naye akatoweka kutoka kwao.+ 32 Nao wakaambiana: “Je, mioyo yetu haikuwa ikiwaka alipokuwa akisema nasi barabarani, alipokuwa akitufungulia Maandiko?” 33 Na saa ileile wakaondoka, wakarudi Yerusalemu, nao wakawakuta wale kumi na mmoja na wale walio pamoja nao wamekusanyika pamoja, 34 wakisema: “Kwa kweli Bwana alifufuliwa naye alimtokea Simoni!”+ 35 Sasa wao wenyewe wakasimulia yale matukio barabarani na jinsi walivyopata kumjua kwa kule kuumega mkate.+
36 Walipokuwa wakisema juu ya mambo hayo yeye mwenyewe akasimama katikati yao [[na kuwaambia: “Na muwe na amani.”]] 37 Lakini kwa sababu wao walikuwa wameogopa,+ na walikuwa na hofu sana, walikuwa wakiwazia wameona roho. 38 Kwa hiyo akawaambia: “Kwa nini mnafadhaika, na kwa nini shaka zinatokea mioyoni mwenu? 39 Oneni mikono na miguu yangu, kwamba ni mimi mwenyewe; niguseni+ mwone, kwa sababu roho haina nyama na mifupa+ kama vile mnavyoniona nilivyo.” 40 [[Naye alipokuwa akisema hilo akawaonyesha mikono yake na miguu yake.]] 41 Lakini walipokuwa bado hawaamini+ kwa ajili ya shangwe tupu na wakiwa wamestaajabu, akawaambia: “Je, mna chakula hapo?”+ 42 Nao wakampa kipande cha samaki wa kuchomwa;+ 43 naye akakichukua, akala+ mbele ya macho yao.
44 Sasa akawaambia: “Haya ndiyo maneno yangu niliyowaambia nilipokuwa ningali pamoja nanyi,+ kwamba mambo yote yaliyoandikwa katika sheria ya Musa na katika Manabii+ na Zaburi+ juu yangu lazima yatimizwe.” 45 Ndipo akafungua akili zao ili kuifahamu maana ya Maandiko,+ 46 naye akawaambia: “Katika njia hii imeandikwa kwamba Kristo angeteseka na kufufuliwa kutoka kati ya wafu siku ya tatu,+ 47 na kwa msingi wa jina lake toba kwa msamaha wa dhambi+ ingehubiriwa katika mataifa yote+—kuanzia Yerusalemu,+ 48 ninyi mnapaswa kuwa mashahidi+ wa mambo haya. 49 Na, tazameni! ninatuma juu yenu kile ambacho kimeahidiwa na Baba yangu. Ingawa hivyo, ninyi kaeni katika jiji mpaka mvikwe nguvu kutoka juu.”+
50 Lakini akawaongoza waende mpaka Bethania, naye akainua mikono yake na kuwabariki.+ 51 Alipokuwa akiwabariki akatenganishwa nao, akaanza kuchukuliwa juu mbinguni.+ 52 Nao wakamsujudia na kurudi Yerusalemu kwa shangwe kubwa.+ 53 Nao sikuzote walikuwa katika hekalu wakimbariki Mungu.+
[Maelezo ya Chini]
Hadesi. Tazama Nyongeza 4.
Bonde la Hinomu. Tazama Nyongeza 2.
Hadesi. Tazama Nyongeza 4.