Kulingana na Yohana
1 Hapo mwanzo+ Neno+ alikuwako, na Neno alikuwa pamoja na Mungu,+ na Neno alikuwa mungu.+ 2 Hapo mwanzo+ huyo alikuwa pamoja na Mungu.+ 3 Vitu vyote vilikuja kuwako kupitia kwake,+ na bila yeye hakuna hata kitu kimoja kilichokuja kuwako.
Kile ambacho kimekuja kuwako 4 kupitia kwake kilikuwa uzima,+ na uzima ndio uliokuwa nuru+ ya wanadamu. 5 Na nuru inang’aa katika giza,+ lakini giza halijaizidi nguvu.
6 Kulitokea mtu aliyetumwa awe mwakilishi wa Mungu:+ jina lake lilikuwa Yohana.+ 7 Mtu huyo alikuja kwa ajili ya ushahidi, ili atoe ushahidi+ juu ya nuru,+ kusudi watu wa namna zote wapate kuamini kupitia kwake.+ 8 Yeye hakuwa nuru hiyo,+ bali alikusudiwa atoe ushahidi+ juu ya nuru hiyo.
9 Nuru+ ya kweli ambayo humpa nuru+ mtu wa kila namna,+ ilikuwa karibu kuja ulimwenguni. 10 Alikuwa ulimwenguni,+ nao ulimwengu ulikuja kuwako kupitia kwake,+ lakini ulimwengu haukumjua. 11 Alikuja nyumbani kwake mwenyewe, lakini watu wake mwenyewe hawakumkaribisha.+ 12 Hata hivyo, wengi kadiri ileile waliompokea,+ aliwapa mamlaka ya kuwa watoto wa Mungu,+ kwa sababu walikuwa wakionyesha imani katika jina lake;+ 13 nao walizaliwa, si kutokana na damu au kutokana na mapenzi ya mwili au kutokana na mapenzi ya mwanadamu, bali kutokana na Mungu.+
14 Kwa hiyo Neno akawa mwili,+ akakaa katikati yetu, nasi tukautazama utukufu wake, utukufu kama ule ulio wa mwana mzaliwa-pekee+ kutoka kwa baba; naye alikuwa amejaa fadhili nyingi zisizostahiliwa na kweli.+ 15 (Yohana alitoa ushahidi juu yake, ndiyo, kwa kweli alipaaza sauti—huyu ndiye aliyesema hilo—akisema: “Yule anayekuja nyuma yangu amekwenda mbele yangu, kwa sababu alikuwako kabla yangu.”)+ 16 Kwa maana sisi sote tulipokea kutokana na wingi alio nao,+ hata fadhili zisizostahiliwa juu ya fadhili zisizostahiliwa.+ 17 Kwa sababu Sheria ilitolewa kupitia Musa,+ fadhili zisizostahiliwa+ na kweli+ zilikuja kupitia Yesu Kristo. 18 Hakuna mwanadamu ambaye amemwona Mungu wakati wowote;+ mungu mzaliwa-pekee+ aliye kifuani+ pa Baba, ndiye ambaye ameeleza juu yake.+
19 Basi huu ndio ushahidi wa Yohana wakati Wayahudi walipowatuma makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu wakamuulize: “Wewe ni nani?”+ 20 Naye alikiri wala hakukana, bali akakiri: “Mimi siye Kristo.”+ 21 Nao wakamuuliza: “Wewe ni nani, basi? Je, wewe ndiye Eliya?”+ Naye akasema: “Mimi siye.” “Je, wewe ndiye Yule Nabii?”+ Naye akajibu: “Hapana!” 22 Kwa hiyo wakamwambia: “Wewe ni nani? ili tupate kuwajibu wale waliotutuma. Unasema nini juu yako mwenyewe?”+ 23 Akasema: “Mimi ni sauti ya mtu anayepaaza sauti nyikani, ‘Nyoosheni njia ya Yehova,’ kama vile nabii Isaya alivyosema.”+ 24 Sasa wale waliotumwa walikuwa wametoka kwa Mafarisayo. 25 Kwa hiyo walimuuliza na kumwambia: “Kwa nini, basi, unabatiza+ ikiwa wewe mwenyewe siye Kristo au Eliya au Yule Nabii?” 26 Yohana akawajibu, akisema: “Mimi ninabatiza katika maji. Kuna mmoja ambaye amesimama katikati+ yenu msiyemjua,+ 27 yule anayekuja nyuma yangu, lakini ambaye kamba ya kiatu chake sistahili kuifungua.”+ 28 Mambo hayo yalitendeka Bethania ng’ambo ya Yordani, ambako Yohana alikuwa akibatizia.+
29 Siku iliyofuata alimwona Yesu akimjia, naye akasema: “Ona, Mwana-Kondoo+ wa Mungu ambaye huondolea mbali dhambi+ ya ulimwengu!+ 30 Huyu ndiye niliyesema juu yake, Nyuma yangu anakuja mwanamume ambaye yuko mbele yangu, kwa sababu alikuwako kabla yangu.+ 31 Hata sikumjua, lakini nilikuja nikibatiza katika maji ili apate kufunuliwa kwa Israeli.”+ 32 Yohana pia alitoa ushahidi, akisema: “Niliona roho ikishuka kama njiwa kutoka mbinguni, nayo ikakaa juu yake.+ 33 Hata sikumjua, bali Yule aliyenituma+ nibatize katika maji aliniambia, ‘Yeyote yule ambaye utaona roho ikishuka na kukaa juu yake, huyo ndiye ambaye hubatiza katika roho takatifu.’+ 34 Nami nimeona, na nimetoa ushahidi kwamba huyo ndiye Mwana wa Mungu.”+
35 Tena siku iliyofuata Yohana alikuwa amesimama na wawili kati ya wanafunzi wake, 36 na alipomtazama Yesu akitembea akasema: “Ona, Mwana-Kondoo+ wa Mungu!” 37 Na wanafunzi hao wawili wakamsikia akisema, nao wakamfuata Yesu. 38 Ndipo Yesu akageuka na, alipowaona wakimfuata, akawaambia: “Mnatafuta nini?” Wakamwambia: “Rabi, (ambalo linapotafsiriwa humaanisha, Mwalimu,) unakaa wapi?” 39 Akawaambia: “Njooni, nanyi mtaona.”+ Basi wakaenda wakaona ni wapi alikokuwa akikaa, nao wakakaa pamoja naye siku hiyo; ilikuwa karibu saa kumi. 40 Andrea+ ndugu ya Simoni Petro alikuwa mmoja kati ya wale wawili waliosikia aliyoyasema Yohana nao wakamfuata Yesu. 41 Kwanza huyu alimpata ndugu yake mwenyewe, Simoni, na kumwambia: “Tumempata Masihi”+ (ambalo linapotafsiriwa humaanisha, Kristo).+ 42 Akampeleka kwa Yesu. Yesu alipomtazama+ akasema: “Wewe ni Simoni+ mwana wa Yohana;+ utaitwa Kefa” (ambalo linatafsiriwa Petro).+
43 Siku iliyofuata alitamani kuondoka kwenda Galilaya. Kwa hiyo Yesu akamkuta Filipo+ na kumwambia: “Uwe mfuasi wangu.”+ 44 Basi Filipo alikuwa mtu wa Bethsaida,+ kutoka jiji la Andrea na Petro. 45 Filipo akamkuta Nathanaeli+ na kumwambia: “Tumempata yule ambaye Musa, katika Sheria,+ na Manabii,+ aliandika juu yake, Yesu, mwana wa Yosefu,+ kutoka Nazareti.” 46 Lakini Nathanaeli akamwambia: “Je, kitu chochote kilicho chema kinaweza kutoka Nazareti?”+ Filipo akamwambia: “Njoo uone.” 47 Yesu akamwona Nathanaeli akimjia na kusema juu yake: “Ona, Mwisraeli kwa uhakika, ambaye hamna udanganyifu ndani yake.”+ 48 Nathanaeli akamwambia: “Umepataje kunijua?” Yesu akajibu, akamwambia: “Kabla ya Filipo kukuita, ulipokuwa chini ya mtini, nilikuona.” 49 Nathanaeli akamjibu: “Rabi, wewe ndiye Mwana wa Mungu,+ wewe ndiye Mfalme+ wa Israeli.” 50 Yesu akajibu, akamwambia: “Je, unaamini kwa sababu nilikuambia nilikuona chini ya mtini? Utaona mambo makubwa zaidi kuliko haya.” 51 Akazidi kumwambia: “Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, Mtaona mbingu imefunguliwa na malaika+ za Mungu wakipanda na kushuka mpaka kwa Mwana wa binadamu.”+
2 Basi siku ya tatu kulikuwa na karamu ya ndoa katika Kana+ ya Galilaya, na mama+ ya Yesu alikuwa huko. 2 Yesu na wanafunzi wake walialikwa pia kwenye karamu hiyo ya ndoa.
3 Divai ilipopungua mama+ ya Yesu akamwambia: “Hawana divai.” 4 Lakini Yesu akamwambia: “Nina nini nawe, mwanamke?+ Saa yangu haijafika bado.”+ 5 Mama yake akawaambia wale wenye kuhudumia: “Lolote atakalowaambia, fanyeni.”+ 6 Kama ilivyokuwa, kulikuwako mitungi sita ya maji ikiwa imekaa hapo kulingana na kanuni za utakaso+ za Wayahudi, kila mmoja ukiwa unaweza kuchukua vipimo viwili au vitatu vya maji. 7 Yesu akawaambia: “Ijazeni maji mitungi ya maji.” Nao wakaijaza pomoni. 8 Akawaambia: “Choteni kiasi fulani sasa na kumpelekea msimamizi wa karamu.” Kwa hiyo wakayapeleka. 9 Basi, msimamizi wa karamu alipoyaonja maji yaliyokuwa yamegeuzwa kuwa divai,+ lakini hakujua chanzo chake, ijapokuwa wale wenye kuhudumia waliokuwa wamechota hayo maji walijua, msimamizi wa karamu akamwita bwana-arusi 10 na kumwambia: “Wengine wote hutoa divai nzuri kwanza,+ na ile hafifu wakati ambapo watu wameingiwa na kileo. Wewe umehifadhi divai nzuri mpaka sasa.” 11 Yesu alifanya jambo hilo katika Kana ya Galilaya likiwa mwanzo wa ishara zake, naye akaufunua utukufu+ wake; na wanafunzi wake wakamwamini.
12 Baada ya hayo, yeye na mama yake na ndugu zake+ na wanafunzi wake wakashuka kwenda Kapernaumu,+ lakini hawakukaa huko siku nyingi.
13 Basi pasaka+ ya Wayahudi ilikuwa karibu, na Yesu akapanda kwenda Yerusalemu.+ 14 Naye akakuta hekaluni wale waliokuwa wakiuza ng’ombe na kondoo na njiwa+ na waliokuwa wakivunja pesa wakiwa wameketi. 15 Kwa hiyo, baada ya kufanya mjeledi wa kamba, akawafukuza hekaluni wale wote wenye kondoo na ng’ombe, akamwaga sarafu za waliokuwa wakibadili pesa na kupindua meza zao.+ 16 Akawaambia wale waliokuwa wakiuza njiwa: “Ondoeni vitu hivi kutoka hapa! Acheni kuifanya nyumba+ ya Baba yangu kuwa nyumba ya biashara!”+ 17 Wanafunzi wake wakakumbuka kwamba imeandikwa: “Bidii kwa ajili ya nyumba yako itanila.”+
18 Kwa hiyo, Wayahudi wakajibu, wakamwambia: “Una ishara+ gani ya kutuonyesha, kwa kuwa unafanya mambo haya?” 19 Yesu akajibu, akawaambia: “Libomoeni hekalu+ hili, na katika siku tatu nitalisimamisha.” 20 Kwa hiyo Wayahudi wakasema: “Hekalu hili lilijengwa kwa miaka 46, nawe je, utalisimamisha katika siku tatu?” 21 Lakini alikuwa akiongea juu ya hekalu+ la mwili wake. 22 Ingawa hivyo, wakati alipofufuliwa kutoka kwa wafu, wanafunzi wake wakakumbuka+ kwamba alikuwa akisema hilo; nao wakaamini Andiko na maneno ambayo Yesu alisema.
23 Hata hivyo, wakati alipokuwa Yerusalemu kwenye pasaka, kwenye sherehe+ yake, watu wengi wakawa na imani katika jina lake,+ wakitazama ishara zake alizokuwa akifanya.+ 24 Lakini Yesu mwenyewe hakuwa akiwatumaini+ kwa sababu aliwajua wote 25 na kwa sababu hakuwa na uhitaji wa mtu yeyote kutoa ushahidi juu ya mwanadamu, kwa maana yeye mwenyewe alijua kile kilichokuwa ndani ya mwanadamu.+
3 Basi kulikuwa na mtu mmoja kati ya Mafarisayo, aliyeitwa Nikodemo,+ mtawala wa Wayahudi. 2 Huyo alimjia wakati wa usiku+ na kumwambia: “Rabi,+ tunajua kwamba wewe ukiwa mwalimu+ umekuja kutoka kwa Mungu;+ kwa maana hakuna anayeweza kufanya ishara+ hizi ambazo unafanya isipokuwa Mungu awe pamoja naye.”+ 3 Yesu akajibu akamwambia:+ “Kwa kweli kabisa ninakuambia, Mtu asipozaliwa tena,+ hawezi kuuona ufalme wa Mungu.”+ 4 Nikodemo akamwambia: “Mtu anawezaje kuzaliwa akiwa mzee? Je, anaweza kuingia katika tumbo la uzazi la mama yake mara ya pili na kuzaliwa?” 5 Yesu akajibu: “Kwa kweli kabisa ninakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji+ na roho,+ hawezi kuingia katika ufalme wa Mungu. 6 Kile ambacho kimezaliwa kwa mwili ni mwili, na kile ambacho kimezaliwa kwa roho ni roho.+ 7 Usistaajabu kwa sababu nimekuambia, Ninyi lazima mzaliwe tena.+ 8 Upepo+ huvuma mahali ambapo unataka, nawe unasikia mvumo wake, lakini hujui mahali ambapo huo unatoka wala mahali unapoenda. Ndivyo alivyo kila mtu ambaye amezaliwa kwa roho.”+
9 Nikodemo akajibu, akamwambia: “Mambo haya yanaweza kutukia jinsi gani?” 10 Yesu akajibu, akamwambia: “Je, wewe ni mwalimu wa Israeli na bado hujui mambo haya?+ 11 Kwa kweli kabisa ninakuambia, Yale tunayoyajua tunayasema na yale ambayo tumeyaona tunatoa ushahidi+ juu yake, lakini ninyi hampokei ushahidi ambao tunatoa.+ 12 Ikiwa nimewaambia ninyi mambo ya duniani na bado hamwamini, mtaamini jinsi gani nikiwaambia mambo ya mbinguni?+ 13 Zaidi ya hayo, hakuna mtu ambaye amepanda kuingia mbinguni+ ila yule aliyeshuka kutoka mbinguni,+ Mwana wa binadamu.+ 14 Na kama vile Musa alivyoinua nyoka+ nyikani, ndivyo Mwana wa binadamu atakavyoinuliwa,+ 15 ili kila mtu anayemwamini apate kuwa na uzima wa milele.+
16 “Kwa maana Mungu aliupenda+ ulimwengu sana hivi kwamba akamtoa Mwana wake mzaliwa-pekee,+ ili kila mtu anayemwamini+ asiangamizwe+ bali awe na uzima wa milele.+ 17 Kwa maana Mungu alimtuma Mwana wake ulimwenguni, si ili auhukumu+ ulimwengu, bali ili ulimwengu uokolewe+ kupitia kwake. 18 Yule anayemwamini hatahukumiwa.+ Yule ambaye hamwamini amehukumiwa tayari, kwa sababu hana imani katika jina la Mwana mzaliwa-pekee wa Mungu.+ 19 Basi huu ndio msingi wa hukumu, kwamba nuru+ imekuja ulimwenguni+ lakini watu wamelipenda giza kuliko nuru,+ kwa maana matendo yao yalikuwa maovu. 20 Kwa maana yule ambaye huzoea kufanya mambo maovu+ huchukia nuru na haji kwenye nuru, ili matendo yake yasipate kukaripiwa.+ 21 Lakini yule ambaye hufanya yaliyo ya kweli huja kwenye nuru,+ ili matendo yake yapate kufunuliwa kuwa tayari yamefanywa kupatana na Mungu.”
22 Baada ya mambo haya Yesu na wanafunzi wake wakaenda katika nchi ya Yudea, na huko akatumia wakati fulani pamoja nao naye alikuwa akibatiza.+ 23 Lakini Yohana+ pia alikuwa akibatiza katika Ainoni karibu na Salimu, kwa sababu kulikuwa na kiasi kikubwa cha maji+ huko, na watu wakawa wakija na kubatizwa;+ 24 kwa maana Yohana alikuwa hajatupwa gerezani bado.+
25 Kwa hiyo bishano likatokea kati ya wanafunzi wa Yohana na Myahudi mmoja kuhusu utakaso.+ 26 Kwa hiyo wakaja kwa Yohana na kumwambia: “Rabi, mtu aliyekuwa pamoja nawe ng’ambo ya Yordani, ambaye umetoa ushahidi+ juu yake, ona, huyu anabatiza na wote wanamwendea.”+ 27 Yohana akajibu, akasema: “Mtu hawezi kupokea hata kitu kimoja isipokuwa awe amepewa kutoka mbinguni.+ 28 Ninyi wenyewe mnanitolea ushahidi kwamba nilisema, Mimi siye Kristo,+ bali, nimetumwa kumtangulia huyo.+ 29 Yeye aliye na bibi-arusi ndiye bwana-arusi.+ Hata hivyo, rafiki ya bwana-arusi, anaposimama na kumsikia, ana shangwe nyingi sana kwa sababu ya sauti ya bwana-arusi. Kwa hiyo shangwe yangu hii imejazwa.+ 30 Lazima huyo aendelee kuongezeka, lakini mimi lazima niendelee kupungua.”
31 Yule anayekuja kutoka juu yuko juu ya wengine wote.+ Yule anayetoka duniani ni wa kutoka duniani na husema kuhusu mambo ya duniani.+ Yule anayekuja kutoka mbinguni yuko juu ya wengine wote.+ 32 Kile ambacho ameona na kusikia, yeye hutoa ushahidi juu yake,+ lakini hakuna mtu anayekubali ushahidi wake.+ 33 Yule ambaye ameukubali ushahidi wake ametia muhuri wake juu ya huo kwamba Mungu ni wa kweli.+ 34 Kwa maana yule ambaye Mungu amemtuma husema maneno ya Mungu,+ kwa maana hatoi roho kwa kipimio.+ 35 Baba humpenda Mwana+ naye ametia vitu vyote mkononi mwake.+ 36 Yule anayemwamini+ Mwana ana uzima wa milele;+ yule asiyemtii Mwana hataona uzima,+ bali ghadhabu ya Mungu hukaa juu yake.+
4 Basi, Bwana alipojua kwamba Mafarisayo walikuwa wamesikia kwamba Yesu alikuwa akifanya na kubatiza+ wanafunzi wengi kuliko Yohana— 2 ijapokuwa, kwa kweli, Yesu mwenyewe hakuwa akibatiza ila wanafunzi wake ndio waliokuwa wakibatiza— 3 aliondoka Yudea na kuelekea tena Galilaya. 4 Lakini ilikuwa lazima apitie Samaria.+ 5 Basi akaja mpaka jiji moja la Samaria linaloitwa Sikari karibu na shamba ambalo Yakobo alimpa Yosefu mwana wake.+ 6 Kwa kweli, chemchemi+ ya Yakobo ilikuwa hapo. Basi Yesu, kwa kuwa alikuwa amechoka kwa sababu ya safari hiyo, alikuwa ameketi kando ya chemchemi kama vile alivyokuwa. Ilikuwa karibu saa sita.
7 Mwanamke mmoja wa Samaria akaja kuteka maji. Yesu akamwambia: “Nipe maji ninywe.” 8 (Kwa maana wanafunzi wake walikuwa wameenda katika jiji kununua chakula.) 9 Kwa hiyo mwanamke huyo Msamaria akamwambia: “Wewe, ujapokuwa Myahudi, unawezaje kuniomba maji ya kunywa, na mimi ni mwanamke Msamaria?” (Kwa maana Wayahudi hawana shughuli na Wasamaria.)+ 10 Yesu akajibu, akamwambia: “Kama ungalijua zawadi+ ya bure inayotoka kwa Mungu, na ni nani+ ambaye anakuambia, ‘Nipe maji ninywe,’ ungalimwomba, naye angalikupa maji yaliyo hai.”+ 11 Akamwambia: “Bwana, huna hata ndoo ya kutekea maji, na kisima ni kirefu. Kwa hiyo, umeyatoa wapi maji hayo yaliyo hai? 12 Je, wewe ni mkuu+ kuliko babu yetu Yakobo, ambaye alitupa kisima hiki na ambaye yeye mwenyewe pamoja na wanawe na mifugo yake walikunywa maji yake?” 13 Yesu akajibu, akamwambia: “Kila mtu anayekunywa maji haya atapatwa na kiu tena. 14 Yule atakayekunywa maji ambayo nitampa hatapatwa na kiu hata kidogo,+ lakini maji ambayo nitampa yatakuwa chemchemi ya maji+ ndani yake, inayobubujika ili kutokeza uzima wa milele.”+ 15 Huyo mwanamke akamwambia: “Bwana, nipe maji hayo, ili nisiwe na kiu wala nisiendelee kuja hapa kuteka maji.”
16 Akamwambia: “Nenda, ukamwite mume wako mje hapa.” 17 Mwanamke huyo akajibu akasema: “Sina mume.” Yesu akamwambia: “Umesema vema, ‘Sina mume.’ 18 Kwa maana umekuwa na waume watano, na mwanamume uliye naye sasa si mume wako. Hapo umesema kweli.” 19 Huyo mwanamke akamwambia: “Bwana, ninaona kwamba wewe ni nabii.+ 20 Mababu zetu waliabudu katika mlima huu;+ lakini ninyi husema kwamba Yerusalemu ndipo mahali ambapo watu wanapaswa kuabudia.”+ 21 Yesu akamwambia: “Niamini mimi, mwanamke, Saa inakuja wakati ambapo mtamwabudu+ Baba si katika mlima huu wala kule Yerusalemu.+ 22 Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tunachokijua,+ kwa sababu wokovu hutokana na Wayahudi.+ 23 Hata hivyo, saa inakuja, nayo ipo sasa, wakati ambapo waabudu wa kweli watamwabudu Baba kwa roho+ na kweli,+ kwa maana, kwa kweli, Baba anawatafuta watu wa namna hiyo wamwabudu.+ 24 Mungu ni Roho,+ na wale wanaomwabudu lazima wamwabudu kwa roho na kweli.”+ 25 Huyo mwanamke akamwambia: “Ninajua kwamba Masihi+ anakuja, anayeitwa Kristo.+ Atakapofika, atatujulisha mambo yote waziwazi.” 26 Yesu akamwambia: “Mimi ninayesema nawe ndiye.”+
27 Ndipo wanafunzi wake wakafika, nao wakaanza kustaajabu kwa sababu alikuwa akisema na mwanamke. Bila shaka, hakuna yeyote aliyesema: “Unatafuta nini?” au, “Kwa nini unaongea naye?” 28 Kwa hiyo, mwanamke huyo akauacha mtungi wake wa maji akaenda zake jijini na kuwaambia watu: 29 “Njooni hapa, mwone mtu aliyeniambia mambo yote niliyofanya. Je, huyu labda ndiye Kristo?”+ 30 Wakatoka jijini na kumwendea.
31 Wakati huohuo wanafunzi walikuwa wakimhimiza, wakisema: “Rabi,+ kula.” 32 Lakini akawaambia: “Mimi nina chakula ambacho hamkijui.” 33 Kwa hiyo wanafunzi wakaanza kusemezana: “Je, kuna mtu ambaye amemletea chakula chochote?” 34 Yesu akawaambia: “Chakula+ changu ni mimi kufanya mapenzi+ yake aliyenituma na kuimaliza kazi yake.+ 35 Je, ninyi hamsemi kwamba bado kuna miezi minne kabla ya mavuno kuja? Tazama! Ninawaambia ninyi: Inueni macho yenu myatazame mashamba, kwamba ni meupe kwa ajili ya kuvunwa.+ Tayari 36 mvunaji anapokea mshahara na kukusanya matunda kwa ajili ya uzima wa milele,+ ili mpandaji+ na mvunaji wapate kushangilia pamoja.+ 37 Katika habari hii, kwa kweli, maneno haya ni kweli, Mpandaji ni mmoja na mvunaji ni mwingine. 38 Niliwatuma ninyi mkavune kile ambacho hamkufanyia kazi. Wengine wamefanya kazi,+ nanyi mmeingia katika faida ya kazi yao.”
39 Sasa wengi wa Wasamaria kutoka jiji hilo walimwamini+ kwa sababu ya neno la yule mwanamke aliyesema hivi kwa ushahidi: “Aliniambia mambo yote niliyofanya.”+ 40 Kwa hiyo Wasamaria walipomjia, wakaanza kumwomba akae pamoja nao; naye akakaa huko siku mbili.+ 41 Kwa hiyo wengi zaidi wakaamini kwa ajili ya aliyoyasema,+ 42 nao wakaanza kumwambia yule mwanamke: “Hatuamini tena kwa sababu ya maneno yako; kwa maana sisi wenyewe+ tumesikia nasi tunajua kwamba mtu huyu kwa hakika ndiye mwokozi+ wa ulimwengu.”
43 Baada ya hizo siku mbili akaondoka huko kwenda Galilaya.+ 44 Hata hivyo, Yesu alitoa ushahidi kwamba nabii hapati heshima katika nchi yake mwenyewe.+ 45 Kwa hiyo, alipofika Galilaya, Wagalilaya wakampokea, kwa sababu walikuwa wameona mambo yote aliyofanya Yerusalemu kwenye sherehe,+ kwa maana wao pia walikuwa wameenda kwenye sherehe.+
46 Basi akaja tena mpaka Kana+ ya Galilaya, ambako alikuwa amegeuza maji yakawa divai.+ Basi kulikuwako mtumishi fulani wa mfalme ambaye mwana wake alikuwa mgonjwa katika Kapernaumu.+ 47 Mtu huyu aliposikia kwamba Yesu alikuwa amekuja kutoka Yudea kuingia Galilaya, akamwendea na kuanza kumwomba ashuke ili amponye mwana wake, kwa maana alikuwa karibu kufa. 48 Hata hivyo, Yesu akamwambia: “Msipoona ishara+ na maajabu,+ hamtaamini kamwe.” 49 Mtumishi wa mfalme akamwambia: “Bwana, shuka uje kabla mtoto wangu mchanga hajafa.” 50 Yesu akamwambia: “Shika njia uende zako;+ mwana wako yuko hai.”+ Yule mtu akaliamini neno ambalo Yesu alikuwa amemwambia, akashika njia na kwenda zake. 51 Lakini tayari alipokuwa akishuka kwenda zake watumwa wake wakakutana naye ili kusema kwamba mvulana wake alikuwa hai.+ 52 Kwa hiyo akaanza kuwauliza saa ambayo alipata nafuu. Basi wakamwambia: “Jana saa saba homa+ ilimwacha.” 53 Kwa hiyo yule baba akajua ilikuwa saa+ ileile ambayo Yesu alimwambia: “Mwana wako yuko hai.” Kisha yeye na watu wote wa nyumbani mwake wakaamini.+ 54 Tena hiyo ilikuwa ndiyo ishara+ ya pili aliyoifanya Yesu alipokuja kutoka Yudea na kuingia Galilaya.
5 Baada ya mambo hayo kulikuwa na sherehe+ ya Wayahudi, na Yesu akapanda kwenda Yerusalemu. 2 Sasa katika Yerusalemu kwenye lango la kondoo+ kuna dimbwi linaloitwa katika Kiebrania Bethzatha, lenye mistari mitano ya nguzo. 3 Hapo umati wa wagonjwa, vipofu, vilema na wale wenye viungo vilivyopooza, walikuwa wamelala chini. 4 —— 5 Lakini kulikuwa na mtu fulani hapo ambaye alikuwa mgonjwa kwa miaka 38. 6 Alipomwona mtu huyu amelala chini, na akiwa anajua kwamba tayari amekuwa mgonjwa muda mrefu,+ Yesu akamwambia: “Je, unataka kuwa na afya nzuri?”+ 7 Mgonjwa huyo akamjibu: “Bwana, sina mtu wa kuniweka ndani ya dimbwi wakati maji yanapotibuliwa; lakini wakati ninapokuwa nikija mwingine hushuka mbele yangu.” 8 Yesu akamwambia: “Simama, chukua kitanda chako, utembee.”+ 9 Ndipo mtu huyo akawa na afya nzuri mara moja, naye akachukua kitanda chake, akaanza kutembea.
Basi siku hiyo ilikuwa siku ya sabato.+ 10 Kwa hiyo Wayahudi wakaanza kumwambia mtu huyo aliyeponywa: “Ni Sabato, na si halali+ ukichukue kitanda.” 11 Lakini akawajibu: “Yule aliyenifanya niwe na afya nzuri aliniambia, ‘Chukua kitanda chako utembee.’ ” 12 Wakamuuliza: “Ni nani huyo aliyekuambia, ‘Kichukue utembee’?” 13 Lakini mwanamume huyo aliyeponywa hakujua alikuwa nani, kwa maana Yesu alikuwa amegeukia kando, mahali hapo pakiwa pana umati.
14 Baada ya mambo haya Yesu alimkuta hekaluni akamwambia: “Ona, una afya nzuri. Usifanye dhambi tena kamwe, ili usipatwe na jambo fulani baya zaidi.” 15 Mtu yule akaenda zake akawaambia Wayahudi kwamba Yesu ndiye aliyemfanya awe na afya nzuri. 16 Kwa hiyo Wayahudi wakamtesa+ Yesu, kwa sababu alikuwa akifanya mambo hayo wakati wa siku ya Sabato. 17 Lakini akawajibu: “Baba yangu anaendelea kufanya kazi mpaka sasa, na mimi ninaendelea kufanya kazi.”+ 18 Kwa kweli, kwa sababu hiyo Wayahudi wakaanza kutafuta hata zaidi kumuua,+ kwa sababu si kwamba tu alikuwa akiivunja Sabato bali pia alikuwa akimwita Mungu Baba+ yake mwenyewe, akijifanya mwenyewe kuwa sawa+ na Mungu.
19 Kwa hiyo, Yesu akajibu, akawaambia: “Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, Mwana hawezi kufanya hata jambo moja kwa uamuzi wake mwenyewe, ila tu lile analomwona Baba akifanya.+ Kwa maana mambo yoyote yale ambayo Yule hufanya, mambo hayo Mwana pia hufanya vivyo hivyo. 20 Kwa maana Baba anampenda Mwana+ na humwonyesha mambo yote anayofanya yeye mwenyewe, naye atamwonyesha kazi zilizo kubwa zaidi kuliko hizi, ili ninyi mpate kustaajabu.+ 21 Kwa maana kama vile Baba anavyowafufua wafu na kuwafanya hai,+ ndivyo Mwana pia anavyowafanya hai wale anaotaka kuwafanya hai.+ 22 Kwa maana Baba hamhukumu mtu yeyote hata kidogo, bali amemkabidhi Mwana kazi yote ya kuhukumu,+ 23 ili wote wapate kumheshimu Mwana+ kama vile wanavyomheshimu Baba. Yule ambaye hamheshimu Mwana hamheshimu Baba aliyemtuma.+ 24 Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, Yule ambaye husikia neno langu na kumwamini yule aliyenituma ana uzima wa milele,+ naye haingii hukumuni bali amevuka kutoka katika kifo na kuingia katika uzima.+
25 “Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, Saa inakuja, nayo ipo sasa, wakati ambapo wafu+ wataisikia sauti+ ya Mwana wa Mungu na wale ambao wamesikiliza wataishi.+ 26 Kwa maana kama vile Baba alivyo na uzima ndani yake mwenyewe,+ ndivyo pia amemruhusu Mwana awe na uzima ndani yake mwenyewe.+ 27 Naye amempa mamlaka ya kuhukumu,+ kwa sababu yeye ndiye Mwana wa binadamu.+ 28 Msistaajabie jambo hili, kwa sababu saa inakuja ambayo wale wote waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho+ wataisikia sauti yake 29 na kutoka, wale waliotenda mambo mema kwenye ufufuo wa uzima,+ wale waliokuwa na zoea la kutenda mambo maovu kwenye ufufuo wa hukumu.+ 30 Mimi siwezi kufanya lolote kwa uamuzi wangu mwenyewe; kama vile ninavyosikia, ndivyo ninavyohukumu; na hukumu ninayotoa ni ya uadilifu,+ kwa sababu ninatafuta, si mapenzi yangu mwenyewe, bali mapenzi+ yake aliyenituma.
31 “Ikiwa mimi peke yangu ninatoa ushahidi+ juu yangu mwenyewe, ushahidi wangu si wa kweli.+ 32 Kuna mwingine ambaye hutoa ushahidi juu yangu, nami ninajua kwamba ushahidi ambao yeye hutoa+ juu yangu ni wa kweli. 33 Ninyi mmetuma watu kwa Yohana, naye ametoa ushahidi kwa ile kweli.+ 34 Hata hivyo, mimi siukubali ushahidi kutoka kwa mwanadamu, bali ninasema mambo hayo ili mpate kuokolewa.+ 35 Mtu huyo alikuwa taa yenye kuwaka na yenye kung’aa, nanyi kwa wakati mfupi mlikuwa na nia ya kushangilia sana katika nuru yake.+ 36 Lakini mimi nina ushahidi ulio mkubwa zaidi kuliko ule wa Yohana, kwa maana kazi zilezile ambazo Baba yangu alinigawia kutimiza, kazi hizo zenyewe ambazo ninafanya,+ hutoa ushahidi juu yangu kwamba Baba alinituma. 37 Pia, Baba aliyenituma yeye mwenyewe ametoa ushahidi juu yangu.+ Ninyi hamjasikia sauti yake wakati wowote wala kuona umbo lake;+ 38 nanyi hamna neno lake likikaa ndani yenu, kwa sababu yuleyule ambaye yeye alimtuma ninyi hammwamini.
39 “Ninyi mnayachunguza Maandiko,+ kwa sababu mnafikiri kwamba kwa njia yake mtakuwa na uzima wa milele; na hayo yenyewe ndiyo yanayotoa ushahidi juu yangu.+ 40 Na bado hamtaki kuja kwangu ili mpate kuwa na uzima.+ 41 Mimi siukubali utukufu kutoka kwa wanadamu,+ 42 lakini ninajua vizuri kwamba ninyi hammpendi Mungu ndani yenu.+ 43 Mimi nimekuja katika jina la Baba yangu,+ lakini ninyi hamnipokei; ikiwa mtu mwingine angefika katika jina lake mwenyewe, mngempokea huyo. 44 Mtawezaje kuamini, wakati ninyi mnakubali utukufu+ kutoka kwa mtu na mwenzake na hamtafuti utukufu unaotoka kwa Mungu wa pekee?+ 45 Msifikiri kwamba nitawashtaki kwa Baba; kuna mmoja ambaye huwashtaki ninyi, Musa,+ ambaye mmemtumaini. 46 Kwa kweli, ikiwa mngalimwamini Musa mngaliniamini mimi, kwa maana huyo aliandika juu yangu.+ 47 Lakini ikiwa hamyaamini maandishi yake huyo,+ mtawezaje kuyaamini maneno yangu?”
6 Baada ya mambo haya Yesu akaondoka kwenda ng’ambo ya bahari ya Galilaya, au Tiberia.+ 2 Lakini umati mkubwa wakamfuata, kwa sababu walikuwa wakiona ishara alizokuwa akifanya juu ya wale waliokuwa wakiugua.+ 3 Kwa hiyo Yesu akapanda mlimani,+ na hapo alikuwa ameketi pamoja na wanafunzi wake. 4 Sasa pasaka,+ ile sherehe ya Wayahudi, ilikuwa karibu. 5 Kwa hiyo, Yesu alipoinua macho yake na kuona kwamba umati mkubwa walikuwa wakimjia, akamwambia Filipo: “Tutanunua wapi mikate ili hawa wale?”+ 6 Hata hivyo, alikuwa akisema hilo ili amjaribu, kwa maana yeye mwenyewe alijua alilokuwa karibu kufanya. 7 Filipo akamjibu: “Mikate yenye thamani ya dinari mia mbili haiwatoshi, hata kwamba kila mmoja aweze kupata kidogo.”+ 8 Mmoja wa wanafunzi wake, Andrea ndugu ya Simoni Petro, akamwambia: 9 “Hapa yupo mvulana mdogo ambaye ana mikate mitano ya shayiri+ na samaki wadogo wawili. Lakini vitu hivi ni nini kwa watu wengi sana hivi?”+
10 Yesu akasema: “Waketisheni watu kama kwenye mlo.”+ Basi kulikuwa na majani mengi hapo. Kwa hiyo wanaume wakaketi, hesabu yao karibu elfu tano.+ 11 Basi Yesu akachukua ile mikate na, baada ya kushukuru, akaigawanya kwa wale waliokuwa wameketi, vivyo hivyo pia wale samaki wadogo kadiri walivyotaka.+ 12 Lakini walipokuwa wameshiba+ akawaambia wanafunzi wake: “Kusanyeni pamoja vipande ambavyo vimebaki, ili chochote kisipotee bure.” 13 Kwa hiyo wakavikusanya pamoja, nao wakajaza vikapu kumi na viwili kwa vipande vya mikate mitano ya shayiri, ambavyo vilibakizwa na wale waliokuwa wamekula.+
14 Kwa hiyo watu hao walipoona ishara alizofanya, wakaanza kusema: “Kwa hakika huyu ndiye nabii+ aliyepaswa kuja ulimwenguni.” 15 Kwa hiyo Yesu, akijua walikuwa karibu kuja kumkamata wamfanye kuwa mfalme, akaondoka+ tena kwenda mlimani akiwa peke yake.
16 Kulipokuwa jioni, wanafunzi wake wakashuka kwenda baharini,+ 17 na, baada ya kupanda mashua, wakaondoka kwenda ng’ambo ya bahari ili waende Kapernaumu. Basi, kufikia sasa, giza lilikuwa limeingia na Yesu alikuwa bado hajaja mahali walipokuwa. 18 Pia, bahari ikaanza kuchafuka kwa sababu upepo wenye nguvu ulikuwa ukivuma.+ 19 Hata hivyo, walipokuwa wamevuta makasia karibu kilometa tano au sita, wakamwona Yesu akitembea juu ya bahari akiwa anaikaribia mashua; nao wakaogopa.+ 20 Lakini akawaambia: “Ni mimi; msiogope!”+ 21 Kwa hiyo walikuwa na nia ya kumchukua ndani ya mashua, na mara hiyo mashua ikawa kwenye nchi kavu walikokuwa wakijaribu kwenda.+
22 Siku iliyofuata umati waliokuwa wamesimama upande ule mwingine wa bahari wakaona kwamba hapakuwa na mashua hapo ila moja ndogo, na kwamba Yesu hakuwa ameingia ndani ya mashua pamoja na wanafunzi wake bali wanafunzi wake tu ndio waliokuwa wameondoka; 23 lakini mashua kutoka Tiberia zilifika karibu na mahali ambapo walikula mkate baada ya Bwana kushukuru. 24 Kwa hiyo umati walipoona kwamba Yesu hakuwa hapo wala wanafunzi wake, wakapanda mashua zao ndogo wakaja mpaka Kapernaumu kumtafuta+ Yesu.
25 Kwa hiyo walipompata ng’ambo ya bahari wakamwambia: “Rabi,+ ulifika hapa wakati gani?” 26 Yesu akawajibu na kusema: “Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, Mnanitafuta, si kwa sababu mliona ishara, bali kwa sababu mlikula mikate mkashiba.+ 27 Fanyeni kazi, si kwa ajili ya chakula ambacho huharibika,+ bali kwa ajili ya chakula ambacho hudumu kufikia uzima wa milele,+ ambacho Mwana wa binadamu atawapa ninyi; kwa maana juu yake huyo, Baba, naam Mungu, ametia muhuri wake wa kibali.”+
28 Kwa hiyo wakamwambia: “Tutafanya nini ili tutende kazi za Mungu?” 29 Yesu akajibu, akawaambia: “Hii ndiyo kazi ya Mungu, kwamba mmwamini+ yule ambaye Huyo alimtuma.”+ 30 Kwa hiyo wakamwambia: “Basi, wewe unafanya ishara+ gani, ili tuione, tukuamini? Ni kazi gani ambayo unafanya? 31 Mababu zetu walikula mana+ nyikani, kama vile ambavyo imeandikwa, ‘Aliwapa mkate kutoka mbinguni ili wale.’ ”+ 32 Kwa sababu hiyo Yesu akawaambia: “Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, Musa hakuwapa ninyi mkate kutoka mbinguni, lakini Baba yangu anawapa ninyi mkate wa kweli kutoka mbinguni.+ 33 Kwa maana mkate wa Mungu ni yule ambaye hushuka kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima.” 34 Kwa hiyo wakamwambia: “Bwana, utupe sikuzote mkate huo.”+
35 Yesu akawaambia: “Mimi ndio mkate wa uzima. Yule ambaye huja kwangu hataona njaa hata kidogo, naye anayeniamini hatapata kiu kamwe.+ 36 Lakini nimewaambia ninyi, hata mmeniona na bado hamwamini.+ 37 Kila kitu anachonipa Baba kitakuja kwangu, naye anayekuja kwangu sitamfukuza kamwe;+ 38 kwa sababu nimeshuka kutoka mbinguni+ kufanya, si mapenzi yangu, bali mapenzi yake aliyenituma.+ 39 Haya ndiyo mapenzi yake aliyenituma, kwamba nisipoteze kitu chochote kati ya vyote ambavyo amenipa bali kwamba nikifufue+ katika siku ya mwisho. 40 Kwa maana haya ndiyo mapenzi ya Baba yangu, kwamba kila mtu ambaye humtazama Mwana na kumwamini awe na uzima wa milele,+ nami nitamfufua katika siku ya mwisho.”+
41 Kwa hiyo Wayahudi wakaanza kumnung’unikia kwa sababu alisema: “Mimi ndio mkate ambao ulishuka kutoka mbinguni”;+ 42 nao wakaanza kusema:+ “Je, huyu si Yesu mwana wa Yosefu,+ ambaye baba na mama yake sisi tunawajua? Anawezaje sasa kusema, ‘Mimi nimeshuka kutoka mbinguni’?” 43 Yesu akajibu, akawaambia: “Acheni kunung’unika kati yenu wenyewe. 44 Hakuna mtu anayeweza kuja kwangu isipokuwa Baba, aliyenituma, amvute;+ nami nitamfufua siku ya mwisho.+ 45 Imeandikwa katika Manabii, ‘Na wote watafundishwa na Yehova.’+ Kila mtu ambaye amesikia kutoka kwa Baba na ambaye amejifunza huja kwangu.+ 46 Si kwamba mwanadamu yeyote amemwona Baba,+ ila yule aliyetoka kwa Mungu; huyo amemwona Baba.+ 47 Kwa kweli kabisa ninawaambia, Yule ambaye huamini ana uzima wa milele.+
48 “Mimi ndio mkate+ wa uzima. 49 Mababu zenu walikula mana+ nyikani na bado wakafa. 50 Huu ndio mkate ambao hushuka kutoka mbinguni, ili yeyote apate kuula na asife. 51 Mimi ndio mkate ulio hai ulioshuka kutoka mbinguni; yeyote akila mkate huu ataishi milele; na, kwa kweli, mkate ambao nitatoa ni mwili+ wangu kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.”+
52 Kwa hiyo Wayahudi wakaanza kushindana, wakisema: “Mtu huyu anawezaje kutupa mwili wake tule?” 53 Basi Yesu akawaambia: “Kwa kweli kabisa ninawaambia, Ninyi msipoula mwili+ wa Mwana wa binadamu na kunywa damu+ yake, hamna uzima+ ndani yenu wenyewe. 54 Yule ambaye hula mwili wangu na kunywa damu yangu ana uzima wa milele, nami nitamfufua+ katika siku ya mwisho; 55 kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli. 56 Yule ambaye hula mwili wangu na kunywa damu yangu hukaa katika muungano nami, na mimi katika muungano naye.+ 57 Kama vile Baba aliye hai+ alivyonituma, nami ninaishi kwa sababu ya Baba, yule ambaye pia hunila mimi, hata huyo ataishi kwa sababu yangu.+ 58 Huu ndio mkate ulioshuka kutoka mbinguni. Si kama wakati mababu zenu walipokula na bado wakafa. Yule ambaye hula mkate huu ataishi milele.”+ 59 Mambo haya aliyasema alipokuwa akifundisha katika kusanyiko la watu wote katika Kapernaumu.
60 Kwa hiyo wengi kati ya wanafunzi wake, waliposikia hilo, wakasema: “Maneno hayo yanashtua; ni nani ambaye anaweza kuyasikiliza?”+ 61 Lakini Yesu, akijua ndani yake mwenyewe kwamba wanafunzi wake walikuwa wakinung’unika juu ya hili, akawaambia: “Je, jambo hili linawakwaza+ ninyi? 62 Kwa hiyo, namna gani ikiwa mtamwona Mwana wa binadamu akipanda kwenda alikokuwa mapema?+ 63 Roho ndiyo inayotokeza uzima;+ mwili hauna faida hata kidogo. Maneno ambayo nimewaambia ni roho+ na ni uzima.+ 64 Lakini kuna wengine kati yenu ambao hawaamini.” Kwa maana tangu mwanzo Yesu alijua ni nani wale waliokuwa hawaamini na ni nani angemsaliti.+ 65 Kwa hiyo akaendelea kusema: “Hii ndiyo sababu nimewaambia ninyi, Hakuna anayeweza kuja kwangu isipokuwa aruhusiwe na Baba.”+
66 Kwa sababu ya hili wengi kati ya wanafunzi wake wakaenda zao kwenye mambo yaliyo nyuma+ wakawa hawatembei tena pamoja naye.+ 67 Kwa hiyo Yesu akawaambia wale kumi na wawili: “Je, ninyi pia mnataka kwenda?” 68 Simoni Petro+ akamjibu: “Bwana, tutaenda kwa nani?+ Wewe una maneno ya uzima wa milele;+ 69 na sisi tumeamini na tumejua kwamba wewe ndiye Mtakatifu wa Mungu.”+ 70 Yesu akawajibu: “Niliwachagua ninyi kumi na wawili,+ sivyo? Lakini mmoja wenu ni mchongezi.”+ 71 Kwa kweli, alikuwa akisema juu ya Yuda mwana wa Simoni Iskariote; kwa maana huyu alikuwa karibu kumsaliti,+ ajapokuwa mmoja wa wale kumi na wawili.
7 Basi baada ya mambo hayo Yesu akaendelea kutembea katika Galilaya, kwa maana hakutaka kutembea katika Yudea, kwa sababu Wayahudi walikuwa wakitafuta kumuua.+ 2 Hata hivyo, sherehe ya Wayahudi, ile sherehe ya vibanda,+ ilikuwa karibu. 3 Kwa hiyo ndugu+ zake wakamwambia: “Ondoka hapa uende Yudea, ili wanafunzi wako pia wapate kuona kazi unazofanya. 4 Kwa maana hakuna mtu anayefanya jambo lolote katika siri huku yeye mwenyewe akitafuta kujulikana hadharani. Ikiwa unafanya mambo hayo, jionyeshe mwenyewe kwa ulimwengu.” 5 Kwa kweli, ndugu+ zake walikuwa hawamwamini.+ 6 Kwa hiyo Yesu akawaambia: “Wakati wangu unaofaa haujafika bado,+ lakini wakati wenu unaofaa upo sikuzote. 7 Ulimwengu hauna sababu ya kuwachukia ninyi, lakini huo unanichukia mimi, kwa sababu ninatoa ushahidi juu yake kwamba kazi zake ni mbovu.+ 8 Pandeni mwende kwenye sherehe; mimi bado sipandi kwenda kwenye sherehe hiyo, kwa sababu wakati wangu unaofaa+ bado haujafika kikamili.”+ 9 Kwa hiyo baada ya kuwaambia mambo haya, akabaki Galilaya.
10 Lakini ndugu zake walipokuwa wamepanda kwenda kwenye sherehe, yeye mwenyewe pia akapanda kwenda, si waziwazi bali kama katika siri.+ 11 Kwa hiyo Wayahudi wakaanza kumtafuta+ kwenye sherehe na kusema: “Yuko wapi yule mtu?” 12 Na umati ulikuwa ukinong’onezana mambo mengi juu yake.+ Baadhi yao wakawa wakisema: “Yeye ni mtu mwema.” Wengine wakawa wakisema: “Sivyo, bali yeye anaupotosha umati.” 13 Bila shaka, hakuna aliyekuwa akisema juu yake hadharani kwa sababu ya kuwaogopa Wayahudi.+
14 Kufikia sasa sherehe ilipokuwa imefika katikati, Yesu akapanda kuingia hekaluni na kuanza kufundisha.+ 15 Kwa hiyo Wayahudi wakaanza kustaajabu, wakisema: “Mtu huyu amepataje ujuzi wa maandishi,+ na yeye hajajifunza shuleni?”+ 16 Yesu naye akawajibu na kusema: “Yale ninayofundisha si yangu, bali ni yake yeye aliyenituma.+ 17 Ikiwa yeyote anatamani kufanya mapenzi Yake, atajua kama fundisho hilo limetoka kwa Mungu+ au kama ninasema mambo ambayo nimetunga mimi mwenyewe. 18 Yule ambaye husema mambo aliyotunga yeye mwenyewe anatafuta utukufu wake mwenyewe; bali yule anayetafuta utukufu+ wake aliyemtuma, huyo ni wa kweli, na hakuna ukosefu wa uadilifu ndani yake. 19 Musa aliwapa ninyi Sheria,+ sivyo? Lakini hakuna hata mmoja kati yenu anayetii Sheria. Kwa nini mnatafuta kuniua?”+ 20 Umati wakajibu: “Wewe una roho mwovu.+ Ni nani anayetaka kukuua?” 21 Yesu akajibu, akawaambia: “Nilifanya tendo moja,+ nanyi nyote mnastaajabu. 22 Kwa sababu hiyo Musa amewapa tohara+—si kwamba inatoka kwa Musa, bali kwamba inatoka kwa mababu+—nanyi mnatahiri mtu siku ya sabato. 23 Ikiwa mtu anatahiriwa siku ya sabato ili sheria ya Musa isivunjwe, je, mnanikasirikia kwa sababu nilimfanya mtu awe na afya nzuri siku ya sabato?+ 24 Acheni kuhukumu kwa sura ya nje, bali hukumuni kwa hukumu ya uadilifu.”+
25 Kwa hiyo baadhi ya wakaaji wa Yerusalemu wakaanza kusema: “Huyu ndiye mtu ambaye wanatafuta kumuua,+ sivyo? 26 Na bado, oneni! anasema hadharani,+ nao hawamwambii jambo lolote. Je, watawala wanajua kwa hakika kwamba huyu ndiye Kristo?+ 27 Badala yake, sisi tunajua mtu huyu ametoka wapi;+ lakini Kristo atakapokuja, hakuna atakayejua ametoka wapi.”+ 28 Kwa hiyo Yesu akapaaza sauti alipokuwa akifundisha katika hekalu na kusema: “Ninyi mnanijua tena mnajua nimetoka wapi.+ Pia, sikuja kwa uamuzi wangu mwenyewe,+ lakini yule aliyenituma ni halisi,+ nanyi hammjui.+ 29 Mimi ninamjua,+ kwa sababu mimi ni mwakilishi kutoka kwake, na Yeye alinituma.”+ 30 Kwa hiyo wakaanza kutafuta kumkamata,+ lakini hakuna aliyemkamata, kwa sababu saa+ yake ilikuwa haijafika bado. 31 Bado, wengi kati ya umati walimwamini;+ nao wakaanza kusema: “Kristo atakapofika, je, atafanya ishara+ zaidi ya zile ambazo mtu huyu amefanya?”
32 Mafarisayo walisikia umati wakinong’onezana mambo hayo juu yake, nao wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakatuma maofisa wamkamate.+ 33 Kwa hiyo Yesu akasema: “Nitaendelea kuwa pamoja nanyi muda kidogo zaidi kabla ya kwenda kwake aliyenituma.+ 34 Mtanitafuta, lakini hamtanipata,+ na mahali nilipo hamwezi kuja.”+ 35 Kwa hiyo Wayahudi wakasema kati yao wenyewe: “Mtu huyu anakusudia kwenda wapi, hata kwamba hatutampata? Je, anakusudia kwenda kwa Wayahudi waliotawanyika+ katikati ya Wagiriki na kuwafundisha Wagiriki? 36 Yanamaanisha nini maneno hayo aliyosema kwamba, ‘Mtanitafuta, lakini hamtanipata, na mahali nilipo hamwezi kuja’?”
37 Basi siku ya mwisho, ile siku kuu ya sherehe,+ Yesu alikuwa amesimama, naye akapaaza sauti, akisema: “Ikiwa yeyote ana kiu,+ acheni aje kwangu na kunywa. 38 Yule ambaye ananiamini,+ kama vile Andiko lilivyosema, ‘Vijito vya maji yaliyo hai vitatiririka kutoka katika sehemu yake ya ndani kabisa.’ ”+ 39 Hata hivyo, alisema hilo kuhusu ile roho ambayo wale waliomwamini wangepokea hivi karibuni; kwa maana kufikia wakati huo roho+ haikuwapo, kwa sababu Yesu hakuwa ametukuzwa+ bado. 40 Kwa hiyo baadhi ya umati ambao walisikia maneno hayo wakaanza kusema: “Kwa hakika huyu ni Yule Nabii.”+ 41 Wengine walikuwa wakisema: “Huyu ndiye Kristo.”+ Lakini wengine walikuwa wakisema: “Je, kwa hakika Kristo+ atakuja kutoka Galilaya?+ 42 Je, Andiko halijasema kwamba Kristo anakuja kutoka kwa uzao wa Daudi,+ na kutoka Bethlehemu+ kijiji ambako Daudi alikaa?”+ 43 Kwa hiyo mgawanyiko juu yake ukatokea kati ya umati.+ 44 Ingawa hivyo, baadhi yao walikuwa wakitafuta kumkamata, lakini hakuna aliyemkamata.
45 Kwa hiyo maofisa wakarudi kwa wakuu wa makuhani na Mafarisayo, na Mafarisayo wakawaambia: “Kwa nini hamkumleta?” 46 Wale maofisa wakajibu: “Mtu mwingine hajapata kamwe kusema kama huyu.”+ 47 Nao Mafarisayo wakajibu: “Je, ninyi pia mmepotoshwa? 48 Je, kuna hata mmoja wa watawala au wa Mafarisayo ambaye amemwamini?+ 49 Lakini umati huu usiojua Sheria ni watu waliolaaniwa.”+ 50 Nikodemo, aliyekuwa amemwendea hapo kwanza, na aliyekuwa mmoja wao, akawaambia: 51 “Je, sheria yetu humhukumu mtu isipokuwa kwanza iwe imesikia+ kutoka kwake na kujua analofanya?” 52 Wakajibu, wakamwambia: “Je, wewe pia umetoka Galilaya? Chunguza uone kwamba hakuna nabii+ atakayeinuliwa kutoka Galilaya.”*
Hati Codex Sinaiticus, Codex Vaticanus, na Sinaitic Syriac codex huondoa mstari wa 53 mpaka sura ya 8, mstari wa 11, ambao husomwa (kukiwa na tofauti fulani-fulani katika maandishi mbalimbali na tafsiri za Kigiriki) kama ifuatavyo:
53 Kwa hiyo wakaenda kila mmoja nyumbani kwake.
8 Lakini Yesu akaenda kwenye Mlima wa Mizeituni. 2 Hata hivyo, wakati wa mapambazuko akajitokeza tena hekaluni, na watu wote wakaanza kumwendea, naye akaketi na kuanza kuwafundisha. 3 Basi waandishi na Mafarisayo wakamleta mwanamke aliyekuwa amepatikana akifanya uzinzi, na, baada ya kumsimamisha katikati yao, 4 wakamwambia: “Mwalimu, mwanamke huyu amepatikana akifanya uzinzi. 5 Katika Sheria Musa aliagiza kwamba tuwapige kwa mawe wanawake kama hawa. Kwa kweli, unasema nini?” 6 Bila shaka, walikuwa wakisema hilo ili kumjaribu, ili wawe na jambo fulani la kumshtakia. Lakini Yesu akainama, akaanza kuandika chini kwa kidole chake. 7 Walipozidi kumuuliza, akainuka na kuwaambia: “Yule kati yenu ambaye hana dhambi awe wa kwanza kumtupia jiwe.” 8 Akainama tena na kuendelea kuandika chini. 9 Lakini wale waliosikia hilo wakaanza kuondoka wakienda, mmoja mmoja, kuanzia na wanaume wazee, naye akabaki peke yake, pamoja na mwanamke aliyekuwa katikati yao. 10 Yesu akainuka, akamwambia: “Mwanamke, wako wapi? Je, hakuna aliyekuhukumu kuwa na hatia?” 11 Yule mwanamke akasema: “Hakuna, bwana.” Yesu akasema: “Wala mimi sikuhukumu kuwa na hatia. Ondoka uende zako; tangu sasa na kuendelea usiendelee kutenda dhambi tena.”
12 Kwa hiyo Yesu akawaambia tena, akisema: “Mimi ndiye nuru+ ya ulimwengu. Yule anayenifuata hatatembea kamwe katika giza,+ bali atakuwa na nuru ya uzima.” 13 Kwa sababu hiyo Mafarisayo wakamwambia: “Wewe unatoa ushahidi juu yako mwenyewe; ushahidi wako si wa kweli.” 14 Yesu akajibu, akawaambia: “Hata ikiwa ninatoa ushahidi juu yangu mwenyewe, ushahidi+ wangu ni wa kweli, kwa sababu ninajua nilikotoka na ninakoenda.+ Lakini ninyi hamjui nilitoka wapi na ninaenda wapi. 15 Ninyi mnahukumu kulingana na mwili;+ mimi sihukumu mtu yeyote hata kidogo.+ 16 Na bado ikiwa ninahukumu, hukumu yangu ni ya kweli, kwa sababu siko peke yangu, bali Baba aliyenituma yuko pamoja nami.+ 17 Pia, katika Sheria yenu wenyewe imeandikwa, ‘Ushahidi wa watu wawili ni wa kweli.’+ 18 Mimi ninatoa ushahidi juu yangu mwenyewe, na Baba aliyenituma hutoa ushahidi juu yangu.”+ 19 Kwa hiyo wakaendelea kumwambia: “Yuko wapi Baba yako?” Yesu akajibu: “Ninyi hamnijui mimi wala Baba yangu.+ Kama mngenijua mimi, mngemjua Baba yangu pia.”+ 20 Alisema maneno hayo katika chumba cha hazina+ alipokuwa akifundisha katika hekalu. Lakini hakuna aliyemkamata,+ kwa sababu saa+ yake ilikuwa haijafika bado.
21 Kwa sababu hiyo akawaambia tena: “Ninaenda zangu, nanyi mtanitafuta,+ na bado mtakufa katika dhambi yenu.+ Ninakoenda hamwezi kuja.” 22 Kwa hiyo Wayahudi wakaanza kusema: “Je, atajiua mwenyewe? Kwa sababu anasema, ‘Ninakoenda hamwezi kuja.’ ”+ 23 Kwa hiyo akaendelea kuwaambia: “Ninyi mnatoka kwenye makao ya chini; mimi ninatoka kwenye makao ya juu.+ Ninyi mnatoka katika ulimwengu+ huu; mimi sitoki katika ulimwengu huu.+ 24 Kwa hiyo niliwaambia ninyi, Mtakufa katika dhambi zenu.+ Kwa maana ikiwa hamwamini kwamba mimi ndiye, mtakufa katika dhambi zenu.”+ 25 Kwa hiyo wakaanza kumwambia: “Wewe ni nani?” Yesu akawaambia: “Kwa nini hata ninasema nanyi? 26 Nina mambo mengi ya kusema juu yenu na kutoa hukumu juu ya mambo hayo. Kwa hakika, yule aliyenituma ni wa kweli, na mambo yale niliyoyasikia kutoka kwake ninayasema ulimwenguni.”+ 27 Hawakufahamu kwamba alikuwa akiwaambia juu ya Baba. 28 Kwa hiyo Yesu akasema: “Mara tu mkiisha kumwinua+ Mwana wa binadamu,+ ndipo mtakapojua kwamba mimi ndiye,+ na kwamba sifanyi jambo lolote kwa uamuzi wangu mwenyewe;+ bali kama vile Baba alivyonifundisha, ndivyo ninavyosema mambo haya.+ 29 Na yule aliyenituma yuko pamoja nami; yeye hakuniacha peke yangu, kwa sababu sikuzote mimi hufanya mambo yanayompendeza.”+ 30 Alipokuwa akisema mambo haya, wengi walimwamini.+
31 Na kwa hiyo, Yesu akaendelea kuwaambia Wayahudi waliokuwa wamemwamini: “Mkikaa katika neno langu,+ ninyi kwa kweli ni wanafunzi wangu, 32 nanyi mtaijua kweli,+ nayo kweli itawaweka ninyi huru.”+ 33 Wakamjibu: “Sisi ni uzao wa Abrahamu+ nasi hatujapata kamwe kuwa watumwa wa mtu yeyote.+ Kwa nini basi unasema, ‘Ninyi mtakuwa huru’?” 34 Yesu akawajibu: “Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, Kila mtendaji wa dhambi ni mtumwa wa dhambi.+ 35 Zaidi ya hayo, mtumwa hakai nyumbani milele; mwana hukaa milele.+ 36 Kwa hiyo Mwana akiwaweka ninyi huru, mtakuwa huru kwelikweli.+ 37 Ninajua kwamba ninyi ni uzao wa Abrahamu; lakini mnatafuta kuniua,+ kwa sababu neno langu halifanyi maendeleo kati yenu.+ 38 Mambo ambayo nimeyaona kwa Baba yangu+ ninayasema;+ na kwa hiyo, fanyeni mambo ambayo mmesikia kutoka kwa baba yenu.” 39 Wakajibu, wakamwambia: “Baba yetu ni Abrahamu.”+ Yesu akawaambia: “Ikiwa ninyi ni watoto wa Abrahamu,+ fanyeni kazi za Abrahamu. 40 Lakini sasa mnatafuta kuniua, mtu ambaye amewaambia kweli ambayo nilisikia kutoka kwa Mungu.+ Abrahamu hakufanya hivyo.+ 41 Ninyi mnafanya kazi za baba yenu.” Wakamwambia: “Sisi hatukuzaliwa kutokana na uasherati; tuna Baba mmoja,+ Mungu.”
42 Yesu akawaambia: “Kama Mungu angekuwa ndiye Baba yenu, mngenipenda,+ kwa maana nilitoka kwa Mungu nami nipo hapa.+ Wala sikuja kwa uamuzi wangu mwenyewe hata kidogo, lakini Huyo alinituma.+ 43 Kwa nini hamjui yale ninayosema? Kwa sababu hamwezi kusikiliza neno langu.+ 44 Ninyi mmetoka kwa baba yenu Ibilisi,+ nanyi mnataka kufanya tamaa za baba yenu.+ Huyo alikuwa muuaji alipoanza,+ naye hakusimama imara katika kweli, kwa sababu kweli haimo ndani yake. Anaposema uwongo, yeye husema kulingana na mwelekeo wake mwenyewe, kwa sababu yeye ni mwongo na ndiye baba ya uwongo.+ 45 Kwa sababu mimi, kwa upande mwingine, ninawaambia ile kweli, hamniamini.+ 46 Ni nani kati yenu anayenihukumu kuwa na hatia ya dhambi?+ Ikiwa ninasema kweli, kwa nini hamniamini? 47 Yule anayetoka kwa Mungu husikiliza maneno ya Mungu.+ Ndiyo sababu hamsikilizi, kwa sababu hamtoki kwa Mungu.”+
48 Wayahudi wakajibu, wakamwambia: “Je, sisi hatusemi kweli kwamba, Wewe ni Msamaria+ na una roho mwovu?”+ 49 Yesu akajibu: “Mimi sina roho mwovu, lakini namheshimu Baba yangu,+ nanyi mnanivunjia heshima. 50 Lakini mimi sijitafutii utukufu;+ kuna Mmoja anayetafuta na anayehukumu.+ 51 Kwa kweli kabisa ninawaambia, Yeyote akishika neno langu, hataona kifo kamwe.”+ 52 Wayahudi wakamwambia: “Sasa tunajua una roho mwovu.+ Abrahamu alikufa,+ pia manabii;+ lakini wewe unasema, ‘Yeyote akishika neno langu, hataonja+ kifo kamwe.’ 53 Je, wewe ni mkuu+ kuliko Abrahamu baba yetu, ambaye alikufa? Pia, manabii walikufa.+ Wewe unadai kuwa nani?” 54 Yesu akajibu: “Ikiwa mimi ninajitukuza mwenyewe, utukufu wangu si kitu. Baba yangu ndiye ambaye hunitukuza,+ yule ambaye ninyi mnasema kwamba ni Mungu wenu; 55 na bado hamjamjua.+ Lakini mimi ninamjua.+ Na ikiwa ningesema simjui ningekuwa mwongo kama ninyi. Lakini mimi ninamjua, nami ninalishika neno lake.+ 56 Baba yenu Abrahamu alishangilia sana katika tazamio la kuona siku yangu,+ naye aliiona na kushangilia.”+ 57 Kwa hiyo Wayahudi wakamwambia: “Wewe hujafika umri wa miaka 50, na bado umemwona Abrahamu?” 58 Yesu akawaambia: “Kwa kweli ninawaambia ninyi, Kabla ya Abrahamu kuwako, mimi nimekuwako.”+ 59 Kwa hiyo wakaokota mawe wamtupie;+ lakini Yesu akajificha na kutoka hekaluni.
9 Basi alipokuwa akipita alimwona mtu aliyekuwa kipofu tangu kuzaliwa. 2 Na wanafunzi wake wakamuuliza: “Rabi,+ ni nani aliyetenda dhambi,+ ni mtu huyu au wazazi wake,+ hata kwamba akazaliwa kipofu?” 3 Yesu akajibu: “Mtu huyu hakutenda dhambi wala wazazi wake, bali ilikuwa hivyo ili kazi za Mungu zipate kufunuliwa katika kisa chake.+ 4 Lazima tufanye kazi zake aliyenituma kukiwa mchana bado;+ usiku+ unakuja wakati ambapo hakuna mtu anayeweza kufanya kazi. 5 Maadamu nimo ulimwenguni, mimi ndiye nuru+ ya ulimwengu.” 6 Baada ya kusema hayo, akatema mate chini akafanyiza udongo kwa mate hayo, akauweka udongo wake juu ya macho ya mtu huyo+ 7 na kumwambia: “Nenda ukanawe+ katika dimbwi la Siloamu”+ (linalotafsiriwa ‘Aliyetumwa’). Na kwa hiyo akaenda na kunawa,+ akarudi akiwa anaona.+
8 Kwa hiyo majirani na wale ambao hapo zamani walikuwa wakimwona akiombaomba wakaanza kusema: “Je, huyu siye yule mtu aliyekuwa akiketi na kuombaomba?”+ 9 Baadhi yao wakawa wakisema: “Huyu ndiye.” Wengine wakawa wakisema: “Sivyo hata kidogo, lakini anafanana na yeye.” Mtu huyo akawa akisema: “Mimi ndiye.” 10 Kwa hiyo wakaanza kumwambia: “Basi, macho yako yalifunguliwaje?”+ 11 Akajibu: “Mtu anayeitwa Yesu alifanyiza udongo akaupaka juu ya macho yangu na kuniambia, ‘Nenda mpaka Siloamu+ ukanawe.’ Kwa hiyo nikaenda, nikanawa na kupata kuona.” 12 Ndipo wakamwambia: “Yuko wapi mtu huyo?” Akasema: “Sijui.”
13 Wakampeleka kwa Mafarisayo mtu huyo aliyekuwa kipofu hapo zamani. 14 Ikawa kwamba siku ambayo Yesu aliufanyiza udongo na kuyafungua macho+ yake ilikuwa siku ya Sabato.+ 15 Kwa hiyo, wakati huo Mafarisayo pia wakazidi kumuuliza jinsi alivyopata kuona.+ Akawaambia: “Aliuweka udongo juu ya macho yangu, nami nikanawa na ninaona.” 16 Basi baadhi ya Mafarisayo wakaanza kusema: “Huyu si mtu anayetoka kwa Mungu, kwa sababu haishiki Sabato.”+ Wengine wakaanza kusema: “Mtu aliye mtenda-dhambi anawezaje kufanya ishara+ kama hizo?” Basi kukawa na mgawanyiko+ kati yao. 17 Kwa sababu hiyo, wakamwambia tena kipofu yule: “Wewe unasema nini juu yake, kwa kuwa aliyafungua macho yako?” Mtu yule akasema: “Yeye ni nabii.”+
18 Hata hivyo, Wayahudi hawakuamini kumhusu yeye kwamba alikuwa kipofu na alikuwa amepata kuona, mpaka walipowaita wazazi wa mtu aliyepata kuona. 19 Nao wakawauliza: “Je, huyu ni mwana wenu ambaye mnasema alizaliwa akiwa kipofu? Basi, imekuwaje kwamba anaona sasa?” 20 Ndipo wazazi wake wakajibu, wakasema: “Sisi tunajua kwamba huyu ni mwana wetu na kwamba alizaliwa akiwa kipofu. 21 Lakini jinsi anavyoweza kuona sasa hatujui, wala hatujui ni nani aliyemfungua macho yake. Muulizeni yeye. Ana umri wa kutosha. Lazima ajisemee mwenyewe.” 22 Wazazi wake walisema mambo hayo kwa sababu walikuwa wakiwaogopa+ Wayahudi, kwa maana Wayahudi walikuwa tayari wamefikia mapatano kwamba, ikiwa yeyote angemkiri kuwa ndiye Kristo, angefukuzwa katika sinagogi.+ 23 Ndiyo sababu wazazi wake walisema: “Ana umri wa kutosha. Muulizeni yeye.”
24 Kwa hiyo wakamwita mara ya pili mtu aliyekuwa kipofu na kumwambia: “Mpe Mungu utukufu;+ sisi tunajua kwamba mtu huyu ni mtenda-dhambi.” 25 Naye akajibu: “Kama yeye ni mtenda-dhambi mimi sijui. Mimi ninajua jambo moja, kwamba, ingawa nilikuwa kipofu, sasa ninaona.” 26 Kwa hiyo wakamwambia: “Alikufanyia nini? Aliyafunguaje macho yako?” 27 Akawajibu: “Tayari nimewaambia, na bado hamkusikiliza. Kwa nini mnataka kusikia tena? Je, ninyi pia mnataka kuwa wanafunzi wake?” 28 Ndipo wakamtukana na kusema: “Wewe ni mwanafunzi wa mtu huyo, lakini sisi ni wanafunzi wa Musa. 29 Sisi tunajua kwamba Mungu amesema na Musa;+ lakini mtu huyo, sisi hatujui anakotoka.”+ 30 Mtu yule akajibu, akawaambia: “Hakika hili ni jambo la kustaajabisha,+ kwamba hamjui anakotoka, naye aliyafungua macho yangu. 31 Tunajua kwamba Mungu hawasikilizi watenda-dhambi,+ bali ikiwa mtu yeyote anamwogopa Mungu na anafanya mapenzi yake, yeye humsikiliza.+ 32 Kutoka zamani za kale haijasikiwa kamwe kwamba mtu yeyote alifungua macho ya mtu aliyezaliwa akiwa kipofu. 33 Kama mtu huyu hangekuwa ametoka kwa Mungu,+ hangeweza kufanya lolote.” 34 Wakajibu, wakamwambia: “Wewe ulizaliwa katika dhambi,+ na bado je, wewe unatufundisha sisi?” Nao wakamfukuza!+
35 Yesu akasikia kwamba walikuwa wamemfukuza, na, alipompata, akasema: “Je, unamwamini Mwana+ wa binadamu?” 36 Mtu huyo akajibu: “Na huyo ni nani, bwana, ili nipate kumwamini?” 37 Yesu akamwambia: “Wewe umemwona na, mbali na hilo, yule anayesema na wewe ndiye huyo.”+ 38 Ndipo akasema: “Ninamwamini, Bwana.” Naye akamsujudia.+ 39 Na Yesu akasema: “Kwa ajili ya hukumu+ hii mimi nilikuja katika ulimwengu huu: ili wale ambao hawaoni+ wapate kuona na wale wanaoona wapate kuwa vipofu.”+ 40 Wale wa Mafarisayo waliokuwa pamoja naye wakasikia mambo hayo, nao wakamwambia: “Je, sisi pia ni vipofu?”+ 41 Yesu akawaambia: “Kama mngekuwa vipofu, hamngekuwa na dhambi. Lakini sasa mnasema, ‘Tunaona.’+ Dhambi+ yenu inabaki.”
10 “Kwa kweli ninawaambia ninyi, Yule asiyeingia katika zizi la kondoo kupitia mlango+ bali hupandia mahali pengine, huyo ni mwizi na mporaji.+ 2 Lakini yule anayeingia kupitia mlango+ ndiye mchungaji+ wa kondoo.+ 3 Mtunza-mlango+ humfungulia huyo, nao kondoo+ huisikiliza sauti yake, naye huwaita kondoo zake mwenyewe kwa jina na kuwatoa nje. 4 Baada ya kuwatoa nje wote walio wake mwenyewe, yeye huenda mbele yao, nao kondoo humfuata,+ kwa sababu wanaijua sauti yake.+ 5 Hawatamfuata mgeni kamwe bali watamkimbia,+ kwa sababu hawaijui sauti ya wageni.”+ 6 Yesu aliwaambia mfano huo; lakini hawakujua mambo aliyowaambia yalimaanisha nini.+
7 Kwa hiyo Yesu akasema tena: “Kwa kweli ninawaambia ninyi, Mimi ndiye mlango+ wa kondoo. 8 Wale wote ambao wamekuja badala yangu ni wezi na waporaji;+ lakini kondoo hawakuwasikiliza.+ 9 Mimi ndiye mlango;+ yeyote yule anayeingia kupitia kwangu ataokolewa, naye ataingia na kutoka na kupata malisho.+ 10 Mwizi+ haji isipokuwa aje kuiba na kuua na kuharibu.+ Mimi nimekuja ili wapate kuwa na uzima na wapate kuwa nao kwa wingi. 11 Mimi ndiye mchungaji+ mwema; mchungaji mwema huitoa nafsi yake kwa ajili ya kondoo.+ 12 Mtu aliyekodiwa,+ ambaye si mchungaji na ambaye kondoo si wake, humwona mbwa-mwitu akija naye huwaacha kondoo na kukimbia—naye mbwa-mwitu huwanyakua na kuwatawanya+— 13 kwa sababu huyo ni mtu aliyekodiwa+ naye hawajali kondoo.+ 14 Mimi ndiye mchungaji mwema, nami ninawajua kondoo+ wangu na kondoo wangu wananijua,+ 15 kama vile Baba anavyonijua mimi nami ninamjua Baba;+ nami ninaitoa nafsi yangu kwa ajili ya kondoo.+
16 “Nami nina kondoo wengine,+ ambao si wa zizi hili;+ hao pia nitawaleta, nao wataisikiliza sauti yangu,+ nao watakuwa kundi moja, mchungaji mmoja.+ 17 Ndiyo sababu Baba ananipenda,+ kwa sababu ninaitoa nafsi yangu,+ ili nipate kuipokea tena. 18 Hakuna mtu ambaye ameichukua kutoka kwangu, bali ninaitoa kwa uamuzi wangu mwenyewe. Nina mamlaka ya kuitoa, nami nina mamlaka ya kuipokea tena.+ Amri+ kuhusu hili niliipokea kutoka kwa Baba yangu.”
19 Tena mgawanyiko+ ukatokea kati ya Wayahudi kwa sababu ya maneno hayo. 20 Wengi wao walikuwa wakisema: “Ana roho mwovu+ naye ana wazimu. Kwa nini mnamsikiliza?” 21 Wengine wakawa wakisema: “Haya si maneno ya mtu mwenye roho mwovu. Je, roho mwovu anaweza kufungua macho ya vipofu?”
22 Wakati huo kulikuwa na sherehe ya wakfu Yerusalemu. Ulikuwa wakati wa majira ya baridi kali, 23 na Yesu alikuwa akitembea hekaluni katika eneo lenye mistari ya nguzo za Sulemani.+ 24 Kwa hiyo Wayahudi wakamzunguka na kuanza kumwambia: “Utaendelea kuzihangaisha nafsi zetu mpaka wakati gani? Ikiwa wewe ndiye Kristo,+ tuambie waziwazi.”+ 25 Yesu akawajibu: “Niliwaambia, na bado hamwamini. Kazi ninazotenda katika jina la Baba yangu, hizo zinatoa ushahidi juu yangu.+ 26 Lakini hamwamini, kwa sababu ninyi hamko kati ya kondoo wangu.+ 27 Kondoo+ wangu huisikiliza sauti yangu, nami ninawajua, nao wananifuata.+ 28 Nami ninawapa hao uzima wa milele,+ nao hawataharibiwa kamwe,+ wala hakuna atakayewanyakua kutoka mkononi mwangu.+ 29 Kile ambacho Baba+ yangu amenipa ni kikubwa zaidi kuliko vingine vyote,+ na hakuna anayeweza kuwanyakua kutoka mkononi mwa Baba.+ 30 Mimi na Baba ni kitu kimoja.”+
31 Wayahudi wakaokota mawe tena ili wampige.+ 32 Yesu akawajibu: “Niliwaonyesha kazi nyingi nzuri kutoka kwa Baba. Kati ya kazi hizo mnataka kunipiga kwa mawe kwa sababu ya kazi gani?” 33 Wayahudi wakamjibu: “Tunakupiga kwa mawe, si kwa sababu ya kazi njema, bali kwa sababu ya kukufuru,+ naam, kwa sababu, ijapokuwa wewe ni mwanadamu, unajifanya kuwa mungu.”+ 34 Yesu akawajibu: “Je, haikuandikwa katika Sheria yenu,+ ‘Mimi nilisema: “Ninyi ni miungu” ’?+ 35 Ikiwa aliwaita ‘miungu’+ wale ambao neno la Mungu lilikuja dhidi yao, na bado Andiko haliwezi kubatilishwa,+ 36 je, mnaniambia mimi ambaye Baba alinitakasa na kunituma ulimwenguni, ‘Unakufuru,’ kwa sababu nilisema, Mimi ni Mwana wa Mungu?+ 37 Ikiwa mimi sitendi kazi+ za Baba, msiniamini. 38 Lakini ikiwa ninazitenda, hata ingawa hamniamini, iweni na imani katika kazi hizo,+ ili mjue na kuendelea kujua kwamba Baba yuko katika muungano pamoja na mimi, nami niko katika muungano pamoja na Baba.”+ 39 Kwa hiyo wakajaribu tena kumkamata;+ lakini akaondoka mikononi mwao.+
40 Kwa hiyo akaenda tena ng’ambo ya Yordani mpaka mahali ambako Yohana alikuwa akibatizia+ hapo kwanza, naye akakaa huko. 41 Na watu wengi wakamjia, nao wakaanza kusema: “Yohana, kwa kweli, hakufanya hata ishara moja, lakini mambo mengi ambayo Yohana alisema juu ya mtu huyu, yote yalikuwa ya kweli.”+ 42 Na wengi wakamwamini huko.+
11 Basi kulikuwa na mtu fulani mgonjwa, Lazaro wa Bethania, wa kijiji cha Maria na cha Martha+ dada yake. 2 Kwa kweli, Maria aliyempaka Bwana mafuta yenye marashi+ na kufuta miguu yake ili kuikausha kwa nywele zake,+ ndiye ambaye Lazaro ndugu yake alikuwa mgonjwa. 3 Kwa hiyo dada zake walipeleka neno kwake, wakisema: “Bwana, ona! yule unayempenda+ ni mgonjwa.” 4 Lakini Yesu aliposikia hilo akasema: “Lengo la ugonjwa huu si kifo, bali ni kwa ajili ya utukufu wa Mungu,+ ili Mwana wa Mungu atukuzwe kupitia huo.”
5 Basi Yesu alimpenda Martha na dada yake na Lazaro. 6 Hata hivyo, aliposikia kwamba alikuwa mgonjwa, ndipo kwa kweli akakaa siku mbili mahali alipokuwa. 7 Kisha baada ya hayo, akawaambia wanafunzi: “Twendeni Yudea tena.” 8 Wanafunzi wakamwambia: “Rabi,+ juzijuzi tu Wayudea walikuwa wakitafuta kukupiga kwa mawe,+ na je, unaenda huko tena?” 9 Yesu akajibu: “Kuna saa kumi na mbili za nuru ya mchana, sivyo? Ikiwa yeyote anatembea katika nuru ya mchana+ hagongi kitu chochote, kwa sababu anaona nuru ya ulimwengu huu. 10 Lakini ikiwa yeyote anatembea usiku,+ yeye hugonga kitu fulani, kwa sababu nuru haimo ndani yake.”
11 Alisema hayo, kisha akawaambia: “Lazaro rafiki yetu anapumzika, lakini ninafunga safari kwenda huko ili kumwamsha kutoka usingizini.”+ 12 Kwa hiyo wanafunzi wakamwambia: “Bwana, ikiwa anapumzika, atapona.” 13 Hata hivyo, Yesu alikuwa amesema juu ya kifo chake. Lakini walifikiri alikuwa akisema juu ya kupumzika katika usingizi. 14 Kwa hiyo, wakati huo, Yesu akawaambia waziwazi: “Lazaro amekufa,+ 15 nami ninashangilia kwa sababu yenu kwamba sikuwa huko, kusudi ninyi mwamini. Lakini twendeni kwake.” 16 Kwa hiyo Tomasi, aliyeitwa Pacha, akawaambia wanafunzi wenzake: “Acheni twende pia, ili tukafe pamoja naye.”+
17 Kwa hiyo Yesu alipofika, alikuta tayari amekwisha kuwa ndani ya kaburi siku nne.+ 18 Basi Bethania ilikuwa karibu na Yerusalemu umbali wa karibu kilometa tatu. 19 Basi wengi kati ya Wayahudi walikuwa wamekuja kwa Martha na Maria ili wawafariji+ kuhusu ndugu yao. 20 Kwa hiyo Martha, aliposikia kwamba Yesu anakuja, alienda kukutana naye; lakini Maria+ akaendelea kuketi nyumbani. 21 Kwa hiyo Martha akamwambia Yesu: “Bwana, kama ungekuwa hapa ndugu yangu hangekufa.+ 22 Hata hivyo sasa ninajua kwamba mambo mengi kadiri unayomwomba Mungu,+ Mungu atakupa.” 23 Yesu akamwambia: “Ndugu yako atafufuka.”+ 24 Martha akamwambia: “Ninajua atafufuka katika ufufuo+ siku ya mwisho.” 25 Yesu akamwambia: “Mimi ndiye ufufuo na uzima.+ Yule anayeniamini, hata akifa, atarudi kwenye uzima;+ 26 na kila mtu aliye hai na ananiamini hatakufa kamwe.+ Je, unaamini hilo?” 27 Akamwambia: “Ndiyo, Bwana; nimeamini kwamba wewe ndiye Kristo Mwana wa Mungu, Yule anayekuja ulimwenguni.”+ 28 Na alipokuwa amesema hilo, akaenda zake na kumwita Maria dada yake, akisema kwa siri: “Mwalimu+ yupo naye anakuita.” 29 Aliposikia hilo, akasimama upesi, akamwendea.
30 Kwa kweli, Yesu alikuwa hajaingia kijijini, lakini bado alikuwa mahali ambapo Martha alikutana naye. 31 Kwa hiyo Wayahudi waliokuwa pamoja naye nyumbani+ na waliokuwa wakimfariji, walipomwona Maria akisimama upesi na kuondoka aende, wakamfuata, wakidhani kwamba alikuwa akienda kwenye kaburi+ ili kulilia huko. 32 Na kwa hiyo Maria, alipofika mahali ambapo Yesu alikuwa na kumwona, akajiangusha miguuni pake, akamwambia: “Bwana, kama ungekuwa hapa, ndugu yangu hangekufa.”+ 33 Kwa hiyo, Yesu alipomwona akilia na Wayahudi waliokuja pamoja naye wakilia, akaugua rohoni na kutaabika;+ 34 naye akasema: “Mmemlaza wapi?” Wakamwambia: “Bwana, njoo uone.” 35 Yesu akatokwa na machozi.+ 36 Kwa hiyo Wayahudi wakaanza kusema: “Ona, jinsi alivyokuwa akimpenda!”+ 37 Lakini baadhi yao wakasema: “Je, mtu huyu aliyefungua macho+ ya mtu aliye kipofu hakuweza kumzuia huyu asife?”
38 Kwa hiyo Yesu, baada ya kuugua tena ndani yake, akaja kwenye lile kaburi.+ Kwa kweli, lilikuwa pango, na jiwe+ lilikuwa limelilalia. 39 Yesu akasema: “Liondoeni jiwe.”+ Martha, dada ya yule aliyekufa, akamwambia: “Bwana, kufikia sasa lazima awe ananuka, kwa maana ni siku nne.” 40 Yesu akamwambia: “Je, sikukuambia kwamba ukiamini utauona utukufu wa Mungu?”+ 41 Kwa hiyo wakaliondoa jiwe. Basi Yesu akainua macho yake kuelekea mbinguni+ na kusema: “Baba, ninakushukuru kwamba umenisikia.+ 42 Kweli, nilijua kwamba sikuzote wewe hunisikia; lakini kwa sababu ya umati+ waliosimama kunizunguka nilisema, ili wapate kuamini kwamba wewe ulinituma.”+ 43 Na alipokuwa amekwisha kusema hayo, akaita kwa sauti kubwa: “Lazaro, njoo huku nje!”+ 44 Huyo mtu aliyekuwa mfu akatoka miguu na mikono yake ikiwa imefungwa vitambaa,+ na uso wake ulikuwa umefungwa-fungwa kwa kitambaa. Yesu akawaambia: “Mfungueni, mmwache aende.”
45 Kwa hiyo wengi kati ya Wayahudi waliokuwa wamekuja kwa Maria na walioona lile alilofanya, wakamwamini;+ 46 lakini baadhi yao wakaenda zao kwa Mafarisayo na kuwaambia mambo aliyoyafanya Yesu.+ 47 Kwa sababu hiyo wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakaikusanya pamoja Sanhedrini+ na kuanza kusema: “Tufanye nini, kwa sababu mtu huyu anafanya ishara nyingi?+ 48 Tukimwacha hivyo, hao wote watamwamini,+ na Waroma+ watakuja na kuondolea mbali mahali+ petu na taifa letu pia.” 49 Lakini mtu fulani kati yao, Kayafa, aliyekuwa kuhani mkuu mwaka huo,+ akawaambia: “Ninyi hamjui lolote kamwe, 50 nanyi hamwoni kwamba ni kwa faida yenu mtu mmoja afe+ kwa ajili ya watu kuliko taifa lote liangamizwe.”+ 51 Ingawa hivyo, hilo hakulisema kwa kujitungia mwenyewe; lakini kwa sababu alikuwa kuhani mkuu mwaka huo, alitoa unabii kwamba Yesu alikusudiwa kufa kwa ajili ya taifa, 52 na si kwa ajili ya taifa hilo tu, bali ili watoto wa Mungu waliotawanyika+ huku na huku yeye apate pia kuwakusanya pamoja kuwa mmoja.+ 53 Kwa hiyo tangu siku hiyo na kuendelea wakakata shauri kumuua.+
54 Kwa sababu hiyo Yesu hakutembea tena huku na huku hadharani+ kati ya Wayahudi,+ bali aliondoka huko mpaka nchi iliyo karibu na nyika, akaingia katika jiji linaloitwa Efraimu,+ na humo akakaa pamoja na wanafunzi. 55 Sasa pasaka+ ya Wayahudi ilikuwa karibu, na watu wengi walipanda kutoka nchi hiyo mpaka Yerusalemu kabla ya pasaka kusudi wajitakase kisherehe.+ 56 Kwa hiyo wakaenda wakimtafuta Yesu nao wakawa wakiambiana huku wakiwa wamesimama kulizunguka hekalu: “Mnaonaje? Kwamba yeye hatakuja kamwe kwenye sherehe?” 57 Ilivyokuwa ni kwamba, wakuu wa makuhani na Mafarisayo walikuwa wametoa maagizo kwamba ikiwa yeyote angepata kujua alikokuwa, anapaswa kufunua hilo, ili wamkamate.
12 Basi, siku sita kabla ya pasaka, Yesu alifika Bethania,+ alikokuwa Lazaro+ ambaye Yesu alikuwa amemfufua kutoka kwa wafu. 2 Kwa hiyo wakamwandalia mlo wa jioni huko, na Martha+ alikuwa akihudumu,+ lakini Lazaro alikuwa mmoja wa wale waliokuwa wameketi mezani pamoja naye.+ 3 Kwa hiyo, Maria akachukua ratili moja ya mafuta yenye marashi, nardo+ halisi, ghali sana, na kuipaka miguu ya Yesu, naye akaikausha miguu yake kwa kuifuta kwa nywele zake.+ Nyumba ikajaa harufu ya mafuta yenye marashi. 4 Lakini Yuda Iskariote,+ mmoja wa wanafunzi wake, aliyekuwa karibu kumsaliti, akasema: 5 “Kwa nini mafuta haya yenye marashi+ hayakuuzwa kwa dinari mia tatu na kupewa maskini?”+ 6 Ingawa hivyo, alisema hilo si kwa sababu aliwahangaikia maskini, bali kwa sababu yeye alikuwa mwizi+ na alikuwa na sanduku la pesa+ na alikuwa akichukua pesa zilizowekwa ndani yake. 7 Kwa hiyo Yesu akasema: “Mwacheni, ili ashike mwadhimisho huu kwa kufikiria siku ya maziko yangu.+ 8 Kwa maana mna maskini+ pamoja nanyi sikuzote, lakini mimi hamtakuwa pamoja nami sikuzote.”
9 Kwa hiyo umati mkubwa wa Wayahudi wakapata kujua kwamba alikuwa huko, nao wakaja, si kwa sababu ya Yesu tu, bali pia wamwone Lazaro, aliyemfufua kutoka kwa wafu.+ 10 Sasa wakuu wa makuhani wakakata shauri kumuua Lazaro pia,+ 11 kwa kuwa wengi kati ya Wayahudi walikuwa wakienda huko na kumwamini Yesu+ kwa sababu yake.
12 Siku iliyofuata umati mkubwa waliokuwa wamekuja kwenye sherehe, waliposikia kwamba Yesu alikuwa akija Yerusalemu, 13 wakachukua matawi ya mitende+ na kutoka nje wakutane naye. Nao wakaanza kupaaza sauti:+ “Mwokoe, tunaomba!+ Aliyebarikiwa ni yule anayekuja katika jina la Yehova,+ naam, mfalme+ wa Israeli!” 14 Lakini Yesu alipompata mwana-punda,+ akaketi juu yake, kama vile ilivyoandikwa: 15 “Usiogope, binti Sayuni. Tazama! Mfalme wako anakuja,+ akiwa ameketi juu ya mwana wa punda.”+ 16 Mambo haya wanafunzi wake hawakuyajali hapo kwanza,+ lakini Yesu alipotukuzwa,+ ndipo walipokumbuka kwamba mambo haya yalikuwa yameandikwa juu yake na kwamba walimtendea mambo hayo.+
17 Basi umati uliokuwa pamoja naye alipomwita Lazaro+ kutoka kaburini na kumfufua kutoka kwa wafu ukaendelea kutoa ushahidi.+ 18 Kwa ajili ya hili umati huo, kwa sababu ulisikia alikuwa amefanya ishara+ hiyo, ukakutana naye pia. 19 Kwa hiyo Mafarisayo+ wakasema kati yao wenyewe: “Ninyi mnaona kwamba hamfanikiwi kamwe. Oneni! Ulimwengu umemfuata.”+
20 Sasa kulikuwa na baadhi ya Wagiriki+ kati ya wale waliopanda kwenda kuabudu kwenye sherehe. 21 Kwa hiyo, hao walimkaribia Filipo+ ambaye alikuwa wa kutoka Bethsaida ya Galilaya, nao wakaanza kumwomba, wakisema: “Bwana, tunataka kumwona Yesu.”+ 22 Filipo akaja akamwambia Andrea. Andrea na Filipo wakaja, wakamwambia Yesu.
23 Lakini Yesu akawajibu, akisema: “Saa imekuja Mwana wa binadamu atukuzwe.+ 24 Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, Mbegu ya ngano isipoanguka katika udongo na kufa, hiyo hubaki ikiwa mbegu moja tu; lakini ikifa,+ ndipo hiyo huzaa matunda mengi. 25 Yule anayeipenda sana nafsi yake huiangamiza, lakini yule anayeichukia nafsi+ yake katika ulimwengu huu atailinda kwa ajili ya uzima wa milele.+ 26 Ikiwa yeyote anataka kunihudumia, acha anifuate, na mahali nilipo hapo ndipo mhudumu wangu atakapokuwa pia.+ Ikiwa yeyote anataka kunihudumia, Baba atamheshimu huyo.+ 27 Sasa nafsi yangu inataabika,+ nami nitasema nini? Baba, niokoe kutoka katika saa hii.+ Hata hivyo, ndiyo sababu nimekuja kwenye saa hii. 28 Baba, litukuze jina lako.” Kwa hiyo sauti+ ikaja kutoka mbinguni: “Nimelitukuza na pia nitalitukuza tena.”+
29 Kwa hiyo umati waliosimama huku na huku na kusikia hilo wakaanza kusema kumekuwa na mngurumo. Wengine wakaanza kusema: “Malaika amesema naye.” 30 Yesu akajibu, akasema: “Sauti hii imetokea, si kwa ajili yangu, bali kwa ajili yenu.+ 31 Sasa ulimwengu huu unahukumiwa; sasa mtawala wa ulimwengu+ huu atatupwa nje.+ 32 Na bado mimi, nikiinuliwa+ kutoka duniani, nitavuta watu wa namna zote kwangu.”+ 33 Kwa kweli hili alikuwa akilisema ili kutoa ishara ni kifo cha namna gani alikuwa karibu kufa.+ 34 Kwa hiyo umati wakamjibu: “Sisi tulisikia kutoka katika Sheria kwamba Kristo hudumu milele;+ basi kwa nini unasema kwamba lazima Mwana wa binadamu ainuliwe?+ Huyo Mwana wa binadamu ni nani?”+ 35 Kwa hiyo Yesu akawaambia: “Nuru itakuwa kati yenu kwa muda kidogo zaidi. Tembeeni wakati mna nuru, ili giza+ lisiwazidi nguvu; na yule ambaye hutembea katika giza hajui anakoenda.+ 36 Wakati mna nuru, iweni na imani katika nuru, ili muwe wana wa nuru.”+
Yesu alisema mambo hayo akaenda zake na kujificha mbali nao. 37 Lakini ijapokuwa alikuwa amefanya ishara nyingi sana mbele yao, hawakuwa wanamwamini, 38 hata kwamba neno la nabii Isaya likatimizwa ambalo alisema: “Yehova, ni nani aliyeliamini jambo ambalo tumesikia?+ Na kwa habari ya mkono wa Yehova, umefunuliwa kwa nani?”+ 39 Wao hawakuamini kwa sababu tena Isaya alisema: 40 “Ameyapofusha macho yao naye ameifanya mioyo yao iwe migumu,+ ili wasione kwa macho yao na kulielewa wazo kwa mioyo yao na kugeuka nami niwaponye.”+ 41 Isaya alisema mambo haya kwa sababu aliona utukufu wake,+ naye alisema juu yake. 42 Hata hivyo, wengi hata kati ya watawala kwa kweli walimwamini,+ lakini kwa sababu ya Mafarisayo wakawa hawamkiri, ili wasifukuzwe katika sinagogi;+ 43 kwa maana waliupenda utukufu wa wanadamu kuliko hata utukufu wa Mungu.+
44 Hata hivyo, Yesu akapaaza sauti na kusema: “Yule ambaye huniamini huamini, si mimi tu, bali pia yule aliyenituma;+ 45 na yule ambaye hunitazama humtazama pia yule aliyenituma.+ 46 Nimekuja nikiwa nuru ulimwenguni,+ ili kila mtu anayeniamini asipate kukaa katika giza.+ 47 Lakini ikiwa yeyote anasikia maneno yangu na hayashiki, simhukumu; kwa maana nilikuja, si kuuhukumu ulimwengu,+ bali kuuokoa ulimwengu.+ 48 Yule ambaye hunipuuza wala hapokei maneno yangu ana wa kumhukumu. Neno+ ambalo nimesema ndilo litakalomhukumu katika siku ya mwisho; 49 kwa sababu sijasema kutokana na msukumo wangu mwenyewe, bali Baba mwenyewe aliyenituma amenipa amri kuhusu jambo la kutangaza na la kusema.+ 50 Pia ninajua kwamba amri yake inamaanisha uzima wa milele.+ Kwa hiyo mambo ninayosema, kama vile Baba alivyoniambia, ndivyo ninavyoyasema.”+
13 Sasa, kwa sababu alijua kabla ya sherehe ya pasaka kwamba saa yake ya kutoka katika ulimwengu huu kwenda kwa Baba ilikuwa imefika,+ Yesu, akiwa amewapenda walio wake mwenyewe waliokuwa ulimwenguni,+ akawapenda mpaka mwisho. 2 Kwa hiyo, mlo wa jioni ulipokuwa ukiendelea, Ibilisi akiwa tayari ameweka ndani ya moyo wa Yuda Iskariote,+ mwana wa Simoni, amsaliti,+ 3 yeye, akijua kwamba Baba alikuwa ametia vitu vyote mikononi mwake+ na kwamba alikuja kutoka kwa Mungu na alikuwa akienda kwa Mungu,+ 4 alisimama kutoka kwenye mlo wa jioni na kuyaweka kando mavazi yake ya nje. Naye akachukua kitambaa, akajifunga kiunoni.+ 5 Kisha akatia maji ndani ya beseni akaanza kuiosha miguu+ ya wanafunzi na kuikausha kwa kitambaa ambacho alikuwa amejifunga kiunoni. 6 Na kwa hiyo akafika kwa Simoni Petro. Huyo akamwambia: “Bwana, je, unaosha miguu yangu?”+ 7 Yesu akajibu, akamwambia: “Ninalofanya huelewi sasa, bali utaelewa baada ya mambo haya.”+ 8 Petro akamwambia: “Hutaosha kamwe miguu yangu.” Yesu akamjibu: “Nisipokuosha,+ wewe huna sehemu pamoja na mimi.” 9 Simoni Petro akamwambia: “Bwana, si miguu yangu tu, bali pia mikono yangu na kichwa changu.” 10 Yesu akamwambia: “Yule ambaye ameoga+ hahitaji kuoshwa zaidi ya miguu yake, bali yuko safi mwili wote. Nanyi mko safi, lakini si ninyi nyote.” 11 Kwa kweli, alimjua mtu anayemsaliti.+ Ndiyo sababu alisema: “Si wote kati yenu walio safi.”
12 Basi, alipokuwa ameosha miguu yao na kuvaa mavazi yake ya nje, akaketi mezani tena, akawaambia: “Je, mnajua jambo ambalo nimewafanyia ninyi? 13 Ninyi huniita, ‘Mwalimu,’+ na, ‘Bwana,’+ nanyi mnasema sawasawa, kwa maana ndivyo nilivyo.+ 14 Kwa hiyo, ikiwa mimi, nijapokuwa Bwana na Mwalimu, niliiosha miguu yenu,+ ninyi pia mnapaswa kuoshana miguu.+ 15 Kwa maana niliweka kielelezo kwa ajili yenu, ili, kama vile nilivyowafanyia ninyi, ninyi pia mfanye hivyo.+ 16 Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, Mtumwa si mkuu kuliko bwana wake, wala yule aliyetumwa si mkuu kuliko yule aliyemtuma.+ 17 Ikiwa mnajua mambo haya, wenye furaha ni ninyi ikiwa mnayatenda.+ 18 Mimi sisemi juu yenu nyote; ninawajua wale ambao nimewachagua.+ Lakini ni ili Andiko lipate kutimizwa,+ ‘Yule aliyekuwa akila mkate wangu amekiinua kisigino chake dhidi yangu.’+ 19 Kuanzia dakika hii na kuendelea ninawaambia ninyi kabla ya hilo kutukia,+ ili litakapotukia mwamini kwamba mimi ndiye. 20 Kwa kweli kabisa ninawaambia, Yule anayempokea yeyote ninayemtuma hunipokea mimi pia.+ Naye anayenipokea mimi, humpokea pia yule aliyenituma.”+
21 Baada ya kusema hayo, Yesu akataabika rohoni, naye akatoa ushahidi na kusema: “Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, Mmoja wenu atanisaliti.”+ 22 Wanafunzi wakaanza kutazamana, wasijue kabisa alikuwa akisema hilo kuhusu nani.+ 23 Mmoja wa wanafunzi wake alikuwa ameegama kifuani pa Yesu, naye Yesu alimpenda.+ 24 Kwa hiyo Simoni Petro akamtolea huyo ishara ya kichwa na kumwambia: “Muulize anasema hilo kuhusu nani.” 25 Kwa hiyo huyo wa mwisho akaegemea nyuma kifuani pa Yesu na kumwambia: “Bwana, ni nani?”+ 26 Kwa hiyo Yesu akajibu: “Ni yule ambaye nitampa tonge ambalo ninachovya.”+ Na kwa hiyo, akiisha kuchovya tonge, akalichukua na kumpa Yuda, mwana wa Simoni Iskariote. 27 Na baada ya hilo tonge ndipo Shetani akaingia ndani ya huyo.+ Kwa hiyo, Yesu akamwambia: “Lile unalofanya lifanye upesi zaidi.” 28 Hata hivyo, hakuna hata mmoja kati ya wale waliokuwa wameketi mezani aliyejua amemwambia hili kwa nini. 29 Kwa kweli, baadhi yao walikuwa wakifikiri, kwa kuwa Yuda alikuwa akilishika sanduku la pesa,+ kwamba Yesu alikuwa akimwambia: “Nunua vitu ambavyo tunahitaji kwa ajili ya sherehe,” au kwamba awape maskini kitu fulani.+ 30 Kwa hiyo, baada ya yeye kulipokea tonge, akatoka nje mara moja, akaenda. Na wakati huo ulikuwa usiku.+
31 Kwa hiyo alipokuwa ameenda, Yesu akasema: “Sasa Mwana wa binadamu ametukuzwa,+ na Mungu ametukuzwa kuhusiana na yeye. 32 Na Mungu mwenyewe atamtukuza,+ naye atamtukuza mara moja. 33 Watoto wadogo,+ nipo pamoja nanyi muda kidogo zaidi. Ninyi mtanitafuta; na kama vile nilivyowaambia Wayahudi, ‘Ninakoenda ninyi hamwezi kuja,’+ ninawaambia ninyi pia sasa. 34 Ninawapa ninyi amri mpya, kwamba mpendane; kama vile ambavyo nimewapenda ninyi,+ ninyi nanyi mpendane vivyo hivyo.+ 35 Kwa jambo hili wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu, mkiwa na upendo kati yenu wenyewe.”+
36 Simoni Petro akamwambia: “Bwana, unaenda wapi?” Yesu akajibu: “Ninakoenda huwezi kunifuata sasa, lakini utanifuata baadaye.”+ 37 Petro akamwambia: “Bwana, kwa nini siwezi kukufuata sasa? Nitatoa nafsi yangu kwa ajili yako.”+ 38 Yesu akajibu: “Je, utaitoa nafsi yako kwa ajili yangu? Kwa kweli kabisa ninakuambia, Jogoo hatawika mpaka uwe umenikana mara tatu.”+
14 “Mioyo yenu isitaabike.+ Iweni na imani katika Mungu,+ iweni na imani pia katika mimi.+ 2 Katika nyumba ya Baba yangu mna makao mengi.+ Kama sivyo, ningaliwaambia ninyi, kwa sababu ninaenda kuwatayarishia ninyi mahali.+ 3 Pia, nikienda na kuwatayarishia ninyi mahali, nitakuja tena+ nami nitawapokea ninyi nyumbani kwangu mwenyewe,+ ili mahali nilipo mimi, ninyi pia muwe hapo.+ 4 Na mahali ninakoenda ninyi mnaijua njia.”
5 Tomasi+ akamwambia: “Bwana, sisi hatujui unaenda wapi.+ Tunaijuaje njia?”
6 Yesu akamwambia: “Mimi ndiye njia+ na kweli+ na uzima.+ Hakuna anayekuja kwa Baba ila kupitia kwangu.+ 7 Kama mngekuwa mmenijua, mngekuwa mmemjua Baba yangu pia; tangu dakika hii na kuendelea ninyi mnamjua na mmemwona.”+
8 Filipo akamwambia: “Bwana, tuonyeshe Baba, na hilo linatutosha.”
9 Yesu akamwambia: “Je, nimekuwa pamoja nanyi kwa muda mrefu sana hivyo, na bado, Filipo, hujanijua? Yule ambaye ameniona mimi amemwona Baba+ pia. Kwa nini unasema, ‘Tuonyeshe Baba’?+ 10 Je, wewe huamini kwamba mimi nimo katika muungano pamoja na Baba na Baba yumo katika muungano pamoja nami?+ Mambo ninayowaambia ninyi sisemi kwa kujitungia mwenyewe; bali Baba ambaye hukaa katika muungano pamoja nami anafanya kazi zake.+ 11 Iweni na imani kwamba nimo katika muungano pamoja na Baba na Baba yumo katika muungano pamoja nami; kama sivyo, iweni na imani kwa sababu ya zile kazi zenyewe.+ 12 Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, Yule anayeniamini, huyo pia atafanya kazi ambazo mimi hufanya; naye atafanya kazi kubwa+ kuliko hizi, kwa sababu ninaenda kwa Baba.+ 13 Pia, lolote lile mtakaloomba katika jina langu, nitalifanya, ili Baba apate kutukuzwa kuhusiana na Mwana.+ 14 Mkiomba jambo lolote katika jina langu, nitalifanya.
15 “Ikiwa mnanipenda, mtazishika amri zangu;+ 16 nami nitamwomba Baba naye atawapa ninyi msaidizi mwingine awe pamoja nanyi milele,+ 17 roho ya ile kweli,+ ambayo ulimwengu hauwezi kuipokea,+ kwa sababu hauioni wala kuijua. Ninyi mnaijua, kwa sababu hiyo hukaa pamoja nanyi na imo ndani yenu.+ 18 Sitawaacha ninyi mayatima.+ Ninakuja kwenu. 19 Bado muda kidogo zaidi na ulimwengu hautaniona tena,+ lakini ninyi mtaniona,+ kwa sababu ninaishi, nanyi mtaishi.+ 20 Siku hiyo mtajua kwamba nimo katika muungano pamoja na Baba yangu nanyi mumo katika muungano pamoja nami, nami nimo katika muungano pamoja nanyi.+ 21 Yule aliye na amri zangu na kuzishika, huyo ndiye ambaye hunipenda.+ Naye anayenipenda atapendwa na Baba yangu, nami nitampenda na kujionyesha wazi kwake.”
22 Yuda,+ si yule Iskariote, akamwambia: “Bwana, ni nini kimetukia hivi kwamba unakusudia kujionyesha wazi kwetu wala si kwa ulimwengu?”+
23 Yesu akajibu, akamwambia: “Ikiwa yeyote ananipenda, atalishika+ neno langu, na Baba yangu atampenda, nasi hakika tutakuja kwake na kukaa pamoja naye.+ 24 Yule ambaye hanipendi hayashiki maneno yangu; na neno mnalolisikia si langu, bali ni la Baba aliyenituma.+
25 “Nilipokuwa nikikaa pamoja nanyi niliwaambia mambo haya. 26 Lakini msaidizi, roho takatifu, ambayo Baba atatuma katika jina langu, hiyo itawafundisha ninyi mambo yote na kuwakumbusha mambo yote niliyowaambia.+ 27 Ninawaachia ninyi amani, ninawapa amani+ yangu. Siwapi ninyi hiyo kwa njia ile ambayo ulimwengu huitoa. Mioyo yenu isitaabike wala kuogopa. 28 Mlisikia kwamba niliwaambia, Ninaenda zangu nami nitakuja tena kwenu. Kama mngenipenda, mngeshangilia kwamba ninaenda kwa Baba, kwa sababu Baba ni mkuu+ kuliko mimi. 29 Kwa hiyo sasa nimewaambia ninyi kabla ya hilo kutukia,+ ili, litakapotukia, mpate kuamini. 30 Sitasema mengi tena kamwe pamoja nanyi, kwa maana mtawala+ wa ulimwengu anakuja. Naye hana uwezo juu yangu,+ 31 lakini, kusudi ulimwengu ujue kwamba ninampenda Baba, kama vile Baba amenipa amri+ kufanya, ndivyo ninavyofanya. Simameni, tuondoke hapa.
15 “Mimi ndiye mzabibu wa kweli,+ na Baba yangu ndiye mkulima.+ 2 Kila tawi ndani yangu lisilozaa matunda yeye huliondolea mbali,+ na kila tawi linalozaa matunda yeye hulisafisha,+ lipate kuzaa matunda zaidi.+ 3 Tayari ninyi ni safi kwa sababu ya neno ambalo nimewaambia.+ 4 Kaeni katika muungano pamoja nami, na mimi katika muungano pamoja nanyi.+ Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa matunda likiwa peke yake lisipokaa katika mzabibu, vivyo hivyo ninyi hamwezi, msipokaa katika muungano pamoja nami.+ 5 Mimi ndiye mzabibu, ninyi ndio matawi. Yule ambaye hukaa katika muungano pamoja nami, na mimi katika muungano pamoja naye, huyo huzaa matunda mengi;+ kwa sababu bila mimi hamwezi kufanya lolote kamwe. 6 Ikiwa yeyote hakai katika muungano pamoja nami, huyo hutupwa nje kama tawi na hukauka; na watu hukusanya matawi hayo na kuyatupa ndani ya moto nayo yanateketezwa.+ 7 Mkikaa katika muungano pamoja nami na maneno yangu yakae ndani yenu, ombeni lolote mnalotaka nalo litatukia kwenu.+ 8 Baba yangu hutukuzwa katika hili, kwamba mwendelee kuzaa matunda mengi na kujionyesha kuwa wanafunzi wangu.+ 9 Kama vile Baba alivyonipenda+ nami nilivyowapenda ninyi, kaeni katika upendo wangu. 10 Mkishika amri zangu,+ mtakaa katika upendo wangu, kama vile mimi nilivyoshika amri za Baba+ na kukaa katika upendo wake.
11 “Mambo haya nimewaambia, ili shangwe yangu ipate kuwa ndani yenu na shangwe yenu ipate kujaa.+ 12 Hii ndiyo amri yangu, kwamba mpendane kama vile nilivyowapenda ninyi.+ 13 Hakuna aliye na upendo mkuu kuliko huu, kwamba mtu aitoe nafsi yake kwa ajili ya rafiki zake.+ 14 Ninyi ni rafiki zangu ikiwa mnafanya ninalowaamuru ninyi.+ 15 Siwaiti ninyi tena watumwa, kwa sababu mtumwa hajui yale ambayo bwana wake anafanya. Lakini nimewaita ninyi rafiki,+ kwa sababu mambo yote ambayo nimeyasikia kutoka kwa Baba yangu nimewajulisha ninyi.+ 16 Ninyi hamkunichagua mimi, bali mimi niliwachagua, nami niliwaweka ninyi msonge mbele na kuendelea kuzaa matunda+ na kwamba matunda yenu yapate kukaa; ili hata mkimwomba Baba jambo gani katika jina langu, apate kuwapa hilo.+
17 “Mambo haya ninawaamuru ninyi, kwamba mpendane.+ 18 Ikiwa ulimwengu unawachukia ninyi, mnajua kwamba umenichukia mimi kabla ya kuwachukia ninyi.+ 19 Kama mngekuwa sehemu ya ulimwengu, ulimwengu ungependa kilicho chake.+ Sasa kwa sababu ninyi si sehemu ya ulimwengu, bali nimewachagua ninyi kutoka ulimwenguni,+ kwa sababu hiyo ulimwengu unawachukia ninyi.+ 20 Kumbukeni neno nililowaambia, Mtumwa si mkuu kuliko bwana wake. Ikiwa wamenitesa mimi, watawatesa ninyi pia;+ ikiwa wamelishika neno langu, watalishika lenu pia. 21 Lakini watawatendea mambo yote haya kwa ajili ya jina langu, kwa sababu hawamjui aliyenituma.+ 22 Kama singekuja na kuwaambia, hawangekuwa na dhambi;+ lakini sasa hawana sababu ya kujitetea kwa ajili ya dhambi yao.+ 23 Anayenichukia anamchukia Baba yangu pia.+ 24 Kama singefanya kati yao kazi ambazo hakuna mwingine aliyezifanya,+ hawangekuwa na dhambi;+ lakini sasa wameniona na pia wamenichukia mimi na vilevile Baba yangu.+ 25 Lakini ni ili neno lililoandikwa katika Sheria yao lipate kutimizwa, ‘Walinichukia bila sababu.’+ 26 Wakati atakapofika msaidizi ambaye nitawapelekea ninyi kutoka kwa Baba,+ roho ya ile kweli, ambayo inatoka kwa Baba, huyo atatoa ushahidi juu yangu;+ 27 nanyi, mtatoa ushahidi,+ kwa sababu mmekuwa pamoja nami kutoka wakati nilipoanza.
16 “Nimewaambia ninyi mambo haya ili msikwazike.+ 2 Watu watawafukuza ninyi katika sinagogi.+ Kwa kweli, saa inakuja wakati ambapo kila mtu anayewaua ninyi atafikiri amemtolea Mungu utumishi mtakatifu.+ 3 Lakini watafanya mambo haya kwa sababu hawamjui Baba wala hawanijui.+ 4 Hata hivyo, nimewaambia ninyi mambo haya ili, saa ya mambo haya itakapofika, mpate kukumbuka niliwaambia mambo haya.+
“Hata hivyo, mambo haya sikuwaambia hapo kwanza, kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi. 5 Lakini sasa ninaenda kwake aliyenituma,+ na bado hakuna hata mmoja wenu anayeniuliza, ‘Unaenda wapi?’ 6 Lakini kwa sababu nimewaambia mambo haya huzuni+ imejaa mioyoni mwenu. 7 Hata hivyo, ninawaambia ninyi kweli, ninaenda zangu kwa faida yenu. Kwa maana nisipoenda zangu, msaidizi+ hatakuja kwenu kamwe; bali nikienda zangu, nitamtuma kwenu. 8 Naye atakapofika ataupa ulimwengu uthibitisho wenye kusadikisha kuhusu dhambi na kuhusu uadilifu na kuhusu hukumu:+ 9 kwanza, kuhusu dhambi,+ kwa sababu hawaniamini;+ 10 kisha kuhusu uadilifu,+ kwa sababu ninaenda kwa Baba nanyi hamtaniona tena; 11 kisha kuhusu hukumu,+ kwa sababu mtawala wa ulimwengu huu amehukumiwa.+
12 “Bado nina mambo mengi ya kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili kwa sasa.+ 13 Hata hivyo, huyo atakapofika, roho ya ile kweli,+ atawaongoza ninyi ndani ya kweli yote, kwa maana hatasema kwa msukumo wake mwenyewe, bali mambo anayoyasikia atasema, naye atawatangazia mambo yanayokuja.+ 14 Huyo atanitukuza,+ kwa sababu atapokea lililo langu na kulitangaza kwenu.+ 15 Yote aliyo nayo Baba ni yangu.+ Ndiyo sababu nilisema yeye hupokea lililo langu na kulitangaza kwenu. 16 Baada ya muda kidogo hamtaniona tena,+ na, tena, baada ya muda kidogo mtaniona.”
17 Kwa hiyo baadhi ya wanafunzi wake wakaambiana: “Hili analotuambia linamaanisha nini, ‘Baada ya muda kidogo hamtaniona, na, tena, baada ya muda kidogo mtaniona,’ na, ‘kwa sababu ninaenda kwa Baba’?” 18 Kwa hiyo walikuwa wakisema: “Hili analosema linamaanisha nini, ‘muda kidogo’? Sisi hatujui analoongea juu yake.” 19 Yesu alijua+ walikuwa wanataka kumuuliza, kwa hiyo akawaambia: “Je, mnaulizana kati yenu wenyewe juu ya hili, kwa sababu nilisema, Baada ya muda kidogo hamtaniona, na, tena, baada ya muda kidogo mtaniona? 20 Kwa kweli kabisa ninawaambia, Ninyi mtalia na kuomboleza, bali ulimwengu utashangilia; mtahuzunika,+ lakini huzuni yenu itageuzwa kuwa shangwe.+ 21 Mwanamke, anapokuwa akizaa, ana huzuni, kwa sababu saa yake imefika;+ lakini baada ya kuzaa mtoto mchanga, haikumbuki tena dhiki kwa sababu ya shangwe ya kwamba mtu amezaliwa ulimwenguni. 22 Kwa hiyo, ninyi pia, sasa, kwa kweli, mna huzuni; lakini nitawaona ninyi tena na mioyo yenu itashangilia,+ na hakuna mtu atakayeichukua shangwe yenu kutoka kwenu. 23 Na siku hiyo+ hamtaniuliza swali kamwe. Kwa kweli kabisa ninawaambia, Mkimwomba Baba jambo lolote+ atawapa katika jina langu.+ 24 Mpaka wakati huu wa sasa ninyi hamjaomba hata jambo moja katika jina langu. Ombeni nanyi mtapokea, ili shangwe yenu ipate kujazwa.+
25 “Nimewaambia ninyi mambo haya kwa mifano.+ Saa inakuja wakati ambapo hakika sitasema nanyi tena kwa mifano, bali nitawaeleza waziwazi kuhusu Baba. 26 Siku hiyo mtaomba katika jina langu, nami siwaambii kwamba nitamwomba Baba kuwahusu ninyi. 27 Kwa maana Baba mwenyewe anawapenda ninyi, kwa sababu mmenipenda+ na mmeamini kwamba mimi nilitoka nikiwa mwakilishi wa Baba.+ 28 Mimi nilitoka kwa Baba na nimekuja ulimwenguni. Na zaidi ya hayo, ninauacha ulimwengu nami ninaenda kwa Baba.”+
29 Wanafunzi wake wakasema: “Unaona! Sasa unasema waziwazi, nawe husemi kwa mifano. 30 Sasa tunajua kwamba unajua mambo yote+ na huhitaji kuulizwa swali na yeyote.+ Kwa hili sisi tunaamini kwamba ulitoka kwa Mungu.”+ 31 Yesu akawajibu: “Je, mnaamini sasa? 32 Tazameni! Saa inakuja, kwa kweli, imekuja, wakati mtakapotawanyika na kwenda kila mmoja kwenye nyumba+ yake nanyi mtaniacha peke yangu; na bado siko peke yangu, kwa sababu Baba yuko pamoja nami.+ 33 Nimewaambia mambo haya ili kupitia kwangu mpate kuwa na amani.+ Ulimwenguni mna dhiki, lakini jipeni moyo! Mimi nimeushinda ulimwengu.”+
17 Yesu alisema mambo haya, akainua macho yake mbinguni,+ akasema: “Baba, saa imefika; mtukuze mwana wako, ili mwana wako apate kukutukuza wewe,+ 2 kulingana na vile ambavyo umempa mamlaka juu ya wote wenye mwili,+ ili, wote ambao umempa,+ yeye apate kuwapa uzima wa milele.+ 3 Uzima wa milele+ ndio huu, waendelee kupata ujuzi+ juu yako wewe, Mungu wa pekee wa kweli,+ na juu ya yule uliyemtuma, Yesu Kristo.+ 4 Nimekutukuza+ duniani, nikiwa nimemaliza kazi ambayo umenipa niifanye.+ 5 Kwa hiyo sasa wewe, Baba, nitukuze kando yako kwa utukufu niliokuwa nao kando yako kabla ya ulimwengu kuwako.+
6 “Nimelifunua jina lako kwa watu ulionipa kutoka ulimwenguni.+ Walikuwa wako, nawe ukanipa, nao wamelishika neno lako. 7 Sasa wamejua kwamba yote uliyonipa yametoka kwako; 8 kwa sababu maneno uliyonipa nimewapa, nao wameyapokea+ na wamejua kwamba nilitoka nikiwa mwakilishi+ wako, nao wameamini kwamba ulinituma.+ 9 Ninaomba juu yao; ninawaombea hao, siuombei ulimwengu,+ bali ninawaombea wale ambao umenipa; kwa sababu ni wako, 10 na vitu vyangu vyote ni vyako na vyako ni vyangu,+ nami nimetukuzwa kati yao.
11 “Pia, mimi simo tena ulimwenguni, bali wao wamo ulimwenguni+ nami ninakuja kwako. Baba Mtakatifu, walinde+ kwa sababu ya jina lako ambalo umenipa, ili wawe kitu kimoja kama vile sisi tulivyo.+ 12 Nilipokuwa pamoja nao nilikuwa nikiwalinda+ kwa sababu ya jina lako ambalo umenipa; nami nimewatunza, na hata mmoja wao hakuangamizwa+ ila yule mwana wa maangamizi,+ ili andiko lipate kutimizwa.+ 13 Lakini sasa ninakuja kwako, nami ninasema mambo haya ulimwenguni ili wao wapate kuwa na shangwe yangu ndani yao wenyewe kwa ukamili.+ 14 Nimewapa neno lako, lakini ulimwengu umewachukia,+ kwa sababu wao si sehemu ya ulimwengu, kama vile ambavyo mimi si sehemu ya ulimwengu.+
15 “Ninakuomba, si kwamba uwatoe ulimwenguni, bali uwalinde kwa sababu ya yule mwovu.+ 16 Wao si sehemu ya ulimwengu,+ kama vile ambavyo mimi si sehemu ya ulimwengu.+ 17 Watakase+ kwa njia ya ile kweli; neno+ lako ni kweli.+ 18 Kama vile ulivyonituma ulimwenguni, vivyo hivyo mimi pia nimewatuma ulimwenguni.+ 19 Nami ninajitakasa kwa ajili yao, ili wao pia watakaswe+ kwa njia ya ile kweli.
20 “Ninawaombea, si hawa tu, bali pia wale wanaoniamini kupitia neno lao;+ 21 ili wote wapate kuwa kitu kimoja,+ kama vile ambavyo wewe, Baba, umo katika muungano pamoja na mimi na mimi nimo katika muungano pamoja na wewe,+ ili wao pia wapate kuwa katika muungano pamoja na sisi,+ ili ulimwengu upate kuamini kwamba ulinituma.+ 22 Pia, nimewapa utukufu ambao umenipa, ili wapate kuwa kitu kimoja kama vile sisi tulivyo kitu kimoja.+ 23 Mimi katika muungano pamoja na wao na wewe katika muungano pamoja na mimi, ili wapate kukamilishwa kuwa kitu kimoja,+ ili ulimwengu upate kujua kwamba wewe ulinituma na kwamba uliwapenda wao kama vile ulivyonipenda mimi. 24 Baba, kwa habari ya kile ambacho umenipa, ninataka kwamba, mahali nilipo, wao pia wapate kuwa pamoja nami,+ ili wauone utukufu wangu ambao umenipa, kwa sababu ulinipenda kabla ya kuwekwa kwa msingi+ wa ulimwengu.+ 25 Baba Mwadilifu,+ kwa kweli, ulimwengu haujakujua wewe;+ lakini mimi nimekujua, na hawa wamejua kwamba ulinituma.+ 26 Nami nimewajulisha+ jina lako nami nitalijulisha, ili upendo ulionipenda nao upate kuwa ndani yao nami katika muungano pamoja nao.”+
18 Akiisha kusema mambo hayo, Yesu akaenda pamoja na wanafunzi wake ng’ambo ya mto wa majira ya baridi kali wa Kidroni+ mpaka mahali palipokuwa na bustani, na yeye na wanafunzi wake wakaingia ndani yake.+ 2 Basi Yuda pia, msaliti wake, alipajua mahali hapo, kwa sababu nyakati nyingi Yesu alikuwa amekutana hapo pamoja na wanafunzi wake.+ 3 Kwa hiyo Yuda akachukua kikosi cha askari-jeshi na maofisa wa wakuu wa makuhani na wa Mafarisayo nao wakaja hapo wakiwa na mienge na taa na silaha.+ 4 Kwa hiyo, Yesu akijua mambo yote ambayo yangempata,+ akatoka na kuwaambia: “Mnamtafuta nani?” 5 Wakamjibu: “Yesu Mnazareti.”+ Akawaambia: “Mimi ndiye.” Basi Yuda, msaliti+ wake, alikuwa pia amesimama pamoja nao.
6 Hata hivyo, alipowaambia: “Mimi ndiye,” wakarudi nyuma+ na kuanguka chini. 7 Kwa hiyo akawauliza tena: “Mnamtafuta nani?” Wakasema: “Yesu Mnazareti.” 8 Yesu akajibu: “Niliwaambia mimi ndiye. Kwa hiyo, ikiwa ni mimi mnayetafuta, acheni hawa waende”; 9 ili neno lipate kutimizwa ambalo yeye alisema: “Kati ya wale ambao umenipa sikumpoteza hata mmoja.”+
10 Ndipo Simoni Petro, kwa kuwa alikuwa na upanga, akauchomoa na kumpiga mtumwa wa kuhani mkuu, akalikata sikio lake la kuume.+ Jina la mtumwa huyo lilikuwa Malko. 11 Hata hivyo, Yesu akamwambia Petro: “Tia upanga ndani ya ala yake.+ Kikombe ambacho Baba amenipa, je, sipaswi kukinywa?”+
12 Basi kikosi cha askari-jeshi na kiongozi wa kijeshi na maofisa wa Wayahudi wakamkamata Yesu na kumfunga, 13 nao wakampeleka kwanza kwa Anasi; kwa maana alikuwa baba-mkwe wa Kayafa, ambaye alikuwa kuhani mkuu mwaka huo.+ 14 Kwa kweli, Kayafa ndiye aliyewashauri Wayahudi kwamba ilikuwa kwa faida yao mtu mmoja afe kwa ajili ya watu.+
15 Sasa Simoni Petro na vilevile mwanafunzi mwingine alikuwa akimfuata Yesu.+ Mwanafunzi huyo alijulikana na kuhani mkuu, naye akaingia pamoja na Yesu ndani ya ua wa kuhani mkuu, 16 lakini Petro alikuwa amesimama nje kwenye mlango.+ Kwa hiyo yule mwanafunzi mwingine, ambaye alijulikana na kuhani mkuu, akatoka nje na kusema na mtunza-mlango, akamwingiza Petro ndani. 17 Basi kijakazi, aliye mtunza-mlango, akamwambia Petro: “Wewe pia ni mmoja wa wanafunzi wa mtu huyu, sivyo?” Akasema: “Hapana.”+ 18 Sasa wale watumwa na maofisa walikuwa wamesimama huku na huku, kwa kuwa walikuwa wamewasha moto wa makaa,+ kwa sababu kulikuwa na baridi, nao walikuwa wakiota moto. Petro pia alikuwa amesimama pamoja nao akiota moto.
19 Na kwa hiyo mkuu wa makuhani akamuuliza Yesu juu ya wanafunzi wake na juu ya fundisho lake. 20 Yesu akamjibu: “Nimesema na ulimwengu hadharani. Sikuzote nilifundisha katika sinagogi na katika hekalu,+ ambapo Wayahudi wote hukusanyika; nami sikusema jambo lolote katika siri. 21 Kwa nini unaniuliza? Waulize wale ambao wamesikia lile nililowaambia. Ona! Hawa wanajua lile nililosema.” 22 Baada ya kusema mambo hayo, mmoja wa maofisa aliyekuwa amesimama kando akampiga Yesu kofi+ usoni na kusema: “Je, hivyo ndivyo unavyomjibu mkuu wa makuhani?” 23 Yesu akamjibu: “Ikiwa nimesema vibaya, toa ushahidi kuhusu ubaya wenyewe; lakini ikiwa nimesema sawasawa, kwa nini unanipiga?” 24 Basi Anasi akaagiza apelekwe kwa Kayafa kuhani mkuu+ akiwa amefungwa.
25 Sasa Simoni Petro alikuwa amesimama akiota moto. Ndipo wakamwambia: “Wewe pia ni mmoja wa wanafunzi wake, sivyo?” Akakana na kusema: “Hapana.”+ 26 Mmoja wa watumwa wa kuhani mkuu, akiwa ni jamaa ya mtu ambaye Petro alikata sikio lake,+ akasema: “Mimi nilikuona katika bustani pamoja naye, sivyo?” 27 Hata hivyo, Petro akakana tena; na mara jogoo akawika.+
28 Basi wakampeleka Yesu kutoka kwa Kayafa mpaka kwenye jumba la gavana.+ Sasa ilikuwa asubuhi. Lakini wao wenyewe hawakuingia ndani ya jumba la gavana, ili wasipate kutiwa unajisi+ bali wapate kula pasaka. 29 Kwa hiyo Pilato akawajia nje na kusema: “Ni shtaka gani ambalo mnaleta juu ya mtu huyu?”+ 30 Wakamwambia: “Kama mtu huyu hangekuwa mkosaji, hatungemtia mkononi mwako.” 31 Kwa sababu hiyo Pilato akawaambia: “Mchukueni ninyi wenyewe na kumhukumu kulingana na sheria yenu.”+ Wayahudi wakamwambia: “Si halali kwetu kumuua mtu yeyote.”+ 32 Kusudi neno la Yesu litimizwe alilosema ili kutoa ishara ni kifo cha namna gani ambacho angekufa.+
33 Kwa hiyo Pilato akaingia tena ndani ya jumba la gavana naye akamwita Yesu na kumwambia: “Je, wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?”+ 34 Yesu akajibu: “Je, jambo unalosema umejitungia mwenyewe, au wengine walikuambia juu yangu?”+ 35 Pilato akajibu: “Je, mimi ni Myahudi? Taifa lako mwenyewe na wakuu wa makuhani walikutia mikononi mwangu.+ Ulifanya nini?” 36 Yesu akajibu:+ “Ufalme wangu si sehemu ya ulimwengu huu.+ Kama ufalme wangu ungekuwa sehemu ya ulimwengu huu, watumishi wangu wangepigana+ ili nisitiwe mikononi mwa Wayahudi. Lakini, kama ilivyo, ufalme wangu hautoki katika chanzo hiki.” 37 Kwa hiyo Pilato akamwambia: “Kwa hiyo, basi, je, wewe ni mfalme?” Yesu akajibu: “Wewe mwenyewe unasema kwamba mimi ni mfalme.+ Kwa ajili ya hili mimi nimezaliwa, na kwa ajili ya hili nimekuja ulimwenguni, ili nitoe ushahidi juu ya ile kweli.+ Kila mtu aliye upande wa ile kweli+ huisikiliza sauti yangu.”+ 38 Pilato akamwambia: “Kweli ni nini?”
Na baada ya kusema hili, akatoka tena kwenda kwa Wayahudi na kuwaambia: “Mimi sioni kosa lolote ndani yake.+ 39 Zaidi ya hayo, ninyi mna desturi kwamba niwafungulie mtu kwenye pasaka.+ Kwa hiyo, je, mnataka niwafungulie mfalme wa Wayahudi?” 40 Basi wakapaaza sauti tena, wakisema: “Si mtu huyu, bali Baraba!” Basi Baraba alikuwa mnyang’anyi.+
19 Kwa hiyo, wakati huo Pilato akamchukua Yesu na kumpiga mijeledi.+ 2 Nao askari-jeshi wakasokota taji la miiba na kuliweka juu ya kichwa chake nao wakampamba kwa vazi la nje la zambarau;+ 3 nao wakaanza kumjia na kusema: “Siku njema, ewe Mfalme wa Wayahudi!” Pia wakawa wakimpiga makofi usoni.+ 4 Naye Pilato akaenda nje tena na kuwaambia: “Oneni! Namleta nje kwenu kusudi mjue kwamba sioni kosa lolote ndani yake.”+ 5 Basi Yesu akaja nje, akiwa amevaa taji lenye miiba na vazi la nje la zambarau. Naye akawaambia: “Tazameni! Mwanamume!” 6 Hata hivyo, wakuu wa makuhani na maofisa walipomwona, wakapaaza sauti, wakisema: “Mtundike mtini! Mtundike mtini!”+ Pilato akawaambia: “Mchukueni ninyi wenyewe mkamtundike mtini, kwa maana mimi sioni kosa lolote ndani yake.”+ 7 Wayahudi wakamjibu: “Sisi tuna sheria,+ na kulingana na sheria anapaswa kufa, kwa sababu alijifanya mwenyewe kuwa mwana wa Mungu.”+
8 Kwa hiyo, Pilato aliposikia maneno hayo, akaogopa zaidi; 9 naye akaingia ndani ya jumba la gavana tena na kumwambia Yesu: “Wewe ni mtu wa kutoka wapi?” Lakini Yesu hakumjibu.+ 10 Kwa sababu hiyo Pilato akamwambia: “Je, husemi nami?+ Je, hujui nina mamlaka ya kukufungua na nina mamlaka ya kukutundika mtini?” 11 Yesu akamjibu: “Wewe hungekuwa na mamlaka hata kidogo juu yangu kama usingepewa kutoka juu.+ Ndiyo sababu mtu aliyenitia mikononi mwako ana dhambi kubwa zaidi.”
12 Kwa sababu hii Pilato akazidi kutafuta jinsi ya kumfungua. Lakini Wayahudi wakapaaza sauti, wakisema: “Ukimfungua mtu huyu, wewe si rafiki ya Kaisari. Kila mtu anayejifanya mfalme anasema vibaya juu ya Kaisari.”+ 13 Kwa hiyo Pilato, baada ya kusikia maneno hayo, akamleta Yesu nje, naye akaketi juu ya kiti cha hukumu mahali panapoitwa Sakafu ya Jiwe, lakini, katika Kiebrania, Gabatha. 14 Sasa kulikuwa na matayarisho+ ya pasaka; karibu saa sita. Naye akawaambia Wayahudi: “Oneni! Mfalme wenu!” 15 Hata hivyo, wakapaaza sauti: “Mwondolee mbali! Mwondolee mbali! Mtundike mtini!” Pilato akawaambia: “Je, nimtundike mtini mfalme wenu?” Wakuu wa makuhani wakajibu: “Sisi hatuna mfalme ila Kaisari.”+ 16 Kwa hiyo, wakati huo akamtia mikononi mwao, wakamtundike mtini.+
Basi wakamchukua Yesu. 17 Naye, akajibebea mti wa mateso,+ akaenda+ pale panapoitwa Mahali pa Fuvu la Kichwa, panapoitwa Golgotha katika Kiebrania;+ 18 na huko wakamtundika mtini,+ na watu wengine wawili pamoja naye, mmoja upande huu na mmoja upande huu, lakini Yesu katikati.+ 19 Pilato akaandika pia tangazo na kuliweka juu ya huo mti wa mateso. Liliandikwa: “Yesu Mnazareti Mfalme wa Wayahudi.”+ 20 Kwa hiyo wengi wa Wayahudi walilisoma tangazo hilo, kwa sababu mahali ambapo Yesu alitundikwa palikuwa karibu na jiji;+ nalo liliandikwa kwa Kiebrania, kwa Kilatini, kwa Kigiriki. 21 Hata hivyo, wakuu wa makuhani wa Wayahudi wakaanza kumwambia Pilato: “Usiandike ‘Mfalme wa Wayahudi,’ bali kwamba alisema, ‘Mimi ni Mfalme wa Wayahudi.’ ” 22 Pilato akajibu: “Yale ambayo nimeandika, nimeandika.”
23 Sasa wakati askari-jeshi walipokuwa wamemtundika Yesu mtini, wakachukua mavazi yake ya nje na kufanya sehemu nne, kwa kila askari-jeshi sehemu moja, na vazi la ndani. Lakini lile vazi la ndani lilikuwa halina mshono, likiwa limefumwa kutoka juu mpaka urefu wake wote.+ 24 Kwa hiyo wakaambiana: “Tusilirarue, bali na tuamue kwa kura juu yake litakuwa la nani.” Hii ilikuwa ili andiko lipate kutimizwa: “Waligawana mavazi yangu ya nje, nalo vazi langu walilipigia kura.”+ Ndivyo hasa hao askari-jeshi walivyofanya mambo hayo.
25 Hata hivyo, kando ya mti wa mateso wa Yesu, walikuwa wamesimama mama+ yake na dada ya mama yake; Maria+ mke wa Klopa, na Maria Magdalene.+ 26 Kwa hiyo Yesu, alipomwona mama yake na mwanafunzi ambaye alimpenda+ wamesimama kando, akamwambia mama yake: “Mwanamke, ona! Mwana wako!” 27 Halafu akamwambia mwanafunzi huyo: “Ona! Mama yako!” Na tangu saa hiyo na kuendelea mwanafunzi huyo akampeleka nyumbani kwake.
28 Baada ya hayo, Yesu alipojua kwamba kufikia sasa mambo yote yalikuwa yametimizwa, ili andiko lipate kutimizwa, akasema: “Nina kiu.”+ 29 Chombo kimoja kilichojaa divai kali kilikuwa hapo. Kwa hiyo wakaweka sifongo iliyojaa divai kali juu ya kijiti cha hisopo na kukileta kwenye kinywa chake.+ 30 Sasa, alipokuwa amepokea ile divai kali, Yesu akasema: “Imetimizwa!”+ na, akiinamisha kichwa chake, akaitoa roho yake.+
31 Basi Wayahudi, kwa kuwa yalikuwa ni Matayarisho,+ ili miili hiyo isipate kukaa+ juu ya miti ya mateso siku ya Sabato, (kwa maana siku ya Sabato hiyo ilikuwa kuu,)+ wakamwomba Pilato aagize miguu yao ivunjwe na miili iondolewe. 32 Kwa hiyo, askari-jeshi wakaja na kuvunja miguu ya mtu wa kwanza na ile ya yule mtu mwingine aliyekuwa ametundikwa mtini pamoja naye. 33 Lakini walipokuja kwa Yesu, kwa kuwa waliona kwamba tayari alikuwa amekufa, hawakuivunja miguu yake. 34 Lakini mmoja wa hao askari-jeshi akauchoma ubavu wake kwa mkuki,+ na mara moja damu na maji vikatoka. 35 Na yeye ambaye ameona hilo ametoa ushahidi, nao ushahidi wake ni wa kweli, na mtu huyo anajua kwamba yeye husema mambo ya kweli, ili ninyi pia mweze kuamini.+ 36 Kwa kweli, mambo haya yalitendeka kusudi andiko litimizwe: “Hakuna mfupa wake hata mmoja utakaovunjwa.”+ 37 Na, tena, andiko tofauti linasema: “Watamtazama Yule waliyemchoma.”+
38 Basi baada ya mambo haya Yosefu kutoka Arimathea, aliyekuwa mwanafunzi wa Yesu lakini kwa siri kwa sababu alikuwa akiwaogopa Wayahudi,+ alimwomba Pilato apate kuondoa mwili wa Yesu; naye Pilato akampa ruhusa.+ Kwa hiyo akaja na kuuondoa mwili wake.+ 39 Nikodemo pia, yule mtu aliyemjia usiku mara ya kwanza, akaja akileta msokoto wa manemane na udi, karibu ratili mia moja.+ 40 Basi wakauchukua mwili wa Yesu na kuufunga kwa vitambaa pamoja na manukato,+ sawa na jinsi Wayahudi walivyo na desturi ya kutayarisha kwa ajili ya maziko. 41 Ilitukia kwamba, mahali alipotundikwa mtini palikuwa na bustani, na katika bustani hiyo kaburi jipya,+ ambalo bado hakuna yeyote aliyekuwa amelazwa ndani yake. 42 Basi, kwa sababu ya matayarisho+ ya Wayahudi, wakamlaza Yesu humo, kwa kuwa kaburi hilo lilikuwa hapo karibu.
20 Siku ya kwanza+ ya juma Maria Magdalene akaja mapema kwenye kaburi, kulipokuwa na giza bado, naye akaona jiwe likiwa tayari limeondolewa kutoka kwenye kaburi.+ 2 Kwa hiyo akakimbia na kuja kwa Simoni Petro na kwa yule mwanafunzi+ mwingine, ambaye Yesu alikuwa anampenda, naye akawaambia: “Wamemwondoa Bwana kutoka katika kaburi,+ nasi hatujui wamemlaza wapi.”
3 Ndipo Petro+ na yule mwanafunzi mwingine wakatoka kwenda kaburini. 4 Ndiyo, hao wawili pamoja wakaanza kukimbia; lakini yule mwanafunzi mwingine akakimbia mbele ya Petro mbio zaidi naye akafika kaburini kwanza. 5 Naye akainama, akaona vitambaa vikiwa chini humo,+ lakini hakuingia. 6 Ndipo Simoni Petro pia akaja akimfuata, naye akaingia ndani ya kaburi. Naye akaona vitambaa vikiwa chini humo,+ 7 pia nguo iliyokuwa juu ya kichwa chake haikuwapo pamoja na vitambaa bali ilikuwa imekunjwa ikiwa peke yake. 8 Kwa hiyo, wakati huo mwanafunzi yule mwingine aliyekuwa amefika kwanza kwenye kaburi akaingia pia, naye akaona na kuamini. 9 Kwa maana bado hawakufahamu andiko kwamba lazima afufuliwe kutoka kwa wafu.+ 10 Na kwa hiyo wanafunzi wakarudi nyumbani kwao.
11 Hata hivyo, Maria akaendelea kusimama nje karibu na kaburi, akilia. Ndipo, alipokuwa akilia, akainama kutazama ndani ya kaburi 12 naye akaona malaika+ wawili waliokuwa wamevaa mavazi meupe wakiwa wameketi mmoja kichwani na mwingine miguuni ambapo mwili wa Yesu ulikuwa umelazwa. 13 Nao wakamwambia: “Mwanamke, kwa nini unalia?” Akawaambia: “Wamemwondoa Bwana wangu, nami sijui wamemlaza wapi.” 14 Baada ya kusema hayo, akageuka na kumwona Yesu akiwa amesimama, lakini hakufahamu ni Yesu.+ 15 Yesu akamwambia: “Mwanamke, kwa nini unalia? Unamtafuta nani?”+ Yeye, akiwaza ni mtunza-bustani, akamwambia: “Bwana, ikiwa umemchukua, niambie umemlaza wapi, nami nitamwondoa.” 16 Yesu akamwambia: “Maria!”+ Alipogeuka, Maria akamwambia, katika Kiebrania: “Raboni!”+ (ambalo linamaanisha “Mwalimu!”) 17 Yesu akamwambia: “Acha kuning’ang’ania. Kwa maana bado sijapanda kwenda kwa Baba. Lakini nenda kwa ndugu+ zangu, nawe uwaambie, ‘Mimi ninapanda kwenda kwa Baba+ yangu na Baba yenu na kwa Mungu wangu+ na Mungu wenu.’ ”+ 18 Maria Magdalene akaja na kuleta habari hizo kwa wanafunzi: “Nimemwona Bwana!” na kwamba alimwambia mambo hayo.+
19 Kwa hiyo, ilipokuwa jioni-jioni siku hiyo, siku ya kwanza ya juma,+ na, ijapokuwa milango ilikuwa imefungwa mahali ambamo wanafunzi walikuwa kwa sababu ya kuwaogopa+ Wayahudi, Yesu alikuja+ na kusimama katikati yao na kuwaambia: “Na muwe na amani.”+ 20 Na baada ya kusema hayo, akawaonyesha mikono yake miwili na ubavu wake.+ Basi wanafunzi hao wakashangilia+ kwa kumwona Bwana. 21 Kwa hiyo, Yesu akawaambia tena: “Na muwe na amani. Kama vile ambavyo Baba amenituma,+ mimi pia ninawatuma ninyi.”+ 22 Na baada ya kusema jambo hilo akapuliza juu yao na kuwaambia: “Pokeeni roho takatifu.+ 23 Mkisamehe dhambi za watu wowote,+ watakuwa wamesamehewa; msiposamehe zile za watu wowote, watakuwa hawajasamehewa.”+
24 Lakini Tomasi,+ mmoja wa wale kumi na wawili, aliyeitwa Pacha, hakuwa pamoja nao Yesu alipokuja. 25 Kwa hiyo wanafunzi wengine wakawa wanamwambia: “Tumemwona Bwana!” Lakini yeye akawaambia: “Nisipoona katika mikono yake alama ya misumari na nitie kidole changu katika alama ya misumari na kuutia mkono wangu ndani ya ubavu wake,+ hakika mimi sitaamini.”+
26 Basi, siku nane baadaye wanafunzi wake walikuwa tena ndani ya nyumba, naye Tomasi alikuwa pamoja nao. Yesu akaja, ijapokuwa milango ilikuwa imefungwa, naye akasimama katikati yao, akasema: “Na muwe na amani.”+ 27 Halafu akamwambia Tomasi: “Weka kidole chako hapa, uone mikono yangu, na chukua mkono+ wako utie ndani ya ubavu wangu, na uache kuwa asiyeamini bali uwe mwenye kuamini.” 28 Tomasi akajibu akamwambia: “Bwana wangu na Mungu wangu!”+ 29 Yesu akamwambia: “Kwa sababu umeniona je, umeamini? Wenye furaha ni wale ambao hawaoni na bado wanaamini.”+
30 Kwa hakika, Yesu alifanya pia ishara nyingine nyingi mbele ya wanafunzi hao, ambazo hazikuandikwa katika kitabu hiki cha kukunjwa.+ 31 Lakini haya yameandikwa+ ili mpate kuamini kwamba Yesu ndiye Kristo Mwana wa Mungu, na kwamba, kwa sababu ya kuamini,+ mpate kuwa na uzima kupitia jina lake.
21 Baada ya mambo haya Yesu alijifunua tena kwa wanafunzi kwenye bahari ya Tiberia; lakini alijifunua hivi. 2 Waliokuwa pamoja ni Simoni Petro na Tomasi, aliyeitwa Pacha,+ na Nathanaeli+ kutoka Kana ya Galilaya na wana wa Zebedayo+ na wengine wawili kati ya wanafunzi wake. 3 Simoni Petro akawaambia: “Ninaenda kuvua samaki.” Wakamwambia: “Sisi pia tutakwenda pamoja nawe.” Wakatoka kwenda, wakapanda ndani ya mashua, lakini usiku huo hawakuvua kitu.+
4 Hata hivyo, ilipokuwa tu inakaribia kuwa asubuhi, Yesu akasimama pwani, lakini wanafunzi, bila shaka, hawakufahamu kwamba ni Yesu.+ 5 Basi Yesu akawaambia: “Watoto, je, mna chakula chochote?” Wakamjibu: “Hapana!” 6 Akawaambia: “Utupeni wavu upande wa kuume wa mashua, nanyi mtapata.”+ Basi wakautupa, lakini hawakuweza tena kuuvuta ndani kwa sababu samaki walikuwa wengi sana.+ 7 Kwa hiyo mwanafunzi ambaye Yesu alikuwa akimpenda,+ akamwambia Petro:+ “Ni Bwana!” Kwa hiyo Simoni Petro, aliposikia kwamba ni Bwana, akajifunga mwenyewe kwa kujizungushia kiunoni vazi lake la juu, kwa maana alikuwa uchi, akajitumbukiza ndani ya bahari. 8 Lakini wale wanafunzi wengine wakaja katika ile mashua ndogo, kwa maana hawakuwa mbali na nchi kavu, karibu umbali wa meta 90 tu, wakiukokota wavu wenye samaki wengi.
9 Hata hivyo, waliposhuka kwenye nchi kavu wakaona moto wa makaa+ na samaki juu yake na mkate. 10 Yesu akawaambia: “Leteni baadhi ya samaki mliowavua sasa hivi.” 11 Kwa hiyo, Simoni Petro akapanda ndani na kuuvuta wavu kwenye nchi kavu ukiwa umejaa samaki wakubwa 153. Lakini ijapokuwa kulikuwako wengi sana wavu haukupasuka. 12 Yesu akawaambia: “Njooni, mpate kiamsha-kinywa chenu.”+ Hakuna hata mmoja wa wanafunzi aliyekuwa na moyo wa kumuuliza: “Wewe ni nani?” kwa sababu walijua ni Bwana. 13 Yesu akaja, akachukua mkate na kuwapa,+ na samaki vivyo hivyo. 14 Sasa hii ilikuwa ni mara ya tatu+ ambayo Yesu aliwatokea wanafunzi baada ya kufufuliwa kwake kutoka kwa wafu.
15 Basi, walipokuwa wamepata kiamsha-kinywa, Yesu akamwambia Simoni Petro: “Simoni mwana wa Yohana, je, unanipenda kuliko hawa?”+ Akamwambia: “Ndiyo, Bwana, unajua ninakupenda.”+ Akamwambia: “Lisha wana-kondoo wangu.”+ 16 Tena akamwambia, mara ya pili: “Simoni mwana wa Yohana, je, unanipenda?”+ Akamwambia: “Ndiyo, Bwana, unajua ninakupenda.” Akamwambia: “Chunga kondoo wangu wadogo.”+ 17 Akamwambia mara ya tatu: “Simoni mwana wa Yohana, je, unanipenda?” Petro akahuzunika kwamba alimwambia mara ya tatu: “Je, unanipenda?” Kwa hiyo akamwambia: “Bwana, wewe unajua mambo yote;+ unajua kwamba ninakupenda.” Yesu akamwambia: “Lisha kondoo wangu wadogo.+ 18 Kwa kweli kabisa ninakuambia, Ulipokuwa kijana, ulikuwa ukijifunga kiuno na kutembea huku na huku kokote ulikotaka. Lakini utakapozeeka utanyoosha mikono yako na mtu mwingine atakufunga kiuno+ na kukupeleka usikotaka wewe.”+ 19 Hilo alisema ili kutoa ishara ni kwa kifo+ cha namna gani yeye angemtukuza Mungu.+ Kwa hiyo, alipokuwa amesema hayo, akamwambia: “Endelea kunifuata.”+
20 Petro alipogeuka, alimwona mwanafunzi ambaye Yesu alikuwa akimpenda,+ akifuata, yule ambaye kwenye mlo wa jioni alikuwa pia ameegemea nyuma kifuani pake akasema: “Bwana, ni nani anayekusaliti?” 21 Basi, alipomwona, Petro akamwambia Yesu: “Bwana, mtu huyu atafanya nini?” 22 Yesu akamwambia: “Ikiwa ni mapenzi yangu akae mpaka nije,+ hilo linakuhusu nini wewe? Wewe endelea kunifuata mimi.” 23 Kwa sababu hiyo, maneno hayo yakaenea kati ya akina ndugu, kwamba mwanafunzi huyo hangekufa. Hata hivyo, Yesu hakumwambia kwamba hangekufa, bali: “Ikiwa ni mapenzi yangu akae+ mpaka nije, hilo linakuhusu nini wewe?”
24 Huyo ndiye mwanafunzi+ ambaye anatoa ushahidi juu ya mambo haya na ambaye aliyaandika mambo haya, na sisi tunajua kwamba ushahidi anaotoa ni wa kweli.+
25 Kwa kweli, kuna mambo mengine mengi pia aliyofanya Yesu, ambayo, kama yangeandikwa kirefu, nadhani ulimwengu wenyewe haungeweza kuwa na nafasi ya kuviweka vitabu vya kukunjwa ambavyo vingeandikwa.+