Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 16:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Kwa maana hutaiacha nafsi yangu katika Kaburi.*+

      Hutamruhusu mshikamanifu wako aone shimo.+

  • Zaburi 22:utangulizi-31
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • Kwa kiongozi juu ya Paa wa Mapambazuko. Muziki wa Daudi.

      22 Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?+

      Kwa nini uko mbali usiniokoe,+

      Mbali na maneno ya mngurumo wangu?+

       2 Ee Mungu wangu, mimi huendelea kuita wakati wa mchana, nawe huitiki;+

      Na wakati wa usiku, wala sinyamazi.+

       3 Lakini wewe ni mtakatifu,+

      Unayekaa juu ya sifa za Israeli.+

       4 Baba zetu walikutegemea wewe;+

      Walikutegemea, nawe ukaendelea kuwaokoa.+

       5 Walikulilia,+ nao wakawa salama;+

      Walikutegemea, nao hawakuona aibu.+

       6 Lakini mimi ni mdudu,+ wala si mtu,

      Shutuma kwa wanadamu na mwenye kudharaulika kwa watu.+

       7 Wale wote wanaoniona mimi, hunidharau;+

      Wanaendelea kufungua vinywa vyao wazi, wanaendelea kutikisa vichwa vyao:+

       8 “Yeye alijitia mikononi mwa Yehova.+ Acha Yeye amwokoe!+

      Na amkomboe, kwa kuwa yeye amependezwa naye!”+

       9 Kwa maana Wewe ndiye uliyenitoa tumboni,+

      Wewe ndiye unayenifanya niwe na tegemeo nilipokuwa kwenye maziwa ya mama yangu.+

      10 Nimetupwa kwako kutoka tumbo la uzazi;+

      Kutoka katika tumbo la mama yangu wewe umekuwa Mungu wangu.+

      11 Usikae mbali nami, kwa sababu taabu iko karibu,+

      Kwa sababu hakuna msaidizi mwingine.+

      12 Ng’ombe-dume wengi wachanga wamenizingira;+

      Wale wenye nguvu wa Bashani wamenizunguka.+

      13 Wamefungua vinywa vyao dhidi yangu,+

      Kama simba anayerarua vipande-vipande na kunguruma.+

      14 Nimemwagwa kama maji,+

      Na mifupa yangu yote imetenganishwa.+

      Moyo wangu umekuwa kama nta;+

      Umeyeyuka ndani katika sehemu zangu za ndani.+

      15 Nguvu zangu zimekauka kama kigae cha udongo,+

      Na ulimi wangu umefanywa ushikamane na ufizi wangu;+

      Nawe unaniweka katika mavumbi ya kifo.+

      16 Kwa maana mbwa wamenizingira;+

      Kusanyiko la watenda-maovu limenizunguka.+

      Wako kwenye mikono yangu na miguu yangu kama simba.+

      17 Naweza kuhesabu mifupa yangu yote.+

      Wao hutazama, hunikazia macho.+

      18 Wanagawana mavazi yangu,+

      Nao wanalipigia kura vazi langu.+

      19 Lakini wewe, Ee Yehova, usikae mbali.+

      Ewe nguvu zangu,+ ufanye haraka kuja kunisaidia.+

      20 Uikomboe nafsi yangu kutokana na upanga,+

      Nafsi yangu ya pekee kutokana na wayo wa mbwa;+

      21 Uniokoe kutokana na kinywa cha simba,+

      Na unijibu na kuniokoa kutokana na pembe za ng’ombe-mwitu.+

      22 Nitalitangaza jina lako+ kwa ndugu zangu;+

      Katikati ya kutaniko nitakusifu wewe.+

      23 Ninyi mnaomwogopa Yehova, msifuni!+

      Enyi nyote mlio uzao wa Yakobo, mtukuzeni!+

      Na mwogopeni yeye, enyi nyote mlio uzao wa Israeli.+

      24 Kwa maana hakudharau+

      Wala kuchoshwa na mateso ya mwenye kuteseka;+

      Naye hakumficha uso wake,+

      Naye alipomlilia amsaidie alisikia.+

      25 Kutoka kwako sifa yangu itakuwa katika kutaniko kubwa;+

      Nadhiri zangu nitazitimiza mbele ya wale wanaomwogopa.+

      26 Wapole watakula na kushiba;+

      Wale wanaomtafuta watamsifu Yehova.+

      Mioyo yenu na iishi milele.+

      27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kurudi kwa Yehova.+

      Na familia zote za mataifa zitainama mbele zako.+

      28 Kwa maana ufalme ni wa Yehova,+

      Naye anayatawala mataifa.+

      29 Wote walio wanono wa dunia watakula na kuinama;+

      Wote wanaoenda chini mavumbini watainama mbele zake,+

      Wala hakuna atakayeihifadhi hai nafsi yake.+

      30 Uzao utamtumikia;+

      Kizazi hicho kitatangaziwa juu ya Yehova.+

      31 Watakuja na kusema juu ya uadilifu wake+

      Kwa kikundi cha watu kitakachozaliwa, kwamba ni yeye amefanya hilo.+

  • Zaburi 34:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Yeye anailinda mifupa yote ya mtu huyo;

      Hakuna hata mmoja uliovunjwa.+

  • Zaburi 41:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  9 Pia mtu mwenye kuwa na amani nami, ambaye nimemtegemea,+

      Ambaye alikuwa akila mkate wangu,+ amekiinua kisigino chake dhidi yangu.+

  • Zaburi 69:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Lakini walinipa mmea wenye sumu kuwa chakula,+

      Na kwa ajili ya kiu yangu wakajaribu kuninywesha siki.+

  • Isaya 53:1-12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 53 Ni nani aliyeliamini jambo ambalo tumesikia?+ Na kwa habari ya mkono wa Yehova,+ umefunuliwa kwa nani?+ 2 Naye atapanda kama tawi+ mbele ya mtu, na kama mzizi kutoka katika nchi isiyo na maji. Yeye hana umbo la fahari,+ wala utukufu wowote; nasi tutakapomwona, hana sura ili kwamba tumtamani.+

      3 Alidharauliwa na kuepukwa na wanadamu,+ mtu aliyekusudiwa maumivu na kuzoeana na ugonjwa.+ Na ilikuwa kana kwamba uso ulifichwa kutoka kwetu.+ Alidharauliwa, nasi tulimhesabu kuwa asiye na maana.+ 4 Kwa kweli yeye mwenyewe aliyachukua magonjwa yetu;+ na kwa habari ya maumivu yetu, yeye aliyabeba.+ Lakini sisi tulimhesabu kama aliyepata mapigo,+ aliyepigwa na Mungu+ na kuteswa.+ 5 Lakini alikuwa akichomwa kwa silaha+ kwa ajili ya ukosaji wetu;+ alikuwa akipondwa kwa ajili ya makosa yetu.+ Adhabu iliyokusudiwa kuleta amani yetu ilikuwa juu yake,+ na kwa sababu ya majeraha+ yake sisi tumeponywa.+ 6 Sisi sote tumeenda huku na huku kama kondoo;+ sisi tumegeuka kwenda kila mmoja kwenye njia yake; na Yehova amefanya kosa letu sote likutane na huyo.+ 7 Alikazwa sana,+ naye alijiachilia ateswe;+ ingawa hivyo hakufungua kinywa chake. Alikuwa akiletwa kama kondoo machinjioni;+ na kama kondoo-jike ambaye amekuwa bubu mbele ya wakataji-manyoya wake, yeye pia hakufungua kinywa chake.+

      8 Kwa sababu ya kizuizi na hukumu yeye aliondolewa mbali;+ na ni nani atakayejishughulisha na habari za kizazi chake?+ Kwa maana aliondolewa+ katika nchi ya walio hai.+ Alipata pigo kwa sababu ya ukosaji wa watu wangu.+ 9 Naye atafanya kaburi lake liwe pamoja na waovu,+ na pamoja na jamii ya matajiri katika kifo chake,+ ingawa yeye hakuwa amefanya jeuri+ wala hapakuwa na udanganyifu kinywani mwake.+

      10 Lakini Yehova alipendezwa kumponda;+ alimfanya kuwa mgonjwa.+ Ukiifanya nafsi yake kuwa toleo la hatia,+ atauona uzao wake,+ ataongeza siku zake,+ na mapendezi+ ya Yehova yatafanikiwa mkononi mwake.+ 11 Kwa sababu ya taabu ya nafsi yake yeye ataona,+ atatosheka.+ Kupitia ujuzi wake mtu mwadilifu, mtumishi wangu,+ atawaletea watu wengi msimamo wa uadilifu;+ naye mwenyewe atayachukua makosa yao.+ 12 Kwa sababu hiyo nitampa fungu katikati ya wengi,+ naye atagawa nyara pamoja na wenye nguvu,+ kwa sababu aliimwaga nafsi yake mpaka kufa,+ naye alihesabiwa pamoja na wakosaji;+ naye mwenyewe aliichukua dhambi ya watu wengi,+ aliingilia kati kwa ajili ya wakosaji.+

  • Mika 5:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 “Wakati huu unajikatakata,+ Ee binti uliyevamiwa; yeye ametuzingira sisi.+ Watalipiga kwa fimbo shavu la mwamuzi wa Israeli.+

  • Zekaria 9:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 “Shangilia sana, Ee binti Sayuni.+ Piga kelele za ushindi,+ Ee binti Yerusalemu. Tazama! mfalme+ wako anakuja kwako.+ Yeye ni mwadilifu, ndiyo, ameokolewa;+ ni mnyenyekevu,+ naye amepanda juu ya punda, juu ya mnyama mkomavu, mwana wa punda-jike.+

  • Zekaria 11:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Ndipo nikawaambia: “Ikiwa vema machoni penu,+ nipeni mshahara wangu; lakini kama sivyo, acheni.” Basi wakalipa mshahara wangu, vipande 30 vya fedha.+

  • Zekaria 13:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 “Ee upanga, amka juu ya mchungaji+ wangu, juu ya mwanamume ambaye ni mwenzangu,”+ asema Yehova wa majeshi. “Mpige mchungaji,+ na wale wa kundi watawanyike;+ nami nitageuza mkono wangu juu ya wale wasio na maana.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki