- 
	                        
            
            Zaburi 22:utangulizi-31Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
- 
                            - 
                                        Kwa kiongozi juu ya Paa wa Mapambazuko. Muziki wa Daudi. 22 Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?+ Kwa nini uko mbali usiniokoe,+ Mbali na maneno ya mngurumo wangu?+ 2 Ee Mungu wangu, mimi huendelea kuita wakati wa mchana, nawe huitiki;+ Na wakati wa usiku, wala sinyamazi.+ 7 Wale wote wanaoniona mimi, hunidharau;+ Wanaendelea kufungua vinywa vyao wazi, wanaendelea kutikisa vichwa vyao:+ 8 “Yeye alijitia mikononi mwa Yehova.+ Acha Yeye amwokoe!+ Na amkomboe, kwa kuwa yeye amependezwa naye!”+ 9 Kwa maana Wewe ndiye uliyenitoa tumboni,+ Wewe ndiye unayenifanya niwe na tegemeo nilipokuwa kwenye maziwa ya mama yangu.+ 10 Nimetupwa kwako kutoka tumbo la uzazi;+ Kutoka katika tumbo la mama yangu wewe umekuwa Mungu wangu.+ Na mifupa yangu yote imetenganishwa.+ Moyo wangu umekuwa kama nta;+ Umeyeyuka ndani katika sehemu zangu za ndani.+ 15 Nguvu zangu zimekauka kama kigae cha udongo,+ Na ulimi wangu umefanywa ushikamane na ufizi wangu;+ Nawe unaniweka katika mavumbi ya kifo.+ 16 Kwa maana mbwa wamenizingira;+ Kusanyiko la watenda-maovu limenizunguka.+ Wako kwenye mikono yangu na miguu yangu kama simba.+ 21 Uniokoe kutokana na kinywa cha simba,+ Na unijibu na kuniokoa kutokana na pembe za ng’ombe-mwitu.+ 23 Ninyi mnaomwogopa Yehova, msifuni!+ Enyi nyote mlio uzao wa Yakobo, mtukuzeni!+ Na mwogopeni yeye, enyi nyote mlio uzao wa Israeli.+ Wala kuchoshwa na mateso ya mwenye kuteseka;+ Naye hakumficha uso wake,+ Naye alipomlilia amsaidie alisikia.+ 25 Kutoka kwako sifa yangu itakuwa katika kutaniko kubwa;+ Nadhiri zangu nitazitimiza mbele ya wale wanaomwogopa.+ 27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kurudi kwa Yehova.+ Na familia zote za mataifa zitainama mbele zako.+ 
 
- 
                                        
- 
	                        
            
            Isaya 53:1-12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
- 
                            - 
                                        53 Ni nani aliyeliamini jambo ambalo tumesikia?+ Na kwa habari ya mkono wa Yehova,+ umefunuliwa kwa nani?+ 2 Naye atapanda kama tawi+ mbele ya mtu, na kama mzizi kutoka katika nchi isiyo na maji. Yeye hana umbo la fahari,+ wala utukufu wowote; nasi tutakapomwona, hana sura ili kwamba tumtamani.+ 3 Alidharauliwa na kuepukwa na wanadamu,+ mtu aliyekusudiwa maumivu na kuzoeana na ugonjwa.+ Na ilikuwa kana kwamba uso ulifichwa kutoka kwetu.+ Alidharauliwa, nasi tulimhesabu kuwa asiye na maana.+ 4 Kwa kweli yeye mwenyewe aliyachukua magonjwa yetu;+ na kwa habari ya maumivu yetu, yeye aliyabeba.+ Lakini sisi tulimhesabu kama aliyepata mapigo,+ aliyepigwa na Mungu+ na kuteswa.+ 5 Lakini alikuwa akichomwa kwa silaha+ kwa ajili ya ukosaji wetu;+ alikuwa akipondwa kwa ajili ya makosa yetu.+ Adhabu iliyokusudiwa kuleta amani yetu ilikuwa juu yake,+ na kwa sababu ya majeraha+ yake sisi tumeponywa.+ 6 Sisi sote tumeenda huku na huku kama kondoo;+ sisi tumegeuka kwenda kila mmoja kwenye njia yake; na Yehova amefanya kosa letu sote likutane na huyo.+ 7 Alikazwa sana,+ naye alijiachilia ateswe;+ ingawa hivyo hakufungua kinywa chake. Alikuwa akiletwa kama kondoo machinjioni;+ na kama kondoo-jike ambaye amekuwa bubu mbele ya wakataji-manyoya wake, yeye pia hakufungua kinywa chake.+ 8 Kwa sababu ya kizuizi na hukumu yeye aliondolewa mbali;+ na ni nani atakayejishughulisha na habari za kizazi chake?+ Kwa maana aliondolewa+ katika nchi ya walio hai.+ Alipata pigo kwa sababu ya ukosaji wa watu wangu.+ 9 Naye atafanya kaburi lake liwe pamoja na waovu,+ na pamoja na jamii ya matajiri katika kifo chake,+ ingawa yeye hakuwa amefanya jeuri+ wala hapakuwa na udanganyifu kinywani mwake.+ 10 Lakini Yehova alipendezwa kumponda;+ alimfanya kuwa mgonjwa.+ Ukiifanya nafsi yake kuwa toleo la hatia,+ atauona uzao wake,+ ataongeza siku zake,+ na mapendezi+ ya Yehova yatafanikiwa mkononi mwake.+ 11 Kwa sababu ya taabu ya nafsi yake yeye ataona,+ atatosheka.+ Kupitia ujuzi wake mtu mwadilifu, mtumishi wangu,+ atawaletea watu wengi msimamo wa uadilifu;+ naye mwenyewe atayachukua makosa yao.+ 12 Kwa sababu hiyo nitampa fungu katikati ya wengi,+ naye atagawa nyara pamoja na wenye nguvu,+ kwa sababu aliimwaga nafsi yake mpaka kufa,+ naye alihesabiwa pamoja na wakosaji;+ naye mwenyewe aliichukua dhambi ya watu wengi,+ aliingilia kati kwa ajili ya wakosaji.+ 
 
-