-
Zaburi 22:utangulizi-31Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
Kwa kiongozi juu ya Paa wa Mapambazuko. Muziki wa Daudi.
22 Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?+
Kwa nini uko mbali usiniokoe,+
Mbali na maneno ya mngurumo wangu?+
2 Ee Mungu wangu, mimi huendelea kuita wakati wa mchana, nawe huitiki;+
Na wakati wa usiku, wala sinyamazi.+
7 Wale wote wanaoniona mimi, hunidharau;+
Wanaendelea kufungua vinywa vyao wazi, wanaendelea kutikisa vichwa vyao:+
8 “Yeye alijitia mikononi mwa Yehova.+ Acha Yeye amwokoe!+
Na amkomboe, kwa kuwa yeye amependezwa naye!”+
9 Kwa maana Wewe ndiye uliyenitoa tumboni,+
Wewe ndiye unayenifanya niwe na tegemeo nilipokuwa kwenye maziwa ya mama yangu.+
10 Nimetupwa kwako kutoka tumbo la uzazi;+
Kutoka katika tumbo la mama yangu wewe umekuwa Mungu wangu.+
Na mifupa yangu yote imetenganishwa.+
Moyo wangu umekuwa kama nta;+
Umeyeyuka ndani katika sehemu zangu za ndani.+
15 Nguvu zangu zimekauka kama kigae cha udongo,+
Na ulimi wangu umefanywa ushikamane na ufizi wangu;+
Nawe unaniweka katika mavumbi ya kifo.+
16 Kwa maana mbwa wamenizingira;+
Kusanyiko la watenda-maovu limenizunguka.+
Wako kwenye mikono yangu na miguu yangu kama simba.+
21 Uniokoe kutokana na kinywa cha simba,+
Na unijibu na kuniokoa kutokana na pembe za ng’ombe-mwitu.+
23 Ninyi mnaomwogopa Yehova, msifuni!+
Enyi nyote mlio uzao wa Yakobo, mtukuzeni!+
Na mwogopeni yeye, enyi nyote mlio uzao wa Israeli.+
Wala kuchoshwa na mateso ya mwenye kuteseka;+
Naye hakumficha uso wake,+
Naye alipomlilia amsaidie alisikia.+
25 Kutoka kwako sifa yangu itakuwa katika kutaniko kubwa;+
Nadhiri zangu nitazitimiza mbele ya wale wanaomwogopa.+
27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kurudi kwa Yehova.+
Na familia zote za mataifa zitainama mbele zako.+
-
-
Isaya 53:1-12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
53 Ni nani aliyeliamini jambo ambalo tumesikia?+ Na kwa habari ya mkono wa Yehova,+ umefunuliwa kwa nani?+ 2 Naye atapanda kama tawi+ mbele ya mtu, na kama mzizi kutoka katika nchi isiyo na maji. Yeye hana umbo la fahari,+ wala utukufu wowote; nasi tutakapomwona, hana sura ili kwamba tumtamani.+
3 Alidharauliwa na kuepukwa na wanadamu,+ mtu aliyekusudiwa maumivu na kuzoeana na ugonjwa.+ Na ilikuwa kana kwamba uso ulifichwa kutoka kwetu.+ Alidharauliwa, nasi tulimhesabu kuwa asiye na maana.+ 4 Kwa kweli yeye mwenyewe aliyachukua magonjwa yetu;+ na kwa habari ya maumivu yetu, yeye aliyabeba.+ Lakini sisi tulimhesabu kama aliyepata mapigo,+ aliyepigwa na Mungu+ na kuteswa.+ 5 Lakini alikuwa akichomwa kwa silaha+ kwa ajili ya ukosaji wetu;+ alikuwa akipondwa kwa ajili ya makosa yetu.+ Adhabu iliyokusudiwa kuleta amani yetu ilikuwa juu yake,+ na kwa sababu ya majeraha+ yake sisi tumeponywa.+ 6 Sisi sote tumeenda huku na huku kama kondoo;+ sisi tumegeuka kwenda kila mmoja kwenye njia yake; na Yehova amefanya kosa letu sote likutane na huyo.+ 7 Alikazwa sana,+ naye alijiachilia ateswe;+ ingawa hivyo hakufungua kinywa chake. Alikuwa akiletwa kama kondoo machinjioni;+ na kama kondoo-jike ambaye amekuwa bubu mbele ya wakataji-manyoya wake, yeye pia hakufungua kinywa chake.+
8 Kwa sababu ya kizuizi na hukumu yeye aliondolewa mbali;+ na ni nani atakayejishughulisha na habari za kizazi chake?+ Kwa maana aliondolewa+ katika nchi ya walio hai.+ Alipata pigo kwa sababu ya ukosaji wa watu wangu.+ 9 Naye atafanya kaburi lake liwe pamoja na waovu,+ na pamoja na jamii ya matajiri katika kifo chake,+ ingawa yeye hakuwa amefanya jeuri+ wala hapakuwa na udanganyifu kinywani mwake.+
10 Lakini Yehova alipendezwa kumponda;+ alimfanya kuwa mgonjwa.+ Ukiifanya nafsi yake kuwa toleo la hatia,+ atauona uzao wake,+ ataongeza siku zake,+ na mapendezi+ ya Yehova yatafanikiwa mkononi mwake.+ 11 Kwa sababu ya taabu ya nafsi yake yeye ataona,+ atatosheka.+ Kupitia ujuzi wake mtu mwadilifu, mtumishi wangu,+ atawaletea watu wengi msimamo wa uadilifu;+ naye mwenyewe atayachukua makosa yao.+ 12 Kwa sababu hiyo nitampa fungu katikati ya wengi,+ naye atagawa nyara pamoja na wenye nguvu,+ kwa sababu aliimwaga nafsi yake mpaka kufa,+ naye alihesabiwa pamoja na wakosaji;+ naye mwenyewe aliichukua dhambi ya watu wengi,+ aliingilia kati kwa ajili ya wakosaji.+
-