2 Wafalme
22 Yosia+ alikuwa na umri wa miaka 8 alipoanza kutawala, naye akatawala miaka 31 katika Yerusalemu. Na jina la mama yake lilikuwa Yedida binti ya Adaya kutoka Boskathi.+ 2 Naye akafanya yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova+ na kutembea katika njia yote ya Daudi babu yake,+ naye hakugeuka kando upande wa kuume wala wa kushoto.+
3 Na ikawa katika mwaka wa kumi na nane wa Mfalme Yosia kwamba mfalme akamtuma Shafani+ mwana wa Azalia mwana wa Meshulamu mwandishi kwenye nyumba ya Yehova, akisema: 4 “Nenda kwa Hilkia+ kuhani mkuu,+ naye ajumlishe pesa+ zinazoletwa katika nyumba ya Yehova+ ambazo watunza-milango+ wamekusanya kutoka kwa watu; 5 nao wazitie mkononi mwa wale wanaofanya kazi,+ waliochaguliwa, katika nyumba ya Yehova, ili wawape wale wanaofanya kazi waliomo katika nyumba ya Yehova ili kurekebisha mipasuko ya nyumba,+ 6 mafundi na wajenzi na waashi, na kununua mbao na mawe yaliyochongwa ili kuirekebisha nyumba.+ 7 Isipokuwa tu hesabu isifanywe ya zile pesa zinazotiwa mkononi mwao,+ kwa maana wanafanya kazi kwa uaminifu.”+
8 Baadaye Hilkia+ kuhani mkuu akamwambia Shafani+ mwandishi:+ “Nimepata kile kitabu chenyewe cha sheria+ katika nyumba ya Yehova.” Basi Hilkia akampa Shafani kile kitabu, naye akaanza kukisoma. 9 Kisha Shafani mwandishi akaingia kwa mfalme, akamjibu mfalme na kusema: “Watumishi wako wamemimina pesa ambazo zilikuwa ndani ya nyumba, nao wanaendelea kuzitia katika mkono wa wale wanaofanya kazi, wale waliochaguliwa, katika nyumba ya Yehova.”+ 10 Na Shafani mwandishi akaendelea kumwambia mfalme, akisema: “Hilkia kuhani amenipa kitabu+ fulani.” Na Shafani akaanza kukisoma mbele ya mfalme.
11 Na ikawa kwamba mara tu mfalme alipoyasikia maneno ya kile kitabu cha ile sheria, akayararua mavazi+ yake mara moja. 12 Kisha mfalme akawaamuru Hilkia kuhani na Ahikamu+ mwana wa Shafani na Akbori mwana wa Mikaya na Shafani mwandishi na Asaya+ mtumishi wa mfalme, akisema: 13 “Nendeni, muulizeni+ Yehova kwa ajili yangu na kwa ajili ya watu na kwa ajili ya Yuda wote kuhusu maneno ya kitabu hiki ambacho kimepatikana; kwa maana ghadhabu ya Yehova+ ni kubwa ambayo imewashwa juu yetu kwa sababu mababu+ zetu hawakuyasikiliza maneno ya kitabu hiki kwa kutenda kulingana na yote ambayo yameandikwa kutuhusu.”+
14 Basi Hilkia kuhani na Ahikamu na Akbori na Shafani na Asaya wakaenda kwa Hulda nabii,+ mke wa Shalumu mwana wa Tikva mwana wa Harhasi, mtunzaji wa mavazi,+ kwa kuwa alikuwa akikaa katika Yerusalemu katika eneo la pili; nao wakaanza kusema naye.+ 15 Naye akawaambia: “Yehova, Mungu wa Israeli, amesema hivi,+ ‘Mwambieni hivi mtu ambaye amewatuma ninyi kwangu: 16 “Yehova amesema hivi, ‘Tazama, ninaleta msiba+ juu ya mahali hapa na juu ya wakaaji+ wake, naam, maneno+ yote ya kile kitabu ambacho mfalme wa Yuda amesoma;+ 17 kwa sababu wameniacha na kwenda kuifukizia moshi wa dhabihu miungu mingine+ ili kunitia uchungu kwa kazi zote za mikono yao,+ na ghadhabu yangu imewashwa juu ya mahali hapa wala haitazimwa.’”’+ 18 Na kwa habari ya mfalme wa Yuda anayewatuma mkamuulize Yehova, mwambieni hivi, ‘Yehova, Mungu wa Israeli, amesema hivi: “Kuhusu yale maneno ambayo umeyasikia,+ 19 kwa sababu moyo+ wako ulikuwa mwororo hivi kwamba ukajinyenyekeza+ kwa sababu ya Yehova uliposikia yale ambayo nimesema juu ya mahali hapa na wakaaji wake ili pawe kitu cha kushangaza na laana,+ nawe ukayararua+ mavazi yako, ukaanza kulia mbele zangu, mimi, naam, mimi nimesikia,” asema Yehova.+ 20 “Ndiyo sababu tazama, nitakukusanya+ wewe kwa mababu zako, nawe hakika utakusanywa kwenye uwanja wa kaburi lako kwa amani,+ na macho yako hayatauona msiba wote ninaouleta juu ya mahali hapa.”’” Nao wakamletea mfalme jibu lile.