Isaya
25 Ee Yehova, wewe ni Mungu wangu.+ Ninakutukuza,+ ninalisifu jina lako,+ kwa maana umetenda mambo ya ajabu,+ mashauri+ kutoka nyakati za kale, kwa uaminifu,+ kwa kutegemeka.+ 2 Kwa maana umefanya jiji kuwa fungu la mawe, mji wenye ngome kuwa bomoko linaloanguka, mnara wa makao ya wageni usiwe jiji, ambalo halitajengwa upya mpaka wakati usio na kipimo.+ 3 Ndiyo sababu wale ambao ni kikundi cha watu wenye nguvu watakutukuza wewe; mji wa mataifa yenye kuonea, watakuogopa.+ 4 Kwa maana umekuwa ngome kwa mtu wa hali ya chini, ngome kwa maskini katika taabu aliyo nayo,+ kimbilio kutokana na dhoruba ya mvua, kivuli+ kutokana na joto, wakati mlipuko wa wenye kuonea ni kama dhoruba ya mvua juu ya ukuta. 5 Kama joto katika nchi isiyo na maji, unazitiisha kelele za wageni, joto kwa kivuli cha wingu.+ Muziki wa watu wenye kuonea unanyamazishwa.+
6 Na Yehova wa majeshi hakika atavifanyia vikundi vyote vya watu,+ katika mlima huu,+ karamu ya vyakula vinono vilivyotiwa mafuta,+ karamu ya divai iliyowekwa kwenye machicha, ya vyakula vinono vilivyotiwa mafuta vilivyojazwa urojorojo,+ ya divai+ iliyowekwa kwenye machicha, iliyochujwa.+ 7 Na katika mlima huu hakika ataumeza uso wa kifuniko kinachovifunika vikundi vyote vya watu,+ na mfumo uliofumwa kwa kusokotana juu ya mataifa yote. 8 Yeye kwa kweli atameza kifo milele,+ na Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova hakika atafuta machozi katika nyuso zote.+ Na shutuma ya watu wake ataiondoa katika dunia yote,+ kwa maana Yehova mwenyewe amesema hayo.
9 Na katika siku hiyo hakika mtu atasema: “Tazama! Huyu ndiye Mungu wetu.+ Tumemtumaini yeye,+ naye atatuokoa.+ Huyu ndiye Yehova.+ Tumemtumaini yeye. Na tuwe na shangwe na kushangilia katika wokovu wake.”+
10 Kwa maana mkono wa Yehova utatua juu ya mlima huu,+ na Moabu atakanyagwa chini+ katika mahali pake kama fungu la majani linavyokanyagwa chini katika mahali penye mbolea.+ 11 Naye atapiga mikono yake katikati yake kama mwogeleaji anavyoifanya mikono yake, naye atashusha majivuno+ yake kwa mwendo wa udanganyifu wa mikono yake. 12 Na lile jiji lenye ngome, pamoja na kuta zako ndefu za usalama, atalilaza chini; atalishusha, ataliangusha chini kwenye dunia, kwenye mavumbi.+