Amosi
5 “Lisikieni neno hili ninalosema juu yenu kama wimbo wa huzuni,+ Ee nyumba ya Israeli:
2 “Israeli, bikira,+ ameanguka;+
Hawezi kusimama tena.+
Ameachwa juu ya nchi yake mwenyewe;
Hakuna anayemsimamisha.+
3 “Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Jiji lililokuwa likitoka nje likiwa na elfu moja litaachwa na mia; na lile lililokuwa likitoka nje likiwa na mia moja litaachwa na kumi, kwa nyumba ya Israeli.’+
4 “Kwa maana Yehova ameiambia hivi nyumba ya Israeli, ‘Nitafuteni mimi,+ mwendelee kuishi.+ 5 Wala msitafute Betheli,+ wala msiende Gilgali,+ wala msivuke Beer-sheba;+ kwa sababu Gilgali litakwenda uhamishoni;+ Betheli nalo litakuwa kitu cha uchawi.+ 6 Mtafuteni Yehova, Ee nyumba ya Yosefu,+ mwendelee kuishi,+ ili asitende kama vile moto,+ nao usije ukateketeza, na Betheli lisikose mtu wa kuuzima,+ 7 enyi mnaoigeuza haki kuwa pakanga tupu,+ ninyi ambao mmeutupa chini uadilifu.+ 8 Mtengenezaji wa kundi-nyota la Kima+ na kundi-nyota+ la Kesili,+ na Yeye ambaye anageuza kivuli kizito+ kiwe asubuhi, na Yeye ambaye amefanya mchana uwe na giza kama usiku,+ Yeye ambaye anaita maji ya bahari, ili ayamwage kwenye uso wa dunia+—Yehova ndilo jina lake;+ 9 yeye ambaye anasababisha uporaji uje ghafula juu ya mtu mwenye nguvu, ili uporaji uje hata juu ya mahali penye ngome.
10 “ ‘Katika lango wao wamemchukia mwenye kukaripia,+ nao humchukia msemaji wa mambo makamilifu.+ 11 Basi, kwa sababu mnamtoza mtu wa hali ya chini kodi ya shamba,+ nanyi mnaendelea kuchukua kutoka kwake ushuru wa nafaka; mmejenga nyumba za mawe yaliyochongwa,+ lakini hamtaendelea kukaa ndani yake; nanyi mmepanda mashamba ya mizabibu yenye kupendeza, lakini hamtaendelea kunywa divai yake.+ 12 Kwa maana nimejua hesabu za maasi+ yenu na jinsi dhambi zenu zilivyo kubwa,+ enyi mnaomwonyesha mtu mwadilifu uadui,+ ninyi mnaochukua pesa za hongo,+ na ambao mmewafukuza watu maskini+ langoni.+ 13 Basi yeye aliye na ufahamu atakaa kimya wakati huo, kwa maana utakuwa wakati wenye taabu.+
14 “ ‘Tafuteni yaliyo mema, wala si yaliyo mabaya,+ kusudi mwendelee kuishi;+ ndipo Yehova Mungu wa majeshi apate kuwa pamoja nanyi, kama vile ambavyo mmesema.+ 15 Chukieni yaliyo mabaya, pendeni yaliyo mema,+ na mwipatie haki nafasi langoni.+ Huenda ikawa Yehova Mungu wa majeshi atawapa kibali+ mabaki ya Yosefu.’+
16 “Basi Yehova aliye Yehova Mungu wa majeshi amesema hivi, ‘Kutakuwako maombolezo katika viwanja vyote vya watu wote,+ na katika barabara zote watu watakuwa wakisema: “Ah! Ah!” Nao watamwita mkulima aje kuomboleza,+ na kuwaita wale wenye uzoefu wa maombolezo waje kulia.’+ 17 ‘Na kutakuwako maombolezo katika mashamba yote ya mizabibu;+ kwa maana nitapita katikati yako,’+ Yehova amesema.
18 “ ‘Ole wao wanaoitamani siku ya Yehova!+ Basi, siku ya Yehova itamaanisha nini kwenu?+ Itakuwa giza, wala si nuru,+ 19 kama vile tu mtu anavyomkimbia simba, kisha dubu anakutana naye; na kama vile alivyoingia ndani ya nyumba akauegemeza mkono wake ukutani, naye nyoka akamuuma.+ 20 Je, siku ya Yehova haitakuwa giza, wala si nuru; na je, haitakuwa na weusi, wala si mwangaza?+ 21 Nimechukia, nimezikataa sherehe zenu,+ wala sitafurahia harufu ya makusanyiko yenu makuu.+ 22 Lakini ninyi mkinitolea matoleo mazima ya kuteketezwa,+ hata katika matoleo yenu ya zawadi sitapata furaha,+ wala sitatazama dhabihu zenu za ushirika za vinono.+ 23 Ondoeni kutoka kwangu mchafuko wa nyimbo zenu; wala sauti tamu ya vinanda vyenu sitaki kusikia.+ 24 Na haki itiririke kama maji,+ na uadilifu kama mto unaotiririka daima.+ 25 Je, mlinisogezea karibu dhabihu na matoleo ya zawadi nyikani miaka 40, Ee nyumba ya Israeli?+ 26 Nanyi mtamchukua Sakuthi mfalme wenu+ na Kaiwani, sanamu zenu, nyota ya mungu wenu, ambaye mlijifanyia ninyi wenyewe.+ 27 Nami nitawafanya mwende uhamishoni ng’ambo ya Damasko,’+ yeye ambaye jina lake ni Yehova Mungu wa majeshi, amesema.”+