Luka
13 Katika majira hayo kulikuwa na watu fulani waliomletea habari juu ya Wagalilaya+ ambao Pilato alikuwa amechanganya damu yao pamoja na dhabihu zao. 2 Kwa hiyo akajibu, akawaambia: “Je, mnafikiri kwamba Wagalilaya hao walikuwa watenda-dhambi+ wabaya zaidi kuliko Wagalilaya wengine wote kwa sababu wamepatwa na mambo hayo? 3 Ninawaambia ninyi, kwa kweli, hapana; lakini, msipotubu, nyote mtaangamizwa vivyo hivyo.+ 4 Au wale kumi na wanane ambao mnara katika Siloamu uliwaangukia, na kuwaua, je, mnafikiri kwamba walikuwa na deni kubwa zaidi kuliko watu wengine wote waliokuwa wakikaa Yerusalemu? 5 Ninawaambia ninyi, kwa kweli, hapana; lakini, msipotubu, ninyi nyote mtaangamizwa vivyo hivyo.”+
6 Ndipo akaendelea kutoa mfano huu: “Mtu fulani alikuwa na mtini umepandwa katika shamba lake la mizabibu,+ naye akaja akitafuta matunda juu yake,+ lakini hakupata yoyote.+ 7 Ndipo akamwambia mtunza-mizabibu, ‘Kwa miaka mitatu+ sasa nimekuwa nikija kutafuta matunda juu ya mtini huu, lakini sijapata yoyote. Ukate!+ Kwa nini huo uufanye udongo ukae bure?’ 8 Akajibu akamwambia, ‘Bwana, uache+ mwaka huu pia, mpaka niupalilie na kuweka mbolea; 9 na ndipo ukizaa matunda wakati ujao, basi ni vema; lakini ikiwa sivyo, utaukata.’ ”+
10 Basi alikuwa akifundisha katika moja la masinagogi siku ya sabato. 11 Na, tazama! mwanamke mwenye roho+ ya udhaifu kwa miaka kumi na minane, naye alikuwa amepindika vibaya na alikuwa hawezi kusimama wima kamwe. 12 Alipomwona mwanamke huyo, Yesu alisema naye na kumwambia: “Mwanamke, umefunguliwa+ kutoka udhaifu wako.” 13 Naye akaweka mikono yake juu ya mwanamke huyo; naye akanyooka+ mara moja, akaanza kumtukuza Mungu. 14 Lakini ofisa-msimamizi wa sinagogi, akiwa ameghadhibika kwa sababu Yesu alimponya siku ya sabato, akajibu na kuanza kuuambia umati: “Kuna siku sita ambapo kazi inapaswa kufanywa;+ kwa hiyo, njooni mponywe katika siku hizo, wala si siku ya sabato.”+ 15 Hata hivyo, Bwana akamjibu na kusema: “Wanafiki,+ je, kila mmoja wenu siku ya sabato hafungui ng’ombe wake au punda wake kutoka kwenye kibanda na kumpeleka akamnyweshe?+ 16 Basi, je, haikuwa haki mwanamke huyu aliye binti ya Abrahamu,+ na ambaye Shetani alikuwa amemfunga, tazama! miaka kumi na minane, afunguliwe kutoka kwenye kifungo hiki siku ya sabato?” 17 Basi, aliposema mambo hayo, wote waliokuwa wakimpinga wakaanza kuona aibu;+ lakini umati wote wakaanza kuyashangilia mambo matukufu yote aliyofanya.+
18 Kwa hiyo akaendelea kusema: “Ufalme wa Mungu ni kama nini, nami nitaulinganisha na nini?+ 19 Ni kama mbegu ya haradali ambayo mtu alichukua akaiweka katika bustani yake, nayo ikakua ikawa mti, nao ndege wa mbinguni+ wakapata makao katika matawi yake.”+
20 Naye tena akasema: “Nitaulinganisha ufalme wa Mungu na nini? 21 Ni kama chachu, ambayo mwanamke alichukua na kuitia katika vipimo vikubwa vitatu vya unga mpaka tonge lote lilipochacha.”+
22 Naye akasafiri kutoka jiji mpaka jiji na kutoka kijiji mpaka kijiji, akifundisha na kuendelea katika safari yake mpaka Yerusalemu.+ 23 Sasa mtu fulani akamwambia: “Bwana, je, wale wanaookolewa ni wachache?”+ Akawaambia: 24 “Jitahidini+ sana ili mwingie kupitia mlango mwembamba,+ kwa sababu wengi, ninawaambia ninyi, watajaribu kuingia lakini hawataweza,+ 25 wakati mwenye nyumba anapomaliza kusimama na kuufunga mlango, nanyi mnaanza kusimama nje na kupiga hodi mlangoni, mkisema, ‘Bwana, tufungulie.’+ Lakini atawajibu na kuwaambia ninyi, ‘Sijui mnatoka wapi.’+ 26 Ndipo mtakapoanza kusema, ‘Tulikula na kunywa mbele yako, na wewe ulifundisha katika njia zetu pana.’+ 27 Lakini atasema na kuwaambia ninyi, ‘Sijui mnatoka wapi. Ondokeni kwangu, ninyi nyote mnaotenda ukosefu wa uadilifu!’+ 28 Hapo ndipo mtalia na kusaga meno yenu,+ wakati mtakapomwona Abrahamu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu,+ lakini ninyi wenyewe mkiwa mmetupwa nje. 29 Zaidi ya hayo, watu watakuja kutoka sehemu za mashariki na za magharibi, na kutoka kaskazini na kusini,+ nao wataketi mezani katika ufalme wa Mungu.+ 30 Na, tazama! kuna wale wa mwisho watakaokuwa wa kwanza, na kuna wale wa kwanza watakaokuwa wa mwisho.”+
31 Saa ileile Mafarisayo fulani wakaja, wakimwambia: “Toka hapa uende zako, kwa sababu Herode anataka kukuua.” 32 Naye akawaambia: “Nendeni mkamwambie mbweha+ huyo, ‘Tazama! Mimi ninatoa roho waovu na kuponya leo na kesho, na siku ya tatu nitakuwa nimemaliza.’+ 33 Hata hivyo, lazima niende zangu leo na kesho na siku inayofuata, kwa sababu haikubaliki nabii kuangamizwa nje ya Yerusalemu.+ 34 Yerusalemu, Yerusalemu, muuaji+ wa manabii na anayewapiga kwa mawe+ hao waliotumwa kwake—ni mara ngapi nilitaka kuwakusanya watoto wako pamoja kama vile ambavyo kuku hukusanya vifaranga chini ya mabawa yake,+ lakini ninyi hamkutaka!+ 35 Tazama! Nyumba+ yenu mmeachiwa hali ya ukiwa. Ninawaambia, Ninyi hamtaniona kamwe mpaka mtakaposema, ‘Aliyebarikiwa ni yule anayekuja katika jina la Yehova!’ ”+