Ufunuo
3 “Na kwa malaika+ wa kutaniko katika Sardi andika: Haya ndiyo mambo anayosema yeye aliye na zile roho saba+ za Mungu na zile nyota saba,+ ‘Mimi nayajua matendo yako, kwamba una jina kuwa uko hai, lakini umekufa.+ 2 Uwe mwenye kulinda,+ na uyatie nguvu+ mambo yanayobaki yaliyokuwa tayari kufa, kwa maana mimi sikuona matendo yako kuwa yamefanywa kwa ukamili mbele za Mungu wangu.+ 3 Kwa hiyo, endelea kukazia akilini jinsi ulivyopokea+ na jinsi ulivyosikia, nawe uendelee kulishika,+ na utubu.+ Hakika usipoamka,+ nitakuja kama mwizi,+ nawe hutajua hata kidogo saa nitakayokuja juu yako.+
4 “ ‘Hata hivyo, una majina+ machache katika Sardi ambayo hayakutia unajisi+ mavazi yao ya nje, nao watatembea pamoja nami wakiwa na mavazi meupe,+ kwa sababu wanastahili.+ 5 Yeye atakayeshinda+ atapambwa hivyo mavazi meupe ya nje;+ nami sitalifuta kwa vyovyote jina lake kutoka katika kitabu cha uzima,+ bali nitalikiri jina lake mbele za Baba+ yangu na mbele ya malaika+ zake. 6 Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo roho+ inayaambia makutaniko.’
7 “Na kwa malaika+ wa kutaniko katika Filadelfia andika: Haya ndiyo mambo anayosema yeye aliye mtakatifu,+ aliye wa kweli,+ aliye na ufunguo wa Daudi,+ ambaye hufungua hivi kwamba hakuna yeyote atakayefunga, na ambaye hufunga hivi kwamba hakuna yeyote anayefungua, 8 ‘Mimi nayajua matendo yako+—tazama! nimeweka mbele yako mlango uliofunguliwa,+ ambao hakuna yeyote anayeweza kuufunga—kwamba una nguvu kidogo, nawe ulilishika neno langu na hukulikana jina langu.+ 9 Tazama! Nitawatoa wale wa sinagogi la Shetani wanaosema ni Wayahudi,+ lakini sivyo walivyo bali wanasema uwongo+—tazama! nitawafanya waje na kusujudu+ mbele ya miguu yako na kuwafanya wajue kwamba nimekupenda wewe. 10 Kwa sababu ulilishika neno juu ya uvumilivu+ wangu, mimi pia nitakulinda+ kutokana na ile saa ya jaribu itakayokuja juu ya dunia nzima inayokaliwa, ili kuwatia katika jaribu wale wanaokaa duniani.+ 11 Mimi ninakuja upesi.+ Endelea kushika sana kile ulicho nacho,+ ili yeyote asilichukue taji+ lako.
12 “ ‘Yeye atakayeshinda—nitamfanya kuwa nguzo+ katika hekalu+ la Mungu wangu,+ naye hataondoka ndani yake tena kwa vyovyote, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu na jina la jiji la Mungu wangu, Yerusalemu+ jipya linaloshuka kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na lile jina langu jipya.+ 13 Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo roho+ inayaambia makutaniko.’
14 “Na kwa malaika wa kutaniko katika Laodikia+ andika: Haya ndiyo mambo anayosema Amina,+ shahidi+ mwaminifu+ na wa kweli,+ mwanzo wa uumbaji wa Mungu,+ 15 ‘Mimi nayajua matendo yako, kwamba wewe si baridi wala si moto. Laiti ungalikuwa baridi au moto. 16 Kwa hiyo, kwa sababu wewe ni vuguvugu na si moto+ wala si baridi,+ nitakutapika kutoka kinywani mwangu. 17 Kwa sababu unasema: “Mimi ni tajiri,+ nimejipatia utajiri na sihitaji kitu chochote hata kidogo,” lakini hujui kwamba wewe ni mwenye taabu na wa kusikitikiwa na maskini na kipofu+ na uchi, 18 ninakushauri ununue kutoka kwangu dhahabu+ iliyosafishwa kwa moto ili uwe tajiri, na mavazi meupe ya nje ili uvikwe na kwamba aibu ya uchi wako isifunuliwe,+ na dawa ya macho ya kupaka katika macho+ yako ili upate kuona.
19 “ ‘Wale wote ninaowapenda, mimi huwakaripia na kuwatia nidhamu.+ Kwa hiyo uwe mwenye bidii na utubu.+ 20 Tazama! Nimesimama mlangoni+ na kupiga hodi. Mtu yeyote akiisikia sauti yangu na kuufungua mlango,+ nitaingia ndani ya nyumba yake na kula mlo wa jioni pamoja naye, yeye naye pamoja nami. 21 Yeye atakayeshinda+ nitampa ruhusa ya kuketi pamoja nami katika kiti changu cha ufalme,+ kama vile nilivyoshinda na kuketi+ pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha ufalme.+ 22 Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo roho+ inayaambia makutaniko.’ ”+