Methali
28 Mwovu hukimbia wakati hakuna anayemfuatilia,+ lakini waadilifu ni kama mwana-simba mwenye uhakika.+
2 Kwa sababu ya makosa ya nchi wakuu wake hufuatana kwa wingi,+ lakini kwa sababu ya mtu mwenye utambuzi aliye na ujuzi wa lililo sawa, mkuu atakaa muda mrefu.+
3 Mwanamume maskini na ambaye anawapunja+ watu wa hali ya chini ni kama mvua ambayo hufagilia mbali na kusababisha ukosefu wa chakula.
4 Wale wanaoiacha sheria humsifu mwovu,+ lakini wale wanaoishika sheria hushindana nao.+
5 Watu wenye mwelekeo wa ubaya hawawezi kuelewa hukumu, lakini wale wanaomtafuta Yehova wanaweza kuelewa kila jambo.+
6 Afadhali maskini anayetembea katika utimilifu wake kuliko mtu yeyote aliyepotoka katika njia zake, ingawa ni tajiri.+
7 Mwana mwenye uelewaji anashika sheria,+ lakini anayeshirikiana na walafi humletea baba yake aibu.+
8 Anayezidisha vitu vyake vyenye thamani kwa faida+ na riba humkusanyia tu mtu anayeonyesha kibali kwa watu wa hali ya chini.+
9 Anayegeuzia mbali sikio lake asiisikie sheria+—hata sala yake ni chukizo.+
10 Anayewapoteza wanyoofu+ waingie katika njia mbaya ataanguka katika shimo lake mwenyewe,+ lakini wasio na kosa watapata mema.+
11 Mtu tajiri ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe,+ lakini mtu wa hali ya chini mwenye utambuzi humchunguza kabisa.+
12 Waadilifu wanaposhangilia,+ kuna uzuri mwingi; lakini waovu wanaposimama, mtu hujifanya asitambulike.+
13 Anayefunika makosa yake hatafanikiwa,+ lakini yeye anayeyaungama na kuyaacha ataonyeshwa rehema.+
14 Mwenye furaha ni mtu anayehofu sikuzote,+ lakini yeye anayeufanya moyo wake kuwa mgumu ataanguka katika msiba.+
15 Kama simba anayenguruma na dubu anayekimbia ili kushambulia ndivyo alivyo mtu mwovu anayetawala watu wa hali ya chini.+
16 Kiongozi anayepungukiwa na utambuzi wa kweli pia ana mazoea mengi ya upunjaji,+ lakini mtu anayechukia faida isiyo ya haki+ atarefusha siku zake.
17 Mtu aliyelemewa na hatia ya damu ya nafsi atalikimbilia shimo.+ Watu wasimzuie.
18 Anayetembea pasipo kosa ataokolewa,+ lakini yule ambaye amepotoka katika njia zake ataanguka mara moja.+
19 Anayelima udongo wake mwenyewe atakuwa na mkate wa kutosha,+ naye anayefuatilia vitu visivyo na thamani atakuwa na umaskini wa kutosha.+
20 Mtu mwenye matendo ya uaminifu atapata baraka nyingi,+ lakini yeye anayefanya haraka kupata utajiri hatabaki pasipo hatia.+
21 Si vema kuonyesha upendeleo,+ wala si vema kwa mwanamume kufanya kosa kwa sababu ya kipande tu cha mkate.
22 Mtu mwenye jicho la wivu hukimbilia vitu vyenye thamani,+ lakini hajui kwamba atakuwa na uhitaji.
23 Anayemkaripia mtu+ atapata kibali zaidi baadaye kuliko yeye anayebembeleza kwa ulimi wake.
24 Anayemnyang’anya baba yake na mama yake+ na kusema: “Si kosa,”+ ni rafiki ya mtu anayesababisha uharibifu.
25 Mwenye kiburi katika nafsi huchochea ugomvi,+ lakini yeye anayemtegemea Yehova atafanywa anenepe.+
26 Anayetegemea moyo wake mwenyewe ni mjinga,+ lakini yeye anayetembea katika hekima ndiye atakayeponyoka.+
27 Anayempa kitu maskini hatakuwa na uhitaji,+ lakini yeye anayeficha macho yake atapata laana nyingi.+
28 Waovu wanaposimama, mtu hujificha;+ lakini wanapoangamia, waadilifu huongezeka.+