Marko
13 Alipokuwa akitoka hekaluni mmoja wa wanafunzi wake akamwambia: “Mwalimu, ona! jinsi yalivyo mawe haya na majengo haya!”+ 2 Hata hivyo, Yesu akamwambia: “Unayaona majengo haya makubwa?+ Hakuna jiwe litakaloachwa hapa juu ya jiwe+ nalo lisiangushwe chini.”+
3 Na alipokuwa ameketi juu ya Mlima wa Mizeituni, hekalu likiwa linaonekana, Petro+ na Yakobo na Yohana na Andrea wakaanza kumuuliza faraghani:+ 4 “Tuambie, mambo haya yatakuwa wakati gani, na ni nini itakayokuwa ishara ya wakati ambapo mambo yote haya yanakusudiwa kufikia mwisho?”+ 5 Kwa hiyo Yesu akaanza kuwaambia: “Jihadharini mtu yeyote asiwapotoshe.+ 6 Wengi watakuja kwa msingi wa jina langu, wakisema, ‘Mimi ndiye,’ nao watawapotosha wengi.+ 7 Zaidi ya hayo, mnaposikia juu ya vita na habari za vita, msiogope; mambo hayo lazima yatukie, lakini ule mwisho bado.+
8 “Kwa maana taifa litasimama kupigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme,+ kutakuwa na matetemeko ya nchi+ mahali pamoja baada ya pengine, kutakuwa na upungufu wa chakula.+ Hayo ni mwanzo wa maumivu ya taabu.+
9 “Kwa habari yenu, jihadharini; watu watawapeleka mahakamani,+ nanyi mtapigwa katika masinagogi+ na kusimamishwa mbele ya magavana na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushahidi kwao.+ 10 Pia, katika mataifa yote lazima habari njema+ ihubiriwe kwanza.+ 11 Lakini wanapowapeleka, msihangaike kimbele juu ya jambo mtakalosema;+ bali jambo lolote mtakalopewa saa hiyo, semeni hilo, kwa maana si ninyi mnaosema, bali ni roho takatifu.+ 12 Zaidi ya hayo, ndugu atamtoa ndugu yake auawe, na baba atamtoa mtoto,+ na watoto watainuka juu ya wazazi na kufanya wauawe;+ 13 nanyi mtachukiwa na watu wote kwa sababu ya jina langu.+ Lakini yule ambaye atavumilia mpaka mwisho+ ndiye atakayeokolewa.+
14 “Hata hivyo, mtakapoona lile chukizo+ linalosababisha ukiwa likiwa+ limesimama mahali ambapo halipaswi (msomaji na atumie utambuzi),+ ndipo wale walio katika Yudea waanze kukimbilia milimani.+ 15 Mtu aliye juu ya paa ya nyumba asishuke, wala asiingie ndani kuchukua kitu chochote kutoka nyumbani mwake;+ 16 na mtu aliye shambani asirudi kwenye vitu vilivyo nyuma kuchukua vazi lake la nje.+ 17 Ole wao wanawake wenye mimba na wale wanaonyonyesha mtoto mchanga katika siku hizo!+ 18 Endeleeni kusali kwamba yasitukie wakati wa majira ya baridi kali;+ 19 kwa maana siku hizo zitakuwa siku za dhiki+ ya namna ambayo haijatukia tangu mwanzo wa uumbaji ambao Mungu aliumba mpaka wakati huo, na haitatukia tena.+ 20 Kwa kweli, kama Yehova+ hangezifupisha siku hizo, hakuna chochote chenye mwili ambacho kingeokolewa. Lakini amezifupisha siku hizo+ kwa sababu ya waliochaguliwa+ ambao amewachagua.+
21 “Ndipo, pia, mtu yeyote akiwaambia, ‘Tazameni! Kristo huyu hapa,’ ‘Tazameni! ndiye yule pale,’+ msiamini.+ 22 Kwa maana Makristo wa uwongo na manabii wa uwongo watatokea+ na kutoa ishara na maajabu+ ili kupotosha, ikiwezekana, wale waliochaguliwa.+ 23 Basi, jihadharini;+ nimewaambia mambo yote kimbele.+
24 “Lakini katika siku hizo, baada ya dhiki hiyo, jua litatiwa giza, na mwezi hautatoa nuru yake, 25 nazo nyota zitakuwa zikianguka kutoka mbinguni na nguvu zilizo mbinguni zitatikiswa.+ 26 Ndipo watakapomwona Mwana wa binadamu+ akija katika mawingu akiwa na nguvu nyingi na utukufu.+ 27 Ndipo atakapowatuma malaika na kuwakusanya pamoja watu wake waliochaguliwa+ kutoka zile pepo nne, kutoka mwisho wa dunia mpaka mwisho wa mbingu.+
28 “Basi kutokana na mtini jifunzeni mfano huu: Mara tu tawi lake changa linapokuwa jororo na kutoa majani yake, mnajua kwamba kiangazi kiko karibu.+ 29 Vivyo hivyo ninyi pia, mnapoona mambo hayo yakitukia, jueni kwamba yuko karibu, milangoni.+ 30 Kwa kweli ninawaambia ninyi kwamba kizazi hiki hakitapitilia mbali kamwe mpaka mambo yote hayo yatukie.+ 31 Mbingu+ na dunia zitapitilia mbali, lakini maneno+ yangu hayatapitilia mbali.+
32 “Kuhusu siku ile au saa ile hakuna mtu anayejua, wala malaika mbinguni wala Mwana, ila Baba.+ 33 Endeleeni kutazama, Endeleeni kukesha,+ kwa maana hamjui wakati uliowekwa ni gani.+ 34 Ni kama mtu anayesafiri kwenda ng’ambo,+ ambaye aliacha nyumba yake na kuwapa mamlaka watumwa wake, kila mmoja kazi yake, na kumwamuru mtunza-mlango aendelee kukesha. 35 Kwa hiyo endeleeni kukesha,+ kwa maana hamjui bwana wa nyumba anakuja wakati gani, kama ni wakati wa jioni au katikati ya usiku au anapowika jogoo au asubuhi na mapema;+ 36 ili anapofika kwa ghafula, asiwakute mkiwa mmelala usingizi.+ 37 Lakini lile ninalowaambia ninyi ninawaambia wote, Endeleeni kukesha.”+