1 Wafalme
19 Kisha Ahabu+ akamwambia Yezebeli+ mambo yote ambayo Eliya alikuwa amefanya na mambo yote kuhusu namna alivyowaua manabii wote kwa upanga.+ 2 Ndipo Yezebeli akatuma mjumbe kwa Eliya, akisema: “Miungu na ifanye hivyo,+ nayo izidishe jambo hilo,+ ikiwa wakati kama huu hapo kesho sitaifanya nafsi yako iwe kama nafsi ya kila mmoja wao!” 3 Naye akaogopa. Basi akaondoka, akaanza kwenda kwa ajili ya nafsi yake,+ akafika Beer-sheba,+ jiji la Yuda.+ Kisha akamwacha mtumishi wake huko. 4 Naye mwenyewe akaingia nyikani safari ya siku moja, mwishowe akafika na kuketi chini ya mretemu fulani.+ Naye akaanza kuomba kwamba nafsi yake ife na kusema: “Inatosha! Sasa, Ee Yehova, iondoe nafsi yangu,+ kwa maana mimi si bora kuliko mababu zangu.”
5 Mwishowe akalala chini, akashikwa na usingizi chini ya ule mretemu.+ Lakini, tazama! Malaika+ akamgusa.+ Ndipo akamwambia: “Amka, ule.” 6 Alipoangalia, na tazama, pale karibu na kichwa chake palikuwa na keki ya mviringo+ juu ya mawe yenye moto na gudulia la maji. Naye akaanza kula na kunywa, kisha akalala chini tena. 7 Baadaye yule malaika+ wa Yehova akarudi mara ya pili, akamgusa na kusema: “Amka, ule, kwa maana safari ni ndefu mno kwako.”+ 8 Basi akaamka, akala na kunywa, naye akazidi kwenda katika nguvu za chakula kile kwa siku 40,+ mchana na usiku, mpaka Horebu, mlima wa Mungu wa kweli.+
9 Mwishowe hapo akaingia pangoni,+ ili alale humo usiku; na tazama! palikuwa na neno la Yehova kwa ajili yake, nalo likamwambia: “Una kazi gani hapa, Eliya?”+ 10 Naye akasema: “Nimekuwa na wivu+ kwelikweli kwa ajili ya Yehova Mungu wa majeshi; kwa maana wana wa Israeli wameliacha agano lako,+ wamezibomoa+ madhabahu zako, nao wamewaua manabii wako kwa upanga,+ hivi kwamba ni mimi peke yangu nimebaki;+ nao wanaanza kuitafuta nafsi yangu ili kuiondoa.”+ 11 Lakini likasema: “Toka, usimame juu ya mlima mbele za Yehova.”+ Na tazama! Yehova alikuwa anapita karibu,+ na upepo mkubwa na wenye nguvu ukawa unapasua milima na kuvunja miamba mbele za Yehova.+ (Yehova hakuwa katika upepo ule.) Na baada ya upepo ule kukawa na tetemeko.+ (Yehova hakuwa katika lile tetemeko.) 12 Na baada ya lile tetemeko kukawa na moto.+ (Yehova hakuwa katika moto ule.) Na baada ya moto ule kukawa na sauti tulivu, ya chini.+ 13 Na ikawa kwamba mara tu Eliya alipoisikia, akafunika uso wake mara moja katika vazi lake rasmi,+ akatoka nje, akasimama mlangoni pa lile pango; na tazama! palikuwa na sauti kwa ajili yake, nayo ikamwambia: “Una kazi gani hapa, Eliya?”+ 14 Naye akasema: “Nimekuwa na wivu kwelikweli kwa ajili ya Yehova Mungu wa majeshi; kwa maana wana wa Israeli wameliacha agano lako,+ wamezibomoa madhabahu zako, nao wamewaua manabii wako kwa upanga, hivi kwamba ni mimi peke yangu nimebaki; nao wanaanza kuitafuta nafsi yangu ili kuiondoa.”+
15 Sasa Yehova akamwambia: “Nenda, rudi katika nyika ya Damasko;+ nawe uingie na kumtia mafuta+ Hazaeli+ kuwa mfalme juu ya Siria. 16 Na Yehu+ mjukuu wa Nimshi+ umtie mafuta kuwa mfalme juu ya Israeli; na Elisha+ mwana wa Shafati kutoka Abel-mehola+ umtie mafuta kuwa nabii mahali pako.+ 17 Na itatukia kwamba yule atakayepona upanga+ wa Hazaeli, Yehu atamuua;+ na yule atakayepona upanga wa Yehu, Elisha atamuua.+ 18 Nami nimewaacha watu elfu saba wabaki katika Israeli,+ magoti yote ambayo hayakumwinamia Baali,+ na kila kinywa ambacho hakikumbusu.”+
19 Basi akaondoka hapo, akamkuta Elisha mwana wa Shafati akilima+ na jozi kumi na mbili za wanyama mbele yake, naye akiwa na ile ya kumi na mbili. Basi Eliya akavuka mpaka pale alipokuwa, akalitupa vazi lake rasmi+ juu yake. 20 Ndipo akawaacha wale ng’ombe, akakimbia kumfuata Eliya na kusema: “Tafadhali, acha nimbusu baba yangu na mama yangu.+ Kisha nitakufuata.” Naye akamwambia: “Nenda, rudi; kwa maana mimi nimekufanyia nini?” 21 Kwa hiyo akarudi, akaacha kumfuata na kisha akachukua jozi moja ya wale ng’ombe na kuwatoa dhabihu,+ na kwa kutumia vifaa+ vya wale ng’ombe, akatokosa nyama yao, akawapa watu, nao wakaanza kula. Kisha akaondoka, akaanza kumfuata Eliya, naye akaanza kumhudumia.+