WIMBO WA SULEMANI
1 Wimbo wa nyimbo,* ambao ni wa Sulemani:+
3 Manukato ya mafuta yako mbalimbali yanapendeza.+
Jina lako ni kama mafuta yaliyomiminwa yenye manukato.+
Ndiyo sababu wasichana wanakupenda.
Mfalme amenileta katika vyumba vyake vya ndani!
Na tufurahi na kukushangilia.
Na tusifu* maonyesho yako ya mapenzi kuliko divai.
Wana* haki ya kukupenda.
5 Mimi ni mweusi, lakini napendeza, enyi mabinti wa Yerusalemu,
Kama mahema ya Kedari,+ kama vitambaa vya mahema+ ya Sulemani.
6 Msinikodolee macho kwa sababu mimi ni mweusi,
Kwa sababu jua limenichoma.
Wana wa mama yangu walinikasirikia;
Walinifanya kuwa mlinzi wa mashamba ya mizabibu,
Lakini sikulinda shamba langu mwenyewe la mizabibu.
7 Niambie, wewe ninayekupenda* sana,
Mahali unapochunga mifugo yako,+
Mahali unapoipumzisha wakati wa adhuhuri.
Kwa nini niwe kama mwanamke aliyefunikwa shela*
Kati ya makundi ya wenzako?”
8 “Ikiwa hujui, ewe mwanamke mrembo kuliko wote,
Nenda ufuate nyayo za mifugo
Na uchunge wanambuzi wako karibu na mahema ya wachungaji.”
9 “Ewe mpenzi wangu, nakufananisha na farasi jike* kati ya magari ya Farao.+
13 Mpenzi wangu ni kama mfuko wa manemane unaonukia manukato+
Unaokaa usiku kucha katikati ya matiti yangu.
14 Mpenzi wangu kwangu mimi ni kama kishada cha maua ya hina+
Kati ya mashamba ya mizabibu ya En-gedi.”+
15 “Tazama! Wewe ni mrembo, mpenzi wangu.
Tazama! Wewe ni mrembo. Macho yako ni macho ya njiwa.”+
16 “Tazama! Wewe ni mrembo,* mpenzi wangu, na unapendeza.+
Kitanda chetu kiko kati ya majani mabichi.
2 “Kama yungiyungi katikati ya miiba
Ndivyo alivyo mpenzi wangu kati ya mabinti.”
3 “Kama mtofaa kati ya miti ya msituni,
Ndivyo alivyo mpenzi wangu miongoni mwa wana.
Natamani sana kukaa katika kivuli chake,
Na tunda lake ni tamu kinywani mwangu.
Msijaribu kuamsha au kuchochea upendo ndani yangu mpaka utakapoamka wenyewe.+
8 Sauti ya mpenzi wangu!
Tazama! Ndiye yule anakuja,
Akipanda milima, akirukaruka juu ya vilima.
9 Mpenzi wangu ni kama swala, kama paa dume mchanga.+
Yule pale, amesimama nyuma ya ukuta wetu,
Akichungulia madirishani,
Akitazama kupitia viunzi vya madirisha.
10 Mpenzi wangu anaongea, ananiambia:
‘Inuka, mpenzi wangu,
Mrembo wangu, njoo twende zetu.
11 Angalia, majira ya baridi* yamepita.
Mvua zimekwisha na kwenda zake.
Inuka, mpenzi wangu, njoo.
Mrembo wangu, njoo twende zetu.
14 Ewe njiwa wangu, kwenye mapango ya miamba,+
Kwenye mashimo ya mlimani,
Acha nikuone na kusikia sauti yako,+
Kwa maana sauti yako inavutia na umbo lako linapendeza.’”+
15 “Tukamatieni mbweha,
Mbweha wadogo wanaoharibu mashamba ya mizabibu,
Kwa maana mashamba yetu ya mizabibu yamechanua.”
16 “Mpenzi wangu ni wangu mimi, na mimi ni wake.+
Anachunga kondoo+ kati ya mayungiyungi.+
17 Mpaka upepo uanze kuvuma* na vivuli kukimbia,
Rudi haraka, ewe mpenzi wangu,
Kama swala+ au paa dume mchanga+ juu ya milima inayotutenganisha.*
Nilimtafuta mwanamume huyo lakini sikumpata.+
Nilimtafuta mwanamume huyo, lakini sikumpata.
3 Nilikutana na walinzi waliokuwa wakizunguka jijini.+
Nikawauliza, ‘Mmemwona ninayempenda?’*
Nikamshika na sikumwacha aende
Mpaka nilipomleta ndani ya nyumba ya mama yangu,+
Katika chumba cha ndani cha aliyenizaa.
5 Nawaapisha, enyi binti za Yerusalemu,
Kwa swala na paa jike wa porini:
Msijaribu kuamsha au kuchochea upendo ndani yangu mpaka utakapoamka wenyewe.”+
6 “Ni nini hiki kinachokuja kutoka nyikani kama nguzo za moshi,
Kilicho na manukato ya manemane na ubani,
Na manukato yote ya ungaunga yanayouzwa na wafanyabiashara?”+
7 “Tazameni! Ni kochi la Sulemani.
Wanaume sitini mashujaa wanalizunguka,
Miongoni mwa wanaume mashujaa wa Israeli,+
8 Wote wamejihami kwa upanga,
Wote wamezoezwa kwa ajili ya vita,
Kila mmoja wao ana upanga kiunoni
Ili akabiliane na mambo yanayotisha wakati wa usiku.”
10 Alitengeneza nguzo zake kwa fedha,
Viegemeo vyake kwa dhahabu.
Kiti chake kwa sufu ya zambarau;
Sehemu yake ya ndani ilipambwa kwa upendo
Na mabinti wa Yerusalemu.”
11 “Tokeni nje, enyi binti za Sayuni,
Mtazameni Mfalme Sulemani
Amevaa taji la harusi* ambalo mama yake+ alimtengenezea
Siku yake ya harusi,
Siku ambayo moyo wake ulishangilia.”
4 “Tazama! Wewe ni mrembo, mpenzi wangu.
Tazama! Wewe ni mrembo.
Macho yako ni macho ya njiwa nyuma ya shela yako.
Nywele zako ni kama kundi la mbuzi
Washukao chini kwenye milima ya Gileadi.+
2 Meno yako ni kama kundi la kondoo waliokatwa manyoya sasa hivi
Ambao wametoka kuoshwa,
Wote wamezaa mapacha,
Na hakuna yeyote aliyepoteza watoto wake.
3 Midomo yako ni kama uzi mwekundu,
Na maneno yako yanapendeza.
Kama kipande cha komamanga
Ndivyo yalivyo mashavu yako nyuma ya shela yako.
4 Shingo yako+ ni kama mnara wa Daudi,+
Uliojengwa kwa safu za mawe
Na ngao elfu zimetundikwa juu yake,
Ngao zote za mviringo za wanaume mashujaa.+
6 “Mpaka upepo uanze kuvuma* na vivuli kukimbia,
Nitakwenda zangu kwenye mlima wa manemane
Na kwenye kilima cha ubani.”+
Shuka kutoka kilele cha Amana,*
Kutoka kilele cha Seniri, kilele cha Hermoni,+
Kutoka kwenye mapango ya simba, kutoka kwenye milima ya chui.
9 Umeuteka moyo wangu,+ dada yangu, bibi harusi wangu,
Umeuteka moyo wangu kwa kunitupia jicho mara moja tu,
Kwa kidani kimoja cha mkufu wako.
10 Maonyesho yako ya upendo yanavutia kwelikweli,+ dada yangu, bibi harusi wangu!
Maonyesho yako ya upendo ni bora zaidi kuliko divai,+
Na manukato ya marashi yako yananukia kuliko kiungo chochote!+
11 Midomo yako, bibi harusi wangu, inadondosha asali ya sega.+
Chini ya ulimi wako kuna asali na maziwa,+
Na manukato ya mavazi yako ni kama manukato ya Lebanoni.
12 Dada yangu, bibi harusi wangu, ni kama bustani iliyofungwa,
Bustani iliyofungwa, chemchemi iliyofunikwa kabisa.
13 Machipukizi* yako ni paradiso* ya makomamanga
Yenye matunda bora kabisa, mimea ya hina na ya nardo,
14 Nardo+ na zafarani, kane*+ na mdalasini,+
Iliyo na miti ya kila aina ya ubani, manemane, na udi,+
Pamoja na marashi yote yaliyo bora kabisa.+
16 Amka, ewe upepo wa kaskazini;
Ingia, ewe upepo wa kusini.
Pumueni* kwenye bustani yangu.
Manukato yake na yaenee.”
“Mpenzi wangu na aje kwenye bustani yake
Ale matunda yake yaliyo bora kabisa.”
Nimekusanya manemane yangu na viungo* vyangu.+
Nimekula sega langu na asali yangu;
Nimekunywa divai yangu na maziwa yangu.”+
“Kuleni, rafiki zangu wapendwa!
Kunyweni, mlewe maonyesho ya upendo!”+
2 “Nimelala usingizi, lakini moyo wangu uko macho.+
Ndiyo hiyo sauti ya mpenzi wangu akipiga hodi!”
“Nifungulie, ewe dada yangu, mpenzi wangu,
Njiwa wangu, mpenzi wangu asiye na kasoro!
Kwa maana kichwa changu kimelowa umande,
Mashungi ya nywele zangu yamejaa unyevu wa usiku.”+
3 “‘Nimevua kanzu yangu.
Ni lazima niivae tena?
Nimeosha miguu yangu.
Ni lazima niichafue tena?’
4 Mpenzi wangu aliondoa mkono wake kwenye tundu la mlango,
Hisia zangu kumwelekea zikasisimka.
5 Niliinuka ili nimfungulie mpenzi wangu;
Mikono yangu ikadondosha manemane,
Na vidole vyangu manemane ya maji,
Ikadondoka kwenye vitasa vya mlango.
6 Nilimfungulia mpenzi wangu,
Lakini mpenzi wangu alikuwa ameondoka, alikuwa ameenda zake.
Nilitamauka* alipoenda.
Nilimtafuta, lakini sikumpata.+
Nikamwita, lakini hakuitika.
7 Nilikutana na walinzi waliokuwa wakizunguka jijini.
Wakanipiga na kunijeruhi.
Walinzi wa kuta wakanivua mtandio wangu.*
8 Nawaapisha, enyi binti za Yerusalemu:
Mkimpata mpenzi wangu,
Mwambieni naugua kwa mapenzi.”
9 “Mpenzi wako ni bora kuliko wapenzi wengine wote jinsi gani,
Ewe mwanamke mrembo kuliko wote?
Mpenzi wako ni bora kuliko mpenzi mwingine yeyote jinsi gani,
Hivi kwamba unatuapisha hivyo?”
10 “Mpenzi wangu anang’aa tena ni mwekundu;
Anavutia zaidi miongoni mwa wanaume elfu kumi.
11 Kichwa chake ni dhahabu, dhahabu bora zaidi.
Mashungi ya nywele zake ni kama majani ya mtende yanayotikisika.*
Nywele zake ni nyeusi kama kunguru.
12 Macho yake ni kama njiwa kando ya vijito vya maji,
Wanaooga ndani ya maziwa,
Wakiwa wameketi kando ya dimbwi lililojaa maji.
Midomo yake ni mayungiyungi, yanayodondosha manemane ya maji.+
14 Mikono yake ni fito za dhahabu, zilizopambwa kwa krisolito.
Tumbo lake ni pembe ya tembo iliyong’arishwa na kufunikwa kwa yakuti.
15 Miguu yake ni nguzo za marumaru zilizowekwa kwenye vikalio vya dhahabu bora zaidi.
Sura yake ni kama Lebanoni, kama mierezi isiyo na kifani.+
Huyu ndiye mpenzi wangu, huyu ndiye mpendwa wangu, enyi binti za Yerusalemu.”
6 “Mpenzi wako ameenda wapi,
Ewe mwanamke mrembo kuliko wote?
Mpenzi wako amegeuka na kufuata njia gani?
Acha tukamtafute pamoja nawe.”
2 “Mpenzi wangu ameshuka kwenda kwenye bustani yake,
Kwenye kitalu cha mimea ya viungo,
Kuchunga kondoo kwenye bustani
Na kuchuma mayungiyungi.+
Anachunga kondoo kati ya mayungiyungi.”+
4 “Wewe ni mrembo, kama Tirsa,*+ mpenzi wangu,+
Unapendeza kama Yerusalemu,+
Unavutia sana kama majeshi yaliyokusanyika kuzunguka bendera zao.+
Nywele zako ni kama kundi la mbuzi
Linaloshuka kwenye miteremko ya Gileadi.+
6 Meno yako ni kama kundi la kondoo
Ambao wametoka kuoshwa,
Wote wamezaa mapacha,
Na hakuna yeyote aliyepoteza watoto wake.
7 Kama kipande cha komamanga
Ndivyo yalivyo mashavu yako nyuma ya shela yako.
8 Hata kukiwa na malkia 60
Na masuria 80
Na wasichana wasiohesabika.+
9 Lakini kuna mmoja tu ambaye ni njiwa wangu,+ mpenzi wangu asiye na kasoro.
Binti pekee kwa mama yake.
Yeye ni kipenzi cha mama yake.*
Mabinti wanapomwona, humtangaza kuwa mwenye furaha;
Malkia na masuria humsifu.
10 ‘Ni mwanamke gani anayeng’aa* kama mapambazuko,
Mrembo kama mwezi mpevu,
Aliye mwangavu kama nuru ya jua,
Mwenye kuvutia sana kama majeshi yaliyokusanyika kuzunguka bendera zao?’”+
11 “Nilishuka kwenye bustani ya miti yenye kokwa+
Ili nione machipukizi bondeni,
Nione ikiwa mzabibu umechipua
Ikiwa mikomamanga imechanua.
13 “Rudi, rudi, ewe Mshulami!
Rudi, rudi,
Ili tukutazame!”
“Kwa nini mnamkodolea macho Mshulami?”+
“Yeye ni kama dansi ya kambi mbili!”*
7 “Miguu yako inapendeza kwelikweli katika viatu vyako,
Ewe binti unayeheshimika!
Umbo la mapaja yako ni kama mapambo,
Kazi ya mikono ya fundi.
2 Kitovu chako ni bakuli la mviringo.
Kisikose kamwe divai iliyotiwa vikolezo.
Tumbo lako ni rundo la ngano,
Lililozungukwa na mayungiyungi.
4 Shingo yako+ ni kama mnara wa pembe ya tembo.+
Pua yako ni kama mnara wa Lebanoni,
Unaoelekea Damasko.
Mfalme ameduwazwa* na nywele zako ndefu.
6 Wewe ni mrembo kwelikweli, nawe unapendeza sana,
Ewe msichana mpendwa, unazidi vyote vinavyopendeza!
8 Nilisema, ‘Nitapanda juu ya mtende
Nishike vitawi vyake vyenye tende.’
Matiti yako na yawe kama vishada vya mizabibu,
Na pumzi yako inanukia kama matofaa,
“Na ishuke taratibu kwa ajili ya mpenzi wangu,
Itiririke taratibu juu ya midomo ya mpenzi wangu.*
12 Tuamke mapema twende kwenye mashamba ya mizabibu
Tuone ikiwa mzabibu umechipuka,
Ikiwa maua yamechanua,+
Ikiwa mikomamanga imechanua.+
Huko nitakuonyesha upendo wangu.+
Mapya na pia ya zamani,
Ewe mpenzi wangu, nimekuhifadhia.
8 “Laiti ungekuwa kama ndugu yangu,
Aliyenyonya matiti ya mama yangu!
Ningekukuta nje, ningekubusu.+
Na hakuna mtu angenidharau.
Ningekupa divai iliyotiwa vikolezo unywe,
Maji matamu ya makomamanga.
4 “Nawaapisha, enyi binti za Yerusalemu:
Msijaribu kuamsha au kuchochea upendo ndani yangu mpaka utakapoamka wenyewe.”+
5 “Ni nani huyu anayekuja kutoka nyikani,
Akiwa amemwegemea mpenzi wake?”
“Chini ya mtofaa nilikuamsha.
Hapo ndipo mama yako alipopata uchungu wa kukuzaa.
Hapo ndipo mama yako alipokuzaa kwa uchungu.
6 Niweke kama muhuri juu ya moyo wako,
Kama muhuri juu ya mkono wako,
Kwa maana upendo una nguvu kama kifo,+
Na kama Kaburi,* ujitoaji kamili haukubali kushindwa.
Miale yake ni moto mkali, mwali wa Yah.*+
Kama mtu angejaribu kuuza mali yote nyumbani mwake kwa ajili ya upendo,
Mali hiyo ingedharauliwa* kabisa.”
Tutamfanyia nini dada yetu
Siku atakapoposwa?”
9 “Akiwa ukuta,
Tutajenga juu yake mnara wa fedha,
Lakini akiwa mlango,
Tutamziba kwa ubao mpana wa mwerezi.”
10 “Mimi ni ukuta,
Na matiti yangu ni kama minara.
Kwa hiyo machoni pake nimekuwa
Kama mtu anayepata amani.
11 Sulemani alikuwa na shamba la mizabibu+ kule Baal-hamoni.
Aliwakabidhi watunzaji shamba hilo la mizabibu.
Kila mmoja wao alikuwa akileta vipande elfu moja vya fedha kwa ajili ya matunda yake.
12 Nina shamba langu mwenyewe la mizabibu.
Hivyo vipande elfu moja vya fedha ni vyako, Ee Sulemani,
Na vipande mia mbili ni vya wale wanaotunza matunda ya shamba hilo.”
Acha niisikie.”+
Au paa dume mchanga
Juu ya milima yenye viungo.”*
Au “Wimbo ulio bora.”
Anayeongea ni msichana.
Tnn., “Nivute nikufuate.”
Au “tusimulie.”
Yaani, wale wasichana.
Au “ambaye nafsi yangu inakupenda.”
Tnn., “shela ya maombolezo.”
Au “farasi jike wangu.”
Au labda, “kati ya nywele zilizosukwa.”
Au “mapambo ya duara ya kichwani.”
Tnn., “Nardo.”
Au “una sura nzuri.”
Au “nyumba yetu kubwa.”
Tnn., “nyumba ya divai.”
Au “majira ya mvua.”
Tnn., “siku ianze kupumua.”
Au labda, “milima yenye nyufa.” Au “milima ya Betheri.”
Au “yule ambaye nafsi yangu inampenda.”
Au “yule ambaye nafsi yangu inampenda.”
Au “yule ambaye nafsi yangu inampenda?”
Au “yule ambaye nafsi yangu inampenda.”
Kochi lililofunikwa ambalo lilitumiwa kuwabeba watu mashuhuri.
Au “shada; koja la maua.”
Tnn., “siku ianze kupumua.”
Au “Milima iliyo ng’ambo ya milima ya Lebanoni.”
Au labda, “Ngozi.”
Au “bustani.”
Utete wenye harufu nzuri.
Au “Vumeni taratibu.”
Yaani, vikolezo.
Au “Nafsi yangu ilizimia.”
Au “shela yangu.”
Au labda, “vishada vya tende.”
Tnn., “Kaakaa lake.”
Au “Jiji Linalopendeza.”
Tnn., “ndiye aliye safi sana kwa yule aliyemzaa.”
Tnn., “anayetazama chini.”
Au “watu wangu walio tayari kusaidia.”
Au “dansi ya Mahanaimu.”
Tnn., “kichwa chako.”
Au “ametekwa.”
Tnn., “kaakaa lako.”
Tnn., “midomo ya wanaolala usingizi.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
“Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au labda, “Angedharauliwa.”
Au “vikolezo.”