Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • nwt Yeremia 1:1-52:34
  • Yeremia

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yeremia
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Yeremia

YEREMIA

1 Haya ndiyo maneno ya Yeremia* mwana wa Hilkia, mumoja wa makuhani katika Anatoti+ katika inchi ya Benyamini. 2 Neno la Yehova likakuja kwake katika siku za Yosia+ mwana wa Amoni,+ mufalme wa Yuda, katika mwaka wa kumi na tatu (13) wa utawala wake. 3 Likakuja pia katika siku za Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda, mupaka kumalizika kwa mwaka wa kumi na moja (11) wa Sedekia+ mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda, mupaka wakati Yerusalemu ilienda katika uhamisho katika mwezi wa tano (5).+

4 Neno la Yehova likakuja kwangu, na kusema:

 5 “Mbele nikuumbe katika tumbo la uzazi nilikujua,*+

Na mbele uzaliwe* nilikutakasa.*+

Nilikufanya kuwa nabii kwa mataifa.”

 6 Lakini nikasema: “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova!

Mimi sijue namna ya kusema,+ kwa maana niko kijana mudogo tu.”+

 7 Kisha Yehova akaniambia:

“Usiseme, ‘Niko kijana mudogo tu.’

Kwa maana unapaswa kuenda kwa wote wenye ninakutuma kwao,

Na unapaswa kusema kila jambo lenye ninakuamuru.+

 8 Usiogope kwa sababu ya namna wanaonekana,+

Kwa maana ‘mimi niko pamoja na wewe ili kukuokoa,’+ ni vile Yehova anasema.”

9 Kisha Yehova akanyoosha mukono wake na kugusa kinywa changu.+ Na Yehova akaniambia: “Nimetia maneno yangu katika kinywa chako.+ 10 Angalia, nimekupatia daraka leo hii ili ukuwe juu ya mataifa na juu ya falme, ili kungoa na kubomoa, ili kuharibu na kuangusha, ili kujenga na kupanda.”+

11 Neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: “Unaona nini, Yeremia?” Basi nikasema: “Ninaona tawi la muti wa lozi.”*

12 Yehova akaniambia: “Umeona muzuri, kwa maana niko macho kabisa juu ya neno langu ili kulitimiza.”

13 Neno la Yehova likakuja kwangu mara ya pili, likisema: “Unaona nini?” Basi nikasema: “Ninaona chungu* chenye kutokota,* na mudomo wake umeinama kutoka kaskazini.” 14 Kisha Yehova akaniambia:

“Musiba utafunguliwa kutoka kaskazini

Juu ya wakaaji wote wa inchi.+

15 Kwa maana ‘ninaita familia zote za falme za kaskazini,’ ni vile Yehova anasema,+

‘Na watakuja; kila mumoja ataweka kiti chake cha ufalme

Kwenye muingilio wa milango mikubwa ya Yerusalemu,+

Kwenye kuta zake kuzunguka pande zote

Na kwenye miji yote ya Yuda.+

16 Na nitatangaza hukumu zangu juu yao kwa sababu ya uovu wao wote,

Kwa sababu wameniacha,+

Na wanachoma zabihu ili zitoe moshi kwa ajili ya miungu mingine+

Na kuinamia kazi za mikono yao wenyewe.’+

17 Lakini unapaswa kujitayarisha ili kutenda,*

Na unapaswa kusimama na kuwaambia kila jambo lenye ninakuamuru.

Usiwaogope,+

Ili nisikuogopeshe mbele yao.

18 Kwa maana leo nimekufanya kuwa muji wenye ngome,

Nguzo ya chuma, na kuta za shaba juu ya inchi yote,+

Kuelekea wafalme wa Yuda na wakubwa wake,

Kuelekea makuhani wake na watu wa inchi.+

19 Na hakika watapigana na wewe,

Lakini hawatakushinda,

Kwa maana ‘Mimi niko pamoja na wewe,’+ ni vile Yehova anasema, ‘ili kukuokoa.’”

2 Neno la Yehova likakuja kwangu, na kusema: 2 “Uende na utangaze katika masikio ya Yerusalemu, ‘Yehova anasema hivi:

“Ninakumbuka muzuri ushikamanifu* wa ujana wako,+

Upendo wenye ulionyesha wakati ulichumbiwa ili kuolewa,+

Namna ulinifuata katika jangwa,

Katika inchi yenye haipandwe mbegu.+

 3 Israeli alikuwa mutakatifu kwa Yehova,+ matunda ya kwanza ya mavuno yake.”’

‘Mutu yeyote mwenye alimumeza alikuwa na hatia.

Musiba ulikuwa unakuja juu yao,’ ni vile Yehova anasema.”+

 4 Musikie neno la Yehova, Ee nyumba ya Yakobo,

Na ninyi wote familia za nyumba ya Israeli.

 5 Yehova anasema hivi:

“Mababu zenu walipata kosa gani ndani yangu,+

Na hivyo wakaenda mbali sana na mimi,

Na wakafuata sanamu zenye hazina mafaa yoyote+ na wao wenyewe wakakuwa wenye hawana mafaa yoyote?+

 6 Hawakuuliza, ‘Yehova iko* wapi,

Yeye mwenye alitutosha katika inchi ya Misri,+

Mwenye alituongoza kupitia jangwa,

Kupitia inchi yenye majangwa+ na mashimo,

Kupitia inchi yenye ukame+ na yenye kivuli kizito,

Kupitia inchi yenye hakuna mutu mwenye anasafiri ndani

Na yenye hakuna wanadamu wenye wanaishi ndani?’

 7 Kisha nikawaleta ninyi katika inchi yenye mashamba ya matunda,

Ili kula matunda yake na vitu vyake vya muzuri.+

Lakini mukaingia na kuchafua inchi yangu;

Mukafanya uriti wangu kuwa kitu chenye kuchukiza.+

 8 Makuhani hawakuuliza, ‘Yehova iko* wapi?’+

Wale wenye kushugulika na Sheria hawakunijua,

Wachungaji waliniasi,+

Manabii walitoa unabii kupitia Baali,+

Na wakafuata wale wenye hawangeleta faida yoyote.

 9 ‘Basi nitashindana zaidi na ninyi,’+ ni vile Yehova anasema,

‘Na nitashindana na wana wa wana wenu.’

10 ‘Lakini muvuke mupaka kwenye inchi za pembeni ya bahari za* Kitimu+ na muone.

Ndiyo, mutume watu Kedari+ na mufikirie kwa uangalifu;

Muone ikiwa jambo kama hili limetendeka.

11 Je, taifa limekwisha kubadilisha miungu yake kwa ajili ya ile yenye haiko miungu?

Lakini watu wangu mwenyewe wamebadilisha utukufu wangu kwa ajili ya kitu chenye hakina mafaa.+

12 Muangalie jambo hili kwa mushangao, ninyi mbingu;

Mutetemeke kwa woga mukubwa kabisa,’ ni vile Yehova anasema,

13 ‘Kwa sababu watu wangu wamefanya mambo mbili ya mubaya:

Wameniacha mimi, chemchemi ya maji ya uzima,+

Na wamejichimbia* matangi,

Matangi yenye kuvunjika, yenye hayawezi kulinda maji.’

14 ‘Je, Israeli ni mutumishi ao ni mutumwa mwenye alizaliwa nyumbani?

Basi sababu gani ametolewa ili akuwe kitu cha kunyanganywa?

15 Wana-simba* wananguruma juu yake;+

Wamepandisha sauti zao.

Walifanya inchi yake kuwa kitu cha kuogopesha.

Miji yake imewashwa moto, na hivyo hakuna mukaaji.

16 Watu wa Nofu*+ na Tahpanesi+ wanakula sehemu ya juu ya katikati ya kichwa chako.

17 Je, haukujiletea jambo hilo

Kwa kumuacha Yehova Mungu wako+

Wakati alikuwa anakuongoza katika njia?

18 Sasa sababu gani unatamani njia ya kuenda Misri+

Ili kunywa maji ya Shihori?*

Sababu gani unatamani njia ya kuenda Ashuru+

Ili kunywa maji ya ule Muto?*

19 Uovu wako unapaswa kukurekebisha,

Na ukosefu wako mwenyewe wa uaminifu unapaswa kukukaripia.

Jua na utambue namna ni jambo la mubaya na lenye uchungu+

Kumuacha Yehova Mungu wako;

Haukuniogopa,’+ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, Yehova wa majeshi anasema.

20 ‘Kwa maana zamani nilivunja-vunja nira yako+

Na kukata pingu zako.

Lakini ulisema: “Mimi sitatumikia,”

Kwa maana juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila muti wenye majani mengi+

Ulilala ukiwa umejinyoosha, ukifanya ukahaba.+

21 Nilikupanda kama muzabibu muzuri sana mwekundu,+ wote ukiwa mbegu safi;

Basi namna gani umebadilika na kuwa machipukizi yenye kuharibika ya muzabibu wa kigeni mbele yangu?’+

22 ‘Hata kama unanawa kwa kutumia chumvi ya asili na unatumia sabuni nyingi,

Hatia yako itabakia kuwa alama mbele yangu,’+ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.

23 Namna gani unaweza kusema, ‘Sikujichafua.

Sikufuata Mabaali’?

Angalia njia yako katika bonde.

Fikiria kile umefanya.

Wewe ni kama ngamia-dike mudogo mwenye ni mwepesi,

Mwenye anakimbia huku na huku bila kusudi katika njia zake,

24 Punda wa pori mwenye kuzoea jangwa,

Mwenye kunusa upepo wakati wa tamaa yake kubwa ya kupandwa na dume.*

Ni nani mwenye anaweza kumuzuia wakati anashikwa na hamu ya kupandwa na dume?

Hakuna mutu yeyote kati ya wale wenye kumutafuta mwenye atajichokesha.

Katika kipindi chake* watamupata.

25 Zuia muguu wako usitembee wazi,

Na koo yako isikuwe na kiu.

Lakini ulisema, ‘Hakuna tumaini!+

Hapana! Nimependa wageni,*+

Na nitawafuata.’+

26 Kama haya ya mwizi wakati anakamatwa,

Ni vile nyumba ya Israeli ilipatishwa haya,

Wao, wafalme wao na wakubwa wao,

Makuhani wao na manabii wao.+

27 Wanaambia muti, ‘Wewe ni baba yangu,’+

Na jiwe, ‘Wewe ulinizaa.’

Lakini mimi wananigeuzia mugongo wao, hapana uso wao.+

Na wakati wa musiba wao watasema,

‘Simama na utuokoe!’+

28 Sasa iko wapi miungu yako yenye ulijitengenezea?+

Isimame kama inaweza kukuokoa wakati wako wa musiba.

Kwa maana miungu yako imekuwa mingi kama miji yako, Ee Yuda.+

29 ‘Sababu gani munaendelea kushindana na mimi?

Sababu gani ninyi wote mumeniasi?’+ ni vile Yehova anasema.

30 Nimepiga wana wenu bila matokeo.+

Hawakubali nizamu yoyote;+

Upanga wenu wenyewe ulimeza manabii wenu,+

Kama simba mwenye kushambulia.

31 Enyi kizazi, mufikirie wenyewe neno la Yehova.

Je, nimekuwa kama jangwa kwa Israeli

Ao inchi yenye giza lenye kukandamiza?

Sababu gani hawa, watu wangu, wamesema, ‘Tunaenda huku na huku tukiwa huru.

Hatutakuja kwako tena’?+

32 Je, bikira anaweza kusahau mapambo yake,

Na bibi-arusi nguo zake za kifua?*

Na bado watu wangu mwenyewe wamenisahau mimi kwa siku zenye hazina hesabu.+

33 Ee mwanamuke, namna unatayarisha njia yako kwa ufundi ili kutafuta upendo!

Umejizoeza katika njia za uovu.+

34 Hata pindo za nguo zako ziko na alama ya damu ya maskini wenye hawana* kosa,+

Hata kama sikuwapata katika tendo la kuvunja na kuingia;

Iko kwenye pindo zote za nguo zako.+

35 Lakini unasema, ‘Sina kosa.

Hakika kasirani yake imegeuka kutoka kwangu.’

Sasa ninaleta hukumu juu yako

Kwa sababu unasema, ‘Sikutenda zambi.’

36 Sababu gani unaona njia yako yenye haiko imara kuwa jambo la kidogo?

Utasikia haya kwa sababu ya Misri pia,+

Kama vile ulisikia haya kwa sababu ya Ashuru.+

37 Kwa sababu hiyo pia utaenda mikono yako ikiwa juu ya kichwa chako,+

Kwa maana Yehova amekataa wale wenye unategemea;

Hawatakuletea mafanikio.”

3 Watu wanauliza: “Kama mwanaume anamufukuza bibi yake na bibi huyo anamuacha na kuwa wa mwanaume mwingine, je, mwanaume huyo anapaswa kumurudilia tena?”

Je, inchi hiyo haikuchafuliwa kabisa?+

“Umefanya ukahaba na marafiki wengi,+

Na je, sasa unapaswa kurudia kwangu?” ni vile Yehova anasema.

 2 “Inua macho yako kuelekea vilima vyenye kuwa wazi na uone.

Ni wapi kwenye haukulalwa kinguvu?

Ulikaa pembeni ya barabara kwa ajili yao,

Kama mutu mwenye kuhama-hama* katika jangwa;

Unaendelea kuchafua inchi

Kwa ukahaba wako na uovu wako.+

 3 Kwa hiyo matone ya mvua yamezuiwa,+

Na hakuna mvua katika kipindi cha mvua ya mwisho.

Uko na uso wenye hauna haya wa* bibi mwenye anafanya ukahaba.

Unakataa kusikia haya.+

 4 Lakini sasa unaniita ukisema,

‘Baba yangu, wewe ni rafiki wa ujana wangu!+

 5 Je, mutu anapaswa kuendelea kuwa na kinyongo milele,

Ao kuwa na uchungu sikuzote?’

Ni vile unasema,

Lakini unaendelea kufanya mambo yote maovu yenye unaweza kufanya.”+

6 Katika siku za mufalme Yosia,+ Yehova aliniambia: “‘Je, umeona jambo lenye Israeli mwenye kukosa uaminifu amefanya? Ameenda juu ya kila mulima murefu na chini ya kila muti wenye majani mengi ili afanye ukahaba.+ 7 Hata kisha kufanya mambo hayo yote, niliendelea kumuambia arudie kwangu,+ lakini hakurudia; na Yuda akaendelea kumuangalia dada yake mudanganyifu.+ 8 Wakati niliona vile, nikafukuza Israeli mwenye kukosa uaminifu akiwa na cheti kamili cha kuvunja ndoa+ kwa sababu ya uzinifu wake.+ Lakini Yuda dada yake mudanganyifu hakuogopa; yeye pia alienda na kufanya ukahaba.+ 9 Aliona ukahaba wake kuwa jambo la kidogo, na akaendelea kuchafua inchi na kufanya uzinifu na majiwe na miti.+ 10 Ijapokuwa mambo hayo yote, Yuda dada yake mudanganyifu hakurudia kwangu kwa moyo wake wote, lakini kwa unafiki tu,’ ni vile Yehova anasema.”

11 Kisha Yehova akaniambia: “Israeli mwenye kukosa uaminifu amejionyesha kuwa mwenye* haki kuliko Yuda mudanganyifu.+ 12 Uende na utangaze maneno haya upande wa kaskazini:+

“‘“Rudia, Ee Israeli mwenye kuasi,” ni vile Yehova anasema.’+ ‘“Sitakuangalia kwa kasirani,*+ kwa maana mimi ni mushikamanifu,” ni vile Yehova anasema.’ ‘“Sitaendelea kuwa na kinyongo milele. 13 Isipokuwa tu ukubali hatia yako, kwa maana umemuasi Yehova Mungu wako. Uliendelea kutawanya wema wako* kwa wageni* chini ya kila muti wenye majani mengi, lakini haukutii sauti yangu,” ni vile Yehova anasema.’”

14 “Murudie, ninyi wana waasi,” ni vile Yehova anasema. “Kwa maana nimekuwa bwana wenu* wa kweli; na nitawakamata ninyi, mumoja kutoka katika muji mumoja na wawili kutoka katika familia moja, na nitawaleta Sayuni.+ 15 Na nitawapatia ninyi wachungaji kulingana na moyo wangu mwenyewe,+ na watawakulisha ninyi kwa ujuzi na ufahamu. 16 Mutakuwa wengi na mutazaa matunda katika inchi katika siku hizo,” ni vile Yehova anasema.+ “Hawatasema tena, ‘Sanduku la agano la Yehova!’ Halitaingia katika moyo, na hawatalikumbuka ao kulitamani, na halitafanywa tena. 17 Wakati huo wataita Yerusalemu kiti cha ufalme cha Yehova;+ na mataifa yote yatakusanywa pamoja kwa jina la Yehova katika Yerusalemu,+ na hawatafuata kwa kichwa-nguvu moyo wao muovu.”

18 “Katika siku hizo watatembea pamoja, nyumba ya Yuda pembeni ya nyumba ya Israeli,+ na pamoja watatoka katika inchi ya kaskazini na kuingia katika inchi yenye nilipatia mababu zenu kuwa uriti.+ 19 Na nilifikiri, ‘Namna nilikuweka kati ya wana na kukupatia inchi yenye kutamanika, uriti muzuri zaidi kati ya mataifa!’*+ Pia nilifikiri mutaniita, ‘Baba yangu!’ na kwamba hamutageuka na kuacha kunifuata. 20 ‘Kwa kweli kama vile bibi anamuacha bwana yake* kwa udanganyifu, ni vile ninyi pia, Ee nyumba ya Israeli, mumenitendea kwa udanganyifu,’+ ni vile Yehova anasema.”

21 Sauti inasikika kwenye vilima vyenye kuwa wazi,

Kulia na kusihi kwa watu wa Israeli,

Kwa maana wamepotosha njia yao;

Wamemusahau Yehova Mungu wao.+

22 “Murudie, ninyi wana waasi.

Nitaponyesha hali yenu ya uasi.”+

“Sisi hawa! Tumekuja kwako,

Kwa maana wewe, Ee Yehova, ni Mungu wetu.+

23 Kwa kweli vilima na muvurugo juu ya milima ni udanganyifu.+

Kwa kweli wokovu wa Israeli uko katika Yehova Mungu wetu.+

24 Lakini jambo la haya limekula* kazi ya nguvu ya mababu zetu tangu ujana wetu,+

Makundi yao na mifugo yao,

Watoto wao wanaume na watoto wao wanamuke.

25 Tulale katika haya yetu,

Na haya yetu itufunike,

Kwa maana tumemutendea zambi Yehova Mungu wetu,+

Sisi na baba zetu tangu ujana wetu mupaka leo hii,+

Na hatukutii sauti ya Yehova Mungu wetu.”

4 “Kama unarudia, Ee Israeli,” ni vile Yehova anasema,

“Kama unarudia kwangu

Na kama unaondoa sanamu zako zenye kuchukiza kutoka mbele yangu,

Basi hautakuwa mukimbizi.+

 2 Na kama unaapa,

‘Kama vile hakika Yehova anaishi!’ katika kweli, haki, na uadilifu,*

Basi mataifa yatajipatia baraka kupitia yeye,

Na yatajisifu katika yeye.”+

3 Kwa maana Yehova anaambia watu wa Yuda na Yerusalemu hivi:

“Mujilimie udongo wenye unafaa kulimwa,

Na musiendelee kupanda kati ya miiba.+

 4 Mujitahiri kwa ajili ya Yehova,

Na kuondoa magovi* ya mioyo yenu,+

Ninyi watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu,

Ili kasirani yangu kali isiwake kama moto

Na iteketeze bila mutu yeyote wa kuizimisha,

Kwa sababu ya matendo yenu maovu.”+

 5 Museme jambo hilo katika Yuda, na kulitangaza katika Yerusalemu.

Museme kwa sauti kubwa na kupiga baragumu katika inchi yote.+

Muite kwa sauti kubwa na kusema: “Mukusanyike pamoja,

Na sisi tukimbilie katika miji yenye ngome.+

 6 Muinue alama* kuelekea Sayuni.

Mutafute mahali pa kukimbilia, na musisimame wima,”

Kwa maana ninaleta musiba kutoka kaskazini,+ kishindo kikubwa.

 7 Ametokea kama simba kutoka katika kichaka chake;*+

Mwenye kuharibu mataifa ameondoka.+

Ametoka mahali pake ili kufanya inchi yako kuwa kitu cha kuogopesha.

Miji yako itafanywa kuwa mabomoko, bila mukaaji.+

 8 Kwa hiyo, muvae nguo za magunia,+

Muomboleze* na kufanya makelele,

Kwa sababu kasirani ya Yehova yenye kuwaka haijageuka kutoka kwetu.

 9 “Katika siku hiyo,” ni vile Yehova anasema, “moyo* wa mufalme utakosa nguvu,+

Pia moyo* wa wakubwa;

Makuhani wataingiwa na woga, na manabii watashangazwa.”+

10 Kisha nikasema: “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova! Kwa kweli umedanganya kabisa watu hawa+ na Yerusalemu, kwa kusema, ‘Mutakuwa na amani,’+ wakati upanga uko kwenye koo zetu.”*

11 Wakati huo watu hawa na Yerusalemu wataambiwa:

“Upepo wenye kukausha kutoka kwenye vilima vyenye kuwa wazi vya jangwa

Utavuma juu ya binti ya* watu wangu;

Haukuje kupepua ao kutakasa.

12 Upepo kamili unavuma kutoka sehemu hizi kwa agizo langu.

Sasa nitatangaza hukumu juu yao.

13 Angalia! Atakuja kama mawingu ya mvua,

Na magari yake ni kama upepo wa zoruba.+

Farasi wake wanaenda haraka kuliko tai.+

Ole wetu, kwa maana tumeharibiwa!

14 Safisha moyo wako ukuwe safi kutokana na uovu, Ee Yerusalemu, ili uokolewe.+

Utaendelea kuwa na mawazo maovu mupaka wakati gani?

15 Kwa maana sauti inatoa habari kutoka Dani,+

Na inatangaza musiba kutoka kwenye milima ya Efraimu.

16 Museme jambo hilo, ndiyo, kwa mataifa;

Mulitangaze juu ya Yerusalemu.”

“Walinzi* wanakuja kutoka inchi ya mbali,

Na watapandisha sauti zao ili kupinga miji ya Yuda.

17 Wanamushambulia pande zote kama walinzi wa eneo lenye kuwa wazi la mashamba,+

Kwa sababu ameniasi,”+ ni vile Yehova anasema.

18 “Njia zako mwenyewe na matendo yako yataletwa juu yako.+

Namna musiba wako ni muchungu,

Kwa maana unafika mupaka kwenye moyo wako!”

19 Ee uchungu wangu,* uchungu wangu!

Ninasikia maumivu makali katika moyo wangu.*

Moyo wangu unapiga-piga ndani yangu.

Siwezi kunyamaza,

Kwa maana nimesikia* sauti ya baragumu,

Mulio wa vita.*+

20 Musiba kisha musiba umesemwa,

Kwa maana inchi yote imeharibiwa.

Kwa kushitukia mahema yangu mwenyewe yameharibiwa,

Kwa wakati kidogo vitambaa vya mahema yangu.+

21 Nitaendelea kuona alama* mupaka wakati gani,

Kuendelea kusikia sauti ya baragumu?+

22 “Kwa maana watu wangu ni wapumbavu;+

Hawanihangaikie mimi.

Wao ni wana wajinga, wenye hawana uelewaji.

Wako na akili* ya kutosha wakati inahusu kutenda mabaya,

Lakini hawajue kutenda mema.

23 Niliona inchi, na angalia! ilikuwa wazi na ukiwa.+

Niliangalia mbingu, na mwangaza wake haukukuwa tena.+

24 Niliona milima, na angalia! ilikuwa inatetemeka,

Na vilima vilikuwa vinatikisika.+

25 Niliona, na angalia! hapakukuwa mutu yeyote,

Na ndege wote wa mbinguni walikuwa wamekimbia.+

26 Niliona, na angalia! shamba la matunda lilikuwa jangwa,

Na miji yake yote ilikuwa imebomolewa.+

Ilikuwa kwa sababu ya Yehova,

Kwa sababu ya kasirani yake yenye kuwaka.

27 Kwa maana Yehova anasema hivi: “Inchi yote itakuwa ukiwa,+

Lakini sitafanya uharibifu kamili.

28 Kwa sababu hiyo inchi itaomboleza,+

Na mbingu juu zitakuwa na giza.+

Ni kwa sababu nimesema, nimeamua,

Na sitabadilisha mawazo yangu,* wala sitarudia nyuma kutoka kwenye jambo hilo.+

29 Kwa sauti ya wapanda-farasi na wapiga-mishale,

Muji muzima unakimbia.+

Wanaingia katika miti midogo-midogo,*

Na wanapanda kwenye miamba.+

Kila muji unaachwa,

Na hakuna mutu mwenye kukaa ndani.”

30 Sasa kwa kuwa umeharibiwa, utafanya nini?

Ulikuwa unavaa nguo ya rangi nyekundu yenye kungaa,

Unajipamba kwa mapambo ya zahabu,

Na kupanua macho yako kwa kuyapakaa rangi nyeusi.*

Lakini ni bure kwamba ulijifanya kuwa na sura na umbo ya muzuri,+

Kwa maana wale wenye kukutamani wamekukataa;

Sasa wanatafuta kuondoa uzima wako.*+

31 Kwa maana nimesikia sauti kama ya mwanamuke mugonjwa,

Taabu kama ya mwanamuke mwenye kuzaa mutoto wake wa kwanza,

Sauti ya binti ya Sayuni mwenye anaendelea kuvuta pumuzi kwa nguvu.

Anasema hivi akinyoosha mikono yake:+

“Ole wangu, kwa maana nimechoka* kwa sababu ya wauaji!”

5 Mutembee huku na huku katika barabara za Yerusalemu.

Muone pande zote na muangalie.

Mutafute katika viwanja vyake vya watu wote ili kuona

Kama munaweza kumupata mutu mwenye kutenda kwa haki,+

Mutu mwenye anatafuta kuwa muaminifu,

Na nitasamehe muji huo.

 2 Hata wakisema: “Kama vile hakika Yehova anaishi!”

Watakuwa bado wanaapa kwa uongo.+

 3 Ee Yehova, je, macho yako hayatafute uaminifu?+

Uliwapiga, lakini hilo halikukuwa na matokeo yoyote juu yao.*

Uliwaharibu, lakini walikataa kukubali nizamu.+

Walifanya nyuso zao zikuwe nguvu kuliko mwamba,+

Na wakakataa kugeuka.+

 4 Lakini nilisema katika moyo wangu: “Hakika hawa wanapaswa kuwa watu wa hali ya chini.

Wanatenda kwa upumbavu, kwa maana hawajue njia ya Yehova,

Hukumu ya Mungu wao.

 5 Nitaenda kwa watu wa maana na kusema nao,

Kwa maana wanapaswa kuwa waliangalia njia ya Yehova,

Hukumu ya Mungu wao.+

Lakini wote walikuwa wamevunja nira

Na kukata vizuizi.”*

 6 Ndiyo sababu simba wa pori anawashambulia,

Imbwa wa pori wa maeneo tambarare ya jangwa anaendelea kuwaharibu,

Chui anakaa macho kwenye miji yao.

Kila mutu mwenye kutoka ndani anapasuliwa vipande-vipande.

Kwa maana makosa yao ni mengi;

Matendo yao ya kukosa uaminifu ni mengi sana.+

 7 Namna gani ninaweza kukusamehe kwa jambo hili?

Wana wako wameniacha,

Na wanaapa kwa kitu chenye hakiko Mungu.+

Nilitimiza mahitaji yao,

Lakini waliendelea kufanya uzinifu,

Na wakakusanyika kwenye nyumba ya kahaba.

 8 Wao ni kama farasi wenye hamu na tamaa ya kupanda dike,

Kila mumoja anamulilia kwa tamaa bibi ya mwanaume mwingine.+

 9 “Je, sipaswe kuwaomba watoe hesabu kwa ajili ya mambo hayo?” ni vile Yehova anasema.

“Je, sipaswe* kujilipizia kisasi juu ya taifa kama hilo?”+

10 “Mushambulie mistari yake ya mizabibu na kuharibu,

Lakini musiharibu kabisa.+

Muondoe machipukizi yake yenye kusambaa,

Kwa maana hayako ya Yehova.

11 Kwa maana nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda

Wamenitendea kwa udanganyifu kabisa,” ni vile Yehova anasema.+

12 “Wamemukana Yehova, na wanaendelea kusema,

‘Hatafanya chochote.*+

Hakuna musiba wowote wenye utakuja juu yetu;

Hatutaona upanga wala njaa.’+

13 Manabii wamejaa upepo,

Na neno* haliko ndani yao.

Acha mambo hayo yawapate!”

14 Kwa hiyo, Yehova, Mungu wa majeshi, anasema:

“Kwa sababu watu hawa wanasema jambo hilo,

Angalia, ninafanya maneno yangu kuwa moto katika kinywa chako,+

Na watu hawa ndio kuni,

Na utawateketeza.”+

15 “Angalia, ninaleta juu yenu taifa kutoka mbali, Ee nyumba ya Israeli,”+ ni vile Yehova anasema.

“Ni taifa lenye kudumu.

Ni taifa la zamani,

Taifa lenye haujue luga yake,

Na hauwezi kuelewa mambo yenye wanasema.+

16 Mufuko wao wa mishale ni kama kaburi lenye kuwa wazi;

Wote ni wapiganaji-vita.

17 Watameza mavuno yako na mukate wako.+

Watameza watoto wako wanaume na watoto wako wanamuke.

Watapasua makundi yako na mifugo yako vipande-vipande.

Watameza mizabibu yako na miti yako ya tini.

Wataharibu kwa upanga miji yako yenye ngome yenye unategemea.”

18 “Lakini hata katika siku hizo,” ni vile Yehova anasema, “Sitawaharibu ninyi kabisa.+ 19 Na wakati wanauliza, ‘Sababu gani Yehova Mungu wetu ametutendea mambo haya yote?’ utawajibu, ‘Kama vile muliniacha ili kutumikia mungu wa kigeni katika inchi yenu, ni vile mutatumikia wageni katika inchi yenye haiko yenu.’”+

20 Mutangaze jambo hili katika nyumba ya Yakobo,

Na kulitangaza katika Yuda, mukisema:

21 “Musikie jambo hili, ninyi watu wapumbavu na wenye hawana akili:*+

Wako na macho lakini hawawezi kuona;+

Wako na masikio lakini hawawezi kusikia.+

22 ‘Je, hamuniogope mimi?’ ni vile Yehova anasema,

‘Je, hamupaswe kutetemeka mbele yangu?

Mimi ndiye niliweka muchanga kuwa mupaka wa bahari,

Sheria yenye kudumu yenye bahari haiwezi kuvuka.

Hata kama mawimbi yake yanajiinua, hayawezi kushinda;

Hata kama yananguruma, bado hayawezi kuivuka.+

23 Lakini watu hawa wako kichwa-nguvu na ni wenye kuasi;

Wamegeuka pembeni na kufuata njia yao wenyewe.+

24 Na hawaseme katika moyo wao:

“Sasa tumuogope Yehova Mungu wetu,

Ule mwenye anatoa mvua katika kipindi chake,

Mvua ya kipindi cha mvua ya kwanza na pia mvua ya kipindi cha mvua ya mwisho,

Ule mwenye kwa ajili yetu analinda majuma yenye yaliwekwa ya mavuno.”+

25 Makosa yenu wenyewe yamezuia mambo haya yasikuje;

Zambi zenu wenyewe zimewaima ninyi mambo mema.+

26 Kwa maana kati ya watu wangu kuko watu waovu.

Wanaendelea kukaza macho, kama vile wakati wawindaji wa ndege wanashutama.

Wanatega mutego hatari.

Wao wananasa watu.

27 Kama kizimba* chenye kujaa ndege,

Ni vile nyumba zao zimejaa udanganyifu.+

Ndiyo sababu wamekuwa wenye nguvu na matajiri.

28 Wamenenepa na kuwa laini;

Wanajaa sana mambo maovu.

Hawatetee kesi ya hukumu ya mwenye hana baba,+

Ili wapate mafanikio;

Na wanaima maskini haki.’”+

29 “Je, sipaswe kuwaomba watoe hesabu kwa sababu ya mambo hayo?” ni vile Yehova anasema.

“Je, sipaswe* kujilipizia kisasi juu ya taifa kama hilo?

30 Jambo la kushangaza na lenye kuchukiza limetokea katika inchi:

31 Manabii wanatoa unabii kwa uongo,+

Na makuhani wanatawala wengine kwa mamlaka yao wenyewe.

Na watu wangu wanapenda mambo yakuwe vile.+

Lakini mutafanya nini wakati mwisho utafika?”

6 Mukimbilie mahali kwenye usalama, Enyi wana wa Benyamini, mbali na Yerusalemu.

Mupige baragumu+ katika Tekoa;+

Muwashe alama ya moto juu ya Bet-hakeremu!

Kwa maana musiba unaangalia kutoka kaskazini, musiba mukubwa.+

 2 Binti ya Sayuni anafanana na mwanamuke mwenye sura na umbo ya muzuri na mwenye kuwa teketeke.+

 3 Wachungaji na makundi yao watakuja.

Watasimamisha mahema yao kumuzunguka pande zote,+

Kila mumoja akikulisha kundi lenye liko chini ya ulinzi wake.+

 4 “Mujitayarishe ili kupigana naye vita!*

Musimame, na tumushambulie katikati ya muchana!”

“Ole wetu, kwa maana muchana unaisha,

Kwa maana vivuli vya mangaribi vinakuwa vya murefu zaidi!”

 5 “Musimame, na tumushambulie usiku

Na kuharibu minara yake yenye ngome.”+

 6 Kwa maana Yehova wa majeshi anasema hivi:

“Mukate miti na mujenge boma la kuzunguka Yerusalemu kwa ajili ya vita.+

Yeye ni muji wenye unapaswa kuombwa utoe hesabu;

Ndani yake muko ukandamizaji tu.+

 7 Kama vile tangi linalinda maji yake yakiwa baridi,

Ni vile anaweka uovu wake ukiwa baridi.

Jeuri na uharibifu vinasikiwa ndani yake;+

Ugonjwa na pigo viko mbele yangu sikuzote.

 8 Upewe onyo, Ee Yerusalemu, ao nitageuka na kukuacha* nikiwa nimechukizwa;+

Nitakufanya ukuwe ukiwa, inchi yenye haina wakaaji.”+

 9 Yehova wa majeshi anasema hivi:

“Wataokota kwa ukamili mabaki ya Israeli kama zabibu za mwisho kwenye muzabibu.

Pitisha mukono wako tena kama mutu mwenye kukusanya zabibu kwenye mizabibu.”

10 “Nitasema na nani na kumupatia onyo?

Ni nani mwenye atasikiliza?

Angalia! Masikio yao yamefungwa,* na hivyo hawawezi kusikiliza.+

Angalia! Neno la Yehova limekuwa kitu chenye wanazarau,+

Hawapendezwe nalo.

11 Basi nimejaa kasirani kali ya Yehova,

Na nimechoka kuibeba.”+

“Uimwange juu ya mutoto katika barabara,+

Juu ya vikundi vya vijana wenye kukusanyika pamoja.

Wote watakamatwa, mwanaume pamoja na bibi yake,

Wenye kuzeeka pamoja na wenye kuzeeka sana.*+

12 Nyumba zao zitapewa watu wengine,

Pamoja na mashamba yao na bibi zao.+

Kwa maana nitanyoosha mukono wangu juu ya wakaaji wa inchi,” ni vile Yehova anasema.

13 “Kwa maana kuanzia mudogo zaidi mupaka mukubwa zaidi, kila mumoja anajipatia faida yenye haiko ya haki;+

Kuanzia nabii mupaka kuhani, kila mumoja anatenda kwa upunjaji.+

14 Na wanajaribu kuponyesha kijuujuu kuvunjika kwa watu wangu, wakisema,

‘Kuko amani! Kuko amani!’

Wakati hakuna amani.+

15 Je, wanasikia haya kwa sababu ya mambo yenye kuchukiza yenye wamefanya?

Hawasikie haya hata kidogo!

Hata hawajue namna ya kufezeheka!+

Basi wataanguka kati ya wale wenye kuanguka.

Wakati nitaleta azabu juu yao watajikwaa,” ni vile Yehova anasema.

16 Yehova anasema hivi:

“Musimame kwenye makutano ya barabara na muone.

Muulize juu ya barabara za zamani,

Muulize njia ya muzuri iko wapi, na mutembee ndani yake,+

Na mupate pumuziko kwa ajili yenu wenyewe.”*

Lakini wanasema: “Hatutatembea ndani yake.”+

17 “Na niliweka walinzi+ wenye walisema,

‘Musikilize sauti ya baragumu!’”+

Lakini wakasema: “Hatutasikiliza.”+

18 “Kwa hiyo musikie, Enyi mataifa!

Na mujue, Ee mukusanyiko,

Jambo lenye litawapata wao.

19 Sikiliza, Ee dunia!

Ninaleta musiba juu ya watu hawa+

Kama matunda ya mipango yao wenyewe,

Kwa maana hawakusikiliza maneno yangu

Na walikataa sheria yangu.”*

20 “Iko na faida gani kwangu kwamba munaleta ubani kutoka Sheba

Na kane* tamu kutoka inchi ya mbali?

Matoleo yenu mazima ya kuteketezwa hayakubalike,

Na zabihu zenu hazinipendeze.”+

21 Kwa hiyo Yehova anasema hivi:

“Angalia, ninawekea watu hawa vikwazo,

Na watajikwaa juu yake,

Baba na wana pamoja,

Jirani na mwenzake,

Na wote wataangamia.”+

22 Yehova anasema hivi:

“Angalia! Watu wanakuja kutoka inchi ya kaskazini,

Na taifa kubwa litaamushwa kutoka sehemu za mbali zaidi za dunia.+

23 Watashika upinde na mukuki mudogo.

Hawana huruma na hawatakuwa na rehema.

Sauti yao itanguruma kama bahari,

Na wanapanda juu ya farasi.+

Wanajipanga katika utaratibu wa vita kama mwanaume wa vita juu yako, Ee binti ya Sayuni.”

24 Tumesikia habari zake.

Mikono yetu imeregea;+

Taabu imetushika,

Uchungu kama wa* mwanamuke mwenye kuzaa.+

25 Usiende katika eneo la mashamba,

Na usitembee katika barabara,

Kwa maana adui iko* na upanga;

Kuko woga kuzunguka pande zote.

26 Ee binti ya watu wangu,

Vaa nguo ya gunia+ na ujizungushe katika majivu.

Omboleza kama vile unamuombolezea mwana wa pekee, kwa kilio cha uchungu,+

Kwa maana mwenye kuharibu atakuja juu yetu kwa kushitukia.+

27 “Nimekufanya wewe* kuwa mupimaji wa metali kati ya watu wangu,

Mutu mwenye kufanya uchunguzi kamili;

Unapaswa kuangalia na kuchunguza njia yao.

28 Wao wote wako kichwa-nguvu sana,+

Wanatembea huku na huku kama wachongezi.+

Wako kama shaba na chuma;

Wote wamepotoka.

29 Vyombo vya kuingiza upepo katika tanuru ya moto vimeunguzwa.*

Risasi inatoka ndani ya moto wao.

Mutu anaendelea kusafisha sana lakini bure,+

Na wale wenye kuwa wabaya hawakutengwa.+

30 Feza yenye kukataliwa ni vile hakika watu watawaita,

Kwa maana Yehova amewakataa.”+

7 Hili ndilo neno lenye lilikuja kwa Yeremia kutoka kwa Yehova, na kusema: 2 “Simama katika mulango mukubwa wa nyumba ya Yehova na utangaze pale ujumbe huu, ‘Musikie neno la Yehova, ninyi wote watu wa Yuda wenye munaingia katika milango hii mikubwa ili kumuinamia Yehova. 3 Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Mubadilishe njia zenu na matendo yenu, na nitawaruhusu muendelee kukaa mahali hapa.+ 4 Musiweke tegemeo lenu katika maneno ya udanganyifu na kusema, ‘Hili ni* hekalu la Yehova, hekalu la Yehova, hekalu la Yehova!’+ 5 Kwa maana kama kwa kweli munabadilisha njia zenu na matendo yenu; kama kwa kweli munatenda haki kati ya mutu na jirani yake;+ 6 kama hamukandamize wakaaji wageni, mayatima,* na wajane;+ kama hamumwange damu yenye haina kosa mahali hapa; na kama hamufuate miungu mingine na kujiletea maumivu ninyi wenyewe;+ 7 basi nitawaruhusu muendelee kukaa mahali hapa, katika inchi yenye nilipatia mababu zenu kwa wakati wote.”’”*

8 “Lakini munaweka tegemeo lenu katika maneno ya udanganyifu+⁠—​jambo hilo halitaleta faida yoyote hata kidogo. 9 Je, munaweza kuiba,+ kuua, kufanya uzinifu, kuapa kwa uongo,+ kumutolea Baali zabihu,*+ na kufuata miungu yenye hamukujua, 10 na kisha mukuje na kusimama mbele yangu katika nyumba hii yenye kubeba jina langu na kusema, ‘Tutaokolewa,’ hata kama munafanya mambo haya yote yenye kuchukiza? 11 Je, nyumba hii yenye kubeba jina langu imekuwa pango la wanyanganyi mbele ya macho yenu?+ Muangalie, nimejionea jambo hilo,” ni vile Yehova anasema.

12 “‘Hata hivyo, sasa muende mahali pangu katika Shilo,+ kwenye pale mwanzo nilifanya jina langu likae,+ na muone kile nilipafanyia kwa sababu ya ubaya wa watu wangu Israeli.+ 13 Lakini muliendelea kufanya mambo hayo yote,’ ni vile Yehova anasema, ‘na hata kama nilisema na ninyi tena na tena,* hamukusikiliza.+ Niliendelea kuwaita ninyi, lakini hamukujibu.+ 14 Ni vile nitatendea nyumba yenye kubeba jina langu,+ yenye munategemea,+ na mahali hapa kwenye niliwapatia ninyi na mababu zenu, kama vile nilitendea Shilo.+ 15 Nitawatupa ninyi kutoka mbele ya macho yangu, kama vile nilitupa ndugu zenu wote, wazao wote wa Efraimu.’+

16 “Na wewe, usisali kwa ajili ya watu hawa. Usilie kwa sauti kubwa ao kutoa sala ao kuniomba kwa ajili yao,+ kwa maana sitakusikiliza.+ 17 Je, hauone mambo yenye wanafanya katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu? 18 Wana wanakusanya kuni, baba wanawasha moto, na bibi wanaponda unga ili kumutengenezea Malkia wa Mbinguni* keki za zabihu,+ na wanamwangia miungu mingine matoleo ya kinywaji ili kunikasirisha.+ 19 ‘Lakini je, ni mimi ndiye wanaumiza?’* ni vile Yehova anasema. ‘Je, hawajiumize wao wenyewe, kwa haya yao wenyewe?’+ 20 Kwa hiyo Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema, ‘Angalia! Hasira yangu na kasirani yangu kali zitamwangwa juu ya mahali hapa,+ juu ya mwanadamu na munyama, juu ya miti ya shamba na mazao ya udongo; itateketeza na haitazimishwa.’+

21 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Muendelee, muongeze matoleo yenu mazima ya kuteketezwa kwenye zabihu zenu zingine, na mukule nyama ninyi wenyewe.+ 22 Kwa maana katika siku yenye nilitosha mababu zenu katika inchi ya Misri, sikusema nao ao kuwaamuru juu ya matoleo mazima ya kuteketezwa na zabihu.+ 23 Lakini niliwapatia amri hii: “Mutii sauti yangu, na nitakuwa Mungu wenu, na ninyi mutakuwa watu wangu.+ Munapaswa kutembea katika njia yote yenye ninaamuru, ili mambo yakuwe muzuri kwenu.”’+ 24 Lakini hawakusikiliza wala kutega sikio lao;+ tofauti na hilo, walitembea katika mipango yao ya mubaya,* na kwa kichwa-nguvu walifuata moyo wao muovu,+ na wakarudia nyuma, hawakuenda mbele, 25 tangu siku yenye mababu zenu walitoka katika inchi ya Misri mupaka leo hii.+ Basi nikaendelea kutuma kwenu watumishi wangu wote manabii, nikiwatuma kila siku, tena na tena.*+ 26 Lakini walikataa kunisikiliza, na hawakutega sikio lao.+ Tofauti na hilo, walikuwa kichwa-nguvu,* na wakatenda mubaya zaidi kuliko mababu zao!

27 “Utawaambia maneno haya yote,+ lakini hawatakusikiliza; utawaita, lakini hawatakujibu. 28 Na utawaambia, ‘Hili ndilo taifa lenye halikutii sauti ya Yehova Mungu wao na walikataa kukubali nizamu. Uaminifu umeangamia na hata hautajwe kati yao.’*+

29 “Nyoa nywele zako zenye hazijakatwa* na kuzitupa mbali, na uimbe wimbo wa huzuni* juu ya vilima vyenye kuwa wazi, kwa maana Yehova amekataa na ataacha kizazi hiki chenye kimemukasirisha sana. 30 ‘Kwa maana watu wa Yuda wamefanya mambo ya mubaya mbele ya macho yangu,’ ni vile Yehova anasema. ‘Wameweka sanamu zao zenye kuchukiza katika nyumba yenye inabeba jina langu, ili kuichafua.+ 31 Wamejenga mahali pa juu pa Tofeti, kwenye kuwa katika Bonde la Mwana wa Hinomu,*+ ili kuteketeza watoto wao wanaume na watoto wao wanamuke katika moto,+ jambo lenye sikukuwa nimeamuru na halijaingia katika moyo wangu* hata kidogo.’+

32 “‘Kwa hiyo angalia! siku zinakuja,’ ni vile Yehova anasema, ‘wakati halitaitwa tena Tofeti ao Bonde la Mwana wa Hinomu* lakini Bonde la Mauaji. Watazika katika Tofeti mupaka kusikuwe nafasi yenye kubakia.+ 33 Na maiti za watu hawa zitakuwa chakula cha ndege wa mbinguni na cha wanyama wa dunia, bila mutu wa kuwaogopesha.+ 34 Nitamaliza sauti ya kufurahi na sauti ya kushangilia, sauti ya bwana-arusi na sauti ya bibi-arusi,+ katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu, kwa maana inchi itafanywa kuwa mabomoko.’”+

8 “Wakati huo,” ni vile Yehova anasema, “mifupa ya wafalme wa Yuda, mifupa ya wakubwa wake, mifupa ya makuhani, mifupa ya manabii, na mifupa ya wakaaji wa Yerusalemu itachukuliwa kutoka katika makaburi yao. 2 Itatandikwa mbele ya jua na mbele ya mwezi na mbele ya jeshi lote la mbinguni vyenye wamependa na kutumikia na kufuata na kutafuta na kuinamia.+ Haitakusanywa, na haitazikwa. Itakuwa kama mbolea juu ya uso wa inchi.”+

3 “Na mabaki ya familia hii yenye uovu wenye wataokoka watachagua kifo kuliko uzima katika sehemu zote kwenye nitawatawanya,” ni vile Yehova wa majeshi anasema.

4 “Na unapaswa kuwaambia, ‘Yehova anasema hivi:

“Je, wataanguka na wasisimame tena?

Kama mutu mumoja anarudia, je, ule mwingine hatarudia pia?

 5 Sababu gani watu hawa, Yerusalemu, wanakosa uaminifu kwa ukosefu wa uaminifu wenye kudumu?

Wanashikilia sana udanganyifu;

Wanakataa kurudia.+

 6 Nilitega sikio na kuendelea kusikiliza, lakini namna walikuwa wanasema haikukuwa sawa.

Hakuna mutu mwenye alitubu uovu wake ao kuuliza, ‘Nimefanya nini?’+

Kila mumoja anaendelea kurudia kwenye njia yenye inapendwa na wengi, kama farasi mwenye anakimbilia kwenye pigano.

 7 Hata korongo katika anga anajua vipindi vyake;*

Njiwa-tetere na ndege teleka na ndege kuruwiji* hawasahau wakati wao wa kurudia.*

Lakini watu wangu mwenyewe hawaelewe hukumu ya Yehova.”’+

 8 ‘Namna gani munaweza kusema: “Tuko na hekima, na tuko na sheria ya* Yehova”?

Kwa maana hakika, kalamu ya uongo+ ya waandishi imetumiwa tu kwa ajili ya uongo.

 9 Wenye hekima wamepatishwa haya.+

Wameingiwa na woga na watakamatwa.

Angalia! Wamekataa neno la Yehova,

Na wako na hekima gani?

10 Basi nitapatia wanaume wengine bibi zao,

Mashamba yao nitayapatia watu wengine;+

Kwa maana kuanzia mudogo zaidi mupaka mukubwa zaidi, kila mumoja anajipatia faida yenye haiko ya haki;+

Kuanzia nabii mupaka kuhani, kila mumoja anatenda kwa upunjaji.+

11 Na wanajaribu kuponyesha kijuujuu kuvunjika kwa binti ya watu wangu, wakisema,

“Kuko amani! Kuko amani!”

Wakati hakuna amani.+

12 Je, wanasikia haya kwa sababu ya mambo yenye kuchukiza yenye wamefanya?

Hawasikie haya hata kidogo!

Hata hawajue namna ya kufezeheka!+

Basi wataanguka kati ya wale wenye kuanguka.

Wakati nitaleta azabu juu yao watajikwaa,”+ ni vile Yehova anasema.

13 ‘Wakati nitawakusanya, nitawafikisha kwenye mwisho wao,’ ni vile Yehova anasema.

‘Hakutakuwa zabibu zenye kubakia kwenye muzabibu, ao tini kwenye muti wa tini, na majani yatakauka.

Na watapoteza kile chenye niliwapatia.’”

14 “Sababu gani tunakaa hapa?

Tukusanyike pamoja na tuingie katika miji yenye ngome+ na tuangamie mule.

Kwa maana Yehova Mungu wetu atatuharibu,

Na anatupatia maji yenye sumu tukunywe,+

Kwa sababu tumemutendea Yehova zambi.

15 Kulikuwa tumaini la kupata amani, lakini hakuna mema yenye yalikuja,

Tumaini la kupata kipindi cha kuponyeshwa, lakini kuko woga!+

16 Kukoroma kwa farasi wake kumesikiwa kutoka Dani.

Kwa sauti ya mulio wa farasi-dume wake,

Inchi nzima inatetemeka.

Wanaingia na kurarua inchi na kila kitu chenye kuwa ndani,

Muji na wakaaji wake.”

17 “Kwa maana angalia, ninatuma nyoka kati yenu,

Nyoka wenye sumu wenye hawawezi kuchezeshwa,

Na hakika watawauma ninyi,” ni vile Yehova anasema.

18 Huzuni yangu haiwezi kupona;

Moyo wangu ni mugonjwa.

19 Kutoka inchi ya mbali kuko kilio cha kuomba musaada

Kutoka kwa binti ya watu wangu:

“Je, Yehova haiko katika Sayuni?

Ao je, mufalme wake haiko ndani yake?”

“Sababu gani wamenikasirisha kupitia sanamu zao za kuchongwa,

Kupitia miungu yao ya kigeni yenye haina mafaa yoyote?”

20 “Mavuno yamepita, kipindi cha joto kimeisha,

Lakini hatukuokolewa!”

21 Nimevunjwa-vunjwa kwa sababu ya kuvunjika kwa binti ya watu wangu;+

Nimehuzunika.

Nimeshikwa na woga.

22 Je, hakuna zeri* katika Gileadi?+

Ao, je, hakuna muponyaji* kule?+

Sababu gani binti ya watu wangu hakuponyeshwa?+

9 Aa! kama tu kichwa changu kingekuwa maji,

Na macho yangu chemchemi ya machozi!+

Basi ningelia muchana na usiku

Kwa ajili ya wenye waliuawa wa watu wangu.

 2 Aa! kama tu ningekuwa na mahali kwenye wasafiri wanakaa katika jangwa!

Basi ningeacha watu wangu na kuenda mbali nao,

Kwa maana wote ni wazinifu,+

Kikundi cha wadanganyifu.

 3 Wanapinda ulimi wao kama upinde;

Uongo unaenea sana katika inchi, hapana uaminifu.+

“Wanatoka kwenye uovu mupaka uovu,

Na hawanisikilize,”+ ni vile Yehova anasema.

 4 “Kila mutu, afanye angalisho na jirani yake,

Na usimutegemee hata ndugu yako.

Kwa maana kila ndugu ni musaliti,+

Na kila jirani ni muchongezi.+

 5 Kila mutu anamudanganya jirani yake,

Na hakuna mwenye kusema kweli.

Wamefundisha ulimi wao kusema uongo.+

Wanajichokesha kwa kufanya makosa.

 6 Unaishi katikati ya udanganyifu.

Katika udanganyifu wao walikataa kunijua,” ni vile Yehova anasema.

 7 Kwa hiyo Yehova wa majeshi anasema hivi:

“Nitawayeyusha na kuwajaribu,+

Kwa maana ni nini kingine chenye ninaweza kumufanyia binti ya watu wangu?

 8 Ulimi wao ni mushale wenye kuua wenye unasema udanganyifu.

Kwa kinywa chake mutu anasema juu ya amani na jirani yake,

Lakini ndani anavizia.”

 9 “Je, sipaswe kuwaomba watoe hesabu kwa sababu ya mambo hayo?” ni vile Yehova anasema.

“Je, sipaswe* kujilipizia kisasi juu ya taifa kama hilo?+

10 Nitalia na kuomboleza kwa ajili ya milima

Na kuimba wimbo wa huzuni* kwa ajili ya malisho ya jangwa,

Kwa maana yameteketezwa na hivyo hakuna mwanadamu mwenye kupita katikati,

Na sauti ya mifugo haisikiwe.

Ndege wa mbinguni na wanyama wamekimbia; wameenda.+

11 Nitafanya Yerusalemu kuwa rundo la majiwe,+ mapango ya mbweha,+

Na nitafanya miji ya Yuda ikuwe ukiwa, bila mukaaji.+

12 Ni nani mwenye hekima vya kutosha ili aweze kuelewa jambo hili?

Kinywa cha Yehova kimesema na nani, ili atangaze jambo hili?

Sababu gani inchi imeangamia?

Sababu gani imeteketezwa kama jangwa,

Na hivyo hakuna mutu mwenye kupita katikati?”

13 Yehova akajibu: “Kwa sababu walikataa sheria yangu yenye* niliweka mbele yao, na kwa sababu hawakuifuata na kutii sauti yangu. 14 Tofauti na hilo, kwa kichwa-nguvu walifuata mioyo yao wenyewe,+ na walifuata sanamu za Baali, kama vile baba zao walikuwa wamewafundisha kufanya.+ 15 Kwa hiyo, Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema, ‘Angalia, ninafanya watu hawa wakule pakanga, na nitawafanya wakunywe maji yenye sumu.+ 16 Nitawatawanya kati ya mataifa yenye wao na baba zao hawakujua,+ na nitatuma upanga uwafuate mupaka wakati nitakuwa nimewaharibu.’+

17 Yehova wa majeshi anasema hivi:

‘Mujiendeshe kwa uelewaji.

Muite wanamuke wenye kuimba nyimbo za huzuni,*+

Na muite wanamuke wenye ufundi wakuje,

18 Ili wafanye haraka na kutuombolezea,

Ili macho yetu yatiririke machozi

Na kope zetu zitiririke maji.+

19 Kwa maana sauti ya maombolezo imesikiwa kutoka Sayuni:+

“Namna tumeharibiwa!

Namna haya yetu ni kubwa!

Kwa maana tumeacha inchi, na wamebomoa nyumba zetu.”+

20 Ninyi wanamuke, musikie neno la Yehova.

Sikio lenu lipokee neno la kinywa chake.

Mufundishe mabinti wenu maombolezo haya,

Na mufundishane wimbo huu wa huzuni.*+

21 Kwa maana kifo kimekuja kupitia madirisha yetu;

Kimeingia ndani ya minara yetu yenye ngome

Ili kuchukua watoto kutoka katika barabara

Na vijana kutoka katika viwanja vya watu wote.’+

22 Sema, ‘Yehova anasema hivi:

“Maiti za watu zitaanguka kama mbolea juu ya uso wa shamba,

Kama mafungu ya nafaka yenye yalikatwa karibuni nyuma ya muvunaji,

Bila mutu wa kuyakusanya.”’”+

23 Yehova anasema hivi:

“Mutu mwenye hekima asijisifu kwa sababu ya hekima yake;+

Mutu mwenye nguvu asijisifu kwa sababu ya nguvu zake;

Na tajiri asijisifu kwa sababu ya utajiri wake.”+

24 “Lakini ule mwenye kujisifu, ajisifu kwa jambo hili:

Kwamba iko* na ufahamu na ujuzi juu yangu,+

Kwamba mimi ni Yehova, Mwenye kuonyesha upendo mushikamanifu, haki, na uadilifu* katika dunia,+

Kwa maana ninapendezwa na mambo hayo,”+ ni vile Yehova anasema.

25 “Muangalie! Siku zinakuja,” ni vile Yehova anasema, “na nitaomba hesabu kwa kila mutu mwenye kutahiriwa na bado hajatahiriwa,+ 26 kwa Misri+ na Yuda+ na Edomu+ na Waamoni+ na Moabu+ na wale wote wenye kuwa na nywele zenye zilikatwa kwenye mataya ya masikio* wenye kukaa katika jangwa;+ kwa maana mataifa yote hayatahiriwe, na nyumba yote ya Israeli haitahiriwe katika moyo.”+

10 Musikie neno lenye Yehova amesema juu yenu, Ee nyumba ya Israeli. 2 Yehova anasema hivi:

“Musijifunze njia ya mataifa,+

Na musiogopeshwe na alama za mbinguni

Kwa sababu mataifa yanaogopeshwa nazo.+

 3 Kwa maana desturi za vikundi vya watu ni udanganyifu.*

Ni muti tu wa pori wenye kukatwa,

Wenye ulifanyiwa kazi na mikono ya fundi kwa chombo chake.*+

 4 Wanaupamba kwa feza na zahabu+

Na wanaupigilia misumari kwa nyundo* ili usianguke.+

 5 Kama sanamu ya kufukuza ndege katika shamba la matango, haziwezi kusema;+

Lazima zibebwe, kwa maana haziwezi kutembea.+

Musiziogope, kwa maana haziwezi kuumiza,

Wala haziwezi kufanya jambo lolote la muzuri.”+

 6 Hakuna mutu yeyote mwenye kuwa kama wewe, Ee Yehova.+

Wewe ni mukubwa, na jina lako ni kubwa na lenye nguvu.

 7 Ni nani mwenye hapaswe kukuogopa, Ee Mufalme wa mataifa,+ kwa maana inafaa;

Kwa sababu kati ya watu wote wenye hekima wa mataifa na kati ya falme zao zote,

Hakuna mutu yeyote hata kidogo mwenye kuwa kama wewe.+

 8 Wote hawatumie akili na ni wajinga.+

Agizo kutoka kwa muti ni udanganyifu* kabisa.+

 9 Mabamba ya feza yanaletwa kutoka Tarshishi+ na zahabu kutoka Ufazi,

Kazi ya fundi, ya mikono ya fundi wa chuma.

Nguo zao ni uzi ya bluu na sufu ya rangi ya zambarau.

Vyote vinatengenezwa na wafanyakazi wenye ufundi.

10 Lakini kwa kweli Yehova ni Mungu.

Yeye ndiye Mungu mwenye kuishi+ na Mufalme wa milele.+

Kwa sababu ya kasirani yake kali dunia itatetemeka,+

Na hakuna mataifa yenye yatavumilia kemeo lake.

11* Munapaswa kuwaambia hivi:

“Miungu yenye haikufanya mbingu na dunia

Itaangamia kutoka katika dunia na kutoka chini ya mbingu hizi.”+

12 Yeye ndiye Mutengenezaji wa dunia kwa nguvu zake,

Ule mwenye alifanya imara inchi yenye kuzaa kwa hekima yake+

Na mwenye alitandika mbingu kwa uelewaji wake.+

13 Wakati anafanya sauti yake isikike,

Maji yenye kuwa mbinguni yanakuwa na muvurugo,+

Na anafanya mawingu yapande* kutoka kwenye miisho ya dunia.+

Anatokeza umeme wa radi* kwa ajili ya mvua,

Na analeta upepo katika madepo yake.+

14 Kila mutu anatenda kwa kukosa akili na bila ujuzi.

Kila fundi wa chuma atapatishwa haya kwa sababu ya sanamu ya kuchongwa;+

Kwa maana sanamu yake ya chuma* ni uongo,

Na hakuna roho* ndani yazo.+

15 Hizo ni udanganyifu,* kazi ya muzaha.+

Wakati siku ya kuziomba zitoe hesabu itakuja, zitaangamia.

16 Fungu la Yakobo haliko kama vitu hivyo,

Kwa maana Yeye ndiye alifanya kila kitu,

Na Israeli ndiyo fimbo ya uriti wake.+

Yehova wa majeshi ndilo jina lake.+

17 Kusanya muzigo wako kutoka chini,

Ee mwanamuke mwenye kuishi ukiwa umezungukwa kwa ajili ya vita.

18 Kwa maana Yehova anasema hivi:

“Angalia, ninatupa* inje wakaaji wa dunia wakati huu,+

Na nitawafanya wapate taabu.”

19 Ole wangu kwa sababu ya kuvunjika kwangu!+

Kidonda changu hakiwezi kupona.

Na nilisema: “Hakika huu ni ugonjwa wangu, na ninapaswa kuuvumilia.

20 Hema yangu imeharibiwa, na kamba zangu zote za mahema zimekatwa.+

Wana wangu wameniacha na hawako tena.+

Hakuna mutu yeyote mwenye kubakia wa kutandika hema yangu ao kuinua vitambaa vyangu vya mahema.

21 Kwa maana wachungaji wamejiendesha bila akili,+

Na hawakumuuliza Yehova.+

Ndiyo sababu hawakutenda kwa ufahamu,

Na makundi yao yote yametawanywa.”+

22 Sikiliza! Habari! Inakuja!

Kishindo kikubwa kutoka inchi ya kaskazini,+

Ili kufanya miji ya Yuda ikuwe ukiwa, mapango ya mbweha.+

23 Ninajua muzuri, Ee Yehova, kwamba njia ya mwanadamu haiko katika uwezo wake.

Mwanadamu mwenye kutembea hana hata uwezo wa kuongoza hatua yake.+

24 Unirekebishe, Ee Yehova, kulingana na hukumu,

Lakini hapana katika kasirani yako,+ ili usinimalize.+

25 Mwanga kasirani yako kali juu ya mataifa yenye yanakupuuza+

Na juu ya familia zenye haziitie jina lako.

Kwa maana wamemumeza Yakobo,+

Ndiyo, wamemumeza mupaka kumuharibu,+

Na wamefanya inchi yake ikuwe ukiwa.+

11 Hili ndilo neno lenye lilikuja kwa Yeremia kutoka kwa Yehova, na kusema: 2 “Musikie maneno ya agano hili, ninyi watu!

“Uyaseme* kwa watu wa Yuda na kwa wakaaji wa Yerusalemu, 3 na uwaambie, ‘Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: “Amelaaniwa mutu mwenye hatii maneno ya agano hili,+ 4 yenye niliamuru mababu zenu siku yenye niliwatosha katika inchi ya Misri,+ kutoka katika tanuru ya kuyeyushia chuma,+ nikisema, ‘Mutii sauti yangu, na mufanye mambo yote yenye ninawaamuru ninyi; na mutakuwa watu wangu na mimi nitakuwa Mungu wenu,+ 5 ili nitimize kiapo chenye niliapia mababu zenu, kuwapatia inchi yenye kutiririka maziwa na asali,+ kama vile hali iko leo.’”’”

Na nikajibu: “Amina,* Ee Yehova.”

6 Kisha Yehova akaniambia: “Tangaza maneno haya yote katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu: ‘Musikie maneno ya agano hili, na muyatimize. 7 Kwa maana nilionya kwa uzito mababu zenu siku yenye niliwatosha katika inchi ya Misri na mupaka leo, nikiwaonya tena na tena:* “Mutii sauti yangu.”+ 8 Lakini hawakusikiliza ao kutega sikio lao; tofauti na hilo, kwa kichwa-nguvu kila mumoja aliendelea kufuata moyo wake muovu.+ Basi nikaleta juu yao maneno yote ya agano hili yenye niliwaamuru wafanye na yenye walikataa kuyatimiza.’”

9 Kisha Yehova akaniambia: “Kuko ujanja kati ya watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu. 10 Wamerudilia makosa ya mababu zao wa zamani, wenye walikataa kutii maneno yangu.+ Wao pia wamefuata miungu mingine na kuitumikia.+ Nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda wamevunja agano langu lenye nilifanya pamoja na mababu zao.+ 11 Kwa hiyo Yehova anasema hivi: ‘Angalia, ninaleta juu yao musiba+ wenye hawataweza kuepuka. Wakati wataniita ili kuomba musaada, sitawasikiliza.+ 12 Kisha miji ya Yuda na wakaaji wa Yerusalemu wataenda kwa miungu yenye wanatolea zabihu* na kuomba musaada,+ lakini haitawaokoa hata kidogo wakati wa musiba wao. 13 Kwa maana miungu yako imekuwa mingi kama miji yako, Ee Yuda, na mumetengeneza mazabahu mengi kama barabara zenye kuwa katika Yerusalemu kwa ajili ya kitu cha haya,* mazabahu za kumutolea Baali zabihu.’+

14 “Na wewe,* usisali kwa ajili ya watu hawa. Usilie kwa sauti kubwa wala kutoa sala kwa ajili yao,+ kwa maana sitasikiliza wakati wataniita kwa sababu ya musiba wao.

15 Mupendwa wangu iko* na haki gani ya kuwa katika nyumba yangu

Wakati wengi wametimiza mipango ya uovu?

Je, kupitia nyama takatifu* watazuia musiba wakati utakuja juu yako?

Je, utafurahi wakati huo?

16 Wakati fulani Yehova alikuita muzeituni wenye kusitawi,

Wenye kupendeza na wenye matunda ya muzuri.

Kwa sauti ya mungurumo mukubwa, amemuwasha moto,

Na wamevunja matawi yake.

17 “Yehova wa majeshi, Mupandaji wako,+ ametangaza kwamba musiba utakuja juu yako kwa sababu ya uovu wenye ulifanywa na nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda, wenye wamenikasirisha kwa kumutolea Baali zabihu.”+

18 Yehova alinijulisha ili nijue;

Wakati huo ulinifanya nione mambo yenye walikuwa wanafanya.

19 Nilikuwa kama mwana-kondoo mutulivu mwenye kuletwa kwenye machinjo.

Sikujua kwamba walikuwa wanapanga mupango mubaya juu yangu:+

“Tuharibu muti na matunda yake,

Na tumuondoe katika inchi ya wazima,

Ili jina lake lisikumbukwe tena.”

20 Lakini Yehova wa majeshi anahukumu kwa haki;

Anachunguza mawazo ya ndani kabisa* na moyo.+

Acha nione kisasi chako juu yao,

Kwa maana nimeleta kesi yangu ya hukumu kwako.

21 Kwa hiyo Yehova anasema hivi juu ya watu wa Anatoti+ wenye wanataka kuondoa uzima wako* na wenye wanasema: “Haupaswe kutoa unabii katika jina la Yehova,+ ao utakufa kwa mukono wetu”; 22 kwa hiyo Yehova wa majeshi anasema hivi: “Angalia, nitawaomba watoe hesabu. Vijana watakufa kwa upanga,+ na watoto wao wanaume na watoto wao wanamuke watakufa kwa njaa.+ 23 Hakuna hata mabaki wenye wataachwa kati yao, kwa sababu nitaleta musiba juu ya watu wa Anatoti+ katika mwaka wao wa kuombwa hesabu.”

12 Wewe ni mwenye haki, Ee Yehova,+ wakati ninakuletea lalamiko langu,

Wakati ninasema na wewe juu ya mambo ya haki.

Lakini sababu gani njia ya waovu imefanikiwa,+

Na sababu gani wadanganyifu hawana wasiwasi?

 2 Uliwapanda, na wametia mizizi.

Wamekomaa na kuzaa matunda.

Wewe uko kwenye midomo yao, lakini mbali na mawazo yao ya ndani kabisa.*+

 3 Lakini unanijua muzuri, Ee Yehova,+ unaniona;

Umechunguza moyo wangu na kuupata ukiwa katika umoja na wewe.+

Uwaweke peke yao kama kondoo wa kuchinjwa,

Na uwatie pembeni kwa ajili ya siku ya kuuawa.

 4 Inchi itaendelea kukauka mupaka wakati gani

Na majani ya kila eneo la mashamba kukauka?+

Kwa sababu ya uovu wa wale wenye kukaa ndani yake,

Wanyama na ndege wamefagiliwa mbali.

Kwa maana wamesema: “Haone kile chenye kitatupata.”

 5 Kama unachoka kwa kukimbia pamoja na watu wenye kuenda kwa miguu,

Namna gani unaweza kushindana mbio na farasi?+

Hata kama uko na uhakika katika inchi ya amani,

Itakuwa namna gani kwako kati ya miti mingi midogo-midogo* pembeni ya Yordani?

 6 Kwa maana hata ndugu zako mwenyewe, nyumba ya baba yako mwenyewe,

Wamekutendea kwa udanganyifu.+

Wamekulalamikia wakiita ubaya juu yako.

Usiwaamini,

Hata kama wanakuambia mambo ya muzuri.

 7 “Nimeacha nyumba yangu;+ nimeacha uriti wangu.+

Nimetia mupendwa wangu* katika mukono wa maadui wake.+

 8 Uriti wangu umekuwa kwangu kama simba katika pori.

Ameningurumia.

Basi nimemuchukia.

 9 Uriti wangu ni kama ndege mwenye kuwinda, mwenye rangi nyingi;*

Ndege wengine wenye kuwinda wanamuzunguka na kumushambulia.+

Mukuje, mukusanyike pamoja, ninyi wote wanyama wa pori,

Mukuje mukule.+

10 Wachungaji wengi wameharibu shamba langu la mizabibu;+

Wamekanyanga fungu langu la udongo.+

Wamegeuza fungu langu la udongo lenye kutamanika kuwa jangwa lenye limeachwa ukiwa.

11 Limekuwa eneo lenye limeachwa;

Limekauka;*

Liko ukiwa mbele yangu.+

Inchi yote imeachwa ukiwa,

Lakini hakuna mutu mwenye kutia jambo hilo katika moyo.+

12 Wenye kuharibu wamekuja kwenye njia zote za kidogo-kidogo zenye zimekanyangwa sana,

Kwa maana upanga wa Yehova unameza kuanzia mwisho mumoja wa inchi mupaka mwisho mwingine.+

Hakuna amani kwa mutu yeyote.*

13 Wamepanda ngano, lakini wamevuna miiba.+

Wamejichokesha, lakini bila faida yoyote.

Watasikia haya kwa sababu ya mazao yao

Kwa sababu ya kasirani ya Yehova yenye kuwaka.”

14 Yehova anasema hivi juu ya majirani wangu wote waovu, wenye wanagusa uriti wenye nilifanya watu wangu Israeli wakuwe nao:+ “Angalia, ninawangoa kutoka kwenye inchi yao,+ na nitangoa nyumba ya Yuda kutoka kati yao. 15 Lakini kisha kuwangoa, nitawaonyesha tena rehema na kurudisha kila mumoja wao kwenye uriti wake na kwenye udongo wake.”

16 “Na kama kwa hakika wanajifunza njia za watu wangu na kuapa kwa jina langu, ‘Kama vile hakika Yehova anaishi!’ kama vile walifundisha watu wangu kuapa kwa jina la Baali, basi watajengwa kati ya watu wangu. 17 Lakini kama wanakataa kutii, mimi pia nitangoa taifa hilo, nitalingoa na kuliharibu,” ni vile Yehova anasema.+

13 Yehova aliniambia hivi: “Uende na ujinunulie mukaba* wa kitani na uuvae kuzunguka kiuno chako, lakini usiutie ndani ya maji.” 2 Basi nikanunua mukaba* kulingana na neno la Yehova na nikauvaa kuzunguka kiuno changu. 3 Na neno la Yehova likakuja kwangu mara ya pili: 4 “Kamata mukaba* wenye ulinunua na wenye umevaa na usimame, uende kwenye Efrati, na uufiche pale katika mupasuko wa mwamba.” 5 Basi nikaenda na nikauficha pembeni ya Efrati, kama vile Yehova alikuwa ameniamuru.

6 Lakini kisha siku nyingi Yehova akaniambia: “Simama, uende kwenye Efrati, na ukamate kutoka kule ule mukaba* wenye nilikuamuru uufiche kule.” 7 Basi nikaenda kwenye Efrati na nikachimba na kukamata ule mukaba* kutoka mahali kwenye nilikuwa nimeuficha, na nikaona kwamba mukaba* huo ulikuwa umeharibika; haukukuwa na mafaa kabisa.

8 Kisha neno la Yehova likakuja kwangu: 9 “Yehova anasema hivi: ‘Kwa njia ileile nitaharibu kiburi cha Yuda na kiburi kingi cha Yerusalemu.+ 10 Watu hawa waovu wenye wanakataa kutii maneno yangu,+ wenye kwa kichwa-nguvu wanafuata moyo wao wenyewe,+ na wenye wanafuata miungu mingine, wakiitumikia na kuiinamia, watakuwa tu kama mukaba* huu wenye hauna mafaa kabisa.’ 11 ‘Kwa maana kama vile mukaba* unashikamana na kiuno cha mutu, ni vile nilifanya nyumba yote ya Israeli na nyumba yote ya Yuda washikamane na mimi,’ ni vile Yehova anasema, ‘ili wakuwe kwangu watu,+ jina,+ sifa, na kitu kizuri. Lakini hawakutii.’+

12 “Na unapaswa pia kuwapatia ujumbe huu, ‘Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: “Kila mutungi mukubwa unapaswa kujazwa divai.”’ Na watakujibu, ‘Je, tayari hatujue kwamba kila mutungi mukubwa unapaswa kujazwa divai?’ 13 Kisha uwaambie, ‘Yehova anasema hivi: “Angalia, ninajaza ulevi wakaaji wote wa inchi hii,+ wafalme wenye kukaa kwenye kiti cha ufalme cha Daudi, makuhani na manabii, na wakaaji wote wa Yerusalemu. 14 Na nitawagonganisha mumoja na mwenzake, baba na wana pia,” ni vile Yehova anasema.+ “Sitawaonea huruma wala kuwa na huzuni wala kuwaonyesha rehema yoyote; hakuna kitu chenye kitanizuia kuwaharibu.”’+

15 Musikie na mukaze uangalifu.

Musikuwe na majivuno, kwa maana Yehova amesema.

16 Mumupatie Yehova Mungu wenu utukufu

Mbele alete giza

Na mbele ya miguu yenu kujikwaa kwenye milima mangaribi.

Mutatumaini kupata mwangaza,

Lakini ataleta kivuli kizito;

Ataugeuza kuwa giza nzito.+

17 Na kama munakataa kusikiliza,

Nitalia* kwa uficho kwa sababu ya kiburi chenu.

Nitatoa machozi mengi, na macho yangu yatatiririka machozi,+

Kwa sababu kundi la Yehova+ limekamatwa na kupelekwa mateka.

18 Mumuambie mufalme na malkia mama ya mufalme,*+ ‘Mukae mahali pa chini,

Kwa maana taji lenu lenye kupendeza litaanguka kutoka kwenye vichwa vyenu.’

19 Miji ya kusini imefungwa,* na hakuna mutu wa kuifungua.

Yuda yote imepelekwa katika uhamisho, imepelekwa katika uhamisho kabisa.+

20 Inua macho yako uone wale wenye wanakuja kutoka kaskazini.+

Liko wapi kundi lenye ulipewa, kondoo wako wenye kupendeza?+

21 Utasema nini wakati azabu yako itafika

Kutoka kwa marafiki wako wa karibu wenye ulifundisha tangu mwanzo?+

Je, maumivu ya kuzaa hayatakushika, kama ya mwanamuke mwenye kuzaa?+

22 Na wakati unasema katika moyo wako, ‘Sababu gani mambo haya yamenipata?’+

Ni kwa sababu ya kosa lako kubwa ndiyo maana umevuliwa pindo zako+

Na visigino vyako vimetendewa kwa jeuri.

23 Je, Mukushi* anaweza kubadilisha ngozi yake, ao chui madoa yake?+

Kama ni vile, basi munaweza kufanya mema,

Ninyi wenye mulizoezwa kufanya mabaya.

24 Basi nitawatawanya kama nyasi zenye kupeperushwa na upepo wa jangwa.+

25 Hii ndiyo kura yako, fungu lenye nimekupimia,” ni vile Yehova anasema,

“Kwa sababu umenisahau+ na unategemea uongo.+

26 Kwa hiyo, nitainua pindo zako juu ya uso wako,

Na haya yako itaonekana,+

27 Matendo yako ya uzinifu+ na milio yako ya tamaa kubwa ya ngono,

Ukahaba wako wenye kupotoka.*

Juu ya vilima, katika eneo la mashamba,

Nimeona mwenendo wako wenye kuchukiza.+

Ole wako, Ee Yerusalemu!

Utaendelea kuwa muchafu mupaka wakati gani?”+

14 Hili ndilo neno la Yehova lenye lilikuja kwa Yeremia kuhusiana na ukame:+

 2 Yuda inaomboleza,+ na milango yake mikubwa imefifia.

Inazama katika udongo kwa sababu ya huzuni,

Na kilio kinapanda kutoka Yerusalemu.

 3 Na mabwana wao wanatuma watumishi wao* walete maji.

Wanaenda kwenye mashimo ya maji* lakini hawapate maji.

Wanarudia vyombo vyao vikiwa wazi.

Wamepata haya na kukata tamaa,

Na wanafunika vichwa vyao.

 4 Kwa sababu udongo umepasuka,

Kwa maana hakuna mvua juu ya inchi,+

Walimaji wamekuwa na woga na wanafunika vichwa vyao.

 5 Hata paa mwenye kuwa katika eneo la mashamba anaacha mutoto wake mwenye ametoka kuzaliwa

Kwa sababu hakuna majani.

 6 Punda wa pori wanasimama kwenye vilima vyenye kuwa wazi.

Wanavutavuta upepo kama mbweha;

Macho yao yamechoka kwa sababu hakuna majani.+

 7 Hata kama makosa yetu wenyewe yanashuhudia juu yetu,

Ee Yehova, tenda kwa ajili ya jina lako.+

Kwa maana matendo yetu ya kukosa uaminifu ni mengi,+

Na ni wewe ndiye tumetendea zambi.

 8 Ee tumaini la Israeli, Mwokozi wake+ nyakati za taabu,

Sababu gani uko kama mugeni katika inchi,

Kama musafiri mwenye anakaa ili kupitisha tu usiku?

 9 Sababu gani uko kama mutu mwenye kushangaa,

Kama mutu mwenye nguvu mwenye hawezi kuokoa?

Kwa maana uko kati yetu, Ee Yehova,+

Na jina lako limeitwa juu yetu.+

Usituache.

10 Yehova anasema hivi juu ya watu hawa: “Wanapenda kutanga-tanga;+ hawakuzuia miguu yao.+ Basi Yehova hapendezwe nao.+ Sasa atakumbuka kosa lao, na atawaomba watoe hesabu kwa sababu ya zambi zao.”+

11 Kisha Yehova akaniambia: “Usisali ili mema ikuje juu ya watu hawa.+ 12 Wakati wanafunga, sisikilize maombi yao,+ na wakati wanatoa matoleo mazima ya kuteketezwa na matoleo ya nafaka, siyafurahie,+ kwa maana nitawaharibu kwa upanga, kwa njaa, na kwa ugonjwa wa kuambukiza.”+

13 Halafu nikasema: “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova! Angalia, manabii wanawaambia, ‘Hamutaona upanga, na njaa haitakuja juu yenu, lakini nitawapatia amani ya kweli mahali hapa.’”+

14 Kisha Yehova akaniambia: “Manabii wanatoa unabii wa uongo katika jina langu.+ Sikuwatuma wala kuwaamuru wala kusema nao.+ Maono ya uongo na uaguzi wenye hauna mafaa yoyote na udanganyifu wa moyo wao wenyewe ndio unabii wenye wanawatolea ninyi.+ 15 Kwa hiyo Yehova anasema hivi juu ya manabii wenye wanatoa unabii katika jina langu, hata kama sikuwatuma, na wenye wanasema kwamba hakuna upanga ao njaa yenye itakuja katika inchi hii: ‘Manabii hao watakufa kwa upanga na kwa njaa.+ 16 Na watu wenye manabii hao wanatolea unabii watatupwa katika barabara za Yerusalemu kwa sababu ya njaa na upanga, bila mutu yeyote wa kuwazika+⁠—​wao, bibi zao, watoto wao wanaume, wala watoto wao wanamuke⁠—​kwa maana nitamwanga juu yao musiba wenye wanastahili.’+

17 “Unapaswa kuwaambia neno hili:

‘Macho yangu yatiririke machozi usiku na muchana, yasiishe,+

Kwa maana binti bikira ya watu wangu amepondwa kabisa na kuvunjwa,+

Kwa kidonda kibaya sana.

18 Kama ninaenda katika eneo la mashamba na kuangalia,

Ninaona wale wenye waliuawa kwa upanga!+

Na kama ninakuja katika muji,

Ninaona magonjwa yenye yaliletwa na njaa!+

Kwa maana nabii na kuhani wamezunguka katika inchi yenye hawajue.’”+

19 Je, umekataa kabisa Yuda, ao, je, umechukia* Sayuni?+

Sababu gani umetupiga, na hivyo hakuna uponyeshaji kwa ajili yetu?+

Kulikuwa tumaini la kupata amani, lakini hakuna mema yenye yalikuja,

Tumaini la kupata kipindi cha kupona, lakini kuko woga!+

20 Tunakubali uovu wetu, Ee Yehova,

Na kosa la mababu zetu,

Kwa maana tumekutendea zambi.+

21 Kwa ajili ya jina lako, usitukatae;+

Usizarau kiti chako cha ufalme chenye utukufu.

Kumbuka, na usivunje agano lako pamoja na sisi.+

22 Kati ya sanamu zenye hazina mafaa yoyote za mataifa, je, kuko sanamu yenye inaweza kuleta mvua,

Ao, je, hata mbingu zinaweza kutuma matone ya mvua kwa kupenda zenyewe?

Je, haiko Wewe tu, Ee Yehova Mungu wetu?+

Na sisi tunakutumaini wewe,

Kwa maana wewe peke yako ndiye ulifanya mambo hayo yote.

15 Kisha Yehova akaniambia: “Hata kama Musa na Samweli wangekuwa wamesimama mbele yangu,+ singeonyesha watu hawa rehema.* Uwafukuze kutoka mbele yangu. Uwaache waende. 2 Na kama wanakuambia, ‘Tuende wapi?’ unapaswa kuwaambia, ‘Yehova anasema hivi:

“Kila mutu mwenye alikusudiwa pigo lenye kuua, aende kwenye pigo lenye kuua!

Kila mutu mwenye alikusudiwa upanga, aende kwenye upanga!+

Kila mutu mwenye alikusudiwa njaa, aende kwenye njaa!

Na kila mutu mwenye alikusudiwa kuenda katika utekwa, aende katika utekwa!”’+

3 “‘Na nitaweka juu yao misiba ine (4),’*+ ni vile Yehova anasema, ‘upanga ili kuua, imbwa ili kukokota, na ndege wa mbinguni na wanyama wa dunia ili kupasua vipande-vipande na kuharibu.+ 4 Na nitawafanya kuwa kitu cha kuogopesha kwa falme zote za dunia+ kwa sababu ya Manase mwana wa Hezekia, mufalme wa Yuda, kwa sababu ya mambo yenye alifanya katika Yerusalemu.+

 5 Ni nani mwenye atakusikilia huruma, Ee Yerusalemu,

Ni nani mwenye atakusikitikia,

Na ni nani mwenye atasimama ili kuuliza juu ya hali yako?’

 6 ‘Umeniacha,’ ni vile Yehova anasema.+

‘Unaendelea kunigeuzia mugongo wako.*+

Basi nitanyoosha mukono wangu juu yako na kukuangamiza.+

Nimechoka kukusikilia huruma.*

 7 Na nitawapepua kwa kanya* katika milango mikubwa ya inchi.

Nitaua watoto wao.+

Nitaharibu watu wangu,

Kwa kuwa wanakataa kugeuka na kuacha njia zao.+

 8 Wajane wao watakuwa wengi mbele yangu kuliko muchanga wa bahari.

Nitaleta mwenye kuharibu juu yao katikati ya muchana, juu ya mama na vijana.

Nitaleta wasiwasi na woga juu yao kwa kushitukia.

 9 Mwanamuke mwenye alizaa watoto saba (7) amekuwa muzaifu sana;

Anapumua* kwa shida.

Jua lake limeshuka wakati ingali muchana,

Na kutokeza haya na fezeha.’*

‘Na watu kidogo wenye kubakia kati yao

Nitawatoa kwa upanga mbele ya maadui wao,’ ni vile Yehova anasema.”+

10 Ole wangu, Ee mama yangu, kwa sababu ulinizaa,+

Mutu mwenye ugomvi na mwenye muzozo na inchi yote.

Sikutoa mukopo ao sikuomba mukopo;

Lakini wote wananilaani.

11 Yehova alisema: “Hakika nitakutumikia upate mema;

Hakika nitakutetea wakati wa musiba,

Wakati wa taabu juu ya adui.

12 Je, mutu yeyote anaweza kuvunja chuma vipande-vipande,

Chuma kutoka kaskazini, na shaba?

13 Nitatoa mali yako na hazina zako ili vinyanganywe,+

Hapana kwa malipo, lakini kwa sababu ya zambi zako zote kila mahali katika maeneo yako yote.

14 Nitavipatia maadui wako

Wavipeleke katika inchi yenye haujue.+

Kwa maana moto umewashwa kwa kasirani yangu,

Na unawaka juu yenu.”+

15 Wewe unajua, Ee Yehova,

Unikumbuke na unikazie uangalifu.

Unilipizie kisasi juu ya wale wenye kunitesa.+

Usiache niangamie* kwa sababu haukasirike haraka.

Ujue kwamba ninabeba haya hii kwa sababu yako.+

16 Maneno yako yalipatikana, na nikayakula;+

Na neno lako likakuwa kwangu furaha na shangwe ya moyo wangu,

Kwa maana jina lako limeitwa juu yangu, Ee Yehova Mungu wa majeshi.

17 Mimi sikae pamoja na watu wenye wanapenda kufurahi na kushangilia.+

Kwa sababu mukono wako uko juu yangu, ninakaa peke yangu,

Kwa maana umenijaza kasirani kali.*+

18 Sababu gani maumivu yangu ni ya kudumu na kidonda changu hakipone?

Kinakataa kupona.

Je, wewe utakuwa kwangu kama chanzo cha maji cha udanganyifu

Chenye hakiwezi kutegemeka?

19 Kwa hiyo Yehova anasema hivi:

“Kama unarudia, basi nitakurudisha kwangu,

Na wewe utasimama mbele yangu.

Kama unatenganisha kitu chenye samani kutoka kwa kitu chenye hakina mafaa yoyote,

Utakuwa kama kinywa changu mwenyewe.*

Watalazimika kuja kwako,

Lakini wewe hautaenda kwao.”

20 “Ninakufanya kuwa ukuta wa shaba wenye ngome kwa watu hawa.+

Hakika watapigana na wewe,

Lakini hawatakushinda,+

Kwa maana mimi niko pamoja na wewe, ili kukuokoa na kukukomboa,” ni vile Yehova anasema.

21 “Na nitakukomboa kutoka katika mukono wa watu waovu

Na kukukomboa kutoka katika mukono wa watu wenye hawana huruma.”

16 Neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 2 “Haupaswe kujichukulia bibi, na haupaswe kuwa na watoto wanaume na watoto wanamuke mahali hapa. 3 Kwa maana Yehova anasema hivi juu ya watoto wanaume na watoto wanamuke wenye wanazaliwa hapa na juu ya mama zao wenye wanawazaa na juu ya baba zao wenye wanawazaa katika inchi hii: 4 ‘Watakufa kwa magonjwa yenye kuua,+ lakini hakuna mwenye atawaombolezea wala kuwazika; watakuwa kama mbolea juu ya uso wa inchi.+ Watakufa kwa upanga na kwa njaa,+ na maiti zao zitakuwa chakula kwa ndege wa mbinguni na kwa wanyama wa dunia.’

 5 Kwa maana Yehova anasema hivi:

‘Usiingie katika nyumba yenye ndani yake munafanyika karamu ya waombolezaji,

Na usiende kuomboleza wala kutoa pole,’+

‘Kwa maana nimeondoa amani yangu kwa watu hawa,’ ni vile Yehova anasema,

‘Pamoja na upendo wangu mushikamanifu na rehema.+

 6 Wakubwa na wadogo pia watakufa katika inchi hii.

Hawatazikwa,

Hakuna mutu mwenye atawaombolezea,

Ao mutu yeyote mwenye atajikata-kata wala kujitia upara kwa ajili yao.*

 7 Na hakuna mutu mwenye atapatia chakula wale wenye kuwa katika maombolezo,

Ili kuwafariji juu ya mutu wao mwenye alikufa;

Na hakuna mutu yeyote mwenye atawapatia kikombe cha faraja

Ili kunywa kwa sababu ya kupoteza baba yao ao mama yao.

 8 Na usiingie katika nyumba ya karamu

Ili kukaa pamoja nao ili kula na kunywa.’

9 “Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Angalia, katika mahali hapa, katika siku zenu na mbele ya macho yenu, nitamaliza sauti za furaha na shangwe, sauti ya bwana-arusi na sauti ya bibi-arusi.’+

10 “Wakati utaambia watu hawa maneno haya yote, watakuuliza, ‘Sababu gani Yehova amesema kuhusu musiba wote huu mukubwa juu yetu? Ni kosa gani na zambi gani tumemutendea Yehova Mungu wetu?’+ 11 Unapaswa kuwajibu, ‘“Kwa sababu mababu zenu waliniacha,”+ ni vile Yehova anasema, “na waliendelea kufuata miungu mingine na kuitumikia na kuiinamia.+ Lakini waliniacha, na sheria yangu hawakuishika.+ 12 Na mumejiendesha mubaya zaidi kuliko mababu zenu,+ na kila mumoja wenu anafuata ugumu wa moyo wake muovu kuliko kunitii.+ 13 Basi nitawatupa ninyi inje ya inchi hii katika inchi yenye ninyi wala mababu zenu hamukujua,+ na kule mutatumikia miungu mingine muchana na usiku,+ kwa sababu sitawaonyesha wema wowote.”’

14 “‘Hata hivyo, siku zinakuja,’ ni vile Yehova anasema, ‘wakati hawatasema tena: “Kama vile hakika Yehova anaishi, mwenye alitosha watu wa Israeli katika inchi ya Misri!”+ 15 lakini tofauti na hilo: “Kama vile hakika Yehova anaishi, mwenye alitosha watu wa Israeli katika inchi ya kaskazini na katika inchi zote kwenye alikuwa amewatawanya!” na nitawarudisha kwenye inchi yao, yenye nilipatia mababu zao.’+

16 ‘Angalia, ninaita wavuvi wengi wa samaki,’ ni vile Yehova anasema,

‘Na watawavua.

Kisha, nitaita wawindaji wengi,

Na watawawinda kwenye kila mulima na kila kilima

Na kutoka katika mipasuko ya miamba.

17 Kwa maana macho yangu yako juu ya kila kitu chenye wanafanya.*

Hawakufichwa kutoka mbele yangu,

Wala kosa lao halikufichwa kutoka mbele ya macho yangu.

18 Kwanza, nitalipa kiasi kamili chenye kustahili kosa lao na zambi yao,+

Kwa maana wamechafua inchi yangu kwa mifano yenye haina uzima ya* sanamu zao zenye kuchukiza

Na wamejaza uriti wangu mambo yao yenye kuchukiza.’”+

19 Ee Yehova, nguvu zangu na ngome yangu,

Mahali pangu pa kukimbilia katika siku ya taabu,+

Kwako mataifa yatakuja kutoka kwenye miisho ya dunia,

Na watasema: “Mababu zetu waliriti uongo kabisa,

Mambo ya bure kabisa* na vitu vyenye havina mafaa, vyenye havina faida yoyote.”+

20 Je, mwanadamu anaweza kujitengenezea miungu

Wakati kwa kweli hiyo haiko miungu?+

21 “Basi nitawafanya wajue;

Wakati huu nitawafanya wajue nguvu zangu na uwezo wangu,

Na watajua kwamba jina langu ni Yehova.”

17 “Zambi ya Yuda imeandikwa kwa kalamu ya chuma.

Imechongwa kwa chongo ya almasi juu ya bamba la moyo wao

Na juu ya pembe za mazabahu zao,

 2 Wakati wana wao wanakumbuka mazabahu zao na miti yao mitakatifu*+

Pembeni ya muti wenye majani mengi, juu ya vilima virefu,+

 3 Juu ya milima katika eneo lenye kuwa wazi la mashamba.

Mali yako, hazina zako zote, nitazitoa ili zinyanganywe+

⁠—​Ndiyo, mahali pako pa juu kwa sababu ya zambi kila mahali katika maeneo yako.+

 4 Utaacha, kwa kupenda kwako mwenyewe, uriti wako wenye nilikupatia.+

Na nitakufanya utumikie maadui wako katika inchi yenye haujue,+

Kwa maana umewasha kasirani yangu kama moto.*+

Itawaka kwa wakati wote.”

 5 Yehova anasema hivi:

“Amelaaniwa mutu* mwenye anategemea wanadamu bure,+

Mwenye anategemea nguvu za mwanadamu,*+

Na mwenye moyo wake unageuka na kumuacha Yehova.

 6 Atakuwa kama muti wenye kuwa peke yake katika jangwa.

Hataona wakati mema yanakuja,

Lakini atakaa mahali kwenye kunakauka katika jangwa,

Katika inchi yenye chumvi yenye hakuna mutu mwenye anaweza kuishi ndani.

 7 Amebarikiwa mutu* mwenye anaweka tegemeo lake katika Yehova,

Mwenye uhakika wake uko katika Yehova.+

 8 Atakuwa kama muti wenye ulipandwa pembeni ya maji,

Wenye unapeleka mizizi yake kwenye muto mudogo.

Hatatambua wakati joto linakuja,

Lakini majani yake yatakuwa mengi sikuzote.+

Na katika mwaka wa ukame hatahangaika,

Wala hataacha kuzaa matunda.

 9 Moyo ni mudanganyifu kuliko kitu kingine chochote na uko hatari.*+

Ni nani anaweza kuujua?

10 Mimi, Yehova, ninachunguza moyo,+

Ninachunguza mawazo ya ndani kabisa,*

Ili kumupatia kila mumoja kulingana na njia zake,

Kulingana na matunda ya matendo yake.+

11 Kama kwale mwenye anakusanya kile chenye hakutaga

Ni vile mutu mwenye anapata utajiri kwa udanganyifu.*+

Huo utamuacha katikati ya maisha,

Na mwishowe ataonekana kuwa hana akili.”

12 Kiti cha ufalme chenye utukufu, chenye kiliinuliwa tangu mwanzo,

Ndipo mahali pa patakatifu petu.+

13 Ee Yehova, tumaini la Israeli,

Wale wote wenye wanakuacha watapatishwa haya.

Wale wenye wanakuasi* wataandikwa katika mavumbi,+

Kwa sababu wamemuacha Yehova, chanzo cha maji ya uzima.+

14 Uniponyeshe, Ee Yehova, na nitapona.

Uniokoe, na nitaokoka,+

Kwa maana wewe ndiye ninasifu.

15 Angalia! Kuko wale wenye wananiambia:

“Neno la Yehova liko wapi?+

Likuje, tafazali!”

16 Lakini mimi, sikukimbia na kuacha kukufuata kama muchungaji,

Wala sikutamani siku ya musiba.

Unajua muzuri mambo yote yenye midomo yangu imesema;

Yote yalitendeka mbele ya uso wako!

17 Usikuwe kwangu kitu cha kuogopesha.

Wewe ni kimbilio langu katika siku ya musiba.

18 Uache wale wenye wananitesa wapatishwe haya,+

Lakini usiache mimi nipatishwe haya.

Uwaache waingiwe na woga,

Lakini usiache mimi niingiwe na woga.

Ulete siku ya musiba juu yao,+

Na uwaponde na kuwaharibu kabisa.*

19 Yehova aliniambia hivi: “Uende na usimame katika mulango mukubwa wa wana wa watu; mulango mukubwa wenye wafalme wa Yuda wanaingilia na kutokea, na katika milango yote mikubwa ya Yerusalemu.+ 20 Unapaswa kuwaambia, ‘Musikie neno la Yehova, ninyi wafalme wa Yuda, watu wote wa Yuda, na wakaaji wote wa Yerusalemu, wenye kuingia kupitia milango hii mikubwa. 21 Yehova anasema hivi: “Mukuwe waangalifu juu yenu wenyewe,* na musibebe muzigo wowote katika siku ya Sabato ao kuuingiza kupitia milango mikubwa ya Yerusalemu.+ 22 Hamupaswe kutosha muzigo wowote katika nyumba zenu katika siku ya Sabato; na hamupaswe kufanya kazi yoyote.+ Mutakase siku ya Sabato, kama vile niliamuru mababu zenu.+ 23 Lakini hawakusikiliza wala kutega sikio lao, na kwa kichwa-nguvu wakakataa* kutii wala kukubali nizamu.”’+

24 “‘“Hata hivyo, kama munanitii kabisa,” ni vile Yehova anasema, “na hamuingize muzigo wowote kupitia milango mikubwa ya muji huu katika siku ya Sabato, na munatakasa siku ya Sabato kwa kukosa kufanya kazi yoyote katika siku hiyo,+ 25 basi wafalme na wakubwa wenye wanakaa kwenye kiti cha ufalme cha Daudi+ wataingia pia kupitia milango mikubwa ya muji huu, wakipanda gari na farasi, wao pamoja na wakubwa wao, watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu;+ na muji huu utaikaliwa sikuzote. 26 Na watu watakuja kutoka katika miji ya Yuda, kutoka maeneo yenye kuzunguka Yerusalemu, kutoka katika inchi ya Benyamini,+ kutoka katika inchi tambarare ya chini,+ kutoka eneo lenye milima, na kutoka Negebu,* wakileta matoleo mazima ya kuteketezwa,+ zabihu,+ matoleo ya nafaka,+ ubani, na zabihu za shukrani ndani ya nyumba ya Yehova.+

27 “‘“Lakini kama hamunitii kwa kutakasa siku ya Sabato na kukosa kubeba mizigo na kuileta kupitia milango mikubwa ya Yerusalemu katika siku ya Sabato, nitawasha moto milango yake mikubwa, na hakika moto huo utateketeza minara yenye ngome ya Yerusalemu+ na hautazimishwa.”’”+

18 Hili ndilo neno lenye lilikuja kwa Yeremia kutoka kwa Yehova: 2 “Simama na ushuke mupaka kwenye nyumba ya mufinyanzi,*+ na pale nitakufanya usikie maneno yangu.”

3 Basi nikashuka mupaka kwenye nyumba ya mufinyanzi,* na alikuwa anafanya kazi kwenye magurudumu* ya mufinyanzi. 4 Lakini chombo chenye mufinyanzi* alikuwa anatengeneza kwa udongo kikaharibika katika mukono wake. Basi mufinyanzi akakitengeneza upya kuwa chombo kingine, kama vile aliona inafaa.*

5 Kisha neno la Yehova likakuja kwangu, na kusema: 6 “‘Je, siwezi kuwatendea ninyi kama vile mufinyanzi* huyu alitenda, Ee nyumba ya Israeli?’ ni vile Yehova anasema. ‘Muangalie! Kama udongo katika mukono wa mufinyanzi, ni vile ninyi muko katika mukono wangu, Ee nyumba ya Israeli.+ 7 Wakati wowote nikisema juu ya kungoa na kubomoa na kuharibu taifa ao ufalme,+ 8 na taifa hilo liache uovu wake wenye nilisema juu yake, mimi pia nitabadilisha mawazo yangu* juu ya musiba wenye nilikusudia kuleta juu yake.+ 9 Lakini wakati wowote nikisema juu ya kujenga na kupanda taifa ao ufalme, 10 na linafanya mambo ya mubaya mbele ya macho yangu na halitii sauti yangu, nitabadilisha mawazo yangu* juu ya mema yenye nilikusudia kulitendea.’

11 “Sasa, tafazali, ambia watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu, ‘Yehova anasema hivi: “Angalia, ninatayarisha* musiba na kufanya mupango mubaya juu yenu. Mugeuke, tafazali, kutoka kwenye njia zenu za mubaya, na murekebishe njia zenu na mazoea yenu.”’”+

12 Lakini wakasema: “Hakuna tumaini!+ Kwa maana tutafuata mawazo yetu wenyewe, na kila mumoja wetu atatenda kulingana na ugumu wa moyo wake muovu.”+

13 Kwa hiyo Yehova anasema hivi:

“Muulize ninyi wenyewe, tafazali, kati ya mataifa.

Ni nani amesikia jambo kama hili?

Bikira wa Israeli amefanya jambo lenye kuchukiza sana.+

14 Je, teluji* ya Lebanoni inapotea kutoka kwenye miamba yenye kuwa kwenye miteremuko yake?

Ao, je, maji baridi yenye kutiririka kutoka mbali yatakauka?

15 Lakini watu wangu wamenisahau.+

Kwa maana wanatoa zabihu kwa* kitu chenye hakina mafaa yoyote,+

Na wanafanya watu wajikwae katika njia zao, njia za zamani,+

Ili wapite kwenye barabara za kidogo-kidogo zenye haziko laini na zenye hazinyooke,*

16 Ili kufanya inchi yao kuwa kitu cha kuogopesha+

Na kitu cha kupigiwa muluzi milele.+

Kila mutu mwenye anapita pembeni yake ataangalia kwa mushangao na kutikisa kichwa chake.+

17 Kama upepo wa mashariki, nitawatawanya mbele ya adui.

Nitawaonyesha mugongo wangu, hapana uso wangu, katika siku ya musiba wao.”+

18 Na wakasema: “Mukuje, tufanye mupango mubaya juu ya Yeremia,+ kwa maana sheria haitaangamia* kutoka kwa makuhani wetu ao shauri kutoka kwa watu wenye hekima ao neno kutoka kwa manabii. Mukuje tuseme juu yake,* na tusisikilize mambo yenye anasema.”

19 Unitegee sikio, Ee Yehova,

Na usikilize mambo yenye wapinzani wangu wanasema.

20 Je, wema unapaswa kulipwa kwa ubaya?

Kwa maana wamechimbia uzima wangu* shimo.+

Kumbuka namna nilisimama mbele yako ili kusema mambo ya muzuri juu yao,

Ili kugeuza kasirani yako kali kutoka kwao.

21 Basi toa wana wao wapate njaa,

Na uwatoe kwenye nguvu za upanga.+

Bibi zao wafiwe na watoto na kuwa wajane.+

Wanaume wao wauawe kwa pigo lenye kuua,

Vijana wao wapigwe na kuuawa kwa upanga katika pigano.+

22 Kilio kisikike kutoka kwenye nyumba zao

Wakati utaleta juu yao wanyanganyi kwa kushitukia.

Kwa maana wamechimba shimo ili kunikamata

Na wameweka mitego kwa ajili ya miguu yangu.+

23 Lakini wewe, Ee Yehova,

Unajua muzuri mipango yao yote juu yangu ili waniue.+

Usifunike kosa lao,

Na usifute zambi yao kutoka mbele yako.

Uwaache wakwazike mbele yako+

Wakati utakamata hatua juu yao katika kasirani yako.+

19 Yehova amesema hivi: “Uende na ununue chupa ya udongo kwa mufinyanzi.*+ Uchukue wazee fulani wa watu na wazee fulani wa makuhani, 2 na uende kwenye Bonde la Mwana wa Hinomu,+ kwenye muingilio wa Mulango Mukubwa wa Vigae. Na pale utangaze maneno yenye ninakuambia. 3 Utasema, ‘Musikie neno la Yehova, ninyi wafalme wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu. Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi:

“‘“Niko karibu kuleta musiba mahali hapa, na masikio ya mutu yeyote mwenye kusikia kuhusu musiba huo yatawasha. 4 Ni kwa sababu waliniacha mimi+ na walifanya mahali hapa pasitambuliwe.+ Mule wanatoa zabihu kwa miungu mingine, yenye wao na mababu zao na wafalme wa Yuda hawakukuwa wamejua, na wamejaza mahali hapa damu ya wenye hawana hatia.+ 5 Walijenga mahali pa juu pa Baali ili kuteketeza wana wao katika moto kama matoleo mazima ya kuteketezwa kwa Baali,+ jambo lenye sikukuwa nimeamuru wala kuzungumuzia na lenye halijaingia katika moyo wangu hata kidogo.”’*+

6 “‘“Kwa hiyo angalia! siku zinakuja,” ni vile Yehova anasema, “wakati mahali hapa hapataitwa tena Tofeti ao Bonde la Mwana wa Hinomu lakini Bonde la Mauaji.+ 7 Nitavunja mipango ya Yuda na Yerusalemu mahali hapa, na nitawaangusha kwa upanga mbele ya maadui wao na kwa mukono wa wale wenye wanatafuta kuchukua uzima wao.* Na maiti zao nitazitoa zikuwe chakula kwa ndege wa mbinguni na kwa wanyama wa dunia.+ 8 Na nitafanya muji huu kuwa kitu cha kuogopesha na kitu cha kupigiwa muluzi. Kila mutu mwenye kupita pembeni yake ataangalia kwa mushangao na kupiga muluzi kwa sababu ya mapigo yake yote.+ 9 Na nitawafanya wakule nyama ya watoto wao wanaume na watoto wao wanamuke, na watakula kila mumoja nyama ya mwenzake, kwa sababu ya kuzungukwa kwa ajili ya vita na kwa sababu ya kukata kwao tamaa wakati watafinywa na maadui wao na wale wenye wanatafuta kuondoa uzima wao.”’*+

10 “Kisha uvunje ile chupa mbele ya macho ya wanaume wenye wanaenda pamoja na wewe, 11 na uwaambie, ‘Yehova wa majeshi anasema hivi: “Ni vile nitavunja watu hawa na muji huu, kama mutu mwenye anavunja chombo cha mufinyanzi* na hivyo hakiwezi kutengenezwa hata kidogo; na watazika wafu katika Tofeti mupaka kusikuwe tena nafasi ya kuwazika.”’+

12 “‘Ni vile nitatendea mahali hapa,’ ni vile Yehova anasema, ‘na wakaaji wake, ili kufanya muji huu kama Tofeti. 13 Na nyumba za Yerusalemu na nyumba za wafalme wa Yuda zitakuwa chafu kama mahali hapa, Tofeti,+ ndiyo, nyumba zote zenye, kwenye sehemu zake za juu, walitolea zabihu jeshi lote la mbinguni+ na kwenye walimwanga matoleo ya kinywaji kwa miungu mingine.’”+

14 Wakati Yeremia alirudia kutoka Tofeti kwenye Yehova alikuwa amemutuma ili atoe unabii, akasimama katika kiwanja cha nyumba ya Yehova na kuambia watu wote: 15 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Angalia, ninaleta juu ya muji huu na juu ya miji yake yote musiba wote wenye nimesema juu yake, kwa sababu walikataa kwa kichwa-nguvu kutii* maneno yangu.’”+

20 Sasa Pashuri mwana wa Imeri, kuhani, mwenye alikuwa pia musimamizi mukubwa katika nyumba ya Yehova, alikuwa anasikiliza wakati Yeremia alikuwa anatoa unabii wa mambo hayo. 2 Kisha Pashuri akamupiga Yeremia nabii na kumuweka katika mikatale+ yenye ilikuwa kwenye Mulango Mukubwa wa Juu wa Benyamini, wenye ulikuwa katika nyumba ya Yehova. 3 Lakini katika siku yenye ilifuata wakati Pashuri alimutosha Yeremia katika ile mikatale, Yeremia akamuambia:

“Yehova amekupatia jina, hapana Pashuri, lakini Woga Pande Zote.+ 4 Kwa maana Yehova anasema hivi: ‘Nitakufanya kuwa kitu cha kuogopesha kwako wewe mwenyewe na kwa marafiki wako wote, na wataanguka kwa upanga wa maadui wao wakati macho yako yatakuwa yanaangalia;+ na nitatia watu wote wa Yuda katika mukono wa mufalme wa Babiloni, na atawapeleka katika uhamisho kule Babiloni na kuwaua kwa upanga.+ 5 Na nitatia utajiri wote wa muji huu, mali yake yote, vitu vyake vyote vyenye samani, na hazina zote za wafalme wa Yuda katika mukono wa maadui wao.+ Na watavinyanganya na kuvikamata na kuvipeleka Babiloni.+ 6 Na wewe, Pashuri, na wote wenye wanaishi katika nyumba yako, mutaenda katika utekwa. Utaenda Babiloni na kufa kule, na utazikwa kule pamoja na marafiki wako wote, kwa sababu umewatolea unabii wa uongo.’”+

 7 Umenipumbaza, Ee Yehova, na nikapumbazika.

Ulitumia nguvu zako ili kunipinga, na ukashinda.+

Nimekuwa kitu cha kuchekwa muchana wote;

Kila mutu ananichekelea.+

 8 Kwa maana kila mara wakati ninasema, ninapaswa kulia na kutangaza,

“Jeuri na uharibifu!”

Kwangu neno la Yehova limekuwa sababu ya kutukanwa na kuchekwa muchana wote.+

 9 Basi nikasema: “Sitamutaja,

Na sitasema tena katika jina lake.”+

Lakini katika moyo wangu hilo lilikuwa kama moto wenye kuwaka wenye kufungiwa katika mifupa yangu,

Na nikachoka kulizuia;

Singeweza tena kuvumilia.+

10 Kwa maana nilisikia habari nyingi za uovu zenye haziko hakika;

Woga ulinizunguka.+

“Mumushitaki; tumushitaki!”

Kila mutu mwenye kunitakia amani alikuwa anangojea nianguke:+

“Pengine atafanya kosa la upumbavu,

Na tunaweza kushinda na kujilipizia kisasi juu yake.”

11 Lakini Yehova alikuwa pamoja na mimi kama mupiganaji-vita mwenye kuogopesha.+

Ndiyo sababu wale wenye kunitesa watajikwaa na hawatashinda.+

Watapatishwa haya kubwa, kwa maana hawatafanikiwa.

Haya yao ya milele haitasahauliwa.+

12 Lakini wewe, Ee Yehova wa majeshi, unachunguza mwenye haki;

Unaona mawazo ya ndani kabisa* na moyo.+

Acha nione kisasi chako juu yao,+

Kwa maana nimeleta kesi yangu ya hukumu kwako.+

13 Mumuimbie Yehova! Mumusifu Yehova!

Kwa maana amekomboa maskini* kutoka katika mukono wa watenda-maovu.

14 Ilaaniwe siku yenye nilizaliwa!

Siku yenye mama yangu alinizaa isibarikiwe!+

15 Alaaniwe mutu mwenye alimuletea baba yangu habari njema, akisema:

“Mwana amezaliwa kwako, kijana mwanaume!”

Na kumufanya afurahi sana.

16 Mutu huyo akuwe kama miji yenye Yehova aliharibu bila kusikitika.

Asikie kilio asubui na sauti ya mulio ya katikati ya muchana.

17 Sababu gani hakuniua ndani ya tumbo la uzazi,

Ili mama yangu akuwe kaburi langu

Na tumbo lake la uzazi likuwe na mimba sikuzote?+

18 Sababu gani iliomba nitoke ndani ya tumbo la uzazi

Ili kuona taabu na huzuni,

Ili kumaliza siku zangu katika haya?+

21 Yeremia alipokea neno kutoka kwa Yehova wakati Mufalme Sedekia+ alituma kwake Pashuri+ mwana wa Malkiya na Sefania+ mwana wa Maaseya, kuhani, ili kutoa ombi hili: 2 “Tafazali umuulize Yehova kwa ajili yetu, kwa sababu Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni anapigana vita na sisi.+ Pengine Yehova atatutendea moja ya matendo yake ya ajabu, na hivyo ataondoka kwetu.”+

3 Yeremia akawaambia: “Mumuambie Sedekia hivi: 4 ‘Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: “Angalia, ninageuza juu yenu* silaha za vita zenye kuwa katika mikono yenu wenyewe, zenye munatumia ili kupigana na mufalme wa Babiloni+ na Wakaldayo wenye kuwa inje ya ukuta wenye wanawazunguka ninyi kwa ajili ya vita. Na nitawakusanya katikati ya muji huu. 5 Na mimi mwenyewe nitapigana na ninyi+ kwa mukono wenye kunyooshwa na kwa mukono wenye nguvu, kwa hasira na kasirani kali na ukali mukubwa.+ 6 Nitapiga wakaaji wa muji huu, mwanadamu na munyama pia. Watakufa kwa ugonjwa mukubwa wa kuambukiza.”’+

7 “‘“Na kisha,” ni vile Yehova anasema, “Nitatia Mufalme Sedekia wa Yuda na watumishi wake na watu wa muji huu⁠—wale wenye wataokoka ugonjwa wa kuambukiza, upanga, na njaa⁠—​nitawatia katika mukono wa Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni, katika mukono wa maadui wao, na katika mukono wa wale wenye wanatafuta kuondoa uzima wao.*+ Atawapiga na kuwaangusha kwa upanga. Hatawasikitikia, ao kuonyesha huruma ao kuwa na rehema yoyote.”’+

8 “Na utaambia watu hawa, ‘Yehova anasema hivi: “Angalia, ninaweka mbele yenu njia ya uzima na njia ya kifo. 9 Wale wenye watabakia katika muji huu watakufa kwa upanga, kwa njaa, na kwa ugonjwa wa kuambukiza. Lakini mutu yeyote mwenye atatoka na kujitia katika mikono ya Wakaldayo wenye wanawazunguka ninyi kwa ajili ya vita ataendelea kuishi, na atapata uzima wake* kama kitu chenye kilichukuliwa katika vita.”’*+

10 “‘“Kwa maana nimekaza uso wangu juu ya muji huu kwa ajili ya musiba haiko kwa ajili ya mema,”+ ni vile Yehova anasema. “Utatiwa katika mukono wa mufalme wa Babiloni,+ na atauteketeza kwa moto.”+

11 “‘Kwa nyumba ya mufalme wa Yuda: Musikie neno la Yehova. 12 Enyi nyumba ya Daudi, Yehova anasema hivi:

“Mutende haki kila asubui,

Na mumukomboe ule mwenye ananyanganywa kutoka katika mukono wa mupunjaji,+

Ili kasirani yangu kali isiwake kama moto+

Na kuteketeza bila mutu wa kuuzimisha

Kwa sababu ya matendo yenu maovu.”’+

13 ‘Angalia, nitapigana na wewe, Ee mukaaji wa bonde,*

Ee mwamba wa inchi tambarare,’ ni vile Yehova anasema.

‘Na ninyi wenye kusema: “Ni nani atashuka kupigana na sisi?

Na ni nani mwenye atashambulia makao yetu?”

14 Nitawaomba ninyi mutoe hesabu

Kulingana na matendo yenu,’+ ni vile Yehova anasema.

‘Na nitawasha moto katika pori lake,

Na utateketeza vitu vyote vyenye kumuzunguka.’”+

22 Yehova anasema hivi: “Shuka kwenye nyumba ya mufalme wa Yuda, na utoe ujumbe huu. 2 Unapaswa kusema, ‘Sikia neno la Yehova, Ee mufalme wa Yuda mwenye kukaa juu ya kiti cha ufalme cha Daudi, wewe pamoja na watumishi wako na watu wako, wale wenye wanaingia kupitia milango hii mikubwa. 3 Yehova anasema hivi: “Mutende haki na uadilifu.* Mukomboe mwenye kunyanganywa kutoka katika mukono wa mupunjaji. Musitendee mubaya mukaaji yeyote mugeni, na musiumize mutoto yeyote mwenye hana baba* ao mujane.+ Na musimwange damu yoyote yenye haina hatia mahali hapa.+ 4 Kwa maana kama munakuwa waangalifu ili kutimiza neno hili, basi wafalme wenye kukaa kwenye kiti cha ufalme cha Daudi+ wataingia kupitia milango mikubwa ya nyumba hii, wakiwa wamepanda katika magari na juu ya farasi, wao pamoja na watumishi wao na watu wao.”’+

5 “‘Lakini kama hamutatii maneno haya, mimi ninaapa kwa nafsi yangu mwenyewe,’ ni vile Yehova anasema, ‘kwamba nyumba hii itakuwa mahali kwenye kuliharibiwa.’+

6 “Kwa maana Yehova anasema hivi juu ya nyumba ya mufalme wa Yuda:

‘Wewe ni kama Gileadi kwangu,

Kama kichwa cha Lebanoni.

Lakini nitakufanya kuwa jangwa;

Hakuna muji wako hata mumoja wenye utaikaliwa.+

 7 Na nitaweka* wenye kuharibu juu yako,

Kila mumoja akiwa na silaha zake.+

Watakata miti yako ya mierezi ya muzuri zaidi

Na kuiangusha ndani ya moto.+

8 Na mataifa mengi yatapita pembeni ya muji huu na kuambiana: “Sababu gani Yehova alitendea hivi muji huu mukubwa?”+ 9 Na watajibu: “Kwa sababu waliacha agano la Yehova Mungu wao na wakainamia miungu mingine na kuitumikia.”’+

10 Musilie kwa sababu ya mutu mwenye alikufa,

Na musisikitike kwa sababu yake.

Tofauti na hilo, mulie sana kwa sababu ya ule mwenye anaenda zake mbali,

Kwa maana hatarudia tena ili kuona inchi yenye alizaliwa ndani.

11 “Kwa maana Yehova anasema hivi juu ya Shalumu*+ mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda mwenye anatawala pa nafasi ya Yosia baba yake+ na mwenye ameondoka mahali hapa: ‘Hatarudia pale tena. 12 Kwa maana atakufa mahali kwenye wamemupeleka katika uhamisho, na hataona tena inchi hii.’+

13 Ole wake mutu mwenye anajenga nyumba yake bila uadilifu*

Na vyumba vyake vya juu bila haki,

Mwenye anafanya mwanadamu mwenzake amutumikie bure,

Na mwenye anakataa kumulipa malipo yake;+

14 Ule mwenye anasema, ‘Nitajijengea nyumba yenye nafasi kubwa

Yenye vyumba vya juu vyenye nafasi kubwa.

Nitaiwekea madirisha

Na nitaifunika kwa mbao za mierezi na nitaipakaa rangi nyekundu sana.’

15 Je, utaendelea kutawala kwa sababu unapita wengine kwa kutumia miti ya mierezi?

Baba yako pia alikula na kunywa,

Lakini alitenda haki na uadilifu,*+

Na mambo yakakuwa muzuri kwake.

16 Alitetea haki ya mwenye kuteseka na maskini,

Basi mambo yakakuwa muzuri.

‘Je, haiko hiyo ndiyo maana ya kunijua?’ ni vile Yehova anasema.

17 ‘Lakini macho yako na moyo wako vinakazia tu faida yako yenye haiko ya haki,

Kumwanga damu yenye haina kosa,

Na kufanya upunjaji na unyanganyi.’

18 “Kwa hiyo Yehova anasema hivi juu ya Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda:

‘Hawatamuombolezea:

“Aa! ndugu yangu! Aa! dada yangu!”

Hawatamuombolezea:

“Aa! Ee bwana! Aa! muheshimiwa mufalme!”

19 Atazikwa kwa maziko ya punda,+

Kwa kukokotwa na kutupwa,

Inje ya milango mikubwa ya Yerusalemu.’+

20 Panda mupaka Lebanoni na useme kwa sauti kubwa,

Pandisha sauti yako katika Bashani,

Na useme kwa sauti kubwa kutoka Abarimu,+

Kwa maana wote wenye wanakupenda kwa tamaa wamepondwa.+

21 Nilisema na wewe wakati ulijisikia kuwa salama.

Lakini ulisema, ‘Sitatii.’+

Hii imekuwa njia yako tangu ujana,

Kwa maana haukutii sauti yangu.+

22 Upepo utachunga wachungaji wako wote,+

Na wale wenye wanakupenda kwa tamaa wataenda katika utekwa.

Kisha utapatishwa haya na kufezeheshwa kwa sababu ya musiba wako wote.

23 Ee wewe mwenye kukaa katika Lebanoni,+

Mwenye kuwa na chicha* kati ya miti ya mierezi,+

Namna utalia kwa maumivu wakati uchungu utakuja juu yako,

Uchungu kama wa* mwanamuke mwenye kuzaa!”+

24 “‘Kama vile hakika ninaishi,’ ni vile Yehova anasema, ‘hata kama Konia*+ mwana wa Yehoyakimu,+ mufalme wa Yuda, angekuwa pete ya muhuri kwenye mukono wangu wa kuume, ningekungoa kutoka pale! 25 Nitakutia katika mukono wa wale wenye wanatafuta kuondoa uzima wako,* katika mukono wa wale wenye unaogopa, katika mukono wa Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni, na katika mukono wa Wakaldayo.+ 26 Na wewe pamoja na mama yako mwenye alikuzaa nitawatupa katika inchi ingine kwenye hamukuzaliwa, na mutakufa kule. 27 Na hawatarudia hata kidogo katika inchi yenye wanatamani.*+

28 Je, mutu huyu Konia ni chungu tu chenye kuzarauliwa, chenye kuvunjika,

Chombo chenye hakuna mutu mwenye anataka?

Sababu gani yeye na wazao wake wametupwa chini

Na kutupwa katika inchi yenye hawajue?’+

29 Ee dunia,* dunia, dunia, sikia neno la Yehova.

30 Yehova anasema hivi:

‘Muandike mutu huyu kwamba hana mutoto,

Kama mutu mwenye hatapata mafanikio yoyote wakati wa maisha yake,*

Kwa maana hakuna mutu yeyote kati ya wazao wake mwenye atafanikiwa

Kukaa kwenye kiti cha ufalme cha Daudi na kutawala tena katika Yuda.’”+

23 “Ole wao wachungaji wenye kuharibu na kutawanya kondoo wa malisho yangu!” ni vile Yehova anasema.+

2 Kwa hiyo Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi juu ya wachungaji wenye wanachunga watu wangu: “Mumetawanya kondoo wangu; muliendelea kuwatawanya, na hamukuwaelekezea uangalifu.”+

“Basi nitawaelekezea ninyi uangalifu wangu kwa sababu ya matendo yenu maovu,” ni vile Yehova anasema.

3 “Kisha nitakusanya pamoja mabaki ya kondoo zangu kutoka katika inchi zote kwenye nilikuwa nimewatawanya,+ na nitawarudisha kwenye malisho yao,+ na watazaa na kuwa wengi.+ 4 Na nitasimamisha juu yao wachungaji wenye kwa kweli watawachunga.+ Hawataogopa tena wala kutetemeshwa, na hakuna mwenye atakosekana,” ni vile Yehova anasema.

5 “Angalia! Siku zinakuja,” ni vile Yehova anasema, “wakati nitasimamishia Daudi chipukizi la* haki.+ Na mufalme atatawala+ na kuonyesha ufahamu na kutenda haki na uadilifu* katika inchi.+ 6 Katika siku zake Yuda ataokolewa,+ na Israeli atakaa kwa usalama.+ Na hili ndilo jina lenye ataitwa: Yehova Ni Haki Yetu.”+

7 “Hata hivyo, siku zinakuja,” ni vile Yehova anasema, “wakati hawatasema tena, ‘Kama vile hakika Yehova anaishi, mwenye alitosha watu wa Israeli katika inchi ya Misri!’+ 8 lakini tofauti na hilo, ‘Kama vile hakika Yehova anaishi, mwenye alitosha na kurudisha wazao wa nyumba ya Israeli katika inchi ya kaskazini na katika inchi zote kwenye nilikuwa nimewatawanya,’ na watakaa katika inchi yao wenyewe.”+

9 Kuhusu manabii:

Moyo wangu umevunjika ndani yangu.

Mifupa yangu yote inatetemeka.

Mimi ni kama mutu mwenye kulewa

Na kama mutu mwenye amelemewa na divai,

Kwa sababu ya Yehova na kwa sababu ya maneno yake matakatifu.

10 Kwa maana inchi imejaa wazinifu;+

Kwa sababu ya laana inchi inaomboleza+

Na malisho ya jangwa yamekauka.+

Njia yao ni ya uovu, na wanatumia nguvu zao mubaya.

11 “Nabii pamoja na kuhani wamechafuliwa.*+

Hata katika nyumba yangu mwenyewe nimepata uovu wao,”+ ni vile Yehova anasema.

12 “Basi njia yao itakuwa na uterezi na giza;+

Watasukumwa na wataanguka.

Kwa maana nitaleta musiba juu yao

Katika mwaka wa kuomba hesabu,” ni vile Yehova anasema.

13 “Na katika manabii wa Samaria+ nimeona jambo lenye kuchukiza.

Unabii wao unachochewa na Baali,

Na wanapotosha watu wangu Israeli.

14 Na katika manabii wa Yerusalemu nimeona mambo yenye kuchukiza sana.

Wanafanya uzinifu+ na kutembea katika uongo;+

Wanatia moyo* watenda-maovu,

Na hawageuke na kuacha uovu wao.

Kwangu wote ni kama Sodoma,+

Na wakaaji wake ni kama Gomora.”+

15 Kwa hiyo Yehova wa majeshi anasema hivi juu ya manabii:

“Angalia, ninawafanya wakule pakanga

Na kuwapatia maji yenye sumu wakunywe.+

Kwa maana kutoka kwa manabii wa Yerusalemu uasi-imani umeenea katika inchi yote.”

16 Yehova wa majeshi anasema hivi:

“Musisikilize maneno ya manabii wenye wanawatolea ninyi unabii.+

Wanawadanganya ninyi.*

Maono yenye wanasema yanatoka katika moyo wao wenyewe,+

Hapana katika kinywa cha Yehova.+

17 Wanaambia tena na tena wale wenye hawaniheshimie,

‘Yehova amesema: “Mutakuwa na amani.”’+

Na kila mutu mwenye anafuata moyo wake mwenyewe mugumu wanamuambia,

‘Hakuna musiba wowote wenye utakuja juu yako.’+

18 Kwa maana ni nani mwenye amesimama katika kikundi cha marafiki wa karibu wa Yehova

Ili aone na kusikia neno lake?

Ni nani mwenye amekazia uangalifu neno lake ili alisikie?

19 Angalia! Zoruba yenye upepo mukali ya Yehova italipuka kwa kasirani kali;

Kama zoruba kali yenye kuzunguka-zunguka itazunguka juu ya kichwa cha waovu.+

20 Kasirani ya Yehova haitarudia nyuma

Mupaka wakati atakuwa ametenda na kutimiza makusudi ya moyo wake.

Katika kipindi cha mwisho cha zile siku ninyi mutaelewa jambo hilo waziwazi.

21 Sikutuma manabii, lakini walikimbia.

Sikusema nao, lakini walitoa unabii.+

22 Lakini kama wangekuwa wamesimama katika kikundi changu cha marafiki wa karibu,

Wangekuwa wamefanya watu wangu wasikie maneno yangu

Na wangekuwa wamefanya warudie kutoka kwenye njia yao ya mubaya na matendo yao maovu.”+

23 “Je, mimi ni Mungu mwenye kuwa karibu tu,” ni vile Yehova anasema, “na pia siko Mungu kutoka mbali?”

24 “Je, mutu yeyote anaweza kujificha mahali pa siri kwenye siwezi kumuona?”+ ni vile Yehova anasema.

“Je, mimi sijaze mbingu na dunia?”+ ni vile Yehova anasema.

25 “Nimesikia manabii wenye wanatoa unabii wa uongo katika jina langu wakisema, ‘Niliota ndoto! Niliota ndoto!’+ 26 Jambo hili litaendelea mupaka wakati gani katika moyo wa manabii, kutoa unabii wa uongo? Wao ni manabii wa udanganyifu wa moyo wao wenyewe.+ 27 Wanakusudia kufanya watu wangu wasahau jina langu kupitia ndoto zenye wanaelezeana, kama vile baba zao walisahau jina langu kwa sababu ya Baali.+ 28 Acha nabii mwenye kuwa na ndoto aeleze ndoto hiyo, lakini ule mwenye kuwa na neno langu anapaswa kusema neno langu kwa ukweli.”

“Nyasi iko na uhusiano gani na nafaka?” ni vile Yehova anasema.

29 “Je, neno langu haliko kama vile moto,”+ ni vile Yehova anasema, “na kama nyundo* ya chuma yenye inavunja mwamba?”+

30 “Basi angalia, ninapinga manabii,” ni vile Yehova anasema, “wenye wanaiba maneno yangu kila mumoja kutoka kwa mwenzake.”+

31 “Angalia, ninapinga manabii,” ni vile Yehova anasema, “wale wenye wanatumia ulimi wao kusema, ‘Anasema!’”+

32 “Angalia, ninapinga manabii wa ndoto za uongo,” ni vile Yehova anasema, “wenye wanazieleza na kupotosha watu wangu kwa sababu ya uongo wao na kujisifu kwao.”+

“Lakini sikuwatuma wala kuwaamuru. Basi hawataletea watu hawa faida hata kidogo,”+ ni vile Yehova anasema.

33 “Na wakati watu hawa ao nabii ao kuhani wanakuuliza, ‘Muzigo* wa Yehova ni nini?’ unapaswa kuwajibu, ‘“Ninyi watu ndio muzigo! Na mimi nitawatupa ninyi,”+ ni vile Yehova anasema.’ 34 Na kuhusu nabii ao kuhani ao watu wenye wanasema, ‘Huu ndio muzigo* wa Yehova!’ Nitakaza uangalifu wangu juu ya mutu huyo na juu ya nyumba yake. 35 Ni hivi kila mumoja wenu anamuambia mwenzake na pia ndugu yake: ‘Yehova ametoa jibu gani? Na Yehova amesema nini?’ 36 Lakini musitaje tena muzigo* wa Yehova, kwa maana muzigo* ni neno la kila mutu mwenyewe, na mumebadilisha maneno ya Mungu mwenye kuishi, Yehova wa majeshi, Mungu wetu.

37 “Utamuambia nabii huyo hivi: ‘Yehova amekupatia jibu gani? Na Yehova amesema nini? 38 Na kama munaendelea kusema, “Muzigo* wa Yehova!” Yehova anasema hivi: “Kwa sababu munasema, ‘Neno hili ndilo muzigo* wa Yehova,’ kisha mimi kuwaambia ninyi, ‘Hamupaswe kusema: “Muzigo* wa Yehova!”’ 39 muangalie! Nitawanyangula ninyi na kuwatupa mbali kutoka mbele yangu, ninyi pamoja na muji wenye niliwapatia ninyi na mababu zenu. 40 Na nitaleta juu yenu haya ya milele na fezeha ya milele, yenye haitasahauliwa.”’”+

24 Kisha Yehova akanionyesha vitunga mbili vya tini vyenye viliwekwa mbele ya hekalu la Yehova, kisha Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni kupeleka katika uhamisho Yekonia*+ mwana wa Yehoyakimu,+ mufalme wa Yuda, pamoja na wakubwa wa Yuda, mafundi, na mafundi wa vyuma;* aliwachukua kutoka Yerusalemu na kuwapeleka Babiloni.+ 2 Kitunga kimoja kilikuwa na tini za muzuri sana, kama tini za kwanza-kwanza, lakini kile kitunga kingine kilikuwa na tini za mubaya sana, na hivyo hazingeweza kukuliwa.

3 Kisha Yehova akaniuliza: “Unaona nini, Yeremia?” Basi nikasema: “Tini; tini za muzuri ni za muzuri sana, lakini tini za mubaya ni za mubaya sana, mubaya sana na hivyo haziwezi kukuliwa.”+

4 Kisha neno la Yehova likakuja kwangu, na kusema: 5 “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Kama hizi tini za muzuri, ni vile nitaona kwa njia ya muzuri wale wahamishwa wa Yuda, wenye nimetosha hapa na kupeleka katika inchi ya Wakaldayo. 6 Nitaweka jicho langu juu yao kwa faida yao, na nitawarudisha katika inchi hii.+ Nitawajenga, na sitabomoa; nitawapanda, na sitangoa.+ 7 Na nitawapatia moyo wa kunijua, kwamba mimi ni Yehova.+ Watakuwa watu wangu, na mimi nitakuwa Mungu wao,+ kwa maana watarudia kwangu kwa moyo wao wote.+

8 “‘Lakini kuhusu zile tini za mubaya zenye ni za mubaya sana na hivyo haziwezi kukuliwa,+ Yehova anasema hivi: “Ni vile nitamuona Mufalme Sedekia+ wa Yuda, wakubwa wake, mabaki ya Yerusalemu wenye waliachwa katika inchi hii, na wale wenye kukaa katika inchi ya Misri.+ 9 Nitawafanya kuwa kitu cha kuogopesha na musiba kwa falme zote za dunia,+ haya, neno la kimezali, kitu cha kuchekelewa, na laana+ kila mahali kwenye ninawatawanya.+ 10 Na nitatuma juu yao upanga,+ njaa, na ugonjwa wa kuambukiza,+ mupaka waangamie kutoka katika inchi yenye niliwapatia wao na mababu zao.”’”

25 Neno lenye lilikuja kwa Yeremia kuhusu watu wote wa Yuda katika mwaka wa ine (4) wa Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda, wenye ulikuwa mwaka wa kwanza wa Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni. 2 Nabii Yeremia alisema hivi kuhusu* watu wote wa Yuda na wakaaji wote wa Yerusalemu:

3 “Tangu mwaka wa kumi na tatu (13) wa Yosia+ mwana wa Amoni, mufalme wa Yuda, mupaka leo, miaka hii makumi mbili na tatu (23), neno la Yehova limekuja kwangu, na nikaendelea kusema na ninyi tena na tena,* lakini hamukusikiliza.+ 4 Na Yehova alituma kwenu watumishi wake wote manabii, akiwatuma tena na tena,* lakini hamukusikiliza wala kutega sikio lenu ili musikie.+ 5 Walisema, ‘Tafazali, mugeuke, kila mumoja wenu kutoka katika njia zenu zenye uovu na matendo yenu maovu;+ kisha mutaendelea kukaa kwa wakati murefu wenye kuja katika inchi yenye Yehova aliwapatia ninyi na mababu zenu zamani. 6 Musifuate miungu mingine na kuitumikia na kuiinamia, mukinikasirisha kupitia kazi ya mikono yenu; tofauti na hilo nitaleta musiba juu yenu.’

7 “‘Lakini hamukunisikiliza,’ ni vile Yehova anasema. ‘Tofauti na hilo mulinikasirisha kupitia kazi ya mikono yenu, na kujiletea musiba.’+

8 “Kwa hiyo Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘“Kwa sababu hamukutii maneno yangu, 9 ninaita familia zote za kaskazini,”+ ni vile Yehova anasema, “ninamuita Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni, mutumishi wangu,+ na nitawaleta juu ya inchi hii+ na juu ya wakaaji wake na juu ya mataifa haya yote ya pembeni-pembeni.+ Nitawaharibu na kuwafanya kuwa kitu cha kuogopesha na kitu cha kupigiwa muluzi na mabomoko ya kudumu. 10 Nitamaliza sauti ya furaha na sauti ya shangwe kutoka kwao,+ sauti ya bwana-arusi na sauti ya bibi-arusi,+ sauti ya jiwe la kusagia la mukono na mwangaza wa taa. 11 Na inchi hii yote itakuwa mabomoko na itakuwa kitu cha kuogopesha, na mataifa haya yatamutumikia mufalme wa Babiloni miaka makumi saba (70).”’+

12 “‘Lakini wakati miaka makumi saba (70) itatimia,+ nitaomba hesabu kwa* mufalme wa Babiloni na taifa hilo kwa sababu ya kosa lao,’+ ni vile Yehova anasema, ‘na nitafanya inchi ya Wakaldayo kuwa inchi yenye imeachwa ukiwa sikuzote.+ 13 Nitaleta juu ya inchi hiyo maneno yangu yote yenye nimesema juu yake, yote yenye kuandikwa katika kitabu hiki yenye Yeremia ametoa unabii juu ya mataifa yote. 14 Kwa maana mataifa mengi na wafalme wakubwa+ watawafanya kuwa watumwa,+ na nitawalipa kulingana na matendo yao na kazi ya mikono yao wenyewe.’”+

15 Kwa maana Yehova Mungu wa Israeli ameniambia hivi: “Kamata kikombe hiki cha divai ya kasirani kali kutoka katika mukono wangu, na ufanye mataifa yote yenye ninakutuma kwao yakikunywe. 16 Na watakunywa na kuyumba-yumba na kutenda kama wenda-wazimu kwa sababu ya upanga wenye ninatuma kati yao.”+

17 Basi nikakamata kile kikombe katika mukono wa Yehova na kufanya mataifa yote yenye Yehova alinituma kwao yakunywe:+ 18 kuanzia Yerusalemu na miji ya Yuda,+ wafalme wake na wakubwa wake, ili kuyafanya kuwa mabomoko, kitu cha kuogopesha, kitu cha kupigiwa muluzi na laana,+ kama vile hali iko leo; 19 kisha Farao mufalme wa Misri na watumishi wake, wakubwa wake, na watu wake wote,+ 20 na watu wote wa mataifa mbalimbali wenye kuchangamana nao; wafalme wote wa inchi ya Usi; wafalme wote wa inchi ya Wafilisti,+ Ashkeloni,+ Gaza, Ekroni, na wenye kubakia wa Ashdodi; 21 Edomu,+ Moabu,+ na Waamoni;+ 22 wafalme wote wa Tiro, wafalme wote wa Sidoni,+ na wafalme wa kisiwa chenye kuwa katika bahari; 23 Dedani,+ Tema, Buzi, na wale wote wenye kuwa na nywele zenye kukatwa kwenye vipaji vya nyuso;+ 24 wafalme wote wa Waarabu+ na wafalme wote wa watu wa mataifa mbalimbali wenye kuchangamana wenye wanakaa katika jangwa; 25 wafalme wote wa Zimri, wafalme wote wa Elamu,+ na wafalme wote wa Wamedi;+ 26 na wafalme wote wa kaskazini wenye kuwa karibu na wenye kuwa mbali, mumoja baada ya mwingine, na falme zingine zote za dunia zenye kuwa juu ya uso wa inchi; na mufalme wa Sheshaki*+ atakunywa kisha wao.

27 “Na unapaswa kuwaambia, ‘Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Mukunywe na mulewe na mutapike na kuanguka na hivyo musiweze kusimama+ kwa sababu ya upanga wenye ninatuma kati yenu.”’ 28 Na kama wanakataa kukamata kikombe kutoka katika mukono wako ili wakunywe, uwaambie, ‘Yehova wa majeshi anasema hivi: “Munapaswa kukikunywa! 29 Kwa maana muangalie! kama ninaleta musiba kwanza juu ya muji wenye kubeba jina langu,+ je, ninyi mutakosa kupewa azabu?”’+

“‘Hamutakosa kupewa azabu, kwa maana ninaita upanga juu ya wakaaji wote wa dunia,’ ni vile Yehova wa majeshi anasema.

30 “Na unapaswa kutoa unabii kwa maneno haya yote na kuwaambia,

‘Yehova atanguruma kutoka juu,

Na kutoka katika makao yake matakatifu atafanya sauti yake isikiwe.

Atanguruma kwa sauti kubwa juu ya makao yake.

Akifanya makelele kama wale wenye wanakanyanga kikamulio cha divai,

Ataimba kwa ushindi juu ya wakaaji wote wa dunia.’

31 ‘Makelele yatasikika mupaka kwenye miisho ya dunia,

Kwa maana Yehova iko* na ubishi na mataifa.

Yeye mwenyewe atahukumu wanadamu wote.*+

Na ataharibu waovu kwa upanga,’ ni vile Yehova anasema.

32 Yehova wa majeshi anasema hivi:

‘Angalia! Musiba unaenea kutoka taifa mupaka taifa,+

Na zoruba kali itaachiliwa kutoka sehemu za mbali zaidi za dunia.+

33 “‘Na wale wenye waliuawa na Yehova katika siku hiyo watakuwa kutoka mwisho mumoja wa dunia mupaka mwisho mwingine wa dunia. Hawataombolezewa, na hawatakusanywa wala kuzikwa. Watakuwa kama mbolea juu ya uso wa inchi.’

34 Muomboleze, ninyi wachungaji, na mulie kwa sauti kubwa!

Mujizungushe-zungushe chini, ninyi watu wenye cheo wa kundi,

Kwa sababu wakati wenu wa kuuawa na kutawanywa umefika,

Na mutaanguka kama chombo chenye samani!

35 Wachungaji hawana mahali pa kukimbilia,

Na watu wenye cheo wa kundi hawawezi kuponyoka.

36 Musikilize! Kilio cha wachungaji

Na maombolezo ya watu wenye cheo wa kundi,

Kwa maana Yehova anaharibu malisho yao.

37 Na makao yenye amani yamefanywa yasikuwe na uzima

Kwa sababu ya kasirani ya Yehova yenye kuwaka.

38 Ametoka katika pango lake kama vile mwana-simba,*+

Kwa maana inchi yao imekuwa kitu cha kuogopesha

Kwa sababu ya upanga wenye kuua sana

Na kwa sababu ya kasirani yake yenye kuwaka.”

26 Katika mwanzo wa utawala wa Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda, neno hili lilikuja kutoka kwa Yehova: 2 “Yehova anasema hivi: ‘Simama katika kiwanja cha nyumba ya Yehova na useme kuhusu* watu wote wa miji ya Yuda wenye wanaingia ili kuabudu* katika nyumba ya Yehova. Uwaambie kila kitu chenye ninakuamuru; usiondoe hata neno moja. 3 Pengine watasikiliza na kila mumoja atageuka na kuacha njia yake yenye uovu, na nitabadilisha mawazo yangu* kuhusu musiba wenye ninakusudia kuleta juu yao kwa sababu ya matendo yao maovu.+ 4 Uwaambie: “Yehova anasema hivi: ‘Kama hamutanisikiliza kwa kufuata sheria yangu yenye* nimeweka mbele yenu, 5 kwa kusikiliza maneno ya watumishi wangu manabii, wenye ninatuma kwenu tena na tena,* wenye hamukusikiliza,+ 6 basi nitafanya nyumba hii kama Shilo,+ na nitafanya muji huu kuwa kitu cha kulaaniwa kwa mataifa yote ya dunia.’”’”+

7 Na makuhani na manabii na watu wote wakasikia Yeremia akisema maneno hayo ndani ya nyumba ya Yehova.+ 8 Basi wakati Yeremia alimaliza kusema mambo yote yenye Yehova alikuwa amemuamuru aambie watu wote, makuhani na manabii na watu wote wakamukamata na kusema: “Hakika utakufa. 9 Sababu gani umetoa unabii katika jina la Yehova, kwa kusema, ‘Nyumba hii itakuwa kama Shilo, na muji huu utaharibiwa na kuachwa bila mukaaji?” Na watu wote wakakusanyika kumuzunguka Yeremia ndani ya nyumba ya Yehova.

10 Wakati wakubwa wa Yuda walisikia maneno hayo, wakapanda kutoka kwenye nyumba ya mufalme wakaenda kwenye nyumba ya Yehova na kukaa kwenye muingilio wa mulango mukubwa mupya wa Yehova.+ 11 Makuhani na manabii wakaambia wakubwa na watu wote: “Mutu huyu anastahili hukumu ya kifo,+ kwa sababu ametoa unabii juu ya muji huu kama vile mumesikia kwa masikio yenu wenyewe.”+

12 Kisha Yeremia akaambia wakubwa wote na watu wote: “Yehova ndiye alinituma kutoa unabii juu ya nyumba hii na juu ya muji huu kwa maneno yote yenye mumesikia.+ 13 Basi sasa, murekebishe njia zenu na matendo yenu na mutii sauti ya Yehova Mungu wenu, na Yehova atabadilisha mawazo yake* juu ya musiba wenye amesema juu yenu.+ 14 Lakini mimi, niko katika mukono wenu. Munitendee jambo lolote lenye munaona kuwa muzuri na sawa mbele ya macho yenu. 15 Lakini mujue hakika kwamba kama munaniua, mutaleta damu yenye haina kosa juu yenu wenyewe na juu ya muji huu na juu ya wakaaji wake, kwa maana kwa kweli Yehova alinituma kwenu ili niseme maneno haya yote katika masikio yenu.”

16 Kisha wakubwa na watu wote wakaambia makuhani na manabii: “Mutu huyu hastahili hukumu ya kifo, kwa maana alisema na sisi katika jina la Yehova Mungu wetu.”

17 Zaidi ya hayo, wazee fulani wa inchi wakasimama na kuanza kuambia kutaniko lote la watu: 18 “Mika+ wa Moresheti alikuwa anatoa unabii katika siku za Mufalme Hezekia+ wa Yuda, na akaambia watu wote wa Yuda, ‘Yehova wa majeshi anasema hivi:

“Sayuni italimwa kama shamba,

Yerusalemu itakuwa marundo ya mabomoko,+

Na mulima wa Nyumba* utakuwa kama mahali pa juu katika pori.”’*+

19 “Je, Mufalme Hezekia wa Yuda na Yuda wote walimuua? Je, hakumuogopa Yehova na kumuomba Yehova wema,* na hivyo Yehova akabadilisha mawazo yake* kuhusu musiba wenye alikuwa amesema juu yao?+ Basi tuko karibu kuleta musiba mukubwa juu yetu* wenyewe.

20 “Na kulikuwa mutu mwingine mwenye kutoa unabii katika jina la Yehova, Uriya mwana wa Shemaya kutoka Kiriat-yearimu,+ mwenye alitoa unabii juu ya muji huu na juu ya inchi hii kwa maneno kama ya Yeremia. 21 Mufalme Yehoyakimu+ na wanaume wake wote wenye nguvu na wakubwa wote wakasikia maneno yake, na mufalme akatafuta kumuua.+ Wakati Uriya alisikia jambo hilo, mara moja akaogopa na kukimbilia Misri. 22 Kisha Mufalme Yehoyakimu akatuma Elnatani+ mwana wa Akbori pamoja na watu wengine kuenda Misri. 23 Wakamuleta Uriya kutoka Misri na wakamupeleka kwa Mufalme Yehoyakimu, mwenye alimupiga na kumuua kwa upanga+ na kutupa maiti yake katika makaburi ya watu wa kawaida.”

24 Lakini Ahikamu+ mwana wa Shafani+ alimusaidia Yeremia, na hivyo hakutiwa katika mikono ya watu na kuuawa.+

27 Katika mwanzo wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda, neno hili lilikuja kwa Yeremia kutoka kwa Yehova: 2 “Yehova ameniambia hivi: ‘Ujitengenezee kamba na nira, na uviweke kwenye shingo yako. 3 Kisha uvitume kwa mufalme wa Edomu,+ mufalme wa Moabu,+ mufalme wa Waamoni,+ mufalme wa Tiro,+ na mufalme wa Sidoni+ kupitia mukono wa wajumbe wenye wamekuja Yerusalemu kwa Mufalme Sedekia wa Yuda. 4 Uwapatie amri hii kwa ajili ya mabwana wao:

“‘“Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: muambie hivi mabwana wenu: 5 ‘Mimi ndiye nilifanya dunia, wanadamu, na wanyama wenye kuwa juu ya uso wa dunia kwa nguvu zangu kubwa na kwa mukono wangu wenye kunyooshwa; na nimeipatia mutu yeyote mwenye ninapenda.*+ 6 Na sasa nimetia inchi hizi zote katika mukono wa mutumishi wangu Mufalme Nebukadneza+ wa Babiloni; nimemupatia hata wanyama wa pori ili wamutumikie. 7 Mataifa yote yatamutumikia yeye na mwana wake na mujukuu wake mupaka wakati wa inchi yake mwenyewe utafika,+ wakati mataifa mengi na wafalme wakubwa watamufanya kuwa mutumwa wao.’+

8 “‘“‘Kama taifa lolote ao ufalme unakataa kumutumikia Mufalme Nebukadneza wa Babiloni na unakataa kuweka shingo yake chini ya nira ya mufalme wa Babiloni, nitapatia taifa hilo azabu kwa upanga,+ kwa njaa, na kwa ugonjwa wa kuambukiza,’ ni vile Yehova anasema, ‘mupaka wakati nitakuwa nimewamaliza kabisa kupitia mukono wake.’

9 “‘“‘Kwa hiyo, musisikilize manabii wenu, waaguzi wenu, waota-ndoto wenu, wachawi wenu, na walozi wenu, wenye wanawaambia ninyi: “Hamutamutumikia mufalme wa Babiloni.” 10 Kwa maana wanawatolea ninyi unabii wa uongo, na hivyo mutapelekwa mbali na inchi yenu na nitawatawanya ninyi na mutaangamia.

11 “‘“‘Lakini taifa lenye linaweka shingo yake chini ya nira ya mufalme wa Babiloni na kumutumikia, nitaliruhusu libakie* kwenye inchi yake,’ ni vile Yehova anasema, ‘ili kuilima na kukaa ndani yake.’”’”

12 Pia Mufalme Sedekia+ wa Yuda nilimuambia maneno yaleyale, kwa kusema: “Muweke shingo zenu chini ya nira ya mufalme wa Babiloni na mumutumikie yeye na watu wake, na mutaendelea kuishi.+ 13 Sababu gani wewe na watu wako mukufe kwa upanga,+ kwa njaa,+ na kwa ugonjwa wa kuambukiza,+ kama vile Yehova alisema kuhusu taifa lenye halitamutumikia mufalme wa Babiloni? 14 Musisikilize maneno ya manabii wenye wanawaambia ninyi, ‘Hamutamutumikia mufalme wa Babiloni,’+ kwa sababu wanawatolea ninyi unabii wa uongo.+

15 “‘Kwa maana sikuwatuma,’ ni vile Yehova anasema, ‘lakini wanatoa unabii wa uongo katika jina langu, ili mwishowe niwatawanye ninyi na muangamie, ninyi na manabii wenye wanawatolea ninyi unabii.’”+

16 Na nikaambia makuhani na watu hawa wote: “Yehova anasema hivi: ‘Musisikilize maneno ya manabii wenu wenye wanawatolea ninyi unabii: “Muangalie! Karibuni vyombo vya nyumba ya Yehova vitarudishwa kutoka Babiloni!”+ kwa maana wanawatolea ninyi unabii wa uongo.+ 17 Musiwasikilize. Mumutumikie mufalme wa Babiloni na mutaendelea kuishi.+ Sababu gani muji huu ukuwe mabomoko? 18 Lakini kama wao ni manabii na kama neno la Yehova liko pamoja nao, tafazali acha waombe Yehova wa majeshi kwamba vyombo vyenye vilibakia katika nyumba ya Yehova, katika nyumba ya mufalme wa Yuda, na katika Yerusalemu visipelekwe Babiloni.’

19 “Kwa maana Yehova wa majeshi anasema hivi kuhusu zile nguzo,+ ile Bahari,*+ yale magari,+ na vyombo vyenye vilibakia vyenye viliachwa katika muji huu, 20 vyenye Mufalme Nebukadneza wa Babiloni hakukamata wakati alimupeleka katika uhamisho Yekonia mwana wa Yehoyakimu, mufalme wa Yuda, kutoka Yerusalemu mupaka Babiloni, pamoja na watu wote wenye vyeo wa Yuda na Yerusalemu;+ 21 ndiyo, Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi kuhusu vyombo vyenye vilibakia kwenye nyumba ya Yehova, katika nyumba ya mufalme wa Yuda, na katika Yerusalemu: 22 ‘“Vitapelekwa Babiloni,+ na vitabakia kule mupaka siku nitavikazia uangalifu,” ni vile Yehova anasema. “Kisha nitavileta na kuvirudisha mahali hapa.”’”+

28 Katika mwaka uleule, katika mwanzo wa utawala wa Mufalme Sedekia+ wa Yuda, katika mwaka wa ine (4), katika mwezi wa tano (5), nabii Hanania mwana wa Azuri kutoka Gibeoni+ aliniambia hivi ndani ya nyumba ya Yehova mbele ya makuhani na watu wote: 2 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Nitavunja nira ya mufalme wa Babiloni.+ 3 Katika muda wa miaka* mbili nitarudisha mahali hapa vyombo vyote vya nyumba ya Yehova vyenye Mufalme Nebukadneza wa Babiloni alichukua kutoka mahali hapa na kupeleka Babiloni.’”+ 4 “‘Na nitamurudisha mahali hapa Yekonia+ mwana wa Yehoyakimu,+ mufalme wa Yuda, na wahamishwa wote wa Yuda wenye wameenda Babiloni,’+ ni vile Yehova anasema, ‘kwa maana nitavunja nira ya mufalme wa Babiloni.’”

5 Kisha Yeremia nabii akasema na Hanania nabii mbele ya makuhani na watu wote wenye walikuwa wamesimama ndani ya nyumba ya Yehova. 6 Yeremia nabii akasema: “Amina!* Yehova afanye vile! Yehova atimize maneno yako yenye umetoa unabii kwa kurudisha mahali hapa vyombo vya nyumba ya Yehova kutoka Babiloni na pia watu wote wenye walihamishwa! 7 Hata hivyo, tafazali, sikia ujumbe huu wenye ninasema katika masikio yako na katika masikio ya watu wote. 8 Zamani sana manabii wenye walinitangulia mimi na wenye walikutangulia wewe walikuwa wanatoa unabii juu ya inchi nyingi na falme kubwa, juu ya vita, musiba, na ugonjwa wa kuambukiza. 9 Kama nabii anatoa unabii juu ya amani na neno la nabii huyo litimie, basi itajulikana kwamba kwa kweli Yehova ametuma nabii huyo.”

10 Halafu Hanania nabii akakamata ile nira kutoka kwenye shingo ya nabii Yeremia na kuivunja.+ 11 Kisha Hanania akasema mbele ya watu wote: “Yehova anasema hivi: ‘Ni hivi nitavunja nira ya Mufalme Nebukadneza wa Babiloni kutoka kwenye shingo ya mataifa yote katika muda wa miaka mbili.’”+ Na Yeremia nabii akaenda zake.

12 Kisha Hanania nabii kuvunja ile nira kutoka kwenye shingo ya Yeremia nabii, ujumbe huu wa Yehova ukakuja kwa Yeremia: 13 “Uende na umuambie Hanania, ‘Yehova anasema hivi: “Umevunja nira za miti,+ lakini pa nafasi yazo utatengeneza nira za chuma.” 14 Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Nitaweka nira ya chuma juu ya shingo ya mataifa haya yote, ili yamutumikie Mufalme Nebukadneza wa Babiloni, na wanapaswa kumutumikia.+ Nitamupatia hata wanyama wa pori.”’”+

15 Kisha Yeremia nabii akamuambia Hanania+ nabii: “Tafazali, sikiliza, Ee Hanania! Yehova hakukutuma, lakini umefanya watu hawa wategemee uongo.+ 16 Kwa hiyo Yehova anasema hivi: ‘Angalia! Ninakuondoa kwenye uso wa inchi. Utakufa mwaka huu, kwa maana umechochea uasi juu ya Yehova.’”+

17 Basi Hanania nabii akakufa mwaka huo, katika mwezi wa saba (7).

29 Haya ndiyo maneno ya barua yenye Yeremia nabii alituma kutoka Yerusalemu kwa wazee wenye walibakia kati ya watu wenye walihamishwa, makuhani, manabii, na watu wote, wenye Nebukadneza alikuwa amepeleka katika uhamisho kutoka Yerusalemu kuenda Babiloni, 2 kisha Mufalme Yekonia,+ malkia mama ya mufalme,*+ maofisa wa makao ya mufalme, wakubwa wa Yuda na Yerusalemu, na mafundi na mafundi wa vyuma* kuondoka Yerusalemu.+ 3 Alituma barua hiyo kupitia mukono wa Elasa mwana wa Shafani+ na Gemaria mwana wa Hilkia, wenye Mufalme Sedekia+ wa Yuda alituma kuenda Babiloni kwa Mufalme Nebukadneza wa Babiloni. Ilisema hivi:

4 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anaambia hivi watu wote wenye walihamishwa, wenye nimepeleka katika uhamisho kutoka Yerusalemu kuenda Babiloni: 5 ‘Mujenge nyumba na mukae ndani yake. Mupande bustani na mukule matunda yake. 6 Muchukue bibi na mupate watoto wanaume na watoto wanamuke; muchukue bibi kwa ajili ya watoto wenu wanaume na mutoe watoto wenu wanamuke ili waolewe, ili wao pia wapate watoto wanaume na watoto wanamuke. Mukuwe wengi kule, na musipunguke. 7 Na mutafute amani ya muji kwenye nimewapeleka katika uhamisho, na musali kwa ajili yake kwa Yehova, kwa maana katika amani yake mutakuwa na amani.+ 8 Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Musiache manabii wenu na waaguzi wenu wenye kuwa kati yenu wawadanganye ninyi,+ na musisikilize ndoto zenye wanaota. 9 Kwa maana ‘wanawatolea ninyi unabii wa uongo katika jina langu. Mimi sikuwatuma,’+ ni vile Yehova anasema.”’”

10 “Kwa maana Yehova anasema hivi: ‘Wakati miaka makumi saba (70) itatimia kule Babiloni, nitawakazia ninyi uangalifu wangu,+ na nitatimiza ahadi yangu kwa kuwarudisha ninyi mahali hapa.’+

11 “‘Kwa maana ninajua muzuri mawazo yenye ninafikiria kuwaelekea ninyi,’ ni vile Yehova anasema, ‘mawazo ya amani, na hapana ya musiba,+ ili kuwapatia ninyi wakati wenye kuja wa muzuri na tumaini.+ 12 Na mutaniita na kuja na kusali kwangu, na nitawasikiliza.’+

13 “‘Mutanitafuta na kunipata,+ kwa maana mutanitafuta kwa moyo wenu wote.+ 14 Na nitawaacha munipate,’+ ni vile Yehova anasema. ‘Na nitakusanya watu wenu wenye walikamatwa mateka na kuwakusanya ninyi pamoja kutoka katika mataifa yote na sehemu zote kwenye niliwatawanya ninyi,’+ ni vile Yehova anasema. ‘Na nitawarudisha mahali kwenye mulikuwa wakati niliwafanya muende katika uhamisho.’+

15 “Lakini mumesema, ‘Yehova ametuinulia manabii katika Babiloni.’

16 “Kwa maana Yehova anamuambia hivi mufalme mwenye anakaa kwenye kiti cha ufalme cha Daudi+ na watu wote wenye wanakaa katika muji huu, ndugu zenu wenye hawakuenda katika uhamisho pamoja na ninyi, 17 ‘Yehova wa majeshi anasema hivi: “Angalia, ninatuma juu yao upanga, njaa, na ugonjwa wa kuambukiza,+ na nitawafanya kuwa kama tini zenye kuoza* zenye ni za mubaya sana na hivyo haziwezi kukuliwa.”’+

18 “‘Na nitawafuatilia kwa upanga,+ kwa njaa, na kwa ugonjwa wa kuambukiza, na nitawafanya kuwa kitu cha kuogopesha kwa falme zote za dunia,+ na laana, na kitu cha kushangaza, kitu cha kupigiwa muluzi,+ na haya kati ya mataifa yote kwenye ninawatawanya,+ 19 kwa sababu hawakusikiliza maneno yangu yenye niliwatumia kupitia watumishi wangu manabii,’ ni vile Yehova anasema, ‘nikiwatuma tena na tena.’*+

“‘Lakini hamukusikiliza,’+ ni vile Yehova anasema.

20 “Kwa hiyo, musikie neno la Yehova, ninyi wote wenye mulihamishwa, wenye nilitosha Yerusalemu na kupeleka Babiloni. 21 Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi juu ya Ahabu mwana wa Kolaya na juu ya Sedekia mwana wa Maaseya, wenye wanawatolea ninyi unabii wa uongo katika jina langu:+ ‘Angalia, nitawatia katika mukono wa Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni, na atawapiga na kuwaua mbele ya macho yenu. 22 Na kile chenye kuwapata kitakuwa laana yenye itazungumuziwa na wahamishwa wote wa Yuda katika Babiloni: “Yehova akufanye kama Sedekia na kama Ahabu, wenye mufalme wa Babiloni alichoma katika moto!” 23 kwa maana wametenda kwa haya katika Israeli,+ kwa kufanya uzinifu na bibi za majirani wao na kusema maneno ya uongo katika jina langu, maneno yenye sikuwaamuru.+

“‘“Mimi ndiye ninajua, na niko shahidi,”+ ni vile Yehova anasema.’”

24 “Na utaambia hivi Shemaya+ wa Nehelamu, 25 ‘Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Kwa sababu ulituma barua katika jina lako kwa watu wote wenye kuwa katika Yerusalemu, kwa Sefania+ mwana wa Maaseya, kuhani, na kwa makuhani wote, kwa kusema, 26 ‘Yehova amekufanya kuwa kuhani pa nafasi ya Yehoyada kuhani ili ukuwe mwangalizi wa nyumba ya Yehova, usimamie mwenda-wazimu yeyote mwenye anatenda kama nabii na kumuweka katika mikatale na katika kongwa;*+ 27 basi, sababu gani haukumukemea Yeremia wa Anatoti,+ mwenye anatenda kama nabii kwa ajili yenu?+ 28 Kwa maana alitutumia hata ujumbe Babiloni, kwa kusema: “Utakuwa wakati murefu! Mujenge nyumba na mukae ndani yake. Mupande mabustani na mukule matunda yake,+⁠—​ ”’”’”

29 Wakati Sefania+ kuhani alisoma barua hiyo katika masikio ya Yeremia nabii, 30 neno la Yehova likakuja kwa Yeremia, na kusema: 31 “Tuma ujumbe kwa watu wote wenye walihamishwa, kwa kusema: ‘Yehova anasema hivi juu ya Shemaya wa Nehelamu: “Kwa sababu Shemaya aliwatolea unabii, hata kama sikumutuma, na alijaribu kuwafanya mutegemee uongo,+ 32 kwa hiyo Yehova anasema hivi: ‘Angalia, ninageuza uangalifu wangu kuelekea Shemaya wa Nehelamu na wazao wake. Hakuna mutu yeyote kati ya watu wake mwenye ataokoka kati ya watu hawa, na hataona mema yenye nitatendea watu wangu,’ ni vile Yehova anasema, ‘kwa maana amechochea uasi juu ya Yehova.’”’”

30 Neno lenye lilikuja kwa Yeremia kutoka kwa Yehova, na kusema: 2 “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Andika katika kitabu maneno yote yenye ninakuambia. 3 Kwa maana “angalia! siku zinakuja,” ni vile Yehova anasema, “wakati nitakusanya watu wangu wenye walikamatwa mateka, Israeli na Yuda,”+ ni vile Yehova anasema, “na nitawarudisha katika inchi yenye nilipatia mababu zao, na watairiti tena.”’”+

4 Haya ndiyo maneno yenye Yehova aliambia Israeli na Yuda.

 5 Yehova anasema hivi:

“Tumesikia sauti za kutetemeka;

Kuko woga, na hakuna amani.

 6 Muulize, tafazali, kama mwanaume anaweza kuzaa.

Basi, sababu gani ninaona kila mwanaume mwenye nguvu akishika tumbo lake*

Kama mwanamuke mwenye kuzaa?+

Sababu gani kila uso umegeuka rangi?

 7 Ole! Kwa maana siku hiyo ni yenye kuogopesha.*+

Hakuna ingine kama hiyo,

Wakati wa taabu kwa Yakobo.

Lakini ataokolewa kutokana nayo.”

8 “Na katika siku hiyo,” ni vile Yehova wa majeshi anasema, “nitavunja nira kutoka kwenye shingo yako, na vifungio vyako nitavikata* katika sehemu mbili; na wageni* hawatamufanya* tena kuwa mutumwa wao. 9 Watatumikia Yehova Mungu wao na Daudi mufalme wao, mwenye nitawasimamishia.”+

10 “Na wewe, mutumishi wangu Yakobo, usiogope,” ni vile Yehova anasema,

“Na usiingiwe na woga, Ee Israeli.+

Kwa maana nitakuokoa kutoka mbali

Na uzao wako kutoka katika inchi yao ya utekwa.+

Yakobo atarudia na kuwa na utulivu na bila usumbufu,

Bila mutu wa kuwaogopesha.”+

11 “Kwa maana mimi niko pamoja na wewe,” ni vile Yehova anasema, “ili nikuokoe.

Lakini nitafanya uharibifu mukubwa kati ya mataifa yote kwenye nimekutawanya;+

Hata hivyo, wewe sitakuharibu kabisa.+

Nitakutia nizamu* kwa kiasi chenye kufaa,

Na sitakuacha hata kidogo bila kukupatia azabu.”+

12 Kwa maana Yehova anasema hivi:

“Hakuna matunzo kwa ajili ya kuvunjika kwako.+

Kidonda chako hakiwezi kupona.

13 Hakuna mutu wa kukutetea,

Hakuna njia ya kuponyesha kidonda chako.

Hakuna matunzo kwa ajili yako.

14 Wote wenye kukupenda kwa tamaa wamekusahau.+

Hawakutafute tena.

Kwa maana nimekupiga kwa pigo la adui,+

Kwa azabu ya mutu mwenye hana huruma,

Kwa sababu ya hatia yako kubwa na zambi zako nyingi.+

15 Sababu gani unalia kwa sauti kubwa kwa sababu ya kuvunjika kwako?

Maumivu yako hayawezi kupona!

Kwa sababu ya hatia yako kubwa na zambi zako nyingi+

Nimekutendea vile.

16 Kwa hiyo wale wote wenye kukumeza watamezwa,+

Na maadui wako wote watakamatwa pia na kuenda katika utekwa.+

Wale wenye kukuiba wataibwa,

Na nitatoa wale wote wenye kunyanganya vitu vyako ili wanyanganywe vitu vyao.”+

17 “Lakini nitakurudishia afya ya muzuri na nitaponyesha vidonda vyako,”+ ni vile Yehova anasema.

“Hata kama walikuita mwenye kutengwa:

‘Sayuni, mwenye hakuna mutu yeyote mwenye anamutafuta.’”+

18 Yehova anasema hivi:

“Angalia, ninakusanya watu wenye walikamatwa mateka wa mahema ya Yakobo,+

Na nitasikilia tabenakulo zake huruma.

Muji utajengwa upya juu ya kilima chake,+

Na munara wenye ngome utasimama mahali pake penye kufaa.

19 Na kutoka kwao kutakuwa shukrani na sauti za kicheko.+

Nitawafanya waongezeke, na hawatakuwa watu kidogo;+

Nitawafanya kuwa wengi,*

Na hawatakuwa watu bure.+

20 Wana wake watakuwa kama zamani,

Na mukusanyiko wake utafanywa kuwa imara kabisa mbele yangu.+

Nitashugulika na wakandamizaji wake wote.+

21 Mutu wake mwenye cheo atakuwa mumoja wa watu wake,

Na mutawala wake atatoka katikati yake.

Nitamufanya akaribie, na atanikaribia.”

“Kwa maana tofauti na hilo, ni nani anaweza kupima kunikaribia?”* ni vile Yehova anasema.

22 “Na mutakuwa watu wangu,+ na mimi nitakuwa Mungu wenu.”+

23 Angalia! Zoruba yenye upepo mukali ya Yehova italipuka kwa kasirani kali,+

Zoruba kali yenye kufagia yenye kuzunguka-zunguka juu ya kichwa cha waovu.

24 Kasirani yenye kuwaka ya Yehova haitarudia nyuma

Mupaka wakati atakuwa ametenda na kutimiza makusudi ya moyo wake.+

Katika kipindi cha mwisho cha zile siku ninyi mutaelewa jambo hilo.+

31 “Wakati huo,” ni vile Yehova anasema, “Nitakuwa Mungu kwa familia zote za Israeli, na watakuwa watu wangu.”+

 2 Yehova anasema hivi:

“Watu wenye waliokoka upanga walionyeshwa wema katika jangwa

Wakati Israeli alikuwa anatembea kuenda mahali pake pa kupumuzikia.”

 3 Kutoka mbali Yehova alinitokea na kusema:

“Nimekupenda kwa upendo wa milele.

Ndiyo sababu nimekuvuta kwangu kwa upendo mushikamanifu.*+

 4 Bado nitakujenga upya na wewe utajengwa upya.+

Ee bikira wa Israeli, utachukua tena ngoma zako za kidogo*

Na kuenda ukicheza dansi kwa furaha.*+

 5 Utapanda tena mashamba ya mizabibu katika milima ya Samaria;+

Wapandaji watapanda na kufurahia matunda yake.+

 6 Kwa maana siku itakuja wakati walinzi katika milima ya Efraimu wataita:

‘Musimame, tupande kuenda Sayuni, kwa Yehova Mungu wetu.’”+

 7 Kwa maana Yehova anasema hivi:

“Mumufanyie Yakobo makelele ya furaha.

Mupige vigelegele vya shangwe kwa sababu muko juu ya mataifa.+

Mutangaze jambo hilo; mutoe sifa na kusema,

‘Ee Yehova, okoa watu wako, mabaki ya Israeli.’+

 8 Ninawarudisha kutoka inchi ya kaskazini.+

Nitawakusanya pamoja kutoka sehemu za mbali zaidi za dunia.+

Kati yao kutakuwa kipofu na kilema wa miguu,+

Mwanamuke mwenye mimba na ule mwenye kuzaa, wote pamoja.

Watarudia hapa wakiwa kutaniko kubwa.+

 9 Watakuja wakilia.+

Nitawaongoza wakati watakuwa wanaomba waonyeshwe rehema.

Nitawaongoza kwenye mito midogo* ya maji,+

Kwenye njia tambarare yenye haitafanya wajikwae.

Kwa maana mimi ni Baba ya Israeli, na Efraimu ni muzaliwa wangu wa kwanza.”+

10 Musikie neno la Yehova, ninyi mataifa,

Na mulitangaze kati ya visiwa vyenye kuwa mbali:+

“Ule mwenye alitawanya Israeli atamukusanya pamoja.

Atamuangalia kama vile muchungaji anafanyia kundi lake.+

11 Kwa maana Yehova atamukomboa Yakobo+

Na kumuokoa* kutoka katika mukono wa ule mwenye kuwa na nguvu kuliko yeye.+

12 Watakuja na kupiga vigelegele vya shangwe kwenye nafasi ya juu ya Sayuni+

Na kungaa kwa sababu ya wema wa* Yehova,

Kwa sababu ya nafaka na divai mupya+ na mafuta,

Na kwa sababu ya watoto wa kundi na wa mifugo.+

Watakuwa* kama bustani yenye kunyweshwa maji muzuri,+

Na hawataregea tena hata siku moja.”+

13 “Wakati huo bikira atacheza kwa furaha,

Pia vijana na wanaume wazee wote pamoja.+

Nitageuza maombolezo yao kuwa furaha.+

Nitawafariji na kuwapatia furaha kuliko huzuni yao.+

14 Nitashibisha makuhani* kwa vitu vingi,*

Na watu wangu watashiba wema wangu,”+ ni vile Yehova anasema.

15 “Yehova anasema hivi:

‘Sauti inasikiwa katika Rama,+ maombolezo na kilio cha uchungu:

Raheli analia wana* wake.+

Amekataa kufarijiwa juu ya wana wake,

Kwa sababu hawako tena.’”+

16 Yehova anasema hivi:

“‘Zuia sauti yako usilie na macho yako yasitoe machozi,

Kwa maana kuko zawabu kwa ajili ya utendaji wako,’ ni vile Yehova anasema.

‘Watarudia kutoka katika inchi ya adui.’+

17 ‘Na kuko tumaini kwa ajili ya wakati wako wenye kuja,’+ ni vile Yehova anasema.

‘Wana wako watarudia katika eneo lao wenyewe.’”+

18 “Hakika nimesikia Efraimu akiomboleza,

‘Umenirekebisha, na nimerekebishwa,

Kama kitoto-dume cha ngombe chenye hakikuzoezwa.

Unirudishe, na nitageuka bila kusita,

Kwa maana wewe ni Yehova Mungu wangu.

19 Kwa maana kisha mimi kugeuka nilisikitika;+

Kisha kusaidiwa kuelewa nilipiga paja langu kwa huzuni.

Nilipata haya na kufezeheka,+

Kwa maana nilibeba haya ya ujana wangu.’”

20 “Je, Efraimu haiko mwana mwenye samani kwangu, mutoto mupendwa?+

Kwa maana kila mara wakati ninasema kwa kumukemea, bado ninamukumbuka.

Ndiyo sababu hisia zangu zimechochewa* kwa ajili yake.+

Na hakika nitamusikilia huruma,” ni vile Yehova anasema.+

21 “Ujiwekee alama za barabara,

Na usimamishe nguzo zenye alama ya kuonyesha njia.+

Kazia uangalifu njia kubwa, njia yenye utapita ndani.+

Rudia, Ee bikira wa Israeli, rudia kwenye miji yako hii.

22 Utaendelea kuyumba-yumba mupaka wakati gani, Ee binti mwenye kukosa uaminifu?

Kwa maana Yehova ameumba jambo la mupya katika dunia:

Mwanamuke atafuatilia mwanaume kwa bidii.”

23 Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Watasema tena maneno haya katika inchi ya Yuda na katika miji yake wakati nitakusanya ili kurudisha watu wao wenye walikamatwa mateka: ‘Yehova akubariki, Ee makao ya haki,+ Ee mulima mutakatifu.’+ 24 Na ndani yake Yuda na miji yake yote watakaa wote pamoja, walimaji na wale wenye kuongoza makundi.+ 25 Kwa maana nitashibisha mwenye kuchoka* na kujaza kila mutu mwenye kuregea.”*+

26 Halafu nikaamuka na kufungua macho yangu, na usingizi wangu ulikuwa mutamu kwangu.

27 “Angalia! Siku zinakuja,” ni vile Yehova anasema, “wakati nitapanda nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda kwa mbegu ya* mwanadamu na kwa mbegu ya mifugo.”+

28 “Na kama vile niliwaangalia ili kungoa, kubomoa, kuangusha, kuharibu, na kuumiza,+ ni vile nitawaangalia ili kujenga na kupanda,”+ ni vile Yehova anasema. 29 “Katika siku hizo hawatasema tena, ‘Baba walikula zabibu chachu, lakini meno ya wana ndiyo yalitiwa ukakasi.’*+ 30 Lakini kila mutu atakufa kwa sababu ya kosa lake mwenyewe. Mutu yeyote mwenye atakula zabibu chachu, atatiwa ukakasi kwenye meno yake mwenyewe.”

31 “Angalia! Siku zinakuja,” ni vile Yehova anasema, “wakati nitafanya agano jipya pamoja na nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda.+ 32 Halitakuwa kama lile agano lenye nilifanya pamoja na mababu zao siku yenye nilishika mukono wao ili kuwaongoza kutoka katika inchi ya Misri,+ ‘agano langu lenye walivunja,+ hata kama nilikuwa bwana wao* wa kweli,’ ni vile Yehova anasema.”

33 “Kwa maana hili ndilo agano lenye nitafanya pamoja na nyumba ya Israeli kisha siku hizo,” ni vile Yehova anasema. “Nitatia sheria yangu ndani yao,+ na nitaiandika katika moyo wao.+ Na nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”+

34 “Na hawatafundishana tena kila mutu na jirani yake na kila mutu na ndugu yake, kwa kusema, ‘Mumujue Yehova!’+ kwa maana wote watanijua, kuanzia mudogo zaidi mupaka mukubwa zaidi kati yao,”+ ni vile Yehova anasema. “Kwa maana nitasamehe kosa lao, na sitakumbuka tena zambi yao.”+

35 Yehova anasema hivi:

Yeye mwenye anatoa jua kwa ajili ya mwangaza muchana,

Sheria za mwezi na nyota kwa ajili ya mwangaza usiku,

Yeye mwenye anachafua bahari na kufanya mawimbi yake yakuwe na muchafuko,

Yeye mwenye jina lake ni Yehova wa majeshi:+

36 “‘Kama masharti haya yangeshindwa,’ ni vile Yehova anasema,

‘Ni pale uzao wa Israeli ungeacha kuwa taifa mbele yangu sikuzote.’”+

37 Yehova anasema hivi: “‘Kama mbingu zenye kuwa juu zingeweza kupimwa na misingi ya dunia yenye kuwa chini ichunguzwe, ni pale ningekataa uzao wote wa Israeli kwa sababu ya mambo yote yenye wamefanya,’ ni vile Yehova anasema.”+

38 “Angalia! Siku zinakuja,” ni vile Yehova anasema, “wakati muji utajengwa+ kwa ajili ya Yehova kutoka Munara wa Hananeli+ mupaka Mulango Mukubwa wa Pembe.+ 39 Na kamba ya kupimia+ itaenda moja kwa moja mupaka kwenye kilima cha Garebu, na itazunguka kuelekea Goa. 40 Na bonde lote* la mizoga na la majivu* na matuta yote mupaka Bonde la Kidroni,+ mupaka kwenye pembe ya Mulango Mukubwa wa Farasi+ kuelekea mashariki, itakuwa kitu kitakatifu kwa Yehova.+ Haitangolewa tena hata kidogo wala kubomolewa.”

32 Neno lenye lilikuja kwa Yeremia kutoka kwa Yehova katika mwaka wa kumi (10) wa Mufalme Sedekia wa Yuda, ni kusema, mwaka wa kumi na munane (18) wa Nebukadneza.*+ 2 Wakati huo majeshi ya mufalme wa Babiloni yalikuwa yanazunguka Yerusalemu kwa ajili ya vita, na Yeremia nabii alikuwa amefungwa katika Kiwanja cha Walinzi+ katika nyumba ya mufalme wa Yuda. 3 Kwa maana Mufalme Sedekia wa Yuda alikuwa amemufunga,+ akisema, “Sababu gani unatoa unabii kama huu? Unasema, ‘Yehova anasema hivi: “Nitatia muji huu katika mukono wa mufalme wa Babiloni, na ataukamata,+ 4 na Mufalme Sedekia wa Yuda hataponyoka kutoka kwa Wakaldayo, kwa maana hakika atatiwa katika mukono wa mufalme wa Babiloni, na atasema naye uso kwa uso na kumuona macho kwa macho.”+ 5 ‘Atamupeleka Sedekia Babiloni, na atabakia kule mupaka wakati nitamukazia uangalifu,’ ni vile Yehova anasema. ‘Hata kama munaendelea kupigana vita na Wakaldayo, hamutafanikiwa.’”+

6 Yeremia akasema: “Neno la Yehova limekuja kwangu, na kusema, 7 ‘Angalia, Hanameli mwana wa Shalumu ndugu ya baba yako atakuja kwako na kusema: “Ujinunulie shamba langu lenye kuwa katika Anatoti,+ kwa sababu uko na haki ya kwanza ya kulikomboa.”’”+

8 Hanameli mwana wa ndugu ya baba yangu akakuja kwangu, kama vile Yehova alikuwa amesema, katika Kiwanja cha Walinzi, na akaniambia: “Tafazali nunua shamba langu lenye kuwa kule Anatoti, katika inchi ya Benyamini, kwa maana uko na haki ya kuliriti na kulikomboa. Ujinunulie shamba hilo.” Halafu nikajua kwamba jambo hilo lilikuwa kupitia neno la Yehova.

9 Basi nikanunua shamba lenye lilikuwa Anatoti kutoka kwa Hanameli mwana wa ndugu ya baba yangu. Nikamupimia feza,+ shekeli* saba (7) na vipande kumi (10) vya feza. 10 Kisha nikaandika kwenye karatasi ya mapatano,+ nikaitia muhuri, nikaita mashahidi,+ na nikapima feza katika mizani.* 11 Nikakamata ile karatasi ya mapatano ya kununua, yenye ilitiwa muhuri kulingana na amri na masharti ya kisheria, na pia karatasi ya mapatano yenye iliachwa bila kutiwa muhuri, 12 na nikapana karatasi ya mapatano ya kununua kwa Baruku+ mwana wa Neria+ mwana wa Mahseya mbele ya Hanameli mwana wa ndugu ya baba yangu, wale mashahidi wenye waliandika katika karatasi ya mapatano ya kununua, na Wayahudi wote wenye walikuwa wamekaa katika Kiwanja cha Walinzi.+

13 Sasa nikamuamuru Baruku mbele yao, kwa kusema: 14 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Kamata karatasi hizi za mapatano, karatasi hii ya mapatano ya kununua, yenye ilitiwa muhuri na ile karatasi ingine ya mapatano yenye iliachwa bila kutiwa muhuri, na uzitie katika chombo cha udongo, ili zichungwe kwa wakati murefu.’ 15 Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Nyumba na mashamba na mashamba ya mizabibu vitanunuliwa tena katika inchi hii.’”+

16 Halafu nikasali kwa Yehova kisha kumupatia Baruku mwana wa Neria ile karatasi ya mapatano ya kununua, kwa kusema: 17 “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova! Angalia! Uliumba mbingu na dunia kwa nguvu zako kubwa+ na kwa mukono wako wenye kunyooshwa. Hakuna jambo lenye kuwa la ajabu sana kwako, 18 wewe Mwenye kuonyesha upendo mushikamanifu kwa maelfu, lakini mwenye kulipa kosa la baba kwa* wana wao kisha wao,+ Mungu wa kweli, mwenye kuwa mukubwa na Mwenye nguvu, wewe mwenye jina lako ni Yehova wa majeshi. 19 Wewe ni mukubwa katika shauri* na mwenye nguvu katika matendo,+ wewe mwenye macho yako yanachunguza njia zote za wanadamu,+ ili kumupatia kila mutu kulingana na njia zake na kulingana na mambo yenye anafanya.+ 20 Umefanya katika inchi ya Misri alama na miujiza yenye inajulikana mupaka leo, na hivyo umejifanyia jina katika Israeli na kati ya wanadamu,+ kama leo hii. 21 Na ukatosha watu wako Israeli katika inchi ya Misri, kwa alama, kwa miujiza, kwa mukono wenye nguvu, kwa mukono wenye kunyooshwa, na kwa matendo yenye kuogopesha.+

22 “Kisha wakati fulani ukawapatia inchi hii yenye uliapa kwamba utapatia mababu zao,+ inchi yenye kutiririka maziwa na asali.+ 23 Na wakaingia na kuiriti, lakini hawakutii sauti yako ao kutembea katika sheria yako. Hawakufanya jambo lolote lenye uliwaamuru wafanye, na hivyo ukafanya musiba huu wote uwaangukie.+ 24 Angalia! Watu wamekuja na maboma ya kuzunguka ili kukamata muji,+ na kwa sababu ya upanga,+ njaa, na ugonjwa wa kuambukiza,+ hakika muji utaanguka katika mikono ya Wakaldayo wenye wanaupiga vita; mambo yenye ulisema yametimia yote, kama vile unaona sasa. 25 Lakini umeniambia, Ee Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova, ‘Ujinunulie shamba kwa feza na uite mashahidi,’ hata kama hakika muji utatiwa katika mukono wa Wakaldayo.”

26 Halafu neno la Yehova likakuja kwa Yeremia, na kusema: 27 “Mimi huyu, Yehova, Mungu wa wanadamu wote.* Je, kuko jambo lolote lenye ni la ajabu sana kwangu? 28 Basi Yehova anasema hivi: ‘Angalia, ninatia muji huu katika mukono wa Wakaldayo na katika mukono wa Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni, na ataukamata.+ 29 Na Wakaldayo wenye wanapigana vita na muji huu wataingia na kuchoma muji huu kwa moto na kuuteketeza+ pamoja na nyumba zenye juu ya sehemu zake za juu watu walitoa zabihu kwa Baali na kutolea miungu mingine matoleo ya kinywaji ili kunikasirisha.’+

30 “‘Kwa maana watu wa Israeli na wa Yuda wamefanya mambo ya mubaya tu mbele ya macho yangu, tangu ujana wao na kuendelea;+ watu wa Israeli wanaendelea kunikasirisha kwa kazi ya mikono yao,’ ni vile Yehova anasema. 31 ‘Kwa maana muji huu, tangu siku waliujenga mupaka leo, umekuwa kwangu tu kitu cha kuchochea hasira na kasirani kali,+ na hivyo lazima uondolewe mbele ya uso wangu,+ 32 kwa sababu ya uovu wote wenye watu wa Israeli na wa Yuda wamefanya ili kunikasirisha⁠—​wao, wafalme wao,+ wakubwa wao,+ makuhani wao, manabii wao,+ na watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu. 33 Waliendelea kunigeuzia migongo yao, hapana nyuso zao;+ hata kama nilijaribu kuwafundisha tena na tena,* hakuna hata mumoja wao mwenye alisikiliza ili kupokea nizamu.+ 34 Na waliweka sanamu zao zenye kuchukiza katika nyumba yenye kubeba jina langu, ili kuichafua.+ 35 Zaidi ya hayo, walijenga mahali pa juu pa Baali katika Bonde la Mwana wa Hinomu,*+ ili kupitisha watoto wao wanaume na watoto wao wanamuke katika moto kwa ajili ya Moleki,+ jambo lenye sikukuwa nimewaamuru+ na lenye halijaingia katika moyo wangu* hata kidogo ili kufanya jambo kama hilo lenye kuchukiza, na kufanya Yuda watende zambi.’

36 “Kwa hiyo Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi juu ya muji huu wenye munasema utatiwa katika mukono wa mufalme wa Babiloni kwa upanga, njaa, na ugonjwa wa kuambukiza, 37 ‘Angalia, nitawakusanya pamoja kutoka katika inchi zote kwenye niliwatawanya katika hasira yangu na katika kasirani yangu kali na katika kasirani kubwa,+ na nitawarudisha mahali hapa na kufanya wakae katika usalama.+ 38 Na watakuwa watu wangu, na mimi nitakuwa Mungu wao.+ 39 Na nitawapatia moyo mumoja+ na njia moja ili waniogope sikuzote, kwa faida yao wenyewe na kwa faida ya watoto wao kisha wao.+ 40 Na nitafanya agano la milele pamoja nao,+ kwamba sitageuka na kuacha kuwatendea mema;+ na nitatia woga wangu katika mioyo yao, na hivyo hawatageuka na kuniacha.+ 41 Nitafurahi juu yao ili kuwatendea mema,+ na nitawapanda imara katika inchi hii,+ kwa moyo wangu wote na kwa nafsi* yangu yote.’”

42 “Kwa maana Yehova anasema hivi: ‘Kama vile nimeletea watu hawa musiba huu wote mukubwa, ni vile nitawaletea mema yote* yenye ninawaahidi.+ 43 Na mashamba yatanunuliwa tena katika inchi hii,+ hata kama munasema: “Ni inchi yenye imeachwa yenye haina mwanadamu na munyama, na imetiwa katika mukono wa Wakaldayo.”’

44 “‘Mashamba yatanunuliwa kwa feza, karatasi za mapatano ya kununua zitaandikwa na kutiwa muhuri, na mashahidi wataitwa katika inchi ya Benyamini,+ katika maeneo yenye kuzunguka Yerusalemu, katika miji ya Yuda,+ katika miji ya eneo lenye milima, na katika miji ya inchi tambarare ya chini,+ na katika miji ya kusini, kwa sababu nitarudisha watu wao wenye walikamatwa mateka,’+ ni vile Yehova anasema.”

33 Neno la Yehova likakuja tena kwa Yeremia mara ya pili, wakati alikuwa angali anafungwa katika Kiwanja cha Walinzi,+ na kusema: 2 “Yehova, Mutengenezaji wa dunia, anasema hivi, Yehova mwenye aliiumba na kuifanya kuwa imara kabisa; Yehova ndilo jina lake, 3 ‘Uniite, na mimi nitakujibu na kukuambia kwa utayari mambo makubwa na yenye hayaeleweke yenye haukujua.’”+

4 “Kwa maana Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi kuhusu nyumba za muji huu na nyumba za wafalme wa Yuda zenye zinabomolewa kwa sababu ya maboma ya kuzunguka kwa ajili ya vita na upanga,+ 5 na kuhusu wale wenye wanakuja kupigana na Wakaldayo, na kujaza maeneo haya mizoga ya wale wenye nilipiga na kuua katika hasira yangu na katika kasirani yangu kali, wale wenye uovu wao umenifanya nifiche uso wangu kutoka kwenye muji huu: 6 ‘Angalia, ninamuponyesha na kumupatia afya,+ na nitawaponyesha na kuwafunulia wingi wa amani na kweli.+ 7 Na nitarudisha watu wa Yuda wenye walikamatwa mateka na watu wa Israeli wenye walikamatwa mateka,+ na nitawajenga kama vile nilifanya pale mwanzo.+ 8 Na nitawatakasa kutokana na hatia yote ya zambi zao zenye walinitendea,+ na nitasamehe hatia yote ya zambi zao na makosa yao yenye walinitendea.+ 9 Na atakuwa kwangu jina la furaha, sifa, na uzuri mbele ya mataifa yote ya dunia yenye yatasikia juu ya wema wote wenye ninawapatia.+ Na wataogopa na kutetemeka+ kwa sababu ya wema wote na amani yenye nitamupatia.’”+

10 “Yehova anasema hivi: ‘Mahali hapa kwenye mutasema kuliachwa, kwenye hakuna mwanadamu wala mifugo, katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu zenye zimeachwa ukiwa, bila mwanadamu wala mukaaji wala mifugo, patasikika tena 11 sauti ya furaha na sauti ya shangwe,+ sauti ya bwana-arusi na sauti ya bibi-arusi, sauti ya wale wenye wanasema: “Mumushukuru Yehova wa majeshi, kwa maana Yehova ni mwema;+ upendo wake mushikamanifu unadumu milele!”’+

“‘Wataleta matoleo ya shukrani katika nyumba ya Yehova,+ kwa maana nitarudisha watu wa inchi wenye walikamatwa mateka, kama pale mwanzo,’ ni vile Yehova anasema.”

12 “Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘Katika eneo hili lenye limeachwa, lenye halina mwanadamu ao mifugo, na katika miji yake yote, kutakuwa tena malisho kwa ajili ya wachungaji ili kupumuzisha makundi yao.’+

13 “‘Katika miji ya eneo lenye milima, katika miji ya inchi tambarare ya chini, katika miji ya kusini, katika inchi ya Benyamini, katika maeneo yenye kuzunguka Yerusalemu,+ na katika miji ya Yuda,+ makundi yatapita tena chini ya mikono ya mutu mwenye kuyahesabu,’ ni vile Yehova anasema.”

14 “‘Angalia! Siku zinakuja,’ ni vile Yehova anasema, ‘wakati nitatimiza ahadi ya muzuri yenye nilisema juu ya nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda.+ 15 Katika siku hizo na wakati huo nitachipushia Daudi chipukizi la* haki,+ na atatenda haki na uadilifu* katika inchi.+ 16 Katika siku hizo Yuda ataokolewa+ na Yerusalemu itakaa katika usalama.+ Na ataitwa hivi: Yehova Ni Haki Yetu.’”+

17 “Kwa maana Yehova anasema hivi: ‘Hakutakosa hata kidogo mwanaume wa ukoo wa Daudi mwenye atakaa kwenye kiti cha ufalme cha nyumba ya Israeli,+ 18 na makuhani Walawi hawatakosa hata siku moja mutu wa kusimama mbele yangu ili kutoa matoleo mazima ya kuteketezwa, kuchoma matoleo ya nafaka, na kutoa zabihu.’”

19 Na neno la Yehova likakuja tena kwa Yeremia, na kusema: 20 “Yehova anasema hivi: ‘Kama munaweza kuvunja agano langu juu ya muchana na agano langu juu ya usiku, ili kuzuia muchana na usiku usikuje kwa wakati wake wenye kufaa,+ 21 basi agano langu pamoja na mutumishi wangu Daudi lingeweza kuvunjwa,+ ili asikuwe na mwana mwenye kutawala akiwa mufalme kwenye kiti chake cha ufalme,+ na pia agano langu pamoja na makuhani Walawi, watumishi wangu.+ 22 Kama vile jeshi la mbinguni haliwezi kuhesabiwa na muchanga wa bahari hauwezi kupimwa, ni vile nitafanya uzao wa mutumishi wangu Daudi na Walawi wenye wananitumikia ukuwe mwingi.’”*

23 Na neno la Yehova likakuja tena kwa Yeremia, na kusema: 24 “Je, haukusikia mambo yenye watu hawa wanasema, ‘Yehova atakataa familia mbili zenye alichagua’? Na wanatendea watu wangu mwenyewe bila heshima, na hawawaone tena kuwa taifa.

25 “Yehova anasema hivi: ‘Kama vile hakika nimefanya imara agano langu juu ya muchana na usiku,+ sheria za mbingu na dunia,+ 26 ni vile sitakataa hata siku moja uzao wa* Yakobo na wa mutumishi wangu Daudi, ili nisikamate kutoka kwa uzao wake* watawala juu ya wazao wa* Abrahamu, Isaka, na Yakobo. Kwa maana nitakusanya watu wao wenye walikamatwa mateka+ na kuwasikilia huruma.’”+

34 Neno lenye lilikuja kwa Yeremia kutoka kwa Yehova, wakati Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni na jeshi lake lote na falme zote za dunia zenye kuwa chini ya mamlaka yake na watu wote walikuwa wanapigana vita juu ya Yerusalemu na miji yake yote:+

2 “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Uende na useme na Mufalme Sedekia+ wa Yuda na umuambie: “Yehova anasema hivi: ‘Angalia, ninatia muji huu katika mukono wa mufalme wa Babiloni, na atauteketeza kwa moto.+ 3 Na hautaponyoka kutoka katika mukono wake, kwa maana hakika utakamatwa na kutiwa katika mukono wake.+ Na utamuona Mufalme wa Babiloni macho kwa macho, na atasema na wewe uso kwa uso, na utaenda Babiloni.’+ 4 Hata hivyo, sikia neno la Yehova, Ee Mufalme Sedekia wa Yuda, ‘Yehova anasema hivi juu yako wewe: “Hautakufa kwa upanga. 5 Utakufa kwa amani,+ na watakufanyia sikukuu ya kuchoma manukato kama vile walifanyia baba zako, wafalme wa zamani wenye walikutangulia, na watakuombolezea, ‘Aa, Ee bwana!’ kwa maana ‘nimesema neno hilo,’ ni vile Yehova anasema.”’”’”

6 Kisha Yeremia nabii akamuambia maneno haya yote Mufalme Sedekia wa Yuda katika Yerusalemu, 7 wakati majeshi ya mufalme wa Babiloni yalikuwa yanapiga vita juu ya Yerusalemu na juu ya miji yote ya Yuda yenye ilibakia,+ juu ya Lakishi+ na juu ya Azeka;+ kwa maana hiyo ndiyo tu ilikuwa miji yenye ngome yenye ilibakia kati ya miji ya Yuda.

8 Neno lenye lilikuja kwa Yeremia kutoka kwa Yehova kisha Mufalme Sedekia kufanya agano pamoja na watu wote wenye walikuwa katika Yerusalemu ili kuwatangazia uhuru,+ 9 kwamba kila mutu aachilie huru watumwa wake Waebrania, wanaume na wanamuke, ili mutu yeyote asiendelee kumufanya Muyahudi mwenzake kuwa mutumwa wake. 10 Basi wakubwa wote na watu wote wakatii. Walikuwa wameingia katika agano kwamba kila mutu aachilie huru watumwa wake wanaume na wanamuke na asiendelee tena kuwafanya kuwa watumwa. Wakatii na wakawaacha waende. 11 Hata hivyo, kisha wakati fulani walirudisha watumwa wao wanaume na wanamuke wenye walikuwa wameachilia huru, na wakawalazimisha kurudia katika utumwa. 12 Basi neno la Yehova likakuja kwa Yeremia kutoka kwa Yehova, na kusema:

13 “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Nilifanya agano pamoja na mababu zenu+ katika siku yenye niliwatosha katika inchi ya Misri, kutoka katika nyumba ya utumwa,+ nikisema: 14 “Kwenye mwisho wa miaka saba (7), kila mumoja wenu anapaswa kumuachilia huru ndugu yake Mwebrania mwenye aliuzishwa kwako na amekutumikia miaka sita (6); unapaswa kumuachilia huru.”+ Lakini mababu zenu hawakunisikiliza wala kunitegea masikio yao. 15 Na hivi karibuni* ninyi wenyewe muligeuka na kufanya mambo yenye kuwa sawa mbele ya macho yangu kwa kutangazia wenzenu uhuru, na mukafanya agano mbele yangu katika nyumba yenye kubeba jina langu. 16 Lakini kisha, muligeuka na kuchafua jina langu+ kwa kurudisha watumwa wenu wanaume na wanamuke wenye mulikuwa mumeachilia huru kama vile walitaka,* na mukawalazimisha kurudia katika utumwa.’

17 “Kwa hiyo Yehova anasema hivi: ‘Hamukunitii katika kutangaza uhuru, kila mutu kwa ndugu yake na kwa mwenzake.+ Basi sasa nitawatangazia ninyi uhuru,’ ni vile Yehova anasema, ‘kwa upanga, ugonjwa wa kuambukiza, na njaa,+ na nitawafanya ninyi kuwa kitu cha kuogopesha kwa falme zote za dunia.+ 18 Na ni hivi itafanyika kwa watu wenye walivunja agano langu kwa kukosa kutenda maneno ya agano lenye walifanya mbele yangu wakati walikata kitoto-dume cha ngombe vipande mbili na kupita katikati ya vile vipande,+ 19 ni kusema, wakubwa wa Yuda, wakubwa wa Yerusalemu, maofisa wa makao ya mufalme, makuhani, na watu wote wa inchi wenye walipita katikati ya vile vipande vya kitoto-dume cha ngombe: 20 Nitawatia katika mukono wa maadui wao na katika mukono wa wale wenye wanatafuta kuondoa uzima wao,* na maiti zao zitakuwa chakula cha ndege wa mbinguni na cha wanyama wa dunia.+ 21 Na nitatia Mufalme Sedekia wa Yuda na wakubwa wake katika mukono wa maadui wao na katika mukono wa wale wenye wanatafuta kuondoa uzima wao* na katika mukono wa majeshi ya mufalme wa Babiloni,+ yenye yanaondoka kuwaacha ninyi.’+

22 “‘Angalia, nitatoa agizo,’ ni vile Yehova anasema, ‘na nitawarudisha katika muji huu, na wataupiga vita na kuukamata na kuuteketeza kwa moto;+ na nitafanya miji ya Yuda kuwa eneo lenye limeachwa, bila mukaaji.’”+

35 Neno lenye lilikuja kwa Yeremia kutoka kwa Yehova katika siku za Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda, na kusema: 2 “Uende katika nyumba ya Warekabu+ na useme nao na kuwaleta katika nyumba ya Yehova, katika kimoja cha vyumba vya kukulia chakula;* na uwapatie divai wakunywe.”

3 Basi nikapeleka Yaazania mwana wa Yeremia mwana wa Habasinia, ndugu zake, wana wake wote, na nyumba yote ya Warekabu 4 katika nyumba ya Yehova. Nikawaleta kwenye chumba cha kukulia chakula cha wana wa Hanani mwana wa Igdalia, mutu wa Mungu wa kweli, chenye kilikuwa pembeni ya chumba cha kukulia chakula cha wakubwa chenye kilikuwa juu ya chumba cha kukulia chakula cha Maaseya mwana wa Shalumu mulinzi wa mulango. 5 Kisha nikaweka vikombe na bilauri vyenye kujaa divai mbele ya watu wa nyumba ya Warekabu na kuwaambia: “Mukunywe divai.”

6 Lakini wakasema: “Hatutakunywa divai, kwa sababu Yehonadabu*+ mwana wa Rekabu, babu yetu, alitupatia amri hii: ‘Ninyi ao wana wenu hamupaswe hata siku moja kunywa divai. 7 Na hamupaswe kujenga nyumba, kupanda mbegu, wala kupanda wala kuwa na shamba la mizabibu. Tofauti na hilo, munapaswa kukaa katika mahema sikuzote, ili muishi wakati murefu katika inchi yenye munaishi ndani mukiwa wageni.’ 8 Basi tunaendelea kutii sauti ya Yehonadabu mwana wa Rekabu babu yetu katika mambo yote yenye alituamuru, kwa kutokunywa hata siku moja divai yoyote⁠—​sisi, bibi zetu, watoto wetu wanaume, na watoto wetu wanamuke. 9 Na hatujenge nyumba za kukaa ndani, na hatuna mizabibu wala mashamba wala mbegu. 10 Tunaendelea kuishi katika mahema na kutii mambo yote yenye Yehonadabu* babu yetu alituamuru. 11 Lakini wakati Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni alipanda ili kushambulia inchi,+ tukasema, ‘Mukuje, tuingie ndani ya Yerusalemu ili kuponyoka jeshi la Wakaldayo na la Wasiria,’ na sasa tunaishi katika Yerusalemu.”

12 Na neno la Yehova likakuja kwa Yeremia, na kusema: 13 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Uende na uambie watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu: “Je, hamukuendelea kuchochewa mutii maneno yangu?”+ ni vile Yehova anasema. 14 “Yehonadabu mwana wa Rekabu aliamuru wazao wake wasikunywe divai, na wamefuata maneno yake kwa kutoikunywa mupaka leo, na hivyo wametii agizo la babu yao.+ Hata hivyo, nimesema na ninyi tena na tena,* lakini hamukunitii.+ 15 Na niliendelea kutuma kwenu watumishi wangu wote manabii, nikiwatuma tena na tena,*+ na kusema, ‘Tafazali, murudie, kila mumoja wenu kutoka kwenye njia zenu za uovu,+ na mufanye mambo yenye kuwa sawa! Musifuate miungu mingine na kuitumikia. Halafu mutaendelea kukaa katika inchi yenye niliwapatia ninyi na mababu zenu.’+ Lakini hamukutega sikio lenu wala kunisikiliza. 16 Wazao wa Yehonadabu mwana wa Rekabu wamefuata agizo lenye babu yao aliwapatia,+ lakini watu hawa, hawakunisikiliza.”’”

17 “Kwa hiyo Yehova, Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Angalia, ninaleta juu ya Yuda na juu ya wakaaji wote wa Yerusalemu musiba wote wenye niliwaonya kuuhusu,+ kwa maana nimesema nao, lakini hawakusikiliza, na niliendelea kuwaita, lakini hawakujibu.’”+

18 Na Yeremia akaambia nyumba ya Warekabu: “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Kwa sababu mumetii agizo la babu yenu Yehonadabu na munaendelea kushika maagizo yake yote, na kufanya kabisa mambo yenye aliwaagiza ninyi, 19 Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Hakutakosekana hata siku moja muzao wa Yehonadabu* mwana wa Rekabu mwenye atatumika mbele yangu.”’”

36 Sasa katika mwaka wa ine (4) wa Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda, neno hili lilikuja kwa Yeremia kutoka kwa Yehova, na kusema: 2 “Kamata kitabu cha kukunjwa na uandike ndani yake maneno yote yenye nimekuambia juu ya Israeli na Yuda+ na mataifa yote,+ tangu siku ya kwanza yenye nilisema na wewe katika siku za Yosia mupaka leo.+ 3 Pengine wakati wale wa nyumba ya Yuda watasikia juu ya musiba wote wenye ninakusudia kuleta juu yao, watageuka na kuacha njia zao zenye uovu, ili nisamehe kosa lao na zambi yao.”+

4 Kisha Yeremia akaita Baruku+ mwana wa Neria, na Yeremia akasema maneno yote yenye Yehova alikuwa amemuambia, na Baruku akayaandika katika kile kitabu cha kukunjwa.+ 5 Kisha Yeremia akamuamuru Baruku: “Nimefungwa na siwezi kuingia katika nyumba ya Yehova. 6 Basi wewe ndiye unapaswa kuingia na kusoma kwa sauti kubwa maneno ya Yehova katika kitabu cha kukunjwa chenye uliandika wakati nilikuwa ninasema. Uyasome katika masikio ya watu kwenye nyumba ya Yehova katika siku ya kufunga; basi utayasomea watu wote wa Yuda wenye wanaingia kutoka katika miji yao. 7 Pengine ombi lao la kuomba rehema litamufikia Yehova, na watageuka, kila mumoja kutoka katika njia zake zenye uovu, kwa maana hasira na kasirani kali yenye Yehova ametangaza juu ya watu hawa ni kubwa.”

8 Basi Baruku mwana wa Neria akafanya mambo yote yenye Yeremia nabii alikuwa amemuamuru; akasoma kwa sauti kubwa katika kile kitabu cha kukunjwa maneno ya Yehova kwenye nyumba ya Yehova.+

9 Sasa katika mwaka wa tano (5) wa Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda, katika mwezi wa kenda (9), watu wote katika Yerusalemu na watu wote wenye walikuja katika Yerusalemu kutoka katika miji ya Yuda wakatangaza kufunga mbele ya Yehova.+ 10 Kisha Baruku akasoma kwa sauti kubwa katika kile kitabu cha kukunjwa maneno ya Yeremia kwenye nyumba ya Yehova, katika chumba* cha Gemaria+ mwana wa Shafani+ mwandikaji,* katika kiwanja cha juu, kwenye muingilio wa mulango mukubwa mupya wa nyumba ya Yehova,+ katika masikio ya watu wote.

11 Wakati Mikaya mwana wa Gemaria mwana wa Shafani alisikia maneno yote ya Yehova katika kile kitabu cha kukunjwa, 12 akashuka kuenda kwenye nyumba ya mufalme, kwenye chumba cha mwandishi. Wakubwa* wote walikuwa wamekaa pale: Elishama+ mwandishi, Delaya mwana wa Shemaya, Elnatani+ mwana wa Akbori,+ Gemaria mwana wa Shafani, Sedekia mwana wa Hanania, na wakubwa wengine wote. 13 Mikaya akawaambia maneno yote yenye alikuwa amesikia wakati Baruku alisoma katika kile kitabu cha kukunjwa katika masikio ya watu.

14 Kisha wakubwa wote wakamutuma Yehudi mwana wa Netania mwana wa Shelemia mwana wa Kushi kwa Baruku, na kusema: “Kuja na ulete kitabu cha kukunjwa chenye ulisoma katika masikio ya watu.” Baruku mwana wa Neria akakamata kile kitabu cha kukunjwa katika mukono wake na akaingia kwao. 15 Wakamuambia: “Kaa, tafazali, na utusomee kwa sauti kubwa kitabu hicho cha kukunjwa.” Basi Baruku akawasomea kitabu hicho cha kukunjwa.

16 Sasa wakati tu walisikia maneno hayo yote, wakaangaliana kwa woga, na wakamuambia Baruku: “Hakika tunapaswa kumuambia mufalme maneno haya yote.” 17 Na wakamuuliza Baruku: “Tafazali, utuambie namna uliandika maneno haya yote. Je, yeye ndiye alikuwa anasema?” 18 Baruku akawajibu: “Aliniambia maneno haya yote, na nikayaandika kwa wino katika kitabu hiki cha kukunjwa.” 19 Wakubwa wakamuambia Baruku: “Uende na mujifiche, wewe pamoja na Yeremia, na musiache mutu yeyote ajue kwenye muko.”+

20 Kisha wakaingia kwa mufalme, kwenye kiwanja, na wakaweka kile kitabu katika chumba cha Elishama mwandishi, na wakamuambia mufalme kila kitu chenye walikuwa wamesikia.

21 Basi mufalme akamutuma Yehudi+ akamate kile kitabu cha kukunjwa, na akakileta kutoka katika chumba cha Elishama mwandishi. Yehudi akaanza kukisoma katika masikio ya mufalme na ya wakubwa wote wenye walikuwa wamesimama pembeni ya mufalme. 22 Mufalme alikuwa amekaa katika nyumba ya kipindi cha baridi, katika mwezi wa kenda (9),* na kulikuwa moto wenye kuwaka katika jiko la makaa mbele yake. 23 Kisha Yehudi kusoma mafungu tatu (3) ao ine (4), mufalme alikuwa anakata sehemu hiyo kwa kisu cha mwandishi na kuitupa katika moto wenye ulikuwa unawaka katika jiko, mupaka kitabu chote cha kukunjwa kikaishia katika moto wenye ulikuwa katika jiko. 24 Na hawakusikia woga wowote; mufalme wala watumishi wake wote wenye walisikia maneno hayo yote hawakupasua nguo zao. 25 Hata kama Elnatani,+ Delaya,+ na Gemaria+ walimuomba mufalme asiteketeze kwa moto kile kitabu cha kukunjwa, hakuwasikiliza. 26 Zaidi ya hayo, mufalme akaamuru Yerahmeeli mwana wa mufalme, Seraya mwana wa Azrieli, na Shelemia mwana wa Abdeeli wakamate Baruku mwandishi na Yeremia nabii, lakini Yehova akaendelea kuwaficha.+

27 Na neno la Yehova likakuja tena kwa Yeremia kisha mufalme kuteketeza kile kitabu cha kukunjwa chenye kilikuwa na maneno yenye Baruku alikuwa ameandika wakati aliambiwa na Yeremia,+ na kusema: 28 “Kamata kitabu kingine cha kukunjwa na uandike juu yake maneno yote yaleyale yenye yalikuwa kwenye kile kitabu cha kukunjwa cha kwanza, chenye Mufalme Yehoyakimu wa Yuda aliteketeza kwa moto.+ 29 Na unapaswa kusema hivi juu ya Mufalme Yehoyakimu wa Yuda, ‘Yehova anasema hivi: “Umeteketeza kwa moto kitabu hiki cha kukunjwa na kusema, ‘Sababu gani umeandika juu yake: “Mufalme wa Babiloni atakuja hakika na kuharibu inchi hii na kuondoa kabisa mwanadamu na munyama kutoka ndani yake”?’+ 30 Kwa hiyo Yehova anasema hivi juu ya Mufalme Yehoyakimu wa Yuda: ‘Hatakuwa na mutu yeyote mwenye atakaa kwenye kiti cha ufalme cha Daudi,+ na maiti yake itaachwa inje kwenye joto wakati wa muchana na baridi kali wakati wa usiku.+ 31 Nitamuomba yeye na wazao wake* na watumishi wake watoe hesabu kwa sababu ya kosa lao, na nitaleta juu yao na juu ya wakaaji wa Yerusalemu na juu ya watu wa Yuda musiba wote wenye nilisema juu yao,+ lakini hawakusikiliza.’”’”+

32 Kisha Yeremia akakamata kitabu kingine cha kukunjwa na kukipatia Baruku mwana wa Neria, mwandishi,+ na akiambiwa na Yeremia, akaandika juu yake maneno yote ya kile kitabu cha kukunjwa chenye Mufalme Yehoyakimu wa Yuda alikuwa ameteketeza katika moto.+ Na maneno mengine mengi kama hayo yakaongezwa.

37 Na Mufalme Sedekia+ mwana wa Yosia akaanza kutawala pa nafasi ya Konia*+ mwana wa Yehoyakimu, kwa maana Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni alimufanya kuwa mufalme katika inchi ya Yuda.+ 2 Lakini yeye na watumishi wake na watu wa inchi hawakusikiliza maneno ya Yehova yenye yalisemwa kupitia Yeremia nabii.

3 Na Mufalme Sedekia akatuma Yehukali+ mwana wa Shelemia na Sefania+ mwana wa Maaseya kuhani kwa Yeremia nabii, na kusema: “Tafazali sali kwa ajili yetu kwa Yehova Mungu wetu.” 4 Yeremia alikuwa anatembea huku na huku kwa uhuru kati ya watu, kwa maana walikuwa hawajamutia katika gereza.+ 5 Sasa jeshi la Farao lilikuwa limeondoka Misri,+ na Wakaldayo wenye walikuwa wanazunguka Yerusalemu kwa ajili ya vita wakasikia habari juu yao. Basi wakaondoka mbele ya Yerusalemu.+ 6 Kisha neno la Yehova likakuja kwa Yeremia nabii, na kusema: 7 “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Mumuambie hivi mufalme wa Yuda, mwenye aliwatuma ninyi kwangu ili kuniuliza: “Angalia! Jeshi la Farao lenye linakuja kuwasaidia ninyi litarudia katika inchi yake, Misri.+ 8 Na Wakaldayo watarudia tena na kupiga vita juu ya muji huu na kuukamata na kuuteketeza kwa moto.”+ 9 Yehova anasema hivi: “Musijidanganye* kwa kusema, ‘Hakika Wakaldayo wataenda kutoka kwetu,’ kwa sababu hawataenda. 10 Hata kama mungepiga na kuua jeshi lote la Wakaldayo wenye wanapigana na ninyi kisha kubakie tu watu wao wenye waliumizwa, bado wangesimama kutoka kwenye mahema yao na kuteketeza muji huu kwa moto.”’”+

11 Wakati jeshi la Wakaldayo lilikuwa limeondoka mbele ya Yerusalemu kwa sababu ya jeshi la Farao,+ 12 Yeremia akaondoka Yerusalemu na kuenda kwenye inchi ya Benyamini+ ili apokee fungu lake kule kati ya watu wake. 13 Lakini wakati alifika kwenye Mulango Mukubwa wa Benyamini, ofisa mwenye alikuwa juu ya walinzi, mwenye jina lake lilikuwa Iriya mwana wa Shelemia mwana wa Hanania, akamukamata Yeremia nabii na kusema: “Unakimbia kuenda kwa Wakaldayo!” 14 Lakini Yeremia akasema: “Haiko kweli! Mimi sikimbie kuenda kwa Wakaldayo.” Lakini hakumusikiliza. Basi Iriya akamukamata Yeremia na kumuingiza kwa wakubwa. 15 Wakubwa wakamukasirikia Yeremia,+ na wakamupiga na kumufunga*+ katika nyumba ya Yehonatani mwandishi, yenye ilikuwa imefanywa kuwa gereza. 16 Yeremia alitiwa katika gereza la chini ya udongo,* katika vyumba vyenye ngome, na akakaa kule siku nyingi.

17 Kisha Mufalme Sedekia akatuma aletwe, na mufalme akamuuliza maulizo kwa siri katika nyumba yake.*+ Akauliza, “Je, kuko neno lolote kutoka kwa Yehova?” Yeremia akasema, “Liko!” na akaendelea, “Utatiwa katika mukono wa mufalme wa Babiloni!”+

18 Pia Yeremia akamuambia Mufalme Sedekia: “Namna gani nimekutendea zambi wewe na watumishi wako na watu hawa, na hivyo mumenitia katika gereza? 19 Wako wapi, sasa, manabii wenu wenye waliwatolea ninyi unabii, ‘Mufalme wa Babiloni hatakuja juu yenu ninyi na juu ya inchi hii’?+ 20 Sasa sikiliza, tafazali, Ee bwana wangu mufalme. Tafazali, kubali ombi langu la kuomba rehema. Usinirudishe katika nyumba ya Yehonatani+ mwandishi, ili nisikufie kule.”+ 21 Basi Mufalme Sedekia akaamuru kwamba Yeremia awekwe katika kifungo katika Kiwanja cha Walinzi,+ na alipewa mukate wa muviringo kila siku kutoka kwenye barabara ya watengenezaji wa mikate+ mupaka wakati mikate yote iliisha katika muji.+ Na Yeremia akaendelea kukaa katika Kiwanja cha Walinzi.

38 Sasa Shefatia mwana wa Matani, Gedalia mwana wa Pashuri, Yukali+ mwana wa Shelemia, na Pashuri+ mwana wa Malkiya wakasikia maneno yenye Yeremia alikuwa anaambia watu wote, akisema: 2 “Yehova anasema hivi: ‘Ule mwenye atabakia katika muji huu atakufa kwa upanga, kwa njaa, na kwa ugonjwa wa kuambukiza.+ Lakini ule mwenye atajitia katika mikono ya* Wakaldayo ataendelea kuishi na atapata uzima wake* kama kitu chenye kilichukuliwa katika vita* na ataishi.’+ 3 Yehova anasema hivi: ‘Hakika muji huu utatiwa katika mukono wa jeshi la mufalme wa Babiloni, na ataukamata.’”+

4 Wakubwa wakamuambia mufalme: “Tafazali agiza mutu huyu auawe,+ kwa maana ni vile anaregeza mioyo* ya maaskari wenye kubakia katika muji huu, na pia mioyo ya watu wote, kwa kuwaambia maneno kama hayo. Kwa maana mutu huyu hatafute amani ya watu hawa, lakini musiba wao.” 5 Mufalme Sedekia akajibu: “Muangalie! Iko* katika mikono yenu, kwa maana mufalme hawezi kufanya jambo lolote ili kuwazuia ninyi.”

6 Basi wakakamata Yeremia na kumutupa ndani ya tangi la maji la Malkiya mwana wa mufalme, lenye lilikuwa katika Kiwanja cha Walinzi.+ Wakashusha Yeremia ndani kwa kamba. Sasa ndani ya lile tangi hamukukuwa maji, matope tu, na Yeremia akaanza kuzama katika yale matope.

7 Ebed-meleki+ Mwetiopia, towashi* katika nyumba ya mufalme, akasikia kwamba wamemutia Yeremia ndani ya tangi. Sasa mufalme alikuwa amekaa katika Mulango Mukubwa wa Benyamini,+ 8 basi Ebed-meleki akatoka katika nyumba ya mufalme na akazungumuza na mufalme, na kusema: 9 “Ee bwana wangu mufalme, mambo yenye watu hawa wamemutendea Yeremia nabii ni maovu! Wamemutupa ndani ya tangi la maji, na atakufia ndani kwa sababu ya njaa, kwa maana hakuna mukate wenye kubakia katika muji.”+

10 Kisha mufalme akamuamuru Ebed-meleki Mwetiopia: “Kamata watu makumi tatu (30) pamoja na wewe kutoka mahali hapa, na umukokote Yeremia nabii kutoka katika lile tangi mbele akufe.” 11 Basi Ebed-meleki akakamata wale watu pamoja naye na kuenda ndani ya nyumba ya mufalme mahali kwenye kulikuwa chini ya hazina,+ na wakakamata pale vitambaa fulani vyenye kuzeeka na vipande vya nguo vyenye kuzeeka na wakavishushia Yeremia ndani ya lile tangi kwa kamba. 12 Kisha Ebed-meleki Mwetiopia akamuambia Yeremia: “Tafazali weka vitambaa na vipande vya nguo kati ya makwapa yako na kamba.” Yeremia akafanya vile, 13 na wakamukokota Yeremia inje kwa zile kamba na kumutosha ndani ya lile tangi. Na Yeremia akaendelea kukaa katika Kiwanja cha Walinzi.+

14 Mufalme Sedekia akatuma watu kwa Yeremia ili akuje kwake kwenye muingilio wa tatu (3), wenye kuwa katika nyumba ya Yehova, na mufalme akamuambia Yeremia: “Niko na jambo fulani la kukuuliza. Usinifiche jambo lolote.” 15 Kisha Yeremia akamuambia Sedekia: “Kama ninakuambia, hakika utaniua. Na kama ninakupatia shauri, hautanisikiliza.” 16 Basi Mufalme Sedekia akamuapia Yeremia kwa siri, na kusema: “Kama vile hakika Yehova anaishi, mwenye ametupatia uzima huu,* sitakuua, na sitakutia katika mukono wa watu hawa wenye wanatafuta kuondoa uzima wako.”*

17 Kisha Yeremia akamuambia Sedekia: “Yehova, Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Kama unajitia katika mikono ya* wakubwa wa mufalme wa Babiloni, uzima wako utaokoka,* na muji huu hautateketezwa kwa moto, na wewe na nyumba yako mutaokoka.+ 18 Lakini kama hautajitia katika mikono ya* wakubwa wa mufalme wa Babiloni, muji huu utatiwa katika mukono wa Wakaldayo, na watauteketeza kwa moto,+ na hautaponyoka kutoka katika mukono wao.’”+

19 Kisha Mufalme Sedekia akamuambia Yeremia: “Ninaogopa Wayahudi wenye wamekimbia kuenda kwa Wakaldayo, kwa maana kama ninatiwa katika mukono wao, wanaweza kunitendea bila huruma.” 20 Lakini Yeremia akasema: “Hautatiwa katika mukono wao. Tafazali, tii sauti ya Yehova katika mambo yenye ninakuambia, na mambo yatakuwa muzuri kwako, na utaendelea* kuishi. 21 Lakini kama unakataa kujitia katika mikono yao,* Yehova amenifunulia jambo hili: 22 Angalia! Wanamuke wote wenye kubakia katika nyumba ya mufalme wa Yuda wanatoshwa inje kwa wakubwa wa mufalme wa Babiloni,+ na wanasema,

‘Watu wenye ulitegemea* wamekudanganya na kukushinda.+

Wamefanya muguu wako uzame katika matope.

Sasa wamegeuka na kurudia nyuma.’

23 Na bibi zako wote na wana wako wanawatosha inje kwa Wakaldayo, na hautaponyoka kutoka katika mukono wao, lakini utakamatwa na mufalme wa Babiloni,+ na kwa sababu yako muji huu utateketezwa kwa moto.”+

24 Kisha Sedekia akamuambia Yeremia: “Usiache mutu yeyote ajue kuhusu mambo haya, ili usikufe. 25 Na kama wakubwa wanasikia kwamba nimesema na wewe na wanakuja na kukuambia, ‘Tafazali, utuambie mambo yenye ulimuambia mufalme. Usitufiche jambo lolote, na hatutakuua.+ Mufalme alikuambia nini?’ 26 unapaswa kuwajibu, ‘Nilikuwa ninamuomba mufalme, kwamba asinirudishe katika nyumba ya Yehonatani ili nisikufie kule.’”+

27 Kisha wakati fulani wakubwa wote wakakuja kwa Yeremia na kumuuliza maulizo. Akawaambia kila kitu chenye mufalme alikuwa amemuamuru kusema. Basi hawakusema tena naye, kwa maana hakuna mutu yeyote mwenye alikuwa amesikia yale mazungumuzo. 28 Mupaka siku yenye Yerusalemu ilikamatwa, Yeremia alikaa katika Kiwanja cha Walinzi;+ alikuwa angali pale wakati Yerusalemu ilikamatwa.+

39 Katika mwaka wa kenda (9) wa Mufalme Sedekia wa Yuda, katika mwezi wa kumi (10), Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni na jeshi lake lote walikuja Yerusalemu, na kuizunguka kwa ajili ya vita.+

2 Katika mwaka wa kumi na moja (11) wa Sedekia, katika mwezi wa ine (4), katika siku ya kenda (9) ya mwezi huo, walipasua ukuta wa muji.+ 3 Na wakubwa wote wa mufalme wa Babiloni wakaingia na kukaa katika Mulango Mukubwa wa Katikati,+ ni kusema, Nergal-shareza ule Samgari, Nebo-sarsekimu ule Rabsarisi,* Nergal-shareza ule Rabmagi,* na wakubwa wengine wote wa mufalme wa Babiloni.

4 Wakati mufalme Sedekia wa Yuda na maaskari wote waliwaona, wakakimbia,+ wakatoka katika muji usiku kupitia njia ya bustani ya mufalme, kupitia mulango mukubwa wenye ulikuwa kati ya zile kuta mbili, na wakaendelea kupitia njia ya Araba.+ 5 Lakini jeshi la Wakaldayo likawafuatilia, na wakamufikia Sedekia katika maeneo tambarare ya jangwa la Yeriko.+ Wakamukamata na kumuleta kwa Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni kule Ribla+ katika inchi ya Hamati,+ wakamuhukumu kule. 6 Mufalme wa Babiloni akaagiza wana wa Sedekia wauawe mbele ya macho yake kule Ribla, na mufalme wa Babiloni akaagiza watu wote wenye vyeo wa Yuda wauawe.+ 7 Halafu akapofusha macho ya Sedekia, kisha akamufunga kwa pingu za shaba ili kumupeleka Babiloni.+

8 Kisha Wakaldayo wakateketeza nyumba ya mufalme na nyumba za watu,+ na wakabomoa kuta za Yerusalemu.+ 9 Nebuzaradani+ mukubwa wa walinzi akapeleka katika uhamisho kule Babiloni watu wenye kubakia wenye waliachwa katika muji, wale wenye walikimbia wenye walikuwa wamejiunga naye, na mutu yeyote mwenye alibakia.

10 Lakini Nebuzaradani mukubwa wa walinzi akaacha katika inchi ya Yuda wamoja kati ya watu maskini zaidi, wenye hawakukuwa na kitu chochote. Katika siku hiyo pia aliwapatia mashamba ya mizabibu na mashamba mengine ili wayalime.*+

11 Sasa Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni akamupatia Nebuzaradani mukubwa wa walinzi maagizo haya juu ya Yeremia: 12 “Umuchukue na umuhangaikie; usimuumize, na umupatie kitu chochote chenye anakuomba.”+

13 Basi Nebuzaradani mukubwa wa walinzi, Nebushazbani ule Rabsarisi,* Nergal-shareza ule Rabmagi,* na wakubwa wote wa mufalme wa Babiloni wakatuma watu 14 na wakaleta Yeremia kutoka katika Kiwanja cha Walinzi+ na kumutia katika mukono wa Gedalia+ mwana wa Ahikamu+ mwana wa Shafani+ ili apelekwe kwenye nyumba yake. Basi akaishi pamoja na watu.

15 Wakati Yeremia alikuwa amefungwa katika Kiwanja cha Walinzi,+ neno la Yehova lilikuja kwake, na kusema: 16 “Uende na umuambie Ebed-meleki+ Mwetiopia, ‘Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Angalia, ninatimiza maneno yangu juu ya muji huu kwa ajili ya musiba na hapana kwa ajili ya mema, na katika siku hiyo utaona hilo likitendeka.”’

17 “‘Lakini nitakukomboa katika siku hiyo,’ ni vile Yehova anasema, ‘na hautatiwa katika mukono wa watu wenye unaogopa.’

18 “‘Kwa maana hakika nitakuokoa, na hautaanguka kwa upanga. Utapata uzima wako* kama kitu chenye kilichukuliwa katika vita,*+ kwa sababu ulinitegemea,’+ ni vile Yehova anasema.”

40 Neno lenye lilikuja kwa Yeremia kutoka kwa Yehova kisha Nebuzaradani+ mukubwa wa walinzi kumuachilia huru kutoka Rama.+ Alikuwa amemupeleka kule akiwa amefungwa pingu za mikono, na alikuwa kati ya wale wote wenye walihamishwa wa Yerusalemu na wa Yuda wenye walikuwa wanapelekwa Babiloni. 2 Kisha mukubwa wa walinzi akamukamata Yeremia na kumuambia: “Yehova Mungu wako alitabiri musiba huu juu ya mahali hapa, 3 na Yehova ametimiza hilo kama vile alisema, kwa sababu mulimutendea Yehova zambi na hamukutii sauti yake. Ndiyo sababu jambo hili limewapata ninyi.+ 4 Sasa ninakuachilia huru leo kutoka kwa pingu za mikono zenye zilikuwa kwenye mikono yako. Kama inaonekana muzuri kwako kuja pamoja na mimi Babiloni, kuja, na nitakuhangaikia. Lakini kama hautaki kuja pamoja na mimi Babiloni, usikuje. Angalia, inchi yote iko mbele yako. Uende mahali popote kwenye unachagua.”+

5 Wakati Yeremia alikuwa bado hajageuka, Nebuzaradani akasema: “Rudia kwa Gedalia+ mwana wa Ahikamu+ mwana wa Shafani,+ mwenye mufalme wa Babiloni ameweka juu ya miji ya Yuda, na ukae pamoja naye kati ya watu; ao uende mahali popote kwenye unachagua.”

Kisha mukubwa wa walinzi akamupatia posho la chakula na zawadi na akamuacha aende. 6 Basi Yeremia akaenda kwa Gedalia mwana wa Ahikamu kule Mispa+ na akakaa pamoja naye kati ya watu wenye walibakia katika inchi.

7 Kisha wakati fulani wakubwa wote wa jeshi wenye walikuwa katika eneo la mashamba pamoja na watu wao wakasikia kwamba mufalme wa Babiloni alikuwa amemuweka Gedalia mwana wa Ahikamu juu ya inchi na kwamba alikuwa amemuweka juu ya wanaume, wanamuke, na watoto kati ya watu maskini wa inchi wenye hawakukuwa wamepelekwa Babiloni.+ 8 Basi wakaenda kwa Gedalia kule Mispa.+ Walikuwa Ishmaeli+ mwana wa Netania, Yohanani+ na Yonatani wana wa Karea, Seraya mwana wa Tanhumeti, wana wa Efai Munetofa, na Yezania+ mwana wa Mumaakati, pamoja na watu wao. 9 Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani akawaapia kiapo, wao pamoja na watu wao, na kusema: “Musiogope kutumikia Wakaldayo. Mukae katika inchi na mumutumikie mufalme wa Babiloni, na mambo yatakuwa muzuri kwenu.+ 10 Lakini mimi, nitakaa katika Mispa ili niwawakilishe ninyi kwa* Wakaldayo wenye wanakuja kwetu. Lakini ninyi munapaswa kukusanya divai, matunda ya kipindi cha joto, na mafuta na kuviweka katika vyombo vyenu vya kuwekea na kukaa katika miji yenye ninyi mulichukua.”+

11 Na Wayahudi wote wenye walikuwa katika Moabu, Amoni, na Edomu, na pia wale wenye walikuwa katika inchi zingine zote, wakasikia pia kama mufalme wa Babiloni alikuwa ameacha mabaki katika Yuda na kama alikuwa ameweka juu yao Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani. 12 Basi Wayahudi wote wakaanza kurudia kutoka kila mahali kwenye walikuwa wametawanywa, na wakakuja katika inchi ya Yuda, kwa Gedalia kule Mispa. Na wakakusanya divai na matunda ya kipindi cha joto kwa wingi sana.

13 Yohanani mwana wa Karea na wakubwa wote wa jeshi wenye walikuwa katika eneo la mashamba wakakuja kwa Gedalia kule Mispa. 14 Wakamuambia: “Je, haujue kama Baalisi, mufalme wa Waamoni,+ amemutuma Ishmaeli mwana wa Netania ili akuue?”*+ Lakini Gedalia mwana wa Ahikamu hakuwaamini.

15 Kisha Yohanani mwana wa Karea akamuambia kwa uficho Gedalia katika Mispa: “Ninataka kuenda na kumupiga na kumuua Ishmaeli mwana wa Netania, na hakuna mutu mwenye atajua. Sababu gani akuue,* na sababu gani watu wote wa Yuda wenye walikusanyika kwako watawanyike na mabaki ya Yuda waangamie?” 16 Lakini Gedalia+ mwana wa Ahikamu akamuambia Yohanani mwana wa Karea: “Usifanye vile, kwa maana mambo yenye unasema juu ya Ishmaeli ni uongo.”

41 Katika mwezi wa saba (7) Ishmaeli+ mwana wa Netania mwana wa Elishama, mwenye alikuwa wa ukoo wa kifalme* na mumoja kati ya wakubwa wa mufalme, akakuja pamoja na watu wengine kumi (10) kwa Gedalia mwana wa Ahikamu kule Mispa.+ Wakati walikuwa wanakula chakula pamoja katika Mispa, 2 Ishmaeli mwana wa Netania na wale watu kumi (10) wenye walikuwa pamoja naye wakasimama na kumupiga na kumuua Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani kwa upanga. Kwa hiyo akamuua mutu mwenye mufalme wa Babiloni alikuwa ameweka juu ya inchi. 3 Ishmaeli akapiga na kuua pia Wayahudi wote wenye walikuwa pamoja na Gedalia katika Mispa, na pia maaskari Wakaldayo wenye walikuwa pale.

4 Katika siku ya pili kisha Gedalia kuuawa, mbele mutu yeyote ajue jambo hilo, 5 watu makumi munane (80) wakakuja kutoka Shekemu,+ kutoka Shilo,+ na kutoka Samaria.+ Ndevu zao zilikuwa zimenyolewa, nguo zao zilikuwa zimepasuliwa, walikuwa wamejikata-kata,+ na walikuwa na matoleo ya nafaka na uvumba+ katika mukono wao ili wavilete kwenye nyumba ya Yehova. 6 Basi Ishmaeli mwana wa Netania akatoka Mispa ili kukutana nao, akilia wakati alikuwa anatembea. Wakati alikutana nao, akawaambia: “Mukuje kwa Gedalia mwana wa Ahikamu.” 7 Lakini wakati waliingia katika muji, Ishmaeli mwana wa Netania na watu wake wakawaua na kuwatupa ndani ya tangi la maji.

8 Lakini kulikuwa watu kumi (10) kati yao wenye walimuambia Ishmaeli: “Usituue, kwa maana tuko na madepo yenye kufichwa ya ngano, shayiri, mafuta, na asali katika eneo la mashamba.” Basi akajizuia kuwaua pamoja na ndugu zao. 9 Sasa Ishmaeli akatupa ndani ya tangi kubwa la maji mizoga yote ya watu wenye alikuwa ameua, tangi lenye Mufalme Asa alikuwa ametengeneza kwa sababu ya Mufalme Baasha wa Israeli.+ Hilo ndilo tangi la maji lenye Ishmaeli mwana wa Netania alijaza watu wenye waliuawa.

10 Watu wote wenye walibakia katika Mispa,+ Ishmaeli akawakamata mateka, kutia ndani mabinti wa mufalme na watu wote wenye walibakia katika Mispa, wenye Nebuzaradani mukubwa wa walinzi alikuwa ameweka chini ya ulinzi wa Gedalia+ mwana wa Ahikamu. Ishmaeli mwana wa Netania akawakamata mateka na kuvuka kuenda kwa Waamoni.+

11 Wakati Yohanani+ mwana wa Karea na wakubwa wote wa jeshi wenye walikuwa pamoja naye walisikia uovu wote wenye Ishmaeli mwana wa Netania alikuwa ametenda, 12 wakakamata watu wote na kuenda kupigana na Ishmaeli mwana wa Netania, na wakamupata pembeni ya maji makubwa* katika Gibeoni.

13 Watu wote wenye walikuwa pamoja na Ishmaeli wakafurahi wakati waliona Yohanani mwana wa Karea na wakubwa wote wa jeshi wenye walikuwa pamoja naye. 14 Kisha watu wote wenye Ishmaeli alikuwa amekamata mateka kule Mispa+ wakageuka na kurudia pamoja na Yohanani mwana wa Karea. 15 Lakini Ishmaeli mwana wa Netania pamoja na watu munane (8) kati ya watu wake wakaponyoka kutoka kwa Yohanani na wakaenda kwa Waamoni.

16 Yohanani mwana wa Karea na wakubwa wote wa jeshi wenye walikuwa pamoja naye wakakamata pamoja nao watu wenye walibakia kutoka Mispa, wale wenye walikuwa wameokoa kutoka kwa Ishmaeli mwana wa Netania kisha yeye kumupiga na kumuua Gedalia+ mwana wa Ahikamu. Wakarudisha wanaume, maaskari, wanamuke, watoto, na maofisa wa makao ya mufalme kutoka Gibeoni. 17 Basi wakaenda na kukaa mahali pa kukaa pa Kimhamu pembeni ya Betlehemu,+ wakikusudia kuendelea na kuingia Misri+ 18 kwa sababu ya Wakaldayo. Kwa maana walikuwa wamewaogopa, kwa kuwa Ishmaeli mwana wa Netania alikuwa amemupiga na kumuua Gedalia mwana wa Ahikamu, mwenye mufalme wa Babiloni alikuwa ameweka juu ya inchi.+

42 Kisha wakubwa wote wa jeshi, na Yohanani+ mwana wa Karea, Yezania mwana wa Hoshaya, na watu wote, kuanzia mudogo zaidi mupaka mukubwa zaidi, wakakaribia 2 na kumuambia Yeremia nabii: “Tafazali, sikia ombi letu la kuomba rehema, na usali kwa ajili yetu kwa Yehova Mungu wako, kwa ajili ya mabaki hawa wote, kwa maana kati ya watu wengi ni watu kidogo tu ndio walibakia,+ kama vile unaona. 3 Yehova Mungu wako atuambie njia yenye tunapaswa kutembea ndani na kile tunapaswa kufanya.”

4 Yeremia nabii akawajibu: “Nimewasikia, na ninasali kwa Yehova Mungu wenu kulingana na ombi lenu; na kila neno lenye Yehova anawajibu, nitawaambia. Sitawaficha neno lolote.”

5 Wakamujibu Yeremia: “Yehova akuwe shahidi wa kweli na muaminifu juu yetu ikiwa hatufanye sawasawa kama vile Yehova Mungu wako anatuagiza kupitia wewe. 6 Likuwe jambo la muzuri ao la mubaya, tutatii sauti ya Yehova Mungu wetu, mwenye tunakutuma kwake, ili mambo yakuwe muzuri kwetu kwa sababu tunatii sauti ya Yehova Mungu wetu.”

7 Sasa kisha siku kumi (10) neno la Yehova likakuja kwa Yeremia. 8 Basi akamuita Yohanani mwana wa Karea na wakubwa wote wa jeshi wenye walikuwa pamoja naye na watu wote, kuanzia mudogo zaidi mupaka mukubwa zaidi.+ 9 Akawaambia: “Yehova Mungu wa Israeli, mwenye mulinituma kwake ili kutoa ombi lenu la kuomba rehema mbele yake, anasema hivi: 10 ‘Kwa kweli kama mutabakia katika inchi hii, basi nitawajenga ninyi na sitawabomoa, na nitawapanda na sitawangoa, kwa maana nitasikitika* juu ya musiba wenye nimewaletea.+ 11 Musiogope kwa sababu ya mufalme wa Babiloni, mwenye munaogopa.’+

“‘Musiogope kwa sababu yake,’ ni vile Yehova anasema, ‘kwa maana niko pamoja na ninyi, ili kuwaokoa ninyi na kuwakomboa kutoka katika mukono wake. 12 Na nitawaonyesha ninyi rehema,+ na atawaonyesha ninyi rehema na kuwarudisha kwenye inchi yenu wenyewe.

13 “‘Lakini kama munasema, “Hapana, hatutabakia katika inchi hii!” na munakosa kutii sauti ya Yehova Mungu wenu 14 kwa kusema: “Hapana, tofauti na hilo tutaenda katika inchi ya Misri,+ kwenye hatutaona vita wala kusikia sauti ya baragumu wala kuwa na njaa kwa kukosa mukate; ni kule tutaishi,” 15 basi musikie neno la Yehova, Enyi mabaki ya Yuda. Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Kama mumeazimia kabisa kuenda Misri na munaenda kukaa* kule, 16 basi upanga uleule wenye munaogopa utawafikia kule katika inchi ya Misri, na njaa ileile yenye munaogopa itawafuata kule Misri, na mutakufia kule.+ 17 Na watu wote wenye wameazimia kuenda Misri ili kukaa kule watakufa kwa upanga, kwa njaa, na kwa ugonjwa wa kuambukiza. Hakuna mutu yeyote kati yao mwenye ataokoka wala kuponyoka musiba wenye nitaleta juu yao.”’

18 “Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Kama vile hasira yangu na kasirani yangu kali vilimwangwa juu ya wakaaji wa Yerusalemu,+ ni vile kasirani yangu kali itamwangwa juu yenu kama munaenda Misri, na mutakuwa laana, kitu cha kuogopesha, tukano, na haya,+ na hamutaona mahali hapa tena hata siku moja.’

19 “Yehova amesema juu yenu, Enyi mabaki ya Yuda. Musiende Misri. Munapaswa kujua hakika kwamba nimewaonya leo 20 kwamba kosa lenu litafanya mulipe uzima wenu.* Kwa maana mulinituma kwa Yehova Mungu wenu, mukisema, ‘Sali kwa ajili yetu kwa Yehova Mungu wetu, na utuambie kila jambo lenye Yehova Mungu wetu anasema, na sisi tutalifanya.’+ 21 Na nimewaambia ninyi leo, lakini hamutatii sauti ya Yehova Mungu wenu ao kufanya jambo lolote lenye alinituma niwaambie ninyi.+ 22 Kwa hiyo, mujue hakika kwamba mutakufa kwa upanga, kwa njaa, na kwa ugonjwa wa kuambukiza katika mahali kwenye munatamani kuenda na kukaa.”+

43 Wakati Yeremia alikuwa amemaliza kuambia watu wote maneno haya yote kutoka kwa Yehova Mungu wao, kila neno lenye Yehova Mungu wao alikuwa amemutuma awaambie, 2 Azaria mwana wa Hoshaya, Yohanani+ mwana wa Karea, na watu wote wenye kimbelembele wakamuambia Yeremia: “Mambo yenye unasema ni ya uongo! Yehova Mungu wetu hakukutuma useme, ‘Musiende Misri kukaa kule.’ 3 Lakini Baruku+ mwana wa Neria anakuchochea juu yetu ili kututia katika mukono wa Wakaldayo, ili kutuua ao kutupeleka katika uhamisho Babiloni.”+

4 Basi Yohanani mwana wa Karea na wakubwa wote wa jeshi na watu wote hawakutii sauti ya Yehova kwamba wabakie katika inchi ya Yuda. 5 Tofauti na hilo, Yohanani mwana wa Karea na wakubwa wote wa jeshi wakakamata pamoja nao mabaki wote wa Yuda wenye walikuwa wamerudia kukaa katika inchi ya Yuda kutoka katika mataifa yote kwenye walikuwa wametawanywa.+ 6 Wakakamata wanaume, wanamuke, watoto, mabinti wa mufalme, na kila mutu mwenye* Nebuzaradani+ mukubwa wa walinzi alikuwa ameacha pamoja na Gedalia+ mwana wa Ahikamu+ mwana wa Shafani,+ na pia Yeremia nabii na Baruku mwana wa Neria. 7 Na wakaingia katika inchi ya Misri, kwa maana hawakutii sauti ya Yehova, na wakaenda mupaka Tahpanhesi.+

8 Kisha neno la Yehova likakuja kwa Yeremia katika Tahpanhesi, na kusema: 9 “Kamata katika mukono wako majiwe makubwa, na uyafiche katika saruji* kwenye ngazi ya matofali yenye kuwa kwenye muingilio wa nyumba ya Farao katika Tahpanhesi, na wanaume Wayahudi wakiangalia. 10 Kisha uwaambie, ‘Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Angalia, ninaita Nebukadneza* mufalme wa Babiloni, mutumishi wangu,+ na nitaweka kiti chake cha ufalme juu ya majiwe haya yenye nimeficha, na atanyoosha hema yake ya kifalme juu yake.+ 11 Na ataingia na kupiga inchi ya Misri.+ Mutu yeyote mwenye alikusudiwa pigo lenye kuua atapigwa kwa pigo lenye kuua, na mutu yeyote mwenye alikusudiwa kuenda katika utekwa ataenda katika utekwa, na mutu yeyote mwenye alikusudiwa upanga atapigwa kwa upanga.+ 12 Na nitawasha moto nyumba za* miungu ya Misri,+ na ataiteketeza na kuipeleka ikiwa imetekwa. Atajifunika inchi ya Misri kumuzunguka kama vile muchungaji anajifunika mwenyewe nguo yake, na ataondoka kule kwa amani.* 13 Na atavunja vipande-vipande nguzo za* Bet-shemeshi* katika inchi ya Misri, na atateketeza kwa moto nyumba za* miungu ya Misri.”’”

44 Neno lenye lilikuja kwa Yeremia kwa ajili ya Wayahudi wote wenye walikuwa wanaishi katika inchi ya Misri,+ wale wenye walikuwa wanaishi kule Migdoli,+ Tahpanhesi,+ Nofu,*+ na inchi ya Patrosi,+ na kusema: 2 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Mumeona musiba wote wenye nilileta juu ya Yerusalemu+ na juu ya miji yote ya Yuda, na leo imekuwa mabomoko, bila mukaaji.+ 3 Ni kwa sababu ya mambo maovu yenye walifanya ili kunikasirisha kwa kuenda na kutoa zabihu+ na kutumikia miungu mingine yenye wao hawakukuwa wanajua, wala ninyi wala mababu zenu.+ 4 Niliendelea kutuma kwenu watumishi wangu wote manabii, nikiwatuma tena na tena,* nikisema: “Tafazali musifanye jambo hili lenye kuchukiza lenye ninachukia.”+ 5 Lakini hawakusikiliza wala kutega sikio lao ili kugeuka kutoka kwenye uovu wao kwa kutokutoa zabihu kwa miungu mingine.+ 6 Basi kasirani yangu kali na kasirani yangu zilimwangwa na kuteketeza katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu, na zikakuwa mabomoko na eneo lenye limeachwa, kama vile ziko leo.’+

7 “Na sasa Yehova, Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Sababu gani munajiletea* musiba mukubwa, na hivyo kila mwanaume na mwanamuke, mutoto na mutoto mudogo, wataangamia kutoka Yuda, na kuwaacha ninyi bila mabaki? 8 Sababu gani munikasirishe kwa kazi za mikono yenu kwa kutoa zabihu kwa miungu mingine katika inchi ya Misri kwenye mumeenda kukaa? Mutaangamia na kuwa kitu cha kulaaniwa na kitu cha haya kati ya mataifa yote ya dunia.+ 9 Je, mumesahau matendo maovu ya mababu zenu na matendo maovu ya wafalme wa Yuda+ na matendo maovu ya bibi zao,+ na pia matendo yenu wenyewe maovu na matendo maovu ya bibi zenu,+ yenye yalifanywa katika inchi ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu? 10 Mupaka leo hawakujinyenyekeza,* hawakuonyesha woga wowote,+ na hawakutembea katika sheria yangu na masharti yangu yenye niliweka mbele yenu ninyi na mababu zenu.’+

11 “Kwa hiyo Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Angalia, nimeazimia kuleta musiba juu yenu, kuharibu Yuda yote. 12 Na nitakamata mabaki ya Yuda wenye walikuwa wameazimia kuenda katika inchi ya Misri ili kukaa kule, na wote wataangamia katika inchi ya Misri.+ Wataanguka kwa upanga na kuangamia kwa njaa; kuanzia mudogo zaidi mupaka mukubwa zaidi, watakufa kwa upanga na kwa njaa. Na watakuwa laana, kitu cha kuogopesha, tukano, na kitu cha haya.+ 13 Nitapatia azabu wale wenye kukaa katika inchi ya Misri kama vile nilipatia Yerusalemu azabu, kwa upanga, kwa njaa, na kwa ugonjwa wa kuambukiza.+ 14 Na mabaki ya Yuda wenye wameenda kukaa katika inchi ya Misri hawataponyoka wala kuokoka ili kurudia kwenye inchi ya Yuda. Watatamani* kurudia na kukaa kule, lakini hawatarudia, isipokuwa watu kidogo wenye wataponyoka.’”

15 Wanaume wote wenye walijua kwamba bibi zao walikuwa wanatolea miungu mingine zabihu na bibi wote wenye walikuwa wamesimama pale, wenye walifanyiza kikundi kikubwa, na watu wote wenye walikuwa wanaishi katika inchi ya Misri,+ katika Patrosi,+ wakamujibu Yeremia: 16 “Hatutasikiliza neno lenye umetuambia katika jina la Yehova. 17 Tofauti na hilo, hakika tutafanya kila neno lenye vinywa vyetu vimesema, kutoa zabihu kwa Malkia wa Mbinguni* na kumumiminia matoleo ya kinywaji,+ kama vile sisi, mababu zetu, wafalme wetu, na wakubwa wetu walifanya katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu wakati tulikuwa tumeshiba mukate na tulikuwa na hali ya muzuri, wakati hatukuona musiba wowote. 18 Tangu wakati tuliacha kutoa zabihu kwa Malkia wa Mbinguni* na kumumiminia matoleo ya kinywaji, tumekosa kila kitu na tumeangamia kwa upanga na kwa njaa.”

19 Wanamuke wakaongeza: “Na wakati tulikuwa tunatoa zabihu kwa Malkia wa Mbinguni* na kumumiminia matoleo ya kinywaji, je, tulitengeneza keki za zabihu zenye zilifanywa kwa umbo yake na kumumwangia matoleo ya kinywaji bila ruhusa ya bwana zetu?”

20 Kisha Yeremia akaambia watu wote, wanaume na bibi zao na watu wote wenye walikuwa wanasema naye: 21 “Zabihu zenye ninyi, mababu zenu, wafalme wenu, wakubwa wenu, na watu wa inchi walitoa katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu+⁠—​Yehova alizikumbuka na zikaingia katika moyo wake! 22 Mwishowe Yehova hangeweza tena kuvumilia mazoea yenu maovu na mambo yenye kuchukiza yenye mulikuwa mumefanya, na inchi yenu ikakuwa mahali kwenye kuliachwa ukiwa, kitu cha kuogopesha na laana, bila mukaaji, kama vile iko leo.+ 23 Ni kwa sababu mumetoa zabihu hizi na kwa sababu mumemutendea Yehova zambi kwa kukosa kutii sauti ya Yehova na kukosa kufuata sheria yake, kanuni zake, na vikumbusho vyake ndiyo sababu musiba huu umekuja juu yenu, kama vile hali iko leo.”+

24 Yeremia akaendelea kuambia watu wote na wanamuke wote: “Musikie neno la Yehova, ninyi wote wa Yuda wenye kuwa katika inchi ya Misri. 25 Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Mambo yenye ninyi na bibi zenu mumesema kwa vinywa vyenu, mumeyatimiza kwa mikono yenu, kwa maana mulisema: “Hakika tutatimiza naziri zetu za kutoa zabihu kwa Malkia wa Mbinguni* na kumumwangia matoleo ya kinywaji.”+ Hakika ninyi wanamuke mutatimiza naziri zenu na kufanya naziri zenu.’

26 “Kwa hiyo musikie neno la Yehova, ninyi wote wa Yuda wenye kuishi katika inchi ya Misri: ‘“Muangalie, ninaapa kwa jina langu mwenyewe lenye ni kubwa,” ni vile Yehova anasema, “kwamba jina langu halitaitwa tena katika kiapo na mutu yeyote wa Yuda+ katika inchi yote ya Misri mwenye anasema, ‘Kama vile hakika Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anaishi!’+ 27 Sasa ninawaangalia ili kuleta musiba na hapana jambo la muzuri;+ watu wote wa Yuda katika inchi ya Misri watakufa kwa upanga na kwa njaa, mupaka wakati hawatakuwa tena.+ 28 Watu kidogo tu ndio wataponyoka upanga na kurudia kutoka katika inchi ya Misri kuenda katika inchi ya Yuda.+ Kisha mabaki wote wa Yuda wenye walikuja katika inchi ya Misri ili kukaa kule watajua ni neno la nani limetimia, langu ao lao!”’”

29 “‘Na hii ndiyo alama kwenu,’ ni vile Yehova anasema, ‘kwamba nitawapatia ninyi azabu mahali hapa, ili mujue kwamba maneno yenye nilisema ya kuahidi musiba juu yenu hakika yatatimia. 30 Yehova anasema hivi: “Angalia, ninatia Farao Hofra, mufalme wa Misri, katika mukono wa maadui wake na katika mukono wa wale wenye wanatafuta kuondoa uzima wake,* kama vile nilitia Mufalme Sedekia wa Yuda katika mukono wa Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni, mwenye alikuwa adui yake na mwenye alitaka kuondoa uzima wake.”’”*+

45 Hili ndilo neno lenye Yeremia nabii alimuambia Baruku+ mwana wa Neria wakati aliandika katika kitabu maneno haya yenye yalisemwa na Yeremia+ katika mwaka wa ine (4) wa Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda:

2 “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi juu yako wewe, Baruku: 3 ‘Umesema: “Ole wangu, kwa maana Yehova ameongeza huzuni kwenye maumivu yangu! Nimechoka kwa sababu ya kilio changu cha maumivu, na sikupata mahali pa kupumuzikia.”’

4 “Umuambie, ‘Yehova anasema hivi: “Angalia! Kile chenye nimejenga ninakibomoa, na kile chenye nimepanda ninakingoa⁠—inchi yote.+ 5 Lakini unajitafutia* mambo makubwa. Acha kutafuta mambo hayo.”’

“‘Kwa maana, niko karibu kuleta musiba juu ya miili yote,’*+ ni vile Yehova anasema, ‘na kila mahali kwenye unaweza kuenda, nitakupatia uzima wako* kama kitu chenye kilichukuliwa katika vita.’”*+

46 Hili ndilo neno la Yehova kwa Yeremia nabii kuhusu mataifa:+ 2 Kwa ajili ya Misri,+ kuhusu jeshi la Farao Neko+ mufalme wa Misri, mwenye alikuwa pembeni ya Muto Efrati na mwenye alishindwa kule Karkemishi na Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni katika mwaka wa ine (4) wa Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda:

 3 “Mutayarishe ngao zenu za kidogo* na ngao zenu za mukubwa,

Na muende kwenye pigano.

 4 Mufunge farasi lijamu* na mupande, ninyi wapanda-farasi.

Musimame na muvae kofia zenu za chuma.

Munoe mikuki na muvae makoti yenu ya chuma.

 5 ‘Sababu gani ninawaona wakiwa na woga?

Wanarudia nyuma, wapiganaji-vita wao wamepondwa.

Wamekimbia kwa woga, wapiganaji-vita wao hawakugeuka.

Kuko woga kuzunguka pande zote,’ ni vile Yehova anasema.

 6 ‘Wenye ni wepesi hawawezi kukimbia, na wapiganaji-vita hawawezi kuponyoka.

Kule kaskazini, kwenye sehemu ya pembeni ya Muto Efrati,

Wamejikwaa na kuanguka.’+

 7 Ni nani huyu mwenye anapanda kama Muto Nile,

Kama mito yenye kujaa sana maji?

 8 Misri inapanda kama vile Muto Nile,+

Kama mito yenye kujaa sana maji,

Na inasema, ‘Nitapanda na kufunika dunia.

Nitaharibu muji na wale wenye kukaa ndani.’

 9 Mupande, ninyi farasi!

Muende kiwazimu, ninyi magari!

Wapiganaji-vita waende,

Kushi na Putu, wenye wanatumia ngao,+

Na Ludimu,+ wenye wanatumia na kupinda* upinde.+

10 “Siku hiyo ni ya Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, Yehova wa majeshi, siku ya kisasi ili kulipiza kisasi juu ya maadui wake. Na upanga utameza na kushiba na kujijaza damu yao, kwa maana Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, Yehova wa majeshi, iko* na zabihu* katika inchi ya kaskazini pembeni ya Muto Efrati.+

11 Panda mupaka Gileadi uchukue zeri,+

Ee binti bikira wa Misri.

Umeongeza bure tu matunzo yako,

Kwa maana hakuna matunzo kwa ajili yako.+

12 Mataifa yamesikia juu ya haya yako,+

Na kilio chako kimejaza inchi.

Kwa maana mupiganaji-vita anajikwaa juu ya mupiganaji-vita,

Na wote wawili wanaanguka pamoja.”

13 Hili ndilo neno lenye Yehova alimuambia Yeremia nabii juu ya kuja kwa Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni ili kupiga inchi ya Misri:+

14 “Muliseme katika Misri, mulitangaze katika Migdoli.+

Mulitangaze katika Nofu* na katika Tahpanhesi.+

Museme, ‘Musimame na mujitayarishe,

Kwa maana upanga utameza kukuzunguka pande zote.

15 Sababu gani watu wako wenye nguvu wamefagiliwa mbali?

Walishindwa kusimama,

Kwa maana Yehova amewasukuma chini.

16 Wanajikwaa na kuanguka kwa wingi.

Wanaambiana:

“Musimame! Turudie kwa watu wetu na kwenye inchi yetu

Kwa sababu ya upanga wenye kuua sana.”’

17 Kule wametangaza,

‘Farao mufalme wa Misri ni makelele yenye hayana maana

Mwenye ameacha nafasi ipite.’*+

18 ‘Kama vile hakika ninaishi,’ ni vile Mufalme anasema, mwenye jina lake ni Yehova wa majeshi,

‘Yeye* ataingia kama Tabori+ kati ya milima

Na kama Karmeli+ pembeni ya bahari.

19 Tayarisha muzigo wako kwa ajili ya uhamisho,

Ee binti mwenye kukaa Misri.

Kwa maana Nofu* itakuwa kitu cha kuogopesha;

Itawashwa moto* na kuachwa bila mukaaji.+

20 Misri ni kama kitoto-dike cha ngombe chenye kupendeza,

Lakini mainzi wenye kuuma watakuja kumushambulia kutoka kaskazini.

21 Hata maaskari wake wenye walikodiwa wenye kuwa katikati yake ni kama vitoto-dume vya ngombe vyenye kunenepa,

Lakini wao pia wamegeuka na kukimbia pamoja.

Walishindwa kusimama,+

Kwa maana siku ya musiba wao imekuja juu yao,

Wakati wao wa kuombwa hesabu.’

22 ‘Sauti yake ni kama ya nyoka mwenye kukimbia,

Kwa maana wanamufuata kwa nguvu, wakiwa na mashoka,

Kama watu wenye kukata miti.*

23 Watakata pori lake,’ ni vile Yehova anasema, ‘hata kama lilionekana haliwezi kuingiwa ndani.

Kwa maana ni wengi kuliko nzige, hawana hesabu.

24 Binti ya Misri atapatishwa haya.

Atatiwa katika mukono wa watu wa kaskazini.’+

25 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema: ‘Sasa ninakaza uangalifu wangu juu ya Amoni+ kutoka No,*+ juu ya Farao, juu ya Misri, juu ya miungu yake,+ na juu ya wafalme wake⁠—​ndiyo, juu ya Farao na wote wenye wanamutegemea.’+

26 “‘Na nitawatia katika mukono wa wale wenye wanatafuta kuondoa uzima wao,* katika mukono wa Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni+ na watumishi wake. Lakini kisha ataikaliwa kama zamani,’ ni vile Yehova anasema.+

27 ‘Na wewe, mutumishi wangu Yakobo, usiogope,

Na usiogopeshwe, Ee Israeli.+

Kwa maana, nitakuokoa kutoka mbali

Na uzao wako* kutoka inchi yao ya utekwa.+

Yakobo atarudia na kuwa na utulivu bila usumbufu,

Bila mutu wa kuwaogopesha.+

28 Basi wewe mutumishi wangu Yakobo, usiogope,’ ni vile Yehova anasema, ‘kwa maana niko pamoja na wewe.

Nitafanya uharibifu mukubwa kati ya mataifa yote kwenye nilikutawanya,+

Lakini wewe sitakuharibu kabisa.+

Nitakutia nizamu* kwa kiasi chenye kufaa,+

Lakini sitakuacha hata kidogo bila kukupatia azabu.’”

47 Hili ndilo neno la Yehova kwa Yeremia nabii kuhusu Wafilisti,+ mbele ya Farao kupiga Gaza. 2 Yehova anasema hivi:

“Angalia! Maji yanakuja kutoka kaskazini.

Yatakuwa muto wenye kujaa sana.

Na yataleta mafuriko juu ya inchi na juu ya kila kitu chenye kuwa ndani yake,

Muji na wale wenye kukaa ndani.

Watu watalia kwa sauti kubwa,

Na kila mutu mwenye anaishi katika inchi ataomboleza.

 3 Kutokana na sauti ya kishindo cha kwato* za farasi-dume wake,

Kutokana na mulio wa magari yake ya vita

Na kunguruma kwa magurudumu* yake,

Baba hawatageuka hata kwa ajili ya wana wao,

Kwa maana mikono yao inaregea,

 4 Kwa sababu siku yenye inakuja itaharibu Wafilisti wote;+

Itaondoa katika Tiro+ na katika Sidoni+ kila musaidizi mwenye kubakia.

Kwa maana Yehova ataharibu Wafilisti,

Wenye wamebakia kutoka kisiwa cha Kaftori.*+

 5 Upara* utakuja Gaza.

Ashkeloni imenyamazishwa.+

Ee mabaki ya bonde lao tambarare,*

Utaendelea kujikata-kata mupaka wakati gani?+

 6 “Aa! Upanga wa Yehova!+

Hautanyamaza mupaka wakati gani?

Rudia ndani ya mufuko wako wa upanga.

Pumuzika na unyamaze.

 7 Namna gani unaweza kukaa kimya

Wakati Yehova ameuamuru?

Juu ya Ashkeloni na eneo la pembeni ya bahari,+

Ni pale amechagua ukuwe.”

48 Kwa ajili ya Moabu,+ Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi:

“Ole wa Nebo,+ kwa maana ameharibiwa!

Kiriataimu+ amepatishwa haya na kukamatwa.

Kimbilio salama limepatishwa* haya na kuvunjwa-vunjwa.+

 2 Hawasifu tena Moabu.

Katika Heshboni+ wamepanga anguko lake:

‘Mukuje, tumumalize asikuwe taifa.’

Wewe pia, Ee Madmeni, unapaswa kukaa kimya,

Kwa maana upanga unakufuata.

 3 Kuko sauti ya kilio kutoka Horonaimu,+

Ya uharibifu na anguko kubwa.

 4 Moabu amevunjwa.

Watoto wake wanalia kwa sauti kubwa.

 5 Kwenye mupando wa Luhiti wanaendelea kulia wakati wanapanda.

Na kwenye njia yenye kushuka kutoka Horonaimu wanasikia vilio vya taabu kwa sababu ya musiba.+

 6 Mukimbie, muponyoke ili kuokoa uzima wenu!*

Munapaswa kuwa kama muti wa muberoshi katika jangwa.

 7 Kwa sababu unategemea kazi zako na hazina zako,

Wewe pia utakamatwa.

Na Kemoshi+ ataenda katika uhamisho,

Pamoja na makuhani wake na wakubwa wake.

 8 Mwenye kuharibu atakuja katika kila muji,

Na hakuna muji wenye utaponyoka.+

Bonde* litaangamia,

Na inchi tambarare* itaharibiwa, kama vile Yehova amesema.

 9 Muwekee Moabu alama,

Kwa maana wakati atakuwa mabomoko atakimbia,

Na miji yake itakuwa kitu cha kuogopesha,

Bila mukaaji.+

10 Alaaniwe mutu mwenye anatimiza kazi ya Yehova kwa uzembe!

Alaaniwe mutu mwenye anazuia upanga wake usimwange damu!

11 Wamoabu hawakusumbuliwa tangu ujana wao,

Kama divai yenye imetulia kwenye machicha.*

Hawakumwangwa kutoka chombo kimoja kuenda kingine,

Na hawakuenda katika uhamisho hata siku moja.

Ndiyo sababu onjo lao limebakia lilelile,

Na harufu yao haikubadilika.

12 “‘Kwa hiyo angalia! siku zinakuja,’ ni vile Yehova anasema, ‘wakati nitatuma watu wawapindue. Watawapindua na kumwanga kile chenye kuwa ndani ya vyombo vyao, na watavunja mitungi yao mikubwa vipande-vipande. 13 Na Wamoabu watapatishwa haya kwa sababu ya Kemoshi, kama vile nyumba ya Israeli imepatishwa haya kwa sababu ya Beteli, yenye ilikuwa tegemeo lao.+

14 Namna gani munapima kusema: “Sisi ni wapiganaji-vita wenye nguvu, tayari kwa ajili ya pigano”?’+

15 ‘Moabu ameharibiwa,

Miji yake imeshambuliwa,+

Na vijana wao wazuri zaidi wameuawa,’+

Ni vile Mufalme anasema, yeye mwenye jina lake ni Yehova wa majeshi.+

16 Musiba juu ya Wamoabu utakuja karibuni,

Na anguko lao linakaribia haraka.+

17 Wale wote wenye kuwazunguka watawasikitikia,

Wale wote wenye wanajua jina lao.

Muwaambie, ‘Namna fimbo yenye nguvu imevunjwa, fimbo ya uzuri!’

18 Shuka kutoka kwenye utukufu wako,

Na ukae katika kiu,* Ee binti mwenye kukaa Diboni,+

Kwa maana mwenye kuharibu wa Moabu amekuja juu yako,

Na atafanya sehemu zako zenye ngome kuwa mabomoko.+

19 Simama pembeni ya barabara na uangalie, wewe mukaaji wa Aroeri.+

Uliza mwanaume mwenye kukimbia na mwanamuke mwenye kuponyoka, ‘Kumetokea nini?’

20 Moabu amepatishwa haya na ameingiwa na woga.

Muomboleze na mulie kwa sauti kubwa.

Mutangaze katika Arnoni+ kwamba Moabu ameangamizwa.

21 “Hukumu imekuja katika inchi tambarare,*+ juu ya Holoni, Yahazi,+ na Mefaati;+ 22 juu ya Diboni,+ Nebo,+ na Bet-diblataimu; 23 juu ya Kiriataimu,+ Bet-gamuli, na Bet-meoni;+ 24 juu ya Kerioti+ na Bosra; na juu ya miji yote ya inchi ya Moabu, yenye kuwa mbali na yenye kuwa karibu.

25 ‘Nguvu za Moabu zimekatwa;*

Mukono wake umevunjwa,’ ni vile Yehova anasema.

26 ‘Mumuleweshe,+ kwa maana amejiinua juu ya Yehova.+

Moabu anajigeuza-geuza katika matapiko yake,

Na ni kitu cha kuchekelewa.

27 Je, Israeli hakukuwa kwako kitu cha kuchekelewa?+

Je, alipatikana kati ya wezi,

Ili utikise kichwa chako na kusema mubaya juu yake?

28 Mutoke katika miji na mukae kwenye mwamba, ninyi wakaaji wa Moabu,

Na mukuwe kama njiwa mwenye anajenga chicha* kwenye kuta za bonde.’”

29 “Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu⁠—​iko* na majivuno sana⁠—​

Juu ya kujisifu kwake, kiburi chake, majivuno yake, na kujiinua kwa moyo wake.”+

30 “‘Ninajua kasirani yake kali,’ ni vile Yehova anasema,

‘Lakini maneno yake yenye hayana maana yatakuwa bure.

Hayatafanya kitu chochote.

31 Ndiyo sababu nitaomboleza juu ya Moabu,

Kwa ajili ya Moabu yote nitalia kwa sauti kubwa

Na kuombolezea watu wa Kir-heresi.+

32 Kwa kilio chenye kupita kilio kwa ajili ya Yazeri,+

Nitalia kwa sababu yako, Ee muzabibu wa Sibma.+

Machipukizi yako yenye kujaa majani yamevuka bahari.

Yamefika mupaka kwenye bahari, mupaka Yazeri.

Juu ya matunda yako ya kipindi cha joto na mavuno yako ya zabibu

Mwenye kuharibu ameshuka.+

33 Kushangilia na kufurahi vimeondolewa katika shamba la matunda

Na katika inchi ya Moabu.+

Nimefanya divai iache kutiririka kutoka katika kikamulio cha divai.

Hakuna mutu mwenye atakanyanga akipiga vigelegele vya furaha.

Vigelegele vitakuwa vigelegele vya namna ingine.’”+

34 “‘Kuko kilio kutoka Heshboni+ mupaka Eleale.+

Wanapandisha sauti yao mupaka Yahazi,+

Kutoka Soari mupaka Horonaimu+ mupaka Eglat-shelishiya.

Hata maji ya Nimrimu yataachwa.+

35 Nitamaliza katika Moabu,’ ni vile Yehova anasema,

‘Mutu mwenye kuleta toleo mahali pa juu

Na mutu mwenye kutoa zabihu kwa mungu wake.

36 Ndiyo sababu moyo wangu utaombolezea* Moabu kama filimbi,*+

Na moyo wangu utaombolezea* watu wa Kir-heresi kama filimbi.*

Kwa maana utajiri wenye ametokeza utaangamia.

37 Kwa maana kila kichwa kiko na upara,+

Na ndevu zote zimekatwa.

Kuko mikato kwenye kila mukono,+

Na kuko nguo za magunia kwenye viuno vyao!’”+

38 “‘Kwenye sehemu zote za juu za nyumba za Moabu

Na katika viwanja vyake vyote vya watu wote,

Kuko maombolezo tu.

Kwa maana nimevunja Moabu

Kama mutungi wenye ulitupwa,’ ni vile Yehova anasema.

39 ‘Namna ameogopa! Muomboleze!

Namna Moabu amegeuza mugongo wake katika haya!

Moabu amekuwa kitu cha kuchekelewa,

Kitu cha kuogopesha kwa wote wenye kumuzunguka.’”

40 “Kwa maana Yehova anasema hivi:

‘Angalia! Kama vile tai mwenye anashuka chini,+

Atanyoosha mabawa yake juu ya Moabu.+

41 Miji itakamatwa,

Na ngome zake zitachukuliwa.

Katika siku hiyo moyo wa wapiganaji-vita wa Moabu

Utakuwa kama moyo wa mwanamuke mwenye kuzaa.’”

42 “‘Na Moabu ataharibiwa ili asikuwe kikundi cha watu,+

Kwa maana amejiinua juu ya Yehova.+

43 Woga na shimo na mutego viko mbele yako,

Ee mukaaji wa Moabu,’ ni vile Yehova anasema.

44 ‘Mutu yeyote mwenye kukimbia woga ataanguka katika shimo,

Na mutu yeyote mwenye kupanda kutoka katika shimo atanaswa katika mutego.’

‘Kwa maana nitaleta juu ya Moabu mwaka wa azabu yao,’ ni vile Yehova anasema.

45 ‘Katika kivuli cha Heshboni, wale wenye kukimbia watasimama bila nguvu.

Kwa maana moto utatoka katika Heshboni

Na mwali wa moto utatoka katikati ya Sihoni.+

Utateketeza paji la uso wa Moabu

Na mufupa wa kichwa wa wana wa fujo.’+

46 ‘Ole wako, Ee Moabu!

Watu wa Kemoshi+ wameangamia.

Kwa maana wana wako wamekamatwa mateka,

Na mabinti wako wamepelekwa katika uhamisho.+

47 Lakini nitakusanya watu wa Moabu wenye walikamatwa mateka katika kipindi cha mwisho cha zile siku,’ ni vile Yehova anasema.

‘Hukumu juu ya Moabu inaishia hapa.’”+

49 Kwa ajili ya Waamoni,+ Yehova anasema hivi:

“Je, Israeli hana wana:

Je, hana muriti?

Sababu gani Malkamu+ ameriti Gadi?+

Na sababu gani watu wake wanakaa katika miji ya Israeli?”

 2 “‘Kwa hiyo muangalie! siku zinakuja,’ ni vile Yehova anasema,

‘Wakati nitafanya mulio wa vita usikiwe* juu ya Raba+ ya Waamoni.+

Atakuwa kilima chenye kimeachwa ukiwa,

Na miji yake ya pembeni-pembeni* itawashwa moto.’

‘Na Israeli atachukua wale wenye walimuchukua,’+ ni vile Yehova anasema.

 3 ‘Omboleza, Ee Heshboni, kwa maana Ai ameharibiwa!

Mulie kwa sauti kubwa, Enyi miji ya pembeni-pembeni ya Raba.

Muvae nguo za magunia.

Muomboleze na muende huku na huku kati ya mazizi ya majiwe,*

Kwa maana Malkamu ataenda katika uhamisho,

Pamoja na makuhani wake na wakubwa wake.+

 4 Sababu gani unajisifu juu ya mabonde,*

Juu ya eneo lako tambarare lenye kutiririka, Ee binti mwenye kukosa uaminifu,

Mwenye kutegemea hazina zake,

Na mwenye kusema: “Ni nani atanishambulia?”’”

 5 “‘Angalia, ninaleta jambo la kuogopesha juu yako,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, Yehova wa majeshi anasema,

‘Kutoka kwa wale wote wenye kukuzunguka.

Utatawanywa kila upande,

Na hakuna mwenye atakusanya wale wenye kukimbia.’”

 6 “‘Lakini kisha nitakusanya watu wa Waamoni wenye walikamatwa mateka,’ ni vile Yehova anasema.”

7 Kwa ajili ya Edomu, Yehova wa majeshi anasema hivi:

“Je, hakuna tena hekima yoyote katika Temani?+

Je, shauri la muzuri limeangamia kutoka kwa wale wenye kuwa na uelewaji?

Je, hekima yao imeoza?

 8 Mukimbie, mugeuke!

Muende mukae katika sehemu za chini kabisa, Enyi wakaaji wa Dedani!+

Kwa maana nitaleta musiba juu ya Esau

Wakati muda wangu wa kumukazia uangalifu utafika.

 9 Kama wakusanya-zabibu wangeingia kwako,

Je, hawangeacha zabibu fulani nyuma kwa ajili ya kukusanywa?

Kama wezi wangeingia usiku,

Wangetokeza uharibifu kwa kiasi tu chenye wanataka.+

10 Lakini nitamuvua Esau akuwe uchi.

Nitafunua mahali pake pa kujificha,

Ili asiweze kujificha.

Watoto wake na ndugu zake na majirani wake wataharibiwa,+

Na hatakuwa tena.+

11 Acha watoto wako wenye hawana baba,

Na nitawalinda wazima,

Na wajane wako watanitegemea.”

12 Kwa maana Yehova anasema hivi: “Angalia! Kama wale wenye hawakuhukumiwa kunywa kikombe wanapaswa kukikunywa, je, wewe utaachwa bila kupewa azabu kabisa? Hautaachwa bila kupewa azabu, kwa maana unapaswa kukikunywa.”+

13 “Kwa maana nimeapa kwa nafsi yangu mwenyewe,” ni vile Yehova anasema, “kwamba Bosra itakuwa kitu cha kuogopesha,+ kitu cha haya, uharibifu, na laana; na miji yake yote itakuwa mabomoko ya kudumu.”+

14 Nimesikia habari kutoka kwa Yehova,

Mujumbe ametumwa kati ya mataifa, akisema:

“Mujikusanye pamoja na mumushambulie;

Mujitayarishe kwa ajili ya pigano.”+

15 “Kwa maana angalia! Nimekufanya kuwa mudogo sana kati ya mataifa,

Mwenye kuzarauliwa kati ya wanadamu.+

16 Mutetemeko wenye ulitokeza umekudanganya,

Kimbelembele cha moyo wako,

Ee wewe mwenye kukaa katika makimbilio ya mwamba,

Mwenye kukaa kwenye kilima kirefu zaidi.

Hata kama unajenga chicha yako* juu kama tai,

Nitakushusha kutoka pale,” ni vile Yehova anasema.

17 “Na Edomu anapaswa kuwa kitu cha kuogopesha.+ Kila mutu mwenye kupita pembeni yake ataangalia kwa woga na kupiga muluzi kwa sababu ya mapigo yake yote. 18 Kama vile katika uharibifu wa Sodoma na Gomora na wa miji yake jirani,”+ Yehova anasema, “hakuna mutu mwenye ataishi pale, na hakuna mutu mwenye atakaa pale.+

19 “Angalia! Mutu fulani atapanda ili kushambulia malisho yenye kuwa salama kama simba+ kutoka kwenye miti mingi midogo-midogo* pembeni ya Yordani, lakini kwa wakati kidogo nitamufanya akimbie kutoka kwake. Na nitaweka juu yake ule mwenye kuchaguliwa. Kwa maana ni nani mwenye kuwa kama mimi, na ni nani mwenye atanipinga? Ni muchungaji gani mwenye anaweza kusimama mbele yangu?+ 20 Kwa hiyo musikie, Enyi watu, uamuzi wenye* Yehova amefanya juu ya Edomu na mambo yenye amefikiria juu ya wakaaji wa Temani:+

Hakika wenye kuwa wadogo wa kundi watakokotwa.

Atafanya makao yao yakuwe ukiwa kwa sababu yao.+

21 Kwa sauti ya kuanguka kwao, dunia imetetemeka.

Kuko kilio!

Sauti imesikiwa mupaka kwenye Bahari Nyekundu.+

22 Angalia! Atapanda na kushuka kama vile tai,+

Na atanyoosha mabawa yake juu ya Bosra.+

Katika siku hiyo moyo wa wapiganaji-vita wa Edomu

Utakuwa kama moyo wa mwanamuke mwenye kuzaa.”

23 Kwa ajili ya Damasko:+

“Hamati+ na Arpadi wamepatishwa haya,

Kwa maana wamesikia habari ya mubaya.

Wanayeyuka kwa woga.

Kuko musukosuko katika bahari wenye hauwezi kutulizwa.

24 Damasko amepoteza bidii.

Amegeuka ili kukimbia, lakini ameshikwa na woga.

Taabu na maumivu vimemushika,

Kama mwanamuke mwenye kuzaa.

25 Namna gani muji wenye sifa haukuachwa,

Muji wa furaha?

26 Kwa maana vijana wake wataanguka katika viwanja vyake vya watu wote,

Na maaskari wote wataangamia katika siku hiyo,” ni vile Yehova wa majeshi anasema.

27 “Nitawasha moto ukuta wa Damasko,

Na utateketeza minara yenye ngome ya Ben-hadadi.”+

28 Kwa ajili ya Kedari+ na falme za Hasori, zenye Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni alipiga, Yehova anasema hivi:

“Musimame, mupande kuenda Kedari,

Na muharibu wana wa Mashariki.

29 Mahema yao na makundi yao yatachukuliwa,

Vitambaa vyao vya mahema na mali zao zote.

Ngamia wao watachukuliwa,

Na watawalalamikia, ‘Kuko woga pande zote!’”

30 “Mukimbie, muende mbali!

Muende na mukae katika sehemu za chini kabisa, Enyi wakaaji wa Hasori,” ni vile Yehova anasema.

“Kwa maana Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni ametunga mbinu juu yenu,

Na amefanya mupango juu yenu.”

31 “Musimame, mupande ili kushambulia taifa lenye kuwa na amani,

Lenye kukaa kwa usalama!” ni vile Yehova anasema.

“Halina milango wala mapingo; wanaishi peke yao.

32 Ngamia wao watanyanganywa,

Na mifugo yao mingi itakuwa vitu vyenye vinachukuliwa katika vita.

Nitawatawanya kwenye kila upepo,*

Wale wenye wanakata nywele zao kwenye vipaji vya nyuso,+

Na nitaleta musiba wao kutoka kila upande,” ni vile Yehova anasema.

33 “Na Hasori atakuwa pango la mbweha,

Mahali kwenye kumeachwa ukiwa sikuzote.

Hakuna mutu mwenye ataishi kule,

Na hakuna mutu mwenye atakaa ndani yake.”

34 Hili ndilo neno la Yehova lenye lilikuja kwa Yeremia nabii kuhusu Elamu+ kwenye mwanzo wa utawala wa Mufalme Sedekia+ wa Yuda: 35 “Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘Angalia, ninavunja upinde wa Elamu,+ chanzo cha* nguvu zao. 36 Nitaleta juu ya Elamu zile pepo ine (4) kutoka kwenye miisho ine ya mbingu, na nitawatawanya kwenye pepo hizi zote. Hakutakuwa taifa kwenye watu wa Elamu wenye walitawanywa hawataenda.’”

37 “Nitavunja-vunja Waelamu mbele ya maadui wao na mbele ya wale wenye wanatafuta kuchukua uzima wao;* na nitaleta musiba juu yao, kasirani yangu yenye kuwaka,” ni vile Yehova anasema. “Na nitatuma upanga uwafuate mupaka wakati nitakuwa nimewaharibu.”

38 “Na nitaweka kiti changu cha ufalme katika Elamu,+ na nitaharibu kutoka pale mufalme na wakubwa,” ni vile Yehova anasema.

39 “Lakini katika kipindi cha mwisho cha zile siku, nitakusanya watu wa Elamu wenye walikamatwa mateka,” ni vile Yehova anasema.

50 Neno lenye Yehova alisema kuhusu Babiloni,+ kuhusu inchi ya Wakaldayo, kupitia Yeremia nabii:

 2 “Museme jambo hilo kati ya mataifa na mulitangaze.

Muinue alama* na mulitangaze.

Musifiche jambo lolote!

Museme, ‘Babiloni amekamatwa.+

Beli amepatishwa haya.+

Merodaki ameingiwa na woga.

Sanamu zake zimepatishwa haya.

Sanamu zake zenye kuchukiza* zimeingiwa na woga.’

 3 Kwa maana taifa limekuja juu yake kutoka kaskazini.+

Linafanya inchi yake kuwa kitu cha kuogopesha;

Hakuna mutu mwenye kukaa ndani yake.

Mwanadamu na pia munyama wamekimbia;

Wameenda zao.”

4 “Katika siku hizo na wakati huo,” ni vile Yehova anasema, “watu wa Israeli na watu wa Yuda watakuja pamoja.+ Watalia wakiwa wanatembea,+ na watamutafuta pamoja Yehova Mungu wao.+ 5 Watauliza njia ya kuenda Sayuni, nyuso zao zikiwa zimeelekezwa upande huo,+ na kusema, ‘Mukuje na tujiunge na Yehova katika agano la milele lenye halitasahauliwa.’+ 6 Watu wangu wamekuwa kundi la kondoo wenye walipotea.+ Wachungaji wao wenyewe waliwafanya wapotee.+ Waliwapeleka kwenye milima, wameenda kutoka mulima mupaka kilima. Wamesahau mahali pao pa kupumuzikia. 7 Wale wote wenye wanawapata wamewameza,+ na maadui wao wamesema, ‘Hatuna hatia, kwa sababu walitenda zambi juu ya Yehova, juu ya makao ya haki na tumaini la mababu zao, Yehova.’”

 8 “Mukimbie kutoka katikati ya Babiloni,

Mutoke katika inchi ya Wakaldayo,+

Na mukuwe kama wanyama wenye kuongoza mbele ya kundi.

 9 Kwa maana angalia, ninaamusha na kuleta juu ya Babiloni

Mukusanyiko wa mataifa makubwa kutoka katika inchi ya kaskazini.+

Watakuja juu yake wakiwa wamejipanga kwa ajili ya vita;

Kutoka pale atakamatwa.

Mishale yao ni kama ya mupiganaji-vita

Yenye inatokeza kufiwa na watoto;+

Hairudie bila matokeo.

10 Ukaldayo utakuwa kitu chenye kinachukuliwa katika vita.+

Wote wenye wanakamata kutoka kwake vitu vyenye vinachukuliwa katika vita watashiba kabisa,”+ ni vile Yehova anasema.

11 “Kwa maana muliendelea kufurahi,+ muliendelea kushangilia

Wakati mulikuwa munanyanganya uriti wangu mwenyewe.+

Kwa maana muliendelea kukanyanga kama kitoto-dike cha ngombe katika majani,

Na muliendelea kulia kama farasi-dume.

12 Mama yenu amepatishwa haya.+

Ule mwenye aliwazaa ninyi amekata tamaa.

Muangalie! Yeye ndiye mudogo zaidi kati ya mataifa,

Nyika yenye haina maji na jangwa.+

13 Kwa sababu ya kasirani kali ya Yehova watu hawatakaa ndani yake;+

Atabakia ukiwa kabisa.+

Mutu yeyote mwenye kupita pembeni ya Babiloni ataangalia kwa woga

Na kupiga muluzi kwa sababu ya mapigo yake yote.+

14 Mukuje juu ya Babiloni mukiwa mumejipanga kwa ajili ya vita kila upande,

Ninyi wote wenye kupinda* upinde.

Mumupige mishale, musiache mushale wowote,+

Kwa maana amemutendea Yehova zambi.+

15 Mufanye makelele ya vita juu yake kila upande.

Amejitia katika mikono ya maadui.*

Nguzo zake zimeanguka, kuta zake zimebomolewa,+

Kwa maana ni kisasi cha Yehova.+

Mujilipizie kisasi juu yake.

Mumutendee kama vile ametenda.+

16 Muondoe mupandaji wa mbegu katika Babiloni

Na ule mwenye kutumia mundu* wakati wa mavuno.+

Kwa sababu ya upanga wenye kuua sana, kila mutu atarudia kwa watu wake mwenyewe,

Kila mutu atakimbilia katika inchi yake mwenyewe.+

17 “Watu wa Israeli ni kondoo wenye walitawanyika.+ Simba wamewatawanya.+ Kwanza mufalme wa Ashuru aliwameza;+ kisha Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni akatafuna mifupa yao.+ 18 Kwa hiyo Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Angalia, nitamutendea mufalme wa Babiloni na inchi yake kama vile nilimutendea mufalme wa Ashuru.+ 19 Na nitarudisha Israeli kwenye malisho yake,+ na atakula majani kwenye Karmeli na kwenye Bashani,+ na kwenye milima ya Efraimu+ na ya Gileadi+ atashiba.’”*

20 “Katika siku hizo na wakati huo,” ni vile Yehova anasema,

“Hatia ya Israeli itatafutwa,

Lakini hakutakuwa yoyote,

Na zambi za Yuda hazitapatikana,

Kwa maana nitasamehe wale wenye nitaacha wabakie.”+

21 “Panda ili kushambulia inchi ya Merataimu na kushambulia wakaaji wa Pekodi.+

Acha wauawe na kuharibiwa kabisa,”* ni vile Yehova anasema.

“Fanya yote yenye nimekuamuru.

22 Kuko sauti ya vita katika inchi,

Musiba mukubwa.

23 Namna nyundo* ya chuma ya dunia yote imekatwa na kuvunjwa!+

Namna Babiloni amekuwa kitu cha kuogopesha kati ya mataifa!+

24 Nimekuwekea mutego, na umekamatwa, Ee Babiloni,

Na haukujua hilo.

Ulipatikana na kukamatwa,+

Kwa maana Yehova ndiye ulipinga.

25 Yehova amefungua depo yake,

Na analeta inje silaha za kasirani yake kali.+

Kwa maana Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, Yehova wa majeshi, iko* na kazi

Katika inchi ya Wakaldayo.

26 Mukuje kumushambulia kutoka sehemu za mbali.+

Mufungue madepo yake.+

Mumurundike kama marundo ya nafaka.

Mumuharibu kabisa.+

Asikuwe na mutu yeyote mwenye kubakia.

27 Muue ngombe-dume wake wote wadogo;+

Washuke kuenda kwenye machinjo.

Ole wao, kwa maana siku yao imekuja,

Wakati wao wa kuombwa watoe hesabu!

28 Kuko sauti ya wale wenye kukimbia,

Wale wenye kuponyoka kutoka inchi ya Babiloni,

Ili kutangaza katika Sayuni kisasi cha Yehova Mungu wetu,

Kisasi kwa ajili ya hekalu lake.+

29 Muite wapiga-mishale ili washambulie Babiloni,

Wote wenye kupinda* upinde.+

Mupige kambi kumuzunguka pande zote; musiache mutu yeyote aponyoke.

Mumulipe kulingana na matendo yake.+

Mumutendee kama vile ametenda.+

Kwa maana ametenda kwa majivuno juu ya Yehova,

Juu ya Mutakatifu wa Israeli.+

30 Basi vijana wake wataanguka katika viwanja vyake vya watu wote,+

Na maaskari wake wote wataangamia* katika siku hiyo,” ni vile Yehova anasema.

31 “Angalia! Nitapigana na wewe,+ Ee mwenye kuwa kichwa-nguvu,”+ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, Yehova wa majeshi anasema,

“Kwa maana siku yako inapaswa kuja, wakati nitakuomba utoe hesabu.

32 Wewe, Ee mwenye kuwa kichwa-nguvu, utajikwaa na kuanguka,

Hakutakuwa mutu wa kukusimamisha.+

Na nitawasha moto miji yako,

Na utateketeza kila kitu chenye kukuzunguka.”

33 Yehova wa majeshi anasema hivi:

“Watu wa Israeli na Yuda wanakandamizwa,

Na wale wote wenye kuwakamata mateka wamewashika.+

Wamekataa kuwaachilia waende.+

34 Lakini Mukombozi wao ni mwenye nguvu.+

Yehova wa majeshi ndilo jina lake.+

Bila shaka atatetea kesi yao ya hukumu,+

Ili kupumuzisha inchi+

Na kuvuruga wakaaji wa Babiloni.”+

35 “Kuko upanga juu ya Wakaldayo,” ni vile Yehova anasema,

“Juu ya wakaaji wa Babiloni na juu ya wakubwa wake na juu ya watu wake wenye hekima.+

36 Kuko upanga juu ya wale wenye kuongea maneno yenye hayana maana,* na watatenda kipumbavu.

Kuko upanga juu ya wapiganaji-vita wake, na wataingiwa na woga.+

37 Kuko upanga juu ya farasi wao na magari yao ya vita,

Na juu ya watu wote wa mataifa mbalimbali wenye kuchangamana wenye kuwa katikati yake,

Na watakuwa kama wanamuke.+

Kuko upanga juu ya hazina zake, na zitanyanganywa.+

38 Kuko uharibifu juu ya maji yake, na yatakaushwa.+

Kwa maana ni inchi ya sanamu za kuchongwa,+

Na kwa sababu ya maono yao yenye kuogopesha wanaendelea kutenda kiwazimu.

39 Kwa hiyo, viumbe vya jangwa vitakaa pamoja na wanyama wenye kufanya makelele,

Na mbuni watakaa ndani yake.+

Hatakaliwa tena hata siku moja,

Na hatakuwa tena mahali pa kukaa kwa vizazi vyote.”+

40 “Kama vile Mungu aliharibu Sodoma na Gomora+ na miji yake jirani,”+ ni vile Yehova anasema, “hakuna mutu mwenye ataishi pale, na hakuna mutu mwenye atakaa pale.+

41 Angalia! Watu wanaingia kutoka kaskazini;

Taifa kubwa na wafalme wakubwa+ watainuliwa

Kutoka sehemu za mbali zaidi za dunia.+

42 Wanatumia upinde na mukuki mudogo.+

Ni wakali na hawataonyesha rehema.+

Sauti yao ni kama bahari yenye kuvuma,+

Wakiwa wamepanda farasi wao.

Kama mutu mumoja, wamejipanga kwa ajili ya vita juu yako, Ee binti ya Babiloni.+

43 Mufalme wa Babiloni amesikia habari juu yao,+

Na mikono yake imeregea.+

Ameshikwa na uchungu,

Maumivu kama ya mwanamuke mwenye kuzaa.

44 “Angalia! Mutu fulani atapanda ili kushambulia malisho yenye kuwa salama kama simba kutoka kwenye miti mingi midogo-midogo* pembeni ya Yordani, lakini kwa wakati kidogo nitawafanya wakimbie kutoka katika inchi. Na nitaweka juu ya inchi hiyo ule mwenye kuchaguliwa.+ Kwa maana ni nani mwenye kuwa kama mimi, na ni nani mwenye atanipinga? Ni muchungaji gani mwenye anaweza kusimama mbele yangu?+ 45 Kwa hiyo musikie, Enyi watu, uamuzi wenye* Yehova amefanya juu ya Babiloni+ na mambo yenye amefikiria juu ya inchi ya Wakaldayo.

Hakika wenye kuwa wadogo wa kundi watakokotwa.

Atafanya makao yao yakuwe ukiwa kwa sababu yao.+

46 Kutokana na sauti ya kukamatwa kwa Babiloni, dunia itatetemeka,

Na kilio kitasikiwa kati ya mataifa.”+

51 Yehova anasema hivi:

“Angalia, ninaamusha upepo wenye kuharibu

Juu ya Babiloni+ na juu ya wakaaji wa Leb-kamai.*

 2 Nitatuma wenye kupepua Babiloni,

Na watamupepua na kufanya inchi yake kuwa wazi;

Watakuja juu yake kwenye pande zote katika siku ya musiba.+

 3 Mupiga-mishale asipinde* upinde wake.

Na mutu yeyote asisimame akiwa amevaa koti yake ya chuma.

Musionyeshe huruma yoyote kwa vijana wake.+

Muharibu jeshi lake lote.

 4 Na wataanguka wakiwa wameuawa katika inchi ya Wakaldayo,

Wakiwa wametobolewa kwa mukuki katika barabara zake.+

 5 Kwa maana Israeli na Yuda hawakufanywa kuwa wajane na Mungu wao, na Yehova wa majeshi.+

Lakini inchi yao* imejaa hatia kwa maoni ya Mutakatifu wa Israeli.

 6 Mukimbie kutoka katikati ya Babiloni,

Na mukimbie ili kuokoa uzima wenu.*+

Musiangamie kwa sababu ya kosa lake.

Kwa maana ni wakati wa kisasi cha Yehova.

Anamulipa kulingana na yenye ametenda.+

 7 Babiloni amekuwa kikombe cha zahabu katika mukono wa Yehova;

Alilewesha dunia yote.

Mataifa yamekunywa kwenye divai yake;+

Ndiyo sababu mataifa yamepatwa na wazimu.+

 8 Babiloni ameanguka kwa kushitukia na amevunjika.+

Muomboleze kwa ajili yake!+

Mulete zeri kwa ajili ya maumivu yake; pengine anaweza kupona.”

 9 “Tulijaribu kuponyesha Babiloni, lakini hakupona.

Mumuache na tuende, kila mumoja kwenye inchi yake.+

Kwa maana hukumu yake imefika mupaka mbinguni;

Iko juu kama mawingu.+

10 Yehova ametutendea haki.+

Mukuje, tueleze katika Sayuni kazi ya Yehova Mungu wetu.”+

11 “Munoe mishale;+ muchukue ngao za muviringo.*

Yehova amechochea roho ya wafalme wa Wamedi,+

Kwa sababu anakusudia kuharibu Babiloni.

Kwa maana hiki ndicho kisasi cha Yehova, kisasi kwa ajili ya hekalu lake.

12 Muinue alama*+ juu ya kuta za Babiloni.

Muimarishe ulinzi, muweke walinzi.

Mutayarishe wale wenye watavizia.

Kwa maana Yehova amefanya mupango,

Na atatimiza kile chenye ameahidi juu ya wakaaji wa Babiloni.”+

13 “Ee mwanamuke mwenye kukaa juu ya maji mengi,+

Mwenye hazina nyingi,+

Mwisho wako umefika, mwisho wako wa* kupata faida.+

14 Yehova wa majeshi ameapa kwa nafsi yake,

‘Nitakujaza watu, watu wengi kama nzige,

Na watapiga vigelegele vya ushindi juu yako.’+

15 Yeye ndiye Mutengenezaji wa dunia kwa nguvu zake,

Ule mwenye alifanya imara inchi yenye kuzaa kwa hekima yake+

Na mwenye alitandika mbingu kwa uelewaji wake.+

16 Wakati anafanya sauti yake isikike,

Maji yenye kuwa mbinguni yanakuwa na muvurugo,

Na anafanya mawingu yapande* kutoka kwenye miisho ya dunia.

Anatokeza umeme wa radi* kwa ajili ya mvua,

Na anatosha upepo katika madepo yake.+

17 Kila mutu anatenda kwa kukosa akili na bila ujuzi.

Kila fundi wa chuma atapatishwa haya kwa sababu ya sanamu ya kuchongwa;+

Kwa maana sanamu yake ya chuma* ni uongo,

Na hakuna roho* ndani yazo.+

18 Hizo ni udanganyifu,*+ kazi ya muzaha.

Wakati siku ya kuziomba zitoe hesabu itakuja, zitaangamia.

19 Fungu la Yakobo haliko kama vitu hivyo,

Kwa maana Yeye ndiye alifanya kila kitu,

Hata fimbo ya uriti wake.+

Yehova wa majeshi ndilo jina lake.”+

20 “Wewe ni gongo* kwangu, silaha kwa ajili ya vita,

Kwa maana nitakutumia kuvunja mataifa.

Nitakutumia ili kuharibu falme.

21 Nitakutumia ili kuvunja farasi na mupandaji wake.

Nitakutumia ili kuvunja gari la vita na mupandaji wake.

22 Nitakutumia ili kuvunja mwanaume na mwanamuke.

Nitakutumia ili kuvunja muzee na kijana mudogo mwanaume.

Nitakutumia ili kuvunja kijana mwanaume na mwanamuke.

23 Nitakutumia ili kuvunja muchungaji na kundi lake.

Nitakutumia ili kuvunja mulimaji na kundi lake la wanyama.

Nitakutumia ili kuvunja magavana na watawala-wasaidizi.

24 Na nitalipa Babiloni na wakaaji wote wa Ukaldayo

Kwa sababu ya uovu wote wenye wametenda katika Sayuni mbele ya macho yenu,”+ ni vile Yehova anasema.

25 “Angalia, nitapigana na wewe,+ Ee mulima wenye uharibifu,” ni vile Yehova anasema,

“Wewe mwenye kuharibu dunia yote.+

Nitanyoosha mukono wangu juu yako na kukuviringisha kutoka kwenye miamba

Na kukufanya kuwa mulima wenye uliteketezwa kwa moto.”

26 “Watu hawatakamata kutoka kwako jiwe la pembe wala jiwe la musingi,

Kwa sababu utakuwa ukiwa milele,”+ ni vile Yehova anasema.

27 “Muinue alama* katika inchi.+

Mupige baragumu kati ya mataifa.

Muweke* mataifa ili yapigane naye.

Muite falme za Ararati ili zipigane naye,+ Mini, na Ashkenazi.+

Muweke juu yake ofisa mwandikishaji.

Mufanye farasi wapande kama nzige wenye kujaa miiba.

28 Muweke* mataifa ili yapigane naye,

Wafalme wa Umedi,+ magavana wake na watawala wake wote wasaidizi

Na inchi zote zenye wanatawala.

29 Na dunia itatetemeka na kutikisika,

Kwa maana mawazo ya Yehova juu ya Babiloni yatatimizwa

Ili kufanya inchi ya Babiloni kuwa kitu cha kuogopesha, bila mukaaji.+

30 Wapiganaji-vita wa Babiloni wameacha kupigana.

Wanakaa katika ngome zao.

Nguvu zao zimeisha.+

Wamekuwa kama wanamuke.+

Nyumba zake zimewashwa moto.

Mapingo* yake yamevunjwa.+

31 Muleta-habari mumoja anakimbia kukutana na muleta-habari mwingine,

Na mujumbe mumoja kukutana na mujumbe mwingine,

Ili kujulisha mufalme wa Babiloni kwamba muji wake umekamatwa kila upande,+

32 Kwamba nafasi za kuvukia zimeshikwa,+

Kwamba mashua* za mafunjo* zimeteketezwa kwa moto,

Na kwamba maaskari wameingiwa na woga.”

33 Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi:

“Binti ya Babiloni ni kama kiwanja cha kupigia-pigia nafaka.

Ni wakati wa kumukanyangia chini ili akuwe mugumu.

Karibuni wakati wa mavuno utakuja kwa ajili yake.”

34 “Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni amenimeza;+

Amenivuruga.

Ameniweka chini kama chombo chenye kuwa wazi.

Amenimeza kama nyoka mukubwa;+

Amejaza tumbo lake kwa vitu vyangu vya muzuri.

Ameniondolea mbali kwa maji.

35 ‘Jeuri yenye nilitendewa mimi na mwili wangu ikuje juu ya Babiloni!’ ni vile mukaaji wa Sayuni anasema.+

‘Na damu yangu ikuwe juu ya wakaaji wa Ukaldayo!’ ni vile Yerusalemu anasema.”

36 Kwa hiyo Yehova anasema hivi:

“Angalia, ninatetea kesi yako ya hukumu,+

Na nitakulipizia kisasi.+

Nitakausha bahari yake na kukausha visima vyake.+

37 Na Babiloni atakuwa marundo ya majiwe,+

Pango la mbweha,+

Kitu cha kuogopesha na kitu cha kupigiwa muluzi,

Bila mukaaji.+

38 Wote pamoja watanguruma kama vile wana-simba.*

Watanguruma kama watoto wa simba.”

39 “Wakati watakuwa wamesisimuka, nitafanya karamu yao na kuwalewesha,

Ili wafurahi;+

Kisha watalala usingizi wa kudumu,

Wenye hawataamuka kutoka ndani,”+ ni vile Yehova anasema.

40 “Nitawashusha kama wana-kondoo wenye kuenda kwenye machinjo,

Kama kondoo-dume pamoja na mbuzi.”

41 “Namna Sheshaki* amekamatwa,+

Namna Sifa ya dunia yote imekamatwa!+

Namna Babiloni amekuwa kitu cha kuogopesha kati ya mataifa!

42 Bahari imekuja juu ya Babiloni.

Amefunikwa kwa wingi wa mawimbi yake.

43 Miji yake imekuwa kitu cha kuogopesha, inchi yenye haina maji na jangwa.

Inchi yenye hakuna mutu mwenye ataishi ndani na hakuna mutu mwenye atapita ndani.+

44 Nitakaza uangalifu wangu juu ya Beli+ katika Babiloni,

Na nitatosha katika kinywa chake kile chenye amemeza.+

Mataifa hayatamiminika kwake tena,

Na ukuta wa Babiloni utaanguka.+

45 Mutoke katikati yake, watu wangu!+

Muponyoke ili kuokoa uzima wenu*+ kutoka kwa kasirani ya Yehova yenye kuwaka!+

46 Musikuwe na moyo wa woga wala kuogopa juu ya habari yenye itasikiwa katika inchi.

Katika mwaka mumoja habari itakuja,

Na mwaka wenye kufuata habari ingine,

Ya jeuri katika inchi na ya mutawala juu ya mutawala.

47 Kwa hiyo muangalie! siku zinakuja

Wakati nitakaza uangalifu wangu juu ya sanamu za kuchongwa za Babiloni.

Inchi yake yote itapatishwa haya,

Na watu wake wote wenye waliuawa wataanguka katikati yake.+

48 Mbingu na dunia na vyote vyenye kuwa ndani

Vitapiga vigelegele vya shangwe juu ya Babiloni,+

Kwa maana wenye kuharibu watakuja kwake kutoka kaskazini,”+ ni vile Yehova anasema.

49 “Babiloni hakutokeza tu kuanguka kwa wenye waliuawa wa Israeli+

Lakini pia kule Babiloni wenye waliuawa wa dunia yote wameanguka.

50 Ninyi wenye kuponyoka upanga, muendelee kuenda, musisimame wima!+

Mukumbuke Yehova kutoka mbali,

Na Yerusalemu aingie katika moyo wenu.”+

51 “Tumepatishwa haya, kwa maana tumesikia zihaka.

Haya imefunika nyuso zetu,

Kwa maana wageni* wameshambulia mahali patakatifu pa nyumba ya Yehova.”+

52 “Kwa hiyo muangalie! siku zinakuja,” ni vile Yehova anasema,

“Wakati nitakaza uangalifu wangu juu ya sanamu zake za kuchongwa,

Na katika inchi yake yote wenye waliumizwa watalia kwa maumivu.”+

53 “Hata Babiloni akipanda mbinguni,+

Hata akiimarisha ngome zake za murefu,

Wenye kumuharibu watakuja kutoka kwangu,”+ ni vile Yehova anasema.

54 “Musikilize! Kuko kilio kutoka Babiloni,+

Sauti ya musiba mukubwa kutoka inchi ya Wakaldayo,+

55 Kwa maana Yehova anaharibu Babiloni,

Atanyamazisha sauti yake kubwa,

Na mawimbi yao yatavuma kama maji mengi.

Makelele ya sauti yao yatasikika.

56 Kwa maana mwenye kuharibu atakuja juu ya Babiloni;+

Wapiganaji-vita wake watakamatwa,+

Pinde zao zitavunjwa-vunjwa,

Kwa maana Yehova ni Mungu wa kisasi.+

Hakika atalipa.+

57 Nitalewesha wakubwa wake na watu wake wenye hekima,+

Magavana wake na watawala wake wasaidizi na wapiganaji-vita wake,

Na watalala usingizi wa kudumu,

Wenye hawataamuka kutoka ndani,”+ ni vile Mufalme anasema, yeye mwenye jina lake ni Yehova wa majeshi.

58 Yehova wa majeshi anasema hivi:

“Ukuta wa Babiloni, hata kama ni mupana, utabomolewa kabisa,+

Na milango yake mikubwa, hata kama ni mirefu, itawashwa moto.

Vikundi vya watu vitafanya kazi ya jasho bure;

Mataifa yatajichokesha ili tu kuchochea moto.”+

59 Hili ndilo neno lenye Yeremia nabii alimuamuru Seraya mwana wa Neria+ mwana wa Mahseya wakati alienda na Mufalme Sedekia wa Yuda kule Babiloni katika mwaka wa ine (4) wa utawala wake; Seraya alikuwa musimamizi wa makao. 60 Yeremia aliandika katika kitabu kimoja musiba wote wenye ungekuja juu ya Babiloni, maneno haya yote yenye yaliandikwa juu ya Babiloni. 61 Zaidi ya hayo, Yeremia alimuambia Seraya: “Wakati utafika Babiloni na kuona muji huo, unapaswa kusoma kwa sauti kubwa maneno haya yote. 62 Kisha useme, ‘Ee Yehova, umesema juu ya mahali hapa kwamba pataharibiwa na kuachwa bila mukaaji, mwanadamu wala munyama, na kwamba atakuwa ukiwa milele.’+ 63 Na wakati utamaliza kusoma kitabu hiki, ukifunge kwenye jiwe na kukitupa katikati ya Efrati. 64 Kisha useme: ‘Ni hivi Babiloni atazama na hatainuka tena hata siku moja+ kwa sababu ya musiba wenye ninaleta juu yake; na watachoka.’”+

Maneno ya Yeremia yanaishia hapa.

52 Sedekia+ alikuwa na miaka makumi mbili na moja (21) wakati alikuwa mufalme, na alitawala kwa miaka kumi na moja (11) katika Yerusalemu. Jina la mama yake lilikuwa Hamutali+ binti ya Yeremia wa Libna. 2 Aliendelea kufanya mambo ya mubaya mbele ya macho ya Yehova, kulingana na mambo yote yenye Yehoyakimu alikuwa amefanya.+ 3 Ni kwa sababu ya kasirani ya Yehova kwamba mambo hayo yalitokea katika Yerusalemu na katika Yuda, mupaka akawatupa kutoka mbele ya macho yake.+ Na Sedekia akamuasi mufalme wa Babiloni.+ 4 Katika mwaka wa kenda (9) wa utawala wa Mufalme Sedekia, katika mwezi wa kumi (10), katika siku ya kumi ya mwezi huo, Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni alikuja pamoja na jeshi lake lote ili kupigana na Yerusalemu. Wakapiga kambi juu yake na kujenga ukuta wa kuzunguka kwa ajili ya vita kuizunguka pande zote.+ 5 Na muji ukazungukwa kwa ajili ya vita mupaka mwaka wa kumi na moja (11) wa Mufalme Sedekia.

6 Katika mwezi wa ine (4), katika siku ya kenda (9) ya mwezi huo,+ njaa ikakuwa kali katika muji, na hapakukuwa chakula kwa ajili ya watu wa inchi.+ 7 Mwishowe ukuta wa muji ukatobolewa tundu kubwa, na maaskari wote wakakimbia kutoka katika muji usiku kupitia mulango mukubwa wenye kuwa kati ya zile kuta mbili karibu na bustani ya mufalme, wakati Wakaldayo walikuwa wanazunguka muji; na wakaendelea kupitia njia ya Araba.+ 8 Lakini jeshi la Wakaldayo likamufuatilia mufalme, na wakamufikia Sedekia+ katika maeneo tambarare ya jangwa la Yeriko, na maaskari wake wote wakatawanyika kutoka pembeni yake. 9 Kisha wakamukamata mufalme na kumuleta mupaka kwa mufalme wa Babiloni kule Ribla katika inchi ya Hamati, na akamuhukumu. 10 Na mufalme wa Babiloni akaua wana wa Sedekia mbele ya macho yake, na pia akaua wakubwa wote wa Yuda kule Ribla. 11 Kisha mufalme wa Babiloni akapofusha macho ya Sedekia,+ akamufunga kwa pingu za shaba, akamupeleka Babiloni, na kumufunga katika gereza mupaka siku ya kifo chake.

12 Katika mwezi wa tano (5), katika siku ya kumi (10) ya mwezi huo, ni kusema, katika mwaka wa kumi na kenda (19) wa Mufalme Nebukadneza* mufalme wa Babiloni, Nebuzaradani mukubwa wa walinzi, mwenye alikuwa mutumishi wa mufalme wa Babiloni, akaingia ndani ya Yerusalemu.+ 13 Akateketeza kwa moto nyumba ya Yehova,+ nyumba ya mufalme, na nyumba zote za Yerusalemu; akateketeza pia kwa moto kila nyumba kubwa. 14 Na kuta zenye kuzunguka Yerusalemu zilibomolewa na jeshi lote la Wakaldayo lenye lilikuwa pamoja na mukubwa wa walinzi.+

15 Nebuzaradani mukubwa wa walinzi akapeleka katika uhamisho wamoja kati ya watu wa hali ya chini na wale watu wengine wenye walibakia wenye waliachwa katika muji. Akakamata pia wale wenye walikimbia wenye walikuwa wamekimbia na kujiunga na mufalme wa Babiloni na pia wenye walibakia kati ya wafanyakazi wenye ufundi.+ 16 Lakini Nebuzaradani mukubwa wa walinzi akaacha wamoja kati ya watu maskini zaidi wa inchi watumike wakiwa watunza-mizabibu na wafanyakazi wa kulazimishwa.+

17 Na Wakaldayo wakavunja vipande-vipande zile nguzo za shaba+ za nyumba ya Yehova na yale magari+ na ile Bahari ya shaba+ vyenye vilikuwa katika nyumba ya Yehova, na wakapeleka shaba yote kule Babiloni.+ 18 Walikamata pia makopo, vipao,* vizimisha-moto, mabakuli,+ vikombe,+ na vyombo vyote vya shaba vyenye vilitumiwa katika utumishi wa hekalu. 19 Mukubwa wa walinzi alikamata beseni,+ vyetezo, mabakuli, makopo, vinara vya taa,+ vikombe, na mabakuli yenye yalikuwa ya zahabu na feza ya kweli.+ 20 Na zile nguzo mbili, ile Bahari, wale ngombe-dume kumi na mbili (12) wa shaba+ wenye walikuwa chini ya ile Bahari, na yale magari yenye Mufalme Sulemani alikuwa ametengeneza kwa ajili ya nyumba ya Yehova, shaba ya vyombo hivyo vyote haingeweza kupimwa.

21 Kuhusu zile nguzo, kila nguzo ilikuwa na urefu kuenda juu wa mikono* kumi na munane (18), na kamba ya kupimia yenye urefu wa mikono kumi na mbili (12) ingeweza kuizunguka;+ unene wake ulikuwa na upana wa vidole* ine (4), na ilikuwa na tundu. 22 Na kifuniko cha nguzo chenye kilikuwa juu yake kilikuwa cha shaba; na urefu wa kifuniko kimoja ulikuwa wa mikono tano (5);+ na wavu* na makomamanga vyenye kuzunguka kifuniko pande zote, vyote vilitengenezwa kwa shaba. Nguzo ya pili ilikuwa vilevile, pia yale makomamanga. 23 Kulikuwa makomamanga makumi kenda na sita (96) pembeni-pembeni; kwa ujumla, kulikuwa makomamanga mia moja (100) kuzunguka wavu huo.*+

24 Mukubwa wa walinzi alimukamata pia Seraya+ mukubwa wa makuhani, Sefania+ kuhani wa pili, na wale walinzi watatu (3) wa milango.+ 25 Na alikamata kutoka katika muji ofisa mumoja wa makao ya mufalme mwenye alikuwa musimamizi wa maaskari, watu saba (7) wenye walishirikiana kwa ukaribu na mufalme wenye walipatikana katika muji, na pia mwandishi wa mukubwa wa jeshi, mwenye kukusanya watu wa inchi, na watu makumi sita (60) kutoka kati ya watu wa kawaida wa inchi wenye walikuwa wangali katika muji. 26 Nebuzaradani mukubwa wa walinzi akawakamata na kuwapeleka kwa mufalme wa Babiloni kule Ribla. 27 Mufalme wa Babiloni akawapiga na kuwaua kule Ribla+ katika inchi ya Hamati. Basi Yuda wakaenda katika uhamisho kutoka katika inchi yao.+

28 Hawa ndio watu wenye Nebukadneza* alipeleka katika uhamisho: katika mwaka wa saba (7), Wayahudi elfu tatu makumi mbili na tatu (3 023).+

29 Katika mwaka wa kumi na munane (18) wa Nebukadneza,*+ watu* mia munane makumi tatu na mbili (832) walichukuliwa kutoka Yerusalemu.

30 Katika mwaka wa makumi mbili na tatu (23) wa Nebukadneza,* Nebuzaradani mukubwa wa walinzi alipeleka Wayahudi katika uhamisho, watu* mia saba makumi ine na tano (745).+

Kwa ujumla, watu* elfu ine mia sita (4 600) walipelekwa katika uhamisho.

31 Kisha katika mwaka wa makumi tatu na saba (37) wa uhamisho wa Mufalme Yehoyakini+ wa Yuda, katika mwezi wa kumi na mbili (12), katika siku ya makumi mbili na tano (25) ya mwezi huo, Mufalme Evil-merodaki wa Babiloni, katika mwaka wenye alikuwa mufalme, akamuachilia huru* Mufalme Yehoyakini wa Yuda na kumutosha katika gereza.+ 32 Alisema naye kwa fazili na akaweka kiti chake cha ufalme juu kuliko viti vya wafalme wengine wenye walikuwa pamoja naye katika Babiloni. 33 Basi Yehoyakini akavua nguo zake za gereza, na alikuwa anakula kwa ukawaida mbele yake siku zote za maisha yake. 34 Alipewa kwa ukawaida posho ya chakula kutoka kwa mufalme wa Babiloni, siku kwa siku, mupaka siku ya kifo chake, siku zote za maisha yake.

Pengine linamaanisha “Yehova Anainua.”

Ao “nilikuchagua.”

Tnn., “mbele utoke katika tumbo la uzazi.”

Ao “nilikutia pembeni.”

Tnn., “muti wenye kuamuka.”

Ao “chungu cha kupikia chenye mudomo mupana.”

Tnn., “chenye kupulizwa;” hilo linaonyesha kwamba chini yake kulikuwa moto wenye kuchochewa.

Tnn., “unapaswa kufunga kiuno chako.”

Ao “upendo mushikamanifu.”

Ao “eko.”

Ao “eko.”

Ao “visiwa vya.”

Ao “wamejichongea,” pengine kwenye mwamba.

Ao “Wana-simba wenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”

Ao “Memfisi.”

Ni kusema, tawi la Muto Nile.

Ni kusema, Efrati.

Ao “wakati wa tamaa ya nafsi yake.”

Tnn., “mwezi wake.”

Ao “miungu ya kigeni.”

Ao “kitambaa chake cha arusi cha kujipamba?”

Ao “nafsi maskini zenye hazina.”

Tnn., “Mwarabu.”

Tnn., “paji la uso la.”

Ao “ameonyesha nafsi yake kuwa yenye.”

Tnn., “Sitafanya uso wangu ukuangukie.”

Tnn., “njia zako.”

Ao “miungu ya kigeni.”

Ao pengine, “bwana yenu.”

Tnn., “wa majeshi ya mataifa.”

Tnn., “rafiki yake.”

Ao “mungu wa haya amekula.”

Angalia Maana ya Maneno.

Govi ni ngozi yenye kufunika sehemu ya mbele ya kiungo cha uzazi cha mwanaume mwenye hajatahiriwa.

Ao “nguzo ya alama.”

Ao “miti yake midogo-midogo.”

Ao “Mupige vifua vyenu.”

Ao “uhodari.”

Ao “uhodari.”

Ao “wakati upanga umefikia nafsi zetu.”

Maneno ya kishairi yenye kutaja kitu kama mutu, pengine yanaonyesha sikitiko ao huruma.

Ni kusema, wale wenye wanaangalia muji ili wajue wakati wa kushambulia.

Tnn., “matumbotumbo yangu.”

Tnn., “katika kuta za moyo wangu.”

Ao “nafsi yangu imesikia.”

Ao pengine, “sauti ya kilio cha pigano.”

Ao “nguzo ya alama.”

Ao “hekima.”

Ao “sitasikitika.”

Ao “vichaka.”

Ao “kivuli cha macho.”

Ao “wanatafuta nafsi yako.”

Ao “nafsi yangu imechoka.”

Tnn., “hawakukuwa wazaifu.”

Tnn., “pingu.”

Ao “nafsi yangu haipaswe.”

Ao pengine, “Haiko.”

Ni kusema, neno la Mungu.

Tnn., “ninyi watu wapumbavu wenye hawana moyo.”

Kizimba ni kitu cha kuchungia ao kubebea wanyama.

Ao “nafsi yangu haipaswe.”

Tnn., “Mutakase vita juu yake.”

Ao “nafsi yangu itageuka na kukuacha.”

Tnn., “Sikio lao halitahiriwe.”

Tnn., “wale wenye kujaa siku.”

Ao “kwa ajili ya nafsi zenu.”

Ao “agizo langu.”

Kane ni utete wenye harufu ya muzuri.

Tnn., “Maumivu ya kuzaa kama ya.”

Ao “eko.”

Ni kusema, Yeremia.

Ao “Mivukuto imeunguzwa.”

Tnn., “Haya ni,” ikizungumuzia majengo yote ya hekalu.

Ao “watoto wenye hawana baba.”

Ao “tangu milele mupaka milele.”

Ao “kuchoma zabihu ili zitoe moshi kwa ajili ya Baali.”

Tnn., “nilikuwa ninaamuka asubui sana na kusema.”

Jina la cheo la mungu mwanamuke mwenye aliabudiwa na Waisraeli waasi-imani; pengine ni mungu mwanamuke wa uzazi.

Ao “wanakasirisha; wanachokoza.”

Ao “shauri lao.”

Tnn., “kila siku nikiamuka asubui sana na kuwatuma.”

Tnn., “walifanya shingo yao kuwa ngumu.”

Tnn., “umeondolewa katika kinywa chao.”

Ao “zimetolewa kwa Mungu.”

Ao “wimbo wa maombolezo.”

Angalia Maana ya Maneno, “Gehena.”

Ao “halijaingia katika mawazo yangu.”

Angalia Maana ya Maneno, “Gehena.”

Ao “nyakati zake zenye ziliwekwa.”

Ao pengine, “korongo.”

Ao “kuhama.”

Ao “agizo la.”

Ao “mafuta yenye kutuliza.”

Ao “munganga.”

Ao “nafsi yangu haipaswe.”

Ao “wimbo wa maombolezo.”

Ao “agizo langu lenye.”

Ao “nyimbo za maombolezo.”

Ao “wimbo wa maombolezo.”

Ao “eko.”

Angalia Maana ya Maneno.

Ni kusema, pembeni ya paji la uso kati ya jicho na sikio.

Ao “ubatili.”

Ao “tezo yake.”

Ao “hama, marteau.”

Ao “ubatili.”

Mwanzoni, mustari wa 11 uliandikwa katika Kiaramu.

Ao “anafanya muvuke upande.”

Ao pengine, “milango.”

Ao “sanamu yake ya kuyeyushwa.”

Ao “pumuzi.”

Ao “ubatili.”

Ao “Ninatupa kwa kombeo.”

Inaonekana Yeremia ndiye anaambiwa.

Ao “Ikuwe vile.”

Tnn., “nikiamuka asubui sana na kuonya.”

Ao “wanachoma zabihu ili zitoe moshi kwa ajili yake.”

Ao “mungu wa haya.”

Ni kusema, Yeremia.

Ao “eko.”

Ni kusema, zabihu zenye zilitolewa katika hekalu.

Ao “hisia za ndani kabisa.” Tnn., “figo.”

Ao “wenye wanatafuta nafsi yako.”

Ao “hisia za ndani kabisa.” Tnn., “figo.”

Ao “vichaka vikubwa.”

Ao “mupendwa wa nafsi yangu.”

Ao “mwenye madoa-madoa.”

Ao pengine, “Linaomboleza.”

Tnn., “mwili wowote.”

Ao “mushipi.”

Ao “mushipi.”

Ao “mushipi.”

Ao “mushipi.”

Ao “mushipi.”

Ao “mushipi.”

Ao “mushipi.”

Ao “mushipi.”

Ao “Nafsi yangu italia.”

Ao “mwanamuke muheshimiwa.”

Ao “imezungukwa kwa ajili ya vita.”

Ao “Mwetiopia.”

Ao “wa haya.”

Ao “wenye ni wadogo wao.”

Ao “mifereji; matangi.”

Ao “nafsi yako imechukia.”

Ao “nafsi yangu haingeelekea watu hawa.”

Ao pengine, “aina ine za hukumu.” Tnn., “familia ine.”

Ao pengine, “Unaendelea kutembea kinyume-nyume.”

Ao “kukusikitikia.”

Ao “uma.”

Ao “Nafsi yake inapumua.”

Ao pengine, “Limepatishwa haya na kufezeheshwa.”

Tnn., “Usiniondolee mbali.”

Ao “ujumbe wa lawama.”

Ao “Utakuwa musemaji wangu.”

Desturi ya kipagani ya kuomboleza yenye inawezekana ilifanywa katika Israeli yenye iliasi imani.

Tnn., “juu ya njia zao zote.”

Tnn., “kwa maiti za.”

Ao “Ubatili.”

Angalia Maana ya Maneno.

Ao pengine, “Kwa maana umewashwa kama moto katika kasirani yangu.”

Ao “mutu mwenye nguvu.”

Tnn., “anafanya mwili kuwa mukono wake.”

Ao “mutu mwenye nguvu.”

Ao pengine, “hauwezi kupona.”

Ao “hisia za ndani kabisa.” Tnn., “figo.”

Ao “lakini hapana kwa haki.”

Tnn., “wenye wananiasi mimi,” pengine maneno haya yanazungumuzia Yehova.

Ao “kuwaharibu mara mbili.”

Ao “nafsi zenu.”

Tnn., “wakafanya shingo zao kuwa ngumu.”

Ao “kusini.”

Angalia Maana ya Maneno.

Angalia Maana ya Maneno.

Ao “mipeto; pneus.”

Angalia Maana ya Maneno.

Tnn., “kama vile ilikuwa sawa katika macho ya mufinyanzi kutengeneza.”

Angalia Maana ya Maneno.

Ao “nitasikitika.”

Ao “nitasikitika.”

Tnn., “ninafanya.”

Ao “neige.”

Ao “wanachoma zabihu ili zitoe moshi kwa ajili ya.”

Ao “zenye hazikutengenezwa.”

Ao “agizo halitaangamia.”

Tnn., “tumupige kwa ulimi.”

Ao “nafsi yangu.”

Angalia Maana ya Maneno.

Ao “halijaingia katika mawazo yangu hata kidogo.”

Ao “wenye wanatafuta nafsi yao.”

Ao “wenye wanatafuta nafsi yao.”

Angalia Maana ya Maneno.

Tnn., “walifanya shingo yao kuwa ngumu ili wasitii.”

Ao “hisia za ndani kabisa.” Tnn., “figo.”

Ao “nafsi ya maskini.”

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Ao “nitawageuzia.”

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Ao “wenye wanatafuta nafsi yao.”

Ao “nafsi yake.”

Ao “ataponyoka na uzima wake.”

Ao “eneo tambarare la chini.”

Angalia Maana ya Maneno.

Ao “yatima yeyote.”

Tnn., “nitatakasa.”

Anaitwa pia Yehoahazi.

Angalia Maana ya Maneno.

Angalia Maana ya Maneno.

Ao “nyumba; kiota.”

Tnn., “Maumivu ya kuzaa kama ya.”

Anaitwa pia Yehoyakini na Yekonia.

Ao “wenye wanatafuta nafsi yako.”

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Ao “kwenye inchi yenye wanainulia nafsi yao.”

Ao “inchi.”

Tnn., “siku zake.”

Ao “muriti wa.”

Angalia Maana ya Maneno.

Ao “ni waasi-imani.”

Tnn., “Wanatia nguvu mikono ya.”

Ao “Wanawajaza ninyi na matumaini ya uongo.”

Ao “hama, marteau.”

Ao “Ujumbe wenye kuchokesha.” Neno hilo la Kiebrania liko na maana mbili: “ujumbe muzito kutoka kwa Mungu” ao “kitu chenye kuchokesha.”

Ao “ujumbe wenye kuchokesha.”

Ao “ujumbe wenye kuchokesha.”

Ao “ujumbe wenye kuchokesha.”

Ao “Ujumbe wenye kuchokesha.”

Ao “ujumbe wenye kuchokesha.”

Ao “Ujumbe wenye kuchokesha.”

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Anaitwa pia Yehoyakini na Konia.

Ao pengine, “wajenzi wa maboma.”

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Ao “na.”

Tnn., “nikiamuka asubui sana na kusema.”

Tnn., “akiamuka asubui sana na kuwatuma.”

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Ao “nitamupatia azabu.”

Inaonekana hili ni jina la siri la Babeli (Babiloni).

Ao “eko.”

Tnn., “kila mwili.”

Ao “mwana-simba mwenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”

Ao “na.”

Ao “kuinama.”

Ao “nitasikitika.”

Ao “agizo langu lenye.”

Tnn., “ninaamuka asubui sana na kutuma.”

Ao “atasikitika.”

Ao “mulima wa hekalu.”

Ao “mahali penye kuinuka penye miti.”

Ao “hakujaribu kutuliza uso wa Yehova.”

Ao “akasikitika.”

Ao “nafsi zetu.”

Tnn., “ule mwenye ni sawa katika macho yangu.”

Tnn., “lipumuzike.”

Ni kusema, “Bahari ya shaba ya hekalu.”

Tnn., “miaka ya siku.”

Ao “Ikuwe vile.”

Ao “mwanamuke muheshimiwa.”

Ao pengine, “wajenzi wa maboma.”

Ao pengine, “zenye kupasuka.”

Tnn., “nikiamuka asubui sana na kuwatuma.”

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Ao “vyuma vya kuwekwa kwenye shingo.”

Ao “viuno vyake.”

Tnn., “ni kubwa.”

Tnn., “pingu zako nitazikata.”

Ao “watu wa inchi ya kigeni.”

Ao “hawatawafanya.”

Ao “Nitakurekebisha.”

Ao pengine, “waheshimiwe.”

Ao “kutoa moyo wake kuwa kitu chenye kinawekeshwa kwa ajili ya mukopo ili kunikaribia?”

Ao “nimeendelea kukuonyesha upendo mushikamanifu.”

Ao “matari yako.”

Ao “utaenda katika dansi ya wale wenye kucheka.”

Ao “mabonde.”

Ao “kumuomba.”

Ao “vitu vizuri kutoka kwa.”

Ao “Nafsi yao itakuwa.”

Ao “nafsi ya makuhani.”

Tnn., “mafuta.”

Ao “watoto.”

Tnn., “matumbotumbo yangu yamechochewa.”

Ao “nafsi yenye kuchoka.”

Ao “kila nafsi yenye kuregea.”

Ao “uzao wa.”

Tnn., “ganzi.”

Ao pengine, “bwana yao.”

Ao “eneo lote tambarare la chini.”

Ao “majivu yenye mafuta,” ni kusema, majivu yenye kujaa mafuta ya zabihu.

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Shekeli moja ilikuwa sawa na grame 11.4 (aunsi troi 0.367). Angalia Nyongeza B14.

Ao “kilo.”

Tnn., “katika kifua cha.”

Ao “mukubwa kuhusiana na makusudi yako.”

Tnn., “kila mwili.”

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Tnn., “nikiamuka asubui sana na kufundisha.”

Angalia Maana ya Maneno, “Gehena.”

Ao “halijaingia katika mawazo yangu.”

Angalia Maana ya Maneno.

Ao “vitu vyote vya muzuri vyenye.”

Ao “muriti wa.”

Angalia Maana ya Maneno.

Tnn., “mbegu ya Daudi na ya Walawi wenye wananitumikia ikuwe nyingi.”

Tnn., “mbegu ya.”

Tnn., “mbegu yake.”

Tnn., “mbegu ya.”

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Tnn., “leo.”

Ao “kama vile nafsi yao ilitaka.”

Ao “wenye wanatafuta nafsi zao.”

Ao “wenye wanatafuta nafsi zao.”

Ao “vyumba.”

Tnn., “Yonadabu,” kifupi cha jina Yehonadabu.

Tnn., “Yonadabu,” kifupi cha jina Yehonadabu.

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Tnn., “nikiamuka asubui sana na kusema.”

Tnn., “nikiamuka asubui sana na kutuma.”

Tnn., “Yonadabu,” kifupi cha jina Yehonadabu.

Ao “chumba cha kukulia chakula.”

Ao “mwandishi.”

Ao “maofisa wa makao ya mufalme.”

Nusu ya pili ya Mwezi wa 11 na nusu ya kwanza ya Mwezi wa 12 kulingana na kalendari yetu. Angalia Nyongeza B15.

Tnn., “mbegu yake.”

Anaitwa pia Yehoyakini na Yekonia.

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Ao “Musidanganye nafsi zenu.”

Tnn., “wakamutia katika nyumba ya pingu.”

Tnn., “nyumba ya tangi la maji.”

Ao “nyumba yake ya kifalme.”

Tnn., “atatoka inje kwa.”

Ao “nafsi yake.”

Ao “ataponyoka na uzima wake.”

Tnn., “mikono.”

Ao “Eko.”

Ao “ofisa wa makao ya mufalme.”

Ao “mwenye alitufanyia nafsi hii.”

Ao “wenye wanatafuta nafsi yako.”

Tnn., “unatoka inje kwa.”

Ao “nafsi yako itaendelea kuishi.”

Tnn., “hautatoka inje kwa.”

Ao “nafsi yako itaendelea.”

Tnn., “kuenda inje.”

Tnn., “Watu wa amani yako.”

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Ao kulingana na mupangilio tofauti wa maneno ya maandishi ya Kiebrania, “Nergal-shareza, Samgari-nebo, Sarsekimu, Rabsarisi.”

Ao “muchawi mukubwa (mwenye elimu ya nyota).”

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Ao pengine, “wafanye kazi za kulazimishwa.”

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Ao “ofisa mukubwa wa makao ya mufalme.”

Ao “muchawi mukubwa (mwenye elimu ya nyota).”

Ao “nafsi yako.”

Ao “utaponyoka na uzima wako.”

Tnn., “nisimame mbele ya.”

Ao “apige nafsi yako?”

Ao “apige nafsi yako.”

Tnn., “wa mbegu ya ufalme.”

Ao pengine, “kisima kikubwa.”

Ao “nitahuzunika.”

Ao “kukaa kwa wakati fulani.”

Ao “nafsi zenu.”

Ao “kila nafsi yenye.”

Ao “mortier.”

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Ao “mahekalu ya.”

Ao “bila kuumizwa.”

Ao “minara ya.”

Ao “Nyumba (Hekalu la) ya Jua,” ni kusema, Heliopolisi.

Ao “mahekalu ya.”

Ao “Memfisi.”

Tnn., “nikiamuka asubui sana na kutuma.”

Ao “munaletea nafsi zenu.”

Ao “hawakujisikia kuwa wamepondwa.”

Ao “Watainua nafsi yao ili.”

Jina la cheo la mungu mwanamuke mwenye aliabudiwa na Waisraeli waasi-imani; pengine mungu mwanamuke wa uzazi.

Jina la cheo la mungu mwanamuke mwenye aliabudiwa na Waisraeli waasi-imani; pengine mungu mwanamuke wa uzazi.

Jina la cheo la mungu mwanamuke mwenye aliabudiwa na Waisraeli waasi-imani; pengine mungu mwanamuke wa uzazi.

Jina la cheo la mungu mwanamuke mwenye aliabudiwa na Waisraeli waasi-imani; pengine mungu mwanamuke wa uzazi.

Ao “wenye wanatafuta nafsi yake.”

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Ao “alikuwa anatafuta nafsi yake.”

Ao “unatazamia.”

Ao “watu wote.”

Ao “nafsi yako.”

Ao “nitaacha uponyoke na uzima wako.”

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Mara nyingi zilibebwa na wapiga-mishale.

Lijamu ni kipande cha chuma chenye kinawekwa kwenye kinywa cha munyama ili kumuongoza na kumuzuia.

Tnn., “kukanyanga.”

Ao “eko.”

Ao “mauaji.”

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Ao “Memfisi.”

Ao “wakati wenye uliwekwa upite.”

Ni kusema, ule mwenye anashinda Misri.

Ao “Memfisi.”

Ao pengine, “itakuwa inchi yenye imeachwa.”

Ao “wenye kukusanya kuni.”

Ni kusema, Tebesi.

Ao “wenye wanatafuta nafsi yao.”

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Tnn., “mbegu yako.”

Ao “Nitakurekebisha.”

Kwato ni sehemu ngumu ya chini ya muguu wa munyama.

Ao “mipeto; pneus.”

Ni kusema, Krete.

Ni kusema, watanyoa vichwa vyao kwa kuomboleza na kwa haya.

Ao “eneo tambarare la chini.”

Ao “Mahali salama pa juu pamepatishwa.”

Ao “nafsi zenu.”

Ao “Eneo tambarare la chini.”

Ao “eneo tambarare la juu.”

Machicha ni masalio ya pombe yenye kubakia chini ya chombo.

Ao pengine, “kwenye inchi kavu.”

Ao “eneo tambarare la juu.”

Tnn., “Pembe ya Moabu imekatwa.”

Ao “nyumba; viota.”

Ao “eko.”

Ao “utakuwa na musukosuko kwa ajili ya.”

Ni kusema, filimbi yenye ilipigwa wakati wa kuomboleza kwenye maziko.

Ao “utakuwa na musukosuko kwa ajili ya.”

Ni kusema, filimbi yenye ilipigwa wakati wa kuomboleza kwenye maziko.

Ao pengine, “sauti ya kilio cha pigano isikiwe.”

Ao “miji yenye kumuzunguka.”

Ao “mazizi ya kondoo.” Zizi ni lupango ya kuchungia wanyama.

Ao “maeneo tambarare ya chini.”

Ao “nyumba yako; kiota chako.”

Ao “vichaka vikubwa.”

Ao “shauri lenye.”

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Ao “kila upande.”

Tnn., “mwanzo wa.”

Ao “wale wenye wanatafuta nafsi yao.”

Ao “nguzo ya alama.”

Pengine neno la Kiebrania lenye linatumiwa hapa linahusiana na maneno “mavi ya wanyama” na linatumiwa ili kuonyesha zarau.

Tnn., “kukanyanga.”

Tnn., “Ametoa mukono wake.”

Mundu ni kisu chenye kujikunja chenye kinatumiwa ili kuvuna.

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Ao “nafsi yake itashiba.”

Ao “uwaharibu.”

Ao “hama, marteau.”

Ao “eko.”

Tnn., “kukanyanga.”

Tnn., “watanyamazishwa.”

Ao “manabii wa uongo.”

Ao “vichaka vikubwa.”

Ao “shauri lenye.”

Inaonekana hili ni jina la siri la Ukaldayo.

Tnn., “asikanyange.”

Ni kusema, inchi ya Wakaldayo.

Ao “nafsi yenu.”

Ao pengine, “mujaze mifuko ya mishale.”

Ao “nguzo ya alama.”

Tnn., “kipimo chako cha.”

Ao “anafanya mivuke ipande.”

Ao pengine, “milango.”

Ao “sanamu yake ya kuyeyushwa.”

Ao “pumuzi.”

Ao “ubatili.”

Gongo ni fimbo yenye kuvimba kwenye mwisho wake mumoja.

Ao “nguzo ya alama.”

Tnn., “Mutakase.”

Tnn., “Mutakase.”

Pingo ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.

Ao “mashua za maji; bateaux.”

Ao “papyrus.” Angalia Maana ya Maneno.

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Ao “wana-simba wenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”

Inaonekana hili ni jina la siri la Babeli (Babiloni).

Ao “nafsi zenu.”

Ao “watu wa inchi ya kigeni.”

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Ao “sepetu; bêches.”

Mukono mumoja ulikuwa sawa na santimetre 44.5 (inchi 17.5). Angalia Nyongeza B14.

Upana wa kidole ulikuwa sawa na santimetre 1.85 (inchi 0.73). Angalia Nyongeza B14.

Ao “makila.”

Ao “makila hiyo.”

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Ao “nafsi.”

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Ao “nafsi.”

Ao “nafsi.”

Tnn., “akainua kichwa cha.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine