Isaya
19 Tangazo juu ya Misri:+ Tazama! Yehova amepanda juu ya wingu jepesi+ na anakuja kuingia Misri. Na miungu ya Misri isiyo na thamani hakika itatetemeka kwa sababu yake,+ na moyo wa Misri utayeyuka katikati yake.+
2 “Nami nitawachochea Wamisri juu ya Wamisri, nao hakika watapigana kila mmoja na ndugu yake, na kila mmoja na mwenzake, jiji juu ya jiji, ufalme juu ya ufalme.+ 3 Na roho ya Misri lazima itatanishwe katikati yake,+ nami nitavuruga shauri lake.+ Nao hakika wataenda kwa miungu isiyo na thamani+ na kwa wachawi na kwa wenye kuwasiliana na pepo na kwa wajuzi wa kubashiri matukio.+ 4 Nami nitaitia Misri katika mkono wa bwana mgumu, na mfalme atakayetawala juu yao atakuwa mwenye nguvu,”+ asema Bwana wa kweli, Yehova wa majeshi.
5 Na maji hakika yatakauka kutoka baharini, na mto utakuwa mkavu na kwa kweli utakauka.+ 6 Na lazima mito itoe harufu mbaya; mifereji ya Nile ya Misri lazima ishuke na kukauka.+ Matete+ na vitete lazima vioze. 7 Mahali palipo wazi kando ya Mto Nile, penye kinywa cha Mto Nile, na kila udongo wa kupanda mbegu wa Mto Nile zitakauka.+ Hakika zitafukuziwa mbali, nazo hazitakuwapo tena. 8 Na wavuvi watalazimika kuomboleza, na wale wote wanaotupa ndoano ndani ya Mto Nile lazima wahuzunike, na hata wale wanaotandaza nyavu za kuvulia juu ya uso wa maji kwa kweli watadhoofika.+ 9 Na wafanyakazi wa kitani+ kilichochambuliwa lazima waone aibu; pia wafumaji wa nguo wa vitambaa vyeupe. 10 Na wafumaji+ wake lazima wapondwe, wafanyakazi wote wa kulipwa wawe na huzuni katika nafsi.
11 Wakuu wa Soani+ ni wapumbavu kwelikweli. Na kwa habari ya wenye hekima wa washauri wa Farao, shauri lao ni kitu kisicho cha akili.+ Ninyi mtamwambiaje Farao: “Mimi ni mwana wa wenye hekima, mwana wa wafalme wa kale”? 12 Basi, wao wako wapi—watu wenu wenye hekima+—ili sasa wawaambie ninyi na ili wajue yale ambayo Yehova wa majeshi ameshauri kuhusu Misri?+ 13 Wakuu wa Soani wametenda kwa upumbavu,+ wakuu wa Nofu+ wamedanganywa, wakuu wa makabila+ yake wamesababisha Misri iende huku na huku. 14 Yehova mwenyewe amechanganya katikati yake roho ya mvurugo;+ nao wamesababisha Misri kwenda huku na huku katika kazi yake yote, kama mtu aliyelewa anavyogaagaa katika matapiko yake.+ 15 Na Misri haitakuwa na kazi yoyote ambayo inaweza kufanywa na kichwa wala mkia, chipukizi wala tete.+
16 Katika siku hiyo Misri itakuwa kama wanawake, nayo hakika itatetemeka+ na kuingiwa na hofu kwa sababu ya kutikiswa kwa mkono wa Yehova wa majeshi ambao anautikisa juu yake.+ 17 Na nchi ya Yuda itakuwa kisababishi cha kuyumba-yumba kwa Misri.+ Kila mtu anayeambiwa juu yake ameingiwa na hofu kwa sababu ya shauri la Yehova wa majeshi ambalo anashauri juu yake.+
18 Katika siku hiyo kutakuwa na majiji matano katika nchi ya Misri+ yanayosema lugha ya Kanaani+ na kuapa+ kwa Yehova wa majeshi. Jiji moja litaitwa Jiji la Kubomoa.
19 Katika siku hiyo kutakuwa na madhabahu kwa Yehova katikati ya nchi ya Misri,+ na nguzo kwa Yehova kando ya mpaka wake. 20 Nayo itakuwa ni ishara na ushahidi kwa Yehova wa majeshi katika nchi ya Misri;+ kwa maana watamlilia Yehova kwa sababu ya wakandamizaji,+ naye atawapelekea mwokozi, aliye mkuu, ambaye kwa kweli atawakomboa.+ 21 Na Yehova hakika atajulikana kwa Wamisri;+ na Wamisri lazima wamjue Yehova katika siku hiyo, nao watatoa dhabihu na zawadi+ nao watamwekea Yehova nadhiri na kuitimiza.+ 22 Na Yehova hakika ataipiga Misri.+ Kutakuwako kupigwa na kuponywa;+ nao lazima warudi kwa Yehova,+ naye atakubali kusihi kwao na kuwaponya.+
23 Katika siku hiyo kutakuwa na njia kuu+ kutoka Misri kwenda Ashuru, na Ashuru kwa kweli watakuja kuingia Misri, na Misri kuingia Ashuru; nao hakika watatoa utumishi, Misri pamoja na Ashuru. 24 Katika siku hiyo Israeli atakuwa wa tatu pamoja na Misri na pamoja na Ashuru,+ yaani, baraka katikati ya dunia,+ 25 kwa sababu Yehova wa majeshi atakuwa amewabariki,+ akisema: “Wabarikiwe watu wangu, Misri, na kazi ya mikono yangu, Ashuru,+ na urithi wangu, Israeli.”+