Isaya
48 Sikieni hili, enyi nyumba ya Yakobo, ninyi mnaojiita wenyewe kwa jina la Israeli+ na ambao mmetoka katika maji ya Yuda,+ ninyi mnaoapa kwa jina la Yehova+ na mnaomtaja Mungu wa Israeli,+ si katika kweli na si katika uadilifu.+ 2 Kwa maana wamejiita kuwa wametoka katika jiji takatifu,+ nao wamejitegemeza juu ya Mungu wa Israeli,+ Yehova wa majeshi ni jina lake.+
3 “Mambo ya kwanza nimeyatangaza tangu wakati ule, nayo yalitoka katika kinywa changu mwenyewe, nami nikaendelea kuyafanya yasikiwe.+ Kwa ghafula nilitenda, na mambo yale yakafika.+ 4 Kwa sababu nilijua kwamba wewe ni mgumu+ na kwamba shingo yako ni kano ya chuma+ na paji la uso wako ni shaba,+ 5 mimi pia niliendelea kukuambia tangu wakati ule. Kabla halijaingia, mimi nilikufanya ulisikie,+ ili usiseme, ‘Sanamu yangu mwenyewe imeyafanya, na sanamu yangu ya kuchongwa na sanamu yangu ya kuyeyushwa zimeyaamuru.’+ 6 Wewe umesikia.+ Yatazame yote.+ Na kwa habari yenu, je, hamtalitangaza?+ Nimekufanya usikie mambo mapya tangu wakati huu, hata mambo yaliyohifadhiwa, ambayo hukuyajua.+ 7 Kwa wakati huu yataumbwa, wala si tangu wakati ule, hata mambo ambayo kabla ya leo hukuyasikia, ili usiseme, ‘Tazama! Tayari nimeyajua.’+
8 “Na zaidi ya hayo, wewe hukusikia,+ wala hukujua, wala tangu wakati ule na kuendelea sikio lako halikufunguliwa. Kwa maana najua vema kwamba bila shaka uliendelea kutenda kwa hila,+ nawe umeitwa ‘mkosaji tangu tumboni.’+ 9 Nitaizuia hasira yangu kwa ajili ya jina langu,+ na kwa ajili ya sifa yangu nitajizuia kukuelekea ili usikatiliwe mbali.+ 10 Tazama! Nimekusafisha, lakini si kwa namna ya fedha.+ Nimekuchagua katika tanuru ya kuyeyushia ya mateso.+ 11 Nitatenda kwa ajili yangu mwenyewe, kwa ajili yangu mwenyewe nitatenda,+ kwani mtu angewezaje kujiachilia mwenyewe atiwe unajisi?+ Nami sitampa mwingine yeyote utukufu wangu mwenyewe.+
12 “Nisikilize mimi, Ee Yakobo, na wewe Israeli mtu wangu niliyemwita. Mimi ni Yeye yuleyule.+ Mimi ndiye wa kwanza.+ Na zaidi ya hayo, mimi ndiye wa mwisho.+ 13 Na zaidi ya hayo, mkono wangu mwenyewe uliuweka msingi wa dunia,+ na mkono wangu mwenyewe wa kuume ulizitandaza mbingu.+ Ninaziita, ili ziendelee kusimama pamoja.+
14 “Kusanyikeni pamoja, ninyi nyote, msikie.+ Ni nani kati yao ameyatangaza mambo haya? Yehova mwenyewe amempenda.+ Atafanya mapendezi yake juu ya Babiloni,+ na mkono wake mwenyewe utakuwa juu ya Wakaldayo.+ 15 Mimi—mimi mwenyewe nimesema. Na zaidi ya hayo, nimemwita yeye.+ Nimemleta, na njia yake itafanikishwa.+
16 “Njooni karibu nami. Sikieni hili. Tangu mwanzo sikusema kutoka katika mahali pa maficho hata kidogo.+ Tangu wakati wa kutokea kwake mimi nimekuwa pale.”
Na sasa Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova mwenyewe amenituma, ndiyo, roho yake.+ 17 Yehova, Mkombozi wako,+ Mtakatifu wa Israeli,+ amesema hivi: “Mimi, Yehova, ni Mungu wako, Yeye anayekufundisha ili ujifaidi mwenyewe,+ Yeye anayekufanya uende katika njia unayopaswa kutembea ndani yake.+ 18 Laiti ungesikiliza amri zangu!+ Ndipo amani yako ingekuwa kama mto,+ na uadilifu wako kama mawimbi ya bahari.+ 19 Na uzao wako ungekuwa kama tu mchanga, na wazao kutoka tumboni mwako wangekuwa kama chembe zake.+ Jina lake halingekatiliwa mbali wala kuangamizwa kutoka mbele zangu.”+
20 Tokeni katika Babiloni!+ Kimbieni kutoka kwa Wakaldayo.+ Tangazeni kwa sauti ya vigelegele vya shangwe, fanyeni hili lisikiwe.+ Lifanyeni liende mpaka mwisho wa dunia.+ Semeni: “Yehova amemkomboa mtumishi wake Yakobo.+ 21 Nao hawakupata kiu+ alipokuwa akiwatembeza kupitia mahali palipo ukiwa.+ Alitiririsha kwa ajili yao maji kutoka katika mwamba, naye aliupasua mwamba ili maji yatiririke.”+