Ufunuo
17 Na mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na mabakuli saba+ akaja, akasema nami, akaniambia: “Njoo, nitakuonyesha hukumu juu ya yule kahaba+ mkubwa anayekaa juu ya maji mengi,+ 2 ambaye wafalme wa dunia walifanya uasherati naye,+ na wale ambao hukaa katika dunia walileweshwa kwa divai ya uasherati wake.”+
3 Naye akanichukua katika nguvu za roho+ kuingia nyikani. Nami nikamwona mwanamke ameketi juu ya mnyama-mwitu+ mwenye rangi nyekundu aliyejaa majina ya makufuru+ na aliyekuwa na vichwa saba+ na pembe kumi. 4 Na mwanamke yule alikuwa amevikwa nguo za rangi ya zambarau+ na nyekundu,+ naye alikuwa amepambwa dhahabu na jiwe la thamani na lulu+ na mkononi mwake alikuwa na kikombe cha dhahabu+ kilichojaa machukizo+ na mambo machafu ya uasherati wake.+ 5 Na juu ya paji la uso wake jina, fumbo,+ lilikuwa limeandikwa: “Babiloni Mkubwa, mama wa makahaba+ na wa machukizo ya dunia.”+ 6 Nami nikaona kwamba yule mwanamke amelewa damu+ ya watakatifu na damu ya mashahidi wa Yesu.+
Basi, nilipomwona nilishangaa kwa mshangao mkubwa.+ 7 Na kwa hiyo yule malaika akaniambia: “Kwa nini ulishangaa? Nitakuambia fumbo la yule mwanamke+ na la yule mnyama-mwitu anayembeba na aliye na vichwa saba na pembe kumi:+ 8 Mnyama-mwitu uliyemwona alikuwako,+ lakini hayuko, na bado yuko karibu kupanda kutoka katika abiso,+ naye ataenda kwenye uharibifu. Na watakapoona jinsi yule mnyama-mwitu alivyokuwako, lakini hayuko, na bado atakuwapo, wale wanaokaa duniani watamsifu kwa mshangao, lakini majina yao hayakuandikwa kwenye kile kitabu cha kukunjwa cha uzima+ tangu kuwekwa kwa msingi wa ulimwengu.+
9 “Hapa ndipo inapohitajiwa akili yenye hekima:+ Vile vichwa saba+ vinamaanisha milima saba,+ ambapo yule mwanamke huketi juu. 10 Na kuna wafalme saba: watano wameanguka,+ mmoja yuko,+ yule mwingine bado hajafika,+ lakini atakapofika lazima adumu kwa muda mfupi.+ 11 Na yule mnyama-mwitu aliyekuwako lakini hayuko,+ yeye mwenyewe pia ni mfalme wa nane, lakini anatokana na wale saba, naye anaenda zake kwenye uharibifu.
12 “Na zile pembe kumi ulizoona zinamaanisha wafalme kumi,+ ambao bado hawajapokea ufalme, lakini wanapokea mamlaka wakiwa wafalme saa moja pamoja na yule mnyama-mwitu. 13 Hawa wana wazo moja, na kwa hiyo wanampa yule mnyama-mwitu nguvu na mamlaka yao.+ 14 Hawa watapigana na Mwana-Kondoo,+ lakini, kwa sababu yeye ni Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme,+ Mwana-Kondoo atawashinda.+ Pia, wale walioitwa na waliochaguliwa na walio waaminifu pamoja naye watawashinda.”+
15 Naye ananiambia: “Yale maji uliyoyaona, ambapo yule kahaba anaketi, yanamaanisha vikundi vya watu na umati na mataifa na lugha.+ 16 Na zile pembe kumi+ ulizoona, na yule mnyama-mwitu,+ hawa watamchukia yule kahaba+ na kumfanya kuwa ukiwa na uchi, nao watakula sehemu zake zenye nyama na kumteketeza kabisa kwa moto.+ 17 Kwa maana Mungu alitia hilo ndani ya mioyo yao ili kutekeleza wazo lake,+ kutekeleza lile wazo lao moja kwa kumpa yule mnyama-mwitu ufalme wao,+ mpaka maneno ya Mungu yatakapokwisha kutimizwa.+ 18 Na yule mwanamke+ uliyemwona anamaanisha lile jiji kubwa lililo na ufalme juu ya wafalme wa dunia.”+