SEFANIA
1 Neno la Yehova lililomjia Sefania* mwana wa Kushi mwana wa Gedalia mwana wa Amaria mwana wa Hezekia katika siku za Yosia+ mwana wa Amoni+ mfalme wa Yuda:
2 “Nitafagilia mbali kabisa kila kitu kutoka katika nchi,” asema Yehova.+
3 “Nitamfagilia mbali mwanadamu na mnyama.
Nitamfagilia mbali ndege wa angani na samaki wa baharini,+
Na pia vitu vinavyokwaza*+ pamoja na waovu;
Nami nitawaondoa wanadamu kutoka katika nchi,” asema Yehova.
4 “Nitaunyoosha mkono wangu dhidi ya watu wa Yuda
Na dhidi ya wakaaji wote wa Yerusalemu,
Nami nitafutilia mbali kutoka mahali hapa kila kitu kinachohusiana na* Baali,+
Jina la makuhani wa miungu ya kigeni pamoja na makuhani wenyewe,+
5 Na wale wanaoliinamia jeshi la mbinguni wakiwa juu ya paa,+
Na wale wanaoinama chini na kuapa kwamba watakuwa washikamanifu kwa Yehova+
Na wakati uleule wakiapa kwamba watakuwa washikamanifu kwa Malkamu;+
6 Na wale wanaogeuka na kuacha kumfuata Yehova+
Na wale wasiomtafuta Yehova wala kuomba ushauri wake.”+
7 Nyamazeni mbele za Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, kwa maana siku ya Yehova iko karibu.+
Yehova ametayarisha dhabihu; amewatakasa wale aliowaalika.
8 “Katika siku ya dhabihu ya Yehova nitawafanya wakuu wawajibike,
Wana wa mfalme,+ na wote wanaovaa mavazi ya kigeni.
9 Siku hiyo nitamfanya kila mtu anayepanda jukwaani* awajibike,
Wale wanaojaza nyumba ya bwana wao ukatili na udanganyifu.
10 Siku hiyo,” asema Yehova,
“Kutakuwa na sauti ya kilio kwenye Lango la Samaki,+
Mayowe katika wilaya ya pili ya jiji,+
Na mshindo mkubwa vilimani.
11 Pigeni mayowe, enyi wakaaji wa Makteshi,*
Kwa maana wafanyabiashara wote wameangamizwa;*
Wote wanaopima fedha wameuawa.
12 Wakati huo nitatumia taa kupekua Yerusalemu kwa makini,
Nami nitawafanya wasiojali* wawajibike, wanaosema moyoni mwao,
‘Yehova hatatenda mema, wala hatatenda mabaya.’+
13 Utajiri wao utaporwa na nyumba zao zitaharibiwa kabisa.+
Watajenga nyumba, lakini hawatakaa ndani yake;
Nao watapanda mashamba ya mizabibu, lakini hawatakunywa divai yake.+
14 Ile siku kuu ya Yehova iko karibu!+
Iko karibu, nayo inakuja haraka sana!*+
Sauti ya siku ya Yehova ni chungu.+
Siku hiyo shujaa atalia kwa sauti.+
15 Siku hiyo ni siku ya ghadhabu,+
Siku ya taabu na maumivu makali,+
Siku ya dhoruba na ukiwa,
Siku ya giza na utusitusi,+
Siku ya mawingu na utusitusi mzito,+
16 Siku ya pembe na ya kelele za vita,+
Dhidi ya majiji yenye ngome na dhidi ya minara mirefu ya pembeni.+
18 Fedha yao wala dhahabu yao haitaweza kuwaokoa katika siku ya ghadhabu ya Yehova;+
Kwa maana dunia yote itateketezwa kwa moto wa bidii yake,+
Kwa sababu atawaangamiza kabisa wakaaji wote wa dunia, kwa kweli yatakuwa maangamizi yenye kutisha.”+
2 Kabla amri haijatekelezwa,
Kabla siku hiyo haijapeperuka kama makapi,
Kabla hasira inayowaka ya Yehova haijaja juu yenu,+
Kabla siku ya hasira ya Yehova haijaja juu yenu,
Utafuteni uadilifu, utafuteni upole.*
Huenda* mtafichwa katika siku ya hasira ya Yehova.+
5 “Ole kwa wale wanaokaa pwani, taifa la Wakerethi!+
Neno la Yehova liko dhidi yenu.
Ee Kanaani, nchi ya Wafilisti, nitakuangamiza,
Hivi kwamba hakuna mkaaji atakayebaki.
6 Na eneo la pwani litakuwa eneo la malisho,
Lenye visima kwa ajili ya wachungaji na mazizi ya mawe kwa ajili ya kondoo.
Jioni watalala chini katika nyumba za Ashkeloni.
8 “Nimesikia shutuma za Moabu+ na matusi ya Waamoni,+
Ambao wamewadhihaki watu wangu na kujigamba kwa vitisho dhidi ya eneo lao.+
9 Kwa hiyo, kwa hakika kama ninavyoishi,” asema Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli,
“Moabu itakuwa tu kama Sodoma,+
Na Waamoni kama Gomora,+
Mahali penye upupu, shimo la chumvi, na nchi iliyoachwa ukiwa milele.+
Watu wangu waliobaki watawapora,
Na watu waliobaki wa taifa langu watamiliki nchi yao.
10 Hayo ndiyo watakayopata badala ya kiburi chao,+
Kwa sababu waliwadhihaki na kujikweza dhidi ya watu wa Yehova wa majeshi.
11 Yehova atawaogopesha sana;*
Kwa maana ataiharibu kabisa* miungu yote ya dunia,
Na visiwa vyote vya mataifa vitamwinamia,*+
Kila kisiwa kikiwa mahali pake.
12 Ninyi Waethiopia mtauawa pia kwa upanga wangu.+
13 Ataunyoosha mkono wake kuelekea kaskazini na kuangamiza Ashuru,
Naye atalifanya Ninawi liwe ukiwa,+ liwe kavu kama jangwa.
14 Mifugo italala ndani yake, kila aina ya wanyama wa mwituni.*
Mwari na nungunungu watalala usiku kati ya nguzo zake zilizoanguka.
Sauti itaimba dirishani.
Kutakuwa na uharibifu kwenye kizingiti;
Kwa maana atafunua mbao za mierezi zinazopamba kuta.
15 Hili ndilo jiji lenye kiburi lililokuwa likikaa kwa usalama,
Lililokuwa likisema moyoni mwake, ‘Mimi ndiye, na hakuna mwingine yeyote.’
Jinsi ambavyo limekuwa kitu chenye kutisha,
Mahali ambapo wanyama wa mwituni wanalala!
Kila mtu anayepita karibu nalo atapiga mluzi na kutikisa ngumi yake.”+
3 Ole kwa jiji lenye uasi, lenye uchafu, lenye ukandamizaji!+
2 Halijatii sauti yoyote;+ halijakubali nidhamu yoyote.+
Halijamtumaini Yehova;+ halijamkaribia Mungu wake.+
3 Wakuu wake walio ndani yake ni simba wanaonguruma.+
Waamuzi wake ni mbwamwitu wakati wa usiku;
Hawaachi hata mfupa mmoja wa kuguguna mpaka asubuhi.
4 Manabii wake ni wakaidi, wanaume wenye hila.+
5 Yehova ni mwadilifu miongoni mwake;+ hatendi kosa lolote.
Asubuhi baada ya asubuhi hutangaza hukumu zake,+
Kama nuru ya mchana isivyokosa kuangaza.
Lakini asiye mwadilifu haoni aibu hata kidogo.+
6 “Niliyaangamiza mataifa; minara yao ya pembeni iliachwa ukiwa.
Niliharibu barabara zao, hivi kwamba hakuna yeyote aliyepita.
Majiji yao yaliachwa magofu, bila mtu yeyote, bila mkaaji yeyote.+
7 Nikasema, ‘Hakika mtaniogopa na kukubali nidhamu,’*+
Lakini walitamani hata zaidi kutenda kwa upotovu.+
8 ‘Kwa hiyo endeleeni kunitarajia,’*+ asema Yehova,
‘Mpaka siku nitakapoinuka ili kuchukua nyara,*
Kwa maana uamuzi wangu wa hukumu ni kuyakusanya mataifa, kuzikusanya falme,
Niwamwagie ghadhabu yangu, hasira yangu yote inayowaka;+
Kwa maana dunia yote itateketezwa kwa moto wa bidii yangu.+
9 Kwa maana wakati huo nitabadili lugha ya mataifa iwe lugha safi,
Ili wote waweze kuliitia jina la Yehova,
10 Kutoka eneo la mito ya Ethiopia,
Wale wanaonisihi, binti ya watu wangu waliotawanywa, wataniletea zawadi.+
Kwa maana wakati huo nitawaondoa kati yenu watu wenye kiburi wanaojigamba;
Nanyi hamtakuwa tena na kiburi katika mlima wangu mtakatifu.+
12 Nitawaruhusu watu wanyenyekevu na wapole wabaki miongoni mwenu,+
Nao watapata kimbilio katika jina la Yehova.
13 Waisraeli watakaobaki+ hawatatenda mambo yasiyo ya uadilifu;+
Hawatasema uwongo, wala hawatakuwa na ndimi za udanganyifu vinywani mwao;
14 Paza sauti kwa shangwe, Ee binti ya Sayuni!
Paza sauti kwa ushindi, Ee Israeli!+
Shangilia na kufurahi kwa moyo wako wote, Ee binti ya Yerusalemu!+
15 Yehova ameondoa hukumu ulizokabili.+
Amemfukuza adui yako.+
Mfalme wa Israeli, Yehova, yuko katikati yako.+
Hutaogopa msiba tena.+
16 Siku hiyo jiji la Yerusalemu litaambiwa:
“Usiogope, Ee Sayuni.+
Usilegeze mikono yako.
17 Yehova Mungu wako yuko katikati yako.+
Akiwa Mwenye nguvu, ataokoa.
Atakushangilia kwa shangwe kubwa.+
Atakaa kimya* katika upendo wake.
Atakushangilia kwa kelele za shangwe.
18 Nitawakusanya pamoja wale wanaohuzunika kwa sababu ya kukosa sherehe zako;+
Hawakuwa pamoja nawe kwa sababu ya kubeba shutuma yake.+
19 Tazama! Wakati huo nitawachukulia hatua wote wanaokukandamiza;+
Nami nitamwokoa yule anayechechemea,+
Nitawakusanya pamoja waliotawanyika.+
Nitawafanya kuwa kitu cha sifa na umaarufu*
Katika kila nchi ambamo waliaibishwa.
20 Wakati huo nitawaleta ndani,
Wakati nitakapowakusanya pamoja.
Kwa maana nitawafanya kuwa kitu cha umaarufu* na sifa+ miongoni mwa mataifa yote duniani,
Nitakapowakusanya mateka wenu mbele ya macho yenu,” asema Yehova.+
Maana yake “Yehova Ameficha (Amesitiri Kama Hazina).”
Inaonekana kwamba ni vitu au mambo yanayohusiana na ibada ya sanamu.
Au “dalili yoyote ya.”
Au “kwenye kizingiti.” Labda ni jukwaa la kiti cha mfalme.
Inaonekana ni eneo la Yerusalemu lililokuwa karibu na Lango la Samaki.
Tnn., “wamenyamazishwa.”
Tnn., “wanaoganda juu ya machicha yao,” kana kwamba wamo ndani ya mtungi wa kushinikizia divai.
Au “inakuja kwa kasi sana!”
Tnn., “matumbo.”
Au “wanyenyekevu.”
Tnn., “hukumu yake.”
Au “unyenyekevu.”
Au “Inaelekea.”
Au “adhuhuri.”
Au “atawatunza.”
Au “atawatisha.”
Au “ataidhoofisha.”
Au “vitamwabudu.”
Tnn., “kila mnyama wa mwituni katika taifa.”
Au “kurekebishwa.”
Au “niliadhibu.”
Au “kuningojea kwa subira.”
Au labda, “nitakapoinuka nikiwa shahidi.”
Au “wamwabudu kwa umoja.”
Au “Watajilisha malishoni.”
Au “Atanyamaza; Atatulia; Ataridhika.”
Tnn., “jina.”
Tnn., “jina.”