Isaya
63 Ni nani huyu anayetoka Edomu,+ aliye na mavazi yenye rangi zinazong’aa kutoka Bosra,+ huyu ambaye ana nguo zenye kuheshimika, anayetembea katika wingi wa nguvu zake?
“Ni mimi, Yeye ambaye husema katika uadilifu,+ Yeye ambaye ni mwingi wa nguvu za kuokoa.”+
2 Kwa nini nguo zako ni nyekundu, na mavazi yako ni kama yale ya mtu anayekanyaga ndani ya shinikizo la divai?+
3 “Mimi mwenyewe nimelikanyaga pipa la divai,+ kulipokuwa hakuna mtu yeyote pamoja nami kutoka katika vikundi vya watu. Nami niliendelea kuwakanyaga katika hasira yangu,+ niliendelea kuwakanyagia chini katika ghadhabu yangu.+ Na damu yao inayobubujika ikaendelea kutawanyika juu ya mavazi yangu,+ nami nimezichafua nguo zangu zote. 4 Kwa maana siku ya kisasi imo moyoni mwangu,+ na ule mwaka wa watu wangu waliokombolewa umekuja. 5 Nami niliendelea kutazama, lakini hapakuwa na msaidizi; nikaanza kushangaa, lakini hapakuwa na yeyote aliyetegemeza.+ Kwa hiyo mkono wangu ukanipa wokovu,+ na ghadhabu+ yangu ndiyo iliyonitegemeza. 6 Nami katika hasira yangu niliendelea kuvikanyagia chini vikundi vya watu, na katika ghadhabu yangu nikaendelea kuwalewesha+ na kuimwaga chini damu yao inayobubujika.”+
7 Nitazisema fadhili zenye upendo za Yehova,+ sifa za Yehova, kulingana na yote ambayo Yehova ametutendea,+ wema mwingi kwa nyumba ya Israeli+ ambao amewatendea kulingana na rehema+ zake na kulingana na wingi wa fadhili zake zenye upendo. 8 Naye aliendelea kusema: “Hakika wao ni watu wangu,+ wana ambao hawataonekana kuwa waongo.”+ Basi akawa Mwokozi+ wao. 9 Wakati wa taabu zao zote hilo lilimtaabisha.+ Na mjumbe wake binafsi akawaokoa.+ Katika upendo wake na katika huruma yake yeye mwenyewe aliwakomboa,+ naye akawainua na kuwachukua siku zote za zamani za kale.+
10 Lakini wao wenyewe waliasi+ na kuihuzunisha roho yake takatifu.+ Sasa alibadilika akawa adui+ yao; yeye mwenyewe alipiga vita juu yao.+ 11 Na mtu akaanza kuzikumbuka siku za zamani za kale, Musa mtumishi wake: “Yuko wapi Yeye aliyewapandisha kutoka katika bahari+ pamoja na wachungaji wa kundi lake?+ Yuko wapi Yeye aliyetia ndani yake roho Yake takatifu?+ 12 Yeye aliyeufanya mkono+ Wake mzuri uende upande wa mkono wa kuume wa Musa; Yeye aliyegawanya maji kutoka mbele yao+ ili kujifanyia mwenyewe jina linalodumu mpaka wakati usio na kipimo;+ 13 Yeye aliyewatembeza kupitia katikati ya maji yenye kututumuka hivi kwamba, kama farasi nyikani, hawakujikwaa?+ 14 Kama vile mnyama anavyoteremka ndani ya nchi tambarare ya bondeni, ndivyo roho ya Yehova ilivyowapumzisha.”+
Hivyo uliwaongoza watu wako ili ujifanyie mwenyewe jina zuri.+
15 Tazama kutoka mbinguni,+ uone kutoka katika makao yako yaliyoinuliwa ya utakatifu na uzuri.+ Iko wapi bidii+ yako na nguvu zako kamili, msukosuko wa sehemu zako za ndani,+ na rehema+ zako? Zimejizuia kunielekea.+ 16 Kwa maana wewe ni Baba yetu,+ ingawa huenda iwe Abrahamu mwenyewe hakutujua na huenda iwe Israeli mwenyewe asitutambue, wewe, Ee Yehova, ni Baba yetu. Mkombozi wetu wa zamani za kale ni jina lako.+ 17 Kwa nini, Ee Yehova, unaendelea kutufanya tutange-tange kutoka katika njia zako? Kwa nini unafanya moyo wetu uwe mgumu ili usikuogope?+ Rudi kwa ajili ya watumishi wako, makabila ya fungu lako la urithi.+ 18 Kwa muda kidogo watu wako watakatifu+ walikuwa na miliki. Adui zetu wenyewe wamepakanyaga patakatifu pako.+ 19 Kwa muda mrefu tumekuwa kama watu ambao hukutawala juu yao, kama wale ambao jina lako halikuwa limeitwa juu yao.+