Kwa Tito
1 Paulo, mtumwa+ wa Mungu na mtume+ wa Yesu Kristo kulingana na imani ya waliochaguliwa+ wa Mungu na ujuzi sahihi+ wa ile kweli+ ambayo inapatana na ujitoaji-kimungu+ 2 juu ya msingi wa tumaini la uzima wa milele+ ambao Mungu, asiyeweza kusema uwongo,+ aliahidi nyakati za zamani za kale,+ 3 lakini katika nyakati zake mwenyewe zinazofaa alifanya neno lake liwe wazi katika kazi ya kuhubiri ambayo nilikabidhiwa,+ chini ya amri ya Mwokozi wetu,+ Mungu; 4 kwa Tito, mtoto wangu+ kwelikweli kulingana na imani inayoshirikiwa kwa pamoja:
Na kuwe na fadhili zisizostahiliwa na amani kutoka kwa Mungu Baba+ na Kristo Yesu Mwokozi wetu.+
5 Kwa sababu hii nilikuacha wewe Krete,+ ili uyarekebishe mambo yaliyokuwa na kasoro na uweke rasmi+ wanaume wazee katika jiji baada ya jiji, kama nilivyokupa maagizo;+ 6 ikiwa kuna mwanamume yeyote asiye na shtaka,+ mume wa mke mmoja,+ mwenye watoto wanaoamini ambao hawako chini ya shtaka la kuwa wapotovu wala la kuwa watundu.+ 7 Kwa maana mwangalizi lazima awe bila shtaka+ kama msimamizi-nyumba+ wa Mungu, asiwe mshupavu,+ asiwe mwepesi wa ghadhabu,+ asiwe mlevi mwenye fujo,+ asiwe mwenye kupiga watu,+ asiwe mwenye pupa ya pato lisilo la haki,+ 8 bali awe mkaribishaji-wageni,+ mpenda-wema, mwenye utimamu wa akili,+ mwadilifu, mshikamanifu,+ mwenye kujizuia,+ 9 akilishika imara neno la uaminifu kuhusiana na ufundi wake wa kufundisha,+ ili aweze kuhimiza kwa fundisho lenye afya+ na pia kuwakaripia+ wale ambao hulipinga.
10 Kwa maana kuna watu wengi watundu, wanaoongea maneno yasiyo na faida,+ na wanaodanganya akili za watu, hasa watu wale ambao hushikamana na tohara.+ 11 Ni jambo la lazima kuvifunga vinywa vya watu hao, kwa kuwa watu hao wanaendelea kuharibu nyumba nzima-nzima+ kwa kufundisha mambo ambayo hawapaswi kufundisha, ili kupata pato lisilo la haki.+ 12 Mtu fulani kati yao, nabii wao wenyewe, alisema: “Wakrete ni waongo sikuzote, wanyama-mwitu wenye kudhuru,+ walafi wasiofanya kazi.”
13 Ushahidi huu ni kweli. Kwa sababu hiyo endelea kuwakaripia kwa ukali,+ ili wawe na afya+ katika imani, 14 bila kusikiliza hadithi zisizo za kweli za Kiyahudi+ na amri za watu+ ambao hugeuka na kuiacha kweli.+ 15 Vitu vyote ni safi kwa watu safi.+ Lakini kwa watu waliotiwa unajisi+ na wasio na imani+ hakuna kitu chochote kilicho safi, bali akili zao na pia dhamiri+ zao zimetiwa unajisi. 16 Wao hutangaza hadharani kwamba wanamjua Mungu,+ lakini humkana kwa matendo yao,+ kwa sababu ni wenye kuchukiza na wasiotii nao si wenye kukubalika+ kwa ajili ya kazi njema ya namna yoyote.
2 Hata hivyo, wewe endelea kusema mambo yale yanayofaa kwa ajili ya fundisho lenye afya.+ 2 Wanaume wenye umri mkubwa+ wawe na kiasi katika mazoea, wenye kuchukua mambo kwa uzito,+ wenye utimamu wa akili, wenye afya katika imani,+ katika upendo, katika uvumilivu.+ 3 Vivyo hivyo wanawake wenye umri mkubwa+ wawe wenye tabia ya kumhofu Mungu, si wachongezi,+ wala si watumwa wa divai nyingi sana, wawe walimu wa yaliyo mema; 4 ili kuziamsha akili za wanawake vijana wawapende waume zao,+ wawapende watoto wao,+ 5 wawe na utimamu wa akili, safi kiadili,+ wafanyakazi nyumbani, wema, wakijitiisha+ kwa waume zao wenyewe, ili neno la Mungu lisitukanwe.+
6 Vivyo hivyo endelea kuwahimiza wanaume vijana wawe na utimamu wa akili,+ 7 katika mambo yote ukijionyesha kuwa kielelezo cha matendo mazuri;+ ukionyesha uaminifu+ katika fundisho lako,+ kuchukua mambo kwa uzito, 8 na kuwa na maneno yenye afya yasiyoweza kulaumiwa;+ ili mtu anayepinga aone aibu, akiwa hana jambo lolote baya la kusema juu yetu.+ 9 Watumwa+ na wajitiishe kwa mabwana wao katika mambo yote,+ na kuwapendeza kikamili, wasiwe wakiwajibu kwa ujeuri,+ 10 wasiwe wakiiba,+ bali wawe wakionyesha uaminifu mwema kwa ukamili,+ ili walipambe fundisho la Mwokozi wetu,+ Mungu, katika mambo yote.
11 Kwa maana fadhili zisizostahiliwa+ za Mungu zinazowaletea watu wa namna zote+ wokovu+ zimeonyeshwa,+ 12 zikitufundisha kukataa kabisa kutomwogopa Mungu+ na tamaa za kilimwengu+ na tuishi kwa utimamu wa akili na uadilifu na ujitoaji-kimungu+ katikati ya mfumo wa mambo wa sasa,+ 13 huku tukilingojea tumaini la furaha+ na kufunuliwa kwenye utukufu+ kwa Mungu mkuu na kwa Mwokozi wetu, Kristo Yesu, 14 aliyejitoa mwenyewe+ kwa ajili yetu ili atukomboe+ sisi kutoka katika kila namna ya uasi-sheria na kujisafishia+ mwenyewe watu walio wake kwa njia ya pekee,+ walio na bidii kwa ajili ya kazi njema.+
15 Endelea kusema mambo haya na kuhimiza na kukaripia kwa mamlaka kamili ya kuamuru.+ Usiache kamwe mtu yeyote akudharau.+
3 Endelea kuwakumbusha wajitiishe+ na kuzitii serikali na mamlaka zikiwa watawala,+ wawe tayari kwa ajili ya kila kazi njema,+ 2 wasiseme vibaya juu ya yeyote, wasiwe wataka-vita,+ wawe wenye usawaziko,+ wakionyesha upole wote kuelekea watu wote.+ 3 Kwa maana hata sisi wakati mmoja tulikuwa watu wasio na akili, wasiotii, tukipotoshwa, tukiwa watumwa wa tamaa na raha za namna mbalimbali, tukiendelea katika ubaya na wivu, wenye kuchukiza, tukichukiana.+
4 Hata hivyo, wakati Mwokozi wetu,+ Mungu, alipoonyesha+ fadhili+ na upendo kwa mwanadamu, 5 si kutokana na matendo yoyote+ ya uadilifu ambayo tulikuwa tumefanya,+ bali kulingana na rehema+ yake alituokoa kupitia kuoshwa+ kulikotuleta kwenye uzima+ na kupitia kutufanya sisi kuwa wapya kwa roho takatifu.+ 6 Roho hii yeye aliimimina kwa wingi juu yetu kupitia Yesu Kristo Mwokozi wetu,+ 7 ili, baada ya kutangazwa kuwa waadilifu+ kwa msingi wa fadhili zisizostahiliwa zake huyo,+ sisi tuwe warithi+ kulingana na tumaini la uzima wa milele.+
8 Neno hilo ni la uaminifu,+ na kuhusu mambo hayo ninatamani usisitize kwa nguvu daima, ili wale ambao wamemwamini Mungu wakaze akili zao juu ya kudumisha matendo yaliyo mazuri.+ Mambo hayo ni mazuri na yenye faida kwa watu.
9 Lakini epuka maswali ya upumbavu+ na kutafuta-tafuta ukoo+ na mizozo+ na mapigano juu ya Sheria,+ kwa maana hayo hayana faida na ni ya ubatili. 10 Kwa habari ya mtu anayeendeleza madhehebu,+ mkatae+ baada ya onyo la kwanza na la pili;+ 11 ukijua kwamba mtu wa namna hiyo amegeuzwa kutoka njiani na anafanya dhambi, yeye akiwa amejihukumia hatia mwenyewe.+
12 Nitakapomtuma Artema au Tikiko+ kwako, fanya yote unayoweza uje kwangu katika Nikopoli, kwa maana nimeamua kukaa huko wakati wa majira ya baridi kali.+ 13 Ili wasikose kitu chochote kwa ajili ya safari yao, kwa uangalifu mpe mahitaji Zena, aliye na ujuzi mwingi wa Sheria, na Apolo.+ 14 Lakini acha watu wetu pia wajifunze kudumisha matendo mazuri ili kutimiza mahitaji yao muhimu,+ ili wasiwe wasiozaa matunda.+
15 Wote walio pamoja nami wanakutumia salamu zao.+ Wape salamu zangu wale wanaotupenda katika imani.
Fadhili zisizostahiliwa na ziwe pamoja nanyi nyote.+