Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bi12 2 Timotheo 1:1-4:22
  • Barua ya Pili kwa Timotheo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Barua ya Pili kwa Timotheo
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Barua ya Pili kwa Timotheo

Barua ya Pili kwa Timotheo

1 Paulo, mtume wa Kristo Yesu kupitia mapenzi ya Mungu+ kulingana na ahadi ya uzima+ ulio katika muungano na Kristo Yesu,+ 2 kwa Timotheo, mtoto mpendwa:+

Na kuwe na fadhili zisizostahiliwa, rehema, amani kutoka kwa Mungu Baba na Kristo Yesu Bwana wetu.+

3 Ninamshukuru Mungu, ninayemtolea utumishi mtakatifu+ kama mababu+ zangu walivyofanya na nikiwa na dhamiri safi,+ kwamba siachi kamwe kukukumbuka katika dua zangu,+ usiku na mchana 4 nikitamani kukuona wewe,+ ninapoyakumbuka machozi yako, ili nijawe na shangwe. 5 Kwa maana naikumbuka imani+ iliyo ndani yako isiyo na unafiki+ wowote, na ambayo ilikaa kwanza katika nyanya yako Loisi na mama yako Eunike, lakini ambayo mimi nina hakika imo ndani yako pia.

6 Kwa sababu hii nakukumbusha wewe uichochee kama moto+ zawadi+ ya Mungu iliyo ndani yako kupitia kuwekwa kwa mikono yangu juu yako.+ 7 Kwa maana Mungu hakutupa sisi roho ya woga,+ bali ile ya nguvu+ na ya upendo na ya utimamu wa akili.+ 8 Kwa hiyo usione aibu juu ya ule ushahidi kumhusu Bwana wetu,+ wala kunihusu mimi mfungwa kwa ajili yake,+ bali shiriki sehemu yako katika kuvumilia+ uovu kwa ajili ya habari njema kulingana na nguvu za Mungu.+ 9 Yeye alituokoa+ na kutuita kwa mwito mtakatifu,+ si kwa sababu ya matendo+ yetu, bali kwa sababu ya kusudi lake mwenyewe na fadhili zisizostahiliwa. Tulipewa hizo kuhusiana na Kristo Yesu kabla ya nyakati za zamani za kale,+ 10 lakini sasa zimefanywa kuwa wazi kabisa kupitia ufunuo+ wa Mwokozi wetu, Kristo Yesu, ambaye amefuta kifo+ lakini ameangaza nuru+ juu ya uzima+ na kutoweza kuharibika+ kupitia habari njema,+ 11 ambayo kwa ajili yake mimi niliwekwa rasmi kuwa mhubiri na mtume na mwalimu.+

12 Kwa sababu hii ninavumilia+ pia mambo haya, lakini sioni aibu.+ Kwa maana namjua yule ambaye nimemwamini, nami nina hakika anaweza kukilinda+ kile ambacho nimeweka amana kwake mpaka siku ile.+ 13 Endelea kushika kielelezo cha maneno yenye afya+ uliyosikia kutoka kwangu pamoja na imani na upendo vinavyohusiana na Kristo Yesu.+ 14 Amana+ hii nzuri ilinde kupitia roho takatifu inayokaa ndani yetu.+

15 Unajua hili, kwamba watu wote katika wilaya ya Asia+ wamegeuka na kuniacha mimi.+ Figelo na Hermogene ni kati ya hao. 16 Bwana na aipe rehema nyumba ya Onesiforo,+ kwa sababu mara nyingi aliniletea kiburudisho,+ naye hakuionea aibu minyororo yangu.+ 17 Kinyume cha hilo, alipokuwa katika Roma, alinitafuta kwa bidii naye akanipata.+ 18 Bwana na amruhusu apate rehema+ kutoka kwa Yehova katika siku ile.+ Na utumishi wote aliotoa katika Efeso wewe unaujua vema kabisa.

2 Kwa hiyo, wewe mtoto wangu,+ endelea kujipatia nguvu+ katika fadhili zisizostahiliwa+ ambazo ni kuhusiana na Kristo Yesu, 2 na mambo uliyoyasikia kutoka kwangu kwa uthibitisho wa mashahidi wengi,+ mambo hayo uwakabidhi watu waaminifu, ambao nao watakuwa na sifa za kustahili vya kutosha kufundisha wengine.+ 3 Ukiwa askari-jeshi+ mwema wa Kristo Yesu shiriki sehemu yako katika kuvumilia uovu.+ 4 Mtu anayetumikia akiwa askari-jeshi+ hajihusishi katika shughuli za kibiashara za maisha,+ ili apate kibali cha yule aliyemwandika kuwa askari-jeshi. 5 Zaidi ya hayo, kama yeyote akishindana hata katika michezo,+ havikwi taji isipokuwa awe ameshindana kulingana na sheria. 6 Mkulima anayefanya kazi kwa bidii lazima awe wa kwanza kula sehemu ya matunda.+ 7 Fikiria daima yale ninayosema; kwa kweli Bwana atakupa wewe utambuzi+ katika mambo yote.

8 Kumbuka kwamba Yesu Kristo alifufuliwa kutoka kwa wafu+ na alikuwa wa uzao wa Daudi,+ kulingana na habari njema ninayohubiri;+ 9 ambayo kwa kuhusiana nayo ninavumilia uovu kufikia hatua ya vifungo vya gereza+ kama mtenda-maovu. Hata hivyo, neno la Mungu halifungwi.+ 10 Kwa hiyo ninaendelea kuvumilia mambo yote kwa sababu ya waliochaguliwa,+ ili wao pia wapate wokovu ulio katika muungano na Kristo Yesu pamoja na utukufu wa milele.+ 11 Neno hili ni la uaminifu:+ Hakika ikiwa tulikufa pamoja, tutaishi pamoja pia;+ 12 tukiendelea kuvumilia, tutatawala pamoja pia tukiwa wafalme;+ tukimkana,+ yeye pia atatukana sisi; 13 tukikosa kuwa waaminifu, yeye anabaki akiwa mwaminifu,+ kwa maana hawezi kujikana mwenyewe.

14 Endelea kuwakumbusha+ mambo haya, ukiwaagiza+ mbele za Mungu kama shahidi,+ wasipigane juu ya maneno,+ hilo ni jambo ambalo halifai hata kidogo kwa sababu huwaharibu wale wanaosikiliza. 15 Fanya kabisa yote unayoweza ili ujitoe kwa Mungu ukiwa mtu aliyekubaliwa,+ mfanyakazi+ asiye na lolote la kuonea aibu,+ ukilitumia sawasawa neno la kweli.+ 16 Lakini epuka kabisa maneno matupu ambayo huchafua mambo matakatifu;+ kwa maana wataendelea kwenye ukosefu wa kumwogopa Mungu ulio mwingi zaidi na zaidi,+ 17 na neno lao litaenea kama kidonda chenye kuoza.+ Himenayo na Fileto ni kati ya hao.+ 18 Watu hao wamegeuka kutoka kwenye kweli,+ wakisema kwamba ufufuo tayari umetukia;+ nao wanaipindua imani ya wengine.+ 19 Hata hivyo, msingi imara wa Mungu unakaa ukiwa umesimama,+ ukiwa na muhuri huu: “Yehova anawajua walio wake,”+ na: “Kila mtu anayelitaja jina la Yehova+ na aukatae ukosefu wa uadilifu.”+

20 Basi ndani ya nyumba kubwa mna vyombo vya dhahabu na fedha, na pia mna vyombo vya miti na vya udongo, na vingine ni kwa ajili ya kusudi lenye kuheshimika lakini vingine ni kwa ajili ya kusudi lenye kukosa heshima.+ 21 Kwa hiyo, kama yeyote akijiepusha kabisa na hawa wa mwisho, atakuwa chombo kwa ajili ya kusudi lenye kuheshimika, kilichotakaswa, chenye faida kwa bwana wake, kilichotayarishwa kwa ajili ya kila kazi njema.+ 22 Kwa hiyo, zikimbie tamaa zinazotukia ujanani,+ lakini fuatilia uadilifu,+ imani, upendo, amani,+ pamoja na wale wanaomwitia Bwana kutokana na moyo safi.+

23 Zaidi ya hayo, kataa maswali ya upumbavu na ya kijinga,+ ukijua hayo hutokeza mapigano.+ 24 Lakini mtumwa wa Bwana hahitaji kupigana,+ bali anahitaji kuwa mpole kwa wote,+ mwenye sifa za kustahili kufundisha,+ akiendelea kujizuia chini ya uovu,+ 25 akiwafundisha kwa upole wale wasio na mwelekeo unaofaa;+ kwa kuwa huenda Mungu akawapa toba+ inayoongoza kwenye ujuzi sahihi juu ya kweli,+ 26 nao warudiwe na fahamu zao nzuri ili watoke katika mtego+ wa Ibilisi, kwa kuwa amewashika wakiwa hai+ kwa ajili ya mapenzi ya huyo.

3 Lakini ujue jambo hili, ya kwamba katika siku za mwisho+ kutakuwa na nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo.+ 2 Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda pesa, wenye kujidai, wenye majivuno, wakufuru, wasiotii wazazi,+ wasio na shukrani, wasio washikamanifu,+ 3 wasio na upendo wa asili,+ wasiotaka makubaliano yoyote,+ wachongezi,+ wasiojizuia, wakali,+ wasiopenda wema,+ 4 wasaliti,+ wenye vichwa vigumu, wenye kujivuna kwa kiburi,+ wanaopenda raha badala ya kumpenda Mungu+ 5 wakiwa na namna ya ujitoaji-kimungu+ lakini wakizikana nguvu zake;+ nawe geukia mbali kutoka kwa hao.+ 6 Kwa maana kutoka kwa watu hao huinuka wale watu wanaojiingiza kwa ujanja katika nyumba+ na kuwachukua mateka wanawake walio dhaifu ambao wamelemewa na mizigo ya dhambi, wanaoongozwa na tamaa za namna mbalimbali,+ 7 wakijifunza sikuzote na bado hawawezi kamwe kufikia ujuzi sahihi juu ya kweli.+

8 Basi katika njia ambayo Yane na Yambre+ walimpinga Musa, vivyo hivyo hawa pia wanaendelea kuipinga kweli,+ watu walioharibika kabisa akilini,+ waliokataliwa kwa habari ya imani.+ 9 Hata hivyo, hawatafanya maendeleo zaidi, kwa maana wazimu wao utakuwa wazi kwa wote, kama vile ulivyokuwa ule wazimu wa watu hao wawili.+ 10 Lakini wewe umefuata kwa ukaribu fundisho langu, mwendo wangu wa maisha,+ kusudi langu, imani yangu, ustahimilivu wangu, upendo wangu, uvumilivu wangu, 11 mateso yangu, masumbufu yangu, namna ya mambo yaliyonipata katika Antiokia,+ katika Ikoniamu,+ katika Listra,+ namna ya mateso ambayo nimevumilia; na bado Bwana alinikomboa mimi kutoka katika hayo yote.+ 12 Kwa kweli, wote wanaotamani kuishi kwa ujitoaji-kimungu katika ushirika na Kristo Yesu watateswa pia.+ 13 Lakini watu waovu na wajanja wataendelea kutoka ubaya mpaka ubaya zaidi, wakipotosha na kupotoshwa.+

14 Hata hivyo, wewe endelea katika mambo uliyojifunza na uliyoshawishiwa kuamini,+ ukijua ni kutoka kwa watu gani ulijifunza hayo+ 15 na kwamba tangu utoto mchanga+ umeyajua maandishi matakatifu, ambayo yanaweza kukufanya uwe mwenye hekima kwa ajili ya wokovu+ kupitia imani kuhusiana na Kristo Yesu.+ 16 Andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu+ nalo ni lenye faida kwa kufundisha,+ kwa kukaripia,+ kwa kunyoosha mambo,+ kwa kutia nidhamu+ katika uadilifu, 17 ili mtu wa Mungu awe na uwezo kamili,+ akiwa na vifaa kamili kwa ajili ya kila kazi njema.+

4 Nakuagiza kwa uzito mbele za Mungu na Kristo Yesu,+ ambaye amekusudiwa kuhukumu+ walio hai na wafu,+ na kwa ufunuo+ wake na ufalme wake, 2 lihubiri neno,+ fanya hivyo kwa bidii katika majira yanayofaa,+ katika majira yenye taabu,+ karipia,+ kemea, himiza, kwa ustahimilivu+ wote na ufundi wa kufundisha. 3 Kwa maana kutakuwa na kipindi cha wakati ambapo hawatalivumilia fundisho lenye afya,+ bali, kwa kupatana na tamaa zao wenyewe, watajikusanyia walimu kwa ajili yao wenyewe ili masikio yao yafurahishwe;+ 4 nao watageuza masikio yao kutoka kwenye kweli, nao watageuzwa kando kufuata hadithi za uwongo.+ 5 Ingawa hivyo, wewe tunza akili zako+ katika mambo yote, vumilia uovu,+ fanya kazi ya mweneza-injili,+ timiza kwa ukamili huduma yako.+

6 Kwa maana mimi tayari ninamiminwa kama toleo la kinywaji,+ na wakati unaofaa wa kufunguliwa+ kwangu umekaribia sana. 7 Nimepigana pigano zuri,+ nimekimbia mwendo mpaka mwisho,+ nimeishika imani.+ 8 Tangu wakati huu na kuendelea nimewekewa akiba ya taji la uadilifu,+ ambalo Bwana, aliye mwamuzi mwadilifu,+ atanipa kuwa thawabu+ katika siku ile,+ lakini si mimi tu, bali pia na wale wote ambao wamependa kufunuliwa kwake.

9 Fanya kabisa yote unayoweza ili uje kwangu upesi.+ 10 Kwa maana Dema+ ameniacha kwa sababu aliupenda mfumo wa mambo+ wa sasa, naye ameenda Thesalonike; Kresensi ameenda Galatia,+ Tito ameenda Dalmatia. 11 Luka peke yake ndiye yupo pamoja nami. Umchukue Marko na uje pamoja naye, kwa maana yeye ni mwenye faida+ kwangu kwa ajili ya huduma. 12 Lakini nimemtuma Tikiko+ aende Efeso. 13 Utakapokuja, ilete ile kanzu niliyomwachia Karpo kule Troa,+ na vile vitabu vya kukunjwa, hasa vile vya ngozi.

14 Aleksanda+ yule fundi wa shaba alinitendea mimi mambo mengi mabaya—Yehova atamlipa kulingana na vitendo vyake+— 15 na wewe pia ujilinde juu yake, kwa maana aliyapinga maneno yetu kwa kadiri kubwa mno.

16 Katika kujitetea kwangu mara ya kwanza hakuna yeyote aliyekuja upande wangu, bali wote waliniacha+—hilo lisihesabiwe kwao+— 17 lakini Bwana alisimama karibu nami+ na kutia nguvu ndani yangu,+ ili kupitia mimi kazi ya kuhubiri itimizwe kwa ukamili na mataifa yote yaisikie;+ nami nilikombolewa kutoka katika kinywa cha simba.+ 18 Bwana atanikomboa kutoka katika kila tendo la uovu+ naye ataniokoa kwa ajili ya ufalme wake wa mbinguni.+ Utukufu na uwe kwake milele na milele. Amina.

19 Uwape salamu zangu Priska+ na Akila na nyumba ya Onesiforo.+

20 Erasto+ alibaki Korintho,+ lakini nilimwacha Trofimo+ akiwa mgonjwa kule Mileto.+ 21 Fanya kabisa yote unayoweza ili ufike kabla ya majira ya baridi kali.

Eubulo anakutumia salamu zake, na pia Pudensi na Lino na Klaudia na ndugu wote.

22 Bwana na awe pamoja na roho unayoonyesha.+ Fadhili zake zisizostahiliwa ziwe pamoja nanyi.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki