Barua ya Kwanza kwa Timotheo
1 Paulo, mtume+ wa Kristo Yesu kwa amri ya Mungu+ Mwokozi+ wetu na ya Kristo Yesu, aliye tumaini letu,+ 2 kwa Timotheo,+ mtoto wangu+ kwelikweli katika imani:
Na kuwe na fadhili zisizostahiliwa, rehema, amani kutoka kwa Mungu Baba na Kristo Yesu Bwana wetu.+
3 Kama vile nilivyokutia moyo ukae Efeso nilipokuwa karibu kuondoka na kwenda Makedonia,+ ndivyo ninavyofanya sasa, ili uwaamuru+ watu fulani wasifundishe fundisho tofauti,+ 4 wala kusikiliza hadithi za uwongo+ na mambo ya kutafuta-tafuta ukoo, ambayo mwisho wake si kitu,+ lakini ambayo hutokeza maswali ya utafiti badala ya kugawa kitu chochote kutoka kwa Mungu kuhusiana na imani. 5 Kwa kweli lengo la amri hii ni upendo+ kutokana na moyo safi+ na kutokana na dhamiri njema+ na kutokana na imani bila unafiki.+ 6 Kwa kugeuka na kutoka katika mambo hayo watu fulani wamegeuzwa kando+ kuingia katika maneno ya kipuuzi,+ 7 wakitaka kuwa walimu+ wa sheria,+ lakini hawafahamu ama mambo wanayosema au mambo ambayo wanayasisitiza kwa nguvu.
8 Basi tunajua kwamba Sheria ni nzuri+ ikiwa mtu anaichukua kisheria+ 9 kwa kujua jambo hili, kwamba sheria huwekwa, si kwa ajili ya mtu mwadilifu, bali kwa ajili ya watu wenye kuasi sheria+ na watundu,+ wasiomwogopa Mungu na watenda-dhambi, wasio na fadhili zenye upendo,+ na wenye kutia unajisi, wauaji wa akina baba na wauaji wa akina mama, wenye kuua watu wengine, 10 waasherati,+ wanaume wanaolala na wanaume, watu wanaoteka watu, waongo, wanaoapa kwa uwongo,+ na jambo lingine lolote linalopinga+ fundisho lenye afya+ 11 kulingana na habari njema yenye utukufu ya Mungu mwenye furaha,+ ambayo mimi nilikabidhiwa.+
12 Mimi namshukuru Kristo Yesu Bwana wetu, aliyenipa nguvu, kwa sababu aliniona kuwa mwaminifu+ kwa kunigawia huduma,+ 13 ijapokuwa hapo zamani nilikuwa mkufuru na mtesaji+ na mtu mwenye dharau.+ Hata hivyo, nilionyeshwa rehema,+ kwa sababu nilikosa ujuzi+ nami nilitenda kwa ukosefu wa imani. 14 Lakini fadhili zisizostahiliwa za Bwana wetu zikawa nyingi+ sana pamoja na imani na upendo ambao ni kuhusiana na Kristo Yesu.+ 15 Lile neno linastahili kukubaliwa kikamilifu, linalosema+ kwamba Kristo Yesu alikuja ulimwenguni ili kuwaokoa watenda-dhambi.+ Kati ya hao mimi ni wa kwanza kabisa.+ 16 Hata hivyo, sababu iliyofanya nionyeshwe rehema+ ilikuwa kwamba kupitia mimi nikiwa ndiye wa kwanza kabisa Kristo Yesu aonyeshe ustahimilivu wake wote kuwa mfano wa wale watakaokuwa na imani+ yao kwake kwa ajili ya uzima wa milele.+
17 Sasa kwa Mfalme wa umilele,+ asiyeweza kuharibika,+ asiyeonekana,+ Mungu pekee,+ kuwe na heshima na utukufu milele na milele.+ Amina.
18 Amri hii+ ninakupa wewe, mtoto, Timotheo, kwa kupatana na matabiri+ yaliyoongoza moja kwa moja mpaka kwako, ili kwa hayo uendelee kupigana vita vizuri;+ 19 ukishika imani na dhamiri njema,+ ambayo wengine wameitupa kando+ na imani yao imevunjika.+ 20 Himenayo+ na Aleksanda+ ni kati ya hao, nami nimewatia mkononi mwa Shetani+ ili wafundishwe kwa nidhamu kutokufuru.+
2 Kwa hiyo ninahimiza, kwanza kabisa, kwamba dua, sala,+ maombezi, kutoa shukrani, yafanywe kwa ajili ya watu wa namna zote,+ 2 kwa ajili ya wafalme+ na wale wote walio katika cheo cha juu;+ ili tuendelee kuishi maisha shwari na matulivu pamoja na ujitoaji-kimungu kamili na kuchukua mambo kwa uzito.+ 3 Hili ni zuri nalo linakubalika+ machoni pa Mwokozi wetu, Mungu,+ 4 ambaye mapenzi yake ni kwamba watu wa namna zote+ waokolewe+ na kupata ujuzi sahihi+ wa kweli.+ 5 Kwa maana kuna Mungu mmoja,+ na mpatanishi+ mmoja kati ya Mungu+ na wanadamu,+ mwanadamu, Kristo Yesu,+ 6 aliyejitoa kuwa fidia inayolingana kwa ajili ya wote+—hili ndilo litakalotolewa ushahidi kwenye nyakati zake maalumu. 7 Kwa kusudi la ushahidi+ huo mimi niliwekwa rasmi kuwa mhubiri na mtume+—ninasema kweli,+ sisemi uwongo—mwalimu wa mataifa+ katika jambo linalohusu imani+ na kweli.
8 Kwa hiyo natamani kwamba kila mahali wanaume waendelee kutoa sala, wakiinua mikono+ yenye ushikamanifu, bila ghadhabu+ na mabishano.+ 9 Vivyo hivyo natamani wanawake wajipambe kwa mavazi yenye mpangilio mzuri, pamoja na kiasi+ na utimamu wa akili, si kwa mitindo ya kusuka nywele na dhahabu au lulu au mavazi yaliyo ghali sana,+ 10 bali kwa njia inayowafaa wanawake wanaodai kumheshimu Mungu,+ yaani, kupitia matendo mema.+
11 Mwanamke na ajifunze akiwa kimya na kwa kujitiisha kikamili.+ 12 Simruhusu mwanamke kufundisha,+ wala kuwa na mamlaka juu ya mwanamume,+ bali kuwa kimya. 13 Kwa maana Adamu aliumbwa kwanza, kisha Hawa.+ 14 Pia, Adamu hakudanganywa,+ bali yule mwanamke alidanganywa+ kabisa naye akaingia katika kosa.+ 15 Hata hivyo, mwanamke atabaki salama kupitia kuzaa watoto,+ bora tu waendelee katika imani na upendo na utakaso pamoja na utimamu wa akili.+
Ikiwa mwanamume yeyote anajitahidi kufikia cheo cha mwangalizi,+ yeye anatamani kazi njema. 2 Kwa hiyo mwangalizi anapaswa kuwa asiyelaumika,+ mume wa mke mmoja, mwenye kiasi+ katika mazoea, mwenye utimamu wa akili,+ mwenye utaratibu,+ mkaribishaji-wageni,+ mwenye sifa za kustahili kufundisha,+ 3 si mlevi mwenye fujo,+ si mwenye kupiga watu,+ bali mwenye usawaziko,+ si mtaka-vita,+ si mwenye kupenda pesa,+ 4 mwanamume anayeisimamia nyumba yake mwenyewe kwa njia nzuri,+ mwenye watoto wanaojitiisha pamoja na kuchukua mambo kwa uzito wote;+ 5 (kwa kweli ikiwa mtu yeyote hajui jinsi ya kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje kutaniko la Mungu?) 6 si mtu aliyegeuka hivi karibuni,+ asije akajivuna kwa kiburi+ na kuanguka katika hukumu iliyopitishwa juu ya Ibilisi.+ 7 Zaidi ya hayo, anapaswa pia kuwa na ushuhuda mzuri kutoka kwa watu walio nje,+ ili asianguke katika shutuma na mtego+ wa Ibilisi.
8 Vivyo hivyo watumishi wa huduma+ wanapaswa kuwa wenye kuchukua mambo kwa uzito, si wenye ndimi mbili, si wenye kunywa divai nyingi, si wenye pupa ya pato lisilo la haki,+ 9 wakiishika siri takatifu+ ya imani kwa dhamiri safi.+
10 Pia, acha hao wajaribiwe+ juu ya kufaa kwanza, kisha watumike wakiwa wahudumu, kwa kuwa hawana shtaka.+
11 Vivyo hivyo wanawake wanapaswa kuwa wenye kuchukua mambo kwa uzito, si wenye uchongezi,+ wawe wenye kiasi+ katika mazoea, waaminifu katika mambo yote.+
12 Watumishi wa huduma na wawe waume wa mke mmoja,+ wakisimamia kwa njia nzuri watoto na nyumba zao wenyewe.+ 13 Kwa maana wanaume wanaohudumu kwa njia nzuri wanajipatia wenyewe msimamo mzuri+ na uhuru mwingi wa kusema+ katika imani kuhusiana na Kristo Yesu.
14 Ninakuandikia mambo haya, ingawa ninatumaini kuja kwako upesi,+ 15 lakini nikichelewa, ili ujue jinsi unavyopaswa kujiendesha katika nyumba ya Mungu,+ ambayo ni kutaniko la Mungu aliye hai, nguzo na tegemezo+ la ile kweli. 16 Kwa kweli, ni jambo lenye kukubalika kwamba siri takatifu+ ya huu ujitoaji-kimungu ni kubwa: ‘Yeye alifunuliwa katika mwili,+ alitangazwa kuwa mwadilifu katika roho,+ alionekana kwa malaika,+ alihubiriwa kati ya mataifa,+ aliaminiwa katika ulimwengu,+ alipokewa juu katika utukufu.’+
4 Hata hivyo, neno lililoongozwa na roho linasema kwa hakika kwamba katika vipindi vya nyakati+ za mwisho wengine wataanguka+ kutoka kwenye imani, wakisikiliza maneno yaliyoongozwa kwa roho yenye kupotosha+ na mafundisho ya roho waovu,+ 2 kwa unafiki wa watu wanaosema uwongo,+ waliotiwa alama katika dhamiri+ zao kama kwa chuma cha kutilia alama; 3 wakikataza kufunga ndoa,+ wakiamuru kujiepusha na vyakula+ ambavyo Mungu aliumba+ viliwe kwa kutoa shukrani na wale walio na imani+ na wanaoijua kweli kwa usahihi. 4 Sababu ya hili ni kwamba kila kiumbe cha Mungu ni kizuri,+ na hakuna kitu kinachopaswa kukataliwa+ kama kinapokewa kwa kutoa shukrani,+ 5 kwa maana kinatakaswa kupitia neno la Mungu na sala juu yake.
6 Kwa kuwapa akina ndugu mashauri haya utakuwa mhudumu mzuri wa Kristo Yesu, mwenye kulishwa maneno ya imani na ya fundisho zuri+ ambalo umefuata kwa ukaribu.+ 7 Lakini kataa hadithi za uwongo+ ambazo huchafua mambo matakatifu na ambazo wanawake wazee husimulia. Kwa upande mwingine, uwe ukijizoeza ujitoaji-kimungu ukiwa ni shabaha yako.+ 8 Kwa maana mazoezi ya kimwili ni yenye faida kidogo; lakini ujitoaji-kimungu+ ni wenye faida kwa mambo yote,+ kwa kuwa una ahadi ya uzima wa sasa na ule utakaokuja.+ 9 Neno hilo ni la uaminifu nalo linastahili kukubaliwa kikamilifu.+ 10 Kwa maana kwa kusudi hili tunafanya kazi kwa bidii na kujikaza wenyewe,+ kwa sababu tumeweka tumaini+ letu juu ya Mungu aliye hai, ambaye ni Mwokozi+ wa watu wa namna zote,+ hasa wa watu waaminifu.+
11 Endelea kutoa amri+ hizi na kuzifundisha.+ 12 Usiache mtu yeyote audharau kamwe ujana wako.+ Badala yake, uwe kielelezo+ kwa waaminifu+ katika kusema, katika mwenendo, katika upendo, katika imani, katika usafi wa kiadili.+ 13 Ninapokuwa nikija, endelea kufanya bidii katika kusoma+ mbele ya watu wote,+ katika kuhimiza, katika kufundisha. 14 Usiwe ukiipuuza zawadi+ iliyo ndani yako uliyopewa kupitia utabiri+ na wakati baraza la wanaume wazee walipoweka mikono+ yao juu yako. 15 Tafakari mambo haya;+ zama katika hayo, ili maendeleo+ yako yawe wazi kwa watu wote. 16 Jiangalie daima wewe mwenyewe+ na kufundisha+ kwako. Kaa katika mambo haya, kwa maana kwa kufanya hivyo utajiokoa wewe mwenyewe na wale wanaokusikiliza pia.+
5 Usimkemee kwa ukali mwanamume mzee.+ Badala yake, msihi kama baba, wanaume vijana kama ndugu, 2 wanawake wazee+ kama mama, wanawake vijana kama dada+ kwa usafi wote wa kiadili.
3 Waheshimu wajane ambao ni wajane kwelikweli.+ 4 Lakini ikiwa mjane yeyote ana watoto au wajukuu, acha hao wajifunze kwanza kuzoea ujitoaji-kimungu nyumbani+ kwao wenyewe na kuendelea kuwalipa wazazi+ na wazazi wa wazazi wao malipo yanayowastahili, kwa maana hilo linakubalika machoni pa Mungu.+ 5 Basi mwanamke ambaye kwa kweli ni mjane na aliyeachwa maskini+ sana ameweka tumaini lake kwa Mungu+ naye anadumu katika dua na sala usiku na mchana.+ 6 Lakini mwanamke anayejiingiza katika tamaa za mwili+ amekufa+ ingawa yuko hai. 7 Kwa hiyo endelea kutoa amri hizi,+ ili wasiwe wenye kulaumika.+ 8 Hakika ikiwa yeyote hawaandalii mahitaji wale walio wake mwenyewe,+ na hasa wale walio washiriki wa nyumba yake,+ ameikana+ imani+ naye ni mbaya kuliko mtu asiye na imani.
9 Na mjane ambaye amekuwa mwenye umri usiopungua miaka 60, mke wa mume mmoja, awekwe katika orodha,+ 10 mwenye kutolewa ushahidi juu ya matendo yaliyo mazuri,+ ikiwa alilea watoto,+ ikiwa alipokea wageni,+ ikiwa aliosha miguu ya watakatifu,+ ikiwa aliwasaidia wale walio katika dhiki,+ ikiwa alifuata kwa bidii kila tendo jema.+
11 Kwa upande mwingine, wakatae wanawake wajane ambao ni vijana, kwa maana tamaa zao za ngono zinapokuja kati yao na Kristo,+ wao hutaka kuolewa, 12 wakiwa na hukumu kwa sababu wamepuuza wonyesho wao wa kwanza wa imani.+ 13 Wakati huohuo wao hujifunza pia kutokuwa na kazi, wakizunguka-zunguka nyumba kwa nyumba; ndiyo, si kwamba hawana kazi tu, bali pia ni wenye kupiga porojo na wenye kujiingiza katika mambo ya watu wengine,+ wakiongea juu ya mambo ambayo hawapaswi. 14 Kwa hiyo natamani wanawake wajane ambao ni vijana waolewe,+ wazae watoto,+ wasimamie nyumba, wasimpe yule mpinzani sababu yoyote ya kutukana.+ 15 Kwa kweli, tayari wengine wamegeuzwa kando kumfuata Shetani. 16 Ikiwa mwanamke yeyote mwamini ana wajane, acha yeye awasaidie wao,+ na acha kutaniko lisiwe chini ya mzigo huo. Ndipo liweze kuwasaidia wale ambao ni wajane kwelikweli.+
17 Wanaume wazee wanaosimamia+ kwa njia nzuri wahesabiwe kustahili heshima+ mara mbili, hasa wale wanaofanya kazi kwa bidii katika kusema na kufundisha.+ 18 Kwa maana andiko linasema: “Hupaswi kumfunga kinywa ng’ombe-dume anapopura nafaka”;+ pia: “Mfanyakazi anastahili mshahara wake.”+ 19 Usikubali shtaka juu ya mwanamume mzee, isipokuwa tu kwa ushuhuda wa mashahidi wawili au watatu.+ 20 Watu walio na mazoea ya kutenda dhambi+ uwakaripie+ mbele ya watazamaji, ili wengine pia waogope.+ 21 Nakuagiza kwa uzito mbele za Mungu na Kristo Yesu+ na malaika waliochaguliwa kwamba uyashike mambo haya bila kuhukumu mapema, bila kufanya jambo lolote kwa mwelekeo wenye ubaguzi.+
22 Usiweke kamwe mikono+ yako juu ya mtu yeyote haraka-haraka; wala usiwe mshiriki katika dhambi za wengine;+ jihifadhi ukiwa safi kiadili.+
23 Usiendelee kunywa maji, bali utumie divai+ kidogo kwa ajili ya tumbo lako na ugonjwa wako wa mara kwa mara.
24 Dhambi za watu wengine huwa wazi+ mbele ya watu wote, zikiongoza moja kwa moja kwenye hukumu, lakini kwa habari ya watu wengine pia dhambi zao huwa wazi baadaye.+ 25 Vivyo hivyo pia matendo mazuri huwa wazi+ mbele ya watu wote na yale ambayo ni kinyume hayawezi kuendelea kufichwa.+
6 Wale wote walio watumwa chini ya nira na waendelee kuwaona mabwana wao kuwa wenye kustahili heshima kamili,+ ili jina la Mungu na fundisho lisisemwe vibaya kamwe.+ 2 Zaidi ya hayo, wale walio na mabwana+ wenye kuamini wasiwadharau,+ kwa sababu wao ni ndugu.+ Kinyume chake, na wawe watumwa kwa utayari zaidi, kwa sababu wale wanaopokea faida ya utumishi wao mwema ni waamini na wapendwa.
Endelea kufundisha mambo haya+ na kutoa mahimizo haya. 3 Kama mtu yeyote akifundisha fundisho lingine+ na hakubaliani na maneno yenye afya,+ yale ya Bwana wetu Yesu Kristo, wala na fundisho ambalo linapatana na ujitoaji-kimungu,+ 4 yeye anajivuna kwa kiburi,+ haelewi jambo lolote,+ bali ni mgonjwa kiakili+ juu ya maswali na mabishano juu ya maneno.+ Mambo hayo hutokeza wivu,+ mizozo, matukano,+ shuku zenye uovu, 5 mabishano makali juu ya mambo madogo-madogo kwa upande wa watu walioharibika katika akili+ na kuporwa ile kweli,+ wakifikiri kwamba ujitoaji-kimungu ni njia ya kupata faida.+ 6 Kwa hakika, huo ni njia ya kupata faida kubwa,+ huu ujitoaji-kimungu+ pamoja na ujitoshelevu.+ 7 Kwa maana hatukuleta chochote katika ulimwengu, wala hatuwezi kuchukua chochote nje.+ 8 Kwa hiyo, tukiwa na chakula na kitu cha kujifunika, tutaridhika na vitu hivyo.+
9 Hata hivyo, wale ambao wameazimia kuwa matajiri huanguka katika jaribu+ na mtego na tamaa nyingi za kijinga na zenye kudhuru,+ ambazo hutumbukiza watu katika maangamizi na uharibifu.+ 10 Kwa maana kupenda+ pesa ni chanzo+ cha mambo mabaya ya namna zote,+ na kwa kujitahidi kufikia upendo huo wengine wamepotoshwa kutoka kwenye imani nao wamejichoma wenyewe kila mahali kwa maumivu mengi.+
11 Hata hivyo, wewe, Ee mtu wa Mungu, yakimbie mambo hayo.+ Lakini fuatilia uadilifu, ujitoaji-kimungu, imani, upendo, uvumilivu, tabia-pole.+ 12 Pigana pigano zuri la imani,+ ushike imara ule uzima wa milele ambao uliitiwa nawe ukatoa tangazo zuri la hadharani+ mbele ya mashahidi wengi.
13 Machoni pa Mungu, ambaye huvihifadhi vitu vyote hai, na machoni pa Kristo Yesu, ambaye akiwa shahidi+ alifanya tangazo zuri la hadharani+ mbele ya Pontio Pilato,+ mimi nakupa wewe maagizo+ 14 kwamba uishike amri katika njia isiyo na doa na isiyolaumika mpaka wakati wa ufunuo+ wa Bwana wetu Yesu Kristo. 15 Ufunuo huo yule Mwenye Uwezo Mkubwa+ aliye wa pekee na mwenye furaha atauonyesha katika nyakati zake wenyewe zilizowekwa,+ yeye Mfalme+ wa wale wanaotawala wakiwa wafalme na Bwana+ wa wale wanaotawala wakiwa mabwana, 16 yeye peke yake asiyeweza kufa,+ anayekaa katika nuru isiyoweza kufikiwa,+ ambaye hakuna hata mmoja kati ya wanadamu amemwona au anaweza kumwona.+ Kwake yeye na kuwe heshima+ na nguvu milele. Amina.
17 Uwape maagizo wale walio matajiri+ katika mfumo wa mambo wa sasa wasitake makuu,+ na waweke tumaini lao, si katika utajiri usio hakika,+ bali katika Mungu, ambaye hutupa sisi vitu vyote kwa wingi ili tuvifurahie;+ 18 wafanye mema,+ wawe matajiri katika matendo mazuri,+ wawe wakarimu, tayari kushiriki,+ 19 wakijiwekea wenyewe kwa usalama hazina+ ya msingi mzuri+ kwa ajili ya wakati ujao, ili waushike imara uzima ulio wa kweli.+
20 Ee Timotheo, linda lililowekwa amana kwako,+ ukigeuka mbali kutoka kwenye maneno matupu ambayo huchafua mambo matakatifu na kutoka kwenye maneno yanayopingana ya ule unaoitwa kwa uwongo “ujuzi.”+ 21 Kwa maana kwa kujisifia ujuzi wa namna hiyo wengine wamegeuka kutoka kwenye imani.+
Fadhili zisizostahiliwa na ziwe pamoja nanyi.