Barua ya Pili ya Petro
1 Simoni Petro, mtumwa+ na mtume+ wa Yesu Kristo, kwa wale ambao wamepata imani, yenye pendeleo lililo sawa na letu,+ kupitia uadilifu+ wa Mungu wetu na Mwokozi Yesu Kristo:+
2 Na mwongezewe fadhili zisizostahiliwa na amani+ kwa ujuzi sahihi+ juu ya Mungu na juu ya Yesu Bwana wetu, 3 kwa maana nguvu zake za kimungu zimetupa sisi bila malipo mambo yote yanayohusu uzima+ na ujitoaji-kimungu,+ kupitia ujuzi sahihi juu ya yeye ambaye alituita+ kupitia utukufu+ na wema wa adili. 4 Kupitia mambo haya ametupa sisi bila malipo ahadi zenye thamani na zilizo bora sana,+ ili kupitia hizi ninyi muwe washiriki katika asili+ ya kimungu,+ mkiwa mmeponyoka kutoka katika uharibifu ulio katika ulimwengu+ kutokana na uchu.
5 Ndiyo, kwa sababu hii, mkiitikia kwa kuchanga kwenu jitihada yote yenye bidii,+ ongezeni kwenye imani yenu wema wa adili,+ kwenye wema wenu wa adili ujuzi,+ 6 kwenye ujuzi wenu kujizuia, kwenye kujizuia+ kwenu uvumilivu, kwenye uvumilivu wenu ujitoaji-kimungu,+ 7 kwenye ujitoaji-kimungu wenu upendo wa kindugu, kwenye upendo wenu wa kindugu upendo.+ 8 Kwa maana mambo hayo yakikaa ndani yenu na kufurika, yatawazuia kuwa ama wasiotenda au wasiozaa matunda+ kuhusiana na ujuzi sahihi juu ya Bwana wetu Yesu Kristo.
9 Kwa maana ikiwa mambo hayo hayapo ndani ya yeyote, yeye ni kipofu, akifunga macho yake yasione nuru,+ naye amesahau+ kutakaswa+ kwake kutoka katika dhambi zake za zamani za kale. 10 Kwa sababu hiyo, akina ndugu, fanyeni hata zaidi yote mnayoweza ili kufanya mwito+ na kuchaguliwa+ kwenu kuwe hakika kwa ajili yenu wenyewe; kwa maana mkiendelea kufanya mambo hayo hamtashindwa hata kidogo.+ 11 Kwa kweli, hivyo ndivyo mtakavyowezeshwa kwa wingi kuingia+ katika ufalme wa milele+ wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo.+
12 Kwa sababu hiyo sikuzote nitakuwa na mwelekeo wa kuwakumbusha+ ninyi kuhusu mambo haya, ijapokuwa mnayajua hayo na mmewekwa imara katika kweli+ iliyo ndani yenu.+ 13 Lakini ninaona hili kuwa sawa, maadamu ningali katika maskani hii,+ kuwaamsha ninyi kwa kuwakumbusha,+ 14 nikijua ninavyojua kwamba kuondolewa kwa maskani yangu kutakuwa hivi karibuni,+ kama vile pia Bwana wetu Yesu Kristo alivyonionyesha.+ 15 Kwa hiyo nitafanya yote ninayoweza pia kila wakati ili, baada ya kuondoka kwangu,+ ninyi mweze kuyataja mambo haya kwa ajili yenu wenyewe.
16 Sivyo, haikuwa kwa kufuata hadithi za uwongo zilizotungwa+ kwa ufundi kwamba tuliwafahamisha ninyi juu ya nguvu na kuwapo kwa Bwana wetu Yesu Kristo,+ lakini ilikuwa kwa sisi kuwa mashahidi wa kujionea fahari yake.+ 17 Kwa maana alipokea kutoka kwa Mungu Baba heshima na utukufu,+ wakati maneno ya namna hii yalipotolewa kwake kwa utukufu wenye fahari: “Huyu ni mwanangu, mpendwa wangu, ambaye mimi mwenyewe nimemkubali.”+ 18 Ndiyo, maneno hayo tuliyasikia+ yakitoka mbinguni tulipokuwa tungali pamoja naye katika ule mlima mtakatifu.+
19 Kwa hiyo tuna neno la kinabii+ likiwa limefanywa hakika zaidi;+ nanyi mnafanya vema kulikazia uangalifu kama vile taa+ inayoangaza mahali penye giza, mpaka siku ipambazuke na nyota ya mchana+ ichomoze, katika mioyo yenu. 20 Kwa maana mnajua hili kwanza, kwamba hakuna unabii wa Andiko unaotokana na fasiri yoyote ya kibinafsi.+ 21 Kwa maana unabii haukuletwa wakati wowote kwa mapenzi ya mwanadamu,+ bali wanadamu walisema yaliyotoka kwa Mungu+ kama walivyoongozwa na roho takatifu.+
2 Hata hivyo, kulikuwa pia na manabii wa uwongo katikati ya wale watu, kama vile pia kutakavyokuwa na walimu wa uwongo katikati yenu.+ Hawa wataingiza ndani kimya-kimya madhehebu yenye kuharibu nao watamkana hata yule bwana aliyewanunua,+ wakijiletea wenyewe maangamizi ya haraka. 2 Zaidi ya hayo, wengi watafuata+ matendo yao ya mwenendo mpotovu,+ na kwa sababu ya hao ile njia ya kweli itatukanwa.+ 3 Pia, kwa tamaa watawatumia ninyi vibaya kwa maneno yasiyo ya kweli.+ Lakini kuwahusu wao, hukumu ya tangu zamani za kale+ haisongi polepole, na maangamizi yao hayalali.+
4 Hakika ikiwa Mungu hakujizuia kuwaadhibu wale malaika+ waliofanya dhambi, bali, kwa kuwatupa ndani ya Tartaro,+ aliwatia ndani ya mashimo yenye giza zito ili wawekwe akiba kwa ajili ya hukumu;+ 5 naye hakujizuia kuuadhibu ulimwengu wa kale,+ bali alimlinda Noa, mhubiri wa uadilifu,+ akiwa salama pamoja na wengine saba+ alipoleta gharika+ juu ya ulimwengu wa watu wasiomwogopa Mungu; 6 na kwa kuyageuza majiji ya Sodoma na Gomora kuwa majivu aliyahukumia adhabu,+ akiweka kielelezo kwa watu wasiomwogopa Mungu juu ya mambo yatakayokuja;+ 7 naye alimkomboa Loti mwadilifu,+ aliyetaabishwa sana na kule kujitia mno katika mwenendo mpotovu kwa watu wanaokaidi sheria+— 8 kwa maana mtu huyo mwadilifu kwa yale ambayo aliona na kusikia alipokuwa akikaa katikati yao siku baada ya siku alikuwa akiitesa nafsi yake yenye uadilifu kwa sababu ya vitendo vyao vya kuasi sheria— 9 Yehova anajua jinsi ya kuwakomboa watu wenye ujitoaji-kimungu kutoka katika jaribu,+ lakini kuwaweka akiba watu wasio waadilifu kwa ajili ya ile siku ya hukumu ili wakatiliwe mbali,+ 10 hasa wale ambao huufuata mwili wakiwa na tamaa ya kuutia unajisi+ na ambao hudharau mamlaka.+
Ni wajasiri, washupavu, hawatetemeki mbele ya watukufu bali hutukana,+ 11 lakini malaika, ijapokuwa wao ni wakuu zaidi katika nguvu na uwezo, hawaleti juu yao shtaka kwa matukano,+ wakiepuka kufanya hivyo kwa sababu ya kumheshimu Yehova.+ 12 Lakini watu hawa, kama wanyama wasiofikiri waliozaliwa kiasili ili kukamatwa na kuangamizwa, katika mambo ambayo wao hawayajui na kuyatukana,+ watapatwa na maangamizi katika mwendo wao wenyewe wa maangamizi, 13 wakijitendea makosa wenyewe+ ikiwa ni thawabu ya kutenda makosa.+
Wao huyaona maisha ya anasa wakati wa mchana kuwa raha.+ Wao ni madoa na dosari, wakijitia mno katika kupendezwa kusikozuiwa katika mafundisho yao ya udanganyifu huku wakila karamu pamoja nanyi.+ 14 Wana macho yenye kujaa uzinzi+ na yasiyoweza kuachana na dhambi,+ nao huzishawishi nafsi zisizo imara. Wana moyo uliozoezwa kutamani.+ Wao ni watoto waliolaaniwa.+ 15 Wameiacha njia iliyo nyoofu, wamepotoshwa. Wameifuata njia ya Balaamu,+ mwana wa Beori, aliyependa thawabu ya kutenda makosa,+ 16 lakini akapata karipio kwa ajili ya yeye mwenyewe kuharibu jambo lililokuwa sawa.+ Mnyama wa kubeba mizigo asiye na sauti, akisema kwa sauti ya mtu,+ aliuzuia mwendo wa wazimu wa nabii huyo.+
17 Hawa ni chemchemi zisizo na maji,+ na ukungu unaoendeshwa na dhoruba kali, nao wamewekewa akiba weusi wa giza.+ 18 Kwa maana wao husema maneno ya kujigamba yasiyo na faida, na kwa tamaa za mwili+ na tabia zenye upotovu wao hushawishi+ wale wanaotoka tu kuponyoka+ kutoka kwa watu ambao hujiendesha kwa njia ya makosa. 19 Huku wakiwaahidia uhuru,+ wao wenyewe ni watumwa wa uharibifu.+ Kwa maana yeyote anayeshindwa na mwingine hufanywa mtumwa na huyu.+ 20 Hakika ikiwa, baada ya kuponyoka kutoka katika mambo ya unajisi ya ulimwengu+ kwa ujuzi sahihi juu ya Bwana na Mwokozi Yesu Kristo, wanajiingiza tena katika mambo haya na kushindwa,+ hali ya mwisho imekuwa mbaya zaidi kwao kuliko ile ya kwanza.+ 21 Kwa maana ingalikuwa afadhali kwao kama hawangalijua kwa usahihi njia ya uadilifu+ kuliko baada ya kuijua kwa usahihi kugeuka kutoka katika amri takatifu waliyopewa.+ 22 Neno la methali ya kweli limewapata: “Mbwa+ ameyarudia matapiko yake mwenyewe, na nguruwe aliyeoshwa amerudi kugaagaa katika matope.”+
3 Wapendwa, hii sasa ndiyo barua ya pili ninayowaandikia ninyi, ambayo katika hiyo, kama katika ile yangu ya kwanza,+ ninaamsha uwezo wenu mzuri wa kufikiri kwa njia ya kikumbusho,+ 2 ili mkumbuke maneno yaliyosemwa hapo zamani na manabii watakatifu+ na amri ya Bwana na Mwokozi kupitia mitume wenu.+ 3 Kwa maana mnajua hili kwanza, kwamba katika siku za mwisho+ watakuja wadhihaki+ na dhihaka zao, wakiendelea kulingana na tamaa zao wenyewe+ 4 na kusema:+ “Huku kuwapo kwake kulikoahidiwa kuko wapi?+ Kwani, tangu siku mababu zetu walipolala katika kifo, mambo yote yanaendelea sawasawa kama tangu mwanzo wa uumbaji.”+
5 Kwa maana, kulingana na kupenda kwao, wao hawalioni jambo hili, kwamba mbingu+ zilikuwapo tangu zamani za kale na dunia ikisimama imara kutoka katika maji+ na katikati ya maji+ kwa neno la Mungu; 6 na kwa njia hizo ulimwengu wa wakati huo uliangamia kwa gharika ya maji.+ 7 Lakini kwa neno hilohilo mbingu+ na dunia+ za sasa zimewekwa akiba kwa ajili ya moto+ nazo zinahifadhiwa mpaka ile siku ya hukumu+ na ya kuangamizwa kwa watu wasiomwogopa Mungu.+
8 Hata hivyo, wapendwa, msikose kujua jambo hili moja, kwamba siku moja kwa Yehova ni kama miaka elfu na miaka elfu ni kama siku moja.+ 9 Yehova hakawii kuhusiana na ahadi yake,+ kama watu fulani wanavyoona kukawia, bali yeye ni mwenye subira kwenu kwa sababu hataki yeyote aangamizwe bali hutaka wote wafikie toba.+ 10 Lakini siku ya Yehova+ itakuja kama mwizi,+ ambayo katika hiyo mbingu zitapitilia mbali+ kwa kelele ya kuvuma,+ lakini vitu vyake vya msingi vikiwa moto sana vitayeyushwa,+ na dunia+ na kazi zilizo ndani yake zitafunuliwa.+
11 Kwa kuwa hivyo vitu vyote vitayeyushwa jinsi hiyo, ninyi mnapaswa kuwa watu wa namna gani katika matendo matakatifu ya mwenendo na vitendo vya ujitoaji-kimungu, 12 mkingojea+ na kuweka karibu akilini kuwapo kwa siku ya Yehova,+ ambayo kupitia hiyo mbingu zikiwa zimewaka moto zitayeyushwa+ na vitu vya msingi vikiwa moto sana vitayeyuka! 13 Lakini kulingana na ahadi yake tunangojea mbingu mpya+ na dunia mpya,+ na humo uadilifu utakaa.+
14 Kwa hiyo, wapendwa, kwa kuwa mnangojea mambo hayo, fanyeni yote mnayoweza ili mwishowe yeye awapate ninyi mkiwa bila doa+ na bila dosari na mkiwa katika amani.+ 15 Zaidi ya hayo, ioneni subira ya Bwana wetu kuwa wokovu, kama ndugu yetu mpendwa Paulo alivyowaandikia+ ninyi kulingana na hekima+ aliyopewa, 16 akisema juu ya mambo hayo kama anavyosema pia katika barua zake zote. Hata hivyo, ndani ya hizo mna mambo fulani yaliyo magumu kuelewa, ambayo wale wasiofundishwa na wasio imara wanayapotosha, kama wanavyofanya na Maandiko+ mengine pia, kwa maangamizi yao wenyewe.
17 Kwa hiyo, ninyi, wapendwa, mkiwa na ujuzi huu wa kimbele,+ jilindeni ili msichukuliwe mbali pamoja nao kwa kosa la watu wanaokaidi sheria, mwanguke kutoka kwenye uimara wenu wenyewe.+ 18 Hapana, bali endeleeni kukua katika fadhili zisizostahiliwa na ujuzi juu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo.+ Kwake yeye na kuwe utukufu sasa na pia mpaka siku ya umilele.+