Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bi12 1 Petro 1:1-5:14
  • Barua ya Kwanza ya Petro

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Barua ya Kwanza ya Petro
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Barua ya Kwanza ya Petro

Barua ya Kwanza ya Petro

1 Petro, mtume+ wa Yesu Kristo, kwa wakaaji wa muda+ waliotawanyika huku na huku+ katika Ponto, Galatia, Kapadokia,+ Asia, na Bithinia, kwa wale waliochaguliwa+ 2 kulingana na ujuzi wa kimbele wa Mungu Baba,+ kwa kutakaswa kwa roho,+ kusudi wawe watiifu na kunyunyiziwa+ damu ya Yesu Kristo:+

Na mwongezwe fadhili zisizostahiliwa na amani.+

3 Abarikiwe Mungu na Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo,+ kwa maana kulingana na rehema yake kubwa alituzaa+ sisi upya kwenye tumaini lililo hai+ kupitia ufufuo+ wa Yesu Kristo kutoka kwa wafu, 4 kwenye urithi usioharibika na usiotiwa unajisi na usiofifia.+ Huo umewekwa akiba mbinguni kwa ajili yenu,+ 5 mnaolindwa kwa nguvu za Mungu kupitia imani+ kwa ajili ya wokovu+ ulio tayari kufunuliwa+ katika kipindi cha mwisho cha wakati.+ 6 Nanyi mnashangilia sana katika jambo hilo, ingawa kwa muda kidogo sasa, ikiwa ni lazima, mmehuzunishwa na majaribu ya namna mbalimbali,+ 7 ili sifa iliyojaribiwa ya imani+ yenu, iliyo na thamani kubwa zaidi kuliko dhahabu ambayo huharibika ijapokuwa hiyo hujaribiwa kwa moto,+ ipatikane kuwa sababu ya sifa na utukufu na heshima wakati wa ufunuo+ wa Yesu Kristo. 8 Ninyi mnampenda,+ ingawa hamkumwona yeye kamwe. Ingawa hammwoni wakati wa sasa, bado mnaonyesha imani katika yeye na mnashangilia sana kwa shangwe isiyosemeka na iliyotukuzwa, 9 huku mkipokea tokeo la mwisho la imani yenu, ule wokovu wa nafsi zenu.+

10 Manabii, waliotoa unabii+ juu ya fadhili zisizostahiliwa zilizokusudiwa ninyi,+ walifanya uchunguzi kwa bidii na kutafuta kwa uangalifu habari kuhusu wokovu huu.+ 11 Waliendelea kuchunguza ni majira gani hasa+ au ni majira ya namna gani ambayo roho+ iliyokuwa ndani yao ilikuwa ikionyesha kumhusu Kristo+ ilipokuwa ikitoa ushahidi kimbele juu ya mateso ya Kristo+ na juu ya utukufu+ ambao ungefuata hayo. 12 Ilifunuliwa kwao kwamba hawakuwa wakijihudumia wenyewe,+ bali walikuwa wakiwahudumia ninyi mambo ambayo sasa mmetangaziwa+ kupitia wale ambao wamewatangazia ninyi habari njema kwa roho takatifu+ iliyotumwa kutoka mbinguni. Malaika wanatamani kuchungulia ndani ya mambo hayo.+

13 Kwa hiyo kazeni akili zenu kwa ajili ya utendaji,+ tunzeni akili zenu kwa ukamili;+ kazeni tumaini lenu juu ya fadhili zisizostahiliwa+ zitakazoletwa kwenu wakati wa ufunuo+ wa Yesu Kristo. 14 Kama watoto watiifu, acheni kufanyizwa+ kulingana na tamaa mlizokuwa nazo hapo zamani katika hali yenu ya kutojua, 15 bali, kwa kupatana na Mtakatifu aliyewaita, ninyi wenyewe pia iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote,+ 16 kwa sababu imeandikwa: “Muwe watakatifu, kwa sababu mimi ni mtakatifu.”+

17 Zaidi ya hayo, ikiwa mnamwitia Baba ambaye huhukumu bila ubaguzi+ kulingana na matendo ya kila mmoja, jiendesheni kwa kuogopa+ katika wakati wa kukaa kwenu ugenini.+ 18 Kwa maana mnajua kuwa si kwa vitu vyenye kuharibika,+ kwa fedha au dhahabu, kwamba mlikombolewa+ kutoka kwenye namna ya mwenendo wenu usiozaa matunda ambao ulipokewa kwa njia ya mapokeo kutoka kwa mababu zenu. 19 Bali ilikuwa kwa damu yenye thamani,+ kama ile ya mwana-kondoo asiye na dosari na asiye na doa,+ ile ya Kristo.+ 20 Ni kweli, yeye alijulikana kimbele kabla ya kuwekwa msingi+ wa ulimwengu, lakini alifunuliwa mwishoni mwa nyakati kwa ajili yenu+ 21 ninyi ambao kupitia yeye ni wenye kumwamini Mungu,+ yeye aliyemfufua kutoka kwa wafu+ na kumpa utukufu;+ ili imani na tumaini lenu viwe katika Mungu.+

22 Sasa kwa kuwa mmezitakasa+ nafsi zenu kwa kuwa watiifu kwa ile kweli tokeo likiwa ni upendo wa kindugu usio na unafiki,+ pendaneni sana kutoka moyoni.+ 23 Kwa maana mmezaliwa upya,+ si kupitia mbegu yenye kuharibika,+ bali kupitia ile isiyoharibika+ yenye kuzaa,+ kupitia neno la Mungu+ aliye hai na anayedumu.+ 24 Kwa maana “wanadamu wote ni kama majani,+ na utukufu wao wote ni kama ua la majani; majani hukauka, na ua huanguka,+ 25 bali neno la Yehova linadumu milele.”+ Basi, hili ndilo “neno,”+ hili ambalo ninyi mmetangaziwa+ kuwa habari njema.

2 Basi, ondoeni ubaya+ wote na udanganyifu wote na unafiki na wivu na namna zote za masengenyo,+ 2 na, kama watoto wachanga waliozaliwa hivi karibuni,+ kuzeni tamaa kwa ajili ya maziwa yasiyochanganywa kitu+ ambayo ni ya lile neno, ili kupitia hayo mkue kufikia wokovu,+ 3 mradi tu mmeonja na kuona kwamba Bwana ni mwenye fadhili.+

4 Mkimjia yeye kama kulijia jiwe lililo hai,+ lililokataliwa,+ ni kweli, na wanadamu,+ bali lililochaguliwa, lenye thamani, kwa Mungu,+ 5 ninyi wenyewe pia kama mawe yaliyo hai mnajengwa kuwa nyumba ya kiroho+ kwa kusudi la ukuhani mtakatifu, ili kutoa dhabihu za kiroho+ zenye kukubalika kwa Mungu kupitia Yesu Kristo.+ 6 Kwa maana imeandikwa katika Andiko: “Tazama! Ninaweka katika Sayuni jiwe, lililochaguliwa, jiwe la pembeni la msingi, lenye thamani; na mtu yeyote anayeonyesha imani katika hilo hatakata tamaa hata kidogo.”+

7 Kwa hiyo, yeye ni mwenye thamani kwenu ninyi, kwa kuwa ninyi ni waamini; lakini kwa wale wasioamini, “jiwe lilelile ambalo wajenzi walilikataa+ limekuwa jiwe kuu la pembeni,”+ 8 na “jiwe la kukwaza na mwamba wa kuangusha.”+ Hawa wanajikwaa kwa sababu si watiifu kwa lile neno. Kwa sababu hiyo pia waliwekwa rasmi.+ 9 Lakini ninyi ni “jamii iliyochaguliwa, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu,+ watu wa kuwa mali ya pekee,+ ili mtangaze kotekote sifa bora”+ zake yeye aliyewaita ninyi kutoka katika giza kuingia katika nuru yake ya ajabu.+ 10 Kwa kuwa wakati mmoja ninyi mlikuwa si watu, lakini sasa ninyi ni watu wa Mungu;+ mlikuwa wale ambao hawakuwa wameonyeshwa rehema, lakini sasa ninyi ni wale ambao wameonyeshwa rehema.+

11 Wapendwa, nawahimiza ninyi kama wageni na wakaaji wa muda+ kwamba mwendelee kujiepusha na tamaa za kimwili,+ ambazo ndizo huendelea kupambana na nafsi.+ 12 Dumisheni mwenendo wenu ukiwa mzuri katikati ya mataifa,+ ili, katika jambo ambalo wanasema juu yenu ya kuwa ninyi ni watenda-maovu, waweze, likiwa tokeo la matendo yenu mazuri+ ambayo wameshuhudia kwa macho, kumtukuza Mungu katika siku ya ukaguzi wake.+

13 Kwa ajili ya Bwana jitiisheni+ wenyewe kwa kila kitu kilichofanywa na binadamu:+ iwe ni kwa mfalme+ akiwa mkubwa 14 au ni kwa magavana wakiwa wametumwa naye kuwapa adhabu watenda-maovu bali kuwasifu watenda-mema.+ 15 Kwa maana ndivyo mapenzi ya Mungu yalivyo, kwamba kwa kutenda mema mzibe maneno ya ujinga ya watu wasio na akili.+ 16 Iweni kama watu huru,+ lakini muwe na uhuru wenu, si kama kifuniko cha ubaya,+ bali kama watumwa wa Mungu.+ 17 Waheshimuni watu wa namna zote,+ upendeni ushirika mzima wa akina ndugu,+ mwogopeni Mungu,+ mheshimuni mfalme.+

18 Watumishi wa nyumbani na wajitiishe+ kwa mabwana wao kwa woga unaofaa,+ si kwa wale walio wema tu na wapole, bali pia kwa wale ambao ni wagumu kupendeza. 19 Kwa maana ikiwa mtu, kwa sababu ya dhamiri kwa Mungu, anavumilia chini ya mambo yenye kuhuzunisha naye anateseka isivyo haki, jambo hilo ni lenye kukubalika.+ 20 Kwa maana kuna sifa gani katika jambo ikiwa mnapofanya dhambi na kupigwa makofi, mnavumilia?+ Lakini ikiwa, mnapotenda mema na kuteseka,+ mnavumilia, jambo hilo ni lenye kukubalika kwa Mungu.+

21 Kwa kweli, mliitwa kwenye mwendo huu, kwa sababu hata Kristo aliteseka kwa ajili yenu,+ akiwaachia ninyi kielelezo ili mfuate hatua zake kwa ukaribu.+ 22 Yeye hakufanya dhambi,+ wala udanganyifu haukupatikana kinywani mwake.+ 23 Alipokuwa akitukanwa,+ hakujibu kwa matukano.+ Alipokuwa akiteseka,+ hakutoa vitisho, bali aliendelea kujiweka mkononi mwa yule+ ambaye anahukumu kwa uadilifu. 24 Yeye mwenyewe alichukua dhambi+ zetu katika mwili wake mwenyewe juu ya mti,+ ili tuachane kabisa na dhambi+ na kuishi kwa uadilifu. Na “kwa mapigo yake mliponywa.”+ 25 Kwa maana mlikuwa kama kondoo, wanaopotea njia;+ lakini sasa mmerudi kwa mchungaji+ na mwangalizi wa nafsi zenu.

3 Vivyo hivyo,+ ninyi wake, jitiisheni+ kwa waume zenu wenyewe, ili, ikiwa wowote si watiifu+ kwa lile neno, wavutwe+ bila neno kupitia mwenendo wa wake zao,+ 2 kwa sababu wamekwisha kushuhudia kwa macho mwenendo+ wenu ulio safi kiadili pamoja na heshima kubwa. 3 Na kujipamba kwenu kusiwe kule kusuka nywele+ kwa nje na kule kujivika mapambo ya dhahabu+ au kuvaa mavazi ya nje, 4 bali kuwe yule mtu wa siri+ wa moyoni katika vazi lisiloharibika+ la roho ya utulivu na ya upole,+ ambayo ni ya thamani kubwa machoni pa Mungu. 5 Kwa maana, pia, ndivyo walivyokuwa wakijipamba wale wanawake watakatifu hapo zamani, waliokuwa wakimtumaini Mungu, wakijitiisha kwa waume zao wenyewe, 6 kama Sara alivyokuwa akimtii Abrahamu, akimwita “bwana.”+ Nanyi mmekuwa watoto wake, mradi tu mnaendelea kutenda mema na kutokuwa na woga kwa sababu ya kitisho chochote.+

7 Enyi waume, endeleeni kukaa nao vivyo hivyo+ kulingana na ujuzi,+ mkiwapa heshima+ kama chombo dhaifu zaidi, yaani, mwanamke, kwa kuwa ninyi pia ni warithi+ pamoja nao wa pendeleo lisilostahiliwa la uzima, kusudi sala zenu zisizuiwe.+

8 Mwishowe, ninyi nyote iweni na akili zinazopatana,+ mkionyesha hisia-mwenzi, mkiwa na upendo wa kindugu, wenye huruma nyororo,+ wanyenyekevu katika akili,+ 9 msilipe ubaya kwa ubaya+ au matukano kwa matukano,+ bali, kinyume chake, mkitoa baraka,+ kwa sababu mliitwa kwenye mwendo huu, ili mrithi baraka.

10 Kwa maana, “yeye ambaye anapenda uzima na kuona siku zilizo njema,+ na auzuie ulimi+ wake kutokana na yaliyo mabaya na midomo yake isiseme udanganyifu,+ 11 bali na ageuke kutoka katika yaliyo mabaya+ na kufanya yaliyo mema; na atafute amani na kuifuatilia.+ 12 Kwa maana macho+ ya Yehova yako juu ya waadilifu, na masikio yake yanaielekea dua yao;+ bali uso wa Yehova uko dhidi ya wale wanaotenda mambo mabaya.”+

13 Kwa kweli, ni nani atakayewadhuru ninyi mkiwa na bidii kwa ajili ya yaliyo mema?+ 14 Lakini hata mkiteseka kwa ajili ya uadilifu, ninyi ni wenye furaha.+ Hata hivyo, msikiogope kile kitu wanachokiogopa,+ wala msifadhaike.+ 15 Bali mtakaseni Kristo kuwa Bwana katika mioyo yenu,+ sikuzote mkiwa tayari kujitetea+ mbele ya kila mtu ambaye hutaka kutoka kwenu sababu ya tumaini lililo ndani yenu, lakini mkifanya hivyo kwa tabia-pole+ na heshima kubwa.

16 Iweni na dhamiri njema,+ ili katika lile jambo ambalo wanasema vibaya juu yenu waweze kupata aibu+ wale wanaosema kwa kuushushia heshima mwenendo wenu mwema kuhusiana na Kristo.+ 17 Kwa maana ni afadhali kuteseka kwa sababu mnatenda mema,+ ikiwa mapenzi ya Mungu yanataka hivyo, kuliko kuteseka kwa sababu mnatenda maovu.+ 18 Ndiyo, hata Kristo alikufa mara moja kwa wakati wote kuzihusu dhambi,+ mtu mwadilifu kwa ajili ya wasio waadilifu,+ ili awaongoze ninyi kwa Mungu,+ yeye aliuawa katika mwili,+ lakini akafanywa kuwa hai katika roho.+ 19 Katika hali hiyo pia alienda zake na kuwahubiria roho walio gerezani,+ 20 ambao wakati fulani hawakuwa watiifu+ wakati subira ya Mungu+ ilipokuwa ikingoja katika siku za Noa, safina ilipokuwa ikijengwa,+ ambayo ndani yake watu wachache, yaani, nafsi nane, walichukuliwa salama kupitia maji.+

21 Lile ambalo linalingana na hili linawaokoa ninyi sasa pia,+ yaani, ubatizo, (si kuondolea mbali uchafu wa mwili, bali ombi linalotolewa kwa Mungu ili kupata dhamiri njema,)+ kupitia ufufuo wa Yesu Kristo.+ 22 Yeye yuko mkono wa kuume wa Mungu,+ kwa maana alienda zake mbinguni; na malaika+ na mamlaka na nguvu vilitiishwa kwake.+

4 Kwa hiyo kwa kuwa Kristo aliteseka katika mwili,+ ninyi pia jivikeni silaha ya mwelekeo uleule wa akili;+ kwa sababu mtu ambaye ameteseka katika mwili ameachana na dhambi,+ 2 kwa kusudi kwamba aishi wakati wake uliobaki katika mwili,+ si kwa ajili ya tamaa za wanadamu tena, bali kwa ajili ya mapenzi ya Mungu.+ 3 Kwa maana wakati+ uliopita uliwatosha kufanya mapenzi ya mataifa+ wakati mlipotembea katika vitendo vya mwenendo mpotovu,+ uchu, divai kupita kiasi,+ karamu za kupindukia, mashindano ya kunywa, na ibada haramu za sanamu.+ 4 Kwa sababu ninyi hamwendelei kukimbia pamoja nao katika mwendo huo kwenda kwenye dimbwi lilelile la chini la upotovu,+ wao wanashangaa na kuendelea kuwatukana ninyi.+ 5 Lakini watu hao watatoa hesabu kwake yeye+ aliye tayari kuhukumu wale walio hai na wale walio wafu.+ 6 Kwa kweli, kwa kusudi hili habari njema ilitangazwa kwa wafu+ pia, ili wahukumiwe kuhusiana na mwili kwa maoni ya wanadamu+ lakini waishi kuhusiana na roho+ kwa maoni ya Mungu.

7 Lakini mwisho wa mambo yote umekaribia.+ Kwa hiyo, iweni na utimamu wa akili,+ na kukesha kuhusiana na sala.+ 8 Zaidi ya mambo yote, iweni na upendo mkubwa ninyi kwa ninyi,+ kwa sababu upendo hufunika dhambi nyingi.+ 9 Mkaribishane bila kunung’unika.+ 10 Kwa kadiri ambayo kila mmoja amepokea zawadi, itumieni katika kuhudumiana kama wasimamizi-nyumba wazuri wa fadhili zisizostahiliwa za Mungu zinazoonyeshwa kwa njia mbalimbali.+ 11 Kama yeyote akisema, na aseme kana kwamba ni maneno matakatifu+ ya Mungu; kama yeyote akihudumu,+ na ahudumu kama anayetegemea nguvu ambazo Mungu hutoa;+ ili katika mambo yote Mungu atukuzwe+ kupitia Yesu Kristo. Utukufu+ na nguvu ni zake milele na milele. Amina.

12 Wapendwa, msishangazwe juu ya moto unaowaka katikati yenu, unaowapata ninyi ili kuwa jaribu,+ kana kwamba jambo geni linawapata. 13 Kinyume chake, endeleeni kushangilia+ kwa maana ninyi ni washiriki katika mateso ya Kristo,+ ili mshangilie na kuwa na shangwe sana pia wakati wa ufunuo+ wa utukufu wake. 14 Ikiwa mnashutumiwa kwa ajili ya jina la Kristo,+ ninyi ni wenye furaha,+ kwa sababu ile roho ya utukufu, yaani roho ya Mungu, inatulia juu yenu.+

15 Hata hivyo, yeyote kati yenu asiteseke+ kwa sababu yeye ni muuaji au mwizi au mtenda-maovu au mwenye kujiingiza katika mambo ya watu wengine.+ 16 Lakini akiteseka+ kwa sababu yeye ni Mkristo, asione aibu,+ bali na aendelee kumtukuza Mungu katika jina hili. 17 Kwa maana ni wakati uliowekwa wa hukumu kuanza na nyumba ya Mungu.+ Sasa ikiwa inaanza na sisi kwanza,+ basi mwisho wa wale wasioitii habari njema ya Mungu utakuwaje?+ 18 “Na ikiwa mtu mwadilifu anaokolewa kwa shida,+ mtu asiyemwogopa Mungu na mtenda-dhambi wataonekana wapi?”+ 19 Kwa hiyo, basi, acheni wale wanaoteseka kwa kupatana na mapenzi ya Mungu waendelee kuzikabidhi nafsi zao kwa Muumba mwaminifu wanapotenda mema.+

5 Kwa hiyo, ninawapa himizo hili wanaume wazee walio kati yenu, kwa kuwa mimi pia ni mwanamume mzee+ pamoja nao na shahidi+ wa mateso ya Kristo, mshiriki hata wa utukufu utakaofunuliwa:+ 2 Lichungeni+ kundi la Mungu+ lililo chini ya uangalizi wenu, si kwa kulazimishwa, bali kwa kupenda;+ wala si kwa kupenda pato lisilo la haki,+ bali kwa hamu; 3 wala si kama kwa kupiga ubwana+ juu ya wale ambao ni urithi wa Mungu,+ bali kuwa vielelezo kwa kundi.+ 4 Na mchungaji mkuu+ akiisha kufunuliwa, mtapokea taji la utukufu+ lisiloweza kufifia.+

5 Vivyo hivyo, enyi vijana, jitiisheni+ kwa wanaume wazee. Lakini ninyi nyote jifungeni unyenyekevu wa akili kuelekeana ninyi wenyewe,+ kwa sababu Mungu huwapinga wenye majivuno, lakini huwapa wanyenyekevu fadhili zisizostahiliwa.+

6 Kwa hiyo, jinyenyekezeni chini ya mkono wenye nguvu wa Mungu, ili awainue ninyi katika wakati unaofaa;+ 7 huku mkitupa mahangaiko+ yenu yote juu yake, kwa sababu yeye anawajali ninyi.+ 8 Tunzeni akili zenu, iweni wenye kulinda.+ Adui yenu, Ibilisi, anatembea huku na huku kama simba anayenguruma, akitafuta kummeza mtu.+ 9 Lakini chukueni msimamo mkampinge yeye,+ mkiwa imara katika imani, mkijua kwamba mambo yaleyale kwa njia ya mateso yanatimizwa katika ushirika mzima wa ndugu zenu ulimwenguni.+ 10 Lakini, mkiisha kuteseka kitambo kidogo,+ Mungu wa fadhili zote zisizostahiliwa, aliyewaita ninyi kwenye utukufu wake wa milele+ katika muungano+ na Kristo, yeye mwenyewe atamaliza mazoezi yenu, atawafanya ninyi kuwa imara,+ atawafanya ninyi kuwa wenye nguvu.+ 11 Kwake yeye na kuwe na nguvu+ milele. Amina.

12 Kupitia Silvano,+ ndugu mwaminifu, kama ninavyomhesabu yeye, nimewaandikia ninyi kwa maneno machache,+ ili kutoa kitia-moyo na ushahidi wa bidii kwamba hizi ndizo fadhili zisizostahiliwa za Mungu zilizo za kweli; katika hizo simameni imara.+ 13 Mwanamke aliye katika Babiloni,+ mchaguliwa kama ninyi, anawatumia ninyi salamu zake, na vilevile Marko+ mwanangu. 14 Salimianeni kwa busu ya upendo.+

Na muwe na amani ninyi nyote mlio katika muungano na Kristo.+

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki