Barua ya Yakobo
1 Yakobo,+ mtumwa+ wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo, kwa makabila+ kumi na mawili yaliyotawanyika+ huku na huku:
Salamu!
2 Oneni yote kuwa shangwe, ndugu zangu, mnapokutana na majaribu ya namna mbalimbali,+ 3 mkijua kwamba sifa iliyojaribiwa ya imani yenu hutokeza uvumilivu.+ 4 Lakini acheni uvumilivu ukamilishe kazi yake, ili muwe kamili+ na timamu katika mambo yote, bila kukosa kitu chochote.+
5 Kwa hiyo, ikiwa yeyote kati yenu anakosa hekima,+ na aendelee kumwomba Mungu,+ kwa maana yeye huwapa wote kwa ukarimu na bila kushutumu;+ naye atapewa hiyo.+ 6 Lakini na aendelee kuomba+ kwa imani, bila kutia shaka hata kidogo,+ kwa maana yeye anayetia shaka ni kama wimbi la bahari linaloendeshwa na upepo+ na kupeperushwa huku na huku. 7 Kwa kweli, mtu huyo asidhani kwamba atapokea kitu chochote kutoka kwa Yehova;+ 8 yeye ni mtu anayesitasita,+ asiye imara+ katika njia zake zote.
9 Lakini ndugu wa hali ya chini na afurahie kuinuliwa kwake,+ 10 na tajiri+ kushushwa kwake, kwa sababu atapitilia mbali kama ua la majani.+ 11 Kwa maana jua huchomoza pamoja na joto lake lenye kuunguza na kuyanyausha majani, na ua lake huanguka na uzuri wa sura yake ya nje huharibika. Vivyo hivyo, pia, mtu tajiri atanyauka katika njia zake za maisha.+
12 Mwenye furaha ni mtu anayeendelea kuvumilia jaribu,+ kwa sababu akiisha kukubaliwa atapokea taji la uzima,+ ambalo Yehova aliwaahidi wale wanaoendelea kumpenda.+ 13 Mtu akiwa chini ya jaribu,+ yeye asiseme: “Mungu ananijaribu.” Kwa maana Mungu hawezi kujaribiwa na mambo maovu wala yeye mwenyewe hamjaribu yeyote. 14 Lakini kila mtu hujaribiwa kwa kuvutwa na kushawishiwa na tamaa yake mwenyewe.+ 15 Kisha tamaa, wakati imetunga mimba, huzaa dhambi;+ nayo dhambi, wakati imetimizwa, huleta kifo.+
16 Msipotoshwe,+ ndugu zangu wapendwa. 17 Kila zawadi njema+ na kila tuzo kamilifu hutoka juu,+ kwa maana hushuka kutoka kwa Baba wa mianga ya mbinguni,+ naye habadiliki, kama kugeuka kwa kivuli.+ 18 Kwa sababu yeye alipenda+ hilo, alituzaa sisi kwa njia ya neno la kweli,+ ili sisi tuwe sehemu fulani ya matunda ya kwanza+ ya viumbe vyake.
19 Jueni hili, ndugu zangu wapendwa. Kila mtu lazima awe mwepesi kuhusu kusikia, si mwepesi wa kusema,+ si mwepesi wa ghadhabu;+ 20 kwa maana ghadhabu ya mwanadamu haitokezi uadilifu wa Mungu.+ 21 Kwa hiyo ondoeni uchafu wote na jambo lile lenye kuzidi, yaani, ubaya,+ na pokeeni kwa upole upandwaji wa neno+ lile linaloweza kuokoa nafsi zenu.+
22 Hata hivyo, iweni watendaji wa neno,+ na si wasikiaji tu, mkijidanganya wenyewe kwa mawazo yasiyo ya kweli.+ 23 Kwa maana ikiwa yeyote ni msikiaji wa neno, na si mtendaji,+ huyo ni kama mtu anayeutazama uso wake wa asili katika kioo. 24 Kwa maana yeye hujitazama, naye huenda zake na kusahau mara moja yeye ni mtu wa namna gani. 25 Lakini yeye anayechunguza ndani ya sheria kamilifu+ iliyo ya uhuru na ambaye hudumu katika hiyo, mtu huyo, kwa sababu amekuwa, si msikiaji msahaulifu, bali mtendaji wa kazi,+ atakuwa mwenye furaha+ katika kuitenda.
26 Ikiwa mtu yeyote anajiona kuwa mwabudu anayeshikilia vizuri namna ya ibada+ na bado hauongozi ulimi wake,+ bali anaendelea kuudanganya moyo wake mwenyewe,+ namna ya ibada ya mtu huyo ni ya ubatili.+ 27 Namna ya ibada iliyo safi+ na isiyotiwa unajisi+ kwa maoni ya Mungu wetu na Baba ni hii: kuwatunza mayatima+ na wajane+ katika dhiki+ yao, na kuendelea kujitunza bila doa+ kutokana na ulimwengu.+
2 Ndugu zangu, je, mnashika imani ya Bwana wetu Yesu Kristo, utukufu wetu,+ kwa matendo ya kupendelea?+ 2 Kwa maana, mtu aliye na pete za dhahabu kwenye vidole vyake na aliyevaa mavazi ya fahari akiingia katika kusanyiko lenu,+ lakini mtu maskini aliyevaa mavazi yenye uchafu akiingia pia,+ 3 mnamtazama kwa kibali+ yule aliyevaa mavazi ya fahari na kumwambia: “Wewe kalia kiti hiki hapa mahali pazuri,” nanyi mnamwambia yule maskini: “Wewe simama,” au: “Kalia kiti kile pale chini ya kiti changu cha miguu,” 4 ninyi mna tofauti za kitabaka katikati yenu wenyewe+ nanyi mmekuwa waamuzi+ wanaotoa maamuzi maovu,+ sivyo?
5 Sikilizeni, ndugu zangu wapendwa. Mungu alichagua walio maskini+ kwa habari ya ulimwengu ili wawe matajiri+ katika imani na warithi wa ufalme, aliowaahidi wale wanaompenda,+ sivyo? 6 Ingawa hivyo, ninyi mmemvunjia heshima mtu maskini. Matajiri huwakandamiza+ ninyi, nao huwakokota ninyi na kuwapeleka mbele ya mahakama,+ sivyo? 7 Wao hulikufuru+ lile jina zuri ambalo kwa hilo mliitwa,+ sivyo? 8 Basi, mkizoea kufanya sheria ya kifalme+ kulingana na andiko: “Mpende jirani yako kama wewe mwenyewe,”+ mnafanya vema kabisa. 9 Lakini mkiendelea kuonyesha upendeleo,+ mnafanya dhambi, kwa maana sheria+ inawakaripia ninyi kuwa ni wakosaji.
10 Kwa maana yeyote anayeshika Sheria yote lakini ajikwae katika jambo moja, amekosa juu ya zote.+ 11 Kwa maana yeye aliyesema: “Usifanye uzinzi,”+ alisema pia: “Usiue.”+ Basi, ikiwa hufanyi uzinzi lakini unaua, umekosa juu ya sheria. 12 Endeleeni kusema na kutenda kama wale watakaohukumiwa kwa sheria ya watu huru.+ 13 Kwa maana yeye asiye na mazoea ya kuonyesha rehema atapata hukumu yake bila rehema.+ Rehema hufurahi kwa njia ya ushindi juu ya hukumu.
14 Ina faida gani, ndugu zangu, kama mtu fulani akisema ana imani+ lakini hana matendo?+ Je, imani hiyo inaweza kumwokoa?+ 15 Ikiwa ndugu au dada yuko uchi naye hana chakula cha kutosha kwa ajili ya siku,+ 16 na mmoja wenu amwambie: “Nenda kwa amani, jipashe moto na kula vizuri,” lakini ninyi mkose kumpa mahitaji ya mwili wake, ina faida gani?+ 17 Vivyo hivyo, pia, imani, ikiwa haina matendo,+ imekufa yenyewe.
18 Hata hivyo, mtu fulani atasema: “Wewe una imani, nami nina matendo. Nionyeshe imani yako bila matendo, nami nitakuonyesha imani yangu kwa matendo yangu.”+ 19 Wewe unaamini kuna Mungu mmoja, sivyo?+ Unafanya vema kabisa. Hata hivyo roho waovu nao wanaamini na kutetemeka.+ 20 Lakini je, unataka kujua, Ee mwanadamu asiye na akili, kwamba imani bila matendo haizai? 21 Je, Abrahamu baba+ yetu hakutangazwa kuwa mwadilifu kwa matendo baada ya kumtoa Isaka mwana wake juu ya madhabahu?+ 22 Mnaona kwamba imani yake ilitenda pamoja na matendo yake na kwa matendo yake imani yake ilikamilishwa,+ 23 na andiko likatimizwa linalosema: “Abrahamu alikuwa na imani katika Yehova, na ikahesabiwa kwake kuwa ni uadilifu,”+ naye akaitwa “rafiki ya Yehova.”+
24 Mnaona kwamba mtu hutangazwa kuwa mwadilifu+ kwa matendo,+ na si kwa imani peke yake.+ 25 Vivyo hivyo, je, Rahabu+ yule kahaba hakutangazwa pia kuwa mwadilifu kwa matendo, baada ya kuwakaribisha wale wajumbe na kuwatoa nje kwa njia nyingine?+ 26 Kwa kweli, kama vile ambavyo mwili bila roho umekufa,+ vivyo hivyo pia imani bila matendo imekufa.+
3 Si wengi kati yenu wanaopaswa kuwa walimu,+ ndugu zangu, mkijua kwamba tutapokea hukumu nzito zaidi.+ 2 Kwa maana sisi sote hujikwaa mara nyingi.+ Ikiwa yeyote hajikwai katika neno,+ huyo ni mtu mkamilifu,+ anayeweza kuuongoza kwa lijamu mwili wake wote pia. 3 Tukiweka lijamu+ katika vinywa vya farasi ili watutii,+ sisi huuongoza mwili wao wote pia. 4 Tazameni! Hata mashua, ingawa ni kubwa sana nazo huendeshwa na pepo kali, hizo huongozwa na mtambo wa usukani+ ulio mdogo sana ili kwenda pale ambapo mwelekeo wa mtu aliye kwenye usukani anataka.
5 Hivyo, pia, ulimi ni kiungo kidogo na bado hujigamba kwa njia kubwa.+ Tazameni! Ni moto mdogo tu unaohitajika ili kuuwasha mwitu mkubwa! 6 Basi, ulimi ni moto.+ Ulimi ni ulimwengu wa ukosefu wa uadilifu kati ya viungo vyetu, kwa maana huutia doa mwili+ wote na kuuwasha moto mzunguko wa uhai wa asili nao huwashwa moto na Gehena.* 7 Kwa maana kila aina ya mnyama-mwitu na vilevile ndege na kitu kinachotambaa na kiumbe cha baharini ni vya kufugwa navyo vimefugwa na binadamu.+ 8 Lakini ulimi, hakuna hata mmoja wa wanadamu anayeweza kuufuga. Huo ni kitu kitundu chenye kudhuru, umejaa sumu yenye kuua.+ 9 Kwa huo sisi humbariki Yehova,+ naam, Baba,+ na bado kwa huo sisi huwalaani+ wanadamu ambao wamekuja kuwako “kwa mfano wa Mungu.”+ 10 Kubariki na kulaani hutoka katika kinywa kilekile.
Haifai, ndugu zangu, mambo haya kuendelea kutendeka kwa njia hiyo.+ 11 Je, chemchemi+ hutokeza matamu na machungu kutoka katika shimo lilelile? 12 Ndugu zangu, je, mtini unaweza kuzaa zeituni au mzabibu kuzaa tini?+ Wala maji ya chumvi hayawezi kutokeza maji matamu.
13 Ni nani aliye na hekima na mwenye uelewaji kati yenu? Na aonyeshe kutokana na mwenendo wake mzuri matendo+ yake kwa upole ulio wa hekima. 14 Lakini ikiwa mna wivu+ mkali na ugomvi+ katika mioyo yenu, msiwe mkijigamba+ na kusema uwongo juu ya ile kweli.+ 15 Hii siyo hekima inayoshuka kutoka juu,+ bali ni ya kidunia,+ ya kinyama, ya roho waovu.+ 16 Kwa maana mahali ambapo pana wivu+ na ugomvi, hapo pana machafuko na kila jambo baya.+
17 Lakini hekima+ inayotoka juu kwanza kabisa ni safi kiadili,+ kisha yenye kufanya amani,+ yenye usawaziko,+ tayari kutii, yenye kujaa rehema na matunda mema,+ haifanyi tofauti zenye ubaguzi,+ si ya kinafiki.+ 18 Zaidi ya hayo, mbegu ya tunda+ la uadilifu+ hupandwa chini ya hali zenye amani+ kwa wale wanaofanya amani.+
4 Vita vinatoka chanzo gani na mapigano yanatoka chanzo gani katikati yenu? Je, havitoki katika chanzo hiki,+ yaani, katika tamaa zenu za mwili zinazoendeleza pambano katika viungo vyenu?+ 2 Mnatamani, na bado hamna kitu. Mnaendelea kuua+ na kutamani+ kwa wivu, na bado hamwezi kupata. Mnaendelea kupigana+ na kufanya vita. Hamna kitu kwa sababu hamwombi. 3 Mnaomba, na bado hampokei, kwa sababu mnaomba kwa kusudi baya,+ ili mvitumie kwa tamaa zenu za mwili.+
4 Enyi wazinzi,+ je, hamjui kwamba urafiki na ulimwengu ni uadui na Mungu?+ Kwa hiyo, yeyote anayetaka kuwa rafiki+ ya ulimwengu anajifanya kuwa adui ya Mungu.+ 5 Au je, inaonekana kwenu kwamba andiko linasema hivi bila kusudi lolote: “Roho+ ambayo imefanya makao ndani yetu hutamani kuwa na mwelekeo wa kuona wivu”? 6 Hata hivyo, fadhili zisizostahiliwa ambazo yeye hutoa ni kubwa zaidi.+ Kwa hiyo, hilo linasema: “Mungu huwapinga wenye majivuno,+ lakini huwapa wanyenyekevu fadhili zisizostahiliwa.”+
7 Basi, jitiisheni+ kwa Mungu; lakini mpingeni Ibilisi,+ naye atawakimbia ninyi.+ 8 Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.+ Safisheni mikono yenu, ninyi watenda-dhambi,+ na takaseni mioyo yenu,+ ninyi wenye kusitasita.+ 9 Iweni na taabu na kuomboleza na kulia.+ Kicheko chenu na kigeuzwe kuwa maombolezo, na shangwe yenu kuwa huzuni.+ 10 Jinyenyekezeni machoni pa Yehova,+ naye atawainua ninyi.+
11 Mwache kusemana wenyewe, akina ndugu.+ Yeye anayesema vibaya juu ya ndugu au anayemhukumu+ ndugu yake husema vibaya juu ya sheria na kuihukumu sheria. Na ikiwa unaihukumu sheria, basi wewe si mtendaji wa sheria, bali ni mwamuzi.+ 12 Kuna mmoja ambaye ni mpaji-sheria na mwamuzi,+ ambaye anaweza kuokoa na kuangamiza.+ Lakini wewe ni nani ili uwe ukimhukumu jirani yako?+
13 Haya, basi, ninyi ambao husema: “Leo au kesho tutasafiri kwenda jiji fulani nasi tutakaa mwaka mmoja huko, tutafanya biashara na kupata faida,”+ 14 ingawa hamjui uzima wenu utakuwa namna gani kesho.+ Kwa maana ninyi ni ukungu unaotokea kwa muda kidogo na kisha kutoweka.+ 15 Badala yake, mnapaswa kusema: “Yehova akipenda,+ tutaishi na pia kufanya hili au lile.”+ 16 Lakini sasa mnajivunia kujigamba kwenu kwa kujidai.+ Majivuno yote ya namna hiyo ni maovu. 17 Kwa hiyo, ikiwa mtu anajua jinsi ya kufanya yaliyo sawa na bado hayafanyi,+ hiyo ni dhambi+ kwake.
5 Haya! basi, enyi matajiri,+ lieni, mkipiga mayowe juu ya taabu zenu zinazokuja juu yenu.+ 2 Utajiri wenu umeoza, na mavazi yenu ya nje yameliwa na nondo.+ 3 Dhahabu na fedha zenu zimeliwa na kutu, na kutu yake itakuwa kama ushahidi juu yenu nayo itakula sehemu zenu zenye nyama. Kitu kama moto+ ndicho mmeweka akiba+ katika siku za mwisho.+ 4 Tazama! Mishahara iliyo haki ya wafanyakazi waliovuna mashamba yenu lakini ambayo mmeizuilia,+ inaendelea kupaaza kilio,+ na vilio vya kuomba msaada+ vya wavunaji vimeingia masikioni+ mwa Yehova wa majeshi. 5 Ninyi mmeishi katika anasa duniani nanyi mmejiingiza katika tamaa za mwili.+ Mmeinonesha mioyo yenu katika siku ya machinjo.+ 6 Mmemhukumia hatia, mmemuua mwadilifu. Je, yeye hawapingi ninyi?+
7 Basi, onyesheni subira, akina ndugu, mpaka kuwapo+ kwa Bwana. Tazama! Mkulima huendelea kungojea matunda yenye thamani ya nchi, anayasubiri mpaka apate mvua ya mapema na mvua ya baadaye.+ 8 Ninyi pia onyesheni subira;+ fanyeni mioyo yenu kuwa imara, kwa sababu kuwapo kwa Bwana kumekaribia.+
9 Msinung’unikiane, akina ndugu, ili msihukumiwe.+ Tazama! Mwamuzi amesimama mbele ya milango.+ 10 Akina ndugu, wachukueni manabii+ kuwa kielelezo+ cha kupatwa na uovu+ na kuonyesha subira,+ wale waliosema katika jina la Yehova.+ 11 Tazama! Tunawatangaza kuwa wenye furaha wale ambao wamevumilia.+ Mmesikia juu ya uvumilivu wa Ayubu+ nanyi mmeona matokeo ambayo Yehova alileta,+ kwamba Yehova ni mwenye upendo mwororo sana na mwenye rehema.+
12 Hata hivyo, akina ndugu, zaidi ya mambo yote, acheni kuapa, naam, ama kwa mbingu ama kwa dunia ama kwa kiapo kingine chochote.+ Bali acheni Ndiyo yenu imaanishe Ndiyo, na Siyo yenu, Siyo, ili msianguke hukumuni.+
13 Je, kuna yeyote kati yenu anayepatwa na uovu? Na aendeleze sala.+ Je, kuna yeyote mwenye roho changamfu? Na aimbe zaburi.+ 14 Je, kuna yeyote mgonjwa kati yenu?+ Na awaite kwake wanaume wazee+ wa kutaniko, nao wasali juu yake, wakimpaka mafuta+ katika jina la Yehova. 15 Na sala ya imani itamponya huyo asiyejisikia vizuri,+ na Yehova atamwinua.+ Pia, ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa.+
16 Kwa hiyo ungameni+ waziwazi dhambi zenu kwa mtu na mwenzake na kusali kwa ajili ya mtu na mwenzake, ili mponywe.+ Dua ya mtu mwadilifu, inapofanya kazi, ina nguvu nyingi.+ 17 Eliya alikuwa mtu mwenye hisia kama zetu,+ na bado katika sala alisali mvua isinyeshe;+ na mvua haikunyesha juu ya nchi kwa miaka mitatu na miezi sita. 18 Naye akasali tena, na mbingu ikatoa mvua na nchi ikazaa matunda yake.+
19 Ndugu zangu, yeyote katikati yenu akipotoshwa kutoka katika kweli na mwingine amrudishe,+ 20 jueni kwamba yeye anayemrudisha mtenda-dhambi kutoka kwenye kosa+ la njia yake ataiokoa nafsi yake kutoka kwenye kifo+ naye atafunika dhambi nyingi.+
[Maelezo ya Chini]
Bonde la Hinomu. Tazama Nyongeza 2.