Kwa Waebrania
1 Mungu, ambaye zamani za kale alisema katika pindi nyingi+ na katika njia nyingi na mababu zetu kupitia manabii,+ 2 mwishoni mwa siku hizi+ amesema nasi kupitia Mwana,+ aliyemweka rasmi kuwa mrithi wa vitu vyote,+ na ambaye kupitia yeye aliifanya+ mifumo ya mambo. 3 Yeye ndiye mng’ao wa utukufu+ wake na mwakilisho sawasawa wa utu wake wenyewe,+ naye hutegemeza vitu vyote kwa neno la nguvu zake;+ na akiisha kuzitakasa dhambi+ zetu aliketi kwenye mkono wa kuume+ wa Ukuu katika mahali pa juu sana.+ 4 Kwa hiyo amekuwa bora kuliko malaika,+ kwa kuwa amerithi jina+ bora kabisa kuliko lao.
5 Kwa mfano, alipata kumwambia nani kati ya malaika: “Wewe ni mwanangu; mimi, leo, nimekuwa baba yako”?+ Na tena: “Mimi mwenyewe nitakuwa baba yake, na yeye mwenyewe atakuwa mwanangu”?+ 6 Lakini anapomleta tena Mzaliwa wake wa kwanza+ katika dunia inayokaliwa, yeye asema: “Malaika+ wote wa Mungu na wamsujudie.”+
7 Pia, kuwahusu malaika yeye anasema: “Naye anawafanya malaika zake kuwa roho, na watumishi wake wa watu wote kuwa mwali wa moto.”+ 8 Lakini kumhusu Mwana: “Mungu ni kiti chako cha ufalme milele+ na milele, na fimbo ya enzi ya ufalme+ wako ni fimbo ya unyoofu.+ 9 Uliupenda uadilifu, nawe ukauchukia uasi-sheria. Ndiyo sababu Mungu, Mungu wako, alikutia mafuta+ kwa mafuta ya kushangilia kuliko wenzako.”+ 10 Na: “Wewe pale mwanzoni, Ee Bwana, uliiweka misingi ya dunia, nazo mbingu ni kazi za mikono yako.+ 11 Hizo zitaangamia, lakini wewe mwenyewe utabaki sikuzote; nazo zote zitachakaa kama vazi la nje,+ 12 nawe utazikunja kama kanzu,+ kama vazi la nje; nazo zitabadilishwa, lakini wewe ni yuleyule, nayo miaka yako haitakwisha kamwe.”+
13 Lakini amepata kusema hivi kuhusu nani kati ya malaika: “Keti kwenye mkono wangu wa kuume, mpaka niwaweke adui zako kuwa kiti cha miguu yako”?+ 14 Je, wao wote si roho+ kwa ajili ya utumishi wa watu wote,+ waliotumwa kuhudumu kwa ajili ya wale watakaorithi+ wokovu?
2 Hiyo ndiyo sababu ni lazima kwetu kuyakazia uangalifu zaidi kuliko ilivyo kawaida mambo tuliyosikia,+ ili tusipeperushwe kamwe.+ 2 Kwa maana ikiwa neno lililosemwa kupitia malaika+ lilikuwa imara, na kila kosa na tendo la kutotii lilipokea malipo kupatana na haki;+ 3 sisi tutaponaje+ ikiwa tumepuuza+ wokovu mkuu+ namna hii kwa kuwa ulianza kusemwa kupitia Bwana+ wetu nasi tukathibitishiwa+ na wale waliomsikia, 4 huku Mungu akijiunga katika kutoa ushahidi kwa ishara na vilevile mambo ya ajabu na matendo mbalimbali yenye nguvu+ na kwa ugawaji+ wa roho takatifu kulingana na mapenzi yake?+
5 Kwa maana yeye hajaitiisha chini ya malaika dunia yenye kukaliwa inayokuja,+ ambayo sisi tunasema kuihusu. 6 Bali shahidi fulani ametoa uthibitisho mahali fulani, akisema: “Mwanadamu ni nini hivi kwamba umweke akilini,+ au mwana wa binadamu hivi kwamba umtunze?+ 7 Ulimfanya mdogo kidogo kuliko malaika; ulimvika taji kwa utukufu na heshima,+ na kumweka juu ya kazi za mikono yako.+ 8 Vitu vyote ulivitiisha chini ya miguu yake.”+ Kwa maana yeye alivitiisha vitu vyote chini yake,+ Mungu hakuacha kitu chochote kisichotiishwa chini yake.+ Ingawa hivyo, sisi bado hatuoni vitu vyote vikiwa vimetiishwa chini yake;+ 9 lakini tunamwona Yesu, ambaye alikuwa amefanywa kuwa mdogo kidogo kuliko malaika,+ amevikwa taji la utukufu+ na heshima kwa kupatwa na kifo,+ ili kwa fadhili zisizostahiliwa za Mungu aonje kifo kwa ajili ya kila mwanadamu.+
10 Kwa maana ilifaa kwa yule ambaye kwa ajili yake vitu vyote vipo+ na kupitia kwake vitu vyote vipo, katika kuleta wana wengi kwenye utukufu,+ amfanye Wakili Mkuu+ wa wokovu wao kuwa mkamilifu kupitia mateso.+ 11 Kwa maana yeye anayetakasa na wale wanaotakaswa+ pia wote hutokana na mmoja,+ na kwa sababu hii yeye haoni aibu kuwaita “ndugu,”+ 12 kama anavyosema: “Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu; katikati ya kutaniko nitakusifu wewe kwa wimbo.”+ 13 Na tena: “Tegemeo langu litakuwa katika yeye.”+ Na tena: “Tazama! mimi na watoto wachanga, ambao Yehova alinipa.”+
14 Basi, kwa kuwa “watoto wachanga” ni washiriki wa damu na mwili, yeye pia vivyo hivyo aliyashiriki mambo hayohayo,+ ili kupitia kifo+ chake apate kumwangamiza+ yule aliye na uwezo wa kusababisha kifo,+ yaani, Ibilisi;+ 15 na ili awaweke huru+ wale wote ambao kwa kuogopa kifo+ walikuwa wametiishwa chini ya utumwa katika maisha yao yote.+ 16 Kwa maana kwa kweli yeye hawasaidii malaika hata kidogo, bali anasaidia uzao wa Abrahamu.+ 17 Kwa hiyo alipaswa kuwa kama “ndugu” zake katika mambo yote,+ ili awe kuhani mkuu mwenye rehema na mwaminifu katika mambo yanayohusiana na Mungu,+ kusudi atoe dhabihu ya upatanisho+ kwa ajili ya dhambi za watu.+ 18 Kwa kuwa yeye mwenyewe ameteseka alipokuwa akijaribiwa,+ anaweza kuwasaidia wale wanaojaribiwa.+
3 Kwa hiyo, ndugu watakatifu, washiriki wa mwito wa mbinguni,+ mfikirieni mtume+ na kuhani mkuu tunayemkiri+—Yesu. 2 Alikuwa mwaminifu+ kwa Huyo aliyemfanya kuwa hivyo, kama Musa+ alivyokuwa pia katika nyumba yote ya Huyo.+ 3 Kwa maana huyu wa mwisho anahesabiwa kustahili utukufu+ kuliko Musa, kwa kuwa yeye+ anayejenga nyumba ana heshima kuliko nyumba yenyewe.+ 4 Bila shaka, kila nyumba hujengwa na mtu fulani, lakini yeye aliyevijenga vitu vyote ni Mungu.+ 5 Na Musa akiwa mtumishi+ alikuwa mwaminifu katika nyumba yote yake Huyo kama ushuhuda wa mambo ambayo yangesemwa baadaye,+ 6 lakini Kristo alikuwa mwaminifu akiwa Mwana+ juu ya nyumba yake Huyo. Sisi ni nyumba yake Huyo,+ ikiwa tunashikilia sana uhuru wetu wa kusema na kujisifu kwetu juu ya tumaini, imara mpaka mwisho.+
7 Kwa sababu hiyo, kama vile inavyosema roho+ takatifu: “Leo ikiwa mtaisikiliza sauti yake,+ 8 msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama ule wakati wa kusababisha hasira kali,+ kama katika ile siku ya kufanya jaribu+ nyikani,+ 9 ambayo mababu zenu walinijaribu kwa uchunguzi, na bado walikuwa wameyaona matendo+ yangu kwa miaka 40.+ 10 Kwa sababu hiyo nikachukizwa na kizazi hiki, nikasema, ‘Wao hupotea sikuzote katika mioyo yao,+ nao wenyewe hawajapata kuzijua njia zangu.’+ 11 Kwa hiyo niliapa kwa hasira yangu, ‘Hawataingia+ katika pumziko langu.’ ”+
12 Jihadharini, akina ndugu, ili moyo mwovu unaokosa imani usije ukasitawi ndani ya yeyote kati yenu kwa kujiondoa kwa Mungu aliye hai;+ 13 lakini endeleeni kuhimizana+ kila siku, maadamu inaweza kuitwa “Leo,”+ ili yeyote kati yenu asije akafanywa kuwa mgumu kwa nguvu za udanganyifu+ za dhambi. 14 Kwa maana sisi kwa kweli tunakuwa washiriki wa Kristo+ ikiwa tu tunaushikilia sana uhakika tuliokuwa nao mwanzoni imara mpaka mwisho,+ 15 huku ikisemwa: “Leo ikiwa mtaisikiliza sauti yake,+ msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama ule wakati wa kusababisha hasira kali.”+
16 Kwa maana ni nani waliosikia na bado wakachochea hasira kali?+ Kwa kweli, je, hawakufanya hivyo wale wote waliotoka Misri chini ya Musa?+ 17 Zaidi ya hayo, Mungu alichukizwa na akina nani kwa miaka 40?+ Je, haikuwa na wale waliotenda dhambi, ambao mizoga yao ilianguka nyikani?+ 18 Lakini aliapa+ kwa akina nani kwamba hawataingia katika pumziko lake isipokuwa kwa wale waliotenda kwa kutotii?+ 19 Kwa hiyo tunaona kwamba hawakuweza kuingia kwa sababu ya kukosa imani.+
4 Kwa hiyo, kwa kuwa ahadi imebaki ya kuingia katika pumziko lake,+ acheni tuogope kwamba wakati fulani yeyote kati yenu asije akaonekana kuwa amepungukiwa.+ 2 Kwa maana sisi pia tumetangaziwa habari njema,+ kama wao pia walivyotangaziwa;+ lakini neno lililosikiwa halikuwa na faida kwao,+ kwa sababu hawakuunganishwa kwa imani+ pamoja na wale waliosikia.+ 3 Kwa maana sisi ambao tumeonyesha imani tunaingia katika pumziko, kama vile ambavyo amesema: “Kwa hiyo niliapa+ katika hasira yangu, ‘Hawataingia+ katika pumziko langu,’ ”+ ijapokuwa kazi zake zilimalizwa+ tangu kuwekwa msingi wa ulimwengu.+ 4 Kwa maana katika mahali fulani yeye amesema hivi juu ya siku ya saba: “Na Mungu akapumzika siku ya saba kutokana na kazi zake zote,”+ 5 na tena katika mahali hapa: “Hawataingia katika pumziko langu.”+
6 Basi, kwa kuwa bado inabaki watu fulani waingie katika hilo, na wale ambao walitangaziwa kwanza habari njema+ hawakuingia kwa sababu ya kutotii,+ 7 yeye tena anaweka siku fulani kwa kusema hivi baada ya wakati mrefu sana katika zaburi ya Daudi “Leo”; kama ilivyosemwa hapo juu: “Leo ikiwa mtaisikiliza sauti yake,+ msiifanye mioyo yenu kuwa migumu.”+ 8 Kwa maana kama Yoshua+ angekuwa amewaingiza katika mahali pa pumziko,+ Mungu hangesema+ baadaye juu ya siku nyingine. 9 Kwa hiyo bado limebaki pumziko la sabato kwa ajili ya watu wa Mungu.+ 10 Kwa maana mtu ambaye ameingia katika pumziko+ la Mungu yeye mwenyewe pia amepumzika kutokana na kazi zake mwenyewe,+ kama Mungu alivyopumzika kutokana na kazi zake mwenyewe.
11 Kwa hiyo acheni sisi tufanye yote tunayoweza ili kuingia katika pumziko hilo, yeyote asije akaanguka katika kielelezo kilekile cha kutotii.+ 12 Kwa maana neno+ la Mungu liko hai+ nalo lina nguvu+ na ni lenye makali zaidi kuliko upanga wowote wenye makali kuwili+ nalo huchoma hata kufikia kugawanya nafsi+ na roho,+ na viungo na urojorojo wake, nalo linaweza kutambua fikira na makusudio ya moyo.+ 13 Na hakuna kiumbe kisichokuwa wazi machoni pake,+ bali vitu vyote viko uchi navyo vimefunuliwa wazi machoni pake yeye ambaye tunatoa hesabu kwake.+
14 Basi, kwa kuwa tuna kuhani mkuu sana ambaye amepita katika mbingu,+ Yesu Mwana wa Mungu,+ acheni tuendelee kumkiri yeye.+ 15 Kwa maana tuna kuhani mkuu, si mtu ambaye hawezi kuusikitikia+ udhaifu wetu, bali yeye ambaye amejaribiwa katika mambo yote kama sisi wenyewe, lakini bila kuwa na dhambi.+ 16 Basi na tukikaribie,+ tukiwa na uhuru wa kusema,+ kiti cha ufalme cha fadhili zisizostahiliwa, ili tupokee rehema na kupata fadhili zisizostahiliwa kuwa msaada kwa wakati unaofaa.+
5 Kwa maana kila kuhani mkuu anayechukuliwa kutoka kati ya wanadamu huwekwa rasmi kwa ajili ya wanadamu juu ya mambo yanayohusiana na Mungu,+ ili atoe zawadi na dhabihu kwa ajili ya dhambi.+ 2 Yeye anaweza kuwatendea kwa kiasi wale wasiojua na wanaokosea kwa kuwa yeye pia amezungukwa na udhaifu wake mwenyewe,+ 3 na kwa sababu ya huo ana wajibu wa kutoa matoleo ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe kama vile kwa ajili ya watu.+
4 Pia, mtu huchukua heshima hii, si kwa kupenda kwake mwenyewe,+ bali tu Mungu anapomwita,+ kama Haruni+ pia alivyoitwa. 5 Vivyo hivyo pia Kristo hakujitukuza mwenyewe+ kwa kuwa kuhani mkuu,+ bali alitukuzwa+ na yeye aliyesema hivi kumhusu: “Wewe ni mwanangu; mimi, leo, nimekuwa baba yako.”+ 6 Kama vile anavyosema pia mahali pengine: “Wewe ni kuhani milele kwa mfano wa Melkizedeki.”+
7 Katika siku za mwili wake wenye nyama Kristo alitoa dua na pia maombi+ kwa Yule aliyekuwa na uwezo wa kumwokoa kutoka katika kifo, pamoja na vilio vyenye nguvu+ na machozi, naye akasikiwa vizuri kwa sababu ya kumwogopa+ Mungu. 8 Ijapokuwa yeye alikuwa Mwana, alijifunza kutii kutokana na mambo aliyoteseka;+ 9 na baada ya yeye kufanywa kuwa mkamilifu+ akawa ndiye mwenye daraka la wokovu+ wa milele kwa wale wote wanaomtii,+ 10 kwa sababu Mungu amemwita jina, kuhani mkuu kwa mfano wa Melkizedeki.+
11 Kumhusu yeye sisi tuna mengi ya kusema na yaliyo magumu kufafanuliwa, kwa kuwa mmekuwa wazito katika kusikia kwenu.+ 12 Kwa maana, kwa kweli, ijapokuwa mnapaswa kuwa walimu+ kwa sababu ya wakati, ninyi mnahitaji tena mtu awafundishe tangu mwanzo mambo ya msingi+ ya maneno matakatifu ya Mungu;+ nanyi mmekuwa kama wanaohitaji maziwa, si chakula kigumu.+ 13 Kwa maana kila mtu anayetumia maziwa hafahamu neno la uadilifu, kwa maana yeye ni mtoto mchanga.+ 14 Lakini chakula kigumu ni cha watu wakomavu, cha wale ambao kwa kutumia, nguvu zao za ufahamu+ zimezoezwa kutofautisha yaliyo sawa na yaliyo makosa pia.+
6 Kwa sababu hiyo, kwa kuwa sasa tumeliacha fundisho la msingi+ juu ya Kristo,+ na tusonge mbele kuelekea ukomavu,+ tusiweke msingi tena,+ yaani, kutubu matendo yaliyokufa,+ na imani kwa Mungu,+ 2 fundisho juu ya mabatizo+ na kuwekewa mikono,+ kufufuliwa kwa wafu+ na hukumu+ ya milele. 3 Na hili tutalifanya, ikiwa kwa kweli Mungu ataruhusu.+
4 Kwa maana haiwezekani kamwe kwa habari ya wale ambao wametiwa nuru+ mara moja kwa wakati wote, na ambao wameonja zawadi ya bure+ ya kimbingu, na ambao wamekuwa washiriki wa roho takatifu,+ 5 na ambao wameonja+ neno zuri la Mungu na nguvu za mfumo wa mambo unaokuja,+ 6 lakini ambao wameanguka,+ kuwarudisha tena kwenye toba,+ kwa sababu wanamtundika upya mtini Mwana wa Mungu kwa ajili yao wenyewe na kumfunua yeye kwenye aibu ya hadharani.+ 7 Kwa mfano, udongo unaokunywa mvua ambayo huja mara nyingi juu yake, na kisha unazaa mimea inayofaa kwa wale ambao huo hulimwa kwa ajili yao,+ hupokea malipo ya baraka kutoka kwa Mungu. 8 Lakini ukizaa miiba na mibaruti, hukataliwa na huwa karibu kulaaniwa;+ nao mwisho wake huchomwa.+
9 Hata hivyo, kwa hali yenu, wapendwa, tunasadiki juu ya mambo yaliyo bora na mambo yanayofuatana na wokovu, ijapokuwa tunasema jinsi hii. 10 Kwa maana Mungu hakosi kuwa mwadilifu hivi kwamba asahau kazi yenu na upendo mlioonyesha kwa ajili ya jina lake,+ kwa kuwa mmewahudumia watakatifu+ nanyi mnaendelea kuhudumu. 11 Lakini tunatamani kila mmoja wenu aonyeshe bidii ileile ili kuwa na uhakikisho kamili+ wa tumaini+ mpaka mwisho,+ 12 ili msiwe goigoi,+ bali muwe waigaji+ wa wale ambao kupitia imani na subira huzirithi ahadi.+
13 Kwa maana Mungu alipoitoa ahadi yake kwa Abrahamu,+ kwa kuwa hangeweza kuapa kwa yeyote aliye mkubwa zaidi, aliapa+ kwa nafsi yake mwenyewe, 14 akisema: “Hakika nitakubariki, nami nitakuzidisha.”+ 15 Na hivyo baada ya Abrahamu kuonyesha subira, aliipata ahadi hiyo.+ 16 Kwa maana watu huapa kwa aliye mkubwa zaidi,+ na kiapo chao ndicho mwisho wa kila bishano, kwa kuwa hicho ni uhakikisho wa kisheria kwao.+ 17 Vivyo hivyo Mungu, alipokusudia kuwaonyesha kwa wingi zaidi warithi+ wa ile ahadi kule kutobadilika+ kwa shauri lake, aliingilia kati kwa kiapo, 18 ili, kupitia mambo mawili yasiyobadilika ambayo katika hayo Mungu hawezi kamwe kusema uwongo,+ sisi ambao tumekimbia kwenda katika kimbilio tupate kuwa na kitia-moyo chenye nguvu kushikilia tumaini+ lililowekwa mbele yetu. 19 Tumaini+ hilo tunalo kama nanga ya nafsi, likiwa hakika na imara, nalo huingia mle ndani ya pazia,+ 20 ambamo mtangulizi ameingia kwa ajili yetu,+ Yesu, ambaye amekuwa kuhani mkuu milele kwa mfano wa Melkizedeki.+
7 Kwa maana Melkizedeki huyu, mfalme wa Salemu, kuhani wa Mungu Aliye Juu Zaidi,+ aliyekutana na Abrahamu akirudi kutoka kuwamaliza wafalme kisha akambariki+ 2 na ambaye Abrahamu alimgawia sehemu ya kumi katika vitu vyote,+ kwanza kabisa, kwa tafsiri, yeye ni “Mfalme wa Uadilifu,” na kisha pia ni mfalme wa Salemu,+ yaani, “Mfalme wa Amani.” 3 Kwa kuwa asiye na baba, asiye na mama, bila ukoo, akiwa hana mwanzo wa siku+ wala mwisho wa uzima, bali akiwa amefanywa kama Mwana wa Mungu,+ anadumu akiwa kuhani daima.+
4 Oneni, basi, jinsi alivyokuwa mkuu mtu huyu ambaye Abrahamu, yule kichwa cha familia, alimtolea sehemu ya kumi kutokana na zile nyara kuu.+ 5 Ni kweli, watu kutoka katika wana wa Lawi+ ambao hupokea cheo chao cha ukuhani wana amri ya kukusanya sehemu za kumi+ kutoka kwa watu+ kulingana na Sheria, yaani, kutoka kwa ndugu zao, hata kama hao wametoka katika viuno vya Abrahamu;+ 6 lakini mtu ambaye ukoo+ wake haukutokana nao alichukua sehemu za kumi kutoka kwa Abrahamu+ na kumbariki yeye ambaye alikuwa na zile ahadi.+ 7 Basi bila mabishano, mdogo hubarikiwa na mkubwa.+ 8 Na katika hali ile moja watu wanaokufa ndio hupokea sehemu za kumi,+ lakini katika hali ile nyingine ni mtu ambaye imeshuhudiwa kwamba anaishi.+ 9 Na, nikitumia neno hili, kupitia Abrahamu hata Lawi ambaye hupokea sehemu za kumi amelipa sehemu za kumi, 10 kwa maana alikuwa bado katika viuno+ vya babu yake wakati Melkizedeki alipokutana naye.+
11 Basi, kama kwa kweli ukamilifu+ ungekuwa ni kupitia ukuhani wa Walawi,+ (kwa maana huo ukiwa sehemu kuu watu walipewa Sheria,)+ kungekuwa na uhitaji gani zaidi+ wa kuhani mwingine kusimama kwa mfano wa Melkizedeki+ na asisemwe kuwa kwa mfano wa Haruni? 12 Maana kwa kuwa ukuhani unabadilishwa,+ basi kunakuja kuwa na uhitaji wa kubadilishwa kwa sheria+ pia. 13 Kwa maana yule mtu ambaye mambo haya yanasemwa kumhusu amekuwa ni mshiriki wa kabila+ lingine, ambalo kutoka kwake hakuna yeyote ambaye ametumikia rasmi kwenye madhabahu.+ 14 Kwa maana ni wazi kabisa kwamba Bwana wetu ametokana na Yuda,+ kabila ambalo Musa hakusema lolote juu yake kuhusiana na makuhani.
15 Na bado ni wazi zaidi kwamba kwa mfano wa Melkizedeki+ anasimama kuhani+ mwingine, 16 ambaye amekuwa hivyo, si kulingana na sheria ya amri inayotegemea mwili,+ bali kulingana na nguvu za uzima usioweza kuharibika,+ 17 kwa maana katika kutoa ushahidi imesemwa: “Wewe ni kuhani milele kwa mfano wa Melkizedeki.”+
18 Hakika, basi, ile amri iliyotangulia inawekwa kando kwa sababu ya udhaifu+ wake na kutofaa+ kwake. 19 Kwa maana Sheria haikufanya kitu chochote kuwa kikamilifu,+ lakini kuingizwa kwa tumaini+ bora kulifanya mambo yawe makamilifu, ambalo kupitia hilo tunamkaribia Mungu.+ 20 Pia, kwa kadiri ambayo haikuwa bila kiapo rasmi, 21 (kwa maana kwa kweli kuna watu ambao wamekuwa makuhani bila kiapo rasmi, lakini kuna mmoja mwenye kiapo rasmi kupitia Yule aliyesema hivi kumhusu: “Yehova ameapa+ (naye hatajuta), ‘Wewe ni kuhani milele,’ ”)+ 22 kwa kadiri hiyo pia Yesu amekuwa yule aliyetolewa kuwa rehani ya agano bora.+ 23 Zaidi ya hayo, ilikuwa lazima wengi wawe makuhani kwa mfuatano+ kwa sababu ya kuzuiwa na kifo+ wasiendelee kuwa hivyo, 24 lakini yeye kwa sababu ya kuendelea kuwa hai milele+ ana ukuhani wake bila kuwa na waandamizi wowote. 25 Kwa hiyo yeye anaweza pia kuwaokoa kwa ukamili wale wanaomkaribia Mungu kupitia yeye, kwa sababu yeye yuko hai sikuzote ili kuwaombea.+
26 Kwa maana kuhani mkuu wa namna hiyo alitufaa sisi,+ mshikamanifu,+ asiye na hila,+ asiye na unajisi,+ aliyetengwa kutoka kwa watenda-dhambi,+ na kuwa juu zaidi kuliko mbingu.+ 27 Yeye hahitaji kila siku,+ kama wale makuhani wakuu wanavyofanya, kutoa dhabihu, kwanza kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe+ kisha kwa ajili ya zile za watu:+ (kwa maana yeye alifanya hilo mara moja+ kwa wakati wote alipojitoa+ mwenyewe;) 28 kwa maana Sheria huweka rasmi kuwa makuhani wakuu+ watu walio na udhaifu,+ lakini neno la kiapo+ rasmi lililokuja baada ya Sheria humweka rasmi Mwana, ambaye amekamilishwa+ milele.
8 Basi kuhusu mambo yanayozungumzwa jambo kuu ni hili: Sisi tuna kuhani mkuu+ wa namna hii, naye ameketi kwenye mkono wa kuume wa kiti cha ufalme cha Ukuu mbinguni,+ 2 mtumishi wa watu wote wa mahali patakatifu+ na wa hema la kweli, ambalo Yehova+ alisimamisha, na si mwanadamu.+ 3 Kwa maana kila kuhani mkuu huwekwa rasmi ili kutoa zawadi na dhabihu;+ kwa hiyo ilikuwa lazima pia kwa huyu kuwa na kitu fulani cha kutoa.+ 4 Sasa, kama angekuwa duniani, hangekuwa kuhani,+ kukiwa na watu ambao hutoa zawadi kulingana na Sheria, 5 lakini watu ambao wanatoa utumishi mtakatifu katika mfano wa uhalisi+ na kivuli+ cha vitu vya mbinguni; kama vile Musa, alipokuwa karibu kumaliza hema,+ alipewa amri ya kimungu:+ Kwa maana yeye anasema: “Uhakikishe kwamba umevifanya vitu vyote kulingana na mfano wake ambao wewe ulionyeshwa mlimani.”+ 6 Lakini sasa Yesu amepata utumishi wa watu wote ulio bora zaidi, hivi kwamba yeye pia ni mpatanishi+ wa agano lililo bora kwa kulinganishwa,+ ambalo limefanywa imara kisheria juu ya ahadi zilizo bora.+
7 Kwa maana ikiwa agano lile la kwanza lingekuwa bila kosa, mahali hapangetafutwa kwa ajili ya la pili;+ 8 kwa maana yeye anawalaumu wale watu anaposema: “ ‘Tazama! Siku zinakuja,’ asema Yehova, ‘nami nitafanya agano jipya pamoja na nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda;+ 9 si kulingana na lile agano+ ambalo nilifanya pamoja na mababu zao katika ile siku nilipowashika mkono na kuwatoa katika nchi ya Misri,+ kwa sababu hawakuendelea kulishika agano langu,+ hivi kwamba nikaacha kuwajali,’ asema Yehova.”+
10 “ ‘Kwa maana hili ndilo agano nitakalofanya pamoja na nyumba ya Israeli baada ya siku hizo,’ asema Yehova. ‘Nitazitia sheria zangu katika akili yao, nami nitaziandika katika mioyo yao.+ Nami nitakuwa Mungu wao,+ nao watakuwa watu wangu.+
11 “ ‘Nao hawatafundishana kwa vyovyote kila mtu na raia mwenzake wala kila mtu na ndugu yake, wakisema: “Mjue Yehova!”+ Kwa maana wote watanijua mimi,+ kuanzia yule aliye mdogo zaidi mpaka yule aliye mkubwa zaidi kati yao. 12 Kwa maana nitaonyesha rehema kwa matendo yao yasiyo ya uadilifu, nami sitazikumbuka+ tena dhambi+ zao hata kidogo.’ ”
13 Kwa kusema “agano jipya,” Yeye amelifanya lile la zamani kuchakaa.+ Basi kile kinachofanywa kuchakaa na kuzeeka kiko karibu kutoweka.+
9 Basi, kwa upande wake, lile agano la zamani lilikuwa na maagizo ya utumishi mtakatifu+ na mahali pake patakatifu pa kidunia.+ 2 Kwa maana kilijengwa chumba cha hema cha kwanza+ ambacho ndani yake mlikuwa kile kinara cha taa+ na pia meza+ na wonyesho wa mikate;+ nacho kinaitwa “Mahali Patakatifu.”+ 3 Lakini nyuma ya pazia+ la pili kulikuwa na chumba cha hema kilichoitwa “Patakatifu Zaidi.”+ 4 Hicho kilikuwa na chetezo+ cha dhahabu na sanduku la agano+ likiwa limefunikwa kuzunguka pande zote kwa dhahabu,+ ambalo ndani yake mlikuwa na mtungi wa dhahabu wenye mana+ na ile fimbo ya Haruni iliyochipuka+ na yale mabamba+ ya agano; 5 lakini upande wake wa juu palikuwa na wale makerubi+ wenye utukufu waliokifunika kile kifuniko cha upatanisho.+ Lakini sasa si wakati wa kusema kirefu habari za vitu hivyo.
6 Baada ya vitu hivyo kujengwa kwa njia hiyo, makuhani huingia katika chumba cha kwanza cha hema+ nyakati zote ili kutoa utumishi mtakatifu;+ 7 lakini ndani ya chumba cha pili kuhani mkuu peke yake huingia mara moja kwa mwaka,+ wala si bila damu,+ ambayo yeye huitoa kwa ajili yake mwenyewe+ na kwa ajili ya dhambi za hali ya watu+ ya kutojua. 8 Hivyo roho takatifu hufanya iwe wazi kwamba njia+ ya kuingia ndani ya mahali patakatifu ilikuwa bado haijafunuliwa wakati lile hema la zamani lilipokuwa limesimama.+ 9 Hema hili ni mfano+ kwa ajili ya wakati uliowekwa ambao upo sasa,+ na kwa kupatana nalo zawadi na dhabihu pia zinatolewa.+ Hata hivyo, hizo haziwezi kumfanya mtu anayetoa utumishi mtakatifu awe mkamilifu+ kuhusiana na dhamiri+ yake, 10 bali zinahusu tu vyakula+ na vinywaji+ na mabatizo+ mbalimbali. Hayo yalikuwa matakwa ya kisheria yanayohusiana na mwili+ nayo yaliamriwa mpaka wakati uliowekwa wa kunyoosha mambo.+
11 Hata hivyo, Kristo alipokuja akiwa kuhani mkuu+ wa mambo mema ambayo yamekwisha kuwa, kupitia hema kubwa zaidi na kamilifu zaidi ambalo halikufanywa kwa mikono, yaani, si la uumbaji huu,+ 12 aliingia, si kwa damu ya mbuzi na ya ng’ombe-dume wachanga,+ bali kwa damu yake mwenyewe,+ mara moja kwa wakati wote ndani ya mahali patakatifu na kupata ukombozi wa milele kwa ajili yetu.+ 13 Kwa maana ikiwa damu ya mbuzi+ na ya ng’ombe-dume+ na majivu+ ya ndama-jike yaliyonyunyizwa juu ya wale ambao wametiwa unajisi+ hutakasa kufikia usafi wa mwili,+ 14 je, si zaidi damu+ ya Kristo, ambaye kupitia roho inayodumu milele alijitoa+ mwenyewe bila dosari kwa Mungu, itazisafisha+ dhamiri zetu kutoka katika matendo yaliyokufa+ ili tutoe utumishi mtakatifu+ kwa Mungu aliye hai?
15 Basi ndiyo sababu yeye ni mpatanishi+ wa agano jipya, ili, kwa sababu kifo kimetokea kwa ajili ya wao kuachiliwa huru kwa fidia+ kutoka kwenye makosa chini ya lile agano la zamani,+ wale ambao wameitwa waipokee ahadi ya urithi unaodumu milele.+ 16 Kwa maana mahali palipo na agano,+ kifo cha yule mwanadamu mwenye kufanya agano kinahitaji kuandaliwa. 17 Kwa maana agano ni halali juu ya watu wafu, kwa kuwa halitendi wakati yule mwanadamu mwenye kufanya agano akiwa hai. 18 Kwa hiyo lile agano la zamani+ halikuzinduliwa bila damu.+ 19 Kwa maana wakati kila amri kulingana na Sheria ilipokuwa imesemwa na Musa kwa watu wote,+ alichukua damu ya wale ng’ombe-dume wachanga na ya wale mbuzi pamoja na maji na sufu nyekundu na hisopo+ na kukinyunyizia kile kitabu na watu wote, 20 akisema: “Hii ndiyo damu ya agano ambalo Mungu ameweka kuwa amri juu yenu.”+ 21 Naye alilinyunyizia lile hema+ na vyombo vyote vya utumishi wa watu wote vivyo hivyo kwa damu.+ 22 Ndiyo, karibu vitu vyote husafishwa kwa damu+ kulingana na Sheria, na damu isipomwagwa+ hakuna msamaha unaotokea.+
23 Kwa hiyo ilikuwa lazima kwamba mifano+ ya uhalisi wa vitu vilivyo mbinguni isafishwe kwa njia hizo,+ lakini vitu vya mbinguni vyenyewe visafishwe kwa dhabihu zilizo bora kuliko dhabihu za namna hiyo. 24 Kwa maana Kristo hakuingia mahali patakatifu palipofanywa kwa mikono,+ ambapo ni mfano wa uhalisi,+ bali aliingia mbinguni kwenyewe,+ ili sasa aonekane mbele za uso wa Mungu kwa ajili yetu.+ 25 Wala si ili ajitoe mwenyewe mara nyingi, kama vile kuhani mkuu anavyoingia mahali patakatifu+ mwaka baada ya mwaka+ akiwa na damu isiyo yake mwenyewe. 26 Kama sivyo, ingekuwa lazima ateseke mara nyingi tangu kuwekwa msingi+ wa ulimwengu. Lakini sasa amejifunua+ mara moja+ kwa wakati wote kwenye umalizio wa mifumo ya mambo+ ili kuondolea mbali dhambi kupitia dhabihu yake mwenyewe.+ 27 Na kama vile watu wamewekewa akiba+ kufa mara moja kwa wakati wote, lakini baada ya hilo ni hukumu,+ 28 vivyo hivyo pia Kristo alitolewa+ mara moja kwa wakati wote ili kubeba dhambi za wengi;+ na mara ya pili+ atakapotokea+ itakuwa ni bila dhambi+ na kwa wale wanaomtazamia kwa bidii kwa ajili ya wokovu wao.+
10 Kwa kuwa Sheria ina kivuli+ cha mambo mema yatakayokuja, lakini si umbo halisi la mambo hayo, watu hawawezi kamwe kuwafanya wale wanaokaribia kuwa wakamilifu+ kwa dhabihu zilezile mwaka baada ya mwaka ambazo wao huendelea kuzitoa. 2 Kama sivyo, je, dhabihu hazingekoma kutolewa, kwa sababu wale wanaotoa utumishi mtakatifu ambao walikuwa wamesafishwa mara moja kwa wakati wote hawangekuwa na ufahamu wa dhambi tena?+ 3 Kinyume cha hilo, kwa dhabihu hizo kuna kukumbusha juu ya dhambi mwaka baada ya mwaka,+ 4 kwa maana haiwezekani damu ya ng’ombe na ya mbuzi kuondolea mbali dhambi.+
5 Kwa hiyo wakati yeye anapokuja katika ulimwengu anasema: “ ‘Dhabihu na toleo wewe hukutaka,+ bali ulinitayarishia mwili.+ 6 Hukukubali matoleo mazima ya kuteketezwa na toleo la dhambi.’+ 7 Ndipo nikasema, ‘Tazama! Nimekuja (katika kitabu cha kukunjwa imeandikwa juu yangu)+ ili kufanya mapenzi yako, Ee Mungu.’ ”+ 8 Baada ya kwanza kusema: “Hukutaka wala hukukubali dhabihu na matoleo na matoleo mazima ya kuteketezwa na toleo la dhambi”+—dhabihu zinazotolewa kulingana na Sheria+— 9 ndipo anasema: “Tazama! nimekuja kufanya mapenzi yako.”+ Anaondolea mbali lile la kwanza ili asimamishe lile la pili.+ 10 Kwa hayo “mapenzi”+ yaliyosemwa sisi tumetakaswa+ kupitia toleo+ la mwili wa Yesu Kristo+ mara moja kwa wakati wote.
11 Pia, kila kuhani husimama mahali pake+ siku baada ya siku+ ili kutoa utumishi wa watu wote na kutoa dhabihu zilezile mara nyingi, kwa kuwa hizo haziwezi kamwe kuondoa kabisa dhambi.+ 12 Lakini mtu huyu alitoa dhabihu moja kwa ajili ya dhambi daima+ na kuketi kwenye mkono wa kuume wa Mungu,+ 13 tangu wakati huo na kuendelea akingojea mpaka adui zake wawekwe kuwa kiti cha miguu yake.+ 14 Kwa maana ni kwa toleo moja la dhabihu+ kwamba yeye amewafanya wale wanaotakaswa wawe wakamilifu+ daima. 15 Zaidi ya hayo, roho takatifu+ pia inatutolea ushahidi, kwa maana baada ya kusema: 16 “ ‘Hili ndilo agano nitakalofanya kwao baada ya siku hizo,’ asema Yehova. ‘Nitazitia sheria zangu katika mioyo yao, nami nitaziandika katika akili zao,’ ”+ 17 inasema baadaye: “Nami sitazikumbuka tena dhambi zao hata kidogo na matendo yao ya kuasi sheria.”+ 18 Sasa mahali palipo na msamaha+ wa mambo hayo, hapana tena toleo kwa ajili ya dhambi.+
19 Kwa hiyo, akina ndugu, kwa kuwa tuna ujasiri wa njia ya kuingia+ katika mahali patakatifu+ kwa damu ya Yesu, 20 aliyotuzindulia kuwa njia mpya na yenye uzima kupitia lile pazia,+ yaani, mwili wake,+ 21 na kwa kuwa tuna kuhani mkuu juu ya nyumba ya Mungu,+ 22 acheni tukaribie tukiwa na mioyo ya kweli katika uhakikisho kamili wa imani, mioyo yetu ikiisha kunyunyizwa kutokana na dhamiri+ ya uovu na miili yetu kuoshwa kwa maji safi.+ 23 Acheni tushike imara tangazo la hadharani la tumaini+ letu bila kuyumba-yumba,+ kwa maana yeye aliyeahidi ni mwaminifu.+ 24 Na acheni tufikiriane ili kuchocheana+ katika upendo na matendo mazuri,+ 25 bila kuacha kukusanyika pamoja sisi wenyewe,+ kama vile wengine walivyo na desturi, bali tutiane moyo,+ na kufanya hivyo zaidi kwa kadiri mnavyoona siku ile kuwa inakaribia.+
26 Kwa maana tukizoea kutenda dhambi kimakusudi+ baada ya kupokea ujuzi sahihi juu ya kweli,+ hakuna tena dhabihu yoyote iliyobaki kwa ajili ya dhambi,+ 27 lakini kuna tarajio hakika lenye kuogopesha la hukumu+ na kuna wivu unaowaka moto ambao utawateketeza wale wanaopinga.+ 28 Mtu yeyote ambaye ameipuuza sheria ya Musa hufa bila huruma, kwa ushuhuda wa watu wawili au watatu.+ 29 Je, mnafikiri atahesabiwa kuwa anastahili adhabu kali zaidi namna gani,+ mtu ambaye amemkanyagia chini+ Mwana wa Mungu na ambaye ameiona kuwa yenye thamani ya kawaida tu damu+ ya agano ambayo kupitia hiyo alitakaswa, na ambaye ameitendea kwa dharau ile roho+ ya fadhili zisizostahiliwa? 30 Kwa maana tunamjua yeye aliyesema: “Kisasi ni changu; mimi nitalipa”;+ na tena: “Yehova atawahukumu watu wake.”+ 31 Ni jambo lenye kuogopesha kuanguka mikononi mwa Mungu aliye hai.+
32 Hata hivyo, endeleeni kuzikumbuka zile siku za zamani ambazo, baada ya kutiwa nuru,+ mlivumilia shindano kubwa chini ya mateso,+ 33 nyakati fulani mkifunuliwa wazi kama katika jumba la maonyesho+ kwenye shutuma na dhiki pia, na nyakati fulani mlipokuwa washiriki pamoja na wale waliokuwa wakipatwa na jambo la namna hiyo.+ 34 Kwa maana mliwasikitikia wale waliokuwa gerezani na pia kwa shangwe mkavumilia kuporwa+ mali zenu, mkijua ninyi wenyewe mna miliki bora na yenye kudumu.+
35 Kwa hiyo, msiutupilie mbali uhuru wenu wa kusema,+ ulio na thawabu+ kubwa ya kulipwa. 36 Kwa maana mnahitaji kuwa na uvumilivu,+ ili kwamba, baada ya kufanya mapenzi ya Mungu,+ mpokee utimizo wa ile ahadi.+ 37 Kwa maana bado “muda kidogo sana,”+ na “yeye anayekuja atafika naye hatakawia.”+ 38 “Lakini mwadilifu wangu ataishi kwa sababu ya imani,”+ na, “akirudi nyuma kwa kutetemeka, nafsi yangu haipendezwi naye.”+ 39 Sasa sisi si namna ya watu wanaorudi nyuma kwenye maangamizi,+ bali sisi ni namna ya watu walio na imani ya kuihifadhi hai nafsi.+
11 Imani+ ni tarajio lililohakikishwa la mambo yanayotumainiwa,+ uthibitisho ulio wazi wa mambo halisi ingawa hayaonekani.+ 2 Kwa maana kwa njia ya imani hiyo watu wa nyakati za zamani walitolewa ushahidi.+
3 Kwa imani tunatambua kwamba mifumo ya mambo+ ilipangwa kwa utaratibu kwa neno la Mungu,+ hivi kwamba kile kinachoonekana kimekuja kutokana na vitu visivyoonekana.+
4 Kwa imani Abeli alimtolea Mungu dhabihu ya thamani kubwa zaidi kuliko Kaini,+ imani ambayo kupitia hiyo alitolewa ushahidi kwamba yeye alikuwa mwadilifu, Mungu akitoa ushahidi+ kuhusu zawadi zake; na kupitia hiyo yeye, ijapokuwa alikufa, bado anasema.+
5 Kwa imani Enoko+ alihamishwa ili asione kifo, naye hakupatikana popote kwa sababu Mungu alikuwa amemhamisha;+ kwa maana kabla ya kuhamishwa kwake alikuwa ametolewa ushahidi kwamba amempendeza Mungu vema.+ 6 Zaidi ya hayo, bila imani+ haiwezekani kamwe kumpendeza vema,+ kwa maana yule anayemkaribia Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko+ na kwamba yeye huwa mthawabishaji+ wa wale wanaomtafuta kwa bidii.+
7 Kwa imani Noa,+ baada ya kupewa onyo la kimungu la mambo ambayo yalikuwa bado hayajaonekana,+ alionyesha woga wa kimungu na kujenga safina+ kwa ajili ya kuiokoa nyumba yake; na kupitia imani hiyo aliuhukumu ulimwengu+ kuwa wenye hatia, naye akawa mrithi wa uadilifu+ unaolingana na imani.
8 Kwa imani Abrahamu,+ alipoitwa, alitii kwa kutoka akaenda na kuingia mahali alipokusudiwa kupokea kuwa urithi; naye akatoka, ijapokuwa hakujua mahali alipokuwa akienda.+ 9 Kwa imani alikaa kama mgeni katika nchi ya ahadi kama katika nchi ya ugenini,+ akakaa katika mahema+ pamoja na Isaka+ na Yakobo,+ warithi pamoja naye wa ahadi ileile.+ 10 Kwa maana alikuwa akingojea jiji+ lililo na misingi ya kweli, ambalo mjenzi na mtengenezaji wa jiji hilo ni Mungu.+
11 Kwa imani Sara+ mwenyewe pia alipokea nguvu ili kuchukua mimba ya uzao, hata alipokuwa amepita mpaka wa umri,+ kwa kuwa alimwona kuwa mwaminifu yeye aliyekuwa ameahidi.+ 12 Kwa sababu hiyo pia kutoka kwa mwanamume mmoja,+ naye akiwa kana kwamba ni mfu,+ kulizaliwa watoto kama vile nyota za mbinguni kwa wingi na kama mchanga ulio kando ya bahari, usiohesabika.+
13 Katika imani hawa wote walikufa,+ ijapokuwa hawakupata utimizo wa zile ahadi,+ bali waliziona kwa mbali+ na kuzikaribisha na kutangaza hadharani kwamba wao ni wageni na wakaaji wa muda katika nchi.+ 14 Kwa maana wale wanaosema mambo ya namna hiyo hutoa uthibitisho wa kwamba wanatafuta kwa bidii mahali pao wenyewe.+ 15 Na bado, kama kwa kweli wangeendelea kukumbuka mahali pale walipokuwa wametoka,+ wangepata nafasi ya kurudi.+ 16 Lakini sasa wanajitahidi kufikia mahali palipo bora, yaani, panapohusiana na mbinguni.+ Kwa hiyo Mungu haoni aibu juu yao, kuitwa akiwa Mungu wao,+ kwa maana ametayarisha jiji+ kwa ajili yao.
17 Kwa imani Abrahamu, alipojaribiwa,+ ni kana kwamba alimtoa Isaka, na huyo mtu aliyekuwa amezipokea ahadi kwa furaha alijaribu kumtoa mwana wake mzaliwa-pekee,+ 18 ijapokuwa alikuwa ameambiwa: “Ule utakaoitwa ‘uzao wako’ utakuwa kupitia Isaka.”+ 19 Lakini alifikia uamuzi kwamba Mungu alikuwa na uwezo wa kumfufua hata kutoka kwa wafu;+ na kutoka huko alimpokea pia kwa njia ya mfano.+
20 Kwa imani pia Isaka alimbariki Yakobo+ na Esau+ kuhusu mambo yatakayokuja.
21 Kwa imani Yakobo, alipokuwa karibu kufa,+ aliwabariki kila mmoja wa wana wa Yosefu+ na kuabudu akiegemea juu ya fimbo yake.+
22 Kwa imani Yosefu, akikaribia mwisho wake, alitaja kuhusu kule kutoka+ kwa wana wa Israeli; naye akatoa amri kuhusu mifupa yake.+
23 Kwa imani Musa alifichwa kwa miezi mitatu na wazazi wake baada ya kuzaliwa kwake,+ kwa sababu waliona kwamba huyo mtoto mchanga alikuwa mwenye kupendeza+ nao hawakuliogopa agizo+ la mfalme. 24 Kwa imani Musa, alipokuwa mtu mzima,+ alikataa kuitwa mwana wa binti ya Farao,+ 25 akachagua kutendewa vibaya pamoja na watu wa Mungu badala ya kufurahia dhambi kwa muda, 26 kwa sababu aliona shutuma ya Kristo+ kuwa ni utajiri mkubwa kuliko hazina za Misri; kwa maana alikaza macho kwenye malipo ya thawabu.+ 27 Kwa imani aliondoka Misri,+ lakini bila kuogopa hasira ya mfalme,+ kwa maana aliendelea kuwa imara kama mtu anayemwona Yeye asiyeonekana.+ 28 Kwa imani alifanya sherehe ya pasaka+ na upakaji wa damu,+ ili mwangamizaji asiwaguse wazaliwa wao wa kwanza.+
29 Kwa imani walipita katikati ya Bahari Nyekundu kana kwamba ni juu ya nchi kavu,+ lakini Wamisri walipothubutu kuipitia wakamezwa.+
30 Kwa imani kuta za Yeriko zilianguka chini baada ya kuzungukwa kwa siku saba.+ 31 Kwa imani Rahabu+ yule kahaba hakuangamia pamoja na wale waliotenda kwa kutotii, kwa sababu aliwapokea wale wapelelezi kwa njia ya amani.+
32 Nami nitasema nini zaidi? Kwa maana nitakosa wakati nikiendelea kusimulia juu ya Gideoni,+ Baraka,+ Samsoni,+ Yeftha,+ Daudi+ na vilevile Samweli+ na wale manabii wengine,+ 33 ambao kupitia imani walishinda falme katika mapambano,+ wakatenda uadilifu,+ wakapata ahadi,+ wakaziba vinywa vya simba,+ 34 wakazuia nguvu za moto,+ wakaponyoka makali ya upanga,+ kutoka hali ya udhaifu wakafanywa kuwa wenye nguvu,+ wakawa mashujaa katika vita,+ wakayashinda kabisa majeshi ya wageni.+ 35 Wanawake waliwapokea wafu wao kwa ufufuo;+ lakini watu wengine waliteswa kwa sababu hawakukubali kuachiliwa huru kupitia fidia fulani, ili waupate ufufuo ulio bora. 36 Ndiyo, wengine walipata jaribu lao kwa dhihaka na mapigo kwa mijeledi, kwa kweli, zaidi ya hayo, kwa vifungo+ na magereza.+ 37 Walipigwa kwa mawe,+ walijaribiwa,+ walikatwa vipande-vipande kwa msumeno, walikufa+ kwa kuuawa kwa upanga, walitembea huku na huku wakiwa wamevikwa ngozi za kondoo,+ wakiwa wamevikwa ngozi za mbuzi, wakiwa katika uhitaji,+ katika dhiki,+ wakitendewa vibaya;+ 38 na ulimwengu haukuwafaa. Walitembea huku na huku katika majangwa na milima na mapango+ na mashimo ya dunia.
39 Na bado hawa wote, ijapokuwa walitolewa ushahidi kupitia imani yao, hawakupata utimizo wa ile ahadi,+ 40 kwa kuwa Mungu aliona kimbele kitu bora+ kwa ajili yetu sisi,+ ili wasifanywe+ kuwa wakamilifu+ bila sisi.+
12 Kwa hiyo, basi, kwa sababu tuna wingu kubwa hivyo la mashahidi+ linalotuzunguka, acheni sisi pia tuondoe kila uzito+ na dhambi ambayo hututatanisha kwa urahisi,+ na acheni tukimbie kwa uvumilivu+ shindano la mbio+ lililowekwa mbele yetu,+ 2 huku tukimtazama kwa makini Wakili Mkuu+ na Mkamilishaji wa imani yetu,+ Yesu. Kwa ajili ya shangwe iliyowekwa mbele yake, yeye alivumilia+ mti wa mateso, akaidharau aibu, naye ameketi kwenye mkono wa kuume wa kiti cha ufalme cha Mungu.+ 3 Kwa kweli, mfikirieni sana yeye ambaye amevumilia maneno ya aina hii yenye kupinga+ yanayotolewa na watenda-dhambi kinyume cha faida zao wenyewe, ili ninyi msichoke na kuzimia katika nafsi zenu.+
4 Katika shindano lenu na dhambi ile bado hamjapinga kamwe mpaka kufikia damu,+ 5 bali mmesahau kabisa lile himizo ambalo linasema nanyi kama wana:+ “Mwanangu, usiipuuze nidhamu kutoka kwa Yehova, wala usizimie wakati anapokurekebisha;+ 6 kwa maana yeye ambaye Yehova anampenda, humtia nidhamu; kwa kweli, humpiga fimbo kila mtu ambaye yeye humpokea kuwa mwana.”+
7 Ninyi mnavumilia kwa ajili ya nidhamu.+ Mungu anawatendea ninyi kama wana.+ Kwa maana ni mwana gani ambaye baba hamtii nidhamu?+ 8 Lakini ikiwa ninyi hamna nidhamu ambayo wote wameishiriki, kwa kweli ninyi ni watoto haramu,+ wala si wana. 9 Zaidi ya hayo, tulikuwa na baba zetu wa mwili waliokuwa wakitutia nidhamu,+ nasi tulikuwa tukiwapa heshima. Kwa nini tusijitiishe zaidi kwa Baba wa maisha yetu ya kiroho na kuishi?+ 10 Kwa maana wao kwa siku chache walikuwa wakitutia nidhamu kulingana na yaliyoonekana kuwa mema kwao,+ lakini yeye hufanya hivyo kwa faida yetu ili tuushiriki utakatifu wake.+ 11 Ni kweli, hakuna nidhamu inayoonekana kwa sasa kuwa yenye shangwe, bali ni yenye kuhuzunisha;+ lakini baadaye kwa wale ambao wamezoezwa nayo hiyo huzaa tunda lenye kufanya amani,+ yaani, uadilifu.+
12 Kwa hiyo inyoosheni mikono inayolegea+ na magoti yaliyo dhaifu,+ 13 nanyi endeleeni kuifanyia miguu+ yenu mapito yaliyonyooka, ili kile ambacho ni kilemavu kisiteguliwe, bali afadhali kiponywe.+ 14 Fuatilieni amani pamoja na watu wote,+ na utakaso+ ambao bila huo hakuna mtu atakayemwona Bwana,+ 15 mkiwa waangalifu kwamba yeyote asinyimwe fadhili zisizostahiliwa za Mungu;+ kwamba mzizi wowote wenye sumu+ usichipuke na kusababisha taabu na kwamba wengi wasitiwe unajisi na huo;+ 16 kwamba kusiwe na mwasherati wala yeyote asiyethamini mambo matakatifu, kama Esau,+ ambaye alitoa haki zake za kuwa mzaliwa wa kwanza kwa kubadilishana na mlo mmoja.+ 17 Kwa maana mnajua kwamba baadaye pia alipotaka kuirithi baraka+ alikataliwa,+ kwa maana, ijapokuwa alitafuta kwa bidii badiliko la akili kwa machozi,+ hakupata nafasi kwa ajili ya jambo hilo.+
18 Kwa maana ninyi hamkukaribia kile kinachoweza kuguswa+ na ambacho kimewashwa kwa moto,+ na wingu jeusi na giza zito na tufani,+ 19 na mlio wa tarumbeta+ na sauti ya maneno;+ sauti ambayo watu walipoisikia waliomba kwamba wasiongezewe neno lolote.+ 20 Kwa maana hawakuweza kuivumilia amri hii: “Na mnyama akiugusa mlima, lazima apigwe kwa mawe.”+ 21 Pia, ule wonyesho ulikuwa wenye kuogopesha sana hivi kwamba Musa akasema: “Nimejawa na woga nami ninatetemeka.”+ 22 Lakini ninyi mmeukaribia Mlima Sayuni+ na jiji+ la Mungu aliye hai, Yerusalemu la mbinguni,+ na makumi ya maelfu ya malaika,+ 23 katika kusanyiko kuu,+ na kutaniko la wazaliwa wa kwanza+ ambao wameandikishwa+ mbinguni, na Mungu Mwamuzi wa wote,+ na maisha ya kiroho+ ya waadilifu ambao wamefanywa wakamilifu,+ 24 na Yesu mpatanishi+ wa agano jipya,+ na damu ya kunyunyiza,+ ambayo husema kwa njia bora zaidi kuliko ile damu ya Abeli.+
25 Angalieni kwamba msimkatae yeye anayesema.+ Kwa maana ikiwa hawakuponyoka, wale waliomkataa yeye aliyekuwa akitoa onyo la kimungu duniani,+ sisi hatutaponyoka hata kidogo tukigeukia mbali kutoka kwake yeye anayesema kutoka mbinguni.+ 26 Wakati huo sauti yake iliitikisa dunia,+ lakini sasa ameahidi, akisema: “Bado mara moja tena nitaitikisa, si dunia peke yake, bali pia na mbingu.”+ 27 Sasa maneno “Bado mara moja tena” yanatoa ishara ya kuondolewa kwa vitu vinavyotikiswa kuwa vitu ambavyo vimefanywa,+ ili vitu ambavyo havitikiswi vibaki.+ 28 Kwa hiyo, kwa kuwa tutapokea ufalme ambao hauwezi kutikiswa,+ acheni tuendelee kuwa na fadhili zisizostahiliwa, ambazo kupitia hizo tunaweza kumtolea Mungu kwa njia inayokubalika utumishi mtakatifu kwa woga wa kimungu na heshima.+ 29 Kwa maana Mungu wetu pia ni moto unaoteketeza.+
13 Upendo wenu wa kindugu na uendelee.+ 2 Msisahau ukaribishaji-wageni,+ kwa maana kupitia huo watu wengine, bila wao wenyewe kujua, waliwakaribisha malaika.+ 3 Wakumbukeni wale walio katika vifungo vya gereza+ kana kwamba ninyi mmefungwa pamoja nao,+ na wale wanaotendewa vibaya,+ kwa kuwa ninyi wenyewe pia bado mko katika mwili. 4 Ndoa na iheshimiwe kati ya wote, na kitanda cha ndoa kiwe bila unajisi,+ kwa maana Mungu atawahukumu waasherati na wazinzi.+ 5 Namna yenu ya maisha iwe bila upendo wa pesa,+ huku mkiridhika+ na vitu vya sasa.+ Kwa maana yeye amesema: “Sitakuacha wala kukutupa hata kidogo.”+ 6 Hivi kwamba tuwe hodari+ na kusema: “Yehova ni msaidizi wangu; sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?”+
7 Wakumbukeni wale ambao wanaongoza katikati yenu,+ ambao wamelisema neno la Mungu kwenu, nanyi mnapotafakari jinsi mwisho wa mwenendo wao unavyokuwa, igeni+ imani yao.+
8 Yesu Kristo ni yuleyule jana na leo, na milele.+
9 Msichukuliwe mbali na mafundisho mbalimbali na yaliyo mageni;+ kwa maana ni vizuri moyo upewe uthabiti kwa fadhili zisizostahiliwa,+ si kwa vyakula,+ ambavyo wale wanaojishughulisha navyo hawajapata faida.
10 Sisi tuna madhabahu ambayo wale wanaofanya utumishi mtakatifu katika hema hawana mamlaka ya kula kutokana nayo.+ 11 Kwa maana miili ya wale wanyama ambao kuhani mkuu hupeleka damu yao ndani ya mahali patakatifu kwa ajili ya dhambi huteketezwa nje ya kambi.+ 12 Kwa hiyo Yesu pia, ili apate kuwatakasa+ watu kwa damu+ yake mwenyewe, aliteseka nje ya lango.+ 13 Basi, acheni sisi twende kwake nje ya kambi, tukiichukua shutuma aliyoibeba,+ 14 kwa maana sisi hatuna hapa jiji linaloendelea kuwako,+ bali tunatafuta kwa bidii lile litakalokuja.+ 15 Kupitia yeye sikuzote na tumtolee Mungu dhabihu ya sifa,+ yaani, tunda la midomo+ ambayo hulifanyia jina lake tangazo la hadharani.+ 16 Zaidi ya hayo, msisahau kutenda mema+ na kushiriki vitu pamoja na wengine, kwa maana Mungu hupendezwa vema na dhabihu za namna hiyo.+
17 Watiini wale wanaoongoza katikati yenu+ na mnyenyekee,+ kwa maana wanaendelea kuzilinda nafsi zenu kama wale watakaotoa hesabu;+ ili wafanye hivyo kwa shangwe na si kwa kuugua, kwa maana kufanya hivyo kungewadhuru ninyi.+
18 Endeleeni kusali+ kwa ajili yetu, kwa maana sisi tuna uhakika kwamba tuna dhamiri nyoofu, kwa kuwa tunataka kujiendesha kwa unyoofu katika mambo yote.+ 19 Lakini ninawahimiza ninyi zaidi hasa mfanye hivyo, ili nirudishwe kwenu upesi inavyowezekana.+
20 Basi Mungu wa amani,+ aliyemrudisha kutoka kwa wafu+ mchungaji+ mkuu wa kondoo+ kwa damu ya agano linalodumu milele,+ Bwana wetu Yesu, 21 na awape ninyi vifaa vyema vya kila namna ili kufanya mapenzi yake, akifanya katika sisi kupitia Yesu Kristo lile ambalo linapendeza vema machoni pake;+ ambaye kwake kuwe na utukufu milele na milele.+ Amina.
22 Basi ninawahimiza ninyi, akina ndugu, mlivumilie neno hili la kutia moyo, kwa maana mimi, kwa kweli, nimewaandikia barua kwa maneno machache.+ 23 Jueni kwamba ndugu yetu Timotheo+ ameachiliwa, naye akija hivi karibuni sana, nitawaona ninyi nikiwa pamoja naye.
24 Wapeni salamu zangu wale wote wanaoongoza+ katikati yenu na watakatifu wote. Wale walio katika Italia+ wanawatumia ninyi salamu zao.
25 Fadhili zisizostahiliwa+ na ziwe pamoja nanyi nyote.