Barua ya Kwanza ya Yohana
1 Kile kilichokuwa tangu mwanzo,+ ambacho tumesikia,+ ambacho tumeona kwa macho yetu,+ ambacho tumetazama+ kwa uangalifu na mikono yetu ikakigusa,+ kuhusu neno la uzima,+ 2 (ndiyo, uzima ulifunuliwa,+ na sisi tumeona na tunatoa ushahidi+ na kuwapa ninyi habari juu ya uzima wa milele+ ambao ulikuwa pamoja na Baba na ukafunuliwa kwetu,) 3 kile ambacho tumeona na kusikia tunawapa ninyi habari pia,+ ili ninyi pia muwe na ushirika pamoja na sisi.+ Zaidi ya hilo, huu ushirika+ wetu ni pamoja na Baba na pamoja na Mwana wake Yesu Kristo.+ 4 Na kwa hiyo tunaandika mambo haya ili shangwe yetu ijae kwa ukamili.+
5 Na huu ndio ujumbe ambao tumesikia kutoka kwake nasi tunawatangazia ninyi,+ kwamba Mungu ni nuru+ na hakuna giza kamwe katika muungano na yeye.+ 6 Kama tukisema: “Tuna ushirika pamoja na yeye,” na bado tunaendelea kutembea katika giza,+ tunasema uwongo nasi hatuzoei kutenda kweli.+ 7 Hata hivyo, ikiwa tunatembea katika nuru kama yeye mwenyewe alivyo katika nuru,+ tuna ushirika sisi kwa sisi,+ na damu+ ya Yesu Mwana wake hutusafisha+ kutoka katika dhambi yote.+
8 Kama tukisema: “Sisi hatuna dhambi yoyote,”+ tunajipotosha wenyewe+ na kweli haimo ndani yetu. 9 Tukiungama dhambi zetu,+ yeye ni mwaminifu na mwadilifu hata atusamehe dhambi zetu na kutusafisha ukosefu wote wa uadilifu.+ 10 Kama tukisema: “Sisi hatujatenda dhambi,” tunamfanya yeye kuwa mwongo, na neno lake halimo ndani yetu.+
2 Watoto wangu wadogo, ninawaandikia ninyi mambo haya ili msitende dhambi.+ Na bado, yeyote akitenda dhambi, tuna msaidizi+ kwa Baba, Yesu Kristo, mtu mwadilifu.+ 2 Na yeye ni dhabihu+ ya upatanisho+ kwa ajili ya dhambi zetu,+ lakini si kwa ajili ya zetu+ tu bali pia kwa ajili ya zile za ulimwengu wote.+ 3 Na kwa jambo hili tunajua kwamba tumemjua yeye, yaani, tukiendelea kuzishika amri zake.+ 4 Yeye anayesema: “Mimi nimemjua,”+ na bado hashiki amri zake,+ ni mwongo, na kweli haimo ndani ya mtu huyo.+ 5 Lakini yeyote anayeshika neno+ lake, kwa kweli katika mtu huyo upendo kwa Mungu umekamilishwa.+ Kwa hili tunajua kwamba sisi tumo katika muungano na yeye.+ 6 Yeye anayesema kwamba anakaa katika muungano+ na yeye yuko chini ya wajibu yeye mwenyewe pia kuendelea kutembea kama vile huyo alivyotembea.+
7 Wapendwa, ninawaandikia ninyi, si amri mpya, bali amri ya zamani+ ambayo mmekuwa nayo tangu mwanzo.+ Amri hii ya zamani ni neno ambalo mlisikia. 8 Tena, ninawaandikia ninyi amri mpya, uhakika ambao ni wa kweli kumhusu yeye na kuwahusu ninyi, kwa sababu giza+ linapitilia mbali na nuru+ ya kweli tayari inaangaza.
9 Yeye anayesema kwamba yumo katika nuru na bado anamchukia+ ndugu yake yumo katika giza hata hivi sasa.+ 10 Yeye anayempenda ndugu yake hukaa katika nuru,+ na hakuna lolote la kumkwaza.+ 11 Lakini yeye anayemchukia ndugu yake yumo katika giza+ na anatembea katika giza, naye hajui anakoenda,+ kwa sababu giza limeyapofusha macho yake.
12 Ninawaandikia ninyi, watoto wadogo, kwa sababu dhambi zenu zimesamehewa kwa ajili ya jina lake.+ 13 Ninawaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye wa tangu mwanzo.+ Ninawaandikia ninyi, vijana,+ kwa sababu mmemshinda yule mwovu.+ Ninawaandikia ninyi, watoto wachanga,+ kwa sababu mmemjua Baba.+ 14 Ninawaandikia ninyi, akina baba,+ kwa sababu mmemjua yeye aliye wa tangu mwanzo.+ Ninawaandikia ninyi, vijana, kwa sababu ninyi ni wenye nguvu+ na neno la Mungu hukaa ndani yenu+ nanyi mmemshinda yule mwovu.+
15 Msiwe mkiupenda ulimwengu au vitu vilivyo katika ulimwengu.+ Yeyote akiupenda ulimwengu, kumpenda Baba hakumo ndani yake;+ 16 kwa sababu kila kitu kilicho katika ulimwengu+—tamaa ya mwili+ na tamaa ya macho+ na mtu kujionyesha mali yake maishani+—hakitokani na Baba, bali hutokana na ulimwengu.+ 17 Zaidi ya hayo, ulimwengu unapitilia mbali na pia tamaa yake,+ lakini yeye anayefanya mapenzi+ ya Mungu anadumu milele.+
18 Watoto wachanga, ni saa ya mwisho,+ na, kama vile ambavyo mmesikia kwamba mpinga-Kristo anakuja,+ hata sasa kumekuwa na wapinga-Kristo wengi;+ uhakika ambao kutokana nao tunajua kwamba ni saa ya mwisho. 19 Wao waliondoka kwetu, lakini hawakuwa wa namna yetu;+ kwa maana ikiwa wangekuwa wa namna yetu, wangebaki pamoja na sisi.+ Lakini wao waliondoka ili ionyeshwe wazi kwamba si wote walio wa namna yetu.+ 20 Nanyi mmepata kutiwa mafuta kutoka kwa yule mtakatifu;+ ninyi nyote mna ujuzi.+ 21 Ninawaandikia ninyi, si kwa sababu hamjui kweli,+ bali kwa sababu mnaijua,+ na kwa sababu hakuna uwongo wowote unaotokana na kweli.+
22 Ni nani aliye mwongo kama si yule anayekana kwamba Yesu ndiye Kristo?+ Huyo ndiye mpinga-Kristo,+ yeye anayemkana Baba na Mwana.+ 23 Kila mtu anayemkana Mwana hana Baba pia.+ Yeye anayemkiri+ Mwana ana Baba pia.+ 24 Kwa habari yenu, acheni lile ambalo mmesikia tangu mwanzo likae ndani yenu.+ Ikiwa lile ambalo mmesikia tangu mwanzo linakaa ndani yenu, ninyi pia mtakaa katika muungano+ na Mwana na katika muungano na Baba.+ 25 Zaidi ya hayo, hili ndilo jambo lililoahidiwa ambalo yeye mwenyewe alituahidi, uzima wa milele.+
26 Mambo haya ninawaandikia ninyi juu ya wale ambao wanajaribu kuwapotosha ninyi.+ 27 Na kwa habari yenu, kule kutiwa mafuta+ ambako mlipokea kutoka kwake hukaa ndani yenu, nanyi hamhitaji yeyote awe akiwafundisha;+ lakini, kama vile kutiwa mafuta kutoka kwake kunavyowafundisha ninyi juu ya mambo yote,+ na ni kweli+ wala si uwongo, na kama vile kumewafundisha ninyi, kaeni katika muungano+ na yeye. 28 Kwa hiyo sasa, watoto wadogo,+ kaeni katika muungano+ na yeye, ili wakati atakapofunuliwa+ sisi tuwe na uhuru wa kusema+ na tusipate aibu kutoka kwake katika kuwapo+ kwake. 29 Mkijua kwamba yeye ni mwadilifu,+ mnajua kwamba kila mtu aliye na mazoea ya kufanya uadilifu amezaliwa kutokana naye.+
3 Oneni namna ya upendo+ ambao Baba ametupa sisi, ili tuitwe watoto wa Mungu;+ na sisi ndivyo tulivyo. Ndiyo sababu ulimwengu+ hautujui sisi, kwa sababu haumjui yeye.+ 2 Wapendwa, sasa sisi ni watoto wa Mungu,+ lakini bado haijafunuliwa jinsi tutakavyokuwa.+ Tunajua kwamba wakati wowote atakapofunuliwa+ tutakuwa kama yeye,+ kwa sababu tutamwona kama vile yeye alivyo.+ 3 Na kila mtu ambaye ana tumaini hili likiwa limekazwa juu yake hujitakasa+ mwenyewe kama vile huyo alivyo mwenye kutakata.+
4 Kila mtu aliye na mazoea ya kufanya dhambi+ anazoea pia kufanya uasi-sheria,+ na kwa hiyo dhambi+ ni uasi-sheria. 5 Mnajua pia kwamba huyo alifunuliwa ili kuondolea mbali dhambi zetu,+ na hakuna dhambi+ ndani yake. 6 Kila mtu anayekaa katika muungano+ na yeye hana mazoea ya kufanya dhambi;+ mtu yeyote aliye na mazoea ya kufanya dhambi hajamwona wala kumjua.+ 7 Watoto wadogo, yeyote asiwapotoshe ninyi; yeye ambaye huendelea kufanya uadilifu ni mwadilifu, kama vile huyo alivyo mwadilifu.+ 8 Yeye ambaye huendelea kufanya dhambi hutokana na Ibilisi, kwa sababu Ibilisi amekuwa akifanya dhambi tangu mwanzo.+ Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alifunuliwa,+ yaani, ili azivunje kazi za Ibilisi.+
9 Kila mtu ambaye amezaliwa kutokana na Mungu haendelei kufanya dhambi,+ kwa sababu mbegu Yake yenye kuzaa hukaa ndani ya mtu huyo, naye hawezi kuwa na mazoea ya kufanya dhambi, kwa sababu amezaliwa kutokana na Mungu.+ 10 Watoto wa Mungu na watoto wa Ibilisi ni wazi kwa jambo hili: Kila mtu ambaye haendelei kufanya uadilifu+ hatokani na Mungu, wala yeye ambaye hampendi ndugu yake.+ 11 Kwa maana huu ndio ujumbe ambao mmesikia tangu mwanzo,+ kwamba tunapaswa kupendana;+ 12 si kama Kaini, aliyetokana na yule mwovu akamuua+ ndugu yake. Naye alimuua kwa nini? Kwa sababu matendo yake mwenyewe yalikuwa maovu,+ lakini yale ya ndugu yake yalikuwa ya uadilifu.+
13 Msistaajabu, akina ndugu, kwamba ulimwengu unawachukia ninyi.+ 14 Sisi tunajua tumevuka kutoka kifo mpaka uzima,+ kwa sababu tunawapenda akina ndugu.+ Yeye ambaye hapendi hukaa katika kifo.+ 15 Kila mtu anayemchukia+ ndugu yake ni muuaji,+ nanyi mnajua kwamba hakuna muuaji+ aliye na uzima wa milele ukikaa ndani yake.+ 16 Kwa hili tumeujua upendo,+ kwa sababu huyo aliitoa nafsi yake kwa ajili yetu;+ na sisi tuko chini ya wajibu kuzitoa nafsi zetu kwa ajili ya ndugu zetu.+ 17 Lakini yeyote aliye na riziki ya ulimwengu huu+ naye amwone ndugu yake akiwa na uhitaji+ na bado amfungie mlango wa huruma zake nyororo,+ ni katika njia gani kumpenda Mungu hukaa ndani yake?+ 18 Watoto wadogo, acheni tupendane,+ si kwa neno wala kwa ulimi,+ bali kwa tendo+ na kweli.+
19 Kwa jambo hili tutajua kwamba sisi tunatokana na kweli,+ nasi tutaihakikishia mioyo yetu mbele zake 20 kwa habari ya lolote ambalo huenda mioyo yetu ikatuhukumu kuwa na hatia,+ kwa sababu Mungu ni mkuu kuliko mioyo yetu naye anajua mambo yote.+ 21 Wapendwa, ikiwa mioyo yetu haituhukumu kuwa na hatia, tuna uhuru wa kusema kwa Mungu;+ 22 na chochote kile tunachoomba tunapokea kutoka kwake,+ kwa sababu tunazishika amri zake na tunafanya mambo yanayopendeza machoni pake.+ 23 Kwa kweli, hii ndiyo amri yake, kwamba tuwe na imani katika jina la Mwana wake Yesu Kristo+ na tuwe tukipendana,+ kama yeye alivyotupa sisi amri. 24 Zaidi ya hayo, yeye ambaye hushika amri zake hukaa katika muungano na yeye, na yeye katika muungano na mtu huyo;+ na kwa jambo hili sisi tunajua kwamba yeye anakaa katika muungano na sisi,+ kwa sababu ya roho+ ambayo alitupa sisi.
4 Wapendwa, msiamini kila neno lililoongozwa na roho,+ lakini yajaribuni maneno yaliyoongozwa na roho ili kuona kama yanatokana na Mungu,+ kwa sababu manabii wengi wa uwongo wameingia ulimwenguni.+
2 Mnalijua neno lililoongozwa na roho kutoka kwa Mungu+ kwa njia hii: Kila neno lililoongozwa na roho linalomkiri Yesu Kristo kuwa alikuja katika mwili hutokana na Mungu,+ 3 lakini kila neno lililoongozwa na roho ambalo halimkiri Yesu halitokani na Mungu.+ Zaidi ya hayo, hili ndilo neno lililoongozwa na roho la yule mpinga-Kristo ambalo mmesikia kwamba linakuja,+ na sasa tayari limo ulimwenguni.+
4 Ninyi mnatokana na Mungu, watoto wadogo, nanyi mmewashinda watu hao,+ kwa sababu yeye aliye katika muungano+ na ninyi ni mkuu+ kuliko yeye aliye katika muungano na ulimwengu.+ 5 Wao hutokana na ulimwengu;+ ndiyo sababu wanasema lile linalotoka kwa ulimwengu na ulimwengu huwasikiliza wao.+ 6 Sisi tunatokana na Mungu.+ Yeye ambaye anamjua Mungu hutusikiliza;+ yeye ambaye hatokani na Mungu hatusikilizi.+ Hivi ndivyo tunavyojua neno la kweli lililoongozwa na roho na neno lenye kosa lililoongozwa na roho.+
7 Wapendwa, acheni tuendelee kupendana,+ kwa sababu upendo+ unatoka kwa Mungu, na kila mtu ambaye hupenda amezaliwa kutokana na Mungu+ na hupata kumjua Mungu.+ 8 Yeye ambaye hapendi hajamjua Mungu, kwa sababu Mungu ni upendo.+ 9 Kwa hili upendo wa Mungu ulifunuliwa kwa habari yetu,+ kwa sababu Mungu alimtuma Mwana+ wake mzaliwa-pekee kuja ulimwenguni ili tupate uzima kupitia yeye.+ 10 Hivi ndivyo upendo ulivyo, si kwamba sisi tumempenda Mungu, bali kwamba yeye alitupenda akamtuma Mwana wake kuwa dhabihu+ ya upatanisho+ kwa ajili ya dhambi zetu.+
11 Wapendwa, ikiwa Mungu alitupenda hivi, basi sisi wenyewe tuko chini ya wajibu wa kupendana.+ 12 Hakuna yeyote ambaye amemwona Mungu wakati wowote.+ Tukiendelea kupendana, Mungu hukaa ndani yetu na upendo wake unakamilishwa ndani yetu.+ 13 Kwa hili sisi tunajua kwamba tunakaa katika muungano+ na yeye na yeye katika muungano na sisi,+ kwa sababu ametupa sisi roho yake.+ 14 Kwa kuongezea, sisi wenyewe tumemwona+ na tunatoa ushahidi+ kwamba Baba amemtuma Mwana wake kuwa Mwokozi wa ulimwengu.+ 15 Yeyote anayekiri kwamba Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu,+ Mungu hukaa katika muungano na mtu huyo na yeye katika muungano na Mungu.+ 16 Na sisi wenyewe tumejua na tumeamini upendo+ ambao Mungu anao kwa habari yetu.
Mungu ni upendo,+ na yeye ambaye hukaa katika upendo+ hukaa katika muungano na Mungu na Mungu hukaa katika muungano+ na yeye. 17 Hivi ndivyo upendo umekamilishwa ndani yetu, kwamba tuwe na uhuru wa kusema+ katika siku ya hukumu,+ kwa sababu, kama vile huyo alivyo, ndivyo tulivyo sisi wenyewe katika ulimwengu huu.+ 18 Hakuna woga katika upendo,+ lakini upendo mkamilifu hutupa woga nje,+ kwa sababu woga hutokeza kizuizi. Kwa kweli, yeye ambaye yuko chini ya woga hajakamilishwa katika upendo.+ 19 Kwa habari yetu, sisi tunaonyesha upendo, kwa sababu yeye alitupenda sisi kwanza.+
20 Yeyote akisema: “Mimi nampenda Mungu,” na bado anamchukia ndugu yake, yeye ni mwongo.+ Kwa maana yeye ambaye hampendi ndugu yake,+ ambaye amemwona, hawezi kuwa anampenda Mungu, ambaye hajamwona.+ 21 Na amri hii tunayo kutoka kwake,+ kwamba yeye ambaye anampenda Mungu anapaswa kuwa akimpenda ndugu yake pia.+
5 Kila mtu anayeamini kwamba Yesu ndiye Kristo amezaliwa kutokana na Mungu,+ na kila mtu ambaye humpenda yule ambaye alisababisha kuzaliwa humpenda yeye ambaye amezaliwa kutokana na huyo.+ 2 Kwa hili sisi tunajua kwamba tunawapenda+ watoto wa Mungu,+ wakati tunapompenda Mungu na kutenda amri zake.+ 3 Kwa maana kumpenda+ Mungu humaanisha hivi, kwamba tuzishike amri zake;+ na bado amri zake si mzigo mzito,+ 4 kwa sababu kila kitu ambacho kimezaliwa+ kutokana na Mungu huushinda ulimwengu.+ Na huu ndio ushindi+ ambao umeushinda+ ulimwengu, imani+ yetu.
5 Ni nani ambaye huushinda+ ulimwengu+ isipokuwa yeye aliye na imani+ kwamba Yesu ndiye Mwana wa Mungu?+ 6 Huyu ndiye aliyekuja kwa njia ya maji na damu, Yesu Kristo; si kwa maji+ tu, bali kwa maji na kwa damu.+ Na roho+ ndiyo inayotoa ushahidi, kwa sababu roho ndiyo kweli. 7 Kwa maana kuna vitatu vinavyotoa ushahidi, 8 roho+ na maji+ na damu,+ na hivyo vitatu vinakubaliana.+
9 Tukipokea ushahidi ambao wanadamu hutoa,+ ushahidi ambao Mungu hutoa ni mkuu zaidi, kwa sababu huu ndio ushahidi ambao Mungu hutoa, jambo la kwamba ametoa ushahidi+ kumhusu Mwana wake. 10 Mtu anayemwamini Mwana wa Mungu, ushahidi+ umetolewa kwa habari yake. Mtu asiye na imani katika Mungu amemfanya yeye kuwa mwongo,+ kwa sababu hakuwa na imani katika ushahidi uliotolewa,+ ambao Mungu akiwa shahidi+ ametoa kumhusu Mwana wake. 11 Na huu ndio ushahidi ambao umetolewa, kwamba Mungu alitupa sisi uzima wa milele,+ na uzima huu umo ndani ya Mwana+ wake. 12 Yeye ambaye ana Mwana ana uzima huu; yeye ambaye hana Mwana wa Mungu hana uzima huu.+
13 Ninawaandikia mambo haya ili mjue kwamba ninyi mnao uzima wa milele,+ ninyi ambao mmekuwa na imani katika jina la Mwana wa Mungu.+ 14 Na huu ndio uhakika ambao tunao kwake,+ kwamba, hata tukiomba nini kulingana na mapenzi yake, yeye hutusikia.+ 15 Zaidi ya hayo, tukijua kwamba yeye hutusikia kwa habari ya jambo lolote tunaloomba,+ tunajua tutapata mambo yaliyoombwa kwa kuwa tumeyaomba kwake.+
16 Yeyote akimwona ndugu yake anafanya dhambi, dhambi ambayo haileti kifo,+ yeye ataomba, naye atampa huyo uzima,+ ndiyo, kwa wale ambao hawafanyi dhambi inayoleta kifo.+ Kuna dhambi ambayo huleta kifo. Ni kuhusu dhambi hiyo kwamba simwambii aombe.+ 17 Ukosefu wote wa uadilifu ni dhambi;+ na bado kuna dhambi ambayo haileti kifo.
18 Tunajua kwamba kila mtu ambaye amezaliwa kutokana na Mungu+ hana mazoea ya kufanya dhambi, lakini yeye hulindwa na Yule+ ambaye amezaliwa kutokana na Mungu, na yule mwovu hamshiki imara.+ 19 Tunajua tunatokana na Mungu,+ lakini ulimwengu mzima unakaa katika nguvu za yule mwovu.+ 20 Lakini tunajua kwamba Mwana wa Mungu amekuja,+ naye ametupa sisi uwezo wa akili+ ili tupate kumjua yule wa kweli.+ Na sisi tumo katika muungano+ na yule wa kweli, kwa njia ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyo ndiye Mungu wa kweli+ na uzima wa milele.+ 21 Watoto wadogo, jilindeni na sanamu.+