Ezekieli
37 Mkono wa Yehova ulikuwa juu yangu,+ hivi kwamba akanichukua katika roho ya Yehova+ na kuniweka chini katikati ya nchi tambarare ya bondeni, nayo ilikuwa imejaa mifupa.+ 2 Naye akanipitisha kando yake pande zote, na, tazama! ilikuwa mingi sana kwenye uso wa hiyo nchi tambarare ya bondeni na, tazama! ilikuwa mikavu sana.+ 3 Naye akaanza kuniambia: “Mwana wa binadamu, je, mifupa hii inaweza kuwa hai?” Nikajibu: “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, wewe mwenyewe unajua vema.”+ 4 Naye akaendelea kuniambia: “Toa unabii juu ya mifupa hii, nawe uiambie, ‘Enyi mifupa mikavu, lisikieni neno la Yehova:
5 “ ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova ameiambia mifupa hii hivi: “Tazama, ninaleta ndani yenu pumzi, nanyi lazima muwe hai.+ 6 Nami nitaweka juu yenu kano na kufanya nyama ije juu yenu, nami nitaitandaza ngozi juu yenu na kutia pumzi ndani yenu, nanyi mtakuwa hai;+ nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.” ’ ”+
7 Nami nikatoa unabii kama nilivyoamriwa.+ Na sauti ikaanza kutokea mara tu nilipotoa unabii, na tazama, kulikuwa na sauti ya kugongana, nayo mifupa ikaanza kukaribiana, mfupa kwa mfupa wake. 8 Nami nikaona, na, tazama! kano na nyama zikaja juu yake na ngozi ikaanza kutandazwa juu yake. Lakini kwa habari ya pumzi, hamkuwa na yoyote ndani yake.
9 Naye akaendelea kuniambia: “Tolea upepo unabii. Toa unabii, Ee mwana wa binadamu, nawe utauambia upepo, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Ingia kutoka kwenye zile pepo nne, Ee upepo, na upulize juu ya watu hawa waliouawa,+ ili wawe hai.” ’ ”+
10 Nami nikatoa unabii kama vile alivyokuwa ameniamuru, nayo pumzi ikaanza kuingia ndani yao, nao wakaanza kuishi na kusimama kwa miguu yao,+ jeshi kubwa, naam, kubwa sana.
11 Naye akaendelea kuniambia: “Mwana wa binadamu, kwa habari ya mifupa hii, hii ni nyumba nzima ya Israeli.+ Tazama, wanasema, ‘Mifupa yetu imekauka, nalo tumaini letu limeangamia.+ Tumekatiliwa mbali, tukabaki peke yetu.’ 12 Kwa hiyo toa unabii, nawe utawaambia, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Tazama ninayafungua makaburi yenu,+ nami nitawatoa kutoka katika makaburi yenu, enyi watu wangu, na kuwaingiza katika nchi ya Israeli.+ 13 Nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova nitakapoyafungua makaburi yenu na nitakapowatoa ninyi kutoka katika makaburi yenu, enyi watu wangu.” ’+ 14 ‘Nami nitaitia roho yangu ndani yenu, nanyi mtakuwa hai,+ nami nitawakalisha katika nchi yenu; nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimesema nami nimelifanya,’ asema Yehova.”+
15 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 16 “Na wewe, Ee mwana wa binadamu, jichukulie kijiti+ na uandike juu yake, ‘Kwa Yuda na kwa wenzake, wana wa Israeli.’+ Na uchukue kijiti kingine na kuandika juu yake, ‘Kwa Yosefu, kijiti cha Efraimu,+ na wenzake, nyumba yote ya Israeli.’+ 17 Na uvifanye vikaribiane viwe kijiti kimoja kwa ajili yako mwenyewe, navyo kwa kweli vitakuwa kimoja tu mkononi mwako.+ 18 Na wana wa watu wako watakapoanza kukuambia, ‘Je, hutatuambia mambo haya yana maana gani kwako?’+ 19 waambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Tazama, ninakichukua kijiti cha Yosefu, kilicho mkononi mwa Efraimu, na wenzake, makabila ya Israeli, nami nitawaweka juu yake, yaani, kijiti cha Yuda, nami kwa kweli nitavifanya kuwa kijiti kimoja,+ navyo vitakuwa kimoja mkononi mwangu.” ’ 20 Navyo vijiti utakavyoandika juu yake vitakuwa mkononi mwako mbele ya macho yao.+
21 “Nawe uwaambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Tazama, ninawachukua wana wa Israeli kutoka katikati ya mataifa ambako wameenda, nami nitawakusanya kutoka pande zote na kuwaleta katika nchi yao.+ 22 Nami kwa kweli nitawafanya kuwa taifa moja katika nchi hiyo,+ kwenye milima ya Israeli, na mfalme mmoja atakuwa mfalme wao wote,+ nao hawataendelea tena kuwa mataifa mawili, wala hawataendelea tena kugawanyika katika falme mbili.+ 23 Nao hawatajitia unajisi tena kwa sanamu zao za mavi na kwa machukizo yao na kwa makosa yao yote;+ nami hakika nitawaokoa kutoka katika makao yao yote ambamo wametenda dhambi ndani yake, nami nitawasafisha,+ nao watakuwa watu wangu, na mimi mwenyewe nitakuwa Mungu wao.+
24 “ ‘ “Na mtumishi wangu Daudi atakuwa mfalme juu yao,+ nao wote watakuwa na mchungaji mmoja;+ nao watatembea katika maamuzi yangu ya hukumu,+ na sheria zangu watazishika,+ nao hakika watazifanya.+ 25 Nao kwa kweli watakaa juu ya nchi niliyompa mtumishi wangu, Yakobo, ambamo mababu zenu walikaa,+ nao kwa kweli watakaa juu yake,+ wao na wana wao na wana wa wana wao mpaka wakati usio na kipimo,+ na Daudi mtumishi wangu atakuwa mkuu wao mpaka wakati usio na kipimo.+
26 “ ‘ “Nami nitafanya agano la amani+ pamoja nao; watakuwa na agano lenye kudumu mpaka wakati usio na kipimo.+ Nami nitawaweka na kuwazidisha+ na kuweka patakatifu pangu katikati yao mpaka wakati usio na kipimo.+ 27 Na maskani yangu kwa kweli itakuwa juu yao,+ nami hakika nitakuwa Mungu wao, na wao wenyewe watakuwa watu wangu.+ 28 Na mataifa watalazimika kujua kwamba mimi, Yehova,+ ninawatakasa Israeli wakati patakatifu pangu patakapokuwa katikati yao mpaka wakati usio na kipimo.” ’ ”+