Luka
20 Siku moja alipokuwa akifundisha watu katika hekalu na kutangaza habari njema, wakuu wa makuhani na waandishi pamoja na wanaume wazee wakaja karibu,+ 2 nao wakasema, wakimwambia: “Tuambie unafanya mambo haya kwa mamlaka gani, au ni nani aliyekupa mamlaka hiyo.”+ 3 Akajibu, akawaambia: “Mimi pia nitawauliza ninyi swali, nanyi mniambie:+ 4 Je, ubatizo wa Yohana ulitoka mbinguni au kwa wanadamu?”+ 5 Ndipo kati yao wenyewe wakafikia kauli, wakisema: “Tukisema, ‘Ulitoka mbinguni,’ atasema, ‘Kwa nini hamkumwamini?’+ 6 Lakini tukisema, ‘Ulitoka kwa wanadamu,’ watu wote watatupiga kwa mawe,+ kwa maana wao wamesadikishwa kwamba Yohana+ alikuwa nabii.”+ 7 Kwa hiyo wakajibu kwamba hawakujua chanzo chake. 8 Naye Yesu akawaambia: “Wala mimi siwaambii ninyi ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani.”+
9 Ndipo akaanza kuwaambia watu mfano huu: “Mtu alipanda shamba la mizabibu+ akalikodisha kwa wakulima, naye akasafiri kwenda ng’ambo kwa muda mrefu.+ 10 Lakini majira yake yalipofika akatuma mtumwa+ kwa wakulima,+ ili wampe sehemu ya matunda ya shamba la mizabibu.+ Hata hivyo, wakulima hao wakamfukuza akiwa mikono mitupu,+ baada ya kumpiga sana. 11 Lakini akatuma tena mtumwa tofauti kwao. Huyo pia wakampiga sana na kumvunjia heshima na kumfukuza akiwa mikono mitupu.+ 12 Na bado tena akamtuma wa tatu;+ huyo pia walimjeruhi na kumtupa nje. 13 Ndipo mwenye shamba la mizabibu akasema, ‘Nitafanya nini? Nitamtuma mwanangu mpendwa.+ Labda watamheshimu huyu.’ 14 Wakulima walipomwona wakaanza kujadiliana, wakisema, ‘Huyu ndiye mrithi; acheni tumuue, ili urithi uwe wetu.’+ 15 Ndipo wakamtupa nje+ ya shamba la mizabibu na kumuua.+ Kwa hiyo, mwenye shamba la mizabibu atawafanya nini?+ 16 Atakuja awaangamize wakulima hao na kuwapa wengine shamba hilo la mizabibu.”+
Waliposikia hilo wakasema: “Jambo hilo lisitukie kamwe!” 17 Lakini akawatazama na kusema: “Basi, hili ambalo limeandikwa humaanisha nini, ‘Jiwe ambalo wajenzi walilikataa,+ limekuwa jiwe kuu la pembeni’?+ 18 Kila mtu anayeanguka juu ya jiwe hilo atavunjwa-vunjwa.+ Na yeyote ambaye litamwangukia,+ litamponda-ponda.”+
19 Waandishi na wakuu wa makuhani sasa wakatafuta kunyoosha mkono ili wamkamate saa ileile, lakini waliwaogopa watu; kwa maana walifahamu kwamba alisema mfano huo juu yao.+ 20 Na, baada ya kumtazama sana, wakatuma watu waliokodiwa kwa siri wasingizie kwamba walikuwa waadilifu, ili wapate kumnasa+ katika maneno, ili wamkabidhi kwa serikali na kwa mamlaka ya gavana.+ 21 Nao wakamuuliza, wakisema: “Mwalimu, tunajua wewe husema na kufundisha kwa usahihi na huonyeshi ubaguzi wowote, bali wewe hufundisha njia ya Mungu kupatana na ile kweli:+ 22 Je, ni halali sisi kumlipa Kaisari kodi au hapana?”+ 23 Lakini akagundua ujanja wao na kuwaambia:+ 24 “Nionyesheni dinari. Ina sanamu na mwandiko wa nani?” Wakasema: “Wa Kaisari.”+ 25 Akawaambia: “Kwa vyovyote, basi, mlipeni Kaisari vitu vya Kaisari,+ lakini mlipeni Mungu vitu vya Mungu.”+ 26 Basi, hawakuweza kumnasa katika maneno haya mbele ya watu, bali, wakiwa wameshangazwa na jibu lake, hawakusema kitu.+
27 Hata hivyo, baadhi ya Masadukayo, wale ambao husema hakuna ufufuo, wakaja+ na kumuuliza swali, 28 wakisema: “Mwalimu, Musa+ alituandikia, ‘Ndugu ya mtu akifa akiwa na mke, lakini hakuwa na mtoto, ndugu yake+ anapaswa kumchukua mke huyo na kumwinulia ndugu yake uzao kutoka kwa mwanamke huyo.’+ 29 Basi kulikuwa na ndugu saba; na wa kwanza akamchukua mke na kufa bila mtoto.+ 30 Na wa pili, 31 na wa tatu, wakamchukua mwanamke huyo. Vivyo hivyo hata wa saba: hawakuacha uzao, bali walikufa mmoja baada ya mwingine.+ 32 Mwishowe, yule mwanamke akafa pia.+ 33 Kwa hiyo, katika ufufuo, atakuwa mke wa nani kati yao? Kwa maana wale saba walimchukua kama mke.”+
34 Yesu akawaambia: “Watoto wa mfumo huu wa mambo huoa+ na huolewa, 35 lakini wale ambao wamehesabiwa kustahili+ kuupata mfumo ule wa mambo+ na ufufuo kutoka kwa wafu+ hawaoi wala hawaolewi. 36 Kwa kweli, wala hawawezi kufa+ tena kamwe, kwa maana wao ni kama malaika, nao ni watoto wa Mungu kwa kuwa watoto wa ufufuo.+ 37 Lakini hata Musa alifunua kwamba wafu watafufuliwa, katika masimulizi juu ya ule mti wa miiba,+ anapomwita Yehova ‘Mungu wa Abrahamu na Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo.’+ 38 Yeye ni Mungu, si wa wafu, bali wa walio hai, kwa maana kwake, hao wote wako hai.”+ 39 Baadhi ya waandishi wakajibu, wakasema: “Mwalimu, umesema vema.” 40 Kwa maana hawakuwa tena na ujasiri wa kumuuliza hata swali moja.
41 Naye akawaambia: “Kwa nini wao husema kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?+ 42 Kwa maana Daudi mwenyewe anasema katika kitabu cha Zaburi, ‘Yehova alimwambia Bwana wangu: “Keti kwenye mkono wangu wa kuume 43 mpaka niwaweke adui zako kuwa kiti cha miguu yako.”’+ 44 Basi, Daudi anamwita ‘Bwana’; kwa hiyo inawezekanaje kwamba yeye ni mwana wake?”
45 Ndipo, watu wote wakiwa wanasikiliza akawaambia wanafunzi:+ 46 “Jihadharini na waandishi ambao hutamani kutembea wakiwa wamevaa kanzu nao hupenda salamu katika masoko na viti vya mbele katika masinagogi na mahali penye kuonekana zaidi kwenye milo ya jioni,+ 47 na ambao humeza nyumba za wajane+ na kutoa sala ndefu kwa kisingizio. Hawa watapokea hukumu nzito zaidi.”+