BARUA YA KWANZA KWA TIMOTHEO
1 Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu na ya Kristo Yesu, tumaini letu,+ 2 kwa Timotheo,*+ mwanangu halisi+ katika imani:
Na uwe na fadhili zisizostahiliwa, rehema, na amani kutoka kwa Mungu Baba na Kristo Yesu Bwana wetu.
3 Kama nilivyokutia moyo ubaki Efeso nilipokuwa karibu kwenda Makedonia, sasa ninakutia moyo ufanye vivyo hivyo, ili uwaamuru watu fulani wasifundishe mambo tofauti, 4 wala kusikiliza hadithi za uwongo+ na kuchunguza-chunguza ukoo. Mambo hayo hayaleti manufaa yoyote+ bali hutokeza maswali badala ya kuleta chochote kutoka kwa Mungu kuhusiana na imani. 5 Kwa kweli, kusudi la agizo hili* ni upendo+ unaotokana na moyo safi na dhamiri njema na imani+ bila unafiki. 6 Kwa kuyaacha mambo hayo, watu fulani wamekengeushwa na kujiingiza katika mazungumzo yasiyo na maana.+ 7 Wanataka kuwa walimu+ wa sheria, lakini hawaelewi mambo wanayosema au mambo wanayosisitiza sana.
8 Sasa tunajua kwamba Sheria ni nzuri ikiwa mtu anaitumia vizuri,* 9 na tunatambua kwamba sheria haiwekwi kwa ajili ya mtu mwadilifu, bali kwa ajili ya watu wanaovunja sheria+ na waasi, watu wasiomwogopa Mungu na watenda dhambi, wasio washikamanifu* na wasioheshimu mambo matakatifu, wale wanaoua akina baba, akina mama, au watu wengine, 10 waasherati,* wanaume wanaofanya ngono na wanaume,* wateka nyara, waongo, wanaotoa ushahidi wa uwongo,* na jambo lingine lolote ambalo ni kinyume cha fundisho lenye manufaa*+ 11 kulingana na habari njema yenye utukufu ya Mungu mwenye furaha, ambayo nilikabidhiwa.+
12 Ninamshukuru Kristo Yesu Bwana wetu, aliyenitia nguvu, kwa sababu aliniona kuwa mwaminifu kwa kunipa huduma,+ 13 ingawa zamani nilikuwa mkufuru na mtesaji na mtu mwenye dharau.+ Hata hivyo, nilionyeshwa rehema, kwa sababu nilitenda bila ujuzi na sikuwa na imani. 14 Lakini fadhili zisizostahiliwa za Bwana wetu zilizidi sana pamoja na imani na upendo ulio katika Kristo Yesu. 15 Maneno haya ni yenye kuaminika na yanastahili kukubaliwa kabisa: Kristo Yesu alikuja ulimwenguni ili kuwaokoa watenda dhambi.+ Kati yao, mimi ndiye wa kwanza kabisa.+ 16 Hata hivyo, nilionyeshwa rehema ili kupitia mimi nikiwa wa kwanza kabisa, Kristo Yesu aonyeshe subira yake yote, nami niwe mfano kwa wote watakaomwamini ili kupata uzima wa milele.+
17 Sasa kwa Mfalme wa umilele,+ asiyeweza kuharibika+ na asiyeonekana,+ Mungu pekee,+ kuwe na heshima na utukufu milele na milele. Amina.
18 Mwanangu Timotheo, ninakukabidhi agizo hili,* ili kulingana na unabii uliotolewa kukuhusu, uendelee kupigana vita vizuri,+ 19 ukishika imani na dhamiri njema,+ ambayo wengine wameitupilia mbali na hivyo imani yao ikavunjika. 20 Himenayo+ na Aleksanda ni kati yao, nami nimewatia mkononi mwa Shetani,+ ili wafundishwe kwa nidhamu wasikufuru.
2 Basi, kwanza kabisa, ninahimiza kwamba dua, shukrani, sala, na maombi yatolewe kwa ajili ya watu wa namna zote, 2 kutia ndani wafalme na wote wenye vyeo vya juu,*+ ili tuendelee kuishi kwa amani na utulivu na ujitoaji-kimungu* kamili na kuchukua mambo kwa uzito.+ 3 Jambo hilo ni zuri na linampendeza Mwokozi wetu, Mungu,+ 4 ambaye mapenzi yake ni kwamba watu wa namna zote waokolewe+ na kupata ujuzi sahihi wa kweli. 5 Kwa maana kuna Mungu mmoja,+ na mpatanishi mmoja+ kati ya Mungu na wanadamu,+ mwanadamu, Kristo Yesu,+ 6 aliyejitoa kuwa fidia inayolingana kwa ajili ya wote*+—hilo litatolewa ushahidi kwa wakati wake unaofaa. 7 Kwa ajili ya ushahidi huo+ niliwekwa rasmi niwe mhubiri na mtume+—ninasema ukweli, sisemi uwongo—mwalimu wa mataifa+ kuhusu imani na kweli.
8 Basi ninatamani kwamba kila mahali wanaume waendelee kusali, wakiinua mikono yenye ushikamanifu,+ bila hasira+ wala mabishano.+ 9 Vivyo hivyo, wanawake wanapaswa kujipamba kwa mavazi yanayofaa,* kwa kiasi na utimamu wa akili,* si kwa mitindo ya kusuka nywele, dhahabu, lulu, au mavazi ya bei ghali sana,+ 10 bali kwa njia inayowafaa wanawake wanaokiri kwamba wanamtumikia Mungu,+ yaani, kupitia matendo mema.
11 Mwanamke na ajifunze akiwa kimya* na kwa ujitiisho kamili.+ 12 Simruhusu mwanamke afundishe wala kuwa na mamlaka juu ya mwanamume, bali akae kimya.*+ 13 Kwa maana Adamu aliumbwa kwanza, kisha Hawa.+ 14 Pia, Adamu hakudanganywa, bali mwanamke alidanganywa kabisa+ akawa mtenda dhambi. 15 Hata hivyo, atalindwa kupitia kuzaa watoto,+ maadamu anaendelea* kuwa na imani, upendo, utakatifu, na utimamu wa akili.*+
3 Maneno haya ni yenye kutegemeka: Ikiwa mwanamume anajitahidi kuwa mwangalizi,+ anatamani kazi njema. 2 Mwangalizi anapaswa kuwa mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi katika mazoea, mwenye utimamu wa akili,*+ mwenye utaratibu, mkaribishaji wageni,*+ mwenye uwezo wa kufundisha,+ 3 si mlevi,+ si mkatili,* bali mwenye usawaziko,+ si mgomvi,+ si mtu anayependa pesa,+ 4 mwanamume anayeisimamia* nyumba yake vizuri, mwenye watoto wanaojitiisha na kuchukua mambo kwa uzito+ 5 (kwa maana ikiwa mtu hajui jinsi ya kuisimamia* nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje kutaniko la Mungu?), 6 si mtu aliyegeuka hivi karibuni,+ ili asije akawa na kiburi na kuanguka katika hukumu aliyohukumiwa Ibilisi. 7 Pia, anapaswa kushuhudiwa vema na* watu walio nje+ ili asianguke katika shutuma* na mtego wa Ibilisi.
8 Vilevile watumishi wa huduma wanapaswa kuchukua mambo kwa uzito, si wenye ndimi mbili,* si wenye kunywa divai nyingi, si wenye pupa ya mapato yasiyo ya haki,+ 9 wakiishika siri takatifu ya imani kwa dhamiri safi.+
10 Pia, wanapaswa kwanza kujaribiwa* kama wanafaa; ndipo watumike wakiwa wahudumu, kwa kuwa hawana shtaka.+
11 Vilevile wanawake wanapaswa kuchukua mambo kwa uzito, wasiwe wachongezi,+ wawe wenye kiasi katika mazoea, na waaminifu katika mambo yote.+
12 Watumishi wa huduma wanapaswa kuwa waume wa mke mmoja, wanaosimamia vizuri watoto wao na nyumba zao wenyewe. 13 Kwa maana wanaume wanaohudumu vizuri wanajipatia sifa nzuri na uhuru mwingi wa kusema katika imani iliyo katika Kristo Yesu.
14 Ninakuandikia mambo haya, ingawa ninatumaini kuja kwako upesi, 15 ili nikichelewa ujue jinsi unavyopaswa kutenda katika nyumba ya Mungu,+ ambayo ni kutaniko la Mungu aliye hai, nguzo na tegemezo la ile kweli. 16 Kwa kweli, siri takatifu ya huu ujitoaji-kimungu* ni kubwa: ‘Alifunuliwa katika mwili,+ alitangazwa kuwa mwadilifu katika roho,+ aliwatokea malaika,+ alihubiriwa kati ya mataifa,+ watu walimwamini ulimwenguni,+ akapokewa mbinguni kwa utukufu.’
4 Hata hivyo, neno lililoongozwa na roho linasema* wazi kwamba wakati ujao watu fulani wataiacha imani, wakisikiliza maneno ya uwongo yaliyoongozwa na roho waovu*+ na mafundisho ya roho waovu, 2 kupitia unafiki wa watu wanaosema uwongo,+ ambao dhamiri zao zimetiwa alama kama kwa chuma cha moto. 3 Wanakataza watu kufunga ndoa+ na kuwaamuru wasile vyakula+ ambavyo Mungu aliumba viliwe+ kwa shukrani na watu wenye imani+ na wanaoijua kweli kwa usahihi. 4 Kwa sababu kila kiumbe cha Mungu ni kizuri,+ na hakuna kitu kinachopaswa kukataliwa+ ikiwa kinapokewa kwa shukrani, 5 kwa maana kinatakaswa kupitia neno la Mungu na kutolewa sala.
6 Ukiwapa akina ndugu mashauri haya utakuwa mhudumu mzuri wa Kristo Yesu, aliyelishwa maneno ya imani na fundisho bora ambalo umefuata kwa makini.+ 7 Lakini kataa hadithi za uwongo zisizo na heshima,+ kama zile zinazosimuliwa na wanawake wazee. Badala yake, endelea kujizoeza ukiwa na lengo la ujitoaji-kimungu.* 8 Kwa maana mazoezi ya kimwili ni yenye faida kidogo, lakini ujitoaji-kimungu* una faida katika mambo yote, kwa kuwa una ahadi ya uhai wa sasa na ule utakaokuja.+ 9 Maneno hayo ni yenye kutegemeka na yanastahili kukubaliwa kabisa. 10 Hiyo ndiyo sababu tunafanya kazi kwa bidii na kujitahidi,+ kwa sababu tumemtumaini Mungu aliye hai, ambaye ni Mwokozi+ wa watu wa namna zote,+ hasa wa walio waaminifu.
11 Endelea kutoa amri hizi na kuzifundisha. 12 Usiruhusu kamwe mtu yeyote audharau ujana wako. Badala yake, uwe mfano mzuri kwa waaminifu katika kusema, katika mwenendo, katika upendo, katika imani, na katika usafi wa kiadili. 13 Mpaka nitakapokuja, endelea kujitahidi kusoma mbele ya watu,+ kuhimiza,* na kufundisha. 14 Usipuuze zawadi uliyo nayo uliyopokea kupitia unabii, baraza la wazee lilipoweka mikono juu yako.+ 15 Tafakari* mambo haya; zama katika hayo, ili maendeleo yako yaonekane wazi kwa watu wote. 16 Jiangalie daima wewe mwenyewe na kufundisha kwako.+ Endelea kufanya mambo haya, kwa maana ukifanya hivyo utajiokoa wewe mwenyewe na wale wanaokusikiliza pia.+
5 Usimkosoe kwa ukali mwanamume mzee.+ Badala yake, msihi kama baba, wanaume vijana kama ndugu, 2 wanawake wazee kama mama, na wanawake vijana kama dada, kwa usafi wote wa kiadili.
3 Wajali* wajane ambao ni wajane kwelikweli.*+ 4 Lakini ikiwa mjane yeyote ana watoto au wajukuu, wanapaswa kwanza kujifunza ujitoaji-kimungu* katika nyumba zao wenyewe+ na kuwalipa wazazi wao na wazazi wa wazazi wao kinachowastahili,+ kwa maana hilo linakubalika machoni pa Mungu.+ 5 Basi mwanamke ambaye ni mjane kwelikweli na aliye maskini anamtumaini Mungu+ naye huendelea kusali na kutoa dua usiku na mchana.+ 6 Lakini mwanamke anayefuatilia tamaa za mwili amekufa ingawa yuko hai. 7 Basi endelea kuwapa maagizo haya,* ili wasiwe na lawama. 8 Hakika ikiwa yeyote hawaandalii mahitaji watu wake mwenyewe, hasa watu wa nyumba yake, ameikana imani naye ni mbaya kuliko mtu asiye na imani.+
9 Mweke kwenye orodha mjane mwenye umri usiopungua miaka 60, ikiwa alikuwa mke wa mume mmoja, 10 alijulikana kwa kutenda mema,+ alilea watoto,+ alikuwa akiwakaribisha wageni,*+ aliiosha miguu ya watakatifu,+ aliwasaidia watu wenye taabu,+ na akajitolea kufanya kila kazi njema.
11 Kwa upande mwingine, usiwaweke kwenye orodha wajane wenye umri mdogo, kwa maana tamaa zao za ngono zinapokuja kati yao na Kristo, wao hutamani kuolewa. 12 Nao watahukumiwa kwa sababu wameacha imani waliyoonyesha mwanzoni.* 13 Vilevile wanakuwa na tabia ya kupoteza muda, wakizunguka kutoka nyumba moja hadi nyingine; ndiyo, hawapotezi muda tu, bali pia wanapiga porojo na kujiingiza katika mambo ya watu wengine,+ wakiongea kuhusu mambo ambayo hawapaswi. 14 Kwa hiyo, ninatamani wanawake wajane walio na umri mdogo waolewe,+ wazae watoto,+ wasimamie nyumba, ili wasimpe mpinzani sababu ya kukosoa. 15 Kwa kweli, tayari baadhi yao wamepotoshwa na kumfuata Shetani. 16 Ikiwa mwanamke yeyote mwamini ana watu wa ukoo ambao ni wajane, inafaa awasaidie ili kutaniko lisibebe mzigo huo, na hivyo liwasaidie wale walio wajane kwelikweli.*+
17 Wazee wanaosimamia kwa njia nzuri+ wanastahili heshima mara mbili,+ hasa wale wanaofanya kazi kwa bidii katika kusema na kufundisha.+ 18 Kwa maana andiko linasema, “Hupaswi kumfunga kinywa ng’ombe dume anapopura nafaka,”+ pia, “Mfanyakazi anastahili mshahara wake.”+ 19 Usikubali mashtaka dhidi ya mwanamume mzee,* isipokuwa kwa ushahidi wa mashahidi wawili au watatu.+ 20 Wakaripie+ hadharani watu wanaozoea kutenda dhambi,+ ili liwe onyo kwa wengine.* 21 Ninakuagiza kwa uzito mbele za Mungu na Kristo Yesu na malaika waliochaguliwa, ufuate maagizo haya bila kubagua wala kupendelea.+
22 Usiharakishe kamwe kuweka mikono yako juu ya* mwanamume yeyote;+ wala usishiriki dhambi za wengine; endelea kuwa safi.
23 Usiendelee kunywa maji,* bali unywe divai kidogo kwa ajili ya tumbo lako na ugonjwa wako wa mara kwa mara.
24 Dhambi za watu fulani hujulikana hadharani, na hivyo wanahukumiwa moja kwa moja, lakini dhambi za watu wengine hujulikana baadaye.+ 25 Vivyo hivyo, matendo mema hujulikana hadharani+ na hata yale yasiyojulikana hayawezi kuendelea kufichwa.+
6 Acheni wale walio chini ya nira ya utumwa waendelee kuwaheshimu kikamili+ mabwana wao, ili watu wasiseme vibaya kuhusu jina la Mungu na lile fundisho.+ 2 Pia, acheni wale walio na mabwana ambao ni waamini wasiwavunjie heshima kwa sababu wao ni ndugu zao. Badala yake, wanapaswa kuwatumikia kwa bidii zaidi, kwa sababu wale wanaonufaika na utumishi wao mzuri ni waamini wenzao wapendwa.
Endelea kuwafundisha na kuwahimiza wafanye mambo haya. 3 Mtu yeyote akifundisha mafundisho tofauti na yanayopingana na fundisho lenye manufaa*+ linalotoka kwa Bwana wetu Yesu Kristo, au mafundisho yasiyopatana na ujitoaji-kimungu,*+ 4 yeye anajivuna kwa kiburi na haelewi chochote.+ Pia, anapenda sana* kubishana na kushindana kuhusu maneno.+ Mambo hayo huleta wivu, mizozo, uchongezi,* na shaka zenye uovu, 5 mabishano ya kawaida kuhusu mambo madogo madogo ya watu waliopotoka kiakili+ na wasiojua kweli, wakifikiri ujitoaji-kimungu* ni njia ya kupata faida.+ 6 Kwa hakika, kuna faida kubwa ya kuwa na ujitoaji-kimungu*+ na kuridhika.* 7 Kwa maana hatukuleta chochote ulimwenguni, wala hatuwezi kuondoka na chochote.+ 8 Basi, tukiwa na chakula* na mavazi,* tutaridhika na vitu hivyo.+
9 Lakini wale ambao wameazimia kuwa matajiri huanguka kwenye majaribu, na mtego,+ na tamaa nyingi za kijinga zenye kudhuru ambazo hutumbukiza watu kwenye maangamizi na uharibifu.+ 10 Kwa maana kupenda pesa ndicho chanzo cha mambo mabaya ya kila aina, na kwa kujitahidi kufikia upendo huo, wengine wamepotoshwa kutoka kwenye imani na kujichoma kila mahali kwa maumivu mengi.+
11 Ingawa hivyo, wewe, mtu wa Mungu, yakimbie mambo hayo. Badala yake, fuatilia uadilifu, ujitoaji-kimungu,* imani, upendo, uvumilivu, na upole.+ 12 Pigana pigano zuri la imani, ushike imara uzima wa milele ulioitiwa nawe ukatoa tangazo zuri la hadharani mbele ya mashahidi wengi.
13 Mbele za Mungu, anayevihifadhi vitu vyote hai, na Kristo Yesu, ambaye akiwa shahidi alitoa tangazo zuri la hadharani mbele ya Pontio Pilato,+ ninakuagiza 14 uishike amri katika njia safi na isiyolaumika mpaka wakati wa ufunuo wa Bwana wetu Yesu Kristo,+ 15 ambao yule Mtawala Mkuu wa pekee na mwenye furaha atauonyesha katika nyakati zake zilizowekwa. Yeye ndiye Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana,+ 16 yeye peke yake asiyeweza kufa,+ anayeishi katika nuru isiyoweza kufikiwa+ na ambaye hakuna mwanadamu amemwona wala anayeweza kumwona.+ Kwake na kuwe na heshima na nguvu milele. Amina.
17 Waagize* wale walio matajiri katika mfumo wa mambo* wa sasa wasijivune* wala wasiutumaini utajiri usiotegemeka,+ bali wamtumaini Mungu, ambaye hutupatia kwa wingi vitu vyote tunavyofurahia.+ 18 Waambie watende mema, wawe matajiri katika matendo mazuri, wawe wakarimu, tayari kushiriki vitu na wengine,+ 19 wakijiwekea salama hazina ya msingi mzuri kwa ajili ya wakati ujao,+ ili waushike imara uzima ulio wa kweli.+
20 Timotheo, linda yote uliyokabidhiwa,+ jiepushe na maneno matupu yanayochafua mambo matakatifu na pia uepuke mawazo yanayopingana ya “ujuzi” wa uwongo.+ 21 Kwa kujisifia ujuzi huo, wengine wameiacha imani.
Fadhili zisizostahiliwa na ziwe pamoja nawe.
Maana yake “Mtu Anayemheshimu Mungu.”
Au “mamlaka hii; amri hii.”
Tnn., “kisheria.”
Au “wasio na upendo mshikamanifu.”
Angalia Kamusi, “Uasherati.”
Tnn., “wanaume wanaolala na wanaume.”
Au “wanaoapa kwa uwongo.”
Au “lenye afya; lenye faida.”
Au “mamlaka hii; amri hii.”
Au “wenye mamlaka.”
Angalia Kamusi.
Au “watu wa namna zote.”
Au “yenye kuheshimika.”
Au “kufanya maamuzi mazuri; busara.”
Au “kwa utulivu.”
Au “awe mtulivu.”
Tnn., “wanaendelea.”
Au “kufanya maamuzi mazuri; busara.”
Au “anayefanya maamuzi mazuri; mwenye busara.”
Au “mkarimu.”
Au “mtu anayepiga watu.”
Au “anayeongoza.”
Au “kuongoza.”
Au “kuwa na sifa nzuri kutoka kwa”
Au “asipate aibu.”
Au “waseme kwa unyoofu.”
Au “wajaribiwe kama wanastahili.”
Angalia Kamusi.
Tnn., “roho inasema.”
Tnn., “roho wadanganyifu.”
Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Au “kutia moyo.”
Au “Fikiria kwa makini.”
Tnn., “Waheshimu.”
Au “wajane maskini”; yaani, wasio na mtu wa kuwasaidia.
Angalia Kamusi.
Au “amri hizi.”
Au “alikuwa mkarimu.”
Au “ahadi waliyotoa mwanzoni.”
Au “wajane maskini”; yaani, wasio na mtu wa kuwasaidia.
Au “mzee.”
Tnn., “ili wengine waogope.”
Yaani, usimweke rasmi mtu yeyote haraka haraka.
Au “Usinywe maji tu.”
Au “lenye afya; lenye faida.”
Angalia Kamusi.
Au “anapenda isivyo kawaida.”
Au “matusi.”
Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Tnn., “pamoja na ujitoshelevu.”
Au “riziki.”
Au “makao.” Tnn., “kitu cha kujifunika.”
Angalia Kamusi.
Au “Waamuru.”
Angalia Kamusi.
Au “wasijitakie makuu.”